Fish

Total Pageviews

Wednesday, 14 March 2012

Kikwete: Globetrotting Interrogated


President Jakaya Kikwete: Bye Bye!?


The editorial of one Swahili Daily, Tanzania Daima of February 22 carried a title: “Msafara wa Rais Nje Upunguzwe,” or literally, the Presidential entourage abroad should be cut down. This has been a thorny issue for Tanzanians especially when it comes to extravagance by their globetrotting ruler, Jakaya Kikwete.
Since he came to power six years ago, Kikwete has made over 300 tours abroad, an average of 50 trips annually or one trip in every two weeks. He is second to none in Africa when it comes to touring foreign countries ahead of presidents Yoweri Museveni (Uganda) and Jacob Zuma (South Africa). Analysts wonder why he conceals the names of his delegates, for during his foreign tour, only his wife is mentioned alongside him. It seems the list of delegates on his trip to Britain leaked.


Kikwete surprised the country when he left for Davos to attend the World Economic Forum (WEF) while back at home, Tanzanian doctors were on strike demanding good payment. Many patients lost their lives as the government maintained that it did not have money to give to doctors. To Kikwete, the doctors’ strike could not stand in his way. Fortunately for him, Tanzanians are ‘peaceful’ as politicians in the country like to refer to them.


If Kikwete does not have any fiscal discipline, what about those under his watch? Since he came to power, Kikwete has been accompanied by friends and controversial businessmen who have allegedly committed grand corruption in the country. Tanzanians want their president to be tamed and be held accountable for the hard-earned taxpayer money.


Despite all noises, Kikwete has kept mum and is doing more of his globetrotting. Tanzanians have consequently nicknamed him ‘Vasco da Gama,’ or ‘Tourist President.’ As of 9/9/2011 when Kikwete toured Kenya, he had already made 316 tours abroad since coming to power in 2005! Even Ian Khama of Botswana with its stable economy has not done this. Kikwete is traveling more often than presidents and PMs of donor countries such as the US, Canada and Britain! For example, as of November 19, 2011 President Barack Obama had made just 24 foreign tours since he came to power. This translates into eight tours annually.


Kikwete is doing exactly what Uganda’s President, Yoweri Museveni has been doing for decades. According to the Observer of February 22, 2012, UShs 3.810 billion was approved for State House travels in the financial year 2010/11 even though figures indicated that Museveni used UShs 7.423 billion to visit 13 countries, host 11 heads of state and foreign dignitaries, and to attend 12 regional and international meetings. That means the Shs 5.055 billion Museveni wants this financial year might actually shoot up.


Tanzanians are agitating that Kikwete’s trips abroad be probed after he left for Britain accompanied by 40 people. How can a country whose budget depends on donors by 40% be extravagant at a time when many strong economies are grappling? When will he sit in office and serve the people?
Source: The African Executive Magazine March 14, 2012.

Nilichojifunza kutoka mgomo wa madaktari, makala iliyoichefua ikulu na kutishia gazeti

INGAWA mgomo wa madaktari wa nchi nzima ni tukio lililosababisha vifo ambavyo si kazi ya Mungu bali serikali, kuna somo umetoa.
Sijui kama watu wengi hasa waathirika wameliangalia kama mimi. Wenye akili wanasema kila tukio limtokealo binadamu mwenye akili ni darasa tosha. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwangu binafsi kama mwana taaluma na mkereketwa, ukiachia mbali kuwa mwanaharakati wa haki za binadamu.
Hata kama siishi Tanzania, bado nayajua masahibu na mazingira ya watu wetu. Hivyo siandiki kutokana na hasira ya kuathiriwa na mgomo wa madaktari kwa vile nilipo sina upungufu wala shida ya huduma ya madaktari, ikichukuliwa kuwa afya ni haki ya msingi ya kila mwananchi (hapa si Tanzania).
Siandiki kujisifu bali kuchochea hasira na welewa wa ndugu zangu Watanzania. Sitaki nieleze hali ya afya hapa Canada ikoje kwa vile kila mtu anajua kuwa kuna mfumo mzuri kuliko hata jirani zetu kusini, yaani Marekani. Ukimwambia Mcanada kuwa afya si haki ya binadamu anaweza kukushauri ukapimwe akili. Hayo tuyaache.
Katika mgomo uliokwisha ambao umezaa mwingine nimejifunza yafuatayo:
Kwanza, rais wetu haambiliki wala hasikii na sijui hii inasababishwa na uwezo wake wa kuelewa au anavyojiona baada ya kuwa rais.
Maana ukiangalia yule Kikwete tuliyeambiwa ni kipenzi cha watu na chaguo la Mungu unashangaa inakuwaje kipenzi cha watu na chaguo la Mungu anakuwa mkatili ambaye hajali hata taarifa kuwa kuna watu wamepoteza maisha kutokana na mgomo.
Unashangaa alipopata mshipa wa hata kuweza kwenda kwenye mkutano usio na umuhimu wala ulazima huku watu anaowaita wake wakifa kutokana na uzembe wa kawaida wa wateule wake! Kama hutajizuia kuhukumu ili usije ukahukumiwa, unaweza kumuita hata majina mengine ambayo si sahihi.
Sitaki nifikie hapo. Unashangaa ni baba au mama gani anaweza kwenda kwenye biashara wakati wale anaowaita watoto wake wakiugua na kufa kutokana na sababu anazoweza kuzuia hata kuingilia, achia mbali kuzuia.
Hivi waliopoteza maisha wangekuwa watoto wa Kikwete hata wapendwa wake kama vile Haji Mponda na Lucy Nkya, angeweza kupata hamasa kwenda Davos huku akiacha wakiteketea kwa kitu kinachohitaji si pesa wala nini, bali tamko lake? Je, huu ni ubinafsi na upogo kiasi gani?
Hakuna haja ya kupindisha maneno, rais wetu, sijui wao, hajali. Maana angekuwa rais wetu angetujali badala ya kujali kujilisha pepo kwenye vikao visivyo na ulazima ikilinganishwa na wapendwa wetu waliopoteza maisha, ukiachia mbali wale wanaouawa na polisi wake.
Siachi kujiuliza si mara moja wala mbili. Hivi hawa waliopoteza maisha wangekuwa watoto wake au hata mkewe angefanya alivyofanya? Lakini atajalije wakati yeye na familia yake wanatibiwa nje kwa pesa ya walalahoi wanaouawa na serikali kwa kuwadharau na kuwanyonya wananchi?
Nasema hivi kutokana na yaliyotokea. kwa wale waliopoteza ndugu zao serikali kwao haina maana na ni mnyonyaji wa kawaida.
Maana walipoichagua walijua itaingilia kwenye hali kama hizi. Kutofanya hivyo kunaifanya kupoteza uhalali mbele ya macho yao hata kama wanaogopa kuifurusha kutokana na woga ujinga na hata kuishi kwa matumaini.
Kitu kingine nilichojifunza ni kwamba Watanzania ni watu wa ajabu ambao hawana tofauti na kondoo kwa kushindwa kuwaunga mkono madaktari. Usishangae ukakuta wanawalaumu madaktari bila kuangalia upande wa pili ambao unatibiwa nje.
Hebu jiulize. Rais anaandamana na watu 40 kwenye ziara ya kutanua huku akiacha umma unateketea. Anapata wapi hiyo pesa ya kufanya hivyo kama si kutojali? Cha msingi cha kuzingatia ni kwamba ni hao hao wadharauliwa na wapuuziwa wanaokatwa pesa itokanayo na kazi na jasho lao kumlipia rais na wapendwa wake kwenda kutanua wakati punda hao hao wanaomwezesha wakipukutika kama wadudu yeye asihangaike hata kutumia akili ya kawaida achia mbali elimu.
Kitu kingine nilichojifunza japo kinatia aibu ni kwamba wateule wa rais si wa kuguswa hata wakifanya madudu kiasi gani. Rejea Mponda na Nkya na wanaodaiwa kughushi vyeti vya taaluma. Yuko wapi bwana EPA bin Kagoda? Si anaendelea kutumia mahakama zetu na za kimataifa kuvuna pesa yetu huku tukijua mchezo wote na tusichukue hatua?
Rais yuko tayari kuwatoa kafara wananchi ili kuwalinda wateule wake ambao kwake ni kila kitu na si wapiga kura.
Hata hivyo ana shida gani na wapiga kura wakati hana mpango wala haki ya kugombea tena? Je, huu si utapeli wa kimfumo ukiachia mbali kuwa unyama wa ajabu ambao hata simba na fisi hawawezi kuufanya?
Kitu kingine ni kwamba Tanzania ina ombwe kubwa la uongozi kuliko ambavyo imewahi kutokea. Kiongozi wetu huyu ni ajali ya kihistoria kutokana na ukosefu wa upendo na heshima kwa wananchi, amembebesha zigo waziri mkuu kiasi cha kuonekana mbaya wakati mbaya si yeye .
Kimsingi, kinacholisumbua taifa ni ibada za sanamu, ambapo rais anaombwa badala ya kuamrishwa kama mtumishi yeyote wa umma. Nashindwa kuendelea.
Chanzo:Tanzania Daima Machi 14, 2012.

