The Chant of Savant

Sunday 31 May 2015

Shehe Ben Membe amependeza

Lowassa anamtishia nani na kwanini?

  • LOWASSA CAN YET STEP TO CANAAN: BY NOVA KAMBOTA.
          Hivi karibuni mmojawapo wa wanaotaka kuwania urais kwa tiketi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, waziri mkuu wa zamani aliyeondolewa na kashfa ya Richmond Edward Lowassa alitoa la moyoni ingawa hakujibu tuhuma za ufisadi dhidi yake. Alikaririwa akisema kuwa mambo mengi wanayomtuhumu kwayo ni uzushi hata yanayoonekana au kujulikana kuwa ya kweli. Wengi wanahoji ni kwanini Lowassa amechukua miaka mingi kujibu au kuongelea tuhuma dhidi yake.
Moja ya kauli iliyofanya wengi wakune vichwa na kuanza kumuogopa Lowassa ni pale aliposema, “Kama kuna mtu ambaye hanitaki ndani ya CCM, yeye ndiye ahame, siyo mimi.” Je Lowassa anamaanisha kuwa hata kama atanyimwa fursa –kama maneno ya rafiki yake yanavyoonyesha –atanywea na kuendelea kuuguza maumivu akiwa ndani ya CCM? Je CCM ni mali yake binafsi au yametimia yale aliyosema Nyerere kuwa CCM imo mifukoni mwa mafisadi? Je atafanya nini iwapo watanzania au wanaCCM wengi wakimkataa?  Mara hii amesahau alivyotishia kutojiuzulu wakati wa kashfa iliyomng’oa madarakani ya Richmond punde tu akajipiga mtama na kuufyata akatimka? Je Lowassa anampiga nani mkwara zaidi ya rafiki yake rais Jakaya Kikwete aliyeanzisha mjadala wa nani anafaa kuwa rais huku akionyesha wazi kuwa hana nafasi ya urafiki kwenye kumsaka mrithi wake? Je ubavu anao? Na hii jeuri anaipata wapi?
Nyerere pamoja na kuanzisha CCM hakuthubutu kukufuru na kutishia kama anavyofanya Lowassa. Nyerere alisema CCM si baba wala mama yake akimaanisha kama ingeendelea kutomridhisha, angejiondoa. Je Lowassa –kwa kuzingatia uzoefu wa mkwara wake wakati wa Richmond –ana mpango wa kukihama CCM hasa ikizingatiwa kuwa husema hili na kutenda lile?
Kuhusiana na tetesi kuwa afya yake imedhoofu, Lowassa alikuwa na haya ya kusema,“Twendeni tukapime tuone nani mgonjwa. Tuonane kwenye uwanja wa mapambano katika mchakamchaka wa maendeleo, ninajua nitawashinda kwa mbali.” Japo napping vitisho vyake, kwa hili la kupima afya naungana na Lowassa kuwa wagombea urais wapime afya zao ili kuepuka kupoteza fedha nyingi kuuguza rais hata kumpoteza rais kama ilivyotokea nchi ya jirani ya Zambia ambapo walimchagua mtu mgonjwa akafa miaka mitatu baada ya kuwa madarakani. Na wafanye hivyo si kwa kukomoana bali mujibu wa sheria ambapo vipimo husika vitafanyika kwa njia halali na si kughushi na kificho.
Akiongelea kashfa iliyomg’oa madaakani kwanza alisema kuwa serikali haikupoteza hata senti moja kabla ya kujipinga na kusema,“Moja ya ushauri wangu wakati ule ilikuwa ni kutaka kuvunja mkataba wa Richmond nikaita wataalamu…..nao wakakutana chini ya Katibu Mkuu Kiongozi na baada ya kukutana wakatoa uamuzi ambao sina haja ya kuujadili. Lakini ubishi ule umetugharimu Dola 120 milioni.” Kama anayosema ni kweli kuwa hakuhusika na kashfa ya Richmond, kwanini haya anayosema sasa hakuyasema alipoitwa kujitetea mbele ya Tume Teule ya Bunge almaarufu kama Tume ya Dk Harrison Mwakyembe hadi akapewa kitanzi apime na kuamua na akaamua kuachia ngazi kwa vile alijiona mkosefu? Kama hakuwa na kosa kweli, kwanini aliamua kujiuzulu badala ya kutaka ukweli ujulikane ili umma ujue nani alileta Richmond na kwanini sheria zilipindwa? Na kwanini sasa si wakati ule?
Hakuna sehemu alipowaacha wengi hoi Lowassa kama kutolea mifano ya watu matajiri huku akimtaja mmoja wapo aliyepata utajiri wake kwa njia ya ufisadi hadi akafukuzwa uwaziri. Alisema, “Nataka watu wawe matajiri, tuache kuwabeza matajiri, matajiri wawe ni mfano kwa wengine, watu kama (Reginald) Mengi, (Said) Bakhressa na (Nazir) Karamagi wanatakiwa kuwa mfano kwa wengine.” Je Lowassa akiwa rais atatengeneza matajiri wangapi wa namna ya huyu mmojawapo kwa kuruhusu waibie umma ili wawe matajiri?
Sehemu alipowaacha wengi hoi ni pale alipokanusha kuwa hajawahi kukataliwa na marehemu baba wa taifa Mwl Julius Nyerere. Alikaririwa akisema, “Jambo hili si la kweli, sijawahi kukataliwa.” Je Lowassa amesahau au anafanya makusudi au kudhani kuwa watanzania wote ni wasahaulifi kirahisi hasa kuhusiana na maneno na matendo ya kipenzi chao Mwl Nyerere ambaye hakumkataa yeye peke yake bali na rafiki na mshirika wake Kikwete baada ya kuuliza pesa ya kukodisha ndege kwenda na kurudi kuchukua fomu za kugombea urais waliipata wapi wasijibu? Tunajua, Lowassa anaweza kumwonyesha Nyerere kama muongo kwa vile hayupo tena ila wengi wanajua Nyerere alivyochefuliwa na kuchukizwa na utajiri wa Lowassa ambao hadi sasa hajawahi kuutolea maelezo.
Huyu kama amefikia kuwatishia wanachama wenzake wajiondoe kwenye chama asicho nacho mamlaka akipata urais si atawaamuru wale wasiompenda kuihama nchi? Je rais wa namna hii anafaa kweli?
Hata hivyo, kwa wanaoujua jinsi siasa za Tanzania zinavyoendeshwa ambapo ndoa mpya hufungwa na za zamani kuvunjwa, Lowassa ameishajua hatima yake kuwa tiketi ya CCM haipati. Kwa vile akipewa tiketi ile CCM itaangushwa kirahisi kutokana na historia ya mhusika na hasa ikizingatiwa legacy anayoacha rafiki na mshirika wake Kikwete.
Tumalizie kwa maneno ya Kikwete yanayomkaanga Lowassa, “Hivyo ni lazima tupate wagombea wanaochagulika na wananchi ambao niwengi kuliko wanaCCM. Hatuwezi kupeleka kwa wananchi watwasiokubalika, watu waliopungukiwa sifa, tukadhani Watanzania watamchagua tu kwa sababu ni mgombea wa CCM.”
Chanzo: Tanzania Daima Mei 31, 2015.

