The Chant of Savant

Wednesday 27 July 2011

JK na Pinda walivyotesa na Uongofleva!



Hii picha hapo juu ni picha ya mwaka ya blog hii. Sijui jamaa waliipigia wapi? Ingawa ni utani unaweza kubeba ujumbe mzito kuwa watawala wetu bado wanafanya mambo ya kitoto. Je wao wanapojiona hupata somo gani? Wanafanya utoto kweli au wanasingiziwa? Hivi kwa mfano Pinda kuwaambia wabunge kuwa kashfa ya wizara ya nishati na madini haivumiliki na JK kuendelea kuwaacha walioiasisi yaani William Ngeleja na naibu wake Adam Malima si utoto? Je kutoana kafara si utoto? Rejea kutolewa kwa bangusilo Ibrahim Msabaha, Edward Lowassa, Rostam Aziz na juzi juzi David Jairo huku wahusika wakuu wakiendelea kunema. Je kuna utoto kama huu jamani? Je Kikwete na Pinda wataacha utoto lini? Hebu tubadili namna ya kuuliza maswali. Picha hii inaonyesha usanii wa hali ya juu. Je usanii wa Kikwete bado ni mali au utoto na pigo la kihistoria kwa taifa? Hii ndiyo maana tumeona tutumie Uongofleva kuwakilisha ujumbe kulingana na aliyesanifu picha alivyolenga kuonyesha utoto wa hawa jamaa.
Kazi kwenu kutafakari wakati mkifaidi picha hii ya mwaka ya blog hii.

Tuesday 26 July 2011

Mwanzo wa ndoa ya Maalim Seif kuvunjika?

Maneno ya katibu wa Fedha na Uchumi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Tegeta hayawezi kupita bila kudurusiwa. Nchemba alikariria na vyombo vya habari mnamo jumanne, 19 julai 2011 akisema, “…Mnakumbuka kule Zanzibar walikufa watu 27 lakini leo Maalim Seif yuko Ikulu na ndevu zake amenyoa, ananawiri tu; je, waliokufa wamefaidika nini…?”

Wengi wanaojua: harakati binafsi za kisiasa za Seif Sharrif Hamad tangu CCM, kuasi na kufungwa hadi kuanzisha chama chake cha CUF na hatimaye kujirejesha CCM wanaweza kukubaliana na maneno ya Nchemba. Kadhalika, wengine wasiomfahamu Hamad vizuri kwa awamu zote alizokuwa serikalini, gerezani, upinzani na sasa serikalini tena wanaweza kubisha. Kwa wanaojua kuwa CUF ni Sharrif na Sharrif ni CUF, hawana shaka na aliyosema Nchemba.

Wanaokubaliana na Nchemba wanaweza kuwa sahihi kutokana na sababu zifuatazo:
Kwanza, CCM wanamjua Shariff vizuri kwa vile alikuwa mwenzao mwanzo akawakimbia, wakamtia adabu na akarejea ili afaidi ulaji nao.

Pili, aliyosema yana ukweli kwa kiwango kikubwa kutokana na Shariff mwenyewe kutokanusha yaliporipotiwa. Si Shariff, ofisi yake hata chama chake waliokanusha maneno ya Nchemba kiasi cha kuyapa uzito na ukweli.

Je ni nini alichosema Nchemba? Kwa ufupi Nchemba aliongelea unafiki, ulafi na usanii vilivyofanywa na Hamad kwa kuwatumia wazanzibari hadi wakamwaga damu ili yeye ale kama anavyofanya sasa chini ya kisingizio cha serikali ya umoja wa kitaifa na kuleta mshikamano Zanzibar. Pia Nchemba aliweka wazi kuwa chama chake kiliua watu kule Zanzibar tofauti na wenzake waliokuwa wakikanusha au kukwepa kuzungumzia mauaji haya ya kinyama yaliyosababishwa na CCM NA Hamad. Maana ukiangalila anachoongelea Nchemba na kinachoendelea unaona ukweli kwa kiasi kikubwa. Kuna baadhi ya maswali ambayo hadi kesho hayajawahi kupewa majibu yanayoingia akilini. Hivi kweli Shariff ameleta mshikamano wa wazanzibari au mshikamano wake na CCM? Hivi umakamu wa rais wa Shariff unawasaidia nini wale aliowahi kuwashawishi wakaingia mkenge na kuandamana hadi wakauawa au kupoteza viungo? Je hili la kutupiwa umakamu wa rais ndilo walilokuwa wakifia wazanzibari?

Sitaki mtu aniambie kuwa alichofanya Shariff ni sawa na walichofanya akina Morgan Tvangirai waziri mkuu wa Zimbabwe au mwenzake wa Kenya Raila Odinga. Wao walishinikizwa na jumuia ya kimataifa wakaunda serikali kwa kugawana madaraka. Ukiangalia Zanzibar, baada ya seif kupewa umakamu wa rais ndiyo ikawa imetoka ukiachia mbali kupewa nafasi mbili za uwaziri. Odinga na Tvangirai wamo kwenye serikali ya umoja wa kitaifa wakisimama kidete kupigania maslahi ya wananchi na vyama vyao na si kugeuzwa nyumba ndogo kama ilivyo hapa kwetu.

Kimsingi, kwa maneno ya Nchemba, alichofanya Shariff ni usaliti wa kawaida ingawa CUF na Hamad wenyewe hawataki kukubali ukweli huu. Ukiangalia maneno ya Nchemba na nafasi yake katika chama chake, unagundua kuwa CCM wanajua fika Shariff alivyofanya usaliti kwa tamaa ya madaraka. Hili halina mjadala na yaweza kudhaniwa ndiyo maana Shariff hakukanusha.

Wengi wanaweza kuchukulia maneno ya Nchemba kirahisi na kudhani ni mawazo yake binafsi na si msimamo wa chama. Je Nchemba katumwa na wakubwa zake ampe ukweli wake Shariff? Je hizi ni dalili za CCM kuanza kumchoka na hatimaye kumtosa Shariff? Wenya akili wanajiuliza nini kitafuatia baada ya muhula huu kuishi na Zanzibar kwenda kwenye uchaguzi. Shariff atawambia nini wazanzibari baada ya kumalizika muhula huu? Kimsingi, alichofanya na kumaanisha Nchemba ni kwamba kama Hamad na wenye mawazo kama yao wanaokula CCM wataendelea na kidomo domo wajue wanaweza kushughulikiwa bado. Kimsingi Nchemba alikuwa akimkumbusha Hamad usaliti wake na hivyo kuhakikisha anaishi kwenye nyumba ya vioo na hivyo asitupe mawe. Tangu kufungwa kwa kile watani wa Shariff huita ndoa hii ya mkeka, faraja pekee ya Shariff ni kelele za Zanzibar kutaka iwe na mamlaka zaidi kwenye muungano. Hii, kimsingi, ndiyo hoja fichi ya Shariff na wanzanzibari wengi waaminio kuwa muungano unawanyima uhuru. Hata hivyo, nje ya muungano Zanzibar itakuwa kama Comoro na isitoshe hawa waliopo madarakani wanalijua hili na hawako tayari kuona muungano ukiuawa.

Swali la Nchemba ni fupi lakini zito na lenye ujumbe mzito sana. Hebu tulirejee. “…Mnakumbuka kule Zanzibar walikufa watu 27 lakini leo Maalim Seif yuko Ikulu na ndevu zake amenyoa, ananawiri tu; je, waliokufa wamefaidika nini…?” Pamoja na kuonekana kumgusa Hamad binafsi, ni ukweli usiopingika kuwa tangu Hamad agawiwe umakamu rais amenawiri na ndevu zake zimepunguzwa. Je wale waliopoteza maisha wamefaidika nini? Jibu la swali hili si rahisi ingawa Nchemba anajaribu kujenga mazingira ya kulipatia jibu. Hata kwa kukangalia maneno ya Nchemba bado hatuwezi kupata jibu sahihi. Maana hatujui wanavyojisikia wale waliopoteza ndugu zao au mali na hata viungo vyao. Je wataendelea kutekwa nyara kwa lugha tamu za makubaliano huku damu zao ama ndugu zao zikiishia kuneemesha kitumbua cha watu wachache waroho waliowahadaa? Ni suala la muda ukweli kufumka na wahusika kujikuta wakizomewa hata kuadhibiwa na historia.

Nchemba anajua wazi kuwa kilichosilimisha Hamad si kingine bali njaa. Anajua fika Hamad asivyo na tofauti na wanasiasa wengine walioamua kujirejesha CCM kinyume nyume kama vile Augustine Mrema, Masumbuko Lamawai, Warid Kaboro, Thomas Ngawaiya, Tambwe Hiza, Shaib Akwilombe, Dk Masha, Stephen Wassira na wengine wengi ambao wanafanya siasa za matumbo kama Hamad.

Je mwanzo wa ndoa ya mkeka baina ya CCM na maalim Seif ndiyo unaanza? Maana inapotokea wale wanaojiona watu wazima kuanza kurushiwa vijembe na matusi ya wazi na watoto wa jana kiumri na kisiasa huku wakubwa wakijifanya kutohusika jua kuna jambo.

Kama Shariff na CUF walikuwa wakidai waliibiwa ushindi mar azote, kama ni kweli, ilikuwaje wakakubali cheo cha kutupiwa tena kwa baadhi ya wakuu wa chama huku umma ukiendelea kuteseka kama awali?
Chanzo: Dira ya Mtanzania Julai 26, 2011.

PUMBA ZA MLEVI MDANGANYIKA


Nichukue fursa hii kujitambulisha rasmi kama mwenyeji wa wasomaji wa gazeti hili. Nimeanzisha safu hii baada ya kuombwa sana na utawala wa gazeti kutokana na kutokuwa na taimu ya kuacha kupiga mma na kuandika.

Kimsingi, safu hii itakuwa kipenzi cha makapuku, walevi na wadanganyika wengine popote walipo kwenye anga hili la wadudi.

CV yangu ni kali. Mie nilizaliwa miaka mingi iliyopita chini ya utawala wa Kaisari wa Kirumi. Kutokana na baba yangu kuwa mlevi maarufu na mama muuza gongo, nilipozaliwa, walinipa jina la biashara yao yaani Mlevi. Nimesoma kwa pesa ya gongo na kukuzwa kwayo. Akili yangu ni ya gongo hata damu yangu. Hivyo nitakachoandika humu kama kitakusumbua usijisumbue kwenda polisi au kuazima kibiriti uchome kibanda changu au bastola kunitoa roho. Nilishajifia zamani hata polisi wanajua hili ndiyo maana wakija Uwanja wa Fisi kuwatoa upepo wauza gongo, madawa na bangi, huwa hawahangaiki nami. Watahangaikaje na jitu lililokwishapigika kulhali?

Niliosoma nao sasa ni wabunge na mawaziri. Hata mheshimiwa Rai--- stoop! Nilisoma naye kule Chalin….. makubwa haya!
Wale akina dada sorry mama niliocheza nao michezo ya kujificha na kujenga nyumba sasa wanaitwa bibi kama sijasahau.

