The Chant of Savant

Sunday 30 June 2013

Mzee Pinder, hold your shibboleths


 
 
When Big Minister Mizengwe Pinder ‘courageously’ encouraged cops to keep on brutalized boozers, many were saddened, sickened and shocked beyond explanation. They said that he did so pointlessly and unreasonably.  Again, this is not our take on mzee Pinder. We’re reporting what boozers thought of him. Some interrogated his way of doing things. Others were baffled by his snap judgment.
Those of us who studied heuristics, the science of experience-based techniques for problem solving; we’d an answer already. In what we call anchoring or getting used to what one is used to, we tend to judge things based on what is in our memory. Methinks, after the govt got away with many killings perpetrated by cops, came to the conclusion that it can get away with everything. It got away with EPA, Richmonduli, Meremeta, Mwananchi Gold, SUKITA and much more stinking stuff. So too, looking at mzee Pinder’s political resume and the way he came to being premier after Eddie Lowassa messed, we’re able to know why he uttered such so-called irresponsible things.
To jog your memory, as boozers, “we remember everything spoken during our kanywaji parliament.” This is how one boozer put it. He went on, “Pinder apart from messing when he’s Minister for Regional Administration and Local Governments, kept on showing how amnesic he is. He once rejected a shangingi so as to give it to another person to use. He pointlessly contradicted his snake oil of saving pauper’s dosh the same way he did recently in Dom when he threw such an expensive party for walaji.” Usanii mtupu!
A big laughter,  and he goes on, “ He once told a lie before the Mjengo when he said that in January 5, 2011 Arusha police killings there was no foreign national while actually there was one Kenyan Paul Njuguna Kayele.” Such utterances caused a stir in the house thereby causing Arusha Town MP Godbless Lema to be kicked out after asserting that mzee Pinder told a lie something Anna Makidamakida did not like.
Another one chipped in, “So too, it’d be known that mzee Pinder had nothing to care about or lose to say what he said given that those killed and beaten were opposition guys. This is the type of rulers we now have.” He went on, “Do you remember how he assured the world he’d take on Dowans that ended up taking him in?”
 Boozers were sickened to see the person they trusted immensely turning against the same people he swore to protect and serve. Up till now we can’t see the ethos, logos even pathos of mzee Pinder’s ‘wisdom’. What makes things worse for him so as to self-dressed down is the fact that the man is a lawyer who’s supposed to know and uphold the law to its spirit and letter.
When mzee Pinder ordered ndata to beat boozers shall they agitate for their rights, one boozer said that this was a sign of aging badly. The other said that mzee Pinder was suffering from malady known as kuvimbiwasis and kulewasis so as to become a wino. This is not our take though. Again, why did mzee Pinder decide to dress down?  Who knows?  Had the victims been his fans he’d have announce a national mourning week and those felled would be made martyrs.
 Imagine. If what mzee Pinder said would come from the opposition telling their members to beat whoever attack them. Obviously, it’d have been branded terrorism and anarchism. Again, from mzee Pinder’s philosophy we learn that there are those who are above the law-those allowed to beat, torture and kill others without being brought to book as it happened in Kibanda’s, Ulimboka’s and Arusha’s cases. Sadly though, this way we’re letting our hunk go to the dogs. Mzee Pinder is lucky. His boss, mzee Jake Kiquette, seems to be at home with his militarism. Boozers were shocked to learn that when terrorists attacked innocent earthlings he swore to protect, he went on enjoying in the country of Brits. To add salt to the injury it came to light that they guy had a ‘very serious business’ of visiting Football Clubs posing for photo-ops while the so-called his people were perishing in the hand of his cops! Such sacrilege needs a great deal of negligence, ignorance or the courage of the mad. If this is the crop of the rulers we’ve, surely, we must brace ourselves for more troubles. If anything, this is vacuity and leadership vacuum that needs to be filled urgently.
Needless to say, mzee Pinder’s hit hard when he jabbered; boozers congratulate him on being able to unearth his true self that he hid for long. Some boozers said that we need to thank mzee Pinder instead of blaming him. First of all, there’s no any of his relatives among those who were felled in Arusha. Secondly, those who died were not the members of his party despite the fact that they were Tanzanians he cares less about. Thirdly, this is the way mzee Pinder shows his love of law and tranquility even if they are enhanced by breaking the law and through carnage and violence. Uhuni mtupu!
Mzee Pinder loves Boozers so dearly that he dispatched his cops to ‘massage’ them. One boozer left us in stitches when said that when Pinder’s regime promised better life for all they meant bitter life for all who are earthlings but not bigwigs. After all, brutality’s become another policy mzee Pinder‘s regime that’s turned boozer into experimental objects. Refer to many killings perpetrated by cops. Refer to oft harassment the opposing parties have been subjected to since the inception of pseudo multiparty democracy that has become 'demoncrazy' if not a crazy demon. Had it been democracy, do you think Jake’d have gone on enjoying in Brit land while walevi were dying? Think again.
Source: Thisday July1, 2013.

Saturday 29 June 2013

Walevi kukata kanywaji na Obama

  Obama beer 1
We’ve a dream. Yes we’ve a big dream of changing the kaya. We’ve a dream to meet with Black Obama and talk business and not politics. We will taaalk and taaaalk and taaaalk.  Walevi have a dream. Lazima kuongea kimombo kuonyesha usomi wetu usio wa kughushi kama akina Lukuwi na Nchimvi.
 