Wanawake wa Nairoberry ni kiboko ya wanaume


Simon Kiguta akiwa kwenye Hospitali ya Nyeri Feb. 11, 2012. Alikatwakatwa mapanga usoni na mkewe baada ya kurejea nyumbani  usiku akiwa amelewa. (Joseph Kanyi/Nation photo)
Baada ya kutoka zangu London juzi nilipitia Nairobi kuongea mawili matatu na wanakijiwe cha River Road na Ngala. Sikukwa na mpango wa kusimama kidogo Nairobi. Ila nikiwa zangu London Mureithi ambaye ni mwenyekiti wa Kijiwe kile alinitwangia simu akiomba nipitie Nairobi lau nitoe ushauri.
Nilifaidi sana uzuri wa mji wa London. Barabara zote zina lami, taa, zinapigwa deki usiambiwe. Nilipofika Heathrow airport, sorry, International Airport nilitaka kuzimia nilipolinganisha na jiji letu la uchafu na ufisadi liitwalo Chafusalama.
Sikuona mgambo wa site mamantilie wala wazee wa mabao kwenye barabara za London. Kitu kimoja kilinistua sana-London kaya inachomwa hadharani na hakuna anayejali! Nilipomuuliza mvuta kaya mmoja akacheka na kusema kuwa kaya haina tatizo kwa taifa bali kwa mtu binafsi. Hivyo, nami niligundua kuwa kumbe hapa kwetu heri turuhusu watu wajichomee kaya kuliko kuruhusu ufisadi. Maana ufisadi unaumiza wengi. hata uchafu wa miji yetu ni hatari kwa kila ajae na aishie kwenye miji yetu. Ni ushahidi wa uchafu wetu wa kitabia.
Najua nikirejea kijiweni kwangu wengi nitakaowasilimulia usafiw a London watanisuta na kuhoji kama naona hivvyo kwa wenzangu nashindwa nini kutekeleza kwangu? Najua wengi wataniona kama juha na mtalii asiyejifunza. Hata hivyo tuache utani. Tuna tatizo tena si dogo. Yaani tunashindwa kujifunza hata mambo ya msingi kama usafi, mipangilio ya miji na mambo madogo kama haya? Au nayo tunataka waje wafadhili watusaidie kama walivyofanya kutuchimbia vyoo tukaishia kuvichafua?
Tukirejea kwenye kijiwe cha River Road Nairoberry ni kwamba siku hizi kule umeibuka mchezo wa akina mama kuwashikisha adabu waume zao. Ukichelewa kurudi unapatiwa. Wajua kupatiwa maana yake nini? Kuadhibiwa. Ukishindwa kufanya shughuli za ndani hasa za night unapatiwa. Ukitoroka kwa nyumba kwenda kula kwa hoteli, ukirudi unapatiana adhabu kama kawaida. Ukinywa sana kanywaji na kushinda kumudu idara zote, unapatiana adabu.
Huwezi kuamini kuwa juzi nilikuwa kwenye mahakama ya Kilimani kushuhudia mama mmoja akikabiliwa na kosa la kumpiga mumewe hadi akazimia. Toka na vipigo vya hapa na pale vya mara kwa mara, walume wa nchi ya Nyayo wameamua kuanzisha chama cha kulinda haki za walume. Kunogesha stori ni kwamba kipindi nilichokuwa kule, walume wote walikuwa wamekubaliana kugoma kula chakula nyumbani ili akina mama wapunguze morali wa Kikyuki.
Hakuna kitu kiliniua kama maongezi haya kijiweni. Mara anakuja Wagacohi na kuamkua, “Kohani atya?”
Njoroge na Wamauseto wanaitikia, “Kutiri na kaolu.”
Wagacohi anaendelea, “Mnajuanga kuwa Ithe wa Kinywa amepigwa na bibi yake hadi akepelekwa hosi?” Hosi maana yake ni hospitali.
Anaendelea, “Nyina wa Kamuyu ameniambia kuwa alipokwenda kunywa akaselewa kurudi akapatiana adhabu kali sana.”
Gathuma anadandia, “Haki mimi bibi yangu akipatiana adhabu na mimi nitaua yeye.” kabla ya kuendelea, Gitau anachomekea, “Kama umeoanga Central hasa Nyeri jua unapigwanga tu. Vinginevyo uwe umeoa kibeti cha Kikamba.” Wamuseto hana mbavu. anasema, “Haki, kwetu Matuu, Mbooni na Woote bibi hapingangi bwana. Sisi wakamba bibi akipinga bwana atalaaniwa aote devu. Kibeti ya Kikamba siyo Kama hii ya Kikuyu.” Anakunywa kahawa yake na kutafuna mirungi kidogo na kuendelea, “Wajua siku moja mimi naona bibi kule Ithekahuno akitwanga bwana hadi bwana anakufa kwa muda?”
Anamalizia, “Ukiona bibi anatwanga wewe understad wewe ni nugu-nyani.”
Mzee Gate anachomekea, “Wacha mabo yako wewe. Bibi akiamua twanga wewe anatwanga tu. Hukuona Luse alivyopiga watu ya habari pale Nation na hakuna ameshitaki yeye? Hata Kebaki mwenyewe hasemangi Luse akileta matata.”
“Kama munene kama Kebaki anapindwa nani wewe ulete nyoko nyoko kwa bibi ya kisasa asitwange wewe?” Mara mzee Gate ananigeukia. “Kama unataka bibi asipige wewe nenda kanunue bibi TZ. Huko nasikianga wanasema tafadhali wacha kuselewa na kurudi usiku badala ya kupatiana adhabu.”
Wamuseto anamuunga mkono mzee Gate, “Nasikianga watz ni wapoa sana. Tena ni wabeautiful.”Mie sina mbavu.
Tukiwa tunaendelea kupata kahawa na kutafuna miraa si alikurupuka rafiki yangu Ndirangu. Anakuja akipiga kelele, “Woi woooi, nakwa nie yaani nakufa mie.” punde si punde mkewe Wanjiku anatokea akiwa ameshika gongo akitaka ammalizie Ndirangu.
wanjiku anahanikiza, “Rehe besha zakwa ngiri igiri na ihenya, yaani leta pesa yangu elfu mbili haraka.” msishangae kusikia elfu inaitwa ngiri. Anaendelea, “Ithe wa Katuru, nuuga rehe besha zakwa naihenya.”
Ndirangu kuona walume wenzie tupo akajitutumua na kusema, “Dhie wega naiwe. Mutumia mworu uyu-yaani nenda salama, mwanamke mbaya huyu.”
“Ati, kama unatusi mimi kwa vile iko mbele ya watu, ukija kwa nyumba napatiana adhabu kali saidi ya Hii. Hii mabo ya kuleta mudomo kwa bibi hapa jua italeta taabu mingi kwa wewe.” Alijibu Wanjiku kwa ukali huku akigeuza kurudi zake nyumbani tayari kumngojea mumewe ili akija ampatie discipline.
Akiwa anaondoka alisema, “Kwa vile hutaki kuleta besha yangu, ile nyama ya roho na mukimo amepika hukulangi leo (anamaanisha nayana ya moyo na ugali). Kama unaweza shukua ngwashee uchomege ukule hapo kwa kahawa.” (Ngwashee ni viazi).
Muiruri anamgeukia Ndirangu na kusema, “Jamba, mabo ya nyuba uwe unamaliza kwa nyuba siyo kuja hapa na kuleta matata.” Anatafuna miraa na kuendelea, “Wewe hapana kamata bibi sawa sawa hadi napata mudomo kukuja hapa na kuropoka bere ya wanaume.”
Izo kumba za moyo sizikwa
Nakoma mabvuto akulobeta mama ine moyo
Moyo wanga ni mabvuto ine moyo
Sunga wa busee
Ndinu oletwa ambuye
Oletwa ndinu
Usanga zose ndinu
Moyo moyooo
Naona bi mkubwa kaja acha nitimke kabla hajanitia discipline.
Chanzo: Tanzania Daima Machi 14, 2012.

Sunday, 11 March 2012

Nilivyoshehekea Siku yangu ya kuzaliwa




Ingawa sikufanya sherehe kubwa zaidi ya kukusanyika na familia yangu, Siku ya kuzaliwa kwangu ilifana si haba.  Ilifanyika wapi?  Altona MB, Kanada.

Thursday, 8 March 2012

Sisi ndiyo winter inaanza




Kwa tunaotokea Ikwete winter ya mwaka huu ilikuwa ni neema. Hatukuwa na theluji wala baridi ya kukata na shoka kama tulivyozoea. Wakati wenzetu wanangojea kufunga kipindi cha winter sisi ndiyo tumekianza. Je hii itaendelea au kuishia hapa. Who knows.

Tuesday, 6 March 2012

Wade: Will He Make It?


Adoulaye Wade and Macky Sall Photo courtesy

Some people are lucky; others are not. Senegalese strong man, Abdulaye Wade is among the luckiest old men even though he behaves like an adolescent. Had it been not for divided and ever-greedy opposition, Wade would have been history now. Voters gave him a very heavy blow in the first round. He secured a leading of 34,8% ahead of his former protégé and PM, Macky Sall who garnered 26.5%. Other former PMs took third and fourth place: Moustapha Niasse with 13.2% and Idrissa Seck with 7.8%.

Such low votes speak volume and signify defeat. This translates into the fact that had the opposition backed one candidate, the results would have been Sall 47% and Wade 34.8%. Again, there wouldn't have been there any run-off that Wade can use to rig votes to fulfil his power-hunger to remain in power.

In other words, Senegalese were able to get rid of Wade in the first round had it not been for the opposition to help him secure a second chance of survival. Will Wade let it go easily without applying traditional African science of survival-rigging and cheating? Shall this happen, will the people and their weak opposition bite the bullet or give him a hard time once again?

One thing though is obvious that that Wade showed maturity for not rigging in the first round. Is it because of being cornered, his belief in democracy or the result of over confidence that he'd have won in the first round? If he allowed justice to take its course, will he keep this ma
turity or cascade back to his dreams of dying in power?

Although Abdulaye Wade, managed to tamper with the constitution to be able to run for a third time aimed at remaining in office, will he manage to manipulate the votes and get away with it. Results conclusively indicated he did not make it outrightly in the first round. This of course dented him badly. Sall gave him a spirited fight so as to change Wade’s tone from braggadacios to conciliatory one. Will this become Wade’s waterloo?

The ballot box can still boot Wade out if not to tame him. Senegalese should maintain the momentum they displayed in the first round whereby Wade lost outrightly. For those who remember his braggadacios that there won’t be any run-off, what happened is victory phase one. If voters fulfil their responsibility for the sake of their nation and democracy, Wade can still lose comfortably so as to be forced to lose in this-game-changer-like run-off.

Voters ought to deny Wade the votes he’s going to use to abuse them and their country. He’s been in power for twelve years. What can he do he did not do in these twelve years? Why should Senegalese voters prefer a centurion to a half ager Sall? If anything, Wade’s plight is squarely in the hands of voters who must punish him for ignoring them and abusing their office and constitution altogether.

Many people wonder where Wade got the guts and wits to tell former Libya strongman, Muamar Gaddafi and Ivorien one, Laurent Gbagbo to relinquish power last year while he cannot do the same now.

Due to the science of aging, we understand: Wade’s brain if wearing off. This contributes to the controversy he’s created apart from his greed to cling unto power. From what he does and says one can surely assert that this old man deserves to retire shall he deserve to be remembered honourably and favourably. Wade’s confusion can be noted in many things. He’s recently quoted saying,"I am president and father of the nation. This is what the Europeans do not understand," he told French weekly Sunday newspaper Le Journal du Dimanche. He added, “My majority is so overwhelming that I think I will be elected with a strong percentage in the first round,” Ask him where is hallucinatory majority went in the first round. He started changing the tone and tune altogether.

It is sad to note that Wade does not know that the father of Senegal is none other than Leopord Sedar Senghor. For Wade to equate himself with Senghor who became the first African leader to voluntarily retire when he was ten years younger than Wade connotes mischief to the nation and Africa in general. Senghor relinquished power in December 1980 retiring in favour of the Prime Minister, Abdou Diouf. After his retirement, Senghor did not involve himself in politics till his death on 20 December 2001.

As banned candidate, Youssou N'Dour put it, “The Senegalese are not stupid.” This will be justified by the votes they will cast in the favour of Sall. Shall Wade rig their votes; they still have the chance to prove that they are not stupid by seeing to it that he is not getting away with it.

Wade is an educated man by all standards. Again, as William Feather put it, “An education is not how much you have committed to memory or how much you know. It is being able to differentiate between what you do know and what you don’t know. It is finding out what you need to know and using the knowledge once you get it. I doubt if Wade knows where to go if he cannot willingly retire. I wonder if Wade knows where to go and get what he deserves-retirement instead of daydreaming going for a third time at such eleventh hour.

Wade, a cliffhanger, who promised crushing first round victory ended up saying this as the results were trickling in, "To all of my supporters, my allies, my sympathisers, I ask that you remain mobilised," Wade was quoted by BBC. He added "At this very hour... everything is still possible - victory or a run-off," Let Senegalese make it possible for Wade to pack and hit the road to oblivion.Will the opposition goof again to let Wade win?


Source: The African Executive Magazine March 6, 2012.

Mama Maria Nyerere anapofunda wasiofundika!

HIVI karibuni mke wa Baba wa Taifa, Maria Nyerere alikaririwa akitoa wosia ufuatao kwa wake wa viongozi. Alisema: “Unapokuwa mke wa kiongozi unapata changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kutoa dira kwa wengine...unapaswa kufikiri kwa niaba ya wengine, iwe ni kwenye ujasiriamali, elimu, afya au masuala ya kijamii hasa namna ya kukabili changamoto za kina mama na watoto.”

Haya maneno ni ya maana kwa wenye kutia akilini. Ni mazito yenye kueleza mengi katika uchache wake. Mama Maria anawataka wake wa viongozi wa sasa na hata waliopita watoe dira.

Hawa wana dira gani zaidi ya kuchuma na kujineemesha? Nani mara hii kasahau, mfano, fuko la Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) lililoishia kuwa mrija wa kutengenezea pesa kwa kisingizio cha kuwainua kina mama?

Nani amesahau Anna Mkapa alivyotokea kuwa milionea baada ya mumewe kuingia madarakani huku akitajwa karibu katika kashfa nyingi asijibu? Alishindwa hata kumshauri mumewe kutangaza mali wakati wa kuondoka.

Kwa kumbukumbu, zama za Mwalimu, jinsi Mama Maria ambavyo alifanya kazi kuu za kumtunza na kumshauri Baba wa Taifa, wanashangaa kuona wake za watawala waliofuatia kuwa marais nyuma ya pazia kwa kuanzisha NGOs zenye kutia kila aina ya shaka. Ukiacha mke wa Mzee Ali Hassan Mwinyi ambaye naye alishutumiwa kutumia ofisi ya mumewe kuwapatia mikopo ndugu zake, wake wa waliofuata wamekuwa kama wafanyabiashara wa kawaida ambao sijui kama wana dira hata mawazo ya kuwashauri waume zao.

Kama kuna ushauri mke wa Mkapa aliompa ni kujitwalia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira ulioishia kuwa aibu ya mwaka kwa ukoo mzima wa Mkapa.

Nani mara hii kasahau kashfa ya Net Group Solution ambayo ilisemekana kuletwa na waliokuwa karibu na ukoo wa bwana mkubwa hasa bi mkubwa?

Ukija kwa mke wa Rais Jakaya Kikwete, Salma, sijui akama anamshauri vizuri mumewe kuhusiana na anavyopasa kutawala zaidi ya kutumia muda mwingi kwenye NGO yake ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) ambayo sawa na EOTF inalalamikiwa sana. Sina ugomvi na NGO hii zaidi ya kuona umma unavyoiangalia kwa jicho baya kutokana na namna inavyoendeshwa.

Swali kuu ni kwanini kuwa na NGO baada ya mume kuingia madarakani? Je, NGO hizi zinaweka wazi taarifa zake za ukaguzi wa mahesabu kila mwaka?

Mama Maria alikuwa na uwezo hata udhu wa kuanzisha NGO na ikawa ya kuwahudumia wanawake hata watoto kweli kuliko hizi za sasa ambazo ni shaka tupu. Lakini hakufanya hivyo kutokana na kuepuka mgongano wa maslahi na kujenga mazingira ya waovu kuweza kuitumia kuchafua uongozi wa mumewe.

Nani hajui kuwa ukichunguza wafadhili wengi wa NGO za wake wa wakubwa si watu wenye nia njema? Hili liko wazi hasa kutokana na ukweli kuwa baada ya waume za wenye NGO kuondoka madarakani, NGO zao hudoda kiasi cha kutovutia tena wafadhili. Je, hapa kinachofadhiliwa ni NGO au zinatumiwa kuwa karibu na jungu kuu kama ilivyo sasa?

Huwa nashangaa kusikia kwa mfano mke wa rais anakwenda kutafuta misaada kwa ajili ya wanawake na watoto wakati huo akishindwa kumshauri, kwa mfano, mumewe kuwashughulikia mafisadi, kupunguza ukubwa wa serikali, safari za nje zisizo na ulazima zaidi ya kuumiza uchumi na mambo mengine kama hayo.

Je, huyu asiyeona haya anaweza kuwa na uchungu na hao anaodai kuwa nao uchungu au kuwatumia kwa faida binafsi? Je, kazi ya wizara ya kina mama na watoto ifanye kazi gani kama kila mke wa rais anayeingia anataka kuwatumikia kina mama na watoto?

Basi tufute wizara, maana wizara ya kina mama na watoto ya First Lady ipo na inapokea misaada.

Kama kwelli hawa wanaochangia wana uchungu na kina mama na watoto kwanini wasichangie hiyo wizara husika ambayo ina waziri, naibu waziri, katibu wa wizara, wataalamu na wafanyakazi lukuki kikatiba? Jamani hapa nani anamdanganya nani na nani anamtumia nani?

Ukiondoa Tanzania, sikumbuki kwa mfano kusikia eti mke wa rais mstaafu wa Kenya Daniel arap Moi au wa sasa Mwai Kibaki kuwa na NGO.

Pamoja na ufisadi wake wa kunuka aliokuwa akifanya, hata Mobutu Sese Seko hakuruhusu mkewe kuwa na NGO.

Turudi kwa Mama Maria na kuwafunda wasiofundika wala kufundwa. Je, aliwaambia aliyowaambia kutokana na kuona hawafanyi hayo au kupwaya? Aliwashauri watoe dira baada ya kugundua kuwa hawana dira?

Je, aliwaambia changamoto kutokana na kugundua kuwa changamoto mojawapo iliyowakabili na kuwashinda ni kujitajirisha kutumia mgongo wa ikulu?

Yote yanawezekana. Je, hawa aliokuwa akiwafunda walikuwa na lolote la maana la kumuonyesha mama gwiji huyu au kujikomba tu?

Anasema: “Unapaswa kufikiri kwa niaba ya wengine, iwe ni kwenye ujasiriamali, elimu, afya au masuala ya kijamii, hasa namna ya kukabili changamoto za kina mama na watoto.”

Je, hawa walengwa wetu wanafikiri kwa niaba ya wengine au familia zao tu? Je, wanakabiliana na changamoto zinazowakabili kina mama na watoto au kuwatumia kuwatupia moja katika kila kumi waisakayo kwa kuwatumia hawa wanyonge na madaraka ya waume zao?

Leo utasikia kwa mfano mke wa rais amejenga shule kwao au mwingine kupeleka miradi kwao au kwa mumewe.

Kwanini asiachane na ubangaizaji akamshauri mumewe akawa na sera safi zenye kuwezesha kujenga hizo shule popote badala ya kwao au kwa kuuweka urais majaribuni kama ilivyo? mie naona ni bora ya Mama Maria ambaye hakuacha nyuma hata shule moja wala utajiri binafsi kuliko kuacha shule mia zitokanazo na kufanyia biashara Ikulu na cheo cha rais.

Sikumbuki kusikia tuhuma zozote dhidi ya Mama Maria, mumewe wala watoto wao. Je, hawa wa sasa hali ikoje?

Kila kona ni tuhuma na bahati mbaya hazikanushwi zaidi ya kutoa vitisho visivyo weza hata kutekelezwa. Hivi tuhuma za mtoto wa Kikwete, kujinufaisha kwa kutumia mgongo wa baba yake ziliishia wapi?

Kimsingi, ingawa mawazo ya Mama Maria ni lulu, ima amewafunda wasiofundika au ameamua kuwapasha kwa hekima. Yote yanawezekana.


Chanzo: Tanzania Daima Machi 6, 2012.

Nakwenda kwa mama kutuliza hangovers

BAADA ya kupona kufa kutokana na migomo ya matabibu, Dk. Mpayukaji Nkwazi Nkuzi Mhango Msemahovyo, na marafiki zake kina Mgosi Machungi, Mzee Maneno, Mchunguliaji na wengine wapatao 50 wamepata ofa ya kwenda kwa Mama kutumia na kupunguza hangovers za kahawa na kinywaji.

Wakati tukipanda pipa na kujitoma zetu kwa mama, wanywa kahawa wengi walikuwa wakilalamika kuwa tumechukua njuluku za kijiwe kwenda kutanua.

Hakuna kilichowakera wanywa kahawa kama mimi kuwa naandamana na marafiki zangu na mke wangu karibu kila mahali. Hakuna kilichonikera kama kusikia upuuzi huu wakati pesa tunayotanulia si yao bali wafadhili wetu ambao leo sitawataja.

Kwanini nisiende kwa mama baada ya kumaliza mgomo wa wachemsha kahawa waliokuwa wakitaka kuongezewa marupurupu hasa kashata na maadazi kutokana na kazi yao ya kuhakikisha uhai wa wanywa kahawa haudhuriwi na uchafu hata polonium kama ile ya daktari Mwakiwembe?

Kabla ya kuendelea, wajua kuwa kijiweni kwetu umetokea mchezo mbaya wa kurogana na kulishana hata kupakana sumu? Juzi Msomi Mkatatamaa alikuwa akilalamika kuwa anahisi amegusishwa Polonium kiasi cha kuanza kuwashwa washwa sehemu za nonihino.

Kwa vile kumalizana imeanza kuwa fasheni kwenye kutafuta ulaji, wanywa kahawa wengi walitaka nitoe maelezo.

Nami kuona zali hili ni kubwa kuliko ubongo wangu wa P’eege nimeamua kwenda kwa mother kutuliza akili ili mambo yapoe kama alivyowahi kusema Willy Mkama kuwa Waingereza wakiona mambo yamepamba moto huunda Royal Commission kuwazuga wajinga kuwa wanachunguza ili mambo yapoe na yakipoa wanaendelea kuhomoa kama ilivyo kwa Bongolalaland ya Danganyika ambapo mafisi na mafisadi hushika kani huku walala njaa wakiendelea kutolewa njuluku na kusota.

Hebu turejee kwenye malalamiko ya wanywa kahawa. You know what. Hawa jamaa wanaungua ugonjwa uitwao Ammaglobulimenia yaani kuwa na mfumo uliovurugika mwilini.

Matokeo yake ni kuugua ugonjwa wa Bulimia unaoandamana na mwingine uitwao Megalomania. Watu wanaougua ugonjwa huu huwa wanajifanya hamnazo. Hata uwambie nini huwa hawashughuliki na kujibu wala kutoa maelezo. Kwa mfano, mgonjwa wa Bulimia ukimwambia kuwa anachofanya ni kibaya hufanya zaidi.

Huwezi kuamini eti wanasema nami naugua Bulimia kwa vile wakiniambia niache matanuzi mimi na marafiki zangu natanua zaidi. These guys are super stupid so to speak. How can a big guy with all ulaji under my control be that silly? Hooey! Samahani nimechonga umombo kwa sana kama maandalizi ya kwenda kuchonga na kwini.

Pia nachonga umombo kuwaonyesha wanaoshuku udaktari wangu wa kupewa kuwa nimebukua hata kama sikupata honours. Hayo tuyaache.

Wanywa kahawa kwa umbea sina hamu. Yaani mie kuandamana na maswahiba zangu 50 imekuwa stori. Je, wanataka niende na wangapi? Mwakani nitakwenda na 800 kama alivyokuwa akifanya shujaa wangu Mobutu Sese Seko Mwizi wa Zabanga kule DRC.

Hawa jamaa hawajui kuwa waliponichagua kuwa mkuu wao hawakujua kuwa sikugombea kuwaendeleza bali kujiendeleza mimi na nyumba yangu.

Hawajui kuwa nilipowaahidi maisha ya kuukata nilimaanisha yangu marafiki zangu na nyumba yangu? Kalagabaho na shauri yao! Imeandikwa kuwa mchungaji atakunywa maziwa ya kondoo awachungao. Kosa langu nini kula pesa ya nyinyi niwachungao? Pia imeandikwa kuwa ya Kaisari muachie Kaisari.

Kwanini wanywa kahawa hawataki kuniachia yangu kuwa yangu? Niliwahi kuuliza swali hili Msomi Mkatataama aakijibu kuwa wanachotaka si ya Kaisari maana kahawa si mali ya Kaisari yaani mimi bali wao. Jamaa mshenzi!

Ana maana kuwa hata walipa kodi wana haki ya kujua kodi yao inatumikaje kwa vile ni yao na si ya mkuu siyo? Wee koma. Sasa unaanza kugusa pabaya! Kama mkuu anawala waliwa wewe yakuhusu nini iwapo nawe unawala wanywa kahawa? Wajinga ndio wafanywao punda.

Sijui niwambie nini hadi waelewe. Huwa nakwenda nje mara kwa mara kubomu ili maisha yasonge mbele. Wengine husema eti nakwenda kufanya biashara na kukagua akaunti zangu huko. Well, hata kama ni hivyo, kwani nimewazuia wao kwenda? Sasa nasema wazi wazi.

Huwa napenda kwenda ughaibuni kutafuta wawekezaji wa kuja kuchukua sorry kuwekeza kwenye kijiwe. Bila mimi kwenda kule wawekezaji watagoma. Mbona watu wanasahau mapema! Bila ya yule jamaa yangu Ni Ziro Kamalagi kwenda kusaini mkataba wa Buzwagiii kule London tungekuwa na wawekezaji kweli? Au wanatumia akili mbovu ya Mzito Kabwela anayetaka kaya iache kuwalipa washikaji wa wakubwa waitwao AIPITIELO matrilioni eti wawekeze kwenye gesi.

Huyu kijana hana adabu. Anataka wazito wale polisi? Inaonyesha hata kwenye kijiwe kuna watu wa Mzito Kabwela. Maana nakumbuka alikuwa akipita kupata kikombe cha kahawa. Huenda aliacha magugu nyuma alipopita. Namshauri akatapeliwe kule Loliyondo kwa kupewa kikombe kichafu cha kutibu ujinga cha mchungaji Ashomile Mwatapeli.

Nasikia jamaa huyu kanogewa na kutangaza miujiza mingine ya kuwatapeli wajinga ndio waliwao waliojazana Bongolalaland ya Danganyika. Kwanini hawatumii vichwa wanatumia masaburi?

Nikifika London lazima nikajinome kwenye mitaa ya Trafagar, nitabembea na bi mkubwa pale Brent Park (Siyo Jomeika ambako iliniwia soo), Hounslow, Richmond, Kingston upon Thames, Buckingham, Gunnesbury, Isle of Dogs na kwingine. Wajua nimekulia London?

Ukiachia upuuzi wa malalamiko ya wanywa kahawa, hawajui kuwa mie huwa sipendi kukaa sana kijiweni. Huwa naboreka kukaa kijiweni nikisikiliza malalamiko mbali mbali ya wanywa kahawa.

Ili kuepuka kuusonesha moyo wangu kwa kuletewa habari mbaya kila siku, huwa napenda kwenda nje kutumia. Hivi utajisikiaje iwapo kila siku utaletewa mashitaka yanayowahusu watu wako hasa mke, watoto na marafiki kuwa wanatumia ukuu wako kujineemesha kwa kukiibia kijiwe? Wanataka nikae kijiweni waje siku moja wanilazimishe kuamrisha watu wangu waaibishwe na mgambo wa city kwa kutumia ulaji wangu kujineemesha?

Hata hivyo kuna kosa gani kwa mke wa mkuu wa kijiwe kuwa mkuu wa wanawake wote au mtoto wa mkuu wa kijiwe kuwa mkuu wa vijana wote?

Naota nakuwa kwini siyo! Pesa ya safari hii imetolewa na kwini. Ila usimwambie mtu.

Chanzo: Tanzania Daima Machi 6, 2012.

Monday, 5 March 2012

Tanzania itakuwa shamba la bibi hadi lini?

Hivi karibuni gazeti moja la kila siku wiki liliripoti kuwa kigogo mmoja wa dini mkoa mmoja kanda ya ziwa angefikishwa mahakamani kwa kosa la kuhujumu uchumi.

Kosa lake ni kwamba alikuwa akitumia dini yake kupata misamaha ya kodi ilhali alichokuwa akifanya hasa kwenye kununua saruji ni kuwasaidi wafanya biashara kukwepa kodi ya mamilioni kila mwezi. je huyu kweli ana dini au ni kafiri wa kawaida? Je ni wangapi wanatumia taasisi zao za kidini zilizochipuka kama uyoga kujitajirisha? Je hiki ndicho chanzo cha utajiri wa ghafla wa viongozi wengi wa madhehebu ya dini?

Nimekuwa nikilalamikia uholela na urahisi wa kusajili madhehebu ya kidini bila kusikilizwa. Nadhani Kwa tukio hili angalau tunaoshuku biashara hii ima ya misamaha hata unga ukiachia mbali kuiba sadaka na kutapeli wananchi tutaanza kusikilizwa kwa makini kama hakuna mkono wa serikali kwenye ushirika huu mtakakitu.

Pia kuna uwezekano kuna maafisa wa serikali wanaojua mchezo huu. Lakini kwa vile wananufaika nao hawataki hata kuishauri serikali kuweka vigezo vigumu kusajili madhehebu ya kidini ambayo siku hizi yamegeuka kama maduka ya kawaida.

Nchi yetu ina utaratibu wa hovyo kwenye mambo mengi kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Shilingi yetu iko chini kuliko sarafu zote kwenye eneo hili. Tunazidiwa na hata na Burundi na DRC pamoja na kukumbwa na misukosuko miaka nenda rudi! Angalia tulivyo na maduka mengi ya madawa tena mengi yakiuza madawa feki na yaliyo expire utadhani nchi yetu ni ya wagonjwa wa akili?

Tazama maduka ya mikorogo yalivyotapakaa huku tukiendelea kuhatarisha afya za watu wetu hasa akina mama. Tazama tulivyowekeza kweney glosari kuliko hata shule. Niliwahi kuliongelea hili kwa kulinganisha na Uganda ambako kuna shule nyingi wakati sisi tuna glosari na guest house za chap chap nyingi. Hili ni tatizo hata tunapodanganywa tuugane na nchi nyingine za Afrika mashariki ambazo hazina raslimali nyingi kama zetu na ardhi. Tatizo jingine ni kwamba hatuna hata mipango mizuri. Bado tunafanya unafiki wa kutangaza matangazo ya kuchochea ngono kwa kisingizio cha kupambana na ukimwi.

Turejee kwenye kuhujumu uchumi kwa kutumia majoho ya dini. Kwanini serikali haitaki kujiuliza ni kwanini madhehebu ya dini yameongezeka huku wanaojipachia uchungaji, ushehe, uaskofu, utume-bado upapa-ni wengi na hawafanyi kazi yoyote zaidi ya kuhuburi lakini bado ni matajiri wa kutupwa? Wasitudanganye kuwa pesa inapatikana toka kwa waumini maskini wanaolalamika kila siku. Lazima kuna njia nyingine nyuma ya pazia na huu ndio motisha wa kila mtu kupenda kufungua makanisa na misikiti. Imefikia mahali hata wageni wanakuja kufungua makanisa Tanzania kwa vile hakuna sheria ya kuwazuia wala kuwachunguza.

Mbona Yesu alipiga marufuku watu kukalia kupiga kelele badala ya kufanya kazi maana binadamu hawezi kuishi kwa neno pekee? Kwa kutilia mkazo mtume Paulo alisema asiyefanya kazi na asile. Ajabu hawa wetu wanakula hata kuwa matajiri bila kulazimishwa na sheria kutoa maelezo walivyopata utajiri wao! Mbona Sayyidina Omar bin Affan aliwazuia waislamu kupoteza muda mwingi kwenye ibada bila kufanya kazi miaka zaidi ya 1,000?

Tunao wezi wengi wanaowaibia watu wetu na kuwahadaa. Kwanini mhasibu au mfanya kazi wa serikali anapoiba ofisini kwake linakuwa kosa la jinai lakini kiongozi wa dini akiliibia kanisa au dhehebu lake haliwi kosa la jinai? Mwizi ni mwizi hata awe askofu au shehe au rais. Kinachokera ni pale serikali inapozidi kuwapumbaza watanzania kuwa ni nchi ya amani wakati ni nchi ya kuibiana. Hivi haya maelfu ya wetu wanaotapeliwa na majizi haya na kutumia nafasi zao kukwepa kodi yanaashiria amani?

Tusipofumbuka macho tutajikuta tuna makampuni yanayoonyesha kunawiri kuliko mengine si kwa sababu ya umahiri katika kufanya biashara bali umahiri katika kukwepa kodi. Kwanini taifa letu hasa viongozi wetu ni wagumu kujifunza? Wawekezaji wengi wamekuja wameiba na kuondoka huku tukizidi kukaribisha wengine kuja kuiba. Wako wapi wahindi waliokuwa ‘wamewekeza’ kwenye shirika la reli? Wako wapi majambazi wa Dowans walioendelea kutuzidi akili kwa kubadilisha majina ya biashara zao? Nenda kwenye mahoteli yetu mashuhuri. Kila baada ya miaka mitano yanabadilishwa majina ili kupewa muda mwingine wa kutuumiza. Angalia makampuni ya simu yanavyobadilisha majina mara leo so tell kesho mot el tel tel tel tel mpaka lini? kwanini msiseme ni stealtel?

Bado makampuni hayo hayo ya simu yanayolangua watu wetu ukiachia mbali kuwalisha huduma mbovu kuliko nchi nyingine za kiafrika. Imefikia mahali watu walioko nje kupiga simu kupitia nchi jirani kuepuka kulanguliwa. Hebu tutoe mfano mdogo. Ukipiga simu toka Kanada kuja Tanzania kwa Tanzania unachajiwa senti 25 za dola ya Kanada wakati Kenya wanakutoza senti 5. Hii maana yake ni kwamba kupiga simu Tanzania ni aghali mara tano kuliko Kenya. Je ni kwanini hali inakuwa hivi kana kwamba hakuna serikali? Hata ukipitishia Uganda hata Burundi bado ni nafuu kuliko kupiga moja kwa moja Tanzania. Hapa bado hujapambana na upuuzi kuwa namba unayopiga haipo mara huna salio la kutosha na ushenzi mwingine mwingi? Je huu ndiyo uwekezaji au uchukuaji? shame on you all!

Nikijumlisha yote hayo hapa juu huwa mara nyingi nafikia hitimisho kuwa nchi yetu imo mikononi mwa ima mataahira au watu wasiojua wanachofanya na kama wanajua basi watu wasiopenda nchi yetu. Imo mikononi mwa watu hatari ambao huko tuendako watasababisha vurugu na balaa kwa taifa. Maana hakuna kisicho kuwa na mwisho. Watu wetu hawawezi kuendelea kugeuzwa mbuzi wa shughuli au bidhaa kwa ajili ya wezi wachache kujitajirisha

Chanzo:Dira Machi, 2012

Mlevi apata PhD katika Utawala


Ambuye muwapatse moyo

Ambuye muwadalitsa

Cholinga Ambuye lololo

Yehova Yire

EL Shaddai

Yehova Tsidkenu

Yehova Shalom

Yehova Shammah

Yehova Nissi

Ndugu zangu toka kule utawasikia wakisema: nyimbo yopembedzera iyi ndipo ndimayikonda

Kwanini nisiimbe kumsifu Mungu kunijali kupata PhD yangu ya Utawala toka kwenye chuo kikuu cha Topchekreti nchini Nohihino. Mie huwa sipendi kutangaza mambo yangu kama wale malimbukeni. nilikuwa nikisoma kisirisiri ili kuepuka wasiniroge au matapeli kuja kunishawishi niachane na kuharibu ubongo wanipe shahada feki kama zile za akina Imma Nchimvi, Makorongo Muhanga, Meli Nyagu, Bill Lukuwi, Dolorous Kamalashomile, Mustaafu Mkulu, Didas Makalio na wengine wengi wanaojiita wasomi na madaktari wakati ni vihiyo. Huwa nachukua shahada mbili yaani za kughushi na kupewa dezodezo. Huu ni ufisadi wa kitaalamu hata kama umebarikiwa na kuhalalishwa na wakubwa wenye maslahi nao.

Mada yangu au thesis ya shahada yangu ilikuwa “Mfumo wa Walevi unahitaji kurekebishwa nan a kutengenezwa mfumo mpya,” kwa kimombo ni “Structural and Sytemic Overhaul of the current corrupt system governing Walevi and the way it must be replaced.”

Pamoja na kwamba ukurasa mmoja hautoshi kueleza nilichokiandika hadi kupewa shahada ya udaktari, nitatongoa machache niliyodurusu hadi maprofesa wa kizungu wakapata kizungumkuti na kunipa shahada yangu hata kabla ya muda wake. Kitu kingine ni kwamba nimeiingi akwenye vitabu vya historia na maajabu kwa kuwa mwanafunzi wa kwanza kufanya shahada ya udaktari katika kipindi kifupi na kupata alama zote. GPA au kiwango changu cha alama kilikuwa 7.0. hii imewahi kufikiwa na Albert Einstein na Newton peke yao. Mie ni binadamu pekee aliye hai kuwahi kufikia kiwango hiki. Hii maana yake ni kwamba maswali yote niliyoulizwa tangu kuanza kujiandaa na mada yangu na mada yenyewe niliyajibu kwa kiwango cha juu kuliko hata walimu wangu.

Kutokana na mafanikio, nimepata mialiko mingi kwenda kufundisha vyuo vikuu hasa jinsi kanywaji kanavyofanya mtu kuwa kipanga.

kwa ufupi ni kwamba mada yangu kama nilivyoieleza ilikuwa ikihusika na mifumo mbali mbali ya kijamii na kisiasa chini ya utawala unakumbwa na ugonjwa uitwao ammaglobulinemia ambao mara nyingi ni mparaganyiko wa muundo wa viasilia. Pia kuna ugonjwa mwingine uitwao bulimia ukiandamana na mwingine uitwao megalomania kama nilivyoueleza hapo juu.

Kwa mfano, nilipofanya analysis-uchambuzi wa kina, juu ya kaya ya Bongolalaland, niligundua kuwa magonjwa haya yalianza kuiandama mwaka 1992 ilipochanganya viasili vya vyama vingi na chama kimoja kiasi cha kuzaa kiumbe wa ajabu aitwaye usanii au coniostosis carcinoma ambayo ni kansa ya hatari sana kisiasa. Kitaalamu hii niliita mitostic anomaly. Kiini hiki cha ugonjwa huu kilionekana katika nchi nyingi kuanzia Maghreb hadi kusini. Ndiyo maana Nato walivujisha fomula ya kukitibu kiasi cha kuzitibu nchi nilizotaja hapo juu.

pia niliweza kujenga dhana au theory ya kupambana na ugonjwa uitwao Kleptocracy au kitaalamu zaidi “kleptogonia” and “criminogonia” nilsema “ we need purebred of Jasmine like mindis that will thwart all alleles resulting from this abnormality in meiosis and mitosis of the cell of the country suffering from kleptocracy so as to become kleptogonia and criminogonia.”

Kusema ukweli sina tafsiri ya nondo hizi nzito ambazo ziliacha wazungu wakikuna vichwa na kugugumia kwa kujua kuwa kumbe kifaa kipo ila kilichelewa kujitokeza. Kanuni hii niliita Jasmin na ndiyo maana hata mapinduzi yote yaliyotokana nayo yanaitwa Jasmin Revolution.

kwa taarifa yenu Jasmine formulae kumbe ndiyo iliyotumiwa na waandamaji kule Libya Masri na Tunisia walikopi kwangu kutokana na fomula yangu kuvujishwa na NATO. Usimwambie mtu kwa sababu waliniomba msamaha yakaisha.

Kitu kingine ambacho kiliwachanganya maprofesa ni ile hali ya kutoka na minor thesis isemayo kwa nchi Matonya zikatiwe misaada ili watu wake wawe kama Jasmin na kufanya kweli. Nilisema wazi kuwa misaada wanayotoa wafadhili haisadii bali kