The Chant of Savant

Saturday 27 June 2009

Thanks section 90 (2) (b) to pass my budget


I am dreaming of being the minister for money Mstaafu Mkulu. This is why, hereunder, I’m revisiting my budget that sailed through thanks to section 90 (b) of the one-party-made-potholed constitution of Bongolala.

I thank Lord. For my budget’s attracting many people who liked it so as to propose I take over after his Excellency finishes his performance. Let me note pointedly. The MPs that bayed to humiliate my budget were themselves humiliated.

Though those who do not know economic-and-reaping matters trashed my budget for nullifying tax exemption for NGOs by offering tax holiday to coconut oil, they missed a point. All is done in order to cope up with economic depression the world faces currently.

Now I am walking thumbs-up thanks to presenting a historic budget. Where else have you ever seen Tshs. 19/-bn set aside just for tea and yum-yum?

Our budget is crystal clear. If compared to those of other countries, one will see the rationale. In other countries, no dime is set aside for drinking water let alone tea and yum-yum. Thank me for the billions set aside for tea.

Other countries anathematized use of shangingis or oil guzzlers. Like crazy, we’ve authorized the purchase of even more so as to make our people happy. And mark my words. This boosts the name of our country internationally.

Vote for us next year. You’ll see even more wonders. We promised better life for all. Setting 19/-bn aside proves this.

Our country is a born again one. That’s why the prices of cold drink and booze are up. This aims at averting the danger of alcoholism, committing sin major one being battering your wives. Also we did this to curb obesity resulting from quaffing too much soda and other sugary stuffs.

Scientists have proved: tea is cure. We thus, by drinking much tea, cure our bodies and the pockets of our tea growers. And this will help the government to garner more tax as it enters Guinness book of wonders.

I know. Protestants will cheat you that we’ve banned soda. To the contrary, you’re allowed to drink during functions and fetes.

Regarding alcohol, rich guys and rulers will sip it on your behalf. You know what. Even if they become intoxicated, they commit no sins and if they do, God and government pardon them. For, verily, they’re the anointed and chosen ones.

Common bin-Adams will only be allowed to sip liquor during next year’s campaigns. Verily, nobody can commit any sin at this time of transfiguration when common paupers become anointed ones like their rulers.

One thing must be underscored. My budget bans small bribes during campaigns. If you intend to offer say a T-shirt, khanga or beer, remember. Instead, one must offer a suit, a crate of beer, a goat in lieu of barbeque and what have you. On the same footing, those prone of offering lift as takrima beware. You are not allowed to offer lift save on plane not shangingi.

To make sure this works, I’ve proposed there must be offered EPA, sorry, bailout money. This will bail the waishiwa out during the campaigns. And to make sure this succeeds, we are putting simple proscriptions in place in order to enable them grab this generously free money. Given we are a born-again country; we offer loans at the rate of two percent despite loaning the same at the rate of 11%.

Don’t worry about where and how the government is to seal the hole. Value Added Tax imposed on rent and other items will serve the purpose.

To make elections successful, we’re intending to increase Waishiwa’s salaries and emoluments thanks for their cooperation despite having a few hardheaded.

As for teachers, we’re going to build houses for them wherever the school is. This is a preferential treatment after one goon drubbed. Instead of buying toys for kids known as laboratory equipments, we’ve favoured teachers. And regarding sitting on stones in the class, this serves to put sense in their heads that education is not luxuries.

Some people are baffled how MPs would pass the budget they promised to foil! You know what? When such shrewdness surfaces, you just tell speaker Six to invoke section 90 (2) (b) of our potholed constitution to put sense in their little heads as it happened recently.

By the way, who could trust politicians that spend most of their time in Bongo doing private business instead of living in their constituencies? When you tell them the president can disband the parliament, they shiver like babies. Money talks.

When it comes to issuing threats, Bongoans are second to none. But when it comes to living up to their words, hell no. they end up hunching. And had they stayed put we’d have reduced their emoluments. Did they think we don’t know they’re more paid than and MPs on earth for doing nothing and sleeping in the house? To jog their minds, even in rich countries their colleagues do not have chauffeurs, guards, garden boys and what not. They don’t even get salutes from military chaps like you.

Let me wrap up by advising our brethren in cloaks. Do you know why we nullified tax exemptions you used to enjoy and other misuse like TRA to print money till the head prefect saved your skin? You’ve been accusing us of corruption little knowing without it nobody would become a politician.

Time is over, may I submit?

Give me rouse applause even if you are furious for being forced to pass the bill.
Source:Thisday June 24, 2009.

Hongera Kikwete kumteua Pita Noni


Japo watu wengi wametilia shaka uteuzi wa ‘mchapakazi’ Pita E M Noni kuwa mnene wa Benki ya Raslimali (TIB), nachukua fursa kuwapongeza wote wawili yaani mteuzi na mteule kwa kutuacha hoi. Si haba. Vitu vyao tumeviona na ujumbe umefika. Sasa mapambano dhidi ya ufisadi yameiva.

Kwanza , ikumbukwe. Noni, kwa wakubwa na maslahi yao , ni mchapakazi hakuna mfano duniani. Alisimamia vilivyo zoezi la EPA kiasi cha kutoacha mwanya wa makosa. Maana hata sanaa za kuwafikisha wahusika mahakamani, zinavyoonyesha, zitaishia kama watuhumiwa wa Richmond ambao hivi karibuni waziri wa bora utawala alisema hawawezi kuwajadili kwa vile sheria za kubuni haziruhusu. Kituko zaidi ni pale mama waziri mwenye jina la mnyama anayetisha alipoongopa eti Richmond haikupewa hata ndururu!

Pamoja na Noni kutajwa vibaya kwenye wizi wa EPA naye asikanushe, bado kwa wakubwa anafaa sana . Wengi walidhani angeingia kwenye kundi la akina Iman Mwankosya. Wamenoa. Haingii mtu mwenye connections.

Rais Jakaya Kikwete amekuwa bingwa wa kuteua watu wanaoamsha hisia na mjadala. Alianza na swahiba yake Edward Lowassa. Bahati mbaya hakudumu baada ya kuonyesha sura yake halisi. Kwa waliojua uhusiano wao na shutuma alizoziacha marehemu Mwalimu Julius Nyerere, walikuna vichwa kiasi cha kuota ukurutu walipotaarifiwa kuwa jamaa angekuwa waziri mkuu. Na kweli, mwanaharamu hata umuweke kwenye chupa atatoa kidole, hakuchelewa kufanya vitu vyake kiasi cha kutimka kabla ya wakati wake!

Uteuzi mwingine ulioamsha hisia na mijadala ni ule wa Joe Mgosi Makamba bingwa wa mipasho kuwa katibu mkubwa wa chama chake. Hadi sasa hakuna anayejua siri na sababu ya kumteua mtu tata kama huyu ambaye si haba amekijenga chama kwa njia ya ‘bomoa tutajenga kesho’. Amesababisha mijadala mingi ndani na nje ya chama. Hii ni kutokana na mipasho yake ambayo kuvuka mipaka hata kuwaudhi walengwa ni jambo la kawaida. Jamaa mwenye breki moja linapokuja suala la kupayuka.

Pia uteuzi wenye kusisimua ni ule wa aliyekuwa waziri wa miundo mbinu na mwanasheria mkuu wa zamani, Andrew Chenge. Akiwa ameboronga sana kwenye utawala kidhabu wa Benjamin Mkapa, hakuna aliyetarajia mtu yeyote mwenye uchungu na nchi, busara na uelewa wa mambo angemteua mtu kama huyu. Lakini alimteua na ukweli ukajidhihirisha baadaye alipogundulika kuwa ametutika mabilioni ya shilingi kisiwani Jersey aliyoyaita vijisenti. Hadi sasa ni ajabu ya maajabu kwa jamaa huyu kuendelea kuwa mheshimiwa huku akilalia mabilioni ya shilingi toka kwenye dili la rada.

Huo ndiyo uteuzi wa bingwa wa kuteua ambaye kwa msimamo hana tofauti na ruba aamuapo lake. Wengi, hadi leo, hawajui siri ya silka hii. Jamaa atakuchekea hata umuudhi vipi ilmradi mwisho wa siku lake linakuwa .

Uteuzi ambao unaweza kuingia kwenye kitabu cha maajabu cha Guiness ni ule wa Rweka Mka-ndala, kada maarufu wa CCM kuwa mkuu wa chuo kikuu cha Manzese. Madhira ya blanda hii wanayajua wengi hasa wanafunzi. Migomo, migongano juu ya mikopo ya elimu ndiyo usiseme.

Uteuzi mwingine ni ule wa Kingungi Ngombaru Mweru kuwa mshauri wa rais na mbunge. Jamaa kwa umri wake, kama tutamtendea haki, alipaswa kukaa nyumbani akacheze na wajukuu. Maana ukiangalia kwenye safu za uongozi nchini, hakuna rika lake hata mmoja.

Uteuzi mwingine uliowaacha wabongo vinywa wazi ni ule Basie Pesatatu Mramba kuwa kwenye baraza la mawaziri huku akiwa anajulikana alivyovurunda kwenye awamu ya tatu. Na hapa si Mramba peke yake, karibu wengi wa waliokuwa wakitiliwa shaka kwenye utawala uliopita aliwateua na anaendelea kufanya vitu vyake nao! Jamaa hatutamsahau hasa kwa nyodo zake za kutwambia tule majani ili anunua dege la rais na ten percent ifanikiwe.