Zama zile najua mkoloni aliyekuwa akitawala nchi yetu alihimiza elimu kiasi cha kuwakamata wazazi wangu na kunipeleka shule. Mwanzoni nilianza vizuri nikiwa na usongo wa kuikomboa familia yangu. Hii ilikuwa ni kabla ya washenzi fulani kunikomoa ili nisiikomboe familia yangu. Nilfanya vizuri kwenye mtihani wa Cambrige kiasi cha kupeana mkono na Malkia wa Uingerezani.

Kutokana na roho mbaya ya waswahili, walipoona nazidi kupaa bila mbawa wakaamua kunipiga kipapai kiasi cha kuishia kwenye vilabu uchwara vya gongo.

Baada ya kuachana na mambo ya shule kutokana na kupigwa kipapai na walimu kuzidi kuwa wanoko, nilijichimbia kwenye unywaji. Shamba langu, ofisi yangu na wakati mwingine kitanda changu vilikuwa baa. Nilikopa sana. Nilikunywa hadi kukufuru. Kuna kipindi mama wa Kichaga aliamrisha nivuliwe suruali baada ya kushindwa kulipia gongo na mapupu kwenye kibanda chake. Niliondoka pale bila nguo isipokuwa Godfather pekee.

Kuna kipindi nilitaka kujitoa roho baada ya kuona maisha yangu yanakosa maana. Nilipokuwa nikitundika kamba mtini ili nijimalize si nyoka akanitoa baruti! Tangu siku hiyo sijawahi kufikiri kujiua tena.

Baada ya jaribio la kujiua kushindwa, niliamua kuachana na gongo. Kwa miezi minane sikunywa gongo wala kuvuta bangi. Afya yangu ilinawiri na wazazi wangu wakaanza kupata matumaini kuwa huenda ningeendelea na kazi ya ukombozi wa familia. Ni kipindi hiki nilipompata aliyekuwa mke wangu bi Domokubwa. Mama alisifika kwa kuchonga.

Mungu ni mjanja. Baada ya kuona nimerudia gongo na kuongezea bwimbwi huku mke wangu naye alianza kubadilika baada ya kugundua kuwa mie si chuma ulete aliyetegemea, Mungu hakutupa mtoto. Maana tungempata angekuwa balaa. Kama angerithi ulevi wangu angekosa maana. Na kama angerithi tamaa ya mama yake kupenda pesa na jeuri ndiyo usiseme angeishia Segerea bure.

Historia yangu ni ndefu kama barabara. Naomba niikatize hapa nizame kwenye pumba zangu. Najua wapo walevi na waharibikiwa wengi kama mimi. Hivyo naamini watakaposoma watafurahi.

Nianze na kisa cha leo. Juzi nilikuwa zangu kwenye banda letu la gongo ambalo sitaki nilitaje ili polisi wasije wakamkamata mama muuza nikaishia kukosa ulabu. Tukiwa tunakamata ulevi si akaja mpambe wa waziri wa Kiza Bill Ngereza. Jamaa alikuwa a na mabulungutu ya pesa kama yale bosi wake alitaka kuwahonga waishiwa sorry waheshimiwa. Aliagiza gongo kwa sana huku akisema ameona wokovu wa kuwapenda walevi na kuwanywesha hadi wafe. Sie kutokana na kudanganyika kwetu na kiu na mawazo tulifakamia gongo kama hatuna akili nzuri. Kumbe jamaa alikuwa na lake. Alitaka kutupa mkanda mzima wa kasheshe ya rushua inayomkabili Devil Jeuri Jero. Jamaa alimtetea bosi wake kuwa hakuwa na habari kuwa kumbe katibu wake alikuwa na mpango wa kuwahonga waishiwa sorry waheshimiwa.

Alimtupia mzigo Bangusilo Jero ambaye inasemekana aliandika waraka huu na kumpasia Milima ya Kigoma kabla ya kupitiwa na Bill mwenyewe. Tusingeyajua haya kama siyo ulimi wa jamaa kuteleza. Kwa vile ulabu ulikuwa umempanda jamaa, alimwaga mtama kibao kwa walevi. Una habari alisema kuwa bosi wake na Jero hawawezi kufukuzwa kibarua kutokana na kuwa na uhusiano mzuri na wanono. Ingawa alitaja majina ya hao wanono tena wengine wakiwa nambari wani, sitawataja kuogopa kuvuruga amani na mshikamano wa walevi wa Danganyika.

Kwa ufupi ni kwamba hata hiki kiza kilichowageuza walevi mende kimetengenezwa na wenye mamlaka ili wazidi kupata mshiko toka kwa wauza majenereta.

Baada ya ulabu kumtoka kidogo jamaa alihoji ni kwanini wahongaji wengine hawashughulikiwi wala wanaopokea hongo zao ili kupitisha mambo yao? Ingawa jamaa alikuwa kalewa akiongea na walevi, alikuwa na hoja. Nilipofika nyumbani kusema ukweli sikulala. Picha ya jamaa akichonga ilizidi kunijia hadi nikajiuliza swali moja kuu. Je Ngereza ni wa kwanza kuwahonga wahusika hata kama wanajifanya kuwa na hasira naye? Nakumbuka. Jamaa alisema kuhongwa na kuhonga ndiyo siri ya jamaa kupitisha kila upuuzi kuanzia mishiko ya makalio, sleeping allowance, suit allowance na makando kando mengine. Jamaa alisema wazi kuwa wote ni wezi ingawa mimi sisemi wala kuamini hivyo.

Alisema ukitaka kujua kuwa wao ni wezi wakubwa tena wasio na aibu, jiulize kwanini wanajadili kutumia bajaj kubeba wajawazito wakati wao wanapanda mishangingi na madege kila uchao? Huko siendi leo. Nakuachia uamue kama ni kweli au la. Halafu kuna upuuzi huu wa kuwasha umeme usiku wa manane. Nani halali anangoja umeme? Achene usanii jamani mtatugombanisha bure.

Leo nashughulishwa na kiza cha Ngereza na kashfa ya mshiko. Mpaka sasa sielewi Ngereza, Milima ya Kigoma na Jero wanangoja nini wanaharamu hawa! Je wao ni wale wasioguswa? Kama hawaguswi kwanini wao wanawagusa wengine kwa kufichua ulaji wao wa sirini? K wa vile mie ni mlevi wa kawaida, nafikiria kilevi na kubwabaja kilevi. Nasema: wote ni majizi tu hakuna cha nini wala nani ni majizi tena makubwa. Heri wangekuwa walevi kama mimi wangedanganyika na wala wasingemuathiri yeyote isipokuwa wao wenyewe. Utajuaje? Huenda nao ni walevi wa uroho na ulafi. Kwani ulevi ni gongo tu?

Kwa vile sina uchache wa kununulia mapupu, ngoja niachie hapa na kuwahi kwa mama Betty lau anikopeshe mapupu na glasi ya gongo. Kulaleki! Nawasilisha.
Mlevi Mdanganyika
Mafichoni
Akili Kichwani
Chanzo: Dira ya Mtanzania Julai 26, 2011.

Wednesday 20 July 2011

Maisha Magumu, nani aliwaroga Watanzania?

HAKUNA ubishi kuwa hali za maisha nchini Tanzania sawa na majirani zake ni mbaya. Kuna uhaba wa chakula na kupanda kwa gharama za maisha kwa ujumla. Nchini Kenya tumeishashuhudia mshike mshike baina ya serikali na wananchi wanaoshinikiza watawala kukidhi matakwa ya umma kama walivyowaahidi kwenye uchaguzi.

Nchini Uganda bado hakieleweki ingawa imla wa nchi hiyo ameendelea kujifanya hamnazo. Nchini Malawi mapambano yameripotiwa jana ambapo mtu mmoja aliuawa na wengine wengi kujeruhiwa kwenye maandamano ya kupinga utawala wa Bingu wa Mutharika kutokana na kupanda gharama za maisha. Tanzania tuna hali ngumu kuliko wote kutokana na kuendelea kukaa kizani kama mende kwa muongo mzima. Je nani alituroga kiasi cha kuwa mashahidi wa mateso yetu wakati wengine wanaamua kuingia mitaani? Nani alidhani kuwa wamalawi waliozoea kuhenyeshwa na uimla wa Banda wangejitambua na kuleta mageuzi makubwa ya kupigiwa mfano?

Wakati wenzetu wakiionyesha dunia walivyo na akili sawa sawa sisi tunawashinda kwenye ushirikina kama ilivyoripotiwa hivi karibuni na shirika la habari la Uingereza BBC bila serikali yetu hata kupinga. Ni aibu namna gani.
Leo hii watanzania wamegeuka hamnazo kiasi cha kuwavumilia hata mawaziri wanaopitisha bajeti kwa kuhonga wabunge! Tunawavumilia wabunge wala rushwa na wanaojilipa posho kwa kuuchapa usingizi na kuongea umbea! Je nani alituroga? Tuguswe wapi ndiyo tuamke? Je hii haimaanishi kuwa watanzania karibu wote ni mafisadi kila mtu kwa nafasi yake?
Kwa yaliyojiri Malawi BONYEZA HAPA na HAPA.

Sasa nimeanzisha Mpayukaji Trust Fund (MTF)

WAPENDWA wasomaji wa kijiwe leo nina furaha si kawaida. Kwanza nafurahia kifo cha kisiasa cha yule jambawazi wa Kagoda yaani Roast Tamu. Pia wakati nikifurahia kifo hiki natangaza vifo vya kisiasa vya Eddie Ewassa na Endelea Chenga vitakavyotokea hivi karibuni katika kijiwe cha Chama Cha Mafisadi wenye magamba.

Ingawa si mada ya leo, tunawashauri walevi wasiridhike na usanii huu hadi gamba kuu yaani aliyepatikana kutokana na ujambazi wa HEPA naye akitoe. Avuliwe kama hataki kujivua. I think you know what I mean.

Pili, ninaleta habari njema ya kuwapasha. Hii ni habari njema kwangu na ukoo wangu ingawa huko tuendako yaweza kuwa habari chafu na mbaya kwa walevi.

Taarifa ya kwanza ni kwamba bi mkubwa mshirika wangu wa Bedroom amepewa ulaji na ndugu yangu mpendwa na mheshimiwa sana mtukutu, mtukufu rahisi wa walevi alhaj Daktari wa kupewa Njaa NK Kaya.

Mtukutu rahisi, sorry mtukufu rahisi, amemteua mshirika wangu kuwa mwakilishi wa walevi kwenye umoja wa mataifa wa walevi kule New Amsterdam kwa Joji Kichaka.

Wale wasiojua historia ya taifa hili jeuri nawaibia kidogo. Sisi wataalamu wa historia hupenda kutumia majina ya zamani. Kwa ufupi New Amsterdam ni New Yoko.

Hivyo ninapoongea ni kwamba nitakuwa nikwahabarisha tokea New Yoko inshallah. Kwa vile mie nahamia kule na mshirika wangu wa Bedroom anihitaji kama hewa na sina kibarua, lazima tukune vichwa nami nipate kibarua cha haja na mashiko.

Katika kutafakari la kufanya, tumekuja na wazo la kuunda Trust Fund ambayo itatuingizia pesa kiasi cha kufanya mie na mshirika wangu kuwa tunakuja kutanua Bongolalaland bila kutumia njuluku zetu.

Pia kuogopa kuitwa kula kulala, tumeanzisha Trust hii ambayo itapewa jina langu ili niwe nazunguka kwa watasha na kuvuna njuluku kama sina akili nzuri.

Hata hivyo, kutokana na kujua tabia yangu ya kupenda kuhonga vimwana, mshirika wa bedroom ameamua awe mwenyekiti wa Trust kiasi cha kunifanya mie nionekane kama kikaragosi hata kama Trust yenyewe imebeba jina langu. Anaogopa nisimalizie mshiko wote kwenye kuwahonga vimwana wa kitasha kule New Yoko.

Ukiangalia jina la kampuni yenyewe, utagundua kuwa inashawishi. Trust kwa kiingilishi ni uaminifu. Nasi tumeamua kutumia sifa hii ingawa nyuma ya pazia ni kinyume.

We uliyepewa siri hii soma kimya kimya na usimwambie mtu nisije nikapigwa talaka kutokana na bi mkubwa kwa sasa kuwa mume nami mke. Si unajua tena. Mwenye nazo si mwenzio aweza kufanya lolote kiasi cha mwanamke kuoa na mwanamume kuolewa.

Tuachane na mambo ya kuolewa na kuoana na talaka. Hayo ni yangu na mamsap wangu. Turejee kwenye ulaji wangu mpya.

Najua watasha wakiona malengo yetu watamwaga njuluku kuliko hata zile wanazomwaga kwa shoga wa bi mkubwa wangu mwenye taasisi ya Ki-siri kali ya MAWAWA yaani Maulaji ya Wake wa Wakubwa aliyoinzisha baada ya mumewe kuukwaa ukuu.

Kwa vile mwakilishi wa rahisi kwenye umoja wa mataifa wa walevi naye ni sawa na rahisi, lazima kuanzia sasa kila mume au mke wa balozi, waziri, mkuu wa mkoa na wilaya waanzishe NGO ili nao kuwa kwenye kundi la ulaji na uheshimiwa.

Na hii ndiyo sababu ya kumwalika sorry, mke wa rahisi kuja kuzindua Trust yetu. Bila kuchelewa hebu tuwape japo kwa ufupi majukumu ya Trust hii tukufu.

Ifahamike kuwa baada ya wafadhili kustukia ufisadi kwenye lisirikali, tumegundua kuwa wanaamini sana Trusts na NGOs. Hii ndiyo maana utagundua kuwa Trusts za uongo na ukweli isipokuwa yetu na NGOs za ulaji isipokuwa MAWAWA, zimeota kama uyoga karibu kila mahali.

Hii imelenga kudaka njuluku za wafadhili na kuzifanyia kweli. Sisi tunakula tukipuuliza siyo kama wale jamaa wa Richmonduli AIPITIELO, HEPA, Meremetuka, SUKITAI, TICKS, TITISIELO, EYA TANZIA na wengine wengi wanaohomola kana kwamba wanawaibia vipofu.

Kwa vile yetu ni Trust Fund, tunawaomba mtuamini hata kama hatuaminiki. Tumejikita kwenye kuhakikisha tunakula na tunawakabili wafadhili kuhakikisha tunapata chetu na pesa ya Madawati kwa ajili ya watoto wa walevi wote wanaoleweshwa na kukalia mawe kama nyani katika karne ya 21.

Tumeamua kushughulikia madawati baada ya kugundua kuwa wabunge wanaopaswa kuyahangaikia wanahangaikia posho ya makalio yao badala ya madawati ya watoto wanaodai kuwawakilisha.

Wabunge wanakalia makochi mazito na kufaidi viyoyozi na kulipwa posho ya makalio wakati wanafunzi wanakalia mawe na hawalipwi posho ya makalio wakati wao ndiyo wanaostahiki kulipwa kwa kuumiza makalio yao kwenye mawe badala ya madawati.

Kwa vile Wazungu wanajali sana elimu maana ndiyo iliwawezesha kututawala sisi watakubaliana na kuingia mkenge wetu wa kuchuma njuluku kwa kisingizio cha kuondoa unyani wa kukaa kwenye mawe na ule wa watawala kuahidi maisha bora wakaishia kuleta maisha mbofu.

Kwa kujua umuhimu wa afya za walevi, tumekuja na mkakati wa kutafuta misaada kwa ajili ya dawa. Tunafanya hivyo kutokana na huruma kwa vile sisi na washirika wetu tunatibiwa nje hata kuangalia mafuta ng’ambo.

Pia tumeamua kushughulikia dawa baada ya kuona watu wakihamanika kwenda Loliondo kutapeliwa na Babu Ambilikile mwasapila kutokana na kutokuwa na dawa za kutosha. Hivyo, hata kama sisi ni wale wale, tunalenga kuepusha utapeli huu kwa kuleta upya.

Ili kuwaingiza Wazungu kwenye mkenge zaidi, tumeorodhesha karibu kila kitu kwenye kazi za Trust yetu.

Tumeorodhesha vitu kama vile vitabu, walimu, madaktari, wawekezaji hata wachakachuaji wa uchaguzi ambao tumewaita wataalamu wa kueneza demokrasia kwenye kaya ya Bongolalaland.

Kwa vile watawala wao wameshindwa kukidhi matakwa yao kama walivyowaahidi, nasi ngoja tuingie kwenye game kama wakombozi ingawa mwisho wa siku watajuta kutuamini.

Ngoja niwahi Airport tayari kupanda pipa kuelekea New Nyoko.

Hivi yule siyo Hassan Maajalala? Mbona anaonekana kama anatoka mitaa ya Roasttamu kama yeye si fisadi?

Ngoja nimfuate nione anaelekea wapi usawa huu.

Kumbe leo ni siku yetu ya mgawo! Acha niwahi kabla vibaka hawajaninyotoa roho.

Chanzo: Tanzania Daima Julai 20, 2011.

Tuesday 19 July 2011

Kikwete vunja baraza la mawaziri


Ingawa rais Jakaya Kikwete ni mugumu kujifunza na kubadilika, kashfa ya hivi karibuni ya wizara ya madini na nishati kutoa rushwa ya shilingi 6,000,000,000 ili kupitisha bajeti yake itamvua nguo kama si kupima usafi wake na serikali yake.

Tangu aingie madarakani miaka sita iliyopita, Kikwete amekuwa na kawaida ya kuwakingia kifua mawaziri wake wenye utendaji usioridhisha.

Si uzushi. Katika baraza la mawaziri la Kikwete kuna vimeo vingi kuanzia Dk Hussein Mwinyi anayewajibika kwa mauaji ya Mbagala na Gongo la Mboto, William Lukuvi, Mary Nagu, Makongoro Mahanga na Emanuel Nchimbi wanaotuhumiwa kughushi shahada.
Pia wamo mawaziri wanaolegalega kama vile Dk Shukuru Kawambwa, Profesa Jumanne Maghembe na Sofia Simba, Hawa Ghasia, Vuai Shamsi Nahodha na William Ngeleja .

Simba anasifika kwa kuwakingia kifua mafisadi wazi wazi huku Ngeleja akijulikana alivyoliingiza taifa kizani huku kila siku akitoa visingizio na uongo kuwa mgao wa umeme utatafutiwa dawa na isipatikane zaidi ya kuongezeka.
Wengi wanashangaa walichomfanyia Kikwete hadi akalitoa taifa kafara ili kuokoa wateule wake.

Sasa wamenogewa kiasi cha kuzidi kumvua nguo. Hivi ni kashfa kiasi gani kwa wizara kutoa rushwa ili kupitisha bajeti yake? Je hapa Ngeleja na Adam Malima na katibu mkuu wa wizara David Jairo wanapaswa kweli kuendelea kulipwa pesa ya umma kwa kutumia vibaya pesa na ofisi za umma? Je nchi na pesa hii ni vya Kikwete kiasi cha watanzania kujiona kama hawahusiki wakati wanahusika? Wao ndiyo waathirika wa mchezo huu mchafu ambao ni mauti kwao na taifa lao. Hizi bilioni sita zimetoka wapi zaidi ya kodi za wananchi? Je bajeti inayotolewa rushwa ili ipite haina mshikeli?
Je wabunge watakubali kuendelea kudhalilishwa na kuonekana kama wapenda rushwa?

Ingawa Ngeleja ameonekana kuwa mmoja wa wateule wasioweza kuguswa na yeyote, kwa hili, kama Kikwete kweli ana busara ya kawaida, hatamvumilia zaidi ya kumtimua mara moja. Je kwanini Kikwete anasitasita kuwawajibisha mawaziri wa hovyo? Je ni ile hali ya kuogopa naye wasiseme yake ya nyuma ya pazia?

Wakati umefika kwa wananchi kumlazimisha Kikwete kuvunja mtandao wake wa walaji wanaochafua ofisi za umma na kutumia vibaya pesa ya umma. Hawa si mawaziri kitu bali mafisadi wa kawaida waliojificha nyuma ya madaraka. Haiingii akilini dhambi kama hizo hapo juu zipite bila kuadhibiwa na wananchi waridhike na utawala wa serikali inayovumilia madudu haya. Je tatizo ni nini? Ni ile wananchi wetu kujifanya watazamaji wakati ndiyo wachezaji?

waziri mkuu Mizengo Pinda ameishafungua mashitaka rasmi kwa rais na wananchi. Tungoje tuone wahusika watachukua hatua zipi. Pinda alikaririwa akisema,"Kwa jinsi jambo hili lilivyokaa, hakuna jinsi mtu unavyoweza kulitetea hata kidogo, nilitamani sana kwamba nije hapa niseme kwamba uamuzi wangu mimi ni huu, lakini haikuwezekana," alisema Pinda na kuongeza: "Kwa dhati kabisa naomba wabunge tuwe na subira, mara tu mheshimiwa Rais atakapotua South Africa (Afrika Kusini) jioni ya leo (jana), nitamuarifu na ninaamini tutaelewana kuhusu hatua za kuchukua."
Je Pinda atalifanyia kazi hili vilivyo au ni sanaa kama kawa? Yetu macho. Tutafakari.

Wednesday 13 July 2011

Rostam Aziz ampiga kibuti Lowassa


1. HOTUBA YA MHE. ROSTAM AZIZ KWA WAZEE WA IGUNGA - TABORA


UTANGULIZI

WAZEE wangu, kwanza kabisa kabla ya kueleza kile ambacho kimenisukuma kuzungumza nanyi leo, napenda kuanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kufikia siku hii ambayo inatukutanisha waja wake.

Wazee wangu wa Igunga, baada ya kufanya hivyo napenda pia kutumia fursa hii kuwashukuru ninyi nyote mmoja mmoja na katika umoja wenu kwa kuitikia wito wangu, kijana wenu, niliyewaomba nije nizungumze nanyi siku hii ya leo.

Nafanya hivyo nikitambua vyema kwamba, kama si nyinyi wazee wangu na wengine wengi ambao hatuko nao hapa leo kwa sababu mbalimbali, ambao mmekuwa na imani kubwa nami nisingeweza kufikia hapa nilipofika sasa.

Wazee wangu, waasisi wa taifa letu walitufundisha kutambua na kuheshimu ukweli kwamba; ‘Uongozi ni Dhamana’ dhana ambayo kila ninapokaa na kutafakari huwa inanirejesha nyuma na kukumbuka jinsi nyinyi mlivyokaa katika umoja wenu na kuniteua mimi, miongoni mwa vijana wenu wengi, kuwa mwakilishi wa Jimbo la Igunga tangu mwaka 1994.

Katika kipindi hicho chote cha utumishi wangu, nyinyi wazee wangu mmekuwa mhimili muhimu ambao umeniwezesha kutimiza wajibu wangu kwa bidii kubwa, maarifa na nidhamu ya hali ya juu nikitambua namna ambavyo mmekuwa na imani kubwa juu yangu.

Ari na moyo wa imani, ushirikiano na mshikamano ambao wazee wangu mmekuwa nao kwangu ndiyo ambao kwa kiwango kikubwa umetuwezesha kufanya kazi kwa pamoja, tukishinda changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikilikabili jimbo letu katika kipindi chote ambacho mmeendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Miongoni mwa mafanikio makubwa tuliyoyafikia kupitia ushirikiano wetu na uongozi wa pamoja ni kwamba, mwaka 1994 Igunga ilikuwa ni wilaya ya mwisho kwa maendeleo mkoani Tabora lakini leo ndiyo ya kwanza, taa za barabarani, bima ya afya kwa kila kaya, zahanati kila kijiji na shule nyingi kuliko idadi ya kata zilizomo kwenye wilaya.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi chote ambacho mmendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi hicho chote hayajaweza kumaliza changamoto zote za maendeleo ambazo zinatukabili.

Wazee wangu, ingawa nimekuwa na kawaida ya kukutana na kuzungumza nanyi mara kwa mara, mmoja mmoja na wakati mwingine katika umoja wenu, wito wangu wa leo una makusudi ambayo kwa kiwango kikubwa ni tofauti na yale ambayo tumeyazoea.

Japokuwa ujumbe ninaotaka kuzungumza nanyi wazee wangu, si mgeni sana masikioni mwenu, tofauti ya leo na mikutano yetu mingine iliyopita ni uamuzi ambao nimekusudia kuufanya na ambao nitayatangaza muda mfupi ujao.

YATOKANAYO

Wazee wangu, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu hali ya siasa nchini na hususani afya ya kisiasa na matukio mengine ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho mimi ni mwanachama wake na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) nikiuwakilisha Mkoa wetu wa Tabora.

Naamini kwamba katika kufuatilia kwenu mtakuwa mmebaini kuwapo kwa matukio ambayo kwa namna moja au nyingine yamekuwa yakitokea huku yakiligusa jina langu na wakati fulani nafasi yangu kama kiongozi wa chama hicho.

Wazee wangu, nayasema hayo kwa sababu mara kwa mara ninapokutana nanyi nikiwa katika ziara zangu jimboni na wakati mwingine mnapowasiliana nami kwa njia mbalimbali mmekuwa mkionesha kuguswa kushitushwa na kutaka kujua kulikoni kuhusu mambo hayo yanayotokea.

Mimi, kama mnavyonijua nyote, ni mtu muwazi na mkweli. Siku zote nimekuwa mwepesi sana wa kuwaeleza kuhusu kila kinachotokea ili kuwaondoa hofu na wakati huo huo kuwahakikishia kwamba masuala yasiyo na msingi hususani yale yanayogusa siasa za kitaifa hayawezi kutuondoa katika mstari sahihi wa kuwahudumia wananchi wa Igunga, mkiwamo nyinyi wazee wangu ambao mmeniamini na kunituma kuwawakilisha.

Nyinyi wenyewe ni mashahidi wazuri kwamba tangu matukio yanayogusa jina langu yaanze kutokea miezi michache tu baada ya Serikali ya Awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikweti kuingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005, tumekuwa tukiyapuuza na tukaendelea kufanya kazi pamoja kwa bidii.

Bado naamini na nitaendelea kuamini kwamba tulifanya uamuzi sahihi wa kuyapuuza matukio hayo kwani mbali ya kuendelea kutimiza malengo mbalimbali yaliyokuwamo katika Ilani yetu ya Uchaguzi ya CCM, pia mliendelea kuniamini kwa nafasi yangu ya kuwa mwakilishi wenu bungeni na hata mkaniruhusu nibebe jukumu jingine kubwa la kuwa Mjumbe wa NEC ninayewakilisha mkoa wetu wa kihistoria wa Tabora.

Wazee wangu, nyinyi ndiyo watu mnaolifahamu vyema jimbo letu la Igunga na hakika nyinyi ni sehemu muhimu ya watu wanaojua historia ya kisiasa ya Mkoa wa Tabora kwa miaka mingi hata kabla ya kuja kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini.

Hakuna shaka hata kidogo kwamba, Tabora ni kitovu hasa cha uasisi wa siasa za vyama vingi hapa nchini. Ni wazi kwamba huwezi ukazungumzia chimbuko la vyama vya upinzani tunavyoviona hapa nchini leo pasipo kugusa mkoa huu ambao umekuwa chimbuko la wanasiasa wenye mizizi hapa na nchini kwa ujumla.

Majina ya wanasiasa wa aina ya wazee wetu, hayati Chifu Said Abdallah Fundikira na Christopher Kassanga Tumbo, Kasela Bantu (Mungu awalaze mahala pema peponi), James Mapalala, Profesa Ibrahim Lipumba na mengi mengine yana mizizi yao katika Mkoa wetu wa Tabora.

Kutokana na ukweli huo basi ni wazi kwamba, nikiwa Mbunge wa Igunga kwa vipindi vinne mfululizo na wakati huo huo nikiwa Mjumbe wa NEC kwa vipindi vitatu mfululizo, moja ya kazi ambazo nimezifanya kwa uaminifu na kwa bidii kubwa huku nikiungwa mkono na kushirikiana nanyi ni ile ya kuhakikisha kwamba mkoa huu pamoja na kuwa kitovu cha upinzani unaendelea kubakia kuwa ngome muhimu ya kisiasa ya CCM.

Si vibaya tukakumbushana kwamba, wakati nachaguliwa kuwa mjumbe wa NEC wa Mkoa mwaka 1997, jimbo moja katika mkoa wetu lilikuwa likishikiliwa na upinzani. Leo hii Tabora ni mkoa pekee miongoni mwa mikoa iliyotuzunguka ambao haukupoteza jimbo hata moja kwenda upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa 2010. Mafanikio haya tuliyafikia kwa pamoja kutokana na ushirikiano wenu wazee wangu.

Wazee wangu, Waswahili wanasema usione vyaelea, vimeundwa. Kazi ya kuijenga CCM katika mazingira yenye mizizi hasa ya upinzani nikiwa mbunge na hususani M-NEC kutoka Mkoa wa Tabora haijapata kuwa rahisi na itaendelea kuwa ngumu na ambayo mapambano yake ni makali sana.

Wazee wangu, kwa namna ya pekee kabisa napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru nyinyi wazee wangu wa Igunga na wananchi wenzangu wote wa Mkoa wa Tabora kwa kushikamana na kuifanya kazi hiyo kwa bidii, uaminifu na mafanikio makubwa.

Matunda ya kazi hiyo kubwa yanaonekana. Pamoja na kuwa kitovu cha kihistoria cha siasa za upinzani, Tabora ndiyo mkoa pekee katika eneo hili ambao unaongozwa na wabunge wote kutoka CCM baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na hata kabla ya hapo.

Kwa sababu hiyo basi, wazee wangu, sote katika umoja wetu ukiacha mafanikio makubwa tuliyopata katika jimbo na Wilaya yetu ya Igunga, tunayo mambo mengine ya msingi ya kujivunia. Kwa moyo wa dhati na kwa unyenyekevu mkubwa napenda kuwapongeza kwa namna mlivyojitoa kukipigania na kukitetea chama chetu kwa ari na nguvu ya kipekee.

KUJIVUA GAMBA

Wazee wangu, chama chetu chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete kimeamua kwa kauli na nia moja kujitathmini na kufanya mabadiliko makubwa ya kimfumo yenye lengo la kukiwezesha kiendelee kubakia chama kinachoaminiwa na kuungwa mkono na Watanzania walio wengi.

Dhamira ya mwelekeo huo wa kufanya mabadiliko ya ndani ya chama chetu ilitangazwa rasmi na Mwenyekiti wetu Rais Kikwete wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM, mjini Dodoma.

Katika hotuba yake hiyo, Rais Kikwete aliyafananisha mabadiliko hayo na tabia ya kawaida na ya asili ya nyoka na wanyama wengine kadhaa ya ‘Kujivua Gamba’.

Wazee wangu hatua ya kwanza ya utekelezaji wa azimio hilo na mwelekeo huo sahihi ilifanyika mjini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati Kuu ya Taifa ya CCM ambacho mimi nilikuwa mjumbe wake.

Wakati wa kikao hicho, wajumbe wote wa Kamati Kuu na wale wa Sekretarieti ya chama chetu wa wakati huo kwa kauli moja tulikubaliana kujiuzulu, lengo likiwa ni kumpa Mwenyekiti wetu fursa nzuri ya kufanya mabadiliko ya uongozi yatakayotoa nafasi ya kupata mwelekeo mpya wa Chama.

Wazee wangu, tulifanya hivyo tukionesha kuunga mkono kwa asilimia 100 kile ambacho bado naendelea kuamini kuwa ni mawazo sahihi na yenye mwelekeo thabiti ya Mwenyekiti wetu ambayo kwa kiwango kikubwa yalikuwa yakiakisi matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa urais, ubunge na udiwani wa Oktoba mwaka jana.

Niliseme kwa maneno machache tu hili. Ingawa ni kweli kwamba Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana umekirudisha madarakani chama chetu kwa kukipa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa urais, ubunge na udiwani kwa Tanzania Bara na Zanzibar, kiwango cha ushindi tulichopata kimeonyesha waziwazi dalili za wananchi kupunguza imani yao kwetu kuilinganisha na ilivyokuwa mwaka 2005.

Tungekuwa ni chama cha siasa cha ovyo iwapo tungepuuza kupungua kwa kura za rais kutoka zaidi ya asilimia 80 tulizopata mwaka 2005 hadi kufikia aislimia 61 mwaka jana kiwango ambacho ni pungufu kwa asilimia 20 ya kura katika kipindi cha miaka mitano tu, hasa ikizingatia ukweli kwamba mgombea urais ni mtu yule yule.

Tungekuwa ni chama cha siasa kilichokosa umakini iwapo tungekaa pasipo kuchukua hatua zozote za kujiimarisha baada ya matokeo ya Uchaguzi Mkuu kuonesha wazi kukua kwa upinzani ambao umeongeza idadi ya wabunge na madiwani katika pande zote mbili za muungano.

Matokeo hayo ya uchaguzi ambayo hapana shaka yamekitikisa chama chetu yalitukumbusha wasia ambao tuliachiwa na Baba wa Taifa aliyesema; ‘Bila ya CCM Madhubuti Nchi Yetu Itayumba’.

Wazee wangu, kwa sababu ya kutambua ukweli kwamba hakuna haki isiyo na wajibu kama nilivyosema awali, mimi na wenzangu tuliokuwa katika Kamati Kuu tuliona ulazima, haja na umuhimu wa kukubali kwa kauli moja wito wa kututaka tujiuzulu ikiwa ni hatua moja ya kujipanga na kukijenga upya chama chetu.

KUJIVUA GAMBA KWAPOTOSHWA

Wazee wangu, kilichotokea baada ya kujiuzulu kwetu kila aliye ndani na nje ya chama chetu amekisikia na anakifahamu. Chama kilipata safu mpya ya uongozi iliyotokana na kuundwa kwa Sekretarieti inayoongozwa na Katibu Mkuu wetu mpya, Mhe. Wilson Mukama, na Kamati Kuu iliyokuwa na sura tofauti na ile ya awali.

Wakati tukitafakari na kuangalia mustakabali mpya wa kisiasa ndani ya chama chetu, ghafla yalianza kutokea mambo ambayo chokochoko zake zilianza kusikika tangu tukiwa ndani ya Kamati Kuu ambayo ilijiuzulu baadaye.

Mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kilichagua wajumbe wapya wa Kamati Kuu na kuidhinisha uundwaji wa Sekretarieti mpya, dhana ya kujivua gamba ambayo naamini Mwenyekiti wetu aliianzisha kwa nia njema ilianza kuenezwa ikichukua tafsiri na mwelekeo tofauti na ule wa awali.

Wajumbe wawili wa Sekretarieti, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), Mhe. John Chiligati, na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Nape Nnauye, walisikika wakitangaza kwamba Halmashauri Kuu ya Taifa ilikuwa imefikia uamuzi wa kuwapa siku tisini wale walioitwa watuhumiwa wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi ndani ya chama kujitoa katika nafasi zao za uongozi vinginevyo watafukuzwa na chama.

Wazee wangu, baada ya kushinikizwa sana na vyombo vya habari wawataje kwa majina wanasiasa waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi ambao ni wajumbe wa NEC na ambao wanapaswa kujiuzulu nyadhifa zao, wajumbe hao wa Sekretarieti walikwenda mbele zaidi.

Baada ya awali kuwaeleza waandishi wa habari kwamba majina ya watuhumiwa hao yalikuwa yakifahamika kutokana na kuhusishwa katika kashfa tofauti kama zile za Richmond, EPA na ununuzi wa rada, mwishoni viongozi hao walikaririwa wakiyataja majina ya wanasiasa watatu kuwa ndiyo ambao walikuwa wakilengwa na maamuzi hayo.

Wazee wangu, nilishangazwa na kushitushwa na namna porojo na fitina za kisiasa zilivyofinyangwa kwa mara nyingine tena baada ya kusikia jina la mbunge wenu ambaye ni mimi, likitajwa kuwa miongoni mwa yale matatu ya viongozi waliokuwa wakitakiwa eti kupima wenyewe na kisha kuchukua uamuzi wa kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya NEC katika kipindi cha siku tisini.

Niliseme hili mapema. Mshangao na mshituko wangu haukusababishwa na kutajwa kwa jina langu, la hasha, bali namna uamuzi halisi wa NEC na hususani dhana nzima ya ‘kujivua gamba’ ilivyoweza kupindishwa na wajanja wachache na kisha kuendeshwa kwa maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu.

Pili, nilishangazwa na kushitushwa na hatua ya viongozi wa chama changu ambacho nimekitumikia kwa bidii na uaminifu mkubwa kufanya juhudi kubwa hata kukivisha kikao kitukufu cha NEC uamuzi ambao msingi wa hoja zake ni vita vya kimakundi ya kisiasa yaliyo ndani ya CCM kwa upande mmoja na propaganda za vyama vya siasa vya upinzani na vyombo vya habari kwa upande mwingine.

Tatu, nilishangazwa na kushitushwa na ujasiri ambao umekuwa ukioneshwa na baadhi ya viongozi wetu wapya wa Sekretarieti wanaolitaja jina langu na kulihusisha na kile wanachokiita ufisadi ambao hata ukweli wa kimazingira na kihistoria ukiachilia mbali ushahidi wa wazi umeshathibitisha kwamba ni porojo za kisiasa zilizotokana na makovu na matarajio ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na ule ujao wa 2015.

Wazee wangu, nyinyi ni mashahidi kwamba, mbali ya mimi mwenyewe kujitokeza kupitia vyombo vya habari na kueleza wazi kwamba sijapata kujihusisha katika vitendo vyovyote vya ukiukwaji wa maadili ya uongozi au vya rushwa, hakuna ushahidi wowote uliotolewa unaonihusisha na kashfa yoyote miongoni mwa zile zilizotajwa.

Wazee wangu, ni wazi kwamba kama chama chenye siasa chenye dhamana ya kuwaoongoza Watanzania kutoka katika lindi la ufukara, maradhi, matatizo ya makaazi na mengineyo siku zote tunapaswa kuwa makini katika kuhakikisha kwamba changamoto za kuwaongoza na kuwakomboa wananchi waliotupa dhamana hazitikiswi na mawimbi ya matakwa ya nyakati ama ya vyombo vya habari au wapinzani wetu wa kisiasa walio nje ya CCM.

Ni kwa sababu ya kulitambua hilo na hasa kuyatambua madhara yanayoweza kukipata chama chetu na nchi yetu iwapo tutaendekeza siasa za kupakana matope pasipo na sababu za msingi, kuchafuana kusikokoma na kulipizana kisasi ndiyo maana nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi wazee wangu ili kuweka kumbukumbu sahihi.

MAAMUZI YANGU

Wazee wangu, nimetafakari sana na kimsingi nimefikia hatua ya kupima yale ambayo yamekuwa yakisemwa na kuandikwa juu yangu na ambayo kwa mtazamo wangu unaoungwa mkono na wanafamilia yangu, marafiki zangu na washirika wangu wa kibiashara walio ndani na nje ya nchi, naona umefika wakati muafaka wa kuchukua hatua.

Kwa sababu ya kutambua uzito wa hatua ninazokusudia kuzichukua, niliona halitakuwa jambo la hekima hata kidogo iwapo ningefanya hivyo pahala pengine popote bali hapa Igunga mbele ya nyie wazee wangu.

Baada ya kukaa na wanafamilia yangu, marafiki na washirika wangu wa kibiashara niliona halitakuwa jambo la busara hata kidogo kuendelea kuvutana na viongozi wa chama changu na wanachama wenzangu wa CCM katika mambo ambayo yanaweza kumalizwa kwa njia muafaka.

Wazee wangu, sina budi niwaeleze kwamba, mbali ya athari za kisiasa na kifamilia, vita vya ovyo vya kisiasa kama hivi tunavyoviendesha na kuviendeleza ndani ya CCM na ndani ya nchi yetu huwa vina athari kubwa katika ulimwengu wa kibiashara. Athari kama hizo za kibiashara huingia ndani zaidi kuliko vichwa vya habari vya magazeti vinavyolenga kuchafuana, na athari hizo huwa kubwa zaidi kwa mtu kama mimi kwa sababu tofauti na wengine wengi hapa nchini, mimi ni mfanyabiashara wa kimataifa.

Katika ulimwengu wa kibiashara wa leo, vita hivi ambavyo vinaweza kuonekana kuwa ni vidogo tu vyenye malengo ya kuchafuana kisiasa, vinakuwa na athari kubwa katika uhusiano wa kibiashara kuliko hata wale wasioelewa wanavyoweza kukadiria. Ndiyo maana nimeona ni afadhali sasa niwape nafasi wale wanaoendesha siasa hizi uchwara na zisizo na tija waendelee na siasa zao hizo ambazo kwa bahati mbaya kwao, mimi sina muda nazo na siwezi kuwa sehemu yake. Na mimi kwa upande wangu niendelee na maisha yangu.

Kutokana na ukweli huo na sababu zote hizo basi, kwa moyo wa dhati na kwa nia thabiti, hatua ya kwanza niliyoiona kuwa ninapaswa kuichukua ilikuwa ni hii ya kuitikia wito unaotokana na msukumo wa ndani ya nafsi yangu wa kuamua kukomesha kabisa malumbano na mivutano isiyo na manufaa kwangu binafsi, kwa viongozi wa chama changu na chama chenyewe.

Msukumo huo si mwingine bali ni ule wa kuamua kuachia nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama, nikianzia na ile ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nikiuwakilisha Mkoa wa Tabora na hii ya ubunge wa Igunga ambazo kama si kwa baraka za chama changu nisingelikuwa nazo.

Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.

Aidha, nimefikia uamuzi huo lengo likiwa ni kuwajengea heshima na imani machoni mwa wanachama na wananchi wengine, viongozi wangu ambao naamini baada ya mimi kujitoa watapata fursa ya kutafakari upya changamoto nyingine mbadala zinazowakabili ambazo msingi wake ni dhamana kubwa walizo nazo za kukiongoza chama chetu na nchi yetu kupitia Serikali yake.

Wakati nachukua uamuzi huu, natambua vyema kwamba, watatokea watu ndani ya chama chetu na nje ambao watafanya kila juhudi kupotosha au kupindisha ukweli kuhusu hatima yangu ya kisiasa baada ya kujiweka kando na kujipa mimi mwenyewe na chama changu fursa ya kutafakari kwa kina majaaliwa yangu na ya nchi yangu katika siku zijazo.

Nafanya hivyo nikiwa na imani thabiti kwamba, uamuzi wangu huu, hususani ule wa kuachia nafasi yangu ya ubunge, yatakipa fursa nyingine CCM ya kuendelea kuliongoza jimbo letu la Igunga katika kipindi cha miaka minne ijayo kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Kwa upande mwingine, uamuzi wangu huu naona ni fursa kwa viongozi wa Chama changu cha CCM kutafakari na kuamua njia wanayoiona wao ni sahihi kuichukua kwa hatima na mustakabali wa chama chetu na ambayo wanaamini itakipa nguvu mpya ya kisiasa dhidi ya vyama vya upinzani.

Sambamba na hilo, ninayo imani thabiti kwamba, uamuzi wangu wa kubakia kuwa mwanachama wa kawaida na mtiifu wa CCM utakuwa chachu kwa chama changu na kwa Serikali yake kuwatumikia wananchi kwa Ari Zaidi, Kasi Zaidi na Nguvu Zaidi.

Mwisho kabisa, nikimalizia naomba nitumie fursa hii kutoa heshima za pekee kwa Rais Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa aliyoifanyia na anayoendelea kuifanyia nchi yetu. Amefanya mengi na makubwa kuiendeleza nchi yetu na watu wake kuliko inavyothaminiwa na kufahamika. Kazi yake kubwa inashindwa kuthaminiwa na kufahamika kutokana na siasa chafu tunazoziendesha Tanzania. Wasia wangu kwa wanasiasa wenzangu, waandishi wa habari na Watanzania wenzangu kwa ujumla ni kuwa tunahitaji kuisaidia nchi yetu kwa kufanya siasa zenye mwelekeo wa kujenga ambazo ndiyo hasa zinapaswa kuwa siasa kwa maana halisi ya neno hilo.

Wazee wangu, baada ya maelezo hayo, nawashukuru sana kwa kunisikiliza na kunielewa.

Ahsanteni sana.

Mwisho…

Tuesday 12 July 2011

South Sudan: One Tribe Takes it All Perilous

When South Sudan embarked on seceding, it became more a fact than a thought that they would vote for freedom. Unstoppable as it was then, we now are waiting for the genesis of a new Nation on 9th July. This is the culmination of decisive vote for freedom. Yeah. Freedom. Everybody wants to be free and, of course, everybody deserves to be free. Freedom means, among other things, honour, sense of belonging and deciding one's destiny.

Now the freedom of South Sudan is a reality, what will north do? It must be noted. Northern Africans calling themselves Arabs or Jallaba , for long, have enslaved, killed, robbed, raped and subjugated southerners. In doing so, they forgot one cardinal thing: all goodies they thought are God given come from south. Look at oil, farm produce, water, pastures for their animals and what not.

Though in the beginning northerners rebuffed the idea of independence of southern Sudan, now that it is the fact, it is time for them to lick their wounds and accept the bitter pill of reality.

Notorious and obnoxious north has always been, it is time for it to behave well. For even Arabs who used to brainwash and use them will go where yum yum is- south. So too, North should stop supporting separatists who are currently fighting for no cause except manipulation from North. Again, it must be noted: currently South Sudanese are facing allegations that Dinka tribe has taken everything and forgot other communities making this new nation. This needs to be addressed and arrested altogether shall South think of forging ahead. Tribalism, corruption and nepotism are not a good beginning. South Sudan as a nation is for all from majority Dinka and Nuer, Shulluk, Azande, Acholi, Kakwa, Shilifi, Bari, Lotuka and others regardless their size.

We're encouraged by the stance once taken by Sudanese dictator Omar Bashir who in the past promised to honor the verdict of Southerners. But as things go, Bashir did not honour his promises.

To us, freedom of South Sudan is the stepping stone for the freedom of Abyei, Nuba Mountains and Darfur. What agonizes to the bone is what BBC recently reported, if it is true, that Southern Sudanese new regime promised Bashir not to support Darfur rebels. This is tarnishing the good name and promise this 54the new nation has. If other countries supported and helped SPLA what is wrong with helping Dafuris? Is this better than thou or reporting out of context?

Obviously, some can assert that when SPLA was fighting Khartoum, Darfur was in bed with Bashir thanks to his propagation of Islam. They, so too, goofed. They need to be forgiven.

I vividly remember the words of the late John Garang de Mabior as if he said them just yesterday . He was addressing the war prisoners from north and some government soldiers from Darfur.

He told them that what they were fighting for was not Islam but criminality dressed in the good suit of Islam. He went further as saying that once north is done with SPLA would turn to Darfur thanks to being regarded as slave simply because of being viewed as black despite identifying themselves as Muslims.

And indeed, Garang's messianic prophecy was fully fulfilled even before his demise. For after signing the CPA, Khartoum turned to Darfur with new vim and zeal. To cut a long story short,what followed is history.

After all, Khartoum has always supported anti-SPLA elements to see to it that south does nary go solo. What's wrong with supporting Darfur?

We understand. Salva Kiir Mayardit and south Sudanese are mature and brave people. Being that is not the end in itself. They need others especially east Africa and other Sudanese states under siege. It is the right time for a new South Sudan to join their true brothers and sisters in the East African Community. In the EA South Sudan is likely to benefit even more thanks to the already established infrastructures to transports her produce. Also North still needs South the same way South needs North. You can choose a friend but not a neighbour. Therefore, there is no way any of the duo can live peacefully without depending on the other. It will be sheer stupidity for any of the duo to think she can live without another. Their border is still the same. Therefore, their peace and tranquility will depend on each other.

So too, Southerners need to abide by the law of reciprocity when it come to help others that are still brutalized by Khartoum whereas they are duty bound to help their brethren in Darfur. Their enemy is one and the same shall she not change. They all suffer the same anathema thanks to being black not a bit lighter like those Arab-duped northerners.

If, indeed, it is true that GOSS intends to expel Darfur fighters, this will indeed defeat its zeal of being an ideal new nation.

We urge south Sudanese not to tarnish their good image. In Africa we have a great saying that when you come across the stick that was used to whack your colleague you burn it. In this case, the adage tells it all. Don't entertain or spare the stick that whacked your friend or neighbour as it has been the case in Sudan.

To avoid wars and unnecessary insecurity in the region, North be told that it can not stop south even if it tries to manipulate some sections to revolt against it. Importantly, the leaders of south should see to it that they embark on judicious manner of running this new nation. Tribalism, nepotism, corruption and the likes are not going to help except to give north the weapon to sabotage this young nation. East African countries and other reasonable neighbours need to come in and see to it that South Sudan is not relegating back to anarchy and conflicts.

More on tribalism, the hell that has already broken loose in Burundi and Rwanda should hammer a lesson to them shall they think one tribe can take it all.

In sum, to know how south is more crucial to north than north is, look at the accompanying map and decide where real life lies. North needs south more than south needs north. So whatever north is promising not just because it is willingly. It is just because she has her back on the wall.

Source: The African Executive Magazine July 13, 2011.

LOWASSA NAYE AFANYA MAAMUZI MAGUMU

Katika makala ya wiki iliyopita tuligusia japo kwa ufupi udhaifu wa waziri mkuu aliyeachia madaraka kutokana na kashfa ya Richmond. Edward Lowassa. Kashfa hii ililiingizia taifa hasara ya zaidi ya dola za Kimarekani 170,000,000 ukiachia mbali kutumbia kizani kwa miaka sasa. Kiasi hiki kwa taifa maskini kama letu si pesa ndogo.

Pia ni kiasi kikubwa sana cha hasara kusababishwa na mtu mmoja kwa maslahi yake binafsi. Je ni mangapi yaliyofichika ya mtu huyu ambayo yalilisababishia taifa hasara? Je Lowassa hapa naye hapaswi kufanya maamuzi magumu na kuyatoboa, kukiri na kuomba msamaha kabla ya kuanza kutuaminisha kuwa ana uchungu na taifa hili alilochangia kusambaratisha? Kwa wanaokumbuka wajumbe wa Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe walivyosema kuwa kuna mengine waliyaacha, atajua tunachomaanisha. Je hii ndiyo sababu ya Lowassa kuachia ngazi kirahisi na kutotaka kujitetea kwa kujua wakitaja yote ataumbuka zaidi?
Kutokana na ufinyu wa nafasi, tumelazimika kurejea mada ya jana ili lau iwe changamoto kwa mhusika kutenda haki anayotaka wengine watende. Hapa lazima tutahadharishe. Hatumaanishi kuwa serikali aliyoishauri Lowassa kufanya maamuzi magumu ikiwemo kumshguhulikia yeye isifanye maamuzi magumu.

Katika makala ya leo, tutatumia fursa hii kukazia maoni tuliyotoa kwa kumtaka rasmi Lowassa naye aongoze kwa mfano kwa kufanya maamuzi magumu anayohimiza wenzake wafanye. Katika kufanya hivyo, ahakikishe anaeleza ukweli kuhusiana na yale yanayomhusu binafsi na kama kiongozi hasa uadilifu wake, malengo yake na yote katika yote ataje mali zake.

Tusingependa kurejea aliyosema Lowassa au tuliyoandika wiki jana. Lakini kama tutaangalia ukweli wa aliyosema Lowassa na nafasi yake katika kutekeleza ushauri aliotoa kwa wengine, tunagundua vitu vya ajabu. Kwa mfano, kuna maswali yanaweza kuibuka. Kwanini Lowassa awashauri wengine kufanya kile alichoshindwa kwa zaidi ya miaka kumi? Je alimaanisha nini aliposema ni heri kufanya maamuzi magumu hata kama ni ya makosa ukalaumiwa kuliko kutofanya maamuzi? Je maamuzi magumu ya hovyo kama Richmond ni bora kuliko kutoyafanya kabisa kweli au tunadanganywa? Maana kama Lowassa, kwa mfano, asingefanya maamuzi "magumu" kama ya Richmond, kwa kutofanya maamuzi haya angeweza kuokoa mabilioni ainishwa hapo juu. Tunajaribu kutoa hizo takwimu kuonyesha kuwa si kila maamuzi magumu ni muhimu. Je uamuzi wa kuingiza taifa hasara katika kashfa ya Richmond ni sehemu ya maamuzi magumu? Je kuendelea kuacha nchi iwe kwenye kiza ni maamuzi magumu? Je kutowafikisha akina Lowassa mahakamani si maamuzi magumu kama Richmond?

Kuna swali gumu ambalo linapaswa kuulizwa tena na tena. Kwanini Lowassa ameauona ugonjwa wa kutofanya maamuzi magumu hata kama yanastahili lawama baada ya kuachia ngazi? Na kwanini Lowassa amekaa kimya zaidi ya miaka 15 sasa tangu kurushiwa shutuma za awali za Mwalimu Nyerere? Tujikumbushe kidogo. Lowassa aliumbuka mwaka 1995 pale baba wa taifa alipoamua kumtolea uvivu akasema alikuwa amejilimbikizia mali nyingi isiyo na maelezo. Wakati ule Nyerere akinadi kile kilichokuja kujulikana kama kinyago cha mpapure ulikuwa ni wakati mwafaka wa kujibu hoja na si kunywea. Ni wakati ule umma ulipokuwa umewapokea Kikwete na Lowassa kama marais watarajiwa kabla ya mwalimu kuwakata makali. Tangu wakati ule Lowassa hajawahi kujitetea ukiachia mbali kuongelea kashfa hii inayoonekana kuwa ukweli mtupu kutokana na ithibati ya mwalimu na Lowassa kula jiwe. Hivyo basi, naye atende haki kwa kufanya maamuzi magumu kuelezea anachojua juu ya shutuma zake. Je ya Lowassa ni yale ya nyani kutoona nonihino lake au usanii mtupu? Bomu jingine la Lowassa ni kuendelea kuuhadaa na kuuaminisha umma kuwa alistaafu wakati alitimuliwa kutokana na kashfa ya Richmond. Kwanini naye asifanye maamuzi magumu akaondokana na huku kudanganya na kujidanganya kuwa ni waziri mkuu mstaafu wakati siyo?

Mbali na sifa ya ustaafu asiyokuwa nayo Lowassa, amekuwa akilipwa marupurupu ya ustaafu. Je Lowassa haoni huu ni wizi wa kawaida kupokea malipo asiyostahiki wakati akijua? Je Lowassa alipoishutumu serikali kutofanya maamuzi magumu hakuona kuwa huu nao ni uamuzi mugumu tena wenye lawama kumlipa mtu mamilioni ya shilingi kinyume cha stahiki na sheria? Je kwanini serikali haifanyi maamuzi mepesi yasiyotaka lawama yaani kusimamisha malipo ya Lowassa? Je kama Lowassa amesema aliyosema kwa kutaka aonyeshe alivyo na uchungu na taifa hili, ni kwanini haoni uchungu pale anapoliibia mamilioni asiyostahiki wakati alishasababisha hasara ya mabilioni na nchi kuingia kizani? Hapa hatujagusa hasara aliyosababisha Lowassa kwa kutumia pesa na muda wa umma kwenda Thailand eti kuleta wataalamu wa kutengeneza mvua ambayo nayo haikutengenezwa.

Hili la Lowassa kuendelea kulipwa marupurupu ya ustaafu lapaswa kuangaliwa sana kisheria na kimantiki. Kwanikuendelea kuvuna marupurupu ya ustaafu wakati muda aliokaa madarakani hauruhusu kisheria ukiachia mbali kutoelezea upande wa ukweli aujuao kuhusiana na kadhia hii ni ufisadi tosha. Je Lowassa alisema aliyosema kwa kusukumwa na kisasi cha kuwa nje ya ulaji au kuusaka urais kama inavyodaiwa na asikanushe? Kama kweli Lowassa anautaka urais kama inavyodaiwa na asikanushe sijui kama naye anaamini kuwa anweza kuwa rais wa taifa hili hapo baadaye! Je atufanyie lipi jema wakati uliyokwisha kututenda yanatosha?

Watanzania wanajua kuwa Lowassa ndiye aliyeanzisha mitandao ya kupakana uchafu kwenye uchaguzi. Je Lowassa yuko tayari kufanya maamuzi magumu na kutoa maelezo yake kuhusiana na hili huku akieleza tunavyoweza kutibu majeraha na madhara yaliyotokana na mitandao hii? Lowassa amezungukwa na maswahiba wenye kutia kila aina ya shaka. Wapo walioghushi hata shahada. Je kwanini hafanyi maamuzi magumu kuwashauri nao wafanye maamuzi magumu waachie ngazi?
Tumalizie mjadala wa leo kwa kumshauri Lowassa afanye maamuzi magumu kwa kuanza kutoa utetezi wa kashfa zake. Afanye hivyo kwa kutoa utetezi unaoingia akilini na uliosheheni ukweli na si siasa na kuukwepa ukweli. Haki Lowassa nawe fanya maamuzi magumu.Kwa kufanya hivyo utakuwa umetenda haki kwako binafsi na kwa watanzania kwa ujumla. Kazi kwako bwana Lowassa.
Chanzo: Dira ya Mtanzania Julai 12,2011.

Nimeamua kufanya maamuzi mepesi

KWA wale waliofuatia sanaa za wiki mbili ziliyopita watakumbuka: wasanii wetu walivyovunja rekodi kama si radio.

Tujikumbushe waliotumbuiza zaidi kiasi cha kupata fursa ya kuandikwa kwenye safu hii tukufu.

Wabunge wetu watukutu, sorry, watukufu walifungua pazia la sanaa kiasi cha kumzidi msanii mkuu aliyekuwa ughaibuni na mamisabu wake wakitanua kwa kodi za makapuku wa Danganyika bint Bongolalaland.

Jamaa hawa waishiwa walilianzisha kwa kutaka mshiko zaidi wa makalio bila kujali kuwa hata walevi wanastahili mishiko ya ukondoo, kuishi kizani, kuibiwa hata na mataahira na matapeli uchwara, kuishi kwa matumaini huku wengi wakijigeuza matapeli vyangu hata waganga wa kienyeji hata wale wanaojiita viongozi wa dini.

Waishiwa hawa waso haya kuondoa wale wa CHAKUDEMA hawakujua au tuseme walijifanya kutojua kuwa walevi wanastahili kulipwa posho ya woga, unafiki hata uongo. Yes. Kama si uongo kwa walevi kulalama ni kwanini hawachukui hatua kama kweli?

Hapa lazima tukumbuke. Walevi na watesi wao walistahiki kulipwa posho ya utegemezi na usanii wa kikaya. Je tatizo hapa ni ile hali ya kaya kudanganyika kiasi cha kuwa taifa la wasanii kuanzia chini hadi juu?

Hebu angalia hali ikoje mume amwibia mke, mke awaibia watoto. Mlevi anatumia pesa nyingi kuliko mapato yake na hakuna anayeuliza.

Wenye nazo nao hawataki kutaja mali zao. Hawataki hata wasio nazo nao watangaze umaskini wao. Mkuu wa kaya anaibia mabenki na wakurugenzi wa mabenki nao wanayaibia mabenki kwa kufuata mfano wake. Yeye anaiba na kuwekeza kwenye uchafuzi wa kisiasa wao uchafuzi wa kimaadili na madili. Nani anajali?

Hebu tuangalie usanii huu wa kitaifa. Matabibu wanawaibia wagonjwa maticha madenti madenti wazazi, viongozi wa dini wafuasi wao na kibaka kila apitaye. Polisi anaitiba wahalifu na muuza baa walevi.

Tuachane na usanii wa kikaya na kuenga wa mtu binafsi. Leo tutafungua pazia na Ewassa muishiwa wa Mundulia. Huyu bwana alikuwa mkubwa wakati fulani kabla ya kuharibu ofisi kwa ulafi wake.

Ajabu, pamoja na kung'olewa kwa kashfa bado analipwa marupurupu ya ustaafu utafikiri hakufukuzwa! Analipwa kwa stahiki ipi? Ajabu jamaa yake halioni kama ni tatizo.

Hiyo cha mtoto. Kwa sababu walevi ni wa kuliwa na kila jambazi mkubwa na mdogo,Nasikia jamaa bado ana ndoto za kuukwaa ukuu ili afanye makuu kuliko yale ya Richmonduli ambayo yaliwafurahisha walevi kwa kuwaweka kizani ili wazalishe vitegemezi kwa saaana tu.

Juzi Ewassa alitoa mpya kwa kumwambia mshirika wake mkuu kuwa afanye maamuzi mepesi. Alisema rafiki yake na genge lake wanaungua ungojwa uitwao kwa kitaalamu Decisive-Decisons Phobia (DPP).

Kwa ufupi, mtu anayeugua ugonjwa huu huwa na tabia ya kuchekacheka hata kwenye msiba huku akifanya vitu kama hamnazo. Mgonjwa wa gonjwa hili hatari kuliko ukimwi hupenda sifa na ukuu hata kama hana sifa wala udhu. Kadhalika, anayeugua ugonjwa huu licha ya kuanguka mara kwa mara, huishiwa kumbukumbu na aibu kiasi cha kufanya mambo ya ajabu kila mara.

Huweza kuahidi vitu ambavyo ukimuuliza kesho yake hakumbuki wala kujua. Muathirika wa DPP huishi kwa kujilisha pepo na uongo bila kujua kuna kesho. Hupenda kutumiwa na majuha na matapeli hasa kwa kumuahidi pepo zaidi hata penye moto.

Baada ya Daktari Ewassa kugundua ugonjwa wa rafiki yake na kumshauri afanye maamuzi mepesi kwa kumsafisha asifanye hivyo kutokana na ima kusahau au kusumbuliwa na DPP, aliamua kuutangazia umma siri ya siri ya swahiba yake kuwa anaumwa DPP.

Alifanya hivyo kwa kisingizio cha kuwapenda walevi wakati ukweli anawachukia kupita hata manonihino yake. Angewapenda angewaweka kizani bila kosa lolote?

Wengi walishangaa ugunduzi huu wa aina yake. Kwa mara ya kwanza ambapo nyani aliweza kuona kungule!Wengi walidhani Dk. Ewassa angekuwa mkweli na kuelekeza ugunduzi wake kwenye gonjwa lake liitwalo Illegal Wealth and Moneyphilia kitaalamu au (IWM).

Gonjwa hili likimpata mtu huwa mlafi kupita hata fisi na panya. Mwenye kusumbuliwa na gonjwa hili anaweza kuwatoa sadaka hata ndugu zake hata mama yake.

Kadhalika mwenye gonjwa hili huishiwa kumbukumbu na huwa haoni aibu hata akitenda mambo ya kuaibisha kiasi gani sawa na mwenye DPP.

Na hii ndiyo maana mara nyingi waathirika wa gonjwa hili huwa marafiki na baadaye kutokana na kutokuwa na kumbukumbu wala aibu hugeukana na kutishiana hata maisha. Mwenye kuugua gonjwa hili hupenda kuchuma kijambazi huku akijidanganya kuwa watu hawajui chafu yake.

Gonjwa hili ni hatari sana. Kuna kipindi hushambulia kabila zima kiasi cha watu kuwa waroho kiasi cha kuchukua hata dada zao ambao nao huwa tayari kulala na kaka zao mradi wapate kuchuma haramu iitwayo pesa au utajiri. Hapa jamaa zangu kule kilimani mnanipata bila shaka.

Hilo leo siyo inshue. Tundelee. Mwenye gonjwa la IWM naye kadhalika hupenda makuu kiasi cha kusahau ukweli. Gonjwa hili kwa mara ya kwanza liligunduliwa na profesa Juliyasi Mchonga Nyereire kutoka chuo kikuu cha Mwitongole kule Kusoma Mara kwa mara.

Kwa vile Profesa Mpayukaji ni gwiji wa magonjwa ya akili na roho, ameamua kufanya ugunduzi wa aina yake. Ugunduzi wenyewe una matokeo yafuatayo:

Mosi mgonjwa wetu wa IWM atapata kichaa baada ya ndoto zake za Alinacha kustukiwa. Kadhalika mgonjwa wa DPP hatakuwa tayari kukubali ushauri wa mgonjwa wa IWM kwa vile anajua anasumbuliwa na ugonjwa wa akili kama wake.

Kimsingi majaribio ya kisayansi yanaonyesha kuwa wagonjwa hawa wawili watachanganyikiwa na kuchanganyana hadi wavuane nguo hasa kuanzia tarehe 10 Julai wakati ambapo mwezi utakuwa mchanga kiasi cha kusumbua akili za wagonjwa hawa.

Pia utafiti umeonyesha kuwa waathirika wa magonjwa haya mawili ni hatari sana kwa kaya kuliko hata ukame na mafuriko. Maana huwa wanatumiwa na kunguru kuchuma na kuibia walevi.

Kutokana na uzoefu wa siku nyingi, Profesa Mpayukaji napendekeza kuwa wagonjwa wataweza kupata nafuu iwapo watakubali kufanya maamuzi mepesi ambayo ni kusema ukweli kuwa wanaumwa sana na wanahitaji msaada toka kwa waganga wa kweli na matapeli pia.

Ikitokea wagonjwa wakagoma au kujifanya wamesahau kufanya maamuzi mepesi basi walevi hufanya maamuzi magumu na kuwatia nari mchana kweupe.

