The Chant of Savant

Wednesday 29 July 2015

Kijiwe kumfuata mkuu ugenini kumuaga

  • Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili katika ...
          Baada ya kungoja muda mrefu mkuu aje kukiaga bila mafanikio, Kijiwe kimekuja na ubunifu mwingine. Kwa vile jamaa amenogewa kwenda kutanua ughaibuni kwa kisingizio cha kuaga wageni utadhani ndio waliompa kula ya kura, basi Kijiwe kimeamua kumfuata huko.
Mgosi Machungi ndiye analinzisha kwa kulalamika, “Jamani hebu tisaidieni. Huyu mkuu mbona kia siku kiguu na njia akienda ughaibuni kuaga kunani jamani? Mbona hatimueewi au ndiyo anaaga njuuku zetu kwa kuzuua zaidi?”
Mijjinga anaamua kukamua mic hata kabla ya Mgosi hajamaliza, “Usemayo ni kweli. Kwani ni juzi tu alikuwa Ufaransa, Norway na Uswizi. Hata kabla hajapoa huyo, Australia. Nadhani kuna biashara ambayo hatujaijua inaendelea.”
Kapende anakula mic, “Wewe unashangaa hii. Juzi ukimsikia rahis Salama naye akiwa ziarani kule Malaya? Hawa inaonekana walilogezewe kuzurura.”
Mpemba anakula mic, “Unasemaje alhaj Kapende eti rahisa? Baba ni rahis na mama rahisa siyo?  Hata hivyo, siamini kama hawa wazurura. Huenda wanayo miradi yao wenda kule kuikagua na kuchaji akaunti zao huku. Humuelewi hii? Hebu fikria kwa mfano umauona rahisa akikagua karakana za kutengeneza treni bila kuwa na waziri wa uchukuzi wala katibu wake mkuu. Anafanya hivyo kama nani kama si mradi wao?”
Machungi anakatua mic tena, “Jamani timfuate huko huko nasi timuage ndipo awaage wapendwa wake. Maana inaonekana kama hatina samani na kua zetu ziipotea bure.”
Mbwamwitu anakwanyua mic, “Acha mwenzenu aage. Maana, katika mambo yatakayomkondesha baada ya kuachia ulaji ni kukosa fursa ya kwenda kutanua ughaibuni. Kama tutapata mtu makini uwezekano wa watu kunyea debe ni mkubwa nawambia aminini.”
Mjumbe mpya Chilumba anaamua naye kula mic kwa mara ya kwanza, “Unadhani mwenzenu anakwenda kutanua tu? Kuna jamaa yangu mmoja wa inteligensia aliniambia kuwa jamaa huwa anahaha kutibu saratani. Ila aliniambia nisimwambie mtu maana hii ni top secret.”
Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kula mic, “We acha uongo. Kama uliambiwa usimwambie mtu kwani sisi unaowaambia ni nyani? Je huyo aliyekwambia alidhani ulikuwa nyani hadi akwambie mambo ambayo watu hawapaswi kujua au ni uongo na ujuha tu?”
Chilumba anajibu tena kwa hasira, “Da Sofi hata kama mimi ni mgeni tuheshimiane pasije kuchimbika bila jembe kwa kutetea huu uoza wako. Unadhani ninakundanganya wakati mimi mwenyewe ni mtu wa usalama?”  Baada ya kutamka hayo tunaangaliana kuonyesha kuwa hii namba sasa hatari. Ni kamba tupu.
Mheshimiwa Bwege anadakia, “Mie ndiyo maana sitafanya kosa nikipe chama cha Maulaji kura yangu. Angalia mzee Tunituni che Nkapa. Alizurura na kuruhusu kimada wake aibe wee. Sasa wako wapi. Alikuja huyu mbayuwayu naye akamruhusi manzi wake aibe wee na kuzurura wee. Sasa yameisha. Nadhani kama tutamchagua mzee Kanywaji naye atageuka Vasco da Gama. Kwani kuzurura ndiyo sera yao tangu enzi za Nkapa che Makapi Tunituni wa Achimwene.”
Msomi Mkatatamaa aliyekuwa akiangalia na kutabasamu anaamua kutia daruga, “Nyinyi humjui. Mara nyingi chaguzi tunazofanya tunapiga kura kama kutimiza mradi tu hasa ikizingatiwa hawa waagwa ndiyo wanaolipia chaguzi na serikali tunazoita zetu. Kimsingi tunachojivunia kuwa uhuru si chochote wala lolote bali ukoloni mamboleo. Mbona mzee Mchonga alipoachia madaraka hakwenda kuaga hao wakoloni? Ni kwa sababu alikuwa hawategemei wala kujigonga gonga kwao.”
“Msomi umetoa mapwenti ya nguvu. Mbona Joji Kichaka alipomaliza muda wake wa kufanya ugaidi hakuja kuaga huku Uswekeni? Kweli nimeamini. Tunapaswa kudai uhuru upya ili tuwe na viongozi badala yak uwa na watawala na wazururaji ombaomba wenye kujigongagonga.” Anajibu Kapende.
“Yote tisa.  Kumi ni pale waliojisahau baada ya kufadhiliwa kujikuta wakiwa uchi mbele ya kadamnasi. Sijui ndugu yangu Salva Rweyependekeza atakuwa mgeni wa nani baada ya Njaa Kaya kutimua?”
“Atarejea kwenye umbea wake na kutafuta wa kusifia ili ampe mlo hata kama ni mabaki ya mezani.”
“Kweli vatu mingi hapana jua kwanini kuu nenda aga ghaibuni. Kama veve nakwenda ombaomba napewa juluku kama hapana aga ile nakuja napata tabu. Fazili hapana nasaidia yeye sikini endesha kaya yake.”
“Kanji acha huni veve. Sasa iko sema kuva tafata Kwete ghaibu aga yeye. Mimi iko pendekeza Somi na Payukaji changia nenda ghaibu fata kuu eleza yote vananchi nataka.” Anachomekea Mbwamwitu kwa lafudhi ya Kihindi.
“Yakhe tuache utani wallahi. Wazo la Nbwamwitu la maana ati. Kwanini tusichangishane njuluku na kumtuma mtu au watu wawili kumfuata huko ghaibu na kumfikishia salamu zetu?” Mpemba anamuunga mkono Mbwamwitu.
Msomi anakula mic, “Hata kama jamaa huwa anajifanya hamnazo, angalau kitendo cha kumfuata kwenye matanuzi yake na kumghasi hakitambadili, kinaweza kumbeep atakayemrithi. Hivyo, naunga mkono mia kwa mia mpango huu ambao kama utafanikiwa unaweza kuwa suto kwa wengi wajao na wababaishaji kwenye ofisi kuu.”
Kijiwe kikiwa kinanoga si ukapita msafara wa raisa Salama Kiwewe! Acha tuutoe mkuku kwa kuuzomea, kuumwagia kashata na kuurushia kahawa! Kimsingi, kwenye uchakachuaji ujao lazima nambari wani ipigwe chini. Maana hata ikimteua Kanywaji bado mambo yatakuwa yale yale. Heri kuwapa wapingaji nao wakajaribu kutuonyesha vitu vyao au vipi?
Chanzo: Tanzania Daima Julai 29, 2015.