Friday 29 May 2015

Mlevi am-tweet, kum-beep na kumtwangia rahis

       Baada ya jamaa mmoja mzalendo mwenye uchungu na kaya kum-SMS muishiwa rahis na kusimamishwa kazi kwa kosa la “kuwasiliana” na rahis wake aliyemchagua kwa kura yake, Mlevi nimeamua kuwasiliana rahis. Kama mbaya mbaya. Kwanza, kwangu si kosa kuwasiliana na rahis. Pili, sijaajiriwa na ngurumbili yeyote. Tatu, ngurumbili tena Songombwingo hawanitishi wala siwajali. Nne, sipendi kujigonga na kujipendekeza kwa ngurumbili awe na madaraka au mchicha. Sana sana huwa napayuka ukweli bila kujali nani ataumia, kununa au kujinyotoa roho. Kwangu, fisadi akijinyotoa au kunyotolewa roho ni sherehe kwenda mbele. Fyatu kama nilivyo, nitajali nini iwapo mafisi na mafisadi yamenifikisha hapa kiasi cha kuishi kwa kutegemea bangi na gongo ili kukwepa kunyotolewa roho na mawazo na hasira za kunyonywa na kugeuzwa asusa huku kaya yangu ikigeuzwa shamba la bibi la mafisi na mafisadi, vinyamkera na songombwingo?
Ngoja nirejee kwenye kisa cha aibu na ghadhabu kilichotekea kule kwa akina Meku ambapo njemba moja iitwayo Poo Mhumbahumba imepewa notisi ya kusimamishwa kazi baada ya ikuu kuichoma kwa kufichua mawasiliano yake ya kuripoti ufisadi kwa big. Kwanza, wanamuonea na kumgwaya. Pili, inaonekana hata mkuu anapenda sana rushwa na ufisadi kiasi cha kushindwa kumpa tafu jamaa huyu asiyependa ufisadi na jinai. Ningekuwa mimi ndiyo big mwenyewe hawa waliomsimamisha kazi mtu mwema kama huyu ningewapiga kalamu na baada ya hapo kuwatupa lupango ili liwe somo kwa wengine wenye viherehere na mawazo mfu na mgando ya kifisadi.
Baada ya Mhumba’ kupigwa chini bila utetezi, nimegundua kuwa kumbe kwenye kaya ya kifisadi ukifichua ufisadi ujue umekwisha! Sasa huyu –kama amepatilizwa kwa kuripoti wizi wa kishenzi wa shilingi mbili –angefichua madude kama escrow angekuwa mgeni wa nani kama siyo kum-Kibanda au kum-Ulimboka? Do you remember these guys and those who tortured them to end up being promoted for that? Wamenikumbusha ushenzi wa wakati wa utawala kidhabi wa Ruxa ambapo mchonga maneno mwenzangu Stan Katabaro alifichua kashfa ya Loliyondo na kunyotelewa roho.
Kwa vile mimi ni kidume kisichoongopa lolote, basi kesho nambeep rahis na baadaye namtweet kisha namtuwangia kumkumbusha aingilie kati kwenye kashfa hii ya Keisiemusii. Haiwezekani mtu mwema aripoti uhalifu halafu afanyiwe kitu mbaya kama kile ambacho mbunge wa Kaagwe ameahidi kumfanyia mkuu wa wilaya hiyo kwa kushirikiana na wahamiaji huku akiwageuza wananchi wahamiaji na wahamiaji wananchi. Tamaa nyingine bwana. Yaani kuu zima la wilaya linajigonga kwa wageni na kuhongwa kiasi cha kusahau kuwa kaya hii ni ya wanakaya. Darling Rwega upo hapa? Kwanini unafwanya mambo ya hovyo hivyo au nawe ni mhamiaji aliyechimbia kayani na kupewa ulaji kama mwenyekiti wa zamani wa mkoa huo aliyegundulika kuwa kumbe ni Mrwanda? Shame on you and all those who are turning a blind eye on you. Hata kama Blunders amefanya blunders zake kama vile kudaiwa kunyang’anya ardhi ya umma na kusimikwa uhishimiwa na Jose Makamba kinyume cha sheria, unadhani anayosema ni urongo? Hivi huyu Rose Kiringini anayekutetea umemtuma au ni shoga yako mnayekula pamoja? Kunani hadi bi huyu atake kuzichapa na Blunders kwa sababu ya blunders zako? Umempa nini huyu Rose hadi anapagawa na kupapatika hivi my friend nshomile Rwega?
Kwa vile nimeamua kumtweet na kumbeep rahis, nasema wazi asipokuwajibisha basi nitawahamasisha walevi wa huko wakushughulikie maana huna maana hadi unawakingia kifua wahamiaji tena haramu. Je wanakupa nini hicho kinachokuchanganya kiasi cha kuwasahau walevi na wachovu wenye kaya dadangu?
Ngoja nimtweet rahis na tweet nyingine. Mheshimiwa rahis, ilikuwaje makamu wako akamteua Eddie Luwasha kumwakilisha kwenye kuchangia masjid halafu akafanya kampeni na kumwaga mifwedha? Je huku si kuanza kampeni kabla ya wakati na kukiuka kifungo cha chama au ilikuwa ni changa la machoni kusema kuwa jamaa yako aliyesema hamjakutana barabarani alisimamishwa wakati watu wake wanaendelea kupeta? Je uliwasikia marafiki wa Luwasha wanavomwaga radhi kila mahali hadi kwenye mlima Kimaranjaro? Hii ni nini kama siyo kampeni? Je hapa mnamdanganya nani na kwanini na hadi lini?
Ngoja nitume tweet nyingine. Nilimsikia juzi jamaa yangu Mwakiwembe akisema kuwa kaya itatuma waangalizi wa uchakachuaji kule Urundi ambako Pyere Nkurumbwiza anataka kung’ang’ania ulaji huku akivunja katiba nanyi mkimgwaya kwa vile nyani wote di dugu moja. Je hamuoni kama mnampa jamaa tafu au ni kwa vile kanchezo anakofanya mmekuwa mkikafanya kwa miaka nenda rudi?
Tweet ya mwisho, nadhani utasoma malalamiko yangu juu ya hekalu lako kufichua jina la jamaa aliyefichua uovu wa KcMc na kusimamishwa kazi ukiachilia mbali kutishwa. Je una lipi la kusema kuhusiana na mzalendo huyu anayedhulumiwa, kutishwa, kuonewa kwa sababu ya uzalendo wake? Nina mpango wa kukupigia na kukuongezea orodha nyingine ya wauza unga. Je utafichua jina langu ukiachia mbali kuiweka kapuni kama zile nyingi za wahalifu ulizosema unazo lakini hutaki kuzifanyia kazi? Kama itakuwa hivyo, naomba unishauri. Twende kwa nani na kwanini usitangaze kuwa ni kuvunja sheria kayani kufichua wizi wa fedha na mali za kaya?
Mheshimiwa sana rahis, naomba nimalizie kwa tweet hii.Tafadhali bin tafadhali mkuu. Chonde chonde ingilia kati mja wako apone na patilizi la mafisadi na washenzi waliomsimamisha kibarua kwa kufichua ujambazi na ufisadi wao. Usipofanya hivyo, walevi tutaingia mitaani na patakuwa hapatoshi ukiachia mbali kujimbika bila jembe. Nashauri uwawajibishe mara moja hawa ngurumbili na songombwingo wanaohujumu walevi na kujifanya wanajua sana sheria hadi kuzipinda na kuwaonea walevi wasio na hatia. Sijawahi kusikia mkuu wa wilaya akitetea wahamiaji haramu badala ya wananchi. Hivi huyu anamwakilisha nani zaidi ya tumbo lake?
Ubarikiwe sana mkuu.
Chanzo: Nipashe Mei 30, 2015.