Baada ya kuzinyaka kuwa rais Black Obama anakuja kutembelea kaya, walevi hatutaki kuachwa nyuma.  Tunajua jamaa ni mwenzetu anapenda sana kanywaji na tufegi ingawa tuliambiwa siku hizi ameacha.  Kwa vile mkiti nilsomea kwao Hawaii na dingi wake, najua akitoka ku-surf lazima apate kanywaji kwanza. Tumemuandalia Boha, Rubisi, Gwagwa, Nkojo, Mnazi, Ulanzi, mapuya, kangara, chibuku, common na madude mengine mengi. Tumeadaa party ya kufa mtu ila msigara mkubwa hatutapiga.  Maana FBY walisema kuwa hawapatani na kitu hii. Yes we can. We indeed can realize Bongo dream of maisha bora kwa wote.
Hivyo, nasi kama walevi wa siasa, tumepanga kumpa kampani bwana ndogo Obama ili akiondoka akumbuke siku moja aje kutupa tafu akiwa nje ya White House. Ila kwenye party yetu Joji Kichaka hatakanyaga. Tutamsusa kama tulivyomsusa rais wa Uchina kutokana na kutujazia machinga. Hata huyu wa Bangla anayekuja hatutakutana naye maana ni apeche alolo anayetafuta pa kubwaga wazamiaji wake.
  Tuna mipango kamambe ya kuhakikisha huyu Jadwong anakumbuka kuwa walevi ni mali kuliko walevi wa siasa. Onyo: Hatutatumia pesa ya walevi kujilisha upepo kumuandalia partya bei mbaya. Tumepanga tumpeleke Uwanja wa Fisi ambayo tutaibadili jina iwe White House ili apate mapupu kidogo na utumbo lau ajue asili yake. Pia, hatutamtumia Obama kuibia walevi kwa kisingizio kuwa pesa yote imetumika kumkirimia. Wala hatutajikanyaga kwake bali tutampa kampani na maongezi ya kikubwa yenye kuonyesha usawa kama walevi na wapenda haki. Yes we can and indeed we should and we will.
Baada ya kukutana na Jadwong Madwong Obama lazima tumwambie kuwa we have a dream awambie ombaomba wavaa masuti waache kunyanyasa ombaomba wavaa manyang’umyang’u kama walevi. Kwa wasiokinyaka kidhuluo Jadwong maana yake ni mtu mkubwa na Madwong ni mkubwa zaidi na mwenye hadhi kama mimi na Obama na Diba Mandela. Jadwong kwa sasa tuko wachache. Kwenye kaya yetu ni mimi pekee nimebakia baada ya Mzee Mchonga bin Musa wa Burito kurejesha namba. Hayo tuyaache. Acha niwape yale tutakayompa Jadwong Madwong mwenzangu:
Mosi, tutampongeza kushinda uchaguzi bila kuchakachua wala kutoa ahadi za kijinga na kitapeli.
Pili, tutawambia fika kuwa Bongo dream imehujumiwa na wahuni na mafisadi fulani kwa kuiba njuluku na kuzipeleka Uswazi aka Uswisi huku wengine wakifunja kwenye kuzurura badala ya kukaa ofisini kutumikia walevi.
Tatu, tutamwambia Obama mambo ambayo baadhi ya wahuni wanaficha na hawataki ayajue. Kwa mfano, tutamwambia kuwa walevi wamesikinishwa kiasi cha kuishi kwa kutegemea ofa na misaada uchwara wakati wana mikono na akili. Hivyo, sisi hatutampiga bomu la njuluku bali kumshauri tufanye biashara kwa usawa na haki.
Nne, tutampa laivu kuwa lazima tufute mikataba yote ya kijambazi ya uwekezaji katika madini ya walevi.
Tano, tutawachomea wahuni wanaotishia maisha na haki za walevi kama wale waliowamuru ndata kutupiga, kututeka hata kutuua kwa vile tunachukia uovu na ujambazi wao.
Sita, tutamshauri next time awe makini. Kabla ya kuja huku Uswekeni ashauriane nasi tumpe picha halisi ya kinachoendelea ili asijikute siku moja anakula sahani moja na wezi, majambazi, wauaji, watesaji  wababaishaji hata wahuni wa kawaida kama ilivyomtokea Tommy Blair wa kwa Mother alipopiga picha na akina Mwamali Kadhaffi wa Kashafi aliyenyotolewa roho kule Libya.
Saba, tutamshauri kuwa next time asije kwa mikwara na mibunduki na mimeli.  Maana huku watu wanalipua wapingaji kama ilivyotokea kule Arusha. Pia asiwe na hofu kwa vile sisi tutampa ulinzi wa mwagwiji wa karate wanaoweza kumeza bomu na lisilipuke.
Nane, tutashauri akija kutupa tafu asitangaze ili kuepuka kuvuruga shughuli za uzalishaji mali kama vile kufunga anga, barabara, mitaa, hata kusumbua watu bila sababu ya msingi. Maana, nilipokuwa Washington sikuona mikwara kama niliyoiona huku Uswazi ambapo kujipendekeza na kujikomba hata kwenye mambo yasiyomhusu kumezidi.  Juzi wakati nikikata kanywaji alitokea ndata aliyetaka kunisachi akidhani eti nilikuwa na bomu la kumdhuru Obama asijue ni mshikaji wangu damu. Baada ya kumkunjia kama kata sita hivi za karate ndata alitoka nduki kama kibaka. Nilimkimbiza na kumkamata na kumuonya asirudie kudhani kila mtu ni fala mwenzie. Hayo tuyaache.
Pia wake zetu wamepanga kum-surprise Mchele bint Wali wa Obama kwa kumuandalia bonge la party ambapo watamshukuru kwa kutowaibia wenzao wa Umarekanini kwa kuunda NGO ya ulaji. Juzi niliwafuma wakipanga mikakati kwenye kikao chao cha maandalizi. Nilimsikia mke wangu akisema lazima wampongeze Mchele kwa kupiga kitabu na kuacha ubabaishaji wa kutumia ulaji wa mumewe. Alisema kuwa amewapa motisha wa kupiga shule na kuwafichua waume zao watakaojaribu kughushi shahada kama wale mawaziri walioghushi Ma PhD. Nimekumbuka. Pia tutamwambia apige marufuku vyuo vya uchochoroni huko Umarekanini vinavyotoa shahada feki kwa vihiyo na waharifu wetu mabingwa wa kughushi wakitumia madaraka ya walevi. Hapa lazima watu kama Bill Lukuvi, Makorongo Mahanga, Marry Nagu, Deodorant Kamala, Emmy Nchimbi na wengine watetemeke. Soma taratibu wasiinyake wakahujumu mpango wetu wa kuwachoma kwa Obama.
Turejee kwenye shinikizo letu kwa Obama, walevi tumepanga kushitaki lile genge liitwalo Coalsced Criminal Mob (CCM- usichanganye na Chama Cha Mapinduzi maana CCM zipo nyingi). Lazima tulishitaki kutokana na ujambazi na undavandava linaofanya kwa walevi hata matumizi mabaya ya ndata kutunyanyasa wakati wakiwalinda waharifu kama vile wauza unga, majambazi, mafisadi. Hili genge la kimafia limekuwa na nguvu kuliko hata serikali ingawa inaonekana kutojua lilipo na linavyofanya kazi.
Tisa, tutambana Obama azuie wazururaji kwenda kutanua majuu kwa njuluku za walevi kama walivyomfanyia yeye asiende kutanua kwenye mbuga za wanyama. Uchumi muhimu yawe! Tutasema wazi wakiomba kwenda Umarekanini awanyime viza na kuwauliza wanakwenda kufanya nini wakati wana matatizo kibao ya kutatua.
 
Kumi, nimenusa harufu ya Air Force One.  Acha niwahi uwanja wa ndege kumpokea Obama.
Welcome to the nether world of wonders such as corruption, nihilism, bootlicking, nepotism, hooliganism especially committed by Pindaboys and whatnot.
Chanzo: Nipashe Jumamosi Juni 29,2013.

Thursday 27 June 2013

Tamaa, upofu, uroho na roho mbaya vitaliangamiza taifa

MATUKIO  ya kushambuliwa kwa mkutano wa CHADEMA kule Soweto Arusha na kupigwa na kuumizwa vibaya kwa wananchi wakiwamo viongozi wa chama hicho hayawezi kupita bila kulaaniwa kwa sauti kali. 
Tanzania ilisifika kuwa kisiwa cha amani. Kwa sasa bila shaka inaanza kusifika kama kisiwa cha vurugu, ubabaishaji, ufisadi, kujuana, kulindana, kukomoana  na hata kudhulumiana.  Hivi ni dhuluma kiasi gani kwa kikundi fulani chenye kuamini kuwa madaraka ni staili yake kuwaumiza na kuwahujumu wananchi wasio na hatia? 
Ni upuuzi na ukosefu wa akili kiasi gani kwa kikundi kidogo cha watu kujiona kama ndicho chenye kujua na kumiliki kila kitu hata ikiwamo akili?
 Je kwanini sisi kama taifa hatutaki kujifunza toka tawala ovu na zandiki zilizofanya haya lakini bado zikaangushwa kwa aibu na kejeli? Walikuwapo akina Muamar Gaddafi (Libya), Hosni Mubarak (Misri) na Saddam Hussein (Iraki). 
Waliogopewa sana na kuamini kuwa wao na waramba viatu wao waliumbika kuwatawala na kuwanyonya wengine wasijue arobaini yao ilikuwa imewadia. Kwanini hatupendi kusoma alama za nyakati kuwa wakati tulio nao si ule wa mwaka 47 ambapo kikundi kidogo cha watu kingeweza kuteka taifa na kulitenda litakavyo? Ni vizuri kutambua kuwa vijana wa sasa si wa kuburuzwa kutishwa wala kuchezewa mahepe.
Ni ajabu kuwa tumegeuka taifa la wakandamizaji na wababaishaji kirahisi hivi. Nani hajui kuwa kwa sasa tumo msambweni tukielekea kuzimu ambapo ulaji umechukua nafasi ya huduma? 
Leo tunaambiwa kwa mfano deni la taifa linazidi kuumka huku wahusika wakitumia kwa hisrafu na kuiba kama vile hakuna kesho. 
Nani hajui, kwa mfano, kuwa hoja ya  kurejesha fedha zilizofichwa Uswizi imeuawa kwa vile wahusika ni wakubwa au marafiki zao. 
Je ni kosa kuyashupalia haya? Je ni kosa kudai ukombozi? Je kupiga mabomu mikutano au kukata watu mapanga kwa vile wanapinga dhuluma ni jibu? 
Hata wenzetu wanaolia na kukumbuka maafa kama Rwanda walianzia huku. Hakika hawa walipaswa kuwa somo kwetu.
Inashangaza kuona kuwa Tanzania imegeuka nchi ya kulipuliwa na mabomu ya kigaidi na hakuna anayekamatwa kwa vile wahusika wana watetezi wao wenye mamlaka. Tunasema hivi si kwa chuki wala uchochezi bali kujibu kilio kilichotolewa na wahanga kule Arusha kuwa walimuona aliyerusha bomu na kutaka kumkamata lakini polisi wakamkingia kifua na kumtorosha. 
Je kama polisi na huyu gaidi lao si moja walimtorosha ili iweje kama siyo kuficha ushahidi? 
Laiti wangemtorosha kunusuru uhai wake ili ahojiwe na kuwataja wenzake ingeingia akilini. Ajabu badala ya kushughulikia kuwasaka waliolipua bomu, polisi inawashughulikia CHADEMA. 
Hali ni mbaya na yenye kutia kinyaa hadi kufikia baadhi ya walevi wa madaraka kusema eti waliolipua bomu ni CHADEMA ili kupata huruma ya wananchi. Hoja dhaifu  na ya aina yake kwa uhovyo. 
Yaani CHADEMA wawaue viongozi wao ili iweje na hiyo ‘huruma’ iwasaidieje kama siyo utaahira wa aina yake? Waingereza wana msemo : Go tell it to the birds. 
Tunadhani badala ya kuingiza siasa kwenye mambo nyeti na mazito kama mashambulizi haya ya kigaidi, serikali iwajibishwe kutuletea wale waliotenda uovu huu. Inashangaza kuona Watanzania wanageuka mateka kwenye nchi yao huku wakiuawa na kuteswa kutokana na kukataa kwako kulala kitanda kimoja na uovu. 
Wako wapi waliomteka na kumtesa Dk Steven Ulimboka na Absalom Kibanda? 
Wako wapi waliomuua Daud Mwangosi? Kwani hawajulikani?
 Je nani anahangaika kuwakamata iwapo walitumwa kutekeleza amri za wakubwa zao walioishiwa? 
Je hili ni jibu na hali itaendelea hivi hadi lini? 
Tumegeuka taifa la kulalamika lalamika. Ni jukumu la wananchi kujiletea ukombozi na kuhakikisha hatima zao zimo mikononi mwao. Tuwawajibishe watawala wetu waache kutuchezea.
Hakuna kitu kilitushangaza kama matamshi ya kizembe  kama yale yaliyotolewa na Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) aliyekaririwa hivi karibuni akirusha lawama kwa wahanga akidai kuwa kumekuwapo na tabia ya wananchi kuchukia jeshi la polisi. Lukuvi anayetuhumiwa kughushi vyeti na sifa za kitaaluma ameonyesha ukweli kwa mada hii. 
Hivi Lukuvi hajui kuwa wananchi wanachukia jeshi la polisi kutokana na kushindwa kuwahudumia?
Ameshindwa kutambua kuwa wananchi wanaona kila uchao  mauaji na manyanyaso yanayotekelezwa na polisi huku wakilipwa kwa kodi za hao hao wanaowaua kama Swala mbugani? 
Imefikia mahali hata wanyama pori wana amani kuliko Watanzania. Je Lukuvi alitaka wananchi wawapende polisi kwa kuendelea kuwaua na kuwadhulumu? 
Je huku ni kufilisika kimawazo kiasi gani? Wengi walidhani kuwa wasemaji ambao ni makada wa chama tawala angalau wangekuwa wastaarabu wakatoa hata salamu za rambirambi badala ya kutonesha donda. 
Kwanini hawajifunzi toka nchi ambapo vyama tawala vilipigwa teke na kutokomea kwenye kaburi la sahau?
Tuhitimishe kwa kulaani kitendo cha wanasiasa uchwara kutetea ugaidi kwa vile unawanufaisha wao baada ya kuishiwa kisiasa. 
Hata hivyo wafahamu kuwa Watanzania si mataahira wala mawe yasiyobadilika. Kuna siku yaja watalia na kusaga meno. 
Kama taifa na jamii tusipoangalia tamaa, upofu, uroho na roho mbaya vitaliangamiza taifa. Tafakarini.
Chanzo Dira Juni27, 2013.

Tuesday 25 June 2013

Brewing Feuds: Will the EAC Survive?

Those who bother to go back to history books will agree with us that bad blood between former Tanzania President Julius Nyerere and Idi Amin, former Uganda President in 1977 stalled the then EA community that aimed at unifying east African countries.
Of late, the bad blood between Presidents Jakaya Kikwete and Paul Kagame is likely to make history repeat itself. It all started when Kikwete urged Rwanda to negotiate with Forces Democratiques de Liberation du Rwanda (FDLR) rebels so as to move forward. Such proposition received all types of insults and salvos from Kigali. Kikwete, for the first time, dubiously and unfairly, was linked to genocide and called a genocider. Soon after, Kikwete urged Rwanda to negotiate with the rebels, Kigali embarked on media campaigns painting Kikwete as an emissary for rebels who essentially are genociders in the eyes of Rwanda.
One wonders how humans are hard when it comes to learn from history! It goes with the saying, “We learn from history that we don't learn from history!” Desmond Tutu. Interestingly, it is the same Tanzania that tried to negotiate dialogue between Juvenal Habyarimana (former president of Rwanda) and Kagame (then leader of the Rwandese Patriotic Front (RPF) rebels).
I am trying to imagine if Habyarimana would have taken the same stance as Kagame has taken. Would Kagame been in power today after being defeated by Habyarimana for long? Who’s fooling who hither? Maybe, Tanzania is paying for its sins of creating Museveni and Kagame. 
While Rwanda is demonizing Kikwete, other SADC countries have supported his move. Sadly though, Rwanda seems to have forgotten the role Tanzania played in ending the Rwanda conflict.  Again, I read one article in the New Times of Rwanda which was quoted as thus, "And so he was because, as Tanzanian foreign affairs minister, he was watching as the Genocide was being planned." If my mind serves me well, Kikwete was not minister for Foreign Affairs during and after the genocide. Why are people telling lies to justify their lies?
Since the installment of a new regime in Kigali under Paul Kagame in 1994, Rwanda has nary tolerated any advice pertaining to dialoguing with rebels or introducing true democracy. Whoever tries to tell Rwanda to think about talking to rebels is painted with the same brush.
What irked Rwanda the most is the fact that Kikwete is seen as preempting and executing a bigger plan backed by other countries. Coincidentally, Kikwete’s advice to Rwanda to negotiate with rebels comes at the same time the US president Barack Obama is expected to tour the country.  One of the Rwandan daily was quoted as saying, "If President Kikwete’s advice was meant to distract, it has done the opposite. It has put people on their guard and made them more determined not to be derailed but to deliver more imihigo." It is sad to note that Rwanda could openly say that Tanzania wants to derail their efforts to build their country.
Those who know Kikwete do not wonder. In his own country, on many occasions, Kikwete has spoken generously. In 2011, he signed a doctored bill that he later annulled. He once told Tanzanians that he did not know why they are poor. He added that when Tanzanians experience traffic jams, they should take them as economic growth.
Regarding reviving the Eat African Community, only Kenya is left with the sanity to mediate this eminent danger given that Tanzania has now become a part to conflict while Uganda is known also to be in vicariously. Burundi has more on its plate.
Source: The African Executive Magazine June 26, 2013.

Pinda afute kauli yake, aombe msamaha



MANENO ya ajabu yaliyotelewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda yametufanya tusononeke na kuogopa. Tunaomjua Pinda hatuamini kama siku hiyo alikuwa barabara.
Yawezekana alikuwa ameficha uhovyo huu ambao ni ushahidi kuwa sasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefilisika na kuishiwa vibaya iwapo watu kama Pinda wako hivi.
Kwa nafasi  yake, Pinda kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, kutoa kauli zenye kuvunja sheria na katiba na  kushabikia jinai, uonevu na vurugu ni aibu na pigo kubwa kwake, serikali yake na chama chake.
Pinda alikaririwa akihimiza fujo na mashambulizi kwa raia hata wanapodai haki zao. Alikaririwa akisema bungeni; “Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.”
Kumbe uongozi wa CCM umechoka wananchi na kuwaona kama wafanya fujo pale wanapodai haki zao? Je, viongozi waliochoka wanapaswa kuendelea kuwa kwenye ofisi za umma?
Je, alitaka wananchi wawapende viongozi waovu na wababaishaji? Je, inapofikia baba akawaambia wanae kuwa amewachoka, kweli baba wa namna hii hajivui ubaba? Je, Pinda hakujua uzito wa nafasi yake na maneno yake? Je, Pinda alikuwa ameficha uhovyo wake kiasi cha kuonekana kuwa mmoja wa viongozi makini wachache wakati siyo?
Japo si nia yetu kumchambua Pinda badala ya hoja, inaonekana ameishiwa, tena vibaya sana. Hivi Pinda anaishi dunia gani asiyejua kuwa Watanzania wameonewa na polisi kwa kiwango cha kutisha? Je, kama wote tutakuwa na mawazo mgando na ya vurugu kama ya Pinda nchi hii itatawalika?
Je, Pinda hajui kuwa umma una nguvu kuliko hilo jeshi lake la polisi ambalo serikali yake imekuwa ikilitegemea kuendelea kuwa madarakani? Nitashangaa kama ataendelea kuwa waziri mkuu japo katika taifa letu kwa sasa lolote linawezekana.
Pinda anawakilisha mawazo ya serikali na bosi wake Rais Jakaya Kikwete aliyeendelea kutanua nchini Uingereza hata baada ya kupata taarifa za kulipuliwa bomu na kuua watu.
Kwa vile alikuwa akijua kilichotokea kama alivyokaririwa akisema, aliona mpira ni bora kuliko wafuasi wa CHADEMA ambao hata hivyo ni Watanzania sawa na yeye.
Tumeshuhudia akina Barack Obama wakiacha mambo mengi kwenda kuhami wahanga na kutoa msimamo kama viongozi waadilifu na wanaojua wanachofanya.
Mtu anafanya madudu na kupandishwa cheo kama ilivyotokea kwa aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda.
Kamanda huyu alipandishwa cheo pamoja na kushutumiwa kusababisha mauaji ya mwandishi Daud Mwangosi.
Ni bahati nzuri kwa watawala kuwa waandishi wa habari wa Tanzania nao wameathirika. Bila hiyo wangegomea kuandika habari za serikali ili waone kama ingefanya kazi.
Pinda licha ya kuwadharau na kuwabagua Watanzania, amehatarisha maisha yao kwa kutoa amri na shinikizo kwa jeshi linalosifika kuwatesa na kuwadhulumu kuwapiga litakavyo.
Hii maana yake ni kwamba tujiandae kushuhudia mauaji mengine kama ya Mwangosi na utekaji na utesaji waliofanyiwa Absalom Kibanda aliye Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation (2006) na Dk. Stephen Ulimboka.
Tutarajie mashambulio mengine ya mabomu kama lile lililotokea Arusha. Je, viongozi wa namna hii ni wa kuvumiliwa au kushughulikiwa na umma? Je, ni kulewa madaraka au kuishiwa?
Wataalamu wa mawasiliano wana kitu kinaitwa ‘frontstage’ na ‘backstage’. Alichosema Pinda ni ‘backstage’ yake ambayo hakupaswa kuonyesha kwa wananchi waliomwamini na kumthamini kama kiongozi wao hata kuendesha maisha yao kwa kodi zao.
Kiongozi asiyejua la kusema mbele ya umma na nyuma ya pazia lazima ima awe ameishiwa, au amekuwa kiongozi kwa bahati mbaya tu. Je, nini kimemsibu Pinda ambaye hupenda kujiita mtoto wa mkulima wakati ni tajiri wa kutupwa anayeweza kuvaa saa ya dhahabu akidhani watu hawaoni?
Je, Pinda, tena mwanasheria, amesahau kuwa kama mauaji ya kinyama na kigaidi yanaweza kutokea chini ya amri yake anaweza kujikuta mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) huko The Hague? Nani atamwokoa Pinda kumshauri aachane na njia ya kupotoka anayochukua kwa hiari yake?
Je, Pinda anathibitisha ile dhana ya CCM kuwa chama ni zaidi ya wananchi wakati asijue kinategemea hao hao wananchi? Kwa kauli yake ya kizembe, naamini hata wanachama wa CCM wataipinga na kuanza kufikiri upya kuendelea kuwa wanachama wa chama kisicho na mwelekeo hadi kushabikia mauaji na mateso ya wananchi.
Pinda alipaswa kujitofautisha na watu kama Mwigulu Nchemba, William Lukuvi na Nape Nnauye ambao wanaweza kujisemea lolote wakati wowote bila kutathmini athari za matamko yao kutokana na uwezo wao haba na ile hali kuwa wanatuhumiwa kughushi sifa zao. Japo tabia yao haikubaliki inaeleweka na inafafanana na uwezo wao kufikiri.
Kwa kiongozi kama Pinda, alipaswa kungoja angalau uchunguzi wa polisi utoe jibu la nani yuko nyuma ya shambulizi la kigaidi la Arusha. Kama serikali na chama chake hawahusiki, ni kwanini amekurupuka?
Je, Pinda aliamua kujipayukia kwa vile katika wahanga hakuna ndugu yake? Je, angekuwa amepoteza mke, dada au mtoto au baba angekuwa anayesema hayo anayosema? Je, kushindwa kuliona hili si ubinafsi wa ajabu?
Kitendo cha Pinda kutoa amri kwa polisi kupiga watu ni kinyume cha sheria na cha kulaaniwa ukiachia mbali kuwa uvunjifu wa sheria wa wazi. Na hii si mara ya kwanza kwa Pinda kuonyesha uhovyo wake.
Aliwahi kukurupuka wakati polisi walipofanya mauaji ya raia huko Arusha waliokuwa kwenye maandamano ya amani yaliyoitishwa na CHADEMA tarehe 5. 1. 2011 na kusema kuwa hakukuwa na raia wa Kenya aliyekuwa ameuawa wakati alikuwapo akijulikana kwa jina la Paul Njuguna Kayele.
Ni bahati mbaya hata kuwa Pinda hakujifunza kufikiri kabla ya kusema. Ni bahati mbaya kuwa Pinda aliendelea kuamini kuwa angeendelea kukingiwa kifua na Spika wa Bunge Anne Makinda aliyefikia hatua ya kumtoa nje Mbunge wa Arusha Godbless Lema alipodai Pinda ni muongo.
Tumalizie kwa kumuasa Pinda aombe msamaha kwa vile ni binadamu, yaishe tuendelee na safari. Ila bila ya kufanya hivyo atazidi kuukoleza moto ambao huko tuendako hataweza kuuzima.

Kijiwe charejea toka vakesheni


SAFU hii inawaleteeni habari njema sana ya ukombozi. Ni kuhusu kumalizika kwa vakesheni ya wanakijiwe ya miezi sita.
Wapenzi wetu walituandikia e-mails wakidhani tumededishwa na mibomu ya Arusha iliyorushwa na magaidi na washenzi wasio na maana.
Hivyo, tulikuta kijiwe kimejaa vumbi. Si unaona kijiweni palivyojaa vumbi? Tunakumbuka ujumbe wa wasiwasi juu ya uhai wa troupe yetu iliyotoka kwa Sheddy Mijjinga wa kule Mza. Hatuwezi kutaja wote waliojali ila tunawashukuru.
Tumerejea kwa kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya, si ya kufanya ufisadi na usanii, bali kuendeleza libeneke ya ukombozi. Tulikwenda vakesheni kutokana na sababu nyingi.
Mosi, kupumzika baada ya kutumikia kijiwe tangu tuliposhinda uchaguzi bila kuchakachua wala mizengwe. Hatukuwa tumepumzika wala kufanya ziara yoyote nje, ukiachia mbali mkiti kwenda kwenye kutoa ushauri kule Masri na Libya wakati wa kitimtim kilichowahenyesha wahuni, kilichomnyima wibari mkia. Pia nilikwenda Kenya kusimamia uchakachuzi uliofanyika Machi 5 ambako Moyi Kibaka aliiba kura na kumpa mkyuki mwenzake Uhuruto.
Pili, tulipata wivu (si wa kike) baada ya kuona mkuu, bi mkubwa wake na waramba viatu wakizurura mara kwa mara kwa njuluku za walevi bila kufanya kazi pevu kama yetu.  Tuliona lau twende kule kuangalia mambo ya maana ili tukirejea tuyafanye kayani na kijiweni.
Mwenzenu nilikuwa sijaenda kuangalia mechi dimbani kwa miaka mingi. Hivyo nilikwenda kwa mama kuona timu kama Asenali, Manchesta, Sandaland na nyingine lau kupata jezi na picha za ukumbusho.
Bi mkubwa wangu naye alipewa tuzo ya kuwatumia wake wa walevi chini ya asasi yake ya Maulaji ya Wake wa Wakubwa (MAWAWA) na kujitengenezea pesa haraka huku watasha wasimstukie. Alikuwa kule kwa Joji Kichaka kuipokea japo sikuhudhuria baada ya kukosana nilipomshauri kwenye kuipokea aongee kimakonde na si kimombo kutokana na kumpiga chenga na kupandisha pressure anapokiongea. Nilihofia angeweza kudedi mbele zangu.
Wakati nikitanua kule New York, Mgosi Machungi alikuwa zake kwa akina Aloha kule Hawaii alikozaliwa Obamiza akipigiwa kifaa kiitwacho ukulele (si kelele ya uswazi). Good news, Mgosi Machungi alibarikiwa kupata mtoto wa kiume aitwaye Shenkhondo. Baada ya bi mkubwa wake Nesaa kujifungua tulikwenda zetu Sauzi kumjulia hali Diba wa Madiba.
Wengine walienda wapi?  Siri kubwa maana walikwenda kujifunza jinsi ya kupiga mtu chini, hasa anapochukua ulaji na kufanya ufisadi badala ya kuwatumikia walevi. Isitoshe tumefanya siri ili magaidi ya kindata yasiwafuatilie na kujua siri zao za kupambana na ugaidi wao na kuanza kuwamiminia risasi.
Kwa vile tulikuwa vakesheni kwa muda mrefu, tumekuta viporo vingi mezani. Kama miezi sita imekuwa hivi, hawa wazururaji wenu ambao kila siku kiguu na njia wataacha viporo kiasi gani kukuuu?
Leo kikao chetu ni cha laana. Tunalaani kwa nguvu zote unyama, uhuni na ushenzi ulioanza kuwa mazoea kama vile kumteka Abusalomu Kijumba. Tunalaani vipigo na uhuni uliofanyika Ntwara kuwazuia walevi wasidai wese lao lisichezewe na mafisadi waliokwishaleta makampuni yao kujenga mibomba ya kukamulia wese.
Tatu, tunalaani mauaji na ugaidi vilivyofanyika Soweto Arusha baada ya magaidindata kushambulia mkutano wa Chakudema huku wakitumia mibunduki kumiminia watu shaba.
Nne, tunalaani ufisadi uliowezesha kujengwa mghorofa wa Ugabacholini ambao uliangukia walevi kibao huku uliobakia ukiendelea kupigwa danadana na mafwisadi wanaolinda ulaji wao.
Tano, tunalaani matamshi ya kishetani na kishenzi yaliyotolewa na wapauuzi fulani wakidai Chakudema eti imejilipua kutaka huruma ya walevi. Hawa walipaswa kuchomwa moto kama vibaka.
Nani mara hii anaweza kuacha kulaani mafyatu kama vile Mizengwe Pindua ambaye amepinda kwelikweli, Nipe Mapepe Ninaye, Mwingurumbili Michembe na Mchunga Kondoo Mtukula? Shame on you goons Ukiondoa Pindua hatukushangaa kusikia vihiyo hawa walioghushi na tapeli aliyejipachika uchunga wakipayuka kwa vile wanathibitisha walivyo matapeli na vihiyo wa kutupwa.
Sita, tunalaani lijibajeti la kijambazi ambapo njuluku nyingi inatengwa kwa shughuli za matanuzi ya wazururaji huku walevi wakiendelea kuumia na kunyotoka roho.
Hivi huyu jamaa tunayeambiwa ni profwesa mbona haonyeshi uprofwesa wake au ni yale yale ya akina J4 Magimbe na wenzake wanaoboronga kila uchao?
Baadhi ya maprofwesa wa Kibongo hovyo kabisa. Hebu muangalie bi mkubwa Anna Kajumuzi Tibainjuke anavyoendelea kuaibika baada ya magabacholi kumzidi kete pamoja na kutangaza ataporomosha mjengo asijue ataporomoka yeye Saba, tunalaani ufisadi wa J4 Kawa-Dog aliyefelisha watoto wa walevi akaendelea kukataa kuachia ngazi.
Tunamlaani hata aliyemteua na kuendelea kumvumilia kwa vile wanatoka kaya moja.  Hakuna Kawa-Dog alipotuacha hoi kama kufuta matokeo ya fomu foo na baadaye kuyarejesha kwa kuwapa ushindi waliosemekana kushindwa. Hivi hapa kihiyo kati ya watoto wa fomu foo failure na Kawa-Dog ni nani?
Nane, tunalaani kitendo cha mkuu mwenyewe kuendelea kutanua kwa Mother akijinoma na timu za uchochoroni za huko, huku walevi wakiendelea kunyotolewa roho na watu wake. This is very serious. Hata hivyo, hatuna wasi wasi. Maana msomi Mkatatamaa kwenye vakesheni yake alikuwa The Hague akiangalia uwezekano wa wahuni hawa kufikishwa kule na kunyea debe.
Hata kwenye kikao changu na Bani Kii Mwezi, katibu mkuu wa YUNO tuliongelea suala hili alipokuwa akinipa michapo juu ya yule mama aliyempa ulaji akaenda pale kuonyesha ushamba wake hatimaye akamtimua na kurejea kwenye genge lake la ulaji ambalo lilimpa ulaji uchwara.
Sina haja ya kumficha kwa vile mnamfahamu kuwa ni   Dakitari Acha Rozi Migiroo. Bwana Bani Kii Mwezi aliniomba nikubali aniteue kurejesha heshima ya kaya nikakataa kwa vile kazi ya kukomboa walevi ni kubwa na ngumu na nyeti kuliko hiyo aliyotaka niifanye.
Hakuna kitu kilimsononesha kama kumpa skandali ya mama mmoja jambazi aliyewahi kupewa uwakilishaji kwa Joji Kichaka na kwa Mother wakati alikuwa mwezeshaji wa ujambazi wa HEPA. Nadhani mwamjua. Ni Mwanawaidd Maajari.
Naona wale ndata wameshika kitu kama bomu. Acha niishie kabla hawajanilipua bure na kusema nimejilipua mwenyewe wakati bado ugali mtamu.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 26, 2013.

Monday 24 June 2013

Get ready to have a boozer president

Though the adage’s that no news is good news, this time around I bring good news for all boozers in Bongolalaland. After the New Constitution Draft came up with ingenuity of allowing an independent candidate to run for presidency, rest assured that this time my name will be on the ballot papers come next general elections. Yesterday I drank like a fish, smoked like a chimney and slept like a queen after the news was broken.
There are a couple of reasons why I’m running for presidency. Firstly, I found that politicians have failed miserably so as to force me into running for this mighty job where you eat free not to forget your friends and family members. I know. I’m not a politician. Again, being patriotic as I always have been, I’m the ideal person to save the hunk.
As an independent candidate, I’m intending to declare independence to the hunk that’s for long been duped of being independent while it actually depends on its former colonial masters. I mean. After ascending to the presidency, I won’t go cup in hand begging as it is today. Why should I beg while I’m president of the hunk endowed with all riches?
Secondly, I’m running just because the constitution has recognized the shortfalls in the current corrupt system of self-serving on the expenses of the boozers.
Thirdly, being more competent than winos we have in power, as a boozer, methinks I deserve to carry this cross so as to emancipate the boozers all over the hunk.
The following are my strategies to see to it that I scoop voters and become the one and only emancipator of this hunk.
Fourthly, I want to fulfill the self-fulfilling prophecy that one day an unexpected boozer will become president of this hunk. Please, when I talk of a boozer I mean a real one. I don’t mean political boozers, thieves and wheel dealers you currently have.
To win your votes, I’m going to see to it that I man a very sizable government of only five ministers. So too, I’ll make sure that I don’t allow anybody or myself to spend your tax money on globetrotting. Even my wife who’s going to be your first lady won’t be allowed to accompany me in foreign tours unnecessarily.
So too, my wife won’t be allowed to form an NGO aimed at screwing you up. As for my children, believe ye me. They won’t be allowed to enjoy my power acting as small presidents just because they are president’s children like Riz and Mira. When I proposed these measures to my family, everybody went berserk.  My wife and children ganged up to see to it that they sabotage my plans of becoming president. Again, when I educated them about what befell Egyptian and Ivorian strong men, their wives and children, they conceded defeat. I advised my wife to go back to school. For, she’s an UPE teacher.
I can see you’re laughing. Don’t laugh. I’m not joking. I seriously intend to bring a new way of doing things in the office of president.
Forget about my family. Let me tell you why I’m the one and only fit to become the head of this hunk.
Firstly, I’m over educated with sacks of genuine PhDs. I’m not like those guys who forged theirs or those using honorariums to brag around. I think chaps such as Bill Lukuvi, Makorongo Mahanga, Emmy Nchimbi, Marry Nagu, Didace Makalio and many more know what I mean.
I also am handsome and beautiful altogether. To see to it that this succeeds, I’ll send my photos to professionals so that they can apply some photo shopping on them so that I can look younger ever. I too will be applying some hair 'blackeners' to keep on look young.  Important of all, I've a clean bill of health. Even when I drink or smoke a joint, I don’t fall like those who fall like leaves. I’m tough and I can tough anything out believe me.
Another asset is: I've my network that will help me in campaigning. The difference from other known mitandao is; Mine don’t spend any stolen money or takrima to win support. We’ll only sell our policies aimed at emancipating everybody. The bigger promise is to make sure that every boozer is empowered to be able to bring pilau, ulabu and other yum-yum on the table. I believe everybody likes swallow. If your religions promise you a swallow after dying and getting into the heaven, what’s wrong for me to make sure that you get all these goodies on earth before death? So guys trust me. I won’t rob your central Bank or indulge myself in Kagodamn and Richmonduli monkey biz.
To make sure I gain your trust, I’ll declare my wealth and that of my wife children and friends.
I’ll order all boozers to campaign in all pubs not in the houses of God like wachovu do. I won’t allow bed to bed campaigns. For it is a good source of miwaya.
Journalists are encouraged to campaign for me so that I can emancipate the hunk.  Make sure you attack my opponents even if it means to tell lies about them. Warning, I’m not going to award them some District or regional 'Commissionership' for this job. My duty’s is make sure that they’re no longer being hijacked and kibandered or mwangosed.
Also I’ll introduce my Mahanjumati, Lipilau and Onions (MLO) party. I’ll annul all districts and regions created for political-motivated reasons.
Folks, I've a hell of things to do. See ya.
Source: Thisday June 23, 2013.

Saturday 22 June 2013

Mghorofa wa Udosini na mkangafu vyamtishia mlevi

 Si juzi mlevi nikajifanya mdosi kwenda kwenye mitaa ya udosini eti kusaka vidosho nisijue vidosho vya kidosi huwa haviolewi wala kuchukuliwa na walevi vinginevyo waende kusoma kule na kuvizoa kama dagaa! Hawa jamaa kwa ubaguzi especially wakiwa huku! Ajabu hawabagui dada zetu wala nyanya na njuluku zetu hasa wakiwa kwenye vigwena vyao na mafwisadi wetu wenye ulaji! Hayo tuaache si mwake leo.
Mlvevi nikiwa nachungulia kwenye maghorofa ya Msajili wa Wadosi si lile ghorafa lililomshinda profwesa Ana Tiba Ijuka likanitazama na kusonya mswahili nakwenda kule kufanya nini. Nilisikia jumba likisema kwa hasira, “We swahili mi taagukia veve dugu yako ikose zika veve.” Nilistuka kusikia jengo likongea.
Bahat nzuri wakati mghorofa ukinitishia nilikuwa na mgosi Machungi yule kichaa wangu toka Mashidei Usambaani. Kusikia vile aliamua kujivuvumua na kulijibu, “Mgosi si uende uangukiane na poofesa Anna Tiba Ijuka mnayeshindana?” Naye alisonya na kuongeza, “Unadhani wote ni wala rushwa kama wale uliowahonga na kukugwaya. Nitakupiga zongo hata uembue mimacho.” Baada ya kumalizia sentensi yake tulitoka mkuku kwenda kusimulia yaliyotusibu udosini.
 Baada ya kutoka pale tulikwenda kuwapa stori walevi wenzetu ya jengo kuongea na kututishia. Hawakutukawiza kutupa laivu kuwa tuache ushamba.  Kwani lisingekuwa linaongea si lingekuwa limeishabomolewa miaka mingi iliyopita? Alichomekea mlevi. “Mmesahau kuwa waziri mzima alijivuvumua kudai livunjwe na wenye nazo wakamzunguka kwa bosi wake na ghorofa likaendelea kupeta? Huoni alivyonywea na kupwakia matapishi yake? Mnacheza na sirikali ndani ya sirikali nini? Nijuavyo mimi hili ghorofa halitaanguka vinginevyo aanguke au kunga’atuka mtu. Huoni akina Mecky Mecky Saidiki walivyoshika bango kuhakikisha haliangushwi?”
Aliendelea, “Huyu porofwesa anapaswa kurejea skuli akajifunze masuala ya ulaji na ufisadi kujuana na kulindana na jinsi ya kuishi nayo au vipi? Nadhani bi mkubwa huyu atakuwa anaomba liporomoke na kuua tena ili wale wanaolinda ujambazi huu watie akilini.”
Baada ya kumalizia nchapo wetu tulivyonusurika kuangukiwa na ghorofa tulibaki kushangaa. Lile ghorofa lilikuwa linatutisha ili kutoa ujumbe kwa waliolishikilia bango wasijue halitabomolewa. Ukitaka kujua kinachoendelea hebu uliza wale jamaa waliBnyakwa baada ya ghorofa dada kuua walevi wamefanywa nini kama siyo kupigwa dana dana ili hasira zipoe waendelee kupeta. Watu wanajifanya hamnazo kama vile hawaijui hii bongo ya kula na kulana? Mtaendelea kuliwa hadi mmalizike msipoacha ujuha wa kuangalia mambo ya hovyo yakitendeka nanyi kujifanya hayawahusu. Au mwangojea waje wafadhili toka Ulaya wabomoe mijengo mibofu kama hii? Mmenoa sana so to speak.
Baada ya kusogoa na mgosi Machungi kuhusiana na ushamba wetu alikuja na nyingine mpya. Aliapa akisema kulikuwa na mkono wa mtu si bure. Maana tukiwa tunarejea toka kwenye kisa cha ghorofa lililowashinda vigogo, alinusurika kugongwa na ngwala ngwala ambalo tulikuwa tumelipita likiwa limesimamisha na wazee wa mabao. Wawajua wazee wa mabao? Usikonde. Ni trafwiki wanaowatoa kitu kidogo na kitu kikubwa madereva al maaruf wafukuza barabara na kuwaacha waendelee kumaliza walevi wasio na hatia kwa kuwagongelea mbali. Naye mgosi kwa ushamba wake akidhani alikuwa akitembea kwenye mitaa ya Mihelo si alinusurika kukongwa!
Tulishindwa kujua kuwa hii kaya ilishabinafishwa kwa kila mwenye kutaka utajiri wa haraka. Nani anabishia hili? Kwani juzi hamkusikia skandali ya jamaa yangu mpiga debe wa zamani aitwaye daktari wakati ni kihiyo wa kutupwa? Wamjua huyu? Si mwingine ni Chris Mzindikaya Maji ya Pwani ambaye nasikia anakodisha houses 15 za umma kwa njuluku 50,000 na kupangisha wageni kwa dolari 400 hadi 500 kwa mwezi. Jamaa amejua kutuibia. Nani hakusikia skandali ya kujenga bwawa kwa njuluku za walevi zipatazo bilioni moja halafu akalitumia kwa matumizi binafsi huku akiwazuia wenye njuluku kwenda kuchota maji? Bongo hii bwana utadhani walevi hawana bongo!
Kaya ikiwa ya walevi basi kila mmoja anafanya vitu vyake kilevi. Hamkuona kule Arushae ambapo magaidindata walipovamia mkutano wa CHAKUDEMA na kuua walevi wasio na hatia huku ndata wakizuia wana CHAKUDEMA kuwakamata wenzao? Haya si maneno yangu. Ndivyo alivyosema bwana mkubwa Mtuhuru Aikaeli aliyenusurika kudedishwa na wabaya wake anaopingana nao. Ajabu wakati walevi wakinyotolewa roho mkuu alikuwa zake kwa Mother akitanua kwenye vilabu vya boli. Angekuwa Obamiza angekatisha ziara na kuja kutoa msimamo na mwelekeo. Kumbe kaya za walevi hazina mwelekeo wala wakuu wenye nao! Wangekuwa nao si mkuu angeacha matanuzi yake na kuja kuwahami wahanga na wafia au kwa vile walikuwa kwenye mkutano wa wapingaji? Hayo tuyaache.
Hata hivyo, nangoja kusikia jamaa zangu mabingwa wa kutengeneza magaidi Saydou Mwema na Mwijuu Nchembe watasemaje. Nangoja sana kusikia akina Lwakatarehe wengine wakikamatwa kama siyo ‘wasaudia’ wengine. Kaya hii bwana mazingaombwe matupu! Hakuna siku nilinawa mikono kama niliposhuhudia mazingaombwe ya ndata ‘walipowanyaka wasaudia’ halafu wakawatema na kufanya mchezo wa kuigiza kuwa ngoma droo. Nani anabisha? Waulize akina Daktari Ulimboka na Dk Absa Kibanda. Tangu wafanyiwe uhayawani hakuna kilichofanyika. Waliowaigondhu bado wanatesa huku wao wakiteseka. Walimnyonga Sokoine na udume wake itakuwa vifaranga!
Baada ya kupiga stori hizi za kutisha na mgosi tulikubalia yaishe na kumwachia Mungu huku tukingoja kuona nani ataporomoka kati ya ule mghorofa na Profwesa Nchomile aka Kaju wa Mulo wa Tiba ya Ijuka. Hakika hiki kipute kati ya Tiba na Mecky tutaona nani zaidi kwenye gemu hili la kulindana.
Baada ya kumalizana na mgosi ilibidi nimpe ofa lau aende kupata boha ili kupoza machungu ya kunusirika kugongwa na mkangafu pamoja na kuangukiwa na mghorofa wa udosini. Maskini hakujua kuwa huu mghorofa uko kwao wakati yeye yuko ugenini tena ukimbizini.
Je wangapi wataliwa? Who knows? Guess what. I know you all are going kuliwa just soon. Tia akilini mtakwisha hivi hivi mkishangashangaa wakati wenzenu wakizidi kuwatumia kulhali. Mbona huko nyuma hamkuwa hivi?
Salamu wa washikaji wote maeneo ya Ilala mitaa ya Shingo Feni. Mpo?
Chanzo: Nipashe Jumamosi Juni 22, 2013.

Wednesday 19 June 2013

The Nile: Why is Egypt Agitated?

Egyptian president Mohamed Mursi’s rhetoric and threats can’t go without being reprimanded. Mursi was quoted as saying, "I confirm that all options are open to deal with this subject," He added, "If a single drop of the Nile is lost, our blood will be the alternative."
Another source quoted Younis Makhyoun, leader of an ultraconservative Islamist party as saying, "If all this fails, then there is no choice left for Egypt but to play the final card, which is using the intelligence service to destroy the dam,"
Mursi was reacting after Ethiopia started constructing The Grand Ethiopian Renaissance Dam that will produced 6000 MV. When Mursi dispatched his threats Ethiopia’s PM Hailemariam Desalegn was in Beijing meeting his Chinese counterpart Li Keqiang after meeting with President Li Jinping. He was quoted as saying that the project is 'unstoppable' and that Egypt must be mad shall it think about war.
How many times ‘many drops’ were lost and Egypt did not do anything. It started when Tanzania wanted to divert water from Lake Nyanza to nourish dry central regions in the country. Despite Egypt’s barking, Tanzania stood its ground and the project was executed as planned.  Up till now, the first phase of the project has already been completed and Egypt has nary done anything.
At the time Mursi issued his empty outbursts Ethiopia parliament endorsed a New Initiative that annuls the 1929 colonial treaty that dubiously gave Egypt an upper hand over Nile waters.  Five other Nile-basin countries - Rwanda, Tanzania, Uganda, Kenya and Burundi have already endorsed a new Nile River Co-operative Framework Agreement that annuls the former. This speaks volumes when it comes to who should have an upper hand over Nile.
 To counter Mursi’s threat Ethiopia was quoted by BBC as saying, "We have a principled stance on the construction of dams. We are determined to see our projects brought to completion."
If Egypt wants to fight over waters that are out of its territory it means that in the future should we fight over clouds hovering over another country simply because they can drift to our country and bring rain?
Canada has the largest clean water in the world that the most powerful nation on earth US needs the most. Again, there’s no time in the history of these two neighbours that they've flexed their muscles against each other just over water.
Methinks water even clouds become the property of a country after the same enters the territory of the said country.  A simple example is of elephants living in Tanzania. These elephants become Kenyan property once they enter its territory. Again, once they cross the border from Kenya to Tanzania they become Tanzania’s property per se as they’re Kenyan property per se.
When it comes to the use of Nile waters, Egypt wrongly and arrogantly thinks has an upper hand. It has reached the stage whereby Egypt has tried to teach the upper regions how to use the water of Nile. Egypt normally bases it claim on the colonial treaty that British colonialist enacted. Who signed the said treaty while current countries were nonexistent legally?
For Egypt to legally employ this bogus treaty, it must deny the independence of the upper Nile countries.
Any war over Nile will suck in all upstream countries knowing that if they don’t aid their colleague over Nile enemy, they’ll follow suit shall one of them be defeated. China ---that’s constructing the disputed dam--- will also be sucked in shall war break.  Ethiopia can use water as a weapon to annihilate Egypt shall war break. After all, Egypt currently can’t confront any country militarily thanks to being paralyzed by her home problems since the Arab Spring kicked in. Egypt’s economy is not in shape currently and international financial institutions have chipped in to help subjecting it under tough conditions.
Essentially, Mursi is issuing threats not just to fulfill them. He does so to please, and thereby, win the confidence of his electorates and citizenry.
Suffice it to say, Mursi needs to face reality and negotiate a deal regarding how to benefit from Nile water instead of basing his claim on pseudo and dubious legal and colonial fallacy. Upper-stream countries are independent country. Joke aside, it laughably striking. Upper-stream countries did not append their signatures on an illegal treaty Egypt bases its claims on. Egypt should stop making a big deal out of nothing.
Source: The African Executive Magazine June 19, 2013.

Tuvunje Muungano au tuungane kweli kweli


Zanzibar watataka serikali tatu kwa vile si mzigo kwao. Pesa ya kuendesha serikali ya Tanganyika haitatoka Zanzibar ingawa pesa ya kuendesha serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar siku zote imetoka Bara. hivyo kwa watu kama hawa ambao hawataonja machungu ya kuwa na utitiri wa serikali kuwa na serikali tatu si tatizo. Pia wazanzibar wangependa serikali tatu ili kuendelea kuukana utanzania na kuukumbatia uzanzibari.  Kama na watanganyika watachangamkia utaifa wao wa asili hakuna shaka utanzania utabakia kuwa kwenye shubaka na nyaraka na thamani yake itatoweka. Kitendo cha namna hii ni kuvunja muungano hata kama hatutaki kusema wazi. Kama tumeridhika na hili basi tukubali kuvunja muungano badala ya kuutetea mchana na kuuvunja usiku. Huu ni unafiki na kutojiamini. Tuachane na muungano na kushikilia maslahi binafsi kama ambavyo ilivyo. Tuseme wazi kuwa maslahi yetu kama bara au visiwani ni zaidi ya muungano ili dunia ituelewe na tupumue au vipi?  Je kuna haja gani kuwa na utaifa usio na mwenye kuubeba kama ambayo itakuwa kwa utanzania ambao hata hivyo umebakia kubebwa na watu wa Bara huku wa Visiwani wakiuepa kwa gharama yoyote vinginevyo kuwepo na maslahi kama uwaziri ubunge au fursa za kuchuma?
Bara watataka serikali moja ili kuondoa mzigo unaowakabili hadi sasa wa kugharimia uendeshaji wa serikali mbili hasa ukilinganisha vyanzo vya uchumi baina ya pande mbili. Ni ajabu kuwa waliokusanya maoni kutoliona hili! Ni ajabu kuwa wabara wanazidi kuongezewa mzigo ili kuwaridhisha wavisiwani. Pia itakuwa ni ajabu kama tutakuwa na serikali tatu bila muungano kuvunjika kulaleki!
Kuna ushahidi wa kutosha kuwa waanzilishi wa muungano waliamua kuwa na serikali mbili ili baadaye waelekee serikali moja pamoja na kutofautiana mwanzoni kutokana na hali ya kisiasa ya wakati ule. Kwa mujibu wa Jaji Mark Bomani alikaririwa hivi karibuni akisema, “Hayati Karume yeye alipendekeza nchi mbili kuungana na kuwa nchi moja mara moja. Hayati Nyerere yeye alisita kidogo kwa kuogopa kwamba ingeonekana Zanzibar imemezwa na Tanganyika na hivyo pengine kuelekeza maasi Zanzibar.” Wakati ule ilikuwa inaingia akilini. Je baada ya kukaa pamoja kwa zaidi ya miaka arobaini bado tunahofia kumezwa? Mbona Kilwa iliyokuwa na hadhi sawa na Zanzibar hailalamikii kumezwa wala Lamu Malindi na Mombasa nchini Kenya? ni ajabu kuwa tunaongeza wingi wa serikali na kujipa moyo kuwa ndiyo kudumisha muungano wakati tunauvunja kijanja!
 
Je kwa kuongeza serikali ya tatu badala ya kupunguza ya pili tunaimarisha muungano au tunaendekeza kila upande na maslahi yake? Kama kweli tunaamisha kuhitajiana basi tuungane na kuwa na serikali moja badala ya utitiri wa serikali ambazo kwa nchi ombaomba kama yetu zaweza kuwa chanzo cha kusambaratika. Muungano ni sawa na ndoa. Kinachoendelea ni sawa na ndoa ya maslahi au chuma ulete ambapo wanandoa hutumiana kwa maslahi tofauti. Ndoa halisi ni kuwa mwili mmoja na kitu kimoja badala ya vipande vipande.
Tufanye kama Marekani. Nchi zilizotengeneza Marekani au Kanada zilipoungana zilibakia kuwa majimbo na nchi zimeshikana na hakuna anayedai kumezwa. Hawaii ni sawa na Zanzibar. Lakini bado haidai wala kujihisi imemezwa na California au Texas kwa sababu ni nchi kubwa ndani ya muungano wa Marekani. Prince Edward Island nchini Kanada ni kijisiwa kidogo lakini hakijawahi kulalamika kuwa kimemezwa na Ontorio au Nanavut kwenye shirikisho pana la Kanada.  Kimsingi, hii hofu ya kumezwa ni ya si ya msingi na haina maana kwa vile kama tutaungana kweli kweli wote tutakuwa watanzania badala ya sasa ambapo tuna wazanzibari, watanganyika, watanzania, wapemba, waunguja na kesho tutakuwa na waMnemba. Kama kweli tunahitajiana haya madai ya Uzanzibari kama utaifa ya nini iwapo watanganyika kwa miaka zaidi ya 40 wameridhika kuitwa watanzania bila kulalamikia utanganyika.  Muungano mara nyingi hujengwa kwa kile waingereza huita give and take and good will. Unapata hiki na kupoteza kile. Unatoa kile unapokea hiki na mambo yanakwenda.
Tuhitimishe kwa kusisitiza kuwa bila kuwa na serikali moja muungano wa Tanganyika na Zanzibar utaendelea kuwa mzigo na kitendawili ambacho baadaye kinaweza kudhoofisha Tanzania. Tuamua tuwe na serikali moja au tuvunje muungano ili kuwe na nchi mbili ambazo kila moja itakuwa na serikali moja. Hivyo, kuondoa mzigo kwa walipa kodi wa nchi hizi. Kuwa na serikali tatu hata mbili ni sawa na kuwa hermaphorodite yaani mnyama mwenye jinsia mbili ambaye si jike wala dume bali kituko. Kama sote ni wamoja kihistoria na kijiografia, kwanini tunaogopa kuungana na kutengeneza nchi moja yenye nguvu na ustawi? 
Chanzo: Tanzania Daima Juni 19, 2013.

Is it the beginning of the end of Museveni?






Recent revelations that Ugandan strong man Yoweri Museveni is grooming his son Major Muhoozi to take over after he leave office is a big blow. One of Museveni's inner sanctum army General David Sejusa recently took a shot at Museveni condemning his ploy to create what he called  a Political Monarchy. Sejusa who fled to Britain openly opposed Museveni attempts to clear a way for his son to take power under what Sejusa called National Project. Museveni has been in power illegally since 1986. Many think that Museveni and other dictators fail to learn from what happened recently in Libya and Egypt. Experience shows that for a dictator to pass the mantle to his child must die in power as it happened to Gnassigbe Eyadema and Omar Bongo.  Given that they are hard to learn, time has decided to remind them the right thing to do before being taught a bitter lesson. Will Museven bow to pressure wanting him to abandon his project? Will he soldier on and face the consequences? Is this the beginning of the end of Museveni dynasty and tribal regime? For more info CLICK HERE.