Sunday 26 July 2015

Kingunge anaibeep CCM au kuitisha?


 Hivi karibuni aliyekuwa mpambe mkuu wa mtia nia ya urais aliyebwagwa hivi karibuni waziri mkuu aliyeachia ngazi kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa, mzee Kingunge Ngombale Mwiru alitoa mpya.  Alikaririwa akisema, Jitihada zote ambazo zimefanywa za kuvunja taratibu zilikuwa zinaelekezwa kwenye kumzuia Lowassa asipate haki. Badala ya yote nani kashinda? Kashinda Lowassa kwa sababu imeonekana wazi kuwa yeye ndio kipenzi cha Watanzania na hakuna kitu kikubwa kama kupendwa na watu.” Kwanza, Kingunge anaonekana hajaridhika na maamuzi ya vyombo vya juu vya chama chake. Pili, anavituhumu kwa kumdhulumu mgombea aliyetaka ashinde. Tatu, ni kama anatishia chama kimtambue lau kumpa prominence mtu wake akitaka awe kile waingereza huita king maker. Je Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitapokea na kutishwa na kitisho cha Kingunge? Je Kingunge anaongea kwa niaba yake binafsi au ametumwa na Lowassa?
Wapo wanaoona kama Kingunge anajisumbua bure kwani maamuzi yameishafanyika na kupita na CCM kimeishapima upepo na kuona uamuzi wake hautakisababishia madhara zaidi ya faida.  Kingunge anasema CCM imuangukie Lowassa ili isishindwe iwapo Lowassa hatamuunga mkono mgombea wa CCM Dk John Pombe Magufuli. Je hii ni kweli kuwa ili Magufuli ashinde anahitaji kushikwa au kuungwa mkono na Lowassa?  Wapo wanaoona kama Lowassa atajitenga na Magufuli, atampunguzia kazi ya kujinadi hasa ikizingatiwa kuwa tuhuma nyingi za ufisadi zinazomkabili Lowassa zinaweza kumharibia Magufuli hata kama Lowassa anaungwa mkono na watu wengi.
Kingunge aliendelea kusema, “Kuanzia sasa wana-CCM tutafute namna ya kushikamana vizuri, tuimarishe umoja wetu maana ndio nguvu yetu na katika hili ndugu Lowassa ana nafasi muhimu na ya kimkakati ana mamilioni ya Watanzania wana imani naye.” Kama tutakuwa wakweli, nani kati ya Lowassa na Magufuli ni kipenzi cha watanzania na kwa sababu gani? Lowassa anasifika kwa kutimliwa madarakani kwa tuhuma za ufisadi.  Pia kwenye mchakato uliopita alisifika kwa kumwaga fedha ambazo hakuzitolea maelezo alivyozipata ukiachia mbali kucheza rafu hadi akapewe adhabu. Kwa upande wake, Magufuli anasifika kwa uchapakazi, kutokuwa na makundi, kutotumia fedha kwenye mchakato na kutokabiliwa na tuhuma za ufisadi. Sijui kwa kuangalia sifa hizi ni nani anapaswa kuwa kipenzi cha watanzania kweli? Ama kweli mwenye mapenzi haoni. Wahenga walisema.
Wapo wanaoona kama Kingunge anatapatapa bure. Maana wenzie chamani wanaonekana kumzoea ukiachia mbali kumchoka. Wapo wanaoona kama Kingunge la Lowassa wataendelea kutafuta kuwa king makers wanaweza kujikuta pabaya hasa pale CCM ikipuuzia kitisho chao na kuamua kuwashughulikia kulingana na historia yao ya nyuma. Sidhani kama kashfa iliyomhusisha mke wa Kingunge na familia yake pale kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani ilishasahulika na kuuawa kiasi cha Kingunge kuwa salama.
Kwa hali ilivyo, CCM haitakubali kutishiwa na Kingunge na Lowassa. Badala yake inaweza kuamua kuwashughulikia na wakasahulika katika siasa za Tanzania. Kwa mfano, mpaka sasa Lowassa analipwa marupurupu ya ustaafu wakati hakustaafu ukiachia mbali kutofikishwa mahakamani. Je Kingunge na Lowassa hawaoni kuwa wakiendelea kuitishatisha CCM inaweza kuamua kufungua upya mafaili yao na wakajikuta badala ya kuwa king maker wakaishia kuwa washitakiwa?
Pia kwa sifa na tabia ya Magufuli sijui kama anaweza kuwa wa hovyo kiasi cha kutegemea kuungwa mkono na Lowassa ili ashinde.
Inaonekana kushindwa kwa Lowassa kumemchanganya vibaya Kingunge. Wakati akitaka CCM ishikamane na kushinda kwa kishindo, haonekani kuamini kuwa haki itatendeka. Katika hili Kingunge alisema, “Mkitaka nchi ijiongoze lazima chama kijiongoze kwa kufuata misingi ya kidemokrasia. Watu wamehukumiwa katika vikao bila kusikilizwa. Kama makao makuu ya CCM yamepuuza haki ya wagombea, vipi kama hilo likitokea katika katika chaguzi za chama za mkoa, wilaya, kata na tawi.” Kimsingi, anachoonyesha Kingunge ni kwamba project yao ilikuwa kubwa. Baada ya Lowassa kubwagwa, sasa wana wasi wasi na watu wao mikoani na wilayani wanaweza kubwagwa.
Wengi wanaojua utaratibu wa CCM wa kushughulikia malalamiko kupitia vikao na taratibu za chama wanashangaa Kingunge kutumia magazeti badala ya vikao na taratibu husika. Je kwa kufanya hivi haoni–kama anazidi kuwachukiza wakubwa wa chama chake ambao kama wataamua kumjibu–wanaweza hata kumpatiliza zaidi tena kwa kuachana na malalamiko yake na badala yake wakamshughulikia kwa kuvunja na kupuuza taratibu za chama?
Kwa wajuzi wa siasa na staili ya CCM wanadhani anachofanya Kingunge hata Lowassa ni kulilia maziwa ambayo yameishamwagika. Hayatazoleka. Sana sana anaweza kuzidi kuwakorofisha wenzake wakaamua kumvua nguo na akamaliza maisha yake ya kisiasa vibaya. Yeye sasa anawatisha. Hawajamjibu wala kumtisha. Je wakiamua kumtisha kweli kweli atakuwa na utetezi upi?
Kwa wanaokumbuka kilichowafika akina Horace Kolimba, Seif Sharriff Hamad na mzee Aboud Jumbe, wanadhani Kingunge anatafuta la kutafuta na likimfika hatakuwa na namna ya kulikwepa wala kujitetea bali kuzama na kusahaulika ama kwenda kumalizia maisha yake kwenye upinzani. Je kama CCM watawapuuza Kingunge na Lowassa watachukua hatua gani au ndiyo mikakati ya kujiengua CCM kama njia ya kuiadhibu? Je Kingunge na Lowassa wanaibeep au kuitisha CCM? Maswali ni mengi kuliko majibu ingawa hali ilivyo, wawili hawa hawana jeuri ya kuihama CCM.
Chanzo: Dira Julai 2015.

Saturday 25 July 2015

Kinamna: Resign or shut up




















          Abdul-joyman Kinamna Gen. Sec of Chama Cha Mizengwe (CCM) is a very cagey character. Whenever he opens his mouth to speak, he does so perilously to his reputation and that of his outfit. On many occasions, this dude’s rants and raves against the powers that be sound dingy, doody and giddy. He says precarious hoo-has that insult human intelligence. One wonders: Why such a bigwig treats other Homo sapiens like beasts intellectually.  You still see him with his swagger wherever he goes adding more words that have no gravitas. Such a person can’t be left to get away with murder easily.
The other day I heard him insulting our hishimiwas saying that they blindly and myopically support all nonsense that the powers that be brought before the house. Again, one wonders: To whose advantage? Has he forgotten that when the hishimiwas gives his party hard time it calls them to Dodoma and threatens them?
I heard him in Mpwapwa saying, “The problem with many CCM members is that they are tolerant of corrupt leaders. But there are others who defend bad leaders. By doing so you are not helping your party.” He spoke as if he is not a member of CCM or the beneficiary of this nasty behaviour. To jog his mind, we need to revisit the allegations that he smuggles some ivories to Asia. Refer to the admission by the then minister for Natural Resources and Tourism Khamis Kagasheki who was quoted as saying, “This business involves rich people and politicians who have formed a very sophisticated network.” To prove how Kagasheki touched the high and the mighty, he was shown the door for blowing their cover.
Again, one wonders: If Kinamna abhors corruption, why is he still in the outfit that is renowned for being corrupt through and through? A fish and bird may fall in love but the two cannot build a home together. What is he waiting for in the party that is bankrupt and corrupt altogether?
Instead of jumping a smoking gun, Boozers would like to hear Kinamna launching his defense or making some clarifications about the allegations instead of keeping mum as he attacks our MPs not to mention misleading people. Boozers know too well that Kinamna wants to portray himself as a do-gooder amongst many political doo-doos. Again, Swahili proverb has it that if one fish rots, it rots all the others in the string.  No way, there is no way one can stay in a corrupt party and pretends to take on it. Get out of it and show who you actually are instead of double standards.
The nasty thing Kinamna does is not to think before talking. Remember when he called ministers burdens to end up swallowing his pride after his boss ignored him by retaining the same mizigo.  For a person with moral authority such a move would have warranted him to abandon the ship. Again, he didn’t. Why? He who lives in a glass house shouldn't throw stones at others.
However smart Kinamna may wrongly think he is Boozers have already known his hat tricks. When Kinamna attacked the hishimiwas one Boozer retorted, “Lao moja.” Literary they’re all the same and what Kinamna was trying to do is usanii like three cards’ conmen. Do you know what conmen known as karata tatu do? They fool lookers-on pretending they are playing cards to win while they actually are the part of the gang hell-bent to rob others through deceptions.
Boozers think that Kinamna must use right strategies and manners to ask for votes instead of fooling them as if they are androids. We’ve brains. We too, have human instincts and intellects. Sometimes, when we talk we need to make sure that there is a connection between our mouths and brains. So, too, we need to appreciate that knowing is an all-human gift but not solely ours however powerful, rich, cunning and shrewd we might think we are. So, when Mr. Kinamna speaks must appreciate the fact that we’re all endowed with this gift of intellect he wrongly uses in trying to dupe us. We’re boozers well. We are undupable so to speak. We truly know that what Kinamna is doing is but the art of deception based on self-deception that he can get away with it.
To crown it all, Kinamna left many shocked and choked when he said, “We want the tendency of transferring a person who has under performed at one place to another to stop immediately. There is no point of moving a person who has stolen from one station and send him to another; you are giving him opportunity to steal again.” Who commits such a crime resulting from nepotism and technical know who? If he were serious why didn’t he go and tell Kiquette such truth. For, he is the one who heads the govt that commits such bunkum.
Suffice it to say, Kinamna, please stop insulting our intelligence. As any bin-Adams, we’re gifted with brains that tell us that what you are doing is dupery by all definitions. Stop it please.
Source: Guardian July 26, 2015.

Kumbe CCM ni chama kabaila na kifisadi!



  • Chama-Cha-Mapinduzi.jpg

Wale waliosoma enzi za ujamaa watakuwa wanakumbuka dhana nzima ya ukabaila ambao ni utajiri unaotaokana na utumiaji ardhi kwa kukodisha kwa wasio nayo. Baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kushika hatamu zama zile kwa ajili ya kulinda maslahi ya wananchi, iliishia kupoteza sifa hii pale ilipojiingiza kweye unyakuzi wa ardhi. Tulizoea kusikia unyakuzi wa ardhi nchi jirani tusijue tutatawaliwa na chama nyakuzi chenye kuwa kabaila huku kikiendeshwa na mabwanyenye na mabepari. Kamusi ya Kiswahili Sanifu ya TUKI uk.297, inauelezea ukabaila kama: tabia au hali ya kumfanya mtu amtumikie huku mwingine akistarehe.Tabia ya kumilki majumba na ardhi kupangisha ili kuwanyonya wengine.

Kwa tafsiri ya kamusi ya TUKI, CCM ina sifa zote za kuitwa chama kabaila au cha kikabaila. Haya si madai yetu bali ukweli uliotoka kwenye vinywa vya kiongozi wake.

Akifungua ukumbi wa mikutano Dodoma hapo tarehe 9 Julai alisema kuwa CCM ina viwanja vingi nchini. Mfano, Dar pekee wana viwanja zaidi ya 400. Je huko kwenye majiji mengine kama vile Arusha, Mwanza, Mbeya, Tanga na kwingineko wana viwanja kiasi gani? Je wanavimilki kihalali hasa ikizingatiwa kuwa viwanja vile vilipatikana wakati wa chama kimoja ambapo serikali na chamavilikuwa kitu kimoja? Je kuna mantiki yoyote ya CCM kuendelea kushikilia, kukalia na kupata kipato toka kwenye ardhi ya umma? Je huu si unyakuzi (land grabbing) tuliozoea kuusikia kwenye nchi jirani? Je chama kinachonyakuwa ardhi ya umma kina tofauti gani na viongozi wanaofanya hivyo?

 Kikwete alikuwa akiwahimiza wenzake kuwa waache kuombaomba na badala yake waendeleze vile viwanja kwa manufaa si ya nchi bali chama.

Alilaumu tabia ya kutegemea wafadhili na kutaka CCM waendeleze vile viwanja. Je wataviendelezaje wakati si vyao?  Kikwete alishangaa ni kwanini chama chenye viwanja vingi namna hivi kutegemea wafadhili. Wengi waliona kama anajisuta bila kujua. Kama anashangaa chama chenye utitiri wa viwanja kutegemea wafadhili basi alipaswa kushangaa nchi yenye raslima lukuki kutegemea kuombaomba na kukopakopa. Alichofanya Kikwete kinakubaliana na msemo wa wahenga kuwa nyani haoni kundule.

Kitu kingine cha kushangaza na kusikitisha ni ile hali ya Kikwete akukiri kutojua hata hiyo pesa inayotokana na viwanja chini ya miradi haramu ya kulaza magari anayeipokea na anachoifanyia. Wengi walitegemea rais lau atumia muda ule kama rais na si kama mwenyekiti wa chama kukikumbusha chama chake kurejesha ardhi ya umma. Maana kwa CCM kuendelea kumilki ardhi ya umma kunatoa picha mbaya kuwa chama nyakuzi wa ardhi hakiwezi kupambana na wanyakuzi wa ardhi wakati mchezo wao ni mmoja.

Wengi wanaweza kuona kama tunaiandama CCM bure. Nchini Kenya, chama tawala cha zamani cha KANU kilipotupwa nje, majengo na vitegauchumi kilichokuwa kikimilki wakati wa serikali ya chama kimoja vilirejeshwa serikalini mojawapo ya mradi mkubwa ukiwa Nyayo House yenye ghorafa 27.

Kikwete aliongeza kusema badala ya CCM kuendeleza viwanja viongozi wamekuwa wakivipora na kujijengea majumba yao. Ajabu pamoja na kukiri hivyo, alisita kusema ni hatua gani zichukuliwe kupambana na wezi hao.

Hivyo, tokana na rais ambaye ni mwenyekiti wa chama kushindwa kukiambia chama chake kirejeshe mali za umma serikalini, unapaswa kuanzishwa mchakato wa kuifikisha CCM mahakamani ili iamriwe kurejesha viwanja vyote vya umma. Pia iamriwe kulipa fidia kwa muda ambao imevitumia kwa faida binafsi huku viongozi wake wakizidi kujineemesha kwa jinai hii. Kuna haja ya wapinzani na wanaharakati wa masuala ya ardhi na haki za binadamu kuingia kazini kuhakikisha CCM inarejesha mali za umma haraka sana iwezekanavyo.

Kwa namna ambavyo CCM imekuwa ikiendesha viwanja vya umma kwa faida binafisi, si tusi wala uzushi kusema kuwa CCM ni chama cha kikabaila ambacho hakina uchungu na wananchi kiasi cha kunyakua viwanja vyao na kutumiwa na viongozi waroho na wasioona mbali wala kujali maslahi ya wananchi.

Wakati Kikwete akifichua –sijui kwa bahati mbaya au maksudi –uoza huu wa CCM, katibu mkuu wa chama Abdulrahaman Kinana ambaye mara nyingi amejitia kuwa na huruma na watanzania, alikuwa akichekelea. Wengi tulitegemea –kama mapenzi ya Kinana kwa umma yangekuwa ya kweli –lau kumsikia akitangaza mkakati wa kurejesha viwanja vya umma serikalini. Badala yake alionekana akitikisa kichwa kukubaliana na pendekezo la Kikwete kuwa aunde tume ya kukagua mali za CCM kukiwemo viwanja ambavyo ni mali ya umma. Nadhani kwa kuangalia ukweli huu, tunagundua ni kwanini majengo yaliyojengwa kwenye viwanja vilivyakuliwa au kutoruhusiwa kama lile la Getrude Rwakatare au la uhindini hayaangushwi kwa vile lao wote ni moja.

Tumalizie kwa kuwataka watanzania wailazimishe CCM:

a) Kurejesha viwanja vya umma

b) Kutangaza wazi kuwa sera yake sasa ni ukabaila hasa unaotokana na unyakuzi wa ardhi na utumiaji ardhi nyakuliwa kulaza magari na kupata viwanja vya viongozi wake kujenga majumba binafsi. Huu ni ufisadi wa kiwango cha juu sana kiasi cha kukifanya CCM kuwa chama cha kifisadi.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 26, 2015.

