The Chant of Savant

Saturday 28 June 2008

CCM, Lowassa and the smoking gun

RECENT findings by Chama Cha Mapinduzi’s National Executive Committee (NEC) that some high profile politicians, including former PM Edward Lowassa, did nothing wrong reminiscent to Richmond is unfair and disturbing.

If anything, this is condoning and sanctioning corruption as CCM does itself a favour. It’s a blow and warning to the hoi polloi that they’ve to find another party to defend them and their resources. What NEC did will remain ridiculous and an insult to the Parliament and the nation.

NEC that sat in Dodoma last month, wrongly and shockingly, exonerated Lowassa and his colleagues. It said they did nothing wrong save they vacated their posts for the good of the party! Moreover, the offbeat NEC didn’t mention which good Lowassa was crucified for! But again, due to the fact that CCM itself was allegedly implicated in all these scams, chances are the good that Lowassa ’died’ for is to conceal the truth by not allowing inquisitorial minds to pull the rat out of the hat and avert the nose-diving of the whole outfit.? And doing this awarded him a slap on the back in lieu of the wrist or in the face. What predatory and nihilistic politics!

As a person who saw and heard everything regarding the Richmond scam, this unfair verdict cannot go without comments. There are some vital questions to be mused and pondered upon. Why was Lowassa axed if at all he did nothing wrong? Isn’t this the Mwenzetu philosophy that CCM has always been blamed for? Does this repugnant move aim at preempting the mizengwe of Lowassa’s bouncing back as it was recently predicted by his cronies and palmistry? Is this the lack of direction the late Horace Kolimba and Mwalimu Julius Nyerere warned CCM of?


Going back to the main question as to why Lowassa had to vacate his position, it is an open secret that the select-committee chaired by Dr Harrison Mwakyembe - Kyela CCM, beyond all shadows of doubts, found Lowassa guilty of abetting with Richmond to steal public money. Scripta manenta - it is written and what is written is for ever. Shall these ballyhoos and hoo-ha go on Dr Mwakyembe and his colleagues must stand and defend the noble job they did to the nation.

For the sake of argument, let’s consent that Lowassa was innocent. But then why did he take the verdict by the select-committee as vindictive and far-fetched? If Lowassa was and still is innocent then who aided Richmond?

To paraphrase the words of the star witness in this scam, Dr Ibrahim Msabaha, he said: Richmond is the project of the prime minister and his business partner. Why didn’t this well known business partner sue for defamation? If he is not behind the whole scam who then is? What is the logic of his addresses being used while he actually does not know anything?

Does this mean that many crucial questions evidence were left untouched? If the evidence was coloured thanks to NEC’s findings, then where are the true ones?

More on Lowassa who alleged he was not ’invited’ to adduce evidence whilst the chance was offered to everybody else, then why didn’t he also sue for loss and defamation? Hey, where do we put allegations by opposition that brought this scam to the fore that some money was donated to CCM’s campaigns? Is this that geared NEC to come with this lugubrious verdict?

Can really Lowassa be palliated or cleansed so as to bounce back? Is CCM such nugatory so as to become myopic and useless this much? Wananchi need to know who ushered Richmond in so that he can legally be dealt with and our money retrieved. And what of Deep Green Finance- that has been reigning supreme reminiscent to corruption? Will CCM one day cleanse itself as it did to Lowassa? If this goes on unabated chances are our country is slowly and systemically being privatized to mafisadi .What rationale did NEC apply?

If this is the way our country is managed, something is horribly wrong somewhere in the upper echelons of power! Will CCM and Lowassa really succeed in their attempts to jump a smoking gun?



One crucial point, if Lowassa is to bounce back and reclaim his poise, I beg you to believe ye me: Our country is heading for hell. But all in all people know between the seeds and the chaffs.

Source: Thisday June 28, 2008.

Wednesday 25 June 2008

CUF pangueni safu za juu ndipo uje muafaka

Mwezi jana, safu hii iliwapayukia CCM na mbinu zao za porini kutaka kukigawanya na hatimaye kukizamisha Chama Cha Wananchi (CUF). Tuliongelea jinsi CCM imekuwa ikipiga dana dana mazungumzo ya kutafuta muafaka ili hatimaye wanachama wa CUF wauasi uongozi wao kutokana na kushindwa kuleta suluhu.

Leo tutaangalia upande wa pili wa shilingi. Waingereza husema, "It takes two to tango." Kwa wafuatiliaji wa mtafaruko wa Zanzibar, watakubaliana nasi kuwa kimsingi kinachoitwa mtafaruko ni kinaweza kutafsiriwa kama ubovu wa muungano, kutawaliwa na katiba mbovu na ya zamani ya chama kimoja, wizi wa kura na uongozi mbovu pande zote yaani CCM na CUF.Mtafaruko ulioigharimu nchi yetu ulianza mwaka 1995 baada ya rais wa Zanzibar wa wakati ule, Salmin Amour kuiba kura.

Ushahidi upo. Uchaguzi tajwa licha ya kushutumiwa na taasisi za kimataifa kuwa ulikuwa wizi mtupu, Tanzania bara ilipeleka majeshi visiwani. Jeshi lilipiga na kunyanyasa wapiga kura na wananchi wa kawaida ukiachia mbali kuua.Bahati mbaya wakati ule nchi ilikuwa ikitawaliwa na watu wawili vichwa maji, Salmin na Benjamin Mkapa.Historia ni ndefu.

Baada ya CUF kuibiwa kura mwaka 1995 wengi tulidhani wangetia akilini na kubadili mbinu ya kupambana na dhuluma. Lakini wapi!Mpaka tunavyoandika ni miaka takribani 13 tangu zahama hili liikumbe nchi na CUF wakiwa na uongozi ule ule wanacheza ngoma ile ile ya jogoo!Katika kukuna vichwa na kutafuta dira ya kuelekea kupatikana suluhu, safu hii imegundua kuwa bila kupangua safu ya juu ya uongozi wa CUF, hakuna la maana litakalofikiwa.Tutatoa sababu.

Kwanza siyo chuki wala chuku, uongozi wa sasa wa CUF wa Profesa Ibrahim Lipumba na Maalim Seif sharrif Hamad umechoka na kuparaganyikiwa. Umeshindwa ku-deliver.Umechusha na kuishiwa kiasi cha kuwekeza kwenye maapizo na maneno zaidi ya matendo. Uulize. Yako wapi matokeo ya mazungumzo ya muafaka? Utasukumia kila lawama kwa CCM.

Lakini tukiangalia mitafaruko tena mikubwa zaidi ya huu kwenye nchi nyingine kama Kenya na Zimbabwe tunapata somo moja kuwa uongozi wa sasa si makini na hauna hoja za msingi licha ya kukosa mikakati na mbinu muafaka.Kwanini Laila Odinga wa Kenya ameweza kwa muda mfupi huku Morgan Tsvangirai wa Zimbabwe akikaribia kufanikiwa?Jibu ni rahisi kuwa wawili hawa wana hoja na wanajua aina ya adui wanayepambana naye tofauti na CUF.Hivi karibuni tuliaminishwa na uongozi wa CUF kuwa sasa suluhu ya mtafarako itafikiwa muda si mrefu.

Tukiwa tunangojea hili, mara CCM wanakuja na usanii wa dana dana kiasi cha kushindwa kufikia suluhu.Mtafaruko ulianza wakati CCM ikiwa chini ya Mkapa na Philip Mangula. Leo CCM imebadili safu yake; kuna Jakaya Kikwete na Yusuf Makamba. CUF kwa upande mwingine, bado ina watu wale wale walioshindwa ku-deliver! Je ni kwanini? Sababu ni uongozi wa juu wa CUF kugeuza chama mali ya watu binafsi wawili yaani Seif na Lipumba.

Kwa mtu anayejua udhaifu wa Kikwete, Makamba na Amani Karume, kama CUF wangekuwa wamejipanga vizuri, wasingekuwa wanaanza arifu na ujiki kila uchao. Maskini wameshindwa kuutumia udhaifu huu!Upungufu mwingine ni pupa na papara kwa upande wa CUF. Wamekuwa wakiukwaa mkenge kutokana na Seif kuangalia kiti cha rais wa Zanzibar kiasi cha kudhoofisha chama bara bila kuangalia vikwazo vya kukifikia. Mbinu ambazo amekuwa akitumia ni zile zile. Hakuzibadili kulingana na wakati na mazingira.

Mchungaji Christopher Mtikila aliwahi kuwataka CUF na upinzani kwa ujumla kugomea chaguzi kutokana na kuandaliwa na CCM katika mazingira yale yale ya kizandiki. Hawakumsikiliza zaidi ya kuingia kwenye uchaguzi bila kuondoa vikwazo vilivyowaangusha siku zote!Kimsingi hoja ya Mtikila ilijikita kwenye ubovu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao umekuwa nidyo chaka la kufanyia dhuluma zilizoshuhudiwa visiwani. Hakuna chaka kubwa kama katiba viraka tuliyo nayo. Huwezi ukawa na katiba iliyoandikwa na watu wachache kinyume cha sheria na taratibu ukafanikisha demokrasia.Katika ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ilitungwa na tume iliyoteuliwa na rais wa mfumo wa chama kimoja ili kufanikisha kuunganisha vyama vya Afro Shiraz na TANU. Haikuwa na ajenda hata moja ya mfumo wa vyama vingi.