Ukienda kwenye uteuzi mwingine kama vile wa mabalozi na majaji hata wakuu wa wilaya na mikoa unabaki kukuna kichwa na kuugulia. Wapo wanaompakazia Kikwete kuwa katika uteuzi wake huwa anaangalia mitandao, imani na wapi mtu atokako. Sie hatukubaliani na hili. Tunajua wazi kwa katiba yetu uoza na viraka, rais anaweza kumteua mkewe hata bibi yake kushika wadhifa wowote atakao kumpa iwe ni fadhila, takrima au vinginevyo.

Uteuzi mwingine ambao uliwaacha wabongo hoi ni ule wa mkurugenzi wa mawasiliano ikulu, Silva Rweye ambaye hakuna ubishi kuwa wakati wa kampeni aliitumia kalamu yake kumjenga Kikwete huku akiwabomoa wengine. Ingawa kufanya hivyo ni kinyume cha taaluma, si haba anapeta ukiachia mbali kuzua utata kutokana na majibu yake ambayo ukiyapima vizuri unahoji what’s up upstairs. Mfano aliwahi kusema kuwa kama serikali ingemtaka Daud Ballali ingemkamata. Ajabu wakati akipayuka hivyo, Ballali alikuwa akitakiwa atiwe mbaroni kujibu tuhuma za ujambazi wa EPA. Hata hivyo maneno ya Rweye yalikuja kuthibitika kuwa ya kweli pale Ballali alipopatikana na kufa kifo cha utata hadi kesho.

Jamaa huyu enzi zake kabla kalamu haijawa biashara mnadani aliweza kuitumia kumtoa fisadi yeyote roho kwa ugonjwa moyo. Wahenga walisema: mchawi mpe mtoto. Baada ya kuonjeshwa mahanjumati ya ukuu na ulaji wa dezo mbona aliweza kuyalamba manonihino yake bila hata chembe ya aibu! Kweli njaa ni ugonjwa mbaya sana hasa inapopanda kichwani.

Bado kuna uteuzi wa wazito kama Daudi. Matakataka, na vunja mbavu huu wa Noni ukiachia mbali ule wa Larensi Masha ambaye licha ya kuwa na uhusiano na mwanae kampuni yake iliguswa kwenye kashfa ya EPA.

Kinachofurahisha ni kwamba awamu ya kwanza ya utawala wa Kikwete umefanya yote haya ukijua changamoto yake kwa wapiga kura. Je kwenye ngwe lala salama tutaona maajabu gani? Ni suala la kukaa na kungoja. Muhimu ni kwa wapiga kura kufikiri mara mbili kama watataka kuepuka na kadhia na jinai kama hizi. Kimsingi dawa ya haya yote wanayo wapiga kura.



Tusisahau uteuzi wa Kikwete kwenye msimamo wa kumkingia kifua mtangulizi wake Benjamin Mkapa na hata harakati za sasa za kutaka kuchota pesa ya wanuka njaa wa Bongo kuipa Kiwira .

Utuzi wa mwisho wa Kikwete uliovutia wengi ni pale alipojiteua hivi karibuni kugombea urais kwa tiketi ya chama hata kabla ya muda kufika!

Tumalizie tulikoanzia. Kwa wale wanaoohoji na kushangaa Noni anakwenda TIB kwa sifa na kazi zipi wakumbuke. TIB ndipo zitakapowekwa pesa zilizorudishwa na majambazi wa EPA ambao Noni anawafahamu vizuri. Hakuna shaka huko nako atazishughulikia pesa hizi na kufanikisha uchaguzi mwakani. Nani hajui kuwa na siasa hasa vyeo vya juu ni investment tosha?

Hongera Kikwete kumteua Noni na wengine tuliowataja hapojuu. Si haba vitu vyako tunaviona na hakika kwa timu kama hii lazima tufike Misri kabla ya kuelekea Kanani.
Chanzo: Tanzania Daima, Juni 24, 2009.

Sherehesho la hotuba ya bajeti


NAMSHUKURU Subhana. Bajeti yangu inazidi kusifiwa na wote. Bajeti hii ya ukombozi na uchaguzi imevunja rekodi kujadiliwa na kupendwa. Jamaa wa majoho wameipenda kiasi cha kutaka niwe mkuu!

Ingawa wasiojua uchumi na kuchuma waliiponda eti kwa kuondoa misamaha ya kodi kwa asasi zisizo za kiserikali na mawese, hawakujua tunabana matumizi ili kupambana na mvurugiko wa uchumi duniani!

Kama waziri wa pesa na kuchuma, najipiga kifua nikisema ni bajeti ya karne. Uliwahi kusikia wapi bajeti yenye kuwatengea walevi bilioni 19 kwa ajili ya chai na vitafunwa? Haijawahi kutokea duniani isipokuwa Bongolala.

Kama tunalia vile! Bajeti iko wazi. Mkiilinganisha na bajeti za nchi nyingine mtaona mantiki. Kwa wenzenu hakuna hata senti moja ya maji ya kunywa wakati ninyi mna mabilioni ya chai na mahanjumati!

Wenzenu wamepiga marufuku mashangingi. Sisi tunataka kuwapa raha. Tunazidi kuyanunua kama hatuna akili nzuri na sifa ya taifa letu inakua.

Kama mtatupa kula tena mwakani, mtegemee bajeti yenye pesa hata ya manywaji kwa sana. Tuliwaahidi maisha bora kwa wote. Sasa mnataka nini iwapo mnakunywa chai ya mabilioni?

Nchi yenu imeokoka na kuslimu. Ndiyo maana tumepandisha bei za ulevi kuwaepushia adha ya kulewa na kutwangana makofi, kutenda maasi na kupayuka hovyo.

Pia tumepandisha bei ya vinywaji baridi ili kuepusha magonjwa ya unene na kisukari. Ndiyo sababu nuzuhu ya kutenga mabilioni kwa ajili ya chai.

Kwa kunywa chai sana , tutapakuza soko ambapo wakulima wa chai watanufaika na nchi kuingiza mapato mengi. Pia nchi itaingia kwenye kitabu cha maajabu cha Guinness kwa kuongoza kunywa chai duniani.

Pia wapingaji wasije wahadaa. Hatujapiga marufuku soda. Mnaruhusiwa kunywa soda wakati wa sherehe.

Na kwa upande wa kilevi, wenye pesa na madaraka watakuwa wanakunywa kwa niaba yenu. Wao hata wakilewa hawatendi dhambi na wakizitenda wanasamehewa. Ni wateule wa Mungu.

Pia wananchi wataruhusiwa kunywa bia wakati wa kampeni za uchafuzi mwakani. Kipindi hiki hawawezi kuhesabiwa dhambi, kwa kitambo, watageuka wateule wa Mungu.

Nisisitize. Takrima mbofu mbofu zinapigwa marufuku. Atakayetaka kutoa takrima atoe suti badala ya fulana na kofia.

Atoe mbuzi mzima baada ya vipande vya nyama choma. Ili kushushia, waheshimiwa watabanwa na sheria watoe kreti ya bia badala ya bia moja moja.

Kuhakikisha hili linafanikiwa, napendekeza serikali itoe pesa chini ya kanuni ya bailout. Hii itawezesha wakubwa kupata mishiko mikubwa kwa ajili ya kufanya mambo makubwa wakati wa kampeni.

Kuonyesha tulivyo mbele ya wengine, tumekopa pesa hii kwa riba ya asilimia 11. Kwa vile tuna huruma na kuna uchaguzi, tutawakopesha wazito kwa riba ya asilimia mbili. Mungu awape nini jamani? Majipu siyo? Kwa taarifa yenu, tumeweka masharti rahisi ya uchukuzi wa pesa hii.

Hakika mwakani mtaona na kuonja maajabu. Lifti za mashangingi zitapigwa marufuku. Na badala yake zitatolewa lifti za ndege ili umma uonje raha tunazokula kwa niaba yake.

Pia serikali itaongeza mshiko tokana na kodi ya ongezeko na thamani (VAT). Baada ya kuzinyakua nyumba za umma tumeona tutoze kodi ya ongezeko la thamani kwa wapangaji ili wawe na uchungu wajenge nyumba zao. Kila nyumba hata iwe ubavu wa dog ikipangishwa tunaitoza VAT ili kukuza uchumi.

Ndugu zangu walimu hili lisiwatishe. Tumepanga kuwajengea nyumba za ghorofa kila ilipo shule. Tumewapendelea baada ya kichaa mmoja kuwalamba bakora.

Badala ya kuwanunulia watoto matoi yaitwayo vifaa vya maabara, tumeona tuanze nanyi. Hata kama watoto wataendelea kukalia mawe msilaumu.

Hatukatai kuwanunulia madawati. Tunataka wakalie mawe ili wasikie uchungu wa kusoma. Maana wakikaa kwenye masofa watajisahau kwa raha na mineso.

Pia tumepanga kuongeza marupurupu na mishahara ya waheshimiwa wabunge kama watapitisha bajeti hii bila ubishi na kuchokoana.

Ingawa mmoja wao juzi katulaani mawaziri, tumemsamehe na tumeishapenyeza watu wetu kumshughulikia ili asiendelee kupayuka hovyo.

Pia wafahamu. Bajeti itapita watake wasitake. Najua wapo waliokamia kuikwamisha wasijue sisi tuna akili na mamlaka kuliko wao!

Chini ya katiba yetu ya ulaji, tutamwambia Bwana Kipaza sauti Six atumie Ibara ya 90 kifungu cha pili sehemu 'B' ya Katiba, nanukuu: mkuu atalazimika kuvunja Bunge iwapo litakataa kupitisha bajeti iliyowasilishwa na Serikali.

Kwa vile waheshimiwa wetu hamna ubavu na hamjiamini kwenye majimbo yenu kutokana na tabia yenu ya kupenda kukaa Bongo mkifanya biashara zenu, ukiondoa wabunge wa upingaji, hakuna mbunge wa genge letu atafanya fyoko zaidi ya kupiga kura ya ndiyo.

Na hii ndiyo sababu tunajiandalia bajeti kwa kuangalia maslahi yetu. Tunajua wazi kifungu cha 90 kipo kuwatia adabu na mkafyata mikia. Upo hapo?

Isitoshe wahishimiwa wa Bongo na wabongo kwa mkwara nawajua sana mtapiga mikwara yenu uchwara lakini serikali itakapochimba wake mtanywea.

Mkijifanya kujua jua hata haya marupurupu tunayowahonga tunayanyofoa tuone kama mtakula polisi.

Angalia bajeti inavyowapendelea. Nchi nyingine zimepiga vita mashangingi. Sisi tunazidi kuwapa kama hatuna akili nzuri.

Nyinyi, kama tutalinganisha na kipato cha taifa letu, mna mishahara na marupurupu makubwa kuliko hata maseneta wa kwa Obama.

Kule ukiwa seneta au mwakilishi hakuna cha dereva, mfagiaji, shamba boy wala mlinzi kama tulivyowafanyia. Wala huko wenzenu hawapigiwi saluti kama nyinyi. Sasa mnataka serikali yenu iwape nini?

Nimalizie kwa kutoa ushauri kwa ndugu zangu wa majoho.

Mnajua ni kwa nini tumeondoa misamaha ya kodi? Pamoja na wenzenu wachache kuitumia kujitajirisha kama jamaa wa TRA, mmechonga sana mkitusakizia kuwa tunaongoza kifisadi na kifisi na hatupambani na ufisadi. Unadhani bila ufisadi kuna mtu angependa siasa. Shauri yenu.

Muda hautoshi. Naomba kutoa hoja na kukaribisha maoni.

Makofi kutoka kwa wahishimiwa hata kama mmenuna kwa kulazimishwa kupitisha silaha za maangamizi kwa pesa ya walalahoi.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 24, 2009.

Wednesday 17 June 2009

Bongo's Death Lesson to Remaining Thieves-in-Chief.

Albert Bernard Omar Bongo Ondimba former Gabonese dictator was but a symbol of rot, greed, shame, myopia, hypocrisy and controversy.

"I'm glad to be honest with you. I know that you don't really rejoice from someone’s death".

One anonymous teacher was quoted as saying when the news of the death of the tyrant surfaced. This tells all regarding how a common man in the street views dictators who pretend to be loved whilst the opposite is true.

Though this can be wrongly seen as preaching recusancy and ridiculing the dead, the truth is, dictators have no good legacy but rot and hatred. How can people love their tormentors and exploiters?

Like Gnassigbe Eyadema ( Togo ) Joseph Desire Mobutu (DRC), Sani Abacha ( Nigeria ) and Felix Hauphet Boigny ( Ivory Coast ), Bongo did nothing for his country but to rob it and bring shame to it. To him Gabon was but his private estate he used he deemed fit. Some will say he built roads even schools and what not. But looking at how much he stole and how much people deserve, all end up being nothing comparably.

Like other living African dictators, Bongo did nary bother about tomorrow. To him, death was an illusion. And this is why even when he was dead, his stooges denied this reality!

He’s now confirmed dead. He died in Spain where he was receiving treatments. But what folly! The nation was told he was in Spain for just check up and holiday not sick!

Swahili sage has it that, he who hides illness death will shame him. Or he who hides fire smoke will shame him as it happened in the death of this despot that plundered his country for a good forty two years.

Bongo, a short put like North Korean Kim Jong Il, that used high heel shoes to conceal his dwarfism, goes down as an illiterate that was used by France to rob his country not to mention killing his opponent when it was impossible to purchase them.

Good news is African has been relieved of another dictator after Eyadema. This is a stalk warning for living dictators who think not about tomorrow. Yesterday we got rid of Eyadema; today Bongo, maybe, tomorrow God will intervene and claim another. Who knows? We can fear or being corrupted by them but not God.

After raping his country, Bongo had nothing left for him to be proud of but presidency he hijacked. Rooted on tribalism and nepotism, his rule was shaped by a few thieves from his family and tribe. His daughter Pascaline was his chief of staff just like Natasha Kainerugaba Museveni Karugira who’s her father’s private secretary, whilst his son Ali Ben-Bongo is minister for defence, like Muhoozi, that has much power in Ugandan military ranks .Bongo’s stooge, the leader of the senate; Rose Francine Rogombe is now constitutionally an interim president paving the way for Bongo Jr. to take his father’s throne! What does this mean? Shall Gabonese not watch Bongo will go on ruling them posthumously just like Eyadema!

Ben-Bongo is touted, like Faure Eyadema, to take the helm after transition period.

One thing I have learnt about dictators is: they like intermarriage and nepotism. Bongo was married to the daughter of Congo ’s dictator, Denis Sassou Ngweso, Edith Lucie who died in March. This is why I have singled Museveni’s family out to show this trait. Muhoozi is married to the daughter of his father’s stooge Sam Kutesa.

Till his death, Bongo was the longest African ruler that ruled for 42. Thereafter comes Muamar Gadaffi, Jose Eduardo Dos Santos, Paul Biya, Hosni Mubarak, Robert Mugabe, Denis Sassou Ngwesso, Yoweri Museveni, Isayaas Afowerki, Zine al-Abidine Ben Ali, Omar Bashir,Teodoro Obiang Nguema, Yahaya Jammeh and Mswati III.

Nonetheless, above potentates behave exactly the same as Bongo; they need to take a page from the book of reality. Life is subject to death and one day they’ll face it.

When Bongo died some wisecracks surfaced from the PM, Jean Eyeghe Ndong. He flatly denied the death of his boss when the news broke quoting Le Monde. Sick dictators and their cronies lack self pity. Within the same day of denial the same sheep like stooge admitted the tyrant was no more!

And this is the main character of all draconian regimes. They live in the state of denial when it comes to the state of the nation. Recently, there were many questions in Uganda with regard to why Ugandan Tyrant Museveni was recently using left hand to greet people whilst the right one is bandaged. As of now, no reasonable answer has ever been advanced with regard to this anomaly!

What’s more, reports regarding the cause of death of Bongo say it is cancer. But Gabonese public was told it is heat attack! Behind the curtains cronies are caught up in the eddy of protocol confusion not to mention manipulation. The tyrant left many things unmet importantly being the successor. Internet was cut off in order to avoid information reaching the people.

And this has always been the shape of Bongo’s thievish regime. Looking at the population of 1.4 million and the income Gabon gets from oil, one would think of having a rich population. But nay! All the moneys from oil, like Congo , Equatorial Guinea , Nigeria and Angola have gone to the ruling cabal of thieves and west countries that keep them in power as opposed to the will of a great unwashed.

This is the main reason Africa is always poor. Many African potentates offer their resources to west countries so as to illegally remain in power. And sadly, western countries do not want to address this anomaly. And this is why we’d stress that stealing from public coffers must be categorized as a crime against humanity.

More on Bongo, differently from other dangerously stinking tyrant, he was smart at one thing he goes down with. Being Mr. Moneybags, he’d buy loyalty from any bunch of self absorbed goons, power hooch and whiners at any cost. This is why he’s able to survive in power for over four decades without felling many opponents. So, buying loyalty does not end up home only. It goes as far as to the so-called international community. This is why Pakistan former dictator Parvez Musharaff was able to sit on nukes whilst the other one in North Korea is always given a heck.

Though he castrated his opponents, the magnitude and number is not as big as other dictators history knows.

In a nutshell, this is the fallen tyrant that was the longest African ruler.

Is It Tax Exemptions or Rip -Off?

IT appalls to call robber by consent tax exemption or whatever sexed-up name and this puts the power that be in the till. Reports that a begging nation like ours lost 587bn/- thanks to tax exemption in a just ten month period are shockingly disturbing.

The Tanzania Revenue Authority (TRA) Board Chair, Dr Marcellina Chijoriga, told the Parliamentary Committee for Finance and Economy recently that the exemptions were made between July 2008 to April 2009 – cool 18.38bn/- of the total amount was given away in Zanzibar.

In this rip-off, as per Chijoriga, Tanzania Investment Centre (TIC) scored high at 83% or 362.6bn/-. One would wonder. Is this investment or rip-off?

Others that befriended include state-owned organisations (5.97bn/-), government institutions (8.8bn/-), religious and other non-governmental organisations (34.7bn/-), while donor-funded projects got exemptions amounting to 21.1bn/-.

Others that gnawed 154.2bn/- in exemptions, mainly by means of duty-free shops, special exemptions and zero rated exemptions! “The exemptions on the Mainland were equal to 30 per cent of the total 1.45tr/- collected by the Customs Department for those ten months only,” Chijoriga keened.

Our budget depends on donors at the tune of over 30%. At the same time, we award almost the same amount to swindlers! What a curse!

I can’t just imagine. How many schools or hospitals this gargantuan amount would build. Help me. How many students this amount would see through in colleges? How many kilometers of our dilapidated roads this amount would build? I don’t know. People in a forgotten region like Kigoma would understand and accept this!

What adds up even more is when we’re offering tax holidays and exemptions to some swindlers, our paupers are sinking in destitution as our rulers crushingly go cup in hand from one rich country to another. Gravely, we still promise them better life! Where do we get this grit for God’s sake?

Whilst this sacrilegious opprobrium is unleashed, a few thieves in high offices make a kill so as to become tycoons as a great many unwashed suffer even more!

The other day I averred that Bongo is richer than other wrongly think. What amiss is but vision and trustworthy, and of course, sane minds in the upper echelons of power.

To grasp what I mean, look at those we offer tax exemption. They blind us by giving our pauper leftover they call misaada. The other day I heard that one lady that heads a certain suspicious church offered over 20,000,000/- to women in Morogoro.

Unfortunately though, nobody asked how she printed such moneys! Isn’t the same money we offered to her briefcase church from which she gets leftover to offer to our women?

Those who know how corruption operates can show you some chaps that man and own religious outfits they use to get tax exemption they extend to business people who pay them after getting their items into the country without paying any tax. And this is why NGOs and religious outfits are mushrooming. It is a lucrative business.

To know what I mean, look at the paupers of yesterday who become tycoons overnight after establishing their churches or whatever outfits. That’s why the number of self-ordained religious leaders is surging every day. Ni ulaji wa dezo.

Are they frying a fish with its own oil? Who knows and who cares if at all corruption is becoming an order of the day?

Somebody has to say something. I condemn this monkey business. No way one can comfortably sit idly by as our money is being swindled.

We always sing good governance. Is there any good governance with all this daylight robbery? While this heinous crime is committed, we still have guts to overtax our paupers! Look at stuffs like VAT, Income tax, payroll tax, stump duty, sales tax, hidden tax and what not. Isn’t this stealing from them really?

We still go thumb-up assuring our paupers that we’ll deliver! Why should we make tax evasion a crime but not tax exemption? Is it because those that exempt other are the high and mighty?

Let’s face it point blank. What is said to be tax exemption sounds as rip-off to me. This way, our country is doomed and shall it remain as this, verily we’re but finished. And this is true not preaching recusancy.
Source: Thisday June 17, 2009.

Kikwete, Musa hadi Farao na Yusufu!

MCHUNGAJI Lawi Mwankuge wa kanisa la Moravian Ruaha Kidatu, Morogoro alikaririwa na TBC1 hivi karibuni akihoji; “yuko wapi Yusufu wetu wa kuwasaidia viongozi wetu”;

Hii ni baada ya kutangazwa bajeti iliyoua misamaha ya kodi kwa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO).

Kwa wanaokumbuka kauli mbinu ya rais Jakaya Kikwete (wakati ule Musa) ya kuwatoa watu Misri (kwa Benjamin Mkapa) kwenda Kanani ( ambako sasa kumegeuka kubaya zaidi ya alipowakuta), watakubaliana nami: kwa sasa, Kikwete hana sifa tena ya kuitwa Musa kama alivyoingia. Mchungaji ametusaidia. Amemlinganisha na Farao.

Kwanza hajatekeleza ahadi hata moja ukiachia mbali kuzidi kuvuruga. Kwa mfano, Kikwete aliahidi kupambana na ufisadi kama njia moja wapo ya kuokoa pesa ambayo ingetumika kuwaletea watu maisha bora chini ya kauli yake mbinu nyingine ya maisha bora kwa wote. Bahati mbaya sana , maisha bora kwa wote yamegeuka kuwa maisha bora kwa wote waliomzunguka Kikwete na si watanzania kama walivyohadaiwa. Mafisadi wanatetewa hata na mawaziri wake bila ya kuogopa wala bosi wao kuwakemea!

Pili, Kikwete aliahidi kuwa na nidhamu ya matumizi ya pesa ya serikali. Kwa taarifa ya ripoti ya mdhibiti mkuu wa fedha za serikali (CAG), tangu aingie madarakani, karibu kila mwaka, serikali yake inapata alama chafu katika suala hili. Amekuwa akitumia pesa nyingi kusafiri nje ukiachia mbali kuwaachia watuhumiwa wa wizi wa mabilioni yanayosemekana kutumika kumuingiza madarakani.

Tatu ameunda serikali kubwa sana kuliko ya mtangulizi wake ukiachia mbali kuwavumilia na kuwateua watu wanaotia shaka. Mfano wa karibuni ni kumteua Peter Mayunga Noni kuwa mkuu wa Benki ya raslimali (TIB) huku Noni akiwa ametajwa wazi wazi kwenye wizi wa pesa toka benki kuu kwenye mfuko wa madeni ya nje (EPA). Rejea kutajwa na mwanasheria Bhyidinka Michael Sanze aliyesema alishuhudia majadiliano ya wizi huu. Bahati mbaya si Noni, wala Mkapa au watajwa wengine wamekanusha madai ya mwanasheria huyu.

Rejea kuendelea kuwanyamazia na kuwabakiza kazini mwanasheria mkuu wa serikali na mkurugenzi wa Takukuru walioguswa moja kwa moja kwenye kashfa ya Richmond .

Ziko wapi nyumba za umma zilizotwaliwa na Mkapa na mawaziri wake na Kikwete akiwamo? Iko wapi vita ya kupambana na wauza mihadarati na majambazi? Ajabu, Kikwete alijitutumua kuwakamata majambazi wakubwa. Lakini baada ya kukuta kuwa kumbe wengi ni wafadhili wa CCM zoezi hili lilikufa kifo cha mende huku Kikwete akiendelea kuuaminisha umma kuwa ataukomboa. Kwa mdomo ameukomboa sana . Kwa matendo ameupeleka hata zaidi ya Misri. Kama tutaangalia rekodi ya Kikwete, bila shaka, tutagundua kuwa umma ulioahidiwa kwenda Kanani umeishakatiza Misri. Karibuni utaingia Sudan !

Ajabu ya maajabu, Kikwete aliwahi kukiri kuwa anayo orodha ya majambazi na wauza mihadarati! Kama kweli anayo kwanini asiwashughulikie? Ana maslahi gani na biashara hii?

Ukimlinganisha na Mkapa aliyemlinganisha na Farao hadi akatunga kauli mbiu ya kuwapeleka watu Kanani, Kikwete ni sawa na kichuguu mbele yam lima .

Tutatoa sababu. Katika muhula wake wa kwanza, Mkapa alijitahidi kubana matumizi ya pesa ya serikali huku akiubana mfumko wa bei. Pia aliziba mianya ya ukwepaji kodi kiasi cha kutunisha mapato ya taifa yatokanayo na kodi. Kwa ufupi alionyesha dira ya taifa ingawa baada ya kulewa madaraka huku akivutiwa na ushawishi wa mkewe mjasirimali, katika muhula wa pili, Mkapa alibomoa kila jema alilokuwa amelijenga. Na laiti asingefanya hivi, angeweza kuvaa hata viatu vya mtu aliyemtengeneza, Mwalimu Julius Nyerere.

Kwani Mkapa alijiingiza kwenye unyakuzi machimbo ya makaa ya mawe ya Kiwira yakiwa ni kongwa atakayokwenda nayo kaburini ukiachia mbali shutuma lukuki kumuelekea mkewe aliyeanza biashara kwa kuanzisha NGO ya Fursa sawa kwa wote ingawa wote walikuwa wote anaowajua yeye na mumewe. Hapa hujaongelea uwekezaji wa kijambazi ulioongozwa na cha juu.

Mkapa atakumbukwa japo kwa ubaya kwa kuigawa benki yetu ya Biashara (NBC) kuihujumu Tanesco kwa kuruhusu shemeji zake waiingize kampuni ya kikaburu ya Net Group Solution ambayo kimsingi iliiua na kuthibitisha ilivyokuwa Net Problems.

Pigo la mwisho la Mkapa ilikuwa ni kulewa madaraka na kuwa na kiburi. Alianza kuwashambulia waliomkosoa (akina Yusufu). Alifikia hatua hata ya kuwafutia wengine uraia na kuwazodoa hadharani kuwa nao walikuwa wachafu kama yeye. Kikwete anatumia mbinu ya kujifanya hasikii. Yote hii ni kibri na ukosefu wa utawala bora.

Ya Mkapa sasa ni historia. Anaishi kwa kulindwa na rais Kikwete. Kitendo hiki kimewashangaza na kuwachukiza wengi. Wazungu husema: show me your friends I will tell you who you are. Nionyeshe marafiki zako nitakwambia wewe ni nani.

Hapa ndipo, kwa mara nyingine u-Musa wa Kikwete unayeyuka kiasi cha mchungaji Mwankuge kumlinganisha na Farao.

Farao aliwatesa waisraeli sawa na Kikwete anavyofanya. Kwani aliwatwisha mzigo wa kunyonywa na kudhalilishwa. Wizi wa EPA, Richmond , Dowan, IPTL, TICT, CIS, NSSF, ANBEN, Tanpower, Fosnik na mwingine mwingi hauna tofauti na matendo ya Faroa.

Kwanini tuendako maneno ya Mwankuge yanaweza kubeba ukweli usiopingika? Kikwete haonyeshi kujifunza wala kurekebika hata abebwe namna gani. Jiulize. Sasa ni mwaka wa tano tangu aingie madarakani. Ameishatimiza ahadi gani? Hata aliposhauriwa kuachana na uwaziri wa mambo ya nchi za nje yaani kupoteza muda mwingi na pesa ughaibuni, hakuacha. Hivi karibuni jarida la kimataifa linaloheshimika la The Economist lilimtolea uvivu na kusema: ziara zake zinalihujumu taifa. Kama kawaida yake, hakujibu wala kujali.

Ameendelea kumvumilia malkia wake kuendesha biashara ya NGO sawa na ya mke wa mtangulizi wake. Ingawa Mkapa anachukiwa kwa aibu na uroho alioonyesha kwa kukwapua mali ya umma, ukiwaweka kwenye mizani na Kikwete, Mkapa anaweza kuwa bora. Maana kwenye muhula wa kwanza angalau alionyesha nini maana ya utawala.

Wachambuzi wengi wa mambo wanakubaliana kuwa kama Kikwete atachaguliwa kwa muhula wa pili na akaendelea kama alivyo sasa, ataiacha nchi pabaya kiasi cha kuweza kuzusha hata vurugu na amani tunayojivunia ikatoweka. Hapawezi kuwa na amani ya kweli bila haki.

Akina Yusufu tumesema hadi makoo yamekauka. Mwenzetu ana kinywa kipana lakini hana masikio kabisa. Anajua kusema si kutenda. Yeye ni mtu wa kucheza na hadhira jukwaani lakini mwoga wa kuingia kwenye medani. Huu ndiyo watani wake huuita usanii. Tatizo si kuwepo Yusufu bali Yusufu wapi awasikilize.

Kama tutamtendea haki Kikwete, si vibaya kumlinganisha na Farao. Hata wakati Farao anaweza kuwa na nafuu. Kwa sababu hakuwaahidi waisraeli ukombozi wowote.
Chanzo : Tanzania Daima Juni 17, 2009.

Bajeti ya Mheshimiwa Mpayukaji Waziri Wa Pesa


HUWEZI kuamini. Jana niliota nikiwa Waziri wa Pesa, Mstaafu Mkulu! Baada ya kula magimbi na mbwanda, kama mlalahoi, nilijibwaga kitandani jirani na Bi Mkubwa.

Tulidurusu tuliyodurusu na kila mmoja akageukia upande wake na kuuchapa usingizi. Mara naanza kuota nikitoka ofisini kwangu Magogoni naelekea Uwanja wa Ndege wa Mwalimu kupanda pipa kuelekea Idodomya kuwadodomya na kuwabamiza mkenge walevi.

Nimekula suti ya bei mbaya niliyoinunua Paris na tai ya udhulungi. Nimeulamba kweli kweli kiasi cha kumuacha Bi. Mkubwa akiugulia, huenda huko nitapata dogodogo wa kuniliwaza baada ya kukausha koo nikiwaweka sawa walevi.

Kufika airport natoa maelezo kwa dereva na wasaidizi wangu na kujitoma VIP lounge tayari kupaa. Haichukui muda wanakuja wasaidizi wangu kuniashiria niingie kwenye lango la kuelekea kwenye pipa.

Ndani ya pipa nawakuta wasichana wenye kutabasamu kila saa. Wananikaribisha na pipa linaanza kutimua kuelekea Kipawa tayari kuelekea Dom. Baada ya kutoka uwanjani naelekea kwenye hoteli ya bei mbaya na kubadili suti tayari kuingia bungeni.

Naingia bungeni nikiwa na mkoba wangu wa maangamizi ya pesa ya umma (MPU). Wapiga picha wa vyombo mbali mbali vya habari wananipiga picha kama hawana akili nzuri.

Kwa mikogo na bashasha, natokomea ukumbini na kwenda moja moja kuanza kusoma bajeti ya serikali yangu ombaomba.

Naanza. Mwishiwa Spika, waishiwa wabunge, mawaziri na wananchi kwa ujumla. Watukutu, ifuatayo ni bajeti ya mwaka wa fedha 2009/10.

Utangulizi

Kwanza niseme wazi, hii ni bajeti ya ukombozi wa mlevi na uchaguzi ambayo haijawahi kutungwa katika historia ya taifa hili.

Mwishiwa Spika

Bajeti ya mwaka huu imeongezwa kwa asilimia 365 kutoka bilioni nonihino hadi zilioni moja na ukwaju. Nakohoa na kuendelea. Shughuli za utawala zitakula asilimia 88 na za maendeleo tisa, huku mengineyo yakitumia idadi iliyobaki.

Nchi yetu imeendelea sana hivyo tumepunguza shughuli za maendeleo na kuongeza utawala ili kuwa na utawala bora.

Pia, tumelenga kumkomboa mlevi hasa katika kipindi hiki cha kuvurugika kwa uchumi wa dunia. Ingawa awali nilichemsha nikasema mtikisiko hautalikumba taifa la walevi, niligundua: wataalamu wangu walitafsiri vibaya Kiingereza.

Nilichomaanisha, taifa lingetikisika sana. Hii ndiyo sababu ya kila tatizo mnaloona nchini. Wanaosingizia ufisadi msiwasikilize. Hawajui mambo ya uchumi na kuchuma.

Mwishiwa Spika

Kama nilivyosema hapo awali, bajeti hii ni ya ukombozi wa walevi. Katika kuiandaa tumeangalia mambo mbalimbali na kuyapa vipaumbele.

Mwishiwa Spika

Mwakani tuna uchaguzi. Tumejitahidi kulegeza masharti kwa wananchi ili waweze kutupa kura za kuula. Kufanya hivyo, tumeondoa kodi ya vitambi na vitimbi.

Pia tumepandisha bei za vileo ili kuwaepushia walevi kulewa na kupiga wake zao ukiachia mbali kusahau kupiga kura.

Mwishiwa Spika

Wananchi wa jimbo langu, la mkuu, waziri wa pesa wa zamani na mengine ya marafiki zangu yatanufaika sana na bajeti hii. Tutatengeneza barabara ziendazo na zitokazo huko kuepusha mashangingi yetu kuharibika.

Pia, tutazijenga na kuwa na njia tano kuepusha usumbufu na upotevu wa muda wa waheshimiwa wanapokwenda huko kwa ajili ya ama sherehe za ndoa, ubarikio ama graduation. Pia itaepusha kuvunjika migongo wanaposafiri kuelekea huko.

Pia, tutaagiza mashangingi mengi hata kwa ajili ya nyumba ndogo zetu hata kama wenzetu Kenya kwa uzembe wao wameyapiga marufuku. Hatuna haja ya kuogopa kutumia mashangingi. Tunatumia pesa ya umma haiumi.

Mwishiwa Spika

Kwa majimbo ambayo barabara zake hazitaonekana kwenye bajeti wavumilie hadi watakapotoa mawaziri wa pesa na wakuu. Pia, wajue hii si adhabu. Tumeacha kuzitengea pesa kwa sababu ya kuepuka kuongezeka kwa machinga jijini.

Barabara zikiwa nzuri, watu watakimbia vijijini kiasi cha kuathiri sekta ya kilimo ambayo ni tako la taifa. Hivyo bila tako taifa litashindwa kukaa hata wakubwa hawataweza kukaa na kufaidi viyoyozi. Tutapanua kilimo vipi? Usitake kujua.

Mwishiwa Spika

Pia, tumepungaza bajeti ya elimu hasa ya juu. Hii ni kutokana na ukweli kuwa walevi wamesoma sana kiasi cha kuwa na wabunge wenye PhD hata kama ni za kuchongwa.

Hivyo hatuhitaji wasomi tena. Hivyo pesa ambayo ingepotea bure huko itaenda kwenye kununua mashangingi mapya na kukarabati ikulu na ofisi za mawaziri.

Mwishiwa Spika

Walevi watafaidika na bajeti hii. Japo wengi walinilaumu kwa kufungua tawi la DESI jimboni mwangu, nilitaka kupata uzoefu jinsi ya kueneza utajiri wa wote ili kutimiza ile ahadi ya maisha bora kwa wote aliyotoa mkuu.

Mwishiwa Spika

Kutokana na sababu za kiusalama, sitataja kiwango cha pesa zilizotengwa kwa baadhi ya taasisi nyeti kama ikulu, ulinzi, huduma za bunge, viwanda na uwekezaji na nyingine zinazoangukia kwenye category hii.

In fwact, I mean. Calculations za bajeti hii zime-base kwenye projection na trajectory ya uchumi wa kisasa wa karne ya sayansi na tekelinalokuijia.

Mwishiwa Spika

Kwa mfano ukitaja bajeti ya viwanda na uwekezaji utawafukuza wawekezaji. Hivyo mwishiwa spika, nisisitize; bajeti hii itamkomboa mlevi kutokana na kupanda kwa asilimia 365.

Mwishiwa Spika

Nitaje vyanzo vya mapato ya serikali.

Kwanza ni kodi. Hii italiingizia taifa pesa sawa na asilimia sitini. Hivyo asilimia arobaini iliyobaki tutakopa na kuomba wakoloni, sorry, wafadhili. Na hapa nisisitize. Walevi wakiona tunakwenda sana ng’ambo waelewe tunakwenda kutafuta pesa ya kujazia kwenye bajeti.

Mitumba itatozwa kodi kubwa isipokuwa ya magari ya kifahari. Hatuwezi kuendekeza mitumba hata kwenye miili hata kama vichwani tu mitumba.

Mwaka huu safari za mawaziri mikoani kuelimisha umma juu ya bajeti hazitakuwapo. Badala yake tutakwenda kuanza kampeni kabla ya tume kutangaza. Pia tutakwenda majuu kuvutia wawekezaji kama waziri wa zamani Niziro Kadamage.

Mwishiwa Spika

Bajeti ya mwaka huu ni ya uwajibikaji na kupambana na ufisadi na wizi wa kura na fadhila. Mwaka unaokwisha wa pesa tulivunja rekodi ya kusamehe kodi. Mwaka huu nitakufa na mtu.

Hapatakuwa na cha EPA, Tax exemption and tax profligacy hata kama inahitajika pesa ya takrima kwenye uchaguzi ujao. Kila mtu ajijue.

Nimetenga asilimia 13 ya bajeti kwa ajili ya kuhakikisha pesa ya bajeti haiibiwi kama ilivyokuwa huko nyuma. Kabla ya kuendelea nasikia miguno na mpuuzi mmoja anasema. “Mbona wizi ndani ya wizi!”

Nikiwa nimefura, nilipayuka kwa hasira nasema. “Mtake msitake mwaka huu mtafunga mikanda ili kunogesha mambo.” Nikiwa naendelea kujiotea si Bi Mkubwa aliniamsha kwa kipepsi akidai nawaota hawara zangu tena kitandani kwake!

Alisema: “Mume wangu, yaani umefikia mahali kuwaambia hawara zako wafungue mikanda ili mambo yanoge mbele yangu!” Najibu. “Mbona nilikuwa naota nikiwa waziri wa pesa nikisoma bajeti bungeni mke wangu.”

Hakieleweki kitu. Mara tunaanza kupigana tukigombea bajeti ya ndoto na maangamizi ya pesa ya umma. Tulirejea kwenye mazonge sawa na mlalahoi yoyote ambaye kwake bajeti ni kilio ili wakubwa watanue.

Na hii ndiyo tuliyomaanisha tuliposema maisha bora kwa wote. Wote sisi, si wote wote. Mwenye akili na aelewe na mwenye masikio na asikie, ili tusianze kulaumiana kuwa hatukutekeleza ahadi zetu.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 17, 2009.

Sunday 14 June 2009

Is Hellen Zelle a racist really?


When the opposition leader in South Africa , Helen Zelle recently called President Jacob Zuma a womanizer that’s ready to put the lives of his three wives in danger’s path, she was branded as a racist.

Zille was quoted as thus, "Zuma is a self-confessed womaniser with deeply sexist views, who put all his wives at risk by having unprotected sex with an HIV-positive woman."

Is there any grain of racism or lie in these remarks? Isn’t Zuma a womanizer that slept with a HIV-Positive girl, (the age of his daughter, Gugulethu), without thinking about his three wives? What’s wrong with telling what happened as it truly did? Is it because Zille is the opposition leader and much more white? When it reaches the point at which people look at who is saying instead of what is said, such people are doomed.

Now Zuma is now slumped in to the front seat steering the nation. Will he avert his history and the challenges it poses? He came to power under the pseudo banner of populism as many hopes were pinned on him. Will he deliver? Will he escape the test of time? Soon, just soon, people will start querying after a true Zuma surfaces.

I’m anxiously waiting to hear what Zuma has to say with regards to Jonathan Shapiro’s recent cartoon depicting him with a shower hanging over his head signifying how he showered after having unprotected with a HIV-positive girl. Will he quell the media for reminding him who he actually is or bite the bullet?

Though Zuma temporarily languishes and banks on being exonerated by the politicized court, his being the devil incarnate will never do away without going through proper legal process. His name will remain mud till he faces the true music. And, indeed, his government will remain in the till until he faces the reality by doing the right thing. All allegations will remain fresh till time they are duly dealt with. Failure to this is just the matter of time. History will slink and tell anyway.

And mark my words. The other day in future, Zuma will see a cartoon showing him with an Indian con man surrounded by weapons, bundles of bills and coins as the moneys change hands. Soon people will ask for him to dance Letu umushini wami; and, as president, he won’t be able to come forth to dance and cheer them up. Hither is where the hell will break loose for him. This is the moment a true Zuma will come to the agora to be counted. In a nutshell, Zuma’s stinky history makes him sit on the ticking-time bomb.

Employing pretexts has become an in-thing for African tarnished rulers. Another monkey business can be found in what transpired with regard to the former rule of Zambia . When the London High Court found former Zambia president guilty of fraud of over $ 58,000,000 (and of course, stealing and squandering) public money, Fredrick Chiluba labeled it racist and trash! But it is true. Chiluba misappropriated public moneys. His wife was recently jailed thanks to the same malady. For how long will our rulers lack about without coming of age?

What’s more, it came to light that some of Chiluba’s 21 associates are not Zambians! If Chiluba were not racist he accuses British of, why did he spend Zambians’ money with non-Zambians?

When it comes to racism, African corrupt rulers are second to none. In essence, racism is corruption. Our rulers prefer doing dirty business with foreigners especially Indians in East Africa and South particularly simply because they can easily dispose them when things get worse and make off with loots and secrets. Refer to Goldenberg and Anglo-Leasing in Kenya and EPA in Tanzania . Behind these scams are Indian con men and rulers!

It’s reported recently that Zambian High Court has delayed ruling against Chiluba. When it was announced that the authorities decided to bring Chiluba to book, many applauded it. But looking at this knuckle-dragging, one can smell a rat so as to call the whole exercise side show. And indeed, this is the test to the new president Rupiah Banda.

If Chiluba was able to steal and spend a million bucks (as it was recently found) in a boutique in Switzerland , what can you call this?

The truth is the same in Malawi where the former tyrant faces same charges. In Tanzania , the current president, Jakaya Kikwete stated publicly: he won’t prosecute the former thief, Benjamin Mkapa simply because he impliedly is acting exactly the same as his predecessor. In Kenya Daniel arap Moi is in bed with Mwai Kibaki. And chances are. He’ll never face the music. How will he if at all sometimes Moi seems better than Kibaki if one compares the time they spent in office?

Back to racism or colonialism as the pretext to get off hook, it’s become a norm for Africa thieves. When they’re cornered, they take camouflage in race, colonialism and other hogwash. But when they go cup in hand begging to west and stashing money to offshore banks, it is not as a big sin as racism!

In a simple definition racism means preferring one race over another. A great many African honchos are at home when they go for medication and leave to Europe . Even their kids are studying there. If they’re true patriots why should they send their kids to west whilst they are many universities in Africa ? They don’t want; just because they’ve already ruined those varsities and their kids being there would tarnish their image. Thanks to how they squander public tax. Also this is racism if it be clinically examined.

When Sudan dictator, Omar Bashir was indicted by the ICC in The Hague , he rushed out to dismiss the move as mere neo-colonialism. But when he’s butchering people in Darfur and introducing Islamic Sharia to non-Muslim Southern Sudan it’s neither colonialism nor barbarism! It’s important to know. Most of African rulers are black colonialists that superimposed themselves over the people they exploit and torture.
How can they stop short of being if at all they’re in power thanks to rigged and bribed elections? Shame on them! Shamelessly, they still get the grit to accuse others of the same things they do through and through! When cornered, the vulture cries wolf.

I recently read the story about Rwandan government's fury after BBC aired the program that allowed free expression. The stick this autocratic regime used to intimidate BBC is BBC was denying the occurrence of genocide.

No sane person can dispute that genocide took place. What many dispute is who perpetrated it and the number of the victims. Rwanda ’s furious just because some of the contributors queried the bodies that were found floating in Lake Nyanza . They were said to be of those that RPF killed. Some even went a mile ahead mentioning current top brass that perpetrated crimes against humanity and genocide.

One fact is still unchecked. If all people who are said to have been killed during genocide were accounted for, what of those that RPF killed? Does it mean, such long time war did not claim any lives?

The fallacy of our rulers is thinking: we’re all fools they can foolishly and easily deceive and take for a ride. We know very well. Most of them are but colonial serfs serving their colonial masters in the west where they hide and spend their loots and dues for vending our souls and bodies.

Off the cuffs I’d like to congratulate Malawi ’s president Bingu wa Mutharika for his convincing re-election after a longtime tussle with his predecessor. One thing is obvious. Mutharika has made a precedent in that one can abandon the ruling party and yet rule the country without any obstacles. Now Mutharika has the edge to nicely and legally bring Bakili Muluzi to book. Though Muluzi showed a good gesture at Mutharika’s inauguration, this should not blind Mutharika.

Many African countries are in shambles thanks to being exploited by ruling parties. Many uncorrupted members fear to abandon them for fear of being left out of politics which means opulence in Africa.

Going back to Zuma, is it racism really or naked truth?
Source: The Executive Magazine June 10, 2009.

Bwana waziri, no more money to Kiwira please!


THIS is the fourth time I'm writing to remind you of your promise to divulge enshrouded owners of Kiwira Coal Mine. Likewise, this is the fourth time you promised and defaulted, in that you didn’t live up to your promises.

What has forced me to write for the fourth time is the report I read recently quoting you as saying: Your government will sink more money into Kiwira in order to produce much needed electricity! The idea is cool save that the means is spooky, so to speak.

Regarding this predatory behaviour, I’ve a few questions to ask you good minister. Is it true that Kiwira Coal and Power Company (KCPC) is a subsidiary company of Tan power (Mkapa’s family company) that is said to have been illegally formed by Mkapa and his family when he was the sitting president that acquired Kiwira illegally?

Why don’t you clarify the issue of ownership that you’ve been subjecting to ping pong? Don't you see, before doing so, spending money on such dubious things is an insult to our taxpayers? What have you to lose for telling the truth that sets free?

Can’t this be taken circumstantially as evidence that the power that be wrongly thinks our people are zombies it intends to rob? How far has it dealt with the EPA profligacy, Kagoda in the main?

Importantly, let me state pointedly: Tell the people the true owners of Kiwira before throwing their money away to monkey business. It appalls to note that the project that was robbed at a throw away price of 70m/- in lieu of actual value of 4trn/- can still ’convince’ the government to cough more money!

If anything, there must be something fishy because I cannot comprehend the rationale of this theft by consent!
Somebody steals your car then you pay for its repair after wrecking it! No. Tell it to the birds. Even a hen cannot do this.

Should this machination-cum- sabotage succeed; believe me, there must be some bigwigs of the current regime with a share in this loot.

And you know what? There are many thieves in high offices and many innocent guys behind bars.
You said: Our begging government owns only 30% of Kiwira? Well done. How come it is taking the burden of rejigging the project whilst it has minority shares compared to 70% owned by Tanpower?

Legally speaking, the shareholder with majority shares is duty bound to see to it that if anything happens, he carries the burden the same rights he enjoys when it comes to manning the project and making decisions.

Good minister sir, you’re quoted as saying, ’’Let bygone be bygone. The aim is to get electricity.’’ Once again, the idea is cool to hear but stinky to subscribe to. How come somebody stole our utility and we still award him more money?

Is Kiwira the only source in the first place? You must be kidding waziri. How come wananchi’s tax money is being offered to the guys that stole their utility so as to produce electricity and hike it back to the same victims?
Looking at your report, it seems the decision to steal, sorry, burn our money has already been reached at.

You said, ’’We’ll revamp the project so that it becomes beneficial to the nation in general.’’ Bwana Waziri, why does the nation always mean a few thieves in power?
Had the ’nation’ been considered, you’d have already brought thieves behind Kiwira to book.

Why should the Wabongo be offended so as to feel the pinch and act? Are they waiting to be sold alive to act? When I look at Kagoda, Richmond , IPTL thefts among others, and now this Kiwira, I feel like committing suicide.

It is in Bongo only where a business man can be alleged to have broken public coffers but instead of apprehending him, a waziri stands up and defends him even by intimidating whistle-blowers!

It is only in Bongo where a minister can be convicted of wrong doing so as to be expelled from office but the same goes on being a member of parliament!

What is said to be saving Kiwira sounds like a pretext of soliciting money. Who knows? The general elections are around the corner. And mark my words; in Bongo, public money is stolen when elections close in.

In a nutshell, no dime should be given to Kiwira before divulging who owns it and how he acquired it. This time I'm sure President Jack will never put his power in danger's path. Enough is enough..

So an important thing to do Bwana waziri is to neuter and castrate the thieves behind the Kiwira crime or retake Kiwira instead of breaking public coffers even more.
If honourable MPs are going to consent to this theft as opposed to wananchi’s will, they should count them out when it comes to next elections.

True, what’s going on is syndicated theft in the name of national development. What is referred to as a nation is nothing but a nation of a few crooks in power but not ours.
Shame on them!
Source: Thisday June 10, 2009.

Kirini mmeshindwa tena vibaya

Ni miaka minne tangu tujitutumue na kujidai. Mbele ya kadamnasi na mataifa tulitembea vifua mbele tusijue tutakuja zamisha vichwa michangani! Kulikoni? Si unakumbuka tulijidanganya: tumeandika historia tusijue tumesaini hati ya kifo! Hatukujua. Ubuguyu-ubuguyu wote kumbe kibafute;mwe!

Bado sijasahau kibapara mie nilivyomnunulia mke wangu kikuba kusherehekea ushindi wa kuondokana na mzee wa majisifu kwa kila aina ya mbwembwe na hoi hoi! Hadi leo nashangaa tabasuri tuliyotumia kuita mafamba tukidhani tunayafukuza! Sijsahau muda niliopoteza kuhudhuria vigwena vyao watulao tukilalamika wasisikie.

Walishapata walichotaka wana shida gani? Japo tunajikaza na nyonde nyonde yetu ambapo kidhabu mmoja habithi na marhuni alitukoga eti twapaa wakati twazama tena kwa kasi. Tukubali mbele yetu kuna vita japo tumeishaula wa chuya Mungu tusitiri na uwapige tafrani na nuksani wasiendelee kutufanyia ngenga ilhali wenzao twaangamia. Watu watung’onga kwa kujikonga tuloonyesha enzi zile!

Nani anaridhika na ulimpyoto,ulafu na ukuba huu? Basi huyu majinuni na afkani wa kuhurumiwa. Uliza twenda’pi au tuseme twaswekwa na kuswagwa kwenda wapi? Utaambwa huku! Huku wapi wakati kote ni huku hata kuno kwaweza kuwa huku? Washikilia huku! Huku huku wapi? Hata machinjioni huku! Peponi na motoni kote huku! Tukubaliane hapa hakuna jema bali hadaa na kupelekwa kisengesenge!

Twaliwa kama DECI na wachungaji fisi waliotamalaki kila kona ya Kaya!

Juzi tuliambiwa nyota tena ya jaha. Ebo! Mbona twapewa mbichi tulipoahidiwa mbivu? Mbona uvumilivu watulisha zilizovia! Jamani hamjastuka nyie mtendewao kama kisagaliwa! Je Mpayukaji nitumie lugha gani lau muenge?

Yule babu babu yuleee. Alisema hili koroma nyie mashikilia nazi! Alisema hili teke teketeke nyie mwaamba tena kwa minato na mbwembwe, kuwa dili. Toba! Dili liso maandili si dili kitu nakataa katu! Baya zaidi eti nao wajitia taraghani kwa sana ! Wanadhani tumesahau maneno ya babu?

Kila siku wenzenu wafaidi maghusubu nyie mwandanda na kudai “tulieni mambo yataiva na nuru itawaangazia wakati kiza ndiyo hicho kinazidi kunema na kushamiri! Ebo! Kweli limbukeni na limpyoto wana mambo tena mambo mambo!

Waachwa wasema wangojewa! Waliwa wasema wala! Wala walani? Kwetu Funzi husema, aso mato akipata mato chunga asemato. Mana yu mteke na weledi hana. Kwani yu agogota na kigovyache asijue wasomi tu wengi! Kama wataraji mwana basi umtegemeaye ana kigwaru shurti azae wafe hata mimba itoke. Kwani pale kwenye mambo ya fulusi hamjaona walivyochota na kuchuma siye tukabakia twalia huu!

Alichotaka ni mali ya mahonyo. Kaisha ipata yeye na kundile mwesha nyie. Mungu ampeni? Kilema au upele? Wenye kazi nyie mliotoa bure ili mliwe bure na kweli mwaliwa si bure! Audhubillahi mina shaitwan rajiiim! Ingekuwa yangu nafasi basi ndumo yangu ingekuwa amkeni kuzacha tumwinde bundi huyu. Ningepiga nyungwanani wasikie hata wa Likawage na Kivinje waje tumtwange kenge lau mayai yapone.

Walau hayo mayai? Ni yale aloacha Mchonga alotarazaki na kuadibu akinena kinabii: mtahadhari wajao si wote wasemao twaweza waweza!

Lahaula! Kumbe kwenye msafara wa kenge na mamba wamo! Mlipuuzia mkidhani alikuwa na lake msijue kumbe lenu mwalikoroga! Nani aliwaroga nyie? Nambe nielewe lau nilizoe gogo lililokingamana njiani mwenu muweze pita.

Hata wavikwe kiswa madhambi yao yatawaandama. Wametutenda kwanini tusiwatende tena kwa ghadhabu na munkari mara mia? Nani alitegemea maharamia yaiokoe meli wakati lengo lao kuizamisha? Ishazama zama gani! Tulonusurika angalau tulo nazo siyo hao hamnazo jama tusikizeni tuwaambacho. Hamkusikia: simbiko halisimbuliki ila kwa mikukuriko? Je m’ tayari lau kuondoa nuksi mambo yende tutegemeavyo? Tusiogopane. Maana tumejaribu kuwaauni.Wemetupuuza na kutuona hamnazo kama wao!

Kama yupo kiumbe namchukia si mwingine. Ni yule jambazi wa enzi za yule Mchonga maneno na meno alosema, “Angalieni wanangu. Si wote wasemao bwana bwana ni wangu” Mbona aliwakataa miaka ile! Wapi wamezaliwa upya tuwarejeshe kwa madoido huku jana waliiba mdomdo? Je anayetudanganya hajidanganyi? Nani huyu awezaye kuiandika historia upya au kuukamata upepo?

Tuwambe waelewe siyo walewe. Tuwambe kini’owalevya ni mali yetu

siyo ya mama zao wala umbu zao. Je wajua? Kama wajua kwanini wajifanya majuha wasijue? Nani aweza kuishinda kadamnasi ikiiamua? Kwanini tungoje iamue iwapo twaweza kurekebisha mambo? Tuseme na kurudia. Bwana mkubwa timua hao mabugu walokijaza kiwingu siyo ukichezee gungu la sivyo kesho tutakuputa wewe.

Heri kufa umesimama kuliko kuishi umepiga magoti. Niulize aliyeapa kututumikia si kututumikisha ni nani? Sasa ushoga watokapi?

Nani huyo alozaliwa jana asojua kuwa tushadoya na kujasisi aloyasema yule babuu? Hatusahau. Ni sehemu ya dafina yetu.

Leo twawapa paka watunze maziwa ya watoto! Watoto watanusurika kukonda, kunyongea na kufa kwa ngoa? Nani anamdanganya nani? Toba!

Tunataka lau tuone kikome kama mazao yapo. Nani anaweza kushiba kwa vikwakwa vyenu wakati siye twanuna?

Yule babu mwenye jina sawa na kikuku alisema, “Msipowauliza wenda kule mbio wana nini na kunani, mtajikuta tafrani” Yameishatufika tukubali. Lazima tulisake jibu hata kama kwa kuchenjiana kama alivyowahi kusema Arawa yule machachari na bingwa wa miruko kwa namnaye kama Mnana.

Husuma hii lazima ipate mwamana. Tusiposema watasema hamkusema. Sasa tumesema na tutasema hata wanetu watasema Mpayukaji alisema na kusema. Jamani nahau au lugha gani nitumie lau muambue japo ndururu!

Kaya yasedekea wao wahazahaza tutulie! Tulotegemea wanene wameingiwa na shake! Nani atawasemea? Neneni mnenalo tujue twendako vinginevyo huko twendako yatakuwa mafutu matupu!. Nani alaumiwe? Kuendelea kunyamaa si jibu bali kukikirika kiasi cha kuzua la kuzua tusijue jinsi ya kulizuia. Kwanini kuzua badala ya kuzuia? Mshaambwa kaya si mali binafsi bali kikoa. Sasa ushoga na uswahiba wajaje? Tuondoleeni maharamia na vipanga kwenye hekalu letu.

Tuleteeni watu wenye udhu siyo wanuka nongo na ugaga tuloambwa tuwatahadhari. Jamani kuna kesho na keshoye siyo mbali.

Nawapeni uchanjaa toune weledi au utobwe wenu japo tushawamaizi bado twawapa fursa japo ya mwisho ili tukiamua kuchegama na kuchenjiana tusionane wabaya.

Naregea nilikoanzia. Jamani jama twambieni basi lau tujue la kushika.
Chanzo: Tanzania Daima Juni.

Ngeleja anamsemea nani kati ya Kikwete, Mkapa na Serikali?


HAKUNA utani na matusi mabaya kwa Watanzania kama uliokaririwa juzi kutoka kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.

Ni kichaa gani hata kuku angekubali kuwa kuna watu na akili zao tena wanaojiita serikali wangepitisha uamuzi wa kijambazi kwa kuunusuru mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira ambao una utata baada ya kutwaliwa na rais mstaafu Benjamin Mkapa, familia yake na marafiki zake?

Hivi karibuni Waziri Ngeleja, alikaririwa akitangaza uamuzi wa serikali “kuinusuru’ Kiwira kwa kutumia pesa ya umma ule ule ulioibiwa mgodi huu! Kwa kutaka kutufumba macho na Ngeleja alisema, “Yaliyopita si ndwele, kubwa ni kupata umeme,” Yapi haya yaliyopita? Kama ni kashfa ya Mkapa bado haijapita. Ili ilipite si budi afikishwe mahakamani na mgodi kurejeshwa kwa umma.

Ngeleja aliendelea, “Tutaukwamua ule mradi ili uwe wa mafanikio kwa taifa na jamii yetu ya Tanzania kwa ujumla.” Hivi kwanini kila anayetaka kuuibia umma anajifanya mkereketwa wa taifa ambalo analibomoa?

Mafanikio kwa taifa ni kuwakamata mafisadi waliaojitwalia Kiwira. Kama kuna taifa hapa si jingine bali lile la mafisadi wanaopitisha maamuzi ya kijambazi kwa kusingizia taifa.

Kwanini serikali iliyojitoa kwenye uchuuzi inajifanya msemaji na mwokozi wa Kiwira na isiwe hujuma dhidi ya umma?

Wakati mkitenda kufuru hii mkubuke. Ni serikali hii imesamehe kodi zipatazo sh 687,000,000 ndani ya miezi 10.

Hii ni sawa na aslimia 30 ya makusanyo yote ya kipindi hiki. Na ni sawa na aslimia 30 ya utegemezi wa bajeti yetu kwa wafadhili. Serikali hii ndiyo imefutika wizi wa EPA na wizi mwingine mkubwa chini ya busati! Je hii serikali ni ya nani kati ya kikundi cha wezi wachache wenye madaraka na wananchi?

EPA, Richmond , IPTL, TICTS na sasa Tanpower mnazidi kufutika chini ya busati na kuiba zaidi! ‘No. This is unbearably too much’.

Ngeleja, amelidanganya Bunge na taifa zaidi ya mara tatu kuwa angewafichua wamiliki wa Kiwira. Lakini mara zote amepiga dana dana na kufunika kombe! Na kama shida ni umeme, kwani Kiwira ndicho chanzo pekee?

Hapa tuambiane ukweli kuwa msimu wa uchaguzi umekaribia na vinatafutwa vyanzo na sababu za kupatia pesa kutoka kwenye hazina ya umma. Haiingii akilini serikali yenye hisa aslimia 30 ibebe mzigo wa kuokoa mradi ilhali mwenye hisa aslimia 70 amekaa tu.

Kisheria mwenye hisa nyingi ndiye mwenye majukumu na mapato mengi. Hata kwenye kuendesha mradi na kutoa maamuzi mwenye hisa nyingi ndiye mwenye sauti. Sasa inakuwaje kanuni hii inapindwa kama hakuna namna?

Tunaambiwa Kiwira Coal and Power Company (KCPC) ambayo ni kampuni tanzu ya Tanpower inamilki asilimia 70. Na hii ni kampuni inayodhaniwa kumilkiwa na Mkapa, familia yake na marafiki zake.

Je inakuwaje serikali inakubali kuingia ubia na kampuni zinazoshutumiwa kupatikana kifisadi tena kwa kuhujumu wananchi inaodai kuwatetea na iliyoapa kuwalinda wao na mali zao?

Kabla ya kodi yetu kuibiwa, waziri atwambie nani wamilki halali wa Kiwira na jinsi walivyoipata. Haiwezekani watu waibe mali ya umma kwa malipo ya sh 70,000,000 badala ya 4,000,000,000 halafu tuwaongezee pesa nyingine pasiwe na mchezo mchafu unaowahusisha wakubwa wetu wa sasa.

Isijekuwa wanaposema familia na washirika wa Mkapa wakamaanisha na mawaziri wake wa zamani ambao wengi ndiyo wanaunda Baraza la Mawaziri la sasa.

Je, bado serikali kwa kukopa maneno ya Mkapa, inadhani Watanzania ni wavivu wa kufikiri kiasi cha kutenda kufuru hizi?

Tuweke msisitizo. Kama serikali haina mpango wa kutuibia, isitoe hata senti moja kwa Kiwira hadi tujue nani mmilki wake na alivyoipata.

Hii ni sawa na jambazi anakuteka anaiba gari lako baada ya kukujeruhi halafu analigongesha na kuja kukuomba pesa ya kulitengenezea. Nawe, kama kichaa, unampa. Hata kuku, pamoja na kuwa na ubongo usiojaa kijiko, hawezi kufanya upuuzi huu.

Piga ua. Hii ni njama ya wakubwa wenye madaraka kutaka kutuibia ili kupata pesa ya kuhonga kwenye uchaguzi. Hakuna maelezo mengine yanayoweza kuingia akilini.

Ingawa rais Kikwete, kwa sababu anazojua mwenyewe, ameendelea kumkingia kifua Mkapa, wabunge wetu nasi kwa ujumla wetu tusimame imara na kuondosha wizi huu.

Ikiwezekana, kama hatajirudi, tumpigie kura ya kutokuwa na imani naye. Maana amekuwa kichaka cha uhujumu wa taifa na wizi wa pesa zetu. Atuambie anatawala kwa ajili ya nani kati ya wananchi na hayo makampuni ya kutia shaka anayokingia kifua.

Ni aibu na hasara kuwa anamaliza miaka mitano bila kutekeleza hata ahadi moja! Yako wapi marekebisho ya mikataba ya kijambazi ya uwekezaji iliyowawezesha kina Mkapa kutwaa mali ya umma? Iko wapi vita ya kupambana na ufisadi iwapo Kagoda inaendelea kuwa serikali ndani ya serikali?

Muhimu, kwa wahusika kutia maanani ni kwamba hata huko Madagascar na kwingineko umma ulipoasi utawala vidhabu walianzia huku tuliko. Kuna mwisho na unakaribia kama wananchi watatambua kuwa kikwazo cha maendeleo na majaliwa yao ni serikali za namna hii zinazo lala kitanda kimoja na mafisadi.

Huwezi kupora mali ya umma na bado ukawa na upogo wa kuchota pesa ya umma ule ule kuwakomboa waliouibia ukaendelea kudai unaujali na kuuheshimu. Hili ni tusi la nguoni kwa umma.

Huwa nauliza swali hili mara kwa mara. Je Watanzania washikwe wapi au wadhalilishwe na kuhujumiwa vipi ndipo wasimame na kuondosha dhuluma? Ajabu akitokea mtu akasema wezi na kina fulani, wanaamka mawaziri, bila aibu, kumtisha wakiwakingia kifua wezi!

Je hawa si wezi wenzao? Je hawa wanafaa kuendelea kuwa kwenye ofisi za umma wanaouhujumu? Wizi wa Kiwira utufungue macho tuasi. Hata farasi hufikia mahali akakataa kubebeshwa mizigo anapogundua anadharauliwa.

Muhimu, serikali iwafikishe mbele ya sheria wezi wa mali za umma badala ya kupanga kuwaongezea pesa nyingine kwa kuvunja hazina ya umma.

Na kama wabunge watabariki wizi huu watajivua uhalali wa kuwasemea wananchi. Watakuwa wameuonyesha walivyo kwenye madaraka kulinda mafisadi huku wakiuhujumu umma wanaotaka uwachague tena.

Isitokee. Shame on them!
Chanzo: Tanzania Daima Juni 10, 2009.