Mlevi achonga na Joni Kanywaji Makufuli

Mpendwa Mheshimiwa Dk Joni Kanywaji Makufuli
Kwa mara ya kwanza anawasiliana naw kwa niaba ya walevi na wachovu wote kayani. Kwanza, nakupongeza kwa kutokatwa jina na kupitishwa kumrithi bwana mkubwa, rafiki yangu Njaa Kaya. Hongera sana mheshimiwa sana na aliyepakwa mafuta na wateule wakuu ili ufanye mambo makuu ila si makufuru.
Sitaki nizungushe japo nipeishaupiga mma na tubangi kidogo. Nachukua fursa hii–kama mzee na msomi mtukuka wa walevi–kukupa wosia kama utafanikiwa kuula.
Kitu ya kwanza nataka ushughulikie vibaka na majambazi ya EPA, Escrow na Richmonduli hata kabla hujakaa kwenye kiti. Maana kitu waliyotufanyia ni mbaya sana kustahiki nao kufanyiwa kitu mbaya zaidi. Walevi wanataka kuona mijambazi kama Jimmy Rugemalayer na Singasinga wakipigwa mawe hadi kufa au kuchomwa moto kama siyo kupelekwa kwa ISIS iwachinje kigaidi ili wanaodhani kaya yetu ni shamba la bibi wakome na kukomaa. Inapendeza? Au siyo?
Pili, walevi wamenituma wakikutaka –si kukuomba –usiteue vihiyo, mafisadi, vibaka na mipaka kwenye baraza lako la mawaziri. Vihiyo –hasa wale walioghushi, japo walikingiwa kifua–wanajulikana. Hata wale waliopewa ubalozi, ukuu wa wilaya na mkoa, ujaji na makandokando mengine watimliwe haraka ili kujenga heshima kwa lisirikali lako tukutu chini ya Chama cha Mizengwe (CcM).
Tatu, walevi wanakutaka ufumue mikataba yote ya uchukuaji unaoitwa uwekezaji. Waliokutangulia walituingiza mkenge na kutufanyia usanii. Si waliahidi wangefumua na kusuka upya mikataba hii wakaishia kuingia mingine ya kishenzi na kijambazi ikiwamo Richmonduli. Hatutaki urudie makosa haya ya kichovu na kipumbavu.
Nne, usiwasahau walevi. Maana bila kukupata wewe huwa hawalali. Sisi ni watu wako –yaani watu wa kanywaji kama jina lako. Hivyo, lazima tukukumbukane hasa ikizingitiwa kuwa kama utawaahidi kanywaji na bangi zaidi watakupa kura za kula kama hawana akili nzuri. Hivyo tukiwa na rahis kanywaji na kanywaji na tubangi kama kawaida nadhani furaha itarejea
Tano, ukiachia mbali kuwakumbuka walevi, hakikisha kwenye ulaji wako hakuna kujuana wala kufadhiliana. Ulipita bila mfadhili. Hivyo, uhitaji kulipa fadhili wala kupendelea.
Sita, tunataka kukuletea ufagio wa chelewa ili uifagie na kuisafisha kaya inayonuka vibaya sana. Tutataka uanzie ikulu ukiwatimua wale wote walioajiriwa kulipwa fadhila kama wale makanjanja wanaojifanya vipaza sauti vya ikulu waliowachafua wenzao kwenye mchakato wa 2005. Siku nyingine tutakupa majina yao. Hata hivyo, unawajua vizuri akina Rweyependekezamo. Hata wale waliopewa ukuu wa wilaya timua kama huna akili nzuri. Mchonga alionya kuwa ikulu hakuna biashara na ni patakatifu pa patakatifu. Kwa vile paligeuzwa patakakitu pa patakitu au pachafu pa pachafu, tunakutaka usafishe kila kitu pale.
Saba, epuka uzururaji wa kupenda kwenda kutanua Ulaya na Amerika. Walevi wanasema kuwa wanachukia jina la Vasco da Gama sana. Hivyo, wanategemea utakaa ofisini na kutatua matatizo yao badala ya kuzurura kwa kisingizo cha kuombaomba. Usikubali kuwa Vasco da Gama Matonya.