Kutokana na udhaifu huu, CCM wakijua wazi, wamekuwa wakiitumia katiba hii kuvuruga uchaguzi wa Zanzibar na hali yote ya kisiasa.Kimsingi CUF bila kuwa na uongozi mpya na wenye madai mapana, hakuna litakalofanyika. Hapa ndipo wasi wasi na ushauri wa Mtikila vinapokuwa dira kwenda kwenye suluhu.Je Lipumba na Seif watakubali kumeza kidonge hiki kichungu kinachowanyang’anya umaarufu na ulaji?

Hakuna ubishi kuwa ushawishi wa Seif visiwani umeporomoka kiasi hata cha yeye kuwa kimya au kusema mambo kupitisha muda. Rejea madai kuwa alirejeshewa maslahi yake kama waziri mkuu kiongozi wa zamani. Kama ni kweli kwanini umma haujui msingi ya kufanya hivyo kisirisiri na kwanini alikuwa amezuiliwa kupewa marupurupu yake? Je kurejeshewa maslahi nyuma ya pazia hakuwezi kuchukuliwa kama rushwa kisiasa?

Hili linathibitishwa na kukosekana uwazi wala msuluhishi huru katika mazungumzo kama ilivyokuwa kwa Kenya.Ukiondoa vyombo vya habari vyenye kuwekwa kinyumba na CCM, vyombo huru vimekuwa vikiliangalia suala la Zanzibar kwa huruma kiasi cha kuepuka kuuangalia ukweli kama ulivyo. Wachambuzi wenge wamekuwa wakiisakama CCM peke yake kana kwamba ndiyo kikwazo pekee cha kupatikana kwa muafaka wasijue na CUF ina mchango mkubwa wa mkwamo huu!Wachambuzi huru watailaumu CUF kwa kutumia mbinu zile zile za kizamani na uongozi uliochoka.

Umefika wakati kwa Seif kung’atuka ili damu mpya ishike hatamu za uongozi wa CUF. Hatakuwa wa kwanza. Al Gore alikuwa anapendwa nchini Marekani hata baada ya kuangusha kiutata na George W Bush. Hata kwenye uchaguzi unaotarajiwa Novemba hii, alishauriwa agombee. Lakini alikataa kutokana na kushindwa kuleta ushindi mwaka 2001.Mzee Edwin Mtei na Bob Makani baada ya kushindwa kuleta ushindi kwa CHADEMA, nao waliamua kung’atuka. Sasa umefika wakati muafaka kwa CUF kubadili uongozi wake ili kusonga mbele badala ya kucheza ngoma ile ile kwa zaidi ya miaka 15-mtafaruko.

Kwa upande wa CCM pamoja na kuwa na uongozi na serikali mpya, nao wafikie mahali wafanye vitu kiutu uzima. Mdharau mwiba mguu huota tende. Watanzania wangetaka suluhu ya mtafaruko wa Zanzibar ili wafanye mambo mengine ya ujenzi wa taifa badala ya kulalia na kukeshea upuuzi kila uchao.Maalim Seif na Lipumba wakubali wameshindwa. Hivyo waachie ngazi ili damu mpya yenye visheni na mikakati mipya itafute suluhu ya mtafaruko wa Zanzibar.Kila la heri.

Source:Dira ya Tanzania Juni 24, 2008.

Kijiwe chawafukuza mafisadi

SIKU hizi Mpayukaji nimepanda cheo. Naitwa Nabii Mpayukaji (Mungu Anizidishie Neema-MAN).

Ndiyo nimerejea kutoka kwenye maulaji ya mkutano wa Sullivan. Kijiwe kimekaa kama kamati ya kuokoa mali za Watanzania na kutoa amri ya kufukuzwa kazi wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi. Tufanyeje baada ya mkuu kututosa? Kwa ufupi nilikaribishwa kwenye mkutano huo. Nilikutana na marafiki zangu wa zamani muhimu akiwamo Olusegun Aremu Okikiola Matthew Obasanjo, rais wa zamani wa Nigeria aliyetoa cheche.

Alitupa hotuba kabla ya kuisoma. Baada ya kupeana mikono na kukumbatiana, nilimsifu kwa hotuba nzuri na ya kusisimua iliyowaacha mafisadi wakubwa wakizizima na kujuta kwanini walimkaribisha mpayukaji Obasanjo na mimi.

Kuna mijitu ilinyimwa aibu! Unajua wakati Obasanjo akimwaga cheche, jamaa lilikuwa likichekelea utadhani utani! Mzee Obasanjo alitoboa kuwa nchi ya Musa sasa imevamiwa na mdudu na inanuka, hivyo mkuu aisafishe akijisafisha na yeye mwenyewe.
Hayo tuyaache. Mgosi Machungi analianzisha: “Wazee timewaita ii kutoa shinikizo na hanikizo kufukuza watu tinaowatuhumu kuuza kaya.”


Kabla ya Mgosi kuendelea, Mbwa Mwitu anadandia mic. “Afadhali. Maana baada ya kusikia mipasho kapa ya Lupaso na kuwa bize na kumzika mkolimbwa Balaliii, hawa wahuni walidhani tutasahau. Hii kaya ni yetu si ya mama zao akiwamo na mkuu. Lazima tuwawajibishe watu kama kijiwe cha Idodomya kilivyowafanyia akina Ewassa, Kadamage na Bangusilo M7ha.”

Makengeza anapaaza sauti na kusema. “Tuwataje kwa majina wajijue tunawajua na tunataka waachie ngazi mara moja.” Mara Wanakijiwe wanahanikiza: “Toboa, Toboa.”
Makengeza anaendelea: “Hakuna haja kuzunguka wala kuogopa. Yupo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kulinda na Kueneza Rushwa, Dk. Ed Oshea. Huyu anatuhumiwa kujilimbikizia mimali itokanayo na ufisadi.”


Anakwanyua kombe lake na kugida kahawa na kuendelea: “Yupo Grei Mgonjwa wa EPA. Anatajwa kwenye mama wa wizi pale Banki Kuu. Pia yupo Emmie ole Naakome wa Thieves and Insiders Community - TIC.”

Kabla ya kuendelea kumwaga razi, wanakijiwe wanahanikiza: “Taja wote mkuu ajue tunajua na hatuwataki hata kama yeye kwa sababu zake anawataka.” Makengeza anaendelea: “Kuna Johnison Mwananyika anayejifanya wakili mkuu. Pia yupo…”

Naye Kapende hajivungi. Anaongeza: “Mbona hujawataja mafisadi tuliowapiga kibuti hivi karibuni wanaong’ang’ania kijiwe cha Idodomya? Acha niwataje. Hawa ni Eddie Ewassa, Niziro Kadamage, Ibra Bangusilo M7ha, Bazee Pesatatu Miramba, Jose Muigai, Endelea Chenga, na wengine.”

Mara Mpemba anadakia: “Yakhe hujataja wote ati. Mboni Sammy Chitaahira aliyeghushi vyeti huntaji? Pia hata Blunders Goosebelt alotoa rushwa?” Mara anakumbuka jambo. “Hata huyu Maasha anayetajwa kuwa nyuma ya pesa ya EPA naye atajwe hata kama amemwajiri Riz, huyu mtoto wa nkuu.”

Anabusu kashata na kuendelea: “Mie siku zote nshangaa nkuu! Adhani hatujuwi hawa wanavonajisi kaya? Watimue hawa ati. Tushachoka nao.” “Mpemba umenena. Jitu bila aibu linang’ang’ania ofisi ya umma utadhani ya mamake! Tumechoka na majambawazi yaitwayo waheshimiwa wakati hayana heshima bali ulafu,” anapayuka Mkurupukaji anayemaliza kuweka nakala ya gazeti la Tanzania Daima mezani linapogombewa kama mpira wa kona.
Mchunguliaji anatia guu. Amekunja uso: “Hii mijitu sijui imeingiliwa na nini? Sijui inampa nini mkuu hadi anaivumilia? Au lao moja sawa na Tunituni?”


Kabla ya kujibu Mbwa Mwitu anajibu: “Hujui! Imeingiliwa na mdudu aitwaye ufisadi! Haina tofauti na mafisi wala mbwa. Pia mnaotegemea mkuu awafukuze wenzake mfikirie upya. Tangu lini ngamia kamcheka nundu ng’ombe? Lao moja tu piga ua.”

Kijiwe hakina mbavu, hasa anapotamka neno kuingiliwa. Maana siku hizi Kiswahili kimevamiwa na wachafuzi wanaobadili maana. Lakini kwa tafsiri na maana yoyote watu hawa wameingiliwa na kitu kisicho cha kawaida. Inashangaza wanavyoweza kuwatumikia mabwana wawili, mali na umma! “Lazima wameingiliwa tu. Huwezi kuwadanganya watu nawe ukajidanganya kama wanavyofanya kukalia ofisi za umma wakiwa hawana udhu, utashi na uwezo,” alitilia mkazo Makengeza.

Kabla ya kuendelea, mara Kapende alikwanyua mic. “We unashangaa uongo wakati ndiyo umekuwa ndiyo sera ya kaya hii! Iko wapi safari ya kwenda kula mana na asali aliyotufunga nayo jamaa? Huoni ndo tunazidi kuchanja mbuga kuelekea Misri? Tutashindaje iwapo Firauni anapewa kila aina ya utetezi na kinga? Sijui kwanini aliamua kumuita mwenzie Firauni!” Bila kutoa taarifa mara Mpemba alidakia na kuja na pwenti iliyoamsha mizuka ya kijiwe. Alikuwa na gazeti moja mkononi lililokuwa limemnukuu mbunge akisema hapatatosha na patachimbika bila jembe kama ufisadi utaendelea hata kama NEKI inawasafisha mafisadi kama TAKUKURU ilivyojaribu ikishindwa.

Akiwa anatikisa kichwa kwa hasira anasema: “Jama mie baada ya kuchangia niliamua kusoma gazeti la leo. mwaona huu mwanko mpya wa wabunge wenye akili? Wakiri kaya ishauzwa zamani. Hapa kazi kwetu kuanka na kuwakabili hawa maruhuni wallahi.”

Msomi Mkatatamaa utadhani kashikwa pabaya! Anakwanyua mic na kuanza kutoa cheche: “Wanaotaka mkuu awafukuze mafisadi waliomo maofisini wanakosa pwenti. Hivi amfukuze nani iwapo wote lao moja? Au hamjajua ubia huu? Hamjui ulaji huu uliosaidiwa na takrima uliwezeshwa na hiki mnachokiita ufisadi?”

Anavuta kombe lake na kupiga tama tatu na kuendelea: “Ukitaka kujua kuwa tunampigia mbuzi gitaa angalia Ewassa alivyotimuliwa na Bunge baada ya mkuu kujifanya hayamhusu. Pia angalia nyuma ya pazia Ewassa na wenzake wanavyozidi kunema.

“Yaani hata kiama kinawasifu kuwa hawakutenda makosa! Tungekuwa na watu wenye akili mbona hata huko Idodomya wangekusikia? Tungekuwa na vichwa si maboga mbona Ukonga ingeishajaa zamani? Nani alianzishe iwapo wote wameoza? Kama nisemavyo daima ni waliodanganyika kuamka na kuchukua chao bila kuchelea lolote wala yeyote.

“Kwanza mafisadi pamoja na kuwa na rungu wameishachoka na kusambaratika, sema wanakaya wanashindwa kumalizia. Baada ya kutimliwa Ewassa wamedhoofu. Ni kama kumsukuma mlevi kama tutataka kuwatoa nishai wanahizaya hawa.”
Anatukana bonge la tusi na kuendelea. “We waacha waendelee kucheza makida makida wasijue alama za nyakati zimebadilika. Nimeona upuuzi wa NEKI. Eti inamsafisha Ewassa! Nani aweza kumfufua maiti? Mbona NEKI imejua kututukana tusi zito!


“Naye anajidanganya anaweza kurudi kwenye ulaji kama mzee Mwinyi! Anacheza na mzimu na laana za Mchonga nini? NEKI imefanya upuuzi kama wa Chitaahira? Ila wajue hatutakubali kuendelea kugeuzwa mashamba yao na mashoga zao na vyangu wenzao.
“Kinachokera sana ni kuona watu wazima wakifanya mambo ya kitoto. Hivi hawajui kuwa kwa kaya yenye neema kama yetu haipaswi kuishi kwa kuomba omba ingawa wakuu wanajisifia na umatonya huu wa mchana?”


Kabla ya kuendelea Mbwa Mwitu anachomekea: “Pakua aa sorry pasua kaka wa kitabu.” Msomi anatabasamu na kuendelea: “Sasa tutoe msimamo. Tuwatake wale wote wenye kuchukia ufisadi waamke tuwakabili mafisadi. Pia kijiwe kiandae maandamano ya kulaani upuuzi wa Neki na kuwaunga mkono wabunge wenye akili kama Annee Kilangoo Malichelea, Lazarus Nyarandi, Silaha na wengine.”

Ananigeukia na kusema: “Muulize Nabii Mpayukaji hapa.” Sisemi kitu natabasamu kwa kupewa maujiko.
Anaendelea: “Mafisadi mliomo maofisini mwetu jiandaeni lazima tutachenjiana siku si nyingi.”
Akiwa anajiandaa mara gari la Stivi wa Tunituni lilipita, tukalirushia mawe na kutawanyika.
Source: Tanzania Daima Juni 25, 2008.

Africa is full of sharks

It is normally annoying when the title honourable is mentioned while referring to our Members of Parliament. You know what? I wonder just because some of waheshimiwa (Kiswahili term for honourables)are thieves to the core.

Take, for example, those spineless corrupt biggies we recently booted out from the government for their dirty deeds. We have them everywhere in Africa. They have undeservedly called and answered to the title mheshimiwa! What type of respect do they have if at all they brought disgrace to our nations? Refer to Goldenberg and Anglo-Leasing in Kenya and EPA and Richmond sagas in Tanzania. At the moment, they are up in arms against taxation of their allowances in Kenya while common peasants pay tax. What a shame!

We know how they ushered in bogus investors that are looting our minerals. Does the person who brought Richmond deserve to be called a mheshimiwa? Is they guy who stole Kiwira a mheshimiwa really? Heck no. This is a footpad. Let us face it. How should he fall short of being if at all he abusively used our office to steal from us? We elect these people to represent us but instead, they rob us.

Though these dotards look like human beings, they’re wolves in sheep skin. Though they live slap-up lives, they are like white man’s dog that lives in house full of goodies. A thief is a thief even if he’s called mheshimiwa. I abhor those calling thieves waheshimiwa. They don’t have the moral integrity to do so. For, in law, the conspirator, abettor or anybody who witnesses the commission of the offence without reporting is an actual thief or he knows the actual thief.

I still can’t believe that thugs behind Richmond , Goldenberg, Anglo-Leasing, Buzwagi, EPA, Kiwira, Net solution, TICTS and other slapdash mishmash are referred to as waheshimiwa!

To begin with, they’ve never mounted any defense to this effect. They’ve maintained silence due to irrefutable truth behind their crimes. Secondly, even when one looks at their slap up lives and the wealth they illegally own, one will never fear calling them any name one deems fit. We told them to declare their wealth. They did not do so for the fear of spilling beans. Any mheshimiwa that does not like to declare his wealth is a shark. We have them almost everywhere; in churches, parliament, mosques and even in our homes.

They like being praised and can even praise themselves. They like to be worshipped and boot-licked. They like to be seen as angels whilst they actually are actually white washed sepulchers full of dead men’s bones! They promise to bring development but end up becoming obstacles to development. Money is stolen and stashed abroad. They rule by lies and brutality. Some counterfeit their certificates. Others offer kickbacks and takrima so as to be voted for.

Note. This slap on the wrist is meant for waheshimiwa that are sharks. So the genuine waheshimiwa should spare me. I have nothing against them save to caution them to distance themselves from honourable sharks.

The wisdom of today comes from Heraclitus: "All things are in a state of flux, thus you cannot step twice in the same river for the river is constantly changing as fresh waters are even flowing. Therefore everything is changing and nothing is permanent except change itself." We need to change the waheshimiwa's corrupt way.


Source: The African Executive Magazine-Nairobi.

Wednesday 18 June 2008

NEC imeamua kuwa chaka la mafisadi?

TAARIFA kwamba Waziri Mkuu mfukuzwa, Edward Lowassa, hakuwa na hatia bali alijiuzulu kuwajibika, ila hakuhusika katika kashfa ya Richmond, ni upuuzi wa mwaka.

Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) iliyokutana hivi karibuni ilitoa tamko hili la kuchusha na kukera kama lilivyokaririwa na vyombo vya habari.

Inashangaza na kukatisha tamaa kama chama kinachojidai kupigania masilahi ya Mtanzania kikiimba wimbo wa maisha bora kinaweza kuja na upuuzi kama huu! .

Kama hakuhusika na kashfa ya Richmond ni kwanini alijiuzulu? Je, ina maana taarifa nzuri ya kamati teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ni upuuzi?

Je, kitendo cha NEC si kulidharau na kulitukana Bunge na kulionyesha kama taasisi inayosema uongo? Je, Bunge limechukuliaje shambulio na kashfa hii? Kama Lowassa hakuhusika na Richmond, alijiuzulu kwa kosa gani au kashfa gani? Huu ni uchovu wa kisiasa usio na mfano. Huu ni mwanzo wa kifo cha CCM!

Badala ya Kamati Kuu ya CCM kufanya kazi za umma ilifanya kazi ya kusafishana. Na hii si mara ya kwanza kwa CCM kufanya hivyo. Mwanzoni akina Lowassa na wenzake walitaka kuitumia Tume ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) .

Nayo bila tahadhari wala kuona mbali ilijaribu kuwasafisha mafisadi hawa bila mafanikio hadi Bunge lilipoamua kuunda kamati iliyoweka historia ya kuwa Bunge la kwanza katika Afrika kumtimua mkuu wa shughuli za serikali bungeni, waziri mkuu.

CCM imekuwa ikipewa kila aina ya majina mabaya kutokana na maamuzi yake mabaya yaliyojikita kwenye kulindana na kubabaisha. Hivi ni Mtanzania gani awe hata mwanachama wa CCM damu asiyejua kuwa Lowassa alifukuzwa kazi na hakujiuzulu? Ni nani hajui kuwa kilichomfukuzisha Lowassa ni ufisadi wa nyuma ya Richmond? .

Kuna siku CCM watakuja kutwambia kuwa Tanzania ni nchi iliyoendelea. Maana wanaweza kujipayukia lolote kana kwamba wanawaambia ‘mataahira’! Baya zaidi wanapodanganya wanajidanganya na wao pia!

Kama tamko la NEC halitatenguliwa, basi hakuna siri, aliyosema Mwalimu Nyerere yanatimia. Mwalimu aliwahi kuionya CCM juu ya kuvamiwa na wafanyabiashara. Wakati ule tulijua wafanyabiashara, tusijue ni mafisadi.

Je, Mwenyekiti wa chama, Rais Jakaya Kikwete anapotuambia ana azima ya kupambana na ufisadi ilhali akikalia kiti kwenye kamati inayopitisha upuuzi na baraka kwa mafisadi, tumweleweje? .

Tunaambiwa kuwa hata waziri Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha, hawakuwa na kosa! Mbona Msabaha aliiambia Kamati Teule ya Bunge kuwa Richmond ulikuwa mradi wa waziri mkuu wa wakati ule na Mwarabu wake? Kwa nini NEC wamesahau kuwa yaliyoandikwa huwa hayaozi (scripta manenta)?

Kama CCM itashikilia upuuzi huu ningeishauri tume teule ya Bunge na Bunge lenyewe kwenda mahakamani kupinga dharau hii na matusi kwake.

Kama Lowassa na wenzake hawakuwa na hatia wala kushiriki kwenye uchafu wa Richmond, basi NEC ituambie nani wako nyuma ya Richmond. Au ni yale yale kuwa Richmond inafutikwa chini ya busati kuepuka kumtaja mhusika wa kweli aliyeiidhinisha? Je, Watanzania nao kwa upande wao watakubali kugeuzwa mabwege kiasi hiki ilhali kila kitu kiliwekwa wazi mbele yao na kamati teule ya Bunge? Enyi Watanzania ‘wapumbavu’, nani aliwaroga hadi mkaaminishwa kuwa Lowassa na wenzake hawakuwa na hatia bali waliwajibika? Mbona Lowassa na wenzake waliwekwa ‘uchi’ mbele zenu mkajionea na kusikia kila kitu! Namna hii inatisha na si vibaya kusema: Sasa, rasmi CCM imeikabidhi nchi kwa mafisadi .

Tuliwahi kuonya kuwa CCM, kwa sasa ina ombwe la uongozi wenye akili timamu. Tulionya kuwa uchafu wa wakuu wa CCM utaiangamiza nchi. Kweli kama Lowassa hahusiki na Richmond, ni kwa nini ametupwa nje? Je, hii inaweza kuwa janja ya kumsafisha ili arudishwe kwa mlango wa nyuma? Je, uswahiba wake na Kikwete umeshinda hata haki? Je, akirudishwa, Watanzania watamkubali na kumpokea? Maana, kupitia wapambe na ‘waganga’ wake aliwahi kukaririwa bila hata chembe ya aibu akijilinganisha na mzee Ali Hassan Mwinyi aliporejea kwenye siasa na kuwa rais baada ya Wizara yake ya Mambo ya Ndani wakati ule kukumbwa na kashfa ya mauaji ya kina Nzegenuka .

Hivi karibuni Katibu Mwenezi wa CCM, John Chiligati, alikaririwa akipindisha maneno ya tume teule ya Bunge kuwa waziri mkuu wa zamani Lowassa, apime na kuamua la kufanya. Baada ya Lowassa kupima aliamua kujiuzulu. Je, huyu kama aliamua mwenyewe kujiuzulu kama tunavyoaminishwa, hii si ishara ya kukiri kuwa alifanya makosa? Kinachonichefua zaidi ni ile hatua ya NEC kuwamwagia sifa mafisadi shutumiwa waliojiuzulu kuwa walikiletea heshima chama hicho! Je, maana yake hii ni nini? Au ni yale kuwa Lowassa aliamua kuachia ngazi ili serikali yote isianguke? Kama Lowassa aliubeba msalaba wa serikali chafu inayonuka, basi iwe ni kwa faida ya walioko nyuma ya kashfa hizi na si kuwahadaa Watanzania kuwa Lowassa na wenzake hawakuwa na makosa .

Kama CCM ingekuwa ni ile ya Nyerere, Lowassa na wenzake walipaswa kufukuzwa kwenye chama hapo hapo na kuchukuliwa hatua za kisheria, badala ya kumwangiwa sifa za uongo na NEC. Kama kuna kitu kimefanywa na NEC kwa kuwatetea na kuwapongeza kina Lowassa, si kingine bali kuonyesha sura halisi ya Kikwete, wenzake na CCM.

Kinachoonekana hapa ni kwamba CCM sasa ni chama cha mafisadi. Kinachojibainisha hapa ni kwamba pesa iliyoibwa na hawa watu na washirika wao si chochote, isipokuwa ushindi kwa CCM! Je, CCM imewapongeza hawa mashujaa wake kutokana na kazi yao njema ya kulihujumu taifa ili CCM ishinde kupitia takrima? .

Kama si hivyo, sasa ni nini kilichoishawishi kamati kuu kufanya upuuzi wa mwaka? Je, wajumbe nao walihongwa kiasi cha kuja na usanii huu usioingia akilini?

CCM sasa inafikia ukingoni. Katika kikao hiki cha NEC, tunaarifiwa kuwa kulikuwa na mgawanyiko. Wana CCM safi walitaka mafisadi wasulubiwe huku wakubwa wao wakiwapinga. Je, wadogo walilazimishwa na wakubwa kuridhia upuuzi huu? Je, NEC imeamua kutoa taarifa yake na si ya wajumbe? Maana hatujaambiwa jinsi walivyofikia kutoa tamko hili hatari kwa nchi na hata kwa chama chenyewe

Je, wale wana CCM safi watakubali kuburuzwa na kuonekana wasaliti kwa taifa lao kwa kuogopa wakubwa wao? Je, tutegemee nini? Wapo watakaojitenga na CCM kuhakikisha haki inatendeka au nao watageuka wanafiki na wachumia tumbo kiasi cha kukubaliana na jinai hii? Hata kama CCM itazika tofauti zake kwa ujanja au nguvu, ukweli ni kwamba ina nyufa nyingi kiasi cha kushindikana kuzibwa. Na hili likiongezewa na kuwa na uongozi mgando usio na visheni wala udhu, siku za CCM zinaanza kuhesabika .

Kama imeweza kutekwa na kushindwa na kundi la wahalifu wachache, kweli kitaweza kupambana na changamoto za kuendesha taifa kubwa kwenye karne hii ya sayansi na teknolojia, ambapo kashfa za wateule wake zinavujishwa kwenye mitandao kila uchao? Je, huu ni mwanzo wa mwisho wa CCM? Nani anajua? Tuhitimishe: Taarifa ya Kamati Kuu ya CCM ni matusi na kejeli kwa Watanzania. Inapingana na anayotuaminisha kila uchao Rais Jayaka Kikwete na mwenyekiti wa CCM. Hakika chama hicho kimegeuka chaka la ufisadi .

Je, kwa CCM hii ya mafisadi tutaweza kuushinda ufisadi na kuwaletea Watanzania maisha bora? Kama CCM inataka kurejea kwenye uchaguzi ujao, basi badala ya kuwasafisha mafisadi, ije na hoja ya kuwabana warejeshe pesa yetu na kushitakiwa kwa ufisadi.

Isiharibu ushahidi utokanao na kuwajibika kwao. Na kama kuna ndoto ya kumrudisha kwenye ulingo wa siasa yeyote kati ya wale tuliokwisha kuwatimua, ijulikane ni ndoto ya mchana.



Source: Tanzania Daima Juni 18, 2008.

Monday 16 June 2008

Uongo wa Mkapa na wa maadui zake upi wa kweli?


Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu, hatimaye, hivi karibuni, rais mstaafu, Benjamin Mkapa aliamua kujitokeza ili ahesabiwe.
Akiwa kijijini kwake ambako alikuwa amepasahau wakati wa utawala wake huko Lupaso, Mkapa alisema wanaomtuhumu kutumia vibaya madaraka, kujipatia na kujilimbikizia mali yeye na mkewe, mwanae, mkamwana, kivyele na marafiki zake ni waongo!
Kauli hii iliyoandamana na nyodo na tambo ikilenga kuwaonyesha watanzania kama wavivu wa kufikiri ilinitibua kiasi cha kupandwa na presha.
Mkapa aliyezoea kuwaita watanzania wavivu wa kufikiri asijue naye ni mtanzania, alijisemea asijue nini itakuwa tafsiri ya maneno yake ambayo wengi wameyachukulia kama uongo na kutapatapa.
Mkapa, bingwa wa kujenga na kubomoa hoja, kipindi hiki alishindwa kuzijenga zaidi ya kuja na hoja zilizombomoa zaidi.
Wengi tulidhani:
-Angeingia kwa undani kwenye shutuma kuwa alijipatia ukwasi mkubwa akiwa madarakani.
-Angeelezea alivyoweza kujenga mahekalu ndani ya miaka kumi kitu kilichomshinda kwenye zaidi ya miaka thelathini aliyokuwa serikalini. Rejea kufichuliwa kwa mahekalu yake ya Mkuzi Lushoto, Sea View na mengine ambayo kadri siku zinavyokwenda yatafichuka.
-Angeongelea ushiriki wa mkewe, mwanae, mkamwana, kivyele na marafiki zake kwenye unyakuzi wa machimbo ya makaa ya mawe ya Kiwira.
-Angeongelea makampuni yake ya ANBEN (vifupisho wa Anna –mkewe na Benjamin).
-Angetoa hata tathmini na ripoti ya utawala wake. Maana aliondoka kimya kimya bila hata kuaga!
Inapofikia mtu mzima tena aliyewahi kuwa kiongozi wa nchi kusema uongo mchana kweupe; akitushinikiza tuuamini uongo wake na kuukataa ‘uongo’ wa wanaosema ukweli, jua ni hatari tena kubwa.
Mkapa bingwa wa salamu ya ‘mambo’ kweli ana mambo tena makubwa!
Ili tusimuonee Mkapa, tuangalie nani anasema uongo na nani anasema ukweli.
Mkapa anasema wanaodai alifuja madaraka ni wale waliokwenda kwake kutafuta upendeleo akawanyima! Mbona kama ni upendeleo, aliufanya. Sema kinachogomba ni kuwapendelea wanafamilia yake na wawekezaji dhidi ya watanzania.
Bila upendeleo mtu kama Daniel Yona angeweza wapi kumilki mgodi wa makaa ya mawe? Bila upendeleo mwanae na mkamwana wake wangewezaje kumilki kampuni la Fosnik (Foster na Nicholas-Mkapa)?
Mkapa anasema wanaomshutumu ni waongo. Huu ni uongo. Mbona wanaomshutumu ni watanzania? Mbona tunaosema hivyo hatumjui Mkapa wala yeye hatujui? Na isitoshe, Mkapa anayeishi kwa hisani ya Kikwete angetoa upendeleo gani kwa mtu ambaye hakuwa karibu naye kama akina Fredrick Sumaye walioishia kuwa muujiza wa miujiza kukaa madarakani mrefu huku wakipwaya?
Mkapa sasa ni mzee. Kuepuka kuwa mtu mzima hovyo, anapaswa kueleza ukweli badala ya kutafuta visingizio. Tumkumbushe. Aliwahi kusema uongo kuwa sera yake ilikuwa uwazi na ukweli ilhali, nyuma ya pazia, ilikuwa kinyume-uongo tena mkubwa.
Mkapa katika utetezi wake ametoka kapa kweli kweli. Mwitikio wa umma juu ya maneno yake umekuwa hasi kiasi cha kutisha.
Tazama kabla ya kuja na utetezi uchwara - kama ambavyo yeye angeuita- aliishazomewa na vijana wadogo kiasi cha serikali kutoa vitisho ikidhani umma utanyamaa!
Chini ya utawala wa Mkapa uongo ulitawala kuliko ukweli. Alitudanganya kuwa uwekezaji ungeleta tija tusijue tija yenyewe ilikuwa kwake na watu wake!
Muulize kwanini serikali ya sasa inafanya majadiliano na wawekezaji kuondoa vipengee vya kijambazi. Muulize, kwa mfano, taifa lilipata faida gani baada ya kuligawa shirika letu la Ndege-Air Tanzania au marehemu Benki ya Biashara-NBC.
Muulize kuna nini pale Tanesco alipoingiza kampuni la kikaburu kwa mtutu wa bunduki. Muulize pale IPTL kuna nini zaidi ya kuwa shimo la kuzamisha pesa ya watanzania huku wakilanguliwa umeme kuliko hata nchi zlizokaa chini ya vita kama Burundi , DRC na Somalia .
Haya ndiyo maswali ya kiutu uzima anayopaswa kujibu Mkapa badala ya kuja na uongo wa kutaka tuamini uongo wake dhidi ya ukweli anaouita uongo.
Siku ya kufa nyani miti huteleza. Mkapa akubali alifanya makosa tena makubwa. Angekuwa safi , nimjuavyo, angewafedhehesha wanaomshutumu badala ya kujifedhehesha mwenyewe.
Kwanini imechukua miaka kujibu ingawa na majibu yenyewe hayana kichwa wala miguu? Mbona aliyemtengeneza, Mwalimu Julius Nyerere aliposhutumiwa na marehemu Oscar Kambona kuwa alikuwa na pesa nyingi nje aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kujibu?
Kwanini Mkapa aende kujibia kijijini kwake? Je alikuwa akiwakimbia waandishi wa habari au kutaka kulifanya suala zima kuwa rahisi na la kisiasa kiasi cha kutoa majibu rahisi kwa maswali magumu? Kwa mtu makini asingesema ni uongo kimkato. Badala yake angeonyesha uongo ni upi na ukweli ni upi. Je imekuwaje Mkapa tuliyemjua kugeuka mfa maji hivi? Ama kweli asiyejua hajui hajui kuwa hajui na akijua kuwa hajui basi huwa hajui.
Je huu nao siyo ukabila na kuishiwa kimkakati? Hii ni tahadhari kwa rais Jakaya Kikwete kukomesha mchezo huu mchafu. Siku hizi umezuka mtindo wa mafisadi kwenda ‘kujitakasia’ majimboni kwao baada ya kutoa takrima ya misaada uchwara. Kwanini misaada leo na siyo wakati alipokuwa madarakani? Kwali hujafa hujaumbika! Na aliyeko juu mgoje chini huku avumaye baharini papa.
Bahati mbaya kwa watu wetu, kutokana na umaskini wa kutengenezwa na tawala fisadi, wanakubali kutumiwa; kama sindano ambayo hushona nguo nyingi ikabaki uchi! Hata hivyo, hii siyo kinga. Pema ujapo pema ukipema si pema tena na sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.
Sisemi Mkapa anafanya utoto. Lakini kuna haja ya kuacha kufanya utoto kwenye mambo ya kiutu uzima. Mtoto huosha tumbo lake akajiridhisha ameoga mwili mzima.
Kwa ubishi na tabia ya Mkapa angekuwa safi asingeishi kutegemea ulinzi wa Kikwete ambaye ni mdogo kwake kwa kila kitu. Kinachoendelea ni ushahidi tosha kwa Mkapa hakuwajibika. Hata Kikwete ambaye serikali yake inakumbwa na kashfa lukuki asingemlinda kama siyo kuchelea yatakayomkuta baada ya kuachia madaraka kama Mkapa.
Tungetaka Mkapa, mkewe, mwanae, mkamwana, kivyele na rafiki zake waeleze ukweli. Wakane au wakubali.
Au kama Mkapa na wenzake ni safi kama tunavyoongopewa basi wakubali:
Kushitaki wale wanaowashutumu kwa kuwachafulia majina na kuwazulia.
Pili Mkapa awataje hadharani hawa wabaya wake wa kuchongwa.
Akubali kuchunguzwa na matokeo ya uchunguzi yaweke hadharani.
Tuhitimishe kwa kumshauri Mkapa aachane na kutafuta visingizio. Badala yake arudishe mali zetu huenda umma unaweza kumsamehe. Na kama ataendelea na majibu yake yasiyoingia akilini atazidi kuudhi umma kiasi cha kuamua kumshughulikia kwa nguvu zake. Pia azingatie kubadilika kwa alama za nyakati. Zamani wateule walikuwa hawaguswi. Leo wameanza na zomea zomea. Kesho wanaweza kufanya kweli ajikute msambweni kama ilivyotokea Zambia na hivi karibuni itakavyotokea Malawi na hatimaye Tanzania .
Hata Edward Lowassa hakujua wala kuamini angetimuliwa kwa aibu kama ilivyotokea.

Source: Dira ya Tanzania Juni 17, 2008.

Wednesday 11 June 2008

Wanalinda maiti inayonuka!

TANGU niache gongo na bangi sikosi ufunuo. Japo si mtume kwa taifa maalum, huwezi kujua. Imeandikwa; walitumwa mitume kwa maelfu. Utajuaje ni mmojawapo? Isitoshe, kila mkataza mabaya akaamrisha mema, ni mtume hata kama haingii msikitini au kanisani.

Si haba, Mpayukaji ni mtume kwa taifa lililodanganyika na kupotea, na ana kila dalili na ushahidi kuthibitisha utume wake. Tuyaache tusije kupigana mawe bure na kutishiana mashingo.

Katika ufunuo niko kwenye nchi iitwayo Tanzia katika mji wa Kufa-as salama. Na huu ndiyo ufunuo. Tazama naona maiti anayenuka akiwa amezungukwa na walinzi waliokonda wakimlinda asikamatwe na kundi la wajoli wenye hasira anaotaka azikwe kuondokana na harufu mbaya na wadudu vimtokavyo maiti huyu.

Pembeni naona mifupa mingi ya watu iliyokauka, inasemekana ilikuwa imeliwa na huyu maiti na wenzake waliokuwa wamewatupia wale askari mithili ya mbwa wamlindao wagugune kama takrima yao.

Wajoli wamehanikiza wakisema: "Azikwe, azikwe tena leo." Mara mkuu wa wale walinzi waliokondoena kwa njaa na dhiki na magonjwa naye anasema: "Nani hapa, nyie si maiti watarajiwa kama mimi?"

Anaendelea: "Muoneeni huruma mwenzenu apumzike kwenye ufu wake. Na liwalo na liwe hazikwi maiti hapa."

Japo kuna wanaomshangaa kwa nini mtu mzima anafanya istizimari hadi kulinda uoza na harufu mbaya wasijue naye alishaugua na kuanza kunuka taratibu! Naye ananuka ingawa amejitona uturi. Anatema wadudu wakavu.

Naona wajoli waliochukia wakimgeukia mkuu na kusema: "Nawe unanuka na tunajua u mfu mtarajiwa kitambo si kirefu. Wewe na nyumba yako mmeishapigwa na majipu ikiwa ni alama ya laana ya kurithi na kuendeleza usaliti wa taifa la Mungu."

Maskini maiti na mkuu wa walinzi. Hawakujaliwa kuota ndoto na kupokea ufunuo! Hawajui, ingawa, wanalindwa bado ni maiti wa kesho! Hajui kuwa wanajua anaugua ugonjwa wa majipu anayoficha kwenye mavazi yake ya thamani! Hajui umma unajua hayo ndiyo matokeo ya laana ya kuhujumu umma!

Japo mkuu ana macho, ukweli ni kwamba ni kipofu asiyeona zaidi ya usawa wa tumbo na pua yake. Maana ni jana tu huyu maiti mtoa harufu anayemlinda alikuwa hai, lakini akalaaniwa kutokana na kula nyama za wenzie huku akijitia kiburi na ushufaa asijue zake zilikuwa zimeisha!

Maskini hajui maiti wake wanayetaka azikwe alikufa kwa ugonjwa huu! Ugonjwa huu uliuua ukoo wake. Ulimuanza yeye. Ukafuatia mkewe, wanae, mashemeji zake hata marafiki. Baya zaidi, alimuambukiza rafiki yake baada ya kumuachia makapi yake ayale!

Hawakujua. Mkuu huyu hata baadhi ya walinzi aliwarithi toka kwa maiti wanayetaka azikwe ilhali mkuu akimlinda kwa gharama yoyote akijua naye kesho yatamkuta!

Wakati nikiendelea kutafakari vita baina ya waja, wagonjwa na marehemu, mara niliona kundi la mbwa na inzi likishabikia harufu ya ile maiti. Pia yalishangilia uamuzi wa mkuu wa walinzi wa maiti kuiacha bila kuizika ili yaendelee kufaidi uoza!

Ni mbwa na mainzi manono ya rangi ya kijani. Yametapakaa kila sehemu kiasi cha kuvuma na kutoa mlio ulioshinda nguvu ile sauti ya wajoli waliotaka maiti izikwe.

Ghafla ajabu ilitokea. Ile maiti, kwa nyodo, ilianza kupayuka ikikana kuwa ilikuwa maiti! Ilisema wanaosema ni maiti apaswaye kuzikwa ili kuondoa harufu ni wale ambao eti walinyimwa kitowoe cha nyama ya watu wakati wa uhai wake, waliokwenda kwake kutafuta vinono akawanyima! Maiti ilitoa wadudu kila ilipopayuka. Ilipayuka kama imepagawa isijue ni maiti.

Nilishangaa kuona maiti ikiongea tena kwa jeuri. Baadaye niling’amua kuwa ilikuwa ikipata kiburi kutokana na kulindwa na walinzi wa yule maiti mtarajiwa. Ilipata kiburi kutokana na kushangiliwa na mainzi ya kijani.

Kutokana na kiburi cha kuzungukwa na mbwa na walinzi watiifu kwa maiti mwenzie mtarajiwa, maiti ile ilihanikiza ikikana kuwa haikuwa inanuka bali wale waliokuwa wakisema ndio wanaonuka! Iliwakejeli waliotaka izikwe ili kuondoa harufu iliyokuwa ikiwakera. Ilipayuka: "Waongo, waongo, waongo mie sinuki wala si maiti."

Maiti ikiwa inashangiliwa na mainzi ilipaaza sauti na kusema: "Nyie mlikuja kwangu wakati wa uhai wangu mkitaka niwaneemeshe msiwe maiti kama mimi nikakataa sasa mnanionea wivu."

Ilizidi kutema wadudu na harufu kiasi cha kuzidi kuwachukiza wale wajoli waliozidi kuhanikiza izikwe ili kuondoa makufuru na harufu katika ardhi takatifu inayonajisiwa na maiti hawa wawili mfu na mtarajiwa.

Ajabu maiti ile ilikuwa imefura kwa kuchimbwa chimbwa na wadudu! Ilizidisha kiburi baada ya kuona mkuu wa walinzi na mbwa wakiilinda. Mara naona nyuki nao wakiungana na wajoli kutaka maiti izikwe.

Mainzi yalishangilia kusikia maiti ikijitetea. Yalishangilia yakijua kuwa kama ingezikwa yangekosa uhondo wa harufu yake ambayo ni machukizo kwa walio hai, lakini burudani kwao.

Maiti mtoa harufu ilisifika kwa uchoyo na roho mbaya ilipokuwa hai. Ndiyo maana baada ya kufa ilipewa adhabu ya kuwa kituko kwa walio hai. Alisifika kwa usahaulifu wake. Maana kama si yule babu aliyemlea wala asingefikia kuwa mkuu wa umma aliyeguguna na kuacha nyuma dhiki na makufuru. Ajabu aliguguna mifugo hata watu!

Lakini yote aliyasahau akafuata njia ya waovu akiongozwa na maiti wengine na mkewe marehemu ambazo nazo hazijazikwa kutokana na kuzungukwa na wale mbwa wa mfuga mbwa marehemu mtarajiwa.

Tazama nikiwa nashangaa jeuri ya maiti na kelele za inzi na mbwa, mara niliona genge la mbwa mwitu wenye sura za watu likiwa linaguguna kila kitu. Ni mbwa waliokuwa wamenona na kunawiri sina mfano. Ni mijibwa kweli kweli.

Nikiwa natafakari hili na lile, mara niliwaona wale mbwa wanaomlinda maiti anayeshabikiwa na mainzi huku akizomewa na wajoli, nao wakianza kung’aka kwa hasira baada ya kugundua kuwa kumbe kwenye mchezo huu wa mauti waliokuwa wakifaidi si wengine bali mfuga mbwa na mainzi, lakini si wale mbwa.

Mbwa wanaanza kujitambua kiasi cha kuacha kuwabwekea hata kutishia kuwararua wale wajoli wanaodai maiti ile izikwe mara moja.

Tazama naona maiti imezidi kufura kwa hasira ikisema inasingiziwa kunuka na kufa ilhali inayonuka ni maiti iishiyo kwa hisani ya mfuga mbwa mpumbavu anayewatumia mbwa kuwahini na kuwashambulia wajoli badala ya kuwalinda!

Nikiwa nakaa vizuri kutafakari, mara harufu ya ile maiti inaniingia puani. Mara na wadudu waliokuwa wakimtoka wananinyemelea. Ghafla naota nikitimka mbio kwenda kutafuta kolego nizike maiti. Salamu kwa Mzee Machungi Mgosi wa Mtibwa na wanakijiwe wote. Namtaka Mgosi twende zetu Ushoto tukatafute tunguli tuwafunge macho walinzi na mbwa na mkuu wao ili maiti yetu izikwe. Yameadhirika vya kutosha.

Nawashaurini watoke kwenye kibuhuti waje tuzike maiti iache kutunukia. Hakika huu ni ufunuo kwa wenye akili na taamuli. Kwa wapumbavu ufunuo huu ni machukizo. Maana inzi mpenda uoza ukipiga uturi lazima akuchukie. Je, maiti yetu itazikwa au?

Kila la heri.

Source: Tanzania Daima Juni 11, 2008.

Obama: Democrats Have Defied Arrogance and Racism

Barrack Obama is finally the flag bearer for the US Democratic Party after trouncing former First Lady Hillary Clinton.

Obama has what it takes to be US president. The Times vol.171, No.10/2008 unveiled how racist the idea that Obama does not qualify to be president of United States because of his colour is. The reasons so given are not convincing enough.

Recently rumors and attacks were deliberately cooked and circulated that Obama is affiliated to Al-Qaeda and Islamism simply because one of his name is Hussein, or Obama that sounds close to 'Osama.' Such moribund allegations!

Another propaganda propelled by detractors is that he was once seen in a traditional garb in Kenya! Detractors went ahead to allege that Obama attended madras (Islamic school) in Indonesia. These smear campaigns are wrong and malicious. The Times also published photos of presidents George Bush, and Bill Clinton in Chinese and Indonesian attires respectively. Obama and Hillary Clinton were pictured in a traditional garb and Eritrea attire.

How will Americans feel shall one say they are affiliated to Islam just because their Capitol Hill looks like a mosque? It has a dome and minaret-like features!

John McCain has his origin in Ireland as per the sound of his name. Bush as well as Clinton are not original inhabitants of America.What is wrong with the person of African origin becoming president of the US? Why is it okay for Jews, Britons, and others to rule America but bad for a black man or woman? This to me, is apartheid. It justifies all machinations against Africa in the first place. It reminds me of the hypocrisy of religions which condemn everything African except her sweat and resources!

I once averred: Africa must be redressed for the evils of slavery, cultural imperialism and colonialism. Why was it possible to redress Jews who were butchered by ghouls like Adolph Hitler and Benito Mussolini; but it has been impossible to redress Africans who suffered under slavery and colonialism? Why is the West paying a blind eye when it comes to redressing countries and people badly affected by small arms and wars resulting from plundering of Africa’s resources in Liberia, DRC, Angola, Mozambique, Zimbabwe, Namibia, South Africa and others?

Opposing Obama due to his skin colour is but unveiling white hypocrisy towards other races especially African. Shall the world need to live in peace and harmony, such issues must be addressed thoroughly otherwise, peace and harmony will remain expensive items to the world.

What we are witnessing in the US is not the war against Obama but a black person whom the white has always regarded as inferior. It is obnoxious white arrogance and supremacy aimed at changing history. Should Obama become president, he will not revenge. Africans are more generous and forgiving than any other race on earth.