Thursday 28 May 2015

As I bid farewell to Kikwete

 Image result for kikwete's cartoons
Go Kikwete go we're tired of you
Go never turn back, we won't miss you
Go without budging though 

fisadi will miss you
Go Kikwete go, we don't need anybody like you
Go Kikwete go, you turned us into bijoux

You acted as an android
Go, you remind us of our goof
We won't repeat the same move
Otherwise boozers forget


Go Kikwete go
Nobody needs you any more
You vended our hunk great deal more
Thank Lord your time is over

Your presidency is no more
Go Jakaya go
If we shall remember you
It is just evil things under you
 

Go Kikwet go, join Ben your mentor
The one that you protected
Mkapa will miss your cover
Mkapa that had us robbed
Go wait for your fate
Who knows?
A sane person may take over
And bring you to book.

Don't look for a stooge
Just like Ben Mkapa did
Wait for your fate to be known

I pray
God give us a sane leader
That will persecute corrupt official
Give us an enlightened person
Who will redress our nation
Give us that person
The one that will reclaim our nation
The nation that's been sold and thrown
To all types of vampires
We need a leader not a ruler
We need a saviour
Not a tick
We need patriot
Not Vasco da Gama the tourist
Indeed we need a sane leader.

Go Kikwete go
Go Kikwete with your lies
Go without fulfilling your promises
Go with all of your bootlickers
Take all of the garbage you filled Ikulu with
We need somebody to clean Ikulu that is now filth
Take all of your rats
Take all of your braggarts
Take them never leave them abaft

 We need a leader
A leader who looks like us.

I call upon voters
Please do stand firm
Guard your votes
Come next elections
Allow them not to rig
We're tired of these venal beings
Go the king of fisadi
Go without turning back
Go Kikwete go
Go please go
Go quickly go
Go to the oblivion go
Go go go go 
Go forever 
 

Tuesday 26 May 2015

Moja ya sifa za Kikwete ni kulea ufisadi

  • and Tanzania president, Jakaya Kikwete (Left), promotes Rostam ...
Rais Jakaya Kikwete karibuni atatundika jezi kama rais wa nchi baada ya kuitawala Tanzania kwa vipi viwili vyenye utata. Hata hivyo, atakumbukwa kwa hisia tofauti kulingana na anayemtathimini alivyouona utawala wake. Kwa waliofaidika na utawala wake –hasa mafisadi –Kikwete atakumbukwa kama rais aliyewakomboa. Kwa wananchi wa kawaida maskini wanaoendelea kuumizwa na ufisadi na kuparaganyika kwa uchumi, watamkumbaka Kikwete kama rais wa hovyo aliyewazamisha zaidi kwenye mateso na mahangaiko bila sababu za msingi.  Rejea kunyamazia ufisadi wa kutisha kama vile escrow ukiachia mbali kutumia fedha za umma vibaya kwa kuizunguka dunia akiandamana na kila watu wenye kutia shaka ambao mara nyingi walifanywa siri.
Pia Kikwete atakumbukwa kama rais ambaye angeweza kujisemea lolote bila kujali athari zake. Rejea alivyosema kuwa wanafunzi wa kike wanaopachikwa mimba ni kwa sababu ya kiherehere chao. Sijui binti zake wangekuwa waathirika kama angeyasema haya.
Nadhani seriali yake itaingia kwenye vitabu vya historia ya Tanzania kama rais aliyesimamia ufisadi wa kutisha mwingine akituhumiwa moja kwa moja kuushiriki bila kutoa maelezo au kukanusha.  Rejea kashfa ya EPA ambayo inasemekana fedha zake ndizo zilimuwezesha kuwashinda wapinzani wake na kuingia madarakani akaendeleza mchezo ule ule. Rejea kashfa ya hivi karibuni ya escrow ambapo watuhumiwa wakubwa licha ya kuwa nje wakitanua, wengine wamesafishwa na ikulu ya Kikwete huyu huyu.
Kikwete atakumbukwa kama bingwa wa kutoa ahadi lukuki za kila aina asizitekeleze. Yako wapi maisha bora kwa wote yaliyogeuka bora maisha kwa wengi hasa ambao hawako karibu naye wala kuwa kwenye utawala wake.
Moja ya mambo ambayo atakumbukwa kwayo Kikwete ni kashfa zilizamisha mabilioni ya shilingi. Kashfa inayovuma kwa sasa –kama ilivyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ni ya serikali kuendelea kuwalipia maafisa wake walioko ughaibuni hata baada ya kustaafu. Je kwanini serikali ilifanya hivyo na kwa faida gani kama hakuna namna?
 Kimsingi, hawa ni wahalifu wanaopaswa kufungwa kwa kuhujumu taifa. Na isitoshe, wengi wa waliofichwa huko ughaibuni ni ndugu, jamaa au watoto wa wakubwa ndiyo maana serikali inatenda jinai hii kwa umma maskini wa watanzania. Wengi wameteuliwa kwa vigezo vya ajabu ukiachilia mbali kwa kificho kikubwa. Hivi watoto kama wa Edward Lowassa, Pius Msekwa, kweli wameteuliwa kwa vigezo gani zaidi ya majina ya wazazi na mitandao ya wazazi wao?
Kichekesho ni pale waziri anayesimamia wizara hii Bernard Membe kuutaka urais wakati anasimamia na kubariki ufisadi. Kama ameshindwa kusimamia wizara moja ataiweza nchi? Nadhani hiki ni kigezo kuwa Membe hafai kabisa kuwa rais kwa vile ameonyesha wazi anavyoshabikia ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma. Taarifa ya CAG inabainisha kuwa jumla ya Sh 543.7 milioni zilitumika kuwalipa watumishi wa balozi za Tanzania waliostaafu, waliokuwa wakifanya kazi bila kuwa na mikataba kutokana na changamoto za malipo ya kurejeshwa nyumbani. Balozi ziliozoongoza kwa wizi huu ni zile za Kinshasa (DRC), Maputo (Msumbiji), Ottawa (Canada) na Washington DC (Marekani). Ajabu ya maajabu, aliyekuwa balozi wa Tanzania Washington Liberata Mulamula alipandishwa cheo hivi karibuni na kuwa katibu wa wizara pamoja na kutajwa kwenye kashfa hii moja kwa moja. Kesho utasikia Shamim Nyanduga (Maputo) na Hemed Mgaza (Kinshasa) wamepandishwa vyeo. Kwa ubalozi wa Ottawa wengi walishuku pale alipoteuliwa mtuhumiwa wa utesajiwa Dk. Steve Ulimboka Jack Zoka.   
Nadhani yote haya ni matunda ya uteuzi wa kujuana na kulipana fadhila ambao kimsingi, unadhoofisha uchumi wa taifa bila sababu za msingi. Kwa sasa Tanzania chini ya Kikwete inajiendesha au tuseme inaendeshwa kihovyohovyo na umma haustuki na kuchukua hatua.
Kikwete atakumbukwa kama rais aliyetamka wazi wazi kuwa ana orodha za wahalifu mbali mbali kuanzia mafisadi, wauza unga, majambazi lakini akasita kuwachukulia hatua pamoja na kupewa majina yao. Kwanini na ana faida gani nao? Nani anajua? Hakuna sehemu aliponiacha hoi Kikwete kama mkuteua Hilda Gondwe kwenye Tume ya Maadili ya Viongozi wakati mhusika anatuhumiwa kujipatia gari la serikali aina aina ya Toyota Land Cruiser VX iliyokuwa imenunuliwa miaka mitatu kabla kwa shilingi 155,000,000 kwa shilingi milioni moja na nusu tu huku akiusababishia umma hasara ya shilingi 149,000,000. Hata angekuwa Obama rais wa taifa tajiri asingemteua mtu huyu licha ya kutokumfikisha mahakamani. Huyu ana maadili gani wakati ni bingwa wa kupiga madili? Inaonekana hii ndiyo aina ya watu anayoitaka Kikwete kwa sababu anazojua mwenyewe.
Kitu kingine ambacho Kikwete atakumbukwa kwacho ni kujenga barabara ambazo hata hivyo hazikidhi viwango wala kulingana na kiwango cha fedha kilichotumika kuzijenga.
Pia Kikwete atakumbukwa kama rais ambaye serikali yake ililitumia vibaya jeshi la polisi kiasi cha kusababisha vifo na mateso ya watu wengi. Rejea mauaji ya mwanahabari Daud Mwangosi na kuteswa kwa daktari Ulimboka na mwandishi wa habari Absalom Kibanda.
Pia Kikwete atakumbukwa kwa kuwa rais wa kwanza kuamuru katiba aindikwe upya lakini akaisaliti na kutaka kupandikiza yake yenye kulinda mafisadi huku akipuuzia mawazo na maoni ya wananchi ukiachia mbali kutumia wahuni kumtisha aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Kukusanya Maoni, jaji Joseph Warioba.
Si rahisi kuorodhesha mambo mengi ya hovyo ambayo Kikwete atakumbukwa kwayo. Hata hivyo, kuna funzo toka kwenye utawala wa Kikwete kuu likiwa ni kwamba watanzania wasirudie makosa kuchagua mtu kwa kuangalia sura, ahadi na ubobeaji wake katika usanii wa kisiasa.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 27, 2015.