Nane, walevi wamenituma nikupe laivu kuwa usimruhusu Bi mkubwa wako aanzishe kampuni almaaruf NGO. Kwa walevi hizi NGO ni vichaka vya wizi wa fedha za umma na matumizi mabaya ya ikulu. Hivyo, ogopa NGO kama ukoma au ukimwi. Kwani mwisho wa siku hukuacha mchafu, asiyeheshimika wala kuaminika. Guess what. Mzee Mchonga wa Musa hakumruhusu Maria wake kuwa na kampuni hii aina ya NGO na bado bi mkubwa huyu anaheshimika kuliko wote waliomfuatia.  Walevi wanataka bi mkubwa wake awe wa pili baada ya Maria Mchonga. Nadhani unajua ninachomaanisha. Pia usiruhusu mashoga zake wapewe vyeo tena wasivyoweza.
Tisa, usiruhusu kitegemezi chako au ndugu yako kuchukua nafasi yako Chato. Cheo si urithi binafsi. Maana, tulizoea kuona uongozi ukigeuzwa private estate. Hii–kwa mtu aliyepiga shule kama wewe –inaweza kukuonyesha ima kama mtu aliyeghushi au ambaye alisoma lakini hakuelimika.  Nakuaminia bro. tunataka ujenga kaya kama barabara.
Sipigi chuku wala kujigonga ili unikumbuke japo si vibaya ukinikumbuka. Kuna mlevi mmoja aliyekuzimia hadi akasema sasa anaona Mchonga na Muringe wakifufuka kupitia kwao kama hutatupiga chini au kutuangusha.
Kumi, walevi wanasema usianze kupiga kampeni kabla ya kipenga kupulizwa. Hata huu upuuzi wa kujitambulisha achana nao. Nani asiyekujua hapa kayani bro? Hivyo, epuka njama za wabaya wako kukuchafua kwa kukushauri upuuzi. Pia usikubali kutumia raslimali za umma kufanyia kampeni. Walevi wanasema kuwa kama hutakuwa na means ongea nao wakupe tafu kuliko kuaibishwa na matumizi mabaya ya raslimali za umma. Pia wanakuonya kuwachunga sana magabacholi wanaopenda kujifanya wanakupenda ili wakutumie na kukuchafulia sifa yako nzuri. Si wema hao. Sana sana uwabane walipe kodi na kuzuia kuchukua nafasi za wamachinga wetu.
Kumi na moja, walevi wanasema wazi kuwa lazima uanzishe upya mchakato wa katiba ili wapate katiba isiyo ya kifisadi na kijambazi. Wanaamini kuwa nawe hukupendezwa na uhuni uliofanywa hadi katiba ya walevi ikauawa huku njuluku zao zikiliwa na muda wao kupotezwa. Tena kabla sijasahau, wale wahuni waliopewa ukuu wa wilaya kwa kumnyanyasa mzee Sinde ambaye ameonyesha kukubali sana lazima uwapige chini. Lazima ofisi zetu za wilaya na mikoa ziheshimike badala ya kuwa chaka la kujaza wahuni na wababaishaji kwa vile wanajuana au kula na wakubwa. Najua sasa wengine matumbo joto kweli kweli hasa wakijua kuwa wewe si mhuni wala mbabaishaji.
Mwisho, soma sana sera za mzee Mchonga unaweza kumaliza muda wako ukiwa baba wa pili wa kaya baada ya wenzio watatu kutoka kapa tokana na upogo, tamaa na uvivu wa kufikiri.
Kwa vile nasikia kanywaji na tubangi vinazidi kupanda upstairs, acha niachie hapa nikingoja kupokea email yako ya majibu ili niwarejeshee walevi waheshimiwa walionituma kwako.
Ubarikiwe sana bro.
Kanywaji hoyeee! Makufuli hoyeee!
Nahene ngosha.
Chanzo: Nipashe Julai 25, 2015.

Friday 24 July 2015

Raisa wa Tanzania anapotembelea Malaysia



Utawala wa rais Jakaya Kikwete utaingia kwenye vitabu vya historia kama utawala wa hovyo uliowahi kuwapo nchini. Kwa kisingizio cha kuaga ughaibuni Kikwete amekuwa akipoteza mamilioni ya shilingi eti kwenda kuaga nje utadhani ndiyo waliomchagua. Anaondoka kesho kuelekea Australia kuaga baada ya kurejea juzi toka Uswizi alikokwenda kuaga. Kama haitoshi na mkewe yupo Malaysia sijui naye anakwenda kuaga au ndiyo hiyo tabia ya kuzurura waliyojizoesha.

Ngoja watoke madarakani tuone kama watazurura kama walivyozoea. Kuna haja ya kubadili katiba kuzuia upuuzi huu wa kuzurura na kuacha kazi zikilala nyumbani. Kwa miaka kumi Kikwete ametuibia tu ukiachia mbali kulea na kushiriki ufisadi.

Thursday 23 July 2015

UKAWA hawana sababu kumuogopa Magufuli

Image result for photos of magufuli and ukawaImage result for photos of magufuli and ukawa
       Hakuna ubishi kuwa mgombea mteule wa urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli ana ushawishi mkubwa nchini. Hata hivyo, hii si sababu ya wapinzani chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kumgwaya.
Baada ya kuteuliwa Magufuli, wengi walisikika wakisema sasa kiatu kimepata mvaaji. Ni kweli, lakini hata UKAWA wanao wavaaji wa kiatu sawa na Magufuli. Katika kuthibitisha hilo Dk Makaidi ambaye pia ni Mwenyekiti wa NLD kinachounda UKAWA alikaririwa akisema, “Hatustushwi na (Dk John) Magufuli kwa lolote na mashambulizi yetu yatakuwa makubwa. Lengo letu la kuiondoa CCM madarakani liko palepale.” Maneno ya Makaidi yana ukweli. Wale wanaodhani wapinzani wanamgwaya Magufuli wanataka apitishwe bila kushiriki uchaguzi?
Nadhani Makaidi ana sababu nzuri tu za kusema hawatishwi na Maguguli. Anasema, “Ajenda na hoja tulizonazo ndizo zitakazotubeba mbele ya wananchi… tutawapelekea ili waamue wakiwa na taarifa sahihi. Kama ni kutowajibika au ufisadi ndani ya CCM, suala hilo linaanzia ngazi ya juu mpaka kwa mwanachama wa kawaida.” UKAWA bado wana imani kuwa wananchi watawaelewa hasa pale watakapowakumbusha utendaji mbovu wa CCM.
Pia ni vizuri tukaamini kuwa kwenye siasa lolote linaweza kutokea. Nani aliamini kuwa rais Uhuru Kenyatta wa Kenya angemshinda waziri mkuu wa zamani Laila Odinga ambaye hata rais wa zamani Mwai Kibaki alimgwaya kama umeme? Japo siasa za Tanzania na za Kenya ni tofauti, bado ni mapema kwa yeyote kusema atashinda. Hatujui wananchi hasa wapiga kura wanafikiri nini na wataamua vipi. Hivyo, ushauri wa maana hapa ni kwa wagombea wote kutobweteka na umaarufu walio nao bali kwenda kwa wananchi na kueleza sera zao ili wapate nafasi nzuri ya kuamua.
Japo Magufuli anajulikana kwa utendaji wake, vile vile chama chake kinajulikana kwa utendaji mbovu. Hii dichotomy, au ndiyo siyo ni vizuri ikazingatiwa katika kuelekea uchaguzi ujao. Sidhani kama wananchi ambao bado hawana barabara maji wala umeme wana wanachoona ni bora kwa Magufuli. Sidhani kama wananchi ambao ardhi yao imetwaliwa ima na wawekezaji au viongozi wa CCM wanacho cha mno wanachokiona CCM. Sidhani wajawazito wanaotimliwa na manesi kiasi cha kuzalia vyooni wanacho cha mno katika CCM.