Hivi ule msafara si wa Njaa Kaya. Ngoja niokote mawe nifanye kama walivyofanya akina Twambombotununu kule Mbe way. Naona kinokia kinaanikiza. Mbona namba kama ya Ewassa! Hello Eddie, How are you my friend? Ushaamua kufanya maamuzi mepesi na kuweka mambo hadharani? Kwa kheri!

Chanzo: Tanzania Daima Julai 13, 2011

Monday 11 July 2011

Hizi ni Trust Funds au vichaka vya pesa za wizi?


Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Salma Kikwete (kulia) akizindua nembo ya (HMT) kwaajili ya uzinduzi ya Taasisi ya Hassan Maajar Trust na kuanzisha kampeni ya kusaidia kutokomeza uhaba wa madawati mashuleni jijini Dar es Salaam (juni 11.2011) (kushoto) ni Makamu Mwenyekiti wa Taasisis hiyo Shariff Hassan Maajar ,akifuatiwa na Mwenyekiti wa HMT Balozi Mwanaidi Maajar.

Kama maelezo hapo juu yalivyo, kuna jambo jema linafanyika ingawa nyuma ya wema huu kunaweza kuwa uchafu wa kutisha. Je tatizo la madawati nchini litaondolewa na taasisi za watu binafsi tena zenye kutia shaka?
Huyu Maajar ni nani? Analipa kodi vilivyo? Ni msafi kimaadili? Ametanganza mali zake na kueleza alivyozichuma? Wahusika wangejibu maswali haya muhimu kabla ya kutuaminisha kuwa wana nia nzuri na taifa letu. Watakuwaje na uchungu na taifa iwapo nao ni sehemu ya waliosababisha hali hii ya umaskini?

Maswali haya yanasababishwa na ukweli kuwa mke wa Hassan Maajar ambaye ni balozi wetu Washington Mwanaidi anatuhumiwa kuwa mmojawapo wa wanasheria waliosaini mikataba ya uhamishaji pesa ya wizi ya EPA.Je huyu Hassan Maajar ni nani na anafanya kazi gani? Tungepewa CV yake na historia ya utendaji wake kabla ya kuaminishwa kuwa mhusika na mkombozi wakati anaweza kuwa wale wale watokanao na urafiki, kulipana fadhila hata familia.

Mtuhumiwa hajawahi kukanusha wala mazingira yaliyomfikisha kwenye cheo hiki cha juu kisiasa hayajulikana zaidi ya mchirizi kuelekea kwenye wizi wa EPA ambao uliwezesha serikali ya sasa kuwa madarakani kwa kuwahonga wapiga kura mbali na kuchakachua kura.

Hata ukitazama historia ya anayefungua taasisi hiyo unaona mauzauza ya ufisadi. Kwani naye ana kampuni yake ya mfukoni ya WAMA inayotumia mgongo wa ikulu kuchumia mali. Nilishwahi kuuliza: kama NGOs za wake za wakubwa zilianzishwa kutokana na uchungu wa zinaodai kuwapigania, kwanini zianzishwe baada ya waume zao kuingia madarakani?
Turejee kwa Maajar. Je ana udhu na uaminifu kuweza kusaka misaada kwa ajili ya madawati na kuifikisha au kujitafutia sifa na ulaji na pa kufichia pesa ya ufisadi. Je anatafuta kutoa huduma au kukwepa kodi kwa kujifanya anahudumia jamii? Kazi kwenu.

Thursday 7 July 2011

Ni ujinga kuruhusu posho za makalio


SIKU hizi narapu kuonyesha mzee mzima nisivyo limbukeni kama waishiwa.

Leo nimeamka na Mwenembago akinihimiza niwakabili waishiwa wala ubuge ili niwaonye waache mchezo mchafu kutuibia njuluku zetu kwa kujilipa posho za makalio au ’sitting allowance.’
Rafiki yangu Msomimkatatamaa huziita hizi posho za majungu au rumour mongering allowance. Mie naseme hizi ni posho za ufisadi. Kwanini mtu akae tena kwenye mikochi ya bei mbaya huku akifaidi viyoyozi alipwe badala ya yeye kulipia maraha haya?

Wakati mkijilisha pepo na matanuzi wenzenu wanatanuliwa na dhiki. Je mnawawakilisha wao au matumbo yenu? Kwani tulipowachagua tuliwaambia mwende kusimama? Mbona wafanyakazi wengine, tena wa haja, hawalipwi hiyo mishiko ya makalio? Kwanza, mnakosea kuita posho ya makalio. Mbona akina Steve Wahasira wanauchapa usingizi kwenye mjengo na hamuwapi mshiko wa usingizi?

Kesho mtakuja na usanii mwingine wa kutaka posho za kulala au sleeping allowances. Hapa bado posho za kupayuka au shouting allowances. Pia nashauri zilipwe posho za kumshangilia madam Microphone na za kuogopa kutoa hoja za mashiko au cheering and fearing allowances.

Wenzenu pale kwa nyayo wanalipa kodi wakati nyinyi mnaendela kucheza makidamakinda! Wenzenu hawana vyanzo vya umeme lakini bado hawana mgawo wakati nyinyi mnavyo mmevikali na kukalia ujambazi mbuzi!

Wenzenu wamepiga maarufu ushambenga wa kutumia mashangingi nyinyi mnazidi kujiongezea mishiko kwa kuwaacha walevi wanyongwe na umaskini! Iko siku iso jina hiyo mishiko itawatokea puani. Shauri yenu. Mwenye akili na atie akilini na mwenye masikio na asikie unabii huu wa kweli.

Kwanini waishiwa wetu (wanaopenda kuitwa waheshimiwa wakati hawanayo) wanapenda kujisahau? Mkienda kwenye kupitisha mikataba ya unyakuzi mnayoiita uwekezaji mnapewa kitu kidogo na kitu kikubwa.

Mkiingia mjengoni mnapitisha kila upuuzi kama ule wa Mstaafu Mukulu aliyeleta libajeti la uongo. Nani kawaroga nyie waishiwa ambao ufisadi umewekwa mbele yenu lakini bado msiouone? Na walevi nao sijui wataacha lini ulevi? Angalieni wenzenu wa Senegali.

Juzi juzi wameamua kuingia mitaani na kupambana na shirika la kiza la nchi yao baada ya kuwaweka kizani kwa saa 48 tu. Nyie mmewekwa gizani sasa ni miaka kumi lakini bado hamuamki! Kumbaff nyote.

Walimu, madaktari na wafanyakazi wengine wanakosa mishahara nyie mnazidi kujirundikia miposho ya uongo na ukweli! Ni ulafi na upogo kiasi gani? Hamuona jinsi mahospitali yalivyojaa magonjwa badala ya madawa? Ama kweli mchoyo hana rafiki na rafiki yake ni tumbo lake.

Inatisha kuona huko madongo poromoka mtokako watoto wanakalia mimawe kama manyani wakati nyingi mnaongezeana posho za makalio. Lipeni basi posho za akili kwa walimu na madaktari badala ya makalio yenu.

Msiseme nawatukana. Hasha, nawapa ukweli ambao wengi wameshindwa kuwapa. Mnapata wapi jeuri ya kujilipa posho za makalio wakati wale mnaodai kuwawakilisha wakifa kwa magonjwa ya senti kumi? Hamjui kiza kinafanya wakaliane na kulaliana na kuongeza utitiri watoto ambao hapo baadaye watateswa na uchoyo wenu pia akili zao zitajaa kiza kutokana na kukaa kizani tangu tumboni?

Hapa lazima niwapongeze CHAKUDEMA kwa kuliona hili hata kama kwenye kambi yao kuna fisi kama lile fisi la kisukusi Joni Kibuda. Walevi hawawezi kuendelea kubeba wezi wanaojipa utukufu na uheshimiwa wakati ni wizi wa kawaida. Never, things must be changed. Why should they own everything and give us usufunctuary as the only rights for us? Thubutu yako! Patachimbika bila jembe na patakuwa hapatoshi.

Mnajilipa posho ya makalio kwa utajiri gani iwapo hata kodi yenyewe hamlipi? Muulize kiranja wao kama analipa kodi. Muulize hata baba yao kama ametaja mali zake. Wanaogopa nini kama si kuumbuka walivyo majizi ya kutupwa yaliyojificha nyuma ya madaraka? Msiseme natukana. Situkani. Kama kusema ukweli ni matusi basi natukana.

Nami napaswa kupewa posho ya Kunena ukweli au truthtelling allowance. Kama wao wanapeana posho za majungu, kwanini mie nisipewe ya kupasua jipu? Mimi ni daktari wao ni wagonjwa. Wao wanauhitaji ukweli wangu ila mimi siwahitaji kwa lolote.

Nani anahitaji mipanya kwenye nyumba yake? Nani anahitaji nyani kwenye shamba lake? Mpumbavu huyo tena hayawani mtu. Basi nasi walevi tulipwe posho ya masikio kwa kusikia urongo wenu kila siku.

Nawapa taarifa kuwa Kijiwe kinajiandaa kuja mjengoni kufanya mapinduzi matakatifu hata kama ni kutumia mawe na nyundo kama kule kw akina yakhe.

Tutahakikisha kila mbunge na kiongozi awe hata wa nyumba kumi anataja mali zake na jinsi alivyozipata bila kujali yeye ni rais au rahisi.

Kwani mlichaguliwa kufanya nini huko mjengoni kama siyo kukaa na kujadiliana? Sasa mnalipwa kwa kazi gani?

Tukikotaka hapo tunakwenda kwenye serikali za mitaa zenye mahesabu mabovu na kuchukua allowance ya corruption. Hapa tunachukua kitu kikubwa na kitu kidogo bila kujali ukubwa wa kosa wala wilaya mradi sisi tuchukue chetu mapema. Nani anajua kama kwenye uchafuzi ujao tutarejea kwenye maulaji kutokana na kiama chetu kuboronga kuliko chochote barani afurika?

Hivi kweli wabunge kama Rwakatarehe mwenye shahada ya kugawiwa wanaweza kurejeshwa hata kwa nafasi za ubwete? Mliinyaka aliyotoa kuwa alijaza mifomu ya madili shetani akainyakua. Hivi kuna shetani kama mama huyu nunga anayehadaa wenzake kuwa anaweza kuwapatia waume kwa maombi? Hayo tuyaache.

Acha nijiimbie wimbo wangu wa barua tena.

Mie mwenzenu leo niko mashakani
Nikiangalia nje kaya ikizani
Nikiangalia naona wezi mjengoni,
naamua kuandika hii barua

Barua hii inanisikitisha
Barua hii inanisononesha
Barua hii hebu chukua usome.

Nilimchagua fulani aniwakilishe mjengoni

Akaenda kule akaanza misheni
Naye akaamua kujiwakilisha
Akaanza naye kugombea mishiko .

Nimeamua kuandika barua hii
Barua hii hebu chukua usome
Barua hii kweli inasikitisha barua hii kweli inasononesha.

Hivi lile shangingi si la muishiwa? Acha nimsogelee nimzabe viba… we koma.


Chanzo: Tanzania Daima Julai 5, 2011.