Kijiwe chalaani ndoa ya dini na sias


          Hivi karibuni wanakijiwe walichukia nusu ya kuanza kuandamana hata kabla mkuu sijatoa ruhusa. Baada ya kushuhudia ndoa iliyofungwa baina ya viongozi wa kiroho na mafisadi ya kisiasa yanayokwenda kumwaga pesa eti kuyachangia, kimekaa kujadili aina hii ya ufisadi.
Mgosi Machungi ndiye mwanzilishi wa mada leo. Anakwayua mic na kusema, “Hivi mimeona jinsi mafisadi wanavyoingiia hata dini kiasi cha kutichanganya? Tinaambiwa dini na siasa havichanganyikani wakati wao wanavichanganya.”
“Hebu rudia. Eti wanaiingilia dini? Unamaanisha nini na wanaingiliaje dini na kupitia wapi?” Mbwamwitu anauliza huku akitabasamu.
Mgosi anamrushia gazeti na Mlevi lenye kichwa kisemacho, “Fisadi Afunika AR.”
“Kumbe unaongelea haya mauzauza ya chama twawala ya makamu wa Rahis kumtuma fisadi Eddie Luwasha amwakilishe kwenye kudhalilisha mahekalu ya God na kutoa hongo kwa viongozi waroho wa kiroho! Sasa nimekuelewa endelea.” anachomekea Kapende.
Kabla ya Mgosi kuendelea, Mpemba anakwanyua mic na kulalama ile mbaya, “Hivi kweli nyumba ya Subhanna yawezachangiwa na wenye dhambi hasa wezi, wauza unga na malaya wa kisiasa kama chama twawala? Wallahi kama waja wangefufuka, bila shaka Sayyidina Umar ibn Al-Khattab angechinja ntu hapa tena hadharani.”
 Mipawa anakubaliana na Mpemba, “Nyumba ya namna hii bila shaka itakuwa chafu na yenye wingi wa madhambi kiasi cha kutoweza kutoa msamaha wa dhambi.” Anapiga funda mbili tatu na kuendelea, “Hata dua zinazoombwa mle huwa hazifiki kwa mujibu wa sisi maulamaa. Ukisikia ukafiri ndiyo huu.”
Mzee Maneno anauliza swali, “Je hawa wanaochangia kuelekea uchaguzi walikuwa wapi?”
Msomi Mkatatamaa anaingia kwa usongo na kusiliba kwa sana tu, “Je hiyo fedha ni halali au ni ya unga, ujambazi na ufisadi? Ni jambo la hatari kwa wachovu kutegemea misaada badala ya kujengewa mazingira ya kujitegemea. Wawezesha wajenge makanisa na misikiti kwa fedha yao halali badala ya fedha chafu na ya fedheha. Kaya haiwezi kuendeshwa kichokoraa na ikawa kaya. Rahis anaombaomba, mashehena wanaombaomba, wachunaji nao kadhalika.”
“Msomi tafadhali usinilize mkanicheka. Huoni kila kitu kayani kinategemea michango na misaada ya kipumbavu tena ya wale wanaotuibia tukiona? Hata hao wanaojifanya kumwaga mabilioni wameyapata kwa kununuliwa na jamaa hawa hawa ambao ni maarufu kwa kuchangia kila kitu kuanzia michezo na kila kitu wakati wakikwepa kulipa kodi na kufanya biashara nyingi haramu. Nadhani mnawajua,” Anazoza Mheshimiwa Bwege huku akimkata jicho Kanji.
Kanji naye anakula mic, “Mimi kwisajua yote tasema hindi. Siyo hindi yote natoa ruswa au kwepa kodi au pewa samaha ya kodi dugu yangu. Hindi nyingine sikini ya Mungu kama veve dugu yangu.”
“Hayo wayasema wewe. Mimi sijataja mtu vinginevyo ajitaje mwenyewe. Ukiona anayelalamika jua yule yule.” Anazoza Mheshimiwa Bwege.
Mijjinga ambaye amerejea hivi karibuni kutoka Kisesa anaamua kula mic kwa fosi, “Ukiona viongozi wa duni wanafunga ndoa na wanasiasa ujue hivi vitu vinachanganyikana. Ubaya ni pale wanasiasa watakapopata watakacho wakaanza kuwageuka wenzao wa dini kiasi cha kulete hali tete kayani.”
“Hawa wanatumiana tu hakuna mwenye mapenzi na mwenzake,” Mbwamwitu anarusha kimondo.
Sofia Lion aka Kanungaembe aliyekuwa kimya muda mrefu anaamua kunyaka mic, “Kanji huna haja ya kujitetea. Ni kuwadharau tu. Watasema  mchana usiku watalala huku mkiendelea kufaidi maisha bora kwa wote wenye kujibidisha. Halo halo!”
“Sofi acha kujichamba. Kama maisha ni kwa wote inakuwaje wewe hatuoni huo ubora zaidi ya kujigongagonga?” Mchunguliaji anaamua kumtolea uvivu Sofi.
Kapende anachomekea, “Mpe dozi yake hadi azimie.” Sofi anamkata jicho la hasira na kugeuka upande mwingine akisonya.
Mpemba anaamua kurejea kwa chati, “Mie wallahinaona huu licha ya kuwa wizi na ni ufisadi wa kisiasa unolenga kueneza ugaidi baadaye. Kwanini hawa wachanganya dini na siasa wakati watwamba sie tusifanye hivo?”
Mipawa anabuna mic, “Leo wamo kitanda kimoja wakiangusha vicheko. Baada ya kugeukana utayasikia wakitishia usalama wa kaya. Hawana maana hao wala ndoa ya kudumu nakwambia.”
Mgosi anaamua kukatua mic, “Waahi hawa mashehe na wachungaji wanaojiahisi kwa wanasiasa si mashehe wala wachungaji kitu bai mashehena na wachunaji. Wanachuna mabuzi ya kisiasa na kujaza matumbo yao ambayo ni shehena bila shaka.”
Mbwamwitu anampa tafu Mgosi,“Hii pwenti nimeikubali. Kweli, machangu wa kisiasa wanawahonga machangu wa kidini kwa uroho wao halafu wanajitia watu wa sir God. Mshindwe na mnyong’onyee mnaochangisha fedha chafu kujenga hekalu la baba yangu.”
Kapende anaronga tena, “Hivi kweli Kanisa au Msikiti unaweza kuchangiwa na mafisadi kama Ewassa kweli? Mbona mnatutia midole machoni na kututukana matusi ya nguoni?”
Msomi naye anarejea kwa chati, “Afunike asifunike lazima kwenye urahis afunikwe. Anapoteza muda wake hasa ikizingatiwa kuwa afya yake kimwili na kisiasa ni ugogoro mtupu. Nani anataka recycled rais kwenye ikulu akaibe na kujineemesha zaidi? Nani anataka rais mgonjwa ambaye atatumia muda na fedha nyingi kwenye matibabu? Hapa kuna haja ya kukpia afya za wanaotaka kugombea urahis.Hivi walioshindwa uwaziri mkubwa watauweza urahis kweli?”
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita fisadi Luwasha mmoja. Wacha tumtoe mkuku!
Chanzo: Tanzania Daima Mei 27, 2015.