Kimsingi, hali ya CCM bado ni ngumu sema unafuu ilio nao ni kuwa na mgombea ambaye hana tuhuma za ufisadi ua uzembe. Kwa umaarufu, uchapakazi na uzalendo alio nao Magufuli anaweza kushinda.  Lakini CCM itegemee kuwa na hali ngumu kwenye ubunge. Maana wabunge wengi wanaomaliza muda walichakachua kiasi cha wengine kuchukiwa vibaya sana kwenye majimbo yao. Sijui wabunge kama hawa watarudi. Sidhani –kwenye uchaguzi ujao –kama wananchi wataruhusu uchakachuaji kama ule tulioushuhudia mwaka 2010. Nadhani wananchi sasa wamechoka na wako tayari kusimamia haki zao kuliko wakati wowote katika historia ya taifa letu. Hivyo, CCM wanapaswa kulizingatia hili huku na wapinzani wakizidi kuhanikiza kufichua maovu ya CCM kama taasisi badala ya kuhangaika na mtu mmoja.
Nadhani Makaidi anaposema tutabebwa na hoja anatoa onyo kwa CCM kuwa wasibwete na Magufuli. Wanajua fika kuwa mtu hawezi kuzidi chama. Wana mifano hai ya watu waliongia wakiitwa Mr Clean wakaondoka wanaitwa Mr Dirt.
Kitu kingine wanachopaswa kuzingatia wananchi si ukubwa jina la mtu wala umaarufu wake bali sera anazokwenda nazo kwao na utekelezaji wake.
CCM pamoja na Magufuli wanapaswa kujifunza toka kwenye mchakato wao ulioisha na kumuibua Magufuli. Nani alijua kuwa Magufuli angewapiku vigogo waliokuwa wanajiamini kuwa ndiyo watakao kuwa wao kwenye kupeperusha bendera ya CCM? Nani alitarajia vigogo kama Edward Lowassa, Bernard Membe na Mark Mwandosya kuangukia pua na kushindwa na rookie kama Magufuli? Huo ndiyo uchaguzi. Si vyema kuwasemea wapiga kura au kujaribu kutabiri watafanya nini. Kinachopaswa kufanya kwa pande zote ni kuheshimu kanuni na kupeleka sera kwa wanachi huku wale walioko madarakani wakitakiwa kutoa maelezo yanayoingia kichwani pale walipoboronga.
Kama watanzania watajifunza tokana na makosa yao, tunaweza hata kutegemea maajabu. Jakaya Kikwete aliingia na sifa nyingi za kweli na za uongo. Je anaondoka na hizo sifa tena? Unategemea nini kama wapinzani watatumia udhaifu wa Kikwete wakiupambanisha na ahadi na sifa alizoingia nazo kumbomoa Magufuli? Kwangu mimi ngoma hii bado ni mbichi na lolote linaweza kutokea kufikia Oktoba.
Mfano mzuri ni ile hali ya Magufuli kuanza kuona hatari inayokabili chama chake hasa kuhusiana na ufisadi. Ameanza kuto ahadi za kutomugopa yeyote wala kumuonea. Je hii inatosha? Atakapokwenda kwa wananchi watamuuliza nini atakachofanya kuhusiana na mazimwi kama EPA, Richmond na Escrow. Majibu atakayotoa na usayansi wake vinaweza kuwa vigezo amuzi kuliko mtaji alio nao wa kuwa mchapakazi bora na kusifika kusimamia ujenzi wa barabara. Je hizo barabara zinakidhi viwango au kulingana na kiasi cha fedha kilichotumika kuzijenga? Maswali mbona yapo mengi kuanzia ya barabara hadi nyumba za umma zilizouzwa chini ya usimamizi wake.
Tumalizie kwa kuzishauri pande zote kujikita kwenye masuala badala ya personalities.
Chanzo: Dira Julai 23, 2015.