Americans ought to lead by example as they shy away from racism and dwell on meritocracy but not white supremacy and arrogance. Vote for or against Obama as an American but not a black, Kenyan or else. After all, Obama is an American.Now that Obama has defied the odds, let all Americans for change rally behind him so that change can be realised.

Source: The African Executive Magazine June 11, 2008.

Tuesday 10 June 2008

Hawa ni wezi au waheshimiwa?


Huwa napata utata na wakati mwingine kinyaa itajwapo heshima sijui cheo cha mheshimiwa! Huwa nashangaa sana hasa nionapo wanaoitwa waheshimiwa. Wengine hawana wala hawastahili heshima. Wananuka ufisadi. Ni mafisadi hadi kwenye mifupa. Ni mafisi.
Chukua mfano watu waliofukuzwa kazi kwa kushiriki kwao ufisadi wanaoendelea kuitwa waheshimiwa. Hivi kweli hawa ni waheshimiwa? Wana heshima gani iwapo walitenda mambo ya aibu? Waliobainika kuiingiza nchi kwenye mikataba ya kiwizi ya uwekezaji kama vile Richmond na mingine mingi, kweli nao ni waheshimiwa? Je hawa waliojichukulia mali na pesa za umma kwa kutumia madaraka siyo wezi kweli hata kama tunawaita waheshimiwa? Wapo wengi wake kwa waume. Ukiwaona wana sura za binadamu. Lakini ndani ni mafisi watupu.
Je sisi tunaowaita waheshimiwa wakati tunajua ni majizi nasi tunastahiki heshima kweli? Je heshima ni maneno au matendo?
Wanasheria wanasema: mharifu ni yule aliyetenda kosa la jinai au aliyeshuhudia asiripoti au aliyeshirikiana na aliyelitenda. Kisheria mharifu ni yoyote anayeshiriki kutenda kosa la jinai ima kwa kujua au kutojua hadi atakapobainika vinginevyo.
Je hawa waliofukuzwa madarakani kutokana na wizi na ufisadi siyo majizi hata majambazi kweli? Kwangu ni majambazi. Nina sababu:
Kwanza hawajawahi na hawataki kujitetea zaidi ya kukaa kimya huku wakifanya maigizo na usanii vya kisiasa ili waonekane hawana makosa wakati wanayo ili muda upite tusahau. Hatutasahau wala hatutawasamehe.
Pili, ukiangalia historia zao na mazingira hata ya ukwasi wao, hutahofia wala kusita kuwaita majizi. Tunao wengi. Wamo bungeni, serikalini,misikitini,makanisani hata majumbani.
Tunao kwa mamia. Wapo wanaotumia madaraka kujitajirisha huku umma ukiendelea kuwa maskini. Wapo hata wanaotumia neno la Mungu kuwaibia watu maskini na wajinga wenye shida za kimaisha. Ukiwaona utawajua. Hupenda kujisifu na kujisifia. Wanapenda kuabudiwa na kuonekana malaika wakati ukweli hawana tofauti na ibilisi mwenyewe. Maana tulionywa. Ibilisi wa mtu ni mtu aweza kuwa wewe hata mimi. Aweza kuwa mtukufu hata tajiri na msomi. Ibilisi ni ibilisi hata aitwe mchungaji, mheshimiwa, kizito na mfadhili na makando kando mengine mengi.
Hivi aliyesababisha watanzania kulanguliwa umeme siyo jizi tena kubwa lao? Na huyu aliyesababisha madini yetu kuwaneemesha wawekezaji ilhali sisi tunazidi kuwa maskini? Aliyeghushi vyetu vya elimu yake na kutoa rushwa wakati wa uchaguzi siyo mwizi kweli? Vipi kuhusu aliyetumia bunduki kuingilia madarakani? Vipi kuhusiana na mtu asiye na sera za kutukomboa bali kututumia badala ya kututumikia?
Tuzidi kuhoji na kuhoji. Vipi mheshimiwa anayejizungushia mabaunsa na walinzi kila aina. Je anamuogopa nani kama siyo matendo yake machafu nyuma ya pazia?
Hebu fikiria juu ya mtu anayetoa toa ahadi asitekeleze hata moja. waswahili husema; haja ya mja kunena, muungwana ni vitendo. Je asiyetimiza hili siyo mshenzi hata akiitwa mheshimiwa?
Mfikirie anayewadanganya watu. Anasema hili leo kesho lile. Je huyu anayostahiki hata chembe kuitwa mheshimiwa? Mbona uheshimiwa umevamiwa kiasi cha kuwa uishiwa? Mbona uheshimiwa umekosa thamani kiasi cha kutumiwa na majambazi?
Sipingi. Kuna watu na heshima zao. Lakini pia wapo wengi waitwao waheshimiwa wasiostahili hata nusu ya heshima. Wapo wenye silha, hulka na tabia za wanyama waitwao waheshimiwa.Kuna watu wanapaswa kuwa gerezani siyo bungeni wala uraiani. Hebu fikiria anayewatisha watu ima kwa bunduki au neno la Mungu wakati yeye ni tapeli. Hebu fikiria mtu anayewaganywa watu ili awatawale kama yule mshenzi wa kiingereza aitwaye Lugard alivyotufanyia.
Jaribu kufikiria zaidi. Hebu jielekeze kwa mtu anayesimama kwenye viwanja kama vile vya Jangwani akatangaza kutenda miujiza wakati hana lolote bali janja ya kuwaibia wajinga wengi.
Je hawa hawapo? Siku moja tulikuwa tunajadili ni kwanini nchi za kiafrika haziendelei ilhali zimekuwa na serikali kwa zaidi ya miaka 50. Tuligundua mdudu mmoja mbaya sana akiziangamiza nchi hizi. Anaitwa ulafu na ubabaishaji.
Tembelea Afrika kuanzia kaskazi hadi kusi mashariki na magharibi. Utakuta watu wanaojifanya wanawapenda watawaliwa waliwa. Watajionyesha kama wapenda maendeleo wakati wao ni vikwazo vya hayo maendeleo ndoto. Wanaishi maisha ya kifalme wakizungukwa na makapuku wa kunuka. Wao na familia zao, kupitia ujambazi fichi wa kimfumo hawana tofauti na kupe. Wanawanyonya watu maskini kwa kisingizio cha upuuzi uitwao kuchaguliwa!
Wanaficha mabilioni ya fedha Ulaya. Wanachekiwa afya zao na kutibiwa Ulaya. Wameua hospitali, zahanati,shule, mashamba,viwanda na kila aina ya mradi. Bado majizi hawa wanawahadaa watu wanaweza kuwaletea maendeleo. Kwao watu ni familia na marafiki zao. Wameishiwa kiasi cha kushindwa hata kujitambua. Bahati mbaya na watawaliwa nao wameendelea kuuziwa mbuzi kwenye gunia kana kwamba hawana akili wala macho! Bado wanahanikiza wakiwaita majambazi waheshimiwa. Mobutu yule jambazi wa Kikongo naye aliitwa hadi mtukufu. Daniel Moi kule Kenya eti naye aliitwa mtukufu! Kenyatta bingwa wa kupora ardhi eti naye anaitwa baba wa taifa! Ameanzisha taifa gani iwapo nusu ya wananchi wa Kenya hawana ardhi? Je huyu siyo fisi mtu aliyekuwa akijificha nyuma ya madaraka na uheshimiwa?
Hata nifungwe au kupigwa mijeledi, sitawaheshimu waheshimwa majambazi waliotamalaki kwenye nchi za kiafrika. Sitaacha kuwaambia kuwa wao ni majizi na siyo waheshimiwa.
Kinachonikere sana ni kuona wezi hawa waheshimiwa wakitukoga kwenye mitaa ya wazito kwa ukwasi wao. Wengine wamezidisha kufuru. Eti bado wamo bungeni badala ya Ukonga! Eti kuna wanaopanga kurejea kwenye medani ya uongozi kwa kishindo baada ya kunyea kambi! Jamani hadi mtajwe majina ndipo mstuke!
Kama kuna waheshimiwa ningependa kuwapa heshima zote si wengine, ni wale waliofungwa kwa makosa madogo madogo kama wizi wa kuku. Ni wale wanaobeba zigo la taka la waheshimiwa wezi.
Tuhitimishe. Kuna haja ya kubadili mfumo wetu wa kijambazi unaotoa uheshimiwa hata kwa majambazi. Kuna kila sababu ya wasomaji na wananchi kwa ujumla kuanza kutafuta jibu la kejeli na matusi haya kuhusiana na cheo cha mheshimiwa. Mheshimiwa au mwizimiwa?
Leo sisemi sana . Nawashauri wale waheshimiwa-fisadi wanaojijua kuwa mibaka na majambazi, waachane na siasa na kwenda kuzimu. Salamu kwa Bilionea wa vijisenti na chenga kwa sana , mvi nyingi Eddie Ewassa, Niziro Kadamage, Pesatatu, Jigoda, Muigai na waheshimiwa mafisadi wengine.

Source: Dira ya Tanzania Juni 10, 2008.

Thursday 5 June 2008

Mpayukaji na mipasho kapa na utumbo ya Lupaso

Baada ya kutoka Ziroziro, kijijini kwa Mkolimbwa, Daudi Ballali, gavana wa zamani wa Banki kuu yenye mawizi makuu na kutokuta matanga nyumbani kwa marehemu, niliamua kutimkia zangu Lupaso kusikiliza mipasho kapa ya Mwana wa Matonya mjasiriamali damu damu.

Sikwenda Lupaso kusaka hisani kwa mtu aso hisani aishie kwa kutegemea hisani ya watu wadogo kwake.

Nilipita Nakapanya nikajionea Chamaki nchanga (panya) anavyotafunwa utadhani hakuna dini!

Nieleze kwanza. Watu wamepigika kule sina mfano. Wamepigika hadi kufakamia uongo na misaada makapi itokanayo na ukwapuzi kwenye kaya! Hayo tuyaache yana pake.

Nikiwa natafakari hili na lile tayari kusikiliza kitakachoongelewa hasa kuhusiana na madai ya ufisadi wa familia nzima na genge la marafiki, mara niliona gari lenye namba za ANBEN likiwa limesheheni misaada yenye nembo za Kanada.

Sijameza mate naona jingine la Tanpower, mara la Fosnik, la Kiwira hilo, la TASAF, mara la Fursa sawa kwa First ladies, mara Kagoda, Deep Green Finance, Tangold na mengine mengi kama haya!

Nikiwa nashangaa shangaa mara mzee wa dole tupu bingwa wa mipasho asiye na bendi anasimama mimbarini kumwaga cheche. Jamaa anaijua mipasho japo zamani ilikuwa viwanja vya wachovu kujimwaga na mitusi yao waliyoiita taarabu.

Mzee huyo. Anaanza kumwaga cheche-longo longo. Ajabu niseme. Anasema uongo mchana kweupe na watu wanauamini kiasi cha kumdanganya naye kwa kumshangilia wakati wanashangilia misaada makapi aliyokuja nayo. Hapa haijulikani anayemgeuza mwenzie bwege!

Anasema kwa kinywa kipana. "Wanaosema nilikwanyua njuluku ni waongo, waongo waongo na huu siyo uongo niaminini"

Anaendelea baada ya kufuta kinywa kilichojaa mapovu. "Hawa hawana lolote isipokuwa chuki ya kuwanyima hisani."

Kweli kuna binadamu walinyimwa aibu. Baba zima linatema uongo na kujisifu limewajibu wabaya wake! Yaani unapayuka uongo mweupe huku ukiwaita watu waongo wakati muongo tena mkubwa wewe!

Moyoni najisemea. "Mbona huyu anajivua nguo hadharani akidhani watu hawajui yake? Au laana za Nchonga;mwe!"

Eti anadai tusisikilize uongo wa wale! Tusikilize wako? Mbona hawa waliotaka fadhila ni wa kuchongwa? Au anaongelea fadhila kwa familia yake na marafiki zake na wawekaji?

Jamani uongo ni uongo hata unenwe na mkubwa au msataafu.

Tulidhani angekana kuwapo na kuwa na uhusiano na ANBEN ambayo tunaambiwa ni vifupi vya majina yake na mamsap wake. Mbona anaumbuka. Mbona naona magari ya ANBEN, Tanpower, Fosnik na upuuzi mwingine yamesheheni hapa?" Nilijiuliza bila kujijibu.

Hivi uongo ni upi? Kudai jamaa alikwapua kiasi cha kupanajisi patakatifu pa patakatifu? Mbona aliyeanza kusema ni Mchonga maneno na vinyago vya Mpapure aliyemchonga yeye? Au naye alinyimwa fadhila? Utajuaje huenda alinyimwa fadhila ya kulindwa Azimio lake la Arusha na watanzania wake.

Give the devil its due. Kwangu kama Yuda angekiri kuwa alipewa vipande vya fedha awe salata wa Mwana wa Adam ni ukweli hata kama Yuda ni salata.

Hivi uongo ni upi? Kusema Kiwira ilitwaliwa tena kijambazi; au kusema Bi Mkubwa alikuwa mfanyabiashara tena Chinga kama nonihino wake tena akiwa patakatifu pa patakatifu? Je uongo ni kusema kuwa Fosnik ni kampuni mtoto au ANBEN ni baba na mama lao?

Jamani tunapelekwa wapi kule ambako watu wazima wanafanya mambo ya kitoto mchana kweupe?

Zamani tuliamini kuwa waganga njaa ni wana muziki peke yao hasa wa mipasho na ndomboro! Kumbe tulinoa. Mbona wapo wengi tena wanacheza ndomboro makanisani huku wengine wakicheza ndomboro kwenye majukwaa ya kisiasa!

Kumbe hata kwenye siasa kuna wachovu na wachumia tumbo tena wenye majina. Mie nilidhani jamaa angetoa hata salamu za rambi rambi kwa mtumishi wake Daudi Ballali mkolimbwa aliyewatumikia wenye matumbo wakaishia kumtoa kafara ili siri zao zisitoke!

Nasikia aliyemkolimba anajulikana na ni mtu ambaye huwezi kumtarajia. Jamaa ana sumu kali. Lakini naye mwoga. Anapenda kupendwa wakati hapendi maendeleo yetu.

Hayo ya Ballali tuwaachie wapayukaji wa pale kukuu wanaosema kwa vinywa utadhani vimegeuka njia ya kutolea uchafu!

Tulidhani Mkahapa angegusia anachojua kuhusiana na Kagoda, Meremeta, Deep Green Finance, Tangold na kutoa maelezo juu ya jinsi alivyoweza kujenga mahekalu pale Mkuzi na Sea View bila kusahau pale YMCA ukweni.

Tulidhani angeelezea anachojua kuhusiana na M bank. Tulidhani angeelezea jinsi dili la Net Group Solution lilivyotoa faida kwa mjasiriamali na shemegi zake.

Tulitegemea angetoa taarifa juu ya mafanikio ya kampuni za kikaburu alizoziamini akazipa Air Tanzania na marehemu NBC ambayo nasikia ilifanya miujiza kurejesha pesa ya manunuzi ndani ya miezi.

Jamaa kwa kukufuru sina mfano. Eti anasema anaishi kwa pensheni! Au ni yale ya akina Fred walioishi kwa kukopa kwenye mifuko ya pensheni wasirudishe ili waonekane wanaishi kwa pensheni?

Hivi jamaa huwa ana washauri au washauri wake ni Nick na Ann na Fossie? Maana matapishi aliyotapika hata kama alitapikia kwao alikokuwa amepapiga kibuti kwa muda mrefu, yamemvua nguo.

Anasema bila aibu eti tunaodai alikwapua tulinyimwa hisani naye! Nani amuombe hisani kiumbe anayelindwa kama mtoto mchanga. Nani atafute hisani kwa mtu ambaye ujio wake ulitokana na kufanyiwa hisani ya kuaminiwa na mzee aliyekuwa hana wa kumrithi asijue alikuwa akimwamini nyoka mayai?

Nani angetaka hisani kwa mtu aliyekuwa hajui atokako wala aendako? Juzi nilisikia wazee wa kizanaki wanataka kumtema kwenye familia yao maana hawana mila ya kuza mibaka. Sijui nao waliposikia mipasho kapa ya Lupaso walisemaje na kujisikiaje?

Hivi na Kikwekwe aliyasikia haya matapishi ya Lupasho? Kama kweli anamaanisha anachosema kuwa anadhamiria kuikomboa kaya toka Misri alipoiacha Filauni Mkahapa, basi inabidi arejee kufikiri upya kuhusu kinga yake ya kishikaji.

Naona nambari wahedi imeishaanza kujitenga na jamaa.

Jamani kuna haja ya kuacha uvuvi wa kufikiri kama jamaa. Kwanini tusimtafutia chumba pale Ukonga ili angalau ajifunze kupima maji kabla ya kutia mguu?

Juzi alizomewa tukatuma Fanya Fokyo Ukome. Ila tujue watu wamechoka na kuna siku wataacha kuzomea wafanye kweli. Maana wanaoibiwa na kudanganywa ni wao wanaoishi maisha ya kipensheni wakati wezi wachache wakiibia mifuko ya pensheni na kuwadhihaki wanaishi kwa pensheni.

Kabla ya kumaliza siwezi kuacha kuonyesha mstuko na unywanywa niliopata baada ya kuona gwiji wa falsafa akigeuka gwiji wa uongo na lugha za kihuni. Kusema ukweli nilistuka na kumuomba Mungu asiniadhiri hadi kufikia hatua kama hii ya kugeuza domo kuwa bomba la kutolea uongo na uchafu.

Nimalizie kwa kumtaka jamaa aache uhuni kama alivyosema jamaa mmoja wa wapingaji. Badala ya kuja na uhuni aje na ukweli. Ikibidi atubie wanakaya ni watu wa amani wanaweza kumsamehe ili mradi arejeshe njuluku zetu na kutoa ushahidi dhidi ya wale aliowapendelea wakaneemeka wakati sisi tukizidi kuteketea na kuongopewa.


Mwisho naomba ukisoma waraka huu uuchane. Maana haukulengwa kuchapishwa magazetini bali inaonekana kuna mhariri kibaka ameuiba na kuutoa. Ni top secret. Nimefanya hivyo ili kumlindia heshima mtu mzima hovyo watoto wasije wakausoma na kujua uhovyo wake wakatucheka wote.
Huo ndio waraka juu ya mipasho kapa toka Lupaso kule kwenye nchi ya wangumi. Hii ni nchi ya kufikirika msije mkaikosea na Lupaso ya Mtwara.

Source: Tanzania Daima Juni 4, 2008.