Monday 25 May 2015

Wabunge mabubu wasirejeshwe bungeni


Hivi karibuni vyombo vya habari vimetoa ripoti ya uchangiaji wa hoja bungeni kwa wabunge. Kwa ujumla wabunge wa upinzani wameonyesha kutoa michango mingi tofauti na wale wa chama tawala. Inashangaza kuona mwakilishi wa wananchi anakaa bungeni kwa miaka mitano bila kutoa mchongo wowote wala kuuliza swali au kuuliza maswali machache kana kwamba huko atokako hakuna matatizo. Je wabunge wa namna hii mabubu wanafaa kurejeshwa tena bungeni wakati hawana cha kufanya kule zaidi ya kupata posho kwa kukaa kimya bungeni? Je wananchi wanapomchagua mtu awawakilishe anakwenda kule kuwa sanamu au chachu ya maendeleo kupitia hoja na michango yake?
          Katika makala hii hatutataja majina ya wabunge waliotajwa ima kwa kuchangia sana au kutofanya hivyo kabisa. Cha msingi, ni kuwataka wapiga kura wawapime wabunge wao wa sasa kutokana na kazi zao bungeni na majimboni. Kama mnagundua kuwa kumbe mliyemchagua awawakilishe aliwakilisha tumbo lake kwa kuvuta posho basi msimrejeshe. Maana kufanya hivyo kutawachelewesha wakati wenzenu wakipaa.
          Kwa wanaojua mantiki ya kuwa na bunge ili kuwakilisha mawazo ya watawaliwa, bungeni si sehemu ya kulala, kukaa kimya au kuvuta posho. Bungeni ni uwanja wa vita ya kuwakilisha mawazo na matatizo ya unaowawakilisha. Ni uwanja wa vita ya maendeleo hoja na michango mbalimbali. Ndiyo maana wabunge wamepewa uhuru kikatiba kuongelea jambo lolote bila kuchelea kufikishwa mahakamani.
          Hata hivyo, kuna haja ya kudurusu ni kwanini wabunge wengi hawachangii bungeni. Wapo wanaolala kutokana na kutoiweza kazi ima kwa ugonjwa, uzee hata kutokuwa na sifa za kuwasemea wenzao. Wengine ni watoro tu kama alivyobainisha spika wa bunge hivi karibuni aliyekaririwa akisema, “Kuna wabunge wanatoka na kusafiri bila ruhusa, hivi mkipata ajali huko mtasemaje?”  Ni bahati mbaya spika hakutaja wanakopenda kusafiri. Hata hivyo, inakuwaje mbunge aage jimboni mwaka anakwenda bungeni aishie kupanga safari nyingine?
          Wananchi hasa wapiga kura wanapaswa kutatua tatizo la wabunge watoro na mabubu kwa vile wanawafahamu. Wengi wanaweza kutochangia hata kutoroka bungeni bila woga na badala yake wakahangaika na kutafuta fedha ya kuhonga wapiga kura ukifika wakati wa uchaguzi. Wananchi wanapaswa kukataa kununuliwa na kuishia kuwa wahanga wa jinai hii. Wakija na fedha walizozipata kwa kutumia ubunge na kutumia muda wa bunge kufanya biashara kuleni na wanyimeni kura hasa ikizingatiwa kura ni siri. Vinginevyo, majimbo yanayoongoza kuwa na wabunge mabubu wasilaumu mabubu hawa watakaposababisha waachwe nyuma kimaendeleo. Mbunge ni mshenga wa wananchi kwa serikali.   Hpaswi kuwa bubu au kwenda kuupiga usingizi bungeni kama ambavyo wengi wamewahi kupigwa picha wakiuchapa usingizi bungeni utadhani bungeni ni nyumba ya kulala wageni. Hawa wanaopenda kulala kama vichanga wasipewe kura ili wakalale vizuri majumbani mwao badala ya kuangusha wananchi waliowaamini na kuwapa dhamana ya kuwawakilisha wakaifuja.
          Nadhani kitu kingine kinachowapa wabunge mabubu motisha na kiburi ni ile hali ya kuawa katiba kielelezo iliyokuwa na vipengele vilivyotaka wananchi wawawajibishe wabunge bila kungoja ukomo wa vipindi vyao. Laiti wananchi wangejua kuwa vipengele hivi vililenga kuwakomboa wasingeruhusu kikundi cha watu kuua katiba hii ya ukombozi na kupandikiziwa ya kifisadi wanayoshawishiwa waipigie kura wakati haina maslahi kwao bali kwa kikundi cha walaji wachache.
          Kimsingi, wabunge mabubu ni zao la mfumo mbovu wa utawala uliojikita nchini ambapo mtu akishapata cheo anakigeuza kuwa mali binafsi badala kuwa dhamana. Mtu wa namna hii haogopi chochote kwa vile anajua wale waliofanya kosa wakampa dhamana hawana ubavu wa kumtimua. Hivyo, sehemu nzuri ya kutimua wabunge mabubu ni kwenye sanduku la kura. Nadhani sababu ya wabunge wengi tena wa chama tawala kutochangia ni ile hali ya kujiamini kuwa chama chao kikiwapitisha kitafanya mambo wapiti kama ilivyotokea kwenye uchaguzi uliopita hata kama wapiga kura watakuwa wamewakataa. Hii maana yake ni kwamba wananchi wanapoamini kuwa aliyepitishwa siyo waliyemchagua basi wamgomee asiapishwe kuwawakilisha. Wananchi wanajua mengi. Wanawajua wabunge waliopandikizwa na chama baada ya kushindwa kwenye sanduku ya kura. Wanajua jinsi wabunge wengi wa chama tawala wapo bungeni kutokana na jinai ya uchakachuaji iliyofanyika kwenye uchaguzi uliopita. Mwaka huu wasiruhusu upuuzi huu kuendelea kuwahujumu wakiachwa nyuma kimaendeleo. Hivyo, uchaguzi ujao uwe ni uwanja wa kuwauliza wabunge wao walichofanya cha maana kwa muda waliokaa bungeni wakipiga usingizi, kutoroka na kugeuka mabubu huku wakivuta posho bila stahiki. 
          Hata bila kuandikwa magazetini, wabunge mabubu na vilaza wanafahamika. Kadhalika wabunge machachari na wahangaikaji wanajulikana. Wabunge wanaokwenda bungeni kupiga dili kama wale walioshutumiwa kuomba rushwa serikali za mitaa ili kupitisha mahesabu yao wanafahamika kwa sura na majina. Wahalifu kama hawa hawapaswi kurejeshwa bungeni. Na hii ikifanyika, itatoa onyo na somo kwa wengine wanaopanga kwenda bungeni kuchapa usingizi au kupiga madili.
          Tumalizie kwa kuhitimisha kuwa wabunge mabubu na wavivu wa kujenga, kutoa hoja na kuuliza maswali hawapaswi kurejeshwa kwenye bunge kwenye uchaguzi ujao. Watakaowarejesha wajilaumu badala ya kulaumu wale waliowachagua wakijua hawafai hata kuwa wawakilishi wa nyumba kumi.
Chanzo: Dira.

Saturday 23 May 2015

Open letter to president Nkurumbwiza

  • ... rise in Burundi protests; protesters vow to remain - StamfordAdvocate
    Dear Monsieur Pyere Nkurumbwiza,
Boozers from Urundi confided me that you want to sip more from the chalice of power. Boozers there are still hell bent to bar you come shine come rain. It is easier to predict the way things could go.  The unfolding crisis you’ve caused is an extraordinary problem that begs for an extraordinary means to reach the solution. See? Slowly the hunk’s cascading into her violent past after having a ten-year reprieve. My ganja tells me that shall any Armageddon happen, you’ll be held accountable.
Guess what. All heavens broke loose when you wanted to run for the third term contrary to the very constitution you appended your signature to protect. Now that you’ve purposely decided to stay put by even being ready to see the hunk go to the dogs so that you cling to power, Boozers’ Organization known as the East African Calamity (EAC), needs to reign in.  Again, when we consider what’s been going on vis-a-vis power hunger and greed, does the EAC have what it takes to take on you while what he’s attempting is not new in the community?  Apart from Nyayo hunk and Bongo, who’s clean enough to tell you to pack and vanish? It is only boozers. Is it possible for the EAC –as a bloc –to take on you?
Again, looking at policy differentials whereby the EAC is divided between CoW and TABU or Tanzia and Urundi, no hunk has any moral authority to reign in. At least Nyayo hunk’s more lucidity compared to the rest. Again, looking at her quandary in Somalia, no way she can add another bone to her plate.  Bongo comes second however it is a close associate of Urundi. Given that Nyayo hunk is already overbusied in Somalia, Bongo needs to put her individual interests aside and take on you knowing that if she looks at personal attachment, shall things go overboard, everything’ll become a very ugly history. Bongo’s the only player that can save EAC’s face. Firstly, it has the strongest and most experienced army. Secondly, she bears the brunt when refugees start thronging on her borders.  When it comes to other members, their heads have already committed the same sacrilege Nkurumbwiza is endeavouring.
Let me tell you point blank: The hunk is more vital than you. What you’re attempting failed in Malawi, Senegal and Zambia among many. If you think you love your hunk as you portend to serve, you’d abandon your project. What’s seen in Buja streets suffices to convince any sane person that the third term is but a knob that’ll signal Urundi to the Armageddon. If your aim is truly to serve Urundi but not to serve your hidden agendas, you’ve all you need to abandon your shot on the third term. Underscoring this means that you’ll put the nation before anything including your love to serve. If those you want to serve have declined, why’d you force? Forcing will be construed as having person interested wrapped in serving the country.
Looking at a very convoluted and violent history of Urundi, whoever loves this tiny country will be ready to sacrifice anything in order to avert her from harm’s way.
However, you might think he’s the point in that your first term in office resulted from being voted for by parliament but not all Urundians. Again, Urundi constitution is clear about this. It says that the president must be voted for and must serve no more than two terms. Now that thousands of Urundians have already fled the country after demonstrations against your third term started. 
All those are but writings on the wall for whoever loves Urundi to call it quits as far as the third term is concerned. If anybody puts the hunk before his personal interest (s), what’s going on in Urundi suffices to convince him to think twice. No ruler can rule a chaotic country. You need to be helped out of this impasse. Tell him to stop his ballyhoos of “My party wants me to run.”  Again, who knows? Things can go out of control so as to guarantee your destination to be The Hague. You ordered army to take control of the situation after saving you from being toppled. You can’t foresee what the minds of those he orders are. One bullet can cause a fatality that can trigger more chaos. Shall this happen, you’ll be answerable.
So, too, underscoring economic dependence Urundi has always faced, one’d think that you’d, so, too, consider it. Urundi is one of the poorest hunks on earth. Give her a break. What transpired in 1972 and 1993 suffice to move any sane and patriotic soul to put whatever hidden or in store for him to the stop for the love of his nation. All boozers in Africa, especially, those in EAC need to be strong on you underscoring the mess your move’ll add on the already deeply felt mess of tampering with the constitutions.
Monsieur, Nkurumbwiza, Urundi is more than your dubious presidency.  Please abandon your third- term project for the love of Burundi. What a wonderful legacy!
Source: Guardian May 24, 2015.

Friday 22 May 2015

Mlevi kumkabili Nkurumbwiza

  • Burundi : le président Nkurunziza appelle à cesser les ...
       Baada ya wachovu wa Urundi kulianzisha wakipinga upuuzi wa mlevi mmoja wa madaraka Pyere Nkurumbwiza kutaka abaki madarakani kinyume cha sheria ili akwanyue zaidi, dunia ilishangaa sana roho mbaya ya njemba hii.
Waurundi walifanya kosa kutaka viranja wa East Africa Calamity waingilie kati wakati nchezo wao ni ule ule. Nani amuonye au kumshugulikia nani wakati nyani wote kazi yao kuiba mahindi? Ukiangalia Bongolalaland, Chama Cha Mang’ang’anizi (CCM) kimekuwa madarakani tangu kikiwa kinda hadi sas kikiwa kikongwe kilichoishiwa si meno bali hata kupofuka na kupoteza kumbukumbu kikigeuka mhimili wa ujambazi, ufisadi na kila jinai
Ukienda pale UG uchafu ni ule ule. Imla wao wa muda mrefu –licha ya kuchanganyikiwa na kudhoofu kimwili na kiakili –bado yumo madarakani akiendelea kuiba na kutanua na genge lake la kikabila.
Pale jirani kwa jamaa zangu wa kunyotoana roho wao kwa wao mambo ni yale yale mchezo ule ule njemba ile ile.
Kwa akina Nyayo ndiyo usiseme. Jitu linachaguliwa kwa vile baba yake alikuwa rahisi ukiachia mbali kupiga kura kikabila. Waulize akina Uhuu Kinyata waliingiaje kwenye maulaji kama si wizi wa kura na ukabila. Je nani awasaidie hawa jamaa walioamua kujitambua na kufanya kweli? Natamani walevi wangu nao wangejitambua hivi na kulianzisha ili kuondokana na huu uoza na ufisi na ufisadi wa genge la mafisadi la Njaa Kaya.
Kimsingi, viranja wa EAC hawana ubavu wa kumwambia Nkurumbwiza asiendelee na mipango yake michafu kwa vile nao ni wachafu tena wengine kuliko yeye hasa ikizingatiwa kuwa yeye si wa kwanza kubadili katiba na kuendelea kuwa madarakani. Waulize akina M7 wametawala vipindi vingapi na wataondoka lini. They have no idea as to when they will relinquish sweet power. Nyani wote wana tabia zinazofanana. Hata hivyo, ni ajabu kwa jeshi kuvunja katiba na kudai linailinda. Kwanini wasiwaache Waurundi waamue wenyewe kwa kuwapa msaada wa kuzuia jeshi na Nkurumbwiza kuendelea kunajisi kaya? Mijitu mingine bwana, linang’ang’ania ikulu utadhani mali ya mama yake. Guess what. Mlevi alizaliwa peke yake.  Hivyo, alipokuwa mdogo aliamini ziwa la mama yake ni mali yake pekee. Hata hivyo, baada ya kupevuka aliachana na mambo haya ya kitoto ambayo yanafanywa na watu wazima tena wanaoitwa rahisi.
Baada ya kuona zali haliishi na wale wanaoonekana kuwa viongozi wakichemsha, Mlevi anajiandaa kutia timu Buja kumpa laivu Nkurumbwiza kukitoa kwa vile wachovu wa kule hawamtaki. Pia hii ni kupinga kutapatapa kwa katibu mkuu wa Un kumteua M7 eti ashughulikie mgogoro aliouanzisha yeye kwa kubadili katiba. Baada ya kumshawishi Bank in the Moon amebatilisha uteuzi wa M7 kwa kuniteua mimi.
 Nitafanya hivyo ili kutuliza hali na kuepuka kuongezeka ghasia kiasi cha kutujazia wakimbizi. Msituletee mbu kwa tamaa zenu ingawa wakubwa wetu wanaonekana kuwa kitanda kimoja na Nkurumbwiza kwa vile wanasifika kwa ung’ang’anizi na wizi wa kura.
Najua kwa anavyochukiwa na kupingwa, bila kuchakachua Nkurumbwiza hawezi kupenya. Sijui kwanini amengoja kiumane wakati kaya ni bora kuliko fisadi mmoja wa maulaji? Amesahau nini ikulu ana anang’ang’ania kulinda jinai gani zaidi ya ufisadi na ufisi?
Kwa vile mlevi ni kidume kisichoogopa mvua radi wala mtutu, nina mpango wa kutia timu kule na kumpa jamaa vipande vyake. Napanga niingie kininja nikiwa nimetinga jezi zangu za karate. Akijifanya hamnazo nitavunja mtu shingo bila huruma. Mdudu mmoja hawezi kujifanya alpha na omega wakati kaya ni mali ya walevi na wachovu. Kama  hawakutaki si uende ukafanya biashara nyingine kwani lazima siasa za urahisi? Si urejee chuoni ukapige lecture na chaki kama ulivyokuwa ukifanya kabla? Kama miaka kumi haikukutosha hata upewe mia haitatosha. Tafadhali bwana Nkurumbwiza. Natoa onyo kabla sijaingia. Kama utaendelea na utoto na uroho huu amini vitakutokea puani. Na ufahamu kabisa kuwa mimi huwa sitishi bali kufanya kweli hasa mibangi na gongo vikishapandisha Mwenembago. Ohooo! Shauri yako utaumia bwana mdogo Nkurumbwiza! Mie siyo kama hawa akina chekacheka wanaokuchekea.
Kama Nkurumbwiza anadhani ninatania basi akaulize kule Burkinabe na Libya nilipokwenda kutia timu hadi mibuyu ikadondoshwa huku wengine wakiuawa kwa kichapo kama vibaka wakati walikuwa mibaka.
Kwa vile mimi ni mpenzi wa demokrasia hata kama ni ya kuazima toka Ulaya, sitakubali ndata au Nkurumbwiza waendelee kuibaka kaya hii kiduchu kama mkoa wa Bongo. Nitahakikisha kinaeleweka na kushuhudia Nkurumbwiza akibwaga manyanga vingine kutachimbika bila jembe na patakuwa hapatoshi kusema ule ukweli.
Haiwezekani waafrika tuendelee kutawaliwa na miunguwatu na wakoloni weusi kana kwamba kaya zetu ni mali zao. Hata hawa waliochakachua katiba ya mzee Jose Waryuba wajiandae. Nikimaliza kutatua mgogoro wa Urundi lazima niwashukie kama sina akili nzuri.
Kwa vile nilipinga kutoa uachama wa EAC kama pipi kwa viichi visivyo na wakubwa wenye adabu, nikimaliza kutatua mgogoro huu lazima niende kwa pilato kupinga uanachama wa kaya zisizofuata demokrasia. Kimsingi, hapa ninachotaka ni kuvunjilia mbali hili genge la EAC ambalo halina maana zaidi ya shoptalk za wakubwa zake. Kama mnataka kufanya kweli basi unganisha bara zima la Afrika ili muionyeshe dunia mlivyojikomboa. Maana hii mipaka na utaifa mnaolingia vilipandikizwa na wakoloni ili kudhoofisha Afrika kwa kuipatia watawala manyag’au iendelee kurudi nyuma. Akina Fredrick Lugard yule bingwa wa Divide and rule and then depart hawapo tena zaidi ya kuwa na Lugard weusi waliojazana kwenye ikulu wakikwamisha muungano wa Afrika. Huwa sipati mantiki ya Afrika kuwa na vipande vya kaya.
Go Nkurumbwiza go
Go never turn back, go
Go Nkurumbwiza go.
Chanzo: Nipashe Mei 23, 2015.

Wednesday 20 May 2015

Na kweli hawa mabuda wako nusu uchi

Kikwete anapouuza twiga akaahidi kutunza mbwamwitu!

  • Kikwete officiates the release of second pack of 15 wild dogs ...
  • Hotel Strand-Café Lang in Langenargen am Bodensee
 
Rais Jakaya Kikwete ni mtu asiyeishiwa vituko. Wakati mwingine akiongea –licha ya kujipinga hata kujipiga kijembe –wenye kuchambua mambo hushangaa kama anasoma hizo hotuba anazoandaliwa kabla au kusema baadhi ya mambo akiwa anajua uhalisia wake. Maana mambo mwengine anayosema yanamsuta na kumuacha akionekana tatanishi kwa umma unaoyapokea. Hivi karibuni Kikwete aliwaacha wengi hoi aliposema, “Kazi niliyoamua kufanya sasa na baada ya kuacha urais ni kusaidia uhifadhi.”  Kwanini baada ya kustaafu na si wakati akiwa madarakani? Nadhani kama rais alikuwa na nia njema na mali na raslimali za taifa wakiwamo wanyama, angetumia rungu lake kama rais kupambana na ujangili ambao unatishia kufuta baadhi ya wanyama wetu kwenye ramani ya nchi na ya dunia.
Vituko na maneno ya Kikwete yanatukumbusha aliposema kuwa wanafunzi wa kike wanaopoachikwa mimba na vishoka ambao hawashughulikiwi wanaponzwa na kiherehere chao wakati umaskini na ufisadi uliotengenezwa na watawala kama yeye una mchango mkubwa pamoja na sababu nyingine. Je halijui hili au hajajulishwa? Je alionaje kuwa ni kiherehere tu na si umaskini, ugumu wa maisha, ukosefu wa huduma kama vile usafiri kwa wanafunzi, walimu wa kutosha na kutamalaki kwa rushwa ya ngono pamoja na mambo mengine? Je hivyo navyo ni kiherehere au waliovisababisha nao wana kiherehere?
Kikwete aliahidi kutumia muda wake wa ustaafu kuwatunza mbwamwitu. Wengi walidhani –kwa vile wanyama kama Tembo na Faru ndiyo wanakaribia kumalizwa –lau angeanza na hawa ingawa nalo laweza kuwa siasa tu majukwaani kutokana na ukweli kuwa  hakuwalinda vilivyo wanyama hawa wakati akiwa madarakani sawa na alivyofanya kwa vitu vingine kama mikataba ya uwekezaji aliyoahidi angeiweka wazi na kuifumua na kuisuka upya asifanye hivyo. Hata hivyo, wanaomfahamu Kikwete kama mtu mwenye kupenda kusema maneno mengi ya kufurahisha na kutoa ahadi kemkem asitekeleze hata moja hawamchukulii seriously. Yako wapi maisha bora kwa wote aliyoahidi akiingia madarakani au nayo atayashughulikia baada ya kustaafu? Inashangaza mantiki ya Kikwete kuona mbwamwitu ndiyo wa kutunzwa wakati tishio la kutoweka kwao wala thamani yao havilingani na la twinga na faru. Ni ajabu kuwa na uchungu na mbwamwitu ukaachia wanyama walio kwenye hatari ya kutoweka kama tajwa hapo juu watoweke.
  Kama wanyamapori wameteketezwa hadi kuuzwa nje wakiwa hai na hakufanya lolote atajitosa kufanya nini na kwanini sasa baada ya wanyama wenyewe kutishia kutoweka? Ina maana Kikwete amesahau mkasa uliotokea chini ya uangalizi wake na asichukue hatua hapo Novemba 26, 2010 ambapo wanyama wapatao 150 wakiwamo twiga hai walisafirishiwa kwa dege la kijeshi kwenda Qatar? Je alifunga wangapi ukiachia mbali serikali yake kujenga mazingira yaliyomwezesha mtuhumiwa toka Pakistan kutoroka kwa hofu ya kuwaumbua wakubwa waliokuwa nyuma ya ufisadi huu wa kishenzi na kutisha? Kwa mtu mwenye uchungu na raslimali za nchi tukio kama hili lingeonyesha uchungu na ukali wake dhidi ya jinai hii, lakini wapi. Kwanini kufanya hivyo baada ya kustaafu ambapo hatakuwa na madaraka na kushindwa kuwatunza alipokuwa na madaraka?
Kikwete alikaririwa akisema, “Ni aibu wanyama hawa muhimu kwa utalii kutoweka kisha baadaye tuwatafute kwa gharama kubwa… Mimi niko tayari kusaidia wanyama hawa wasipotee.”  Je hao wanyama waliosafirishwa kwenda Qatar wakiwa hai hapo mnamo tarehe hawakuwa wanyama? Kama ni aibu basi mwenye kuistahili na aliyeilete si mwingine ni Kikwete ambaye serikali yake ilishiriki kikamilifu kuwatorosha wanyama huku katibu wa wizara wa wakati ule aliyetuhumiwa moja kwa moja kusuka na kutekeleza uhujumu huu akiteuliwa balozi kwenye nchi moja jirani. Kama Kikwete ana uchungu na wanyama kama anavyotaka aonekane, ilikuwaje akampandisha cheo mtu mwenye kushutumiwa ambaye ukiachia hilo alipaswa amwajibishwe kwa sababu wizara yake ilishindwa majukumu yake kiasi cha kuruhusu wanyama hai wasafirishwe tena kupitia kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Je serikali ya Kikwete inaweza kukwepa lawama kwa hili iwapo hata walinzi wa uwanja wa ndege hawakuwa na uwezo wa kuzuia hao wanyama kutosafirishwa kwa vile ulikuwa ni mzigo wa wakubwa? Je hapa Kikwete ana tofauti na rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ambaye chini ya utawala wake mbuga maarufu ya Loliondo iliuzwa kwa waarabu hao hao kutoka Ghuba? Je huku si kukumbuka blanketi asubuhi kama siyo porojo za kisiasa?
Tumalizie kwa kumshauri Kikwete aache kututia vidole machoni na kutudhihaki kuwa atatunza wanyama wakati serikali yake ilihalalisha ujangili kiasi cha kutisha.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 20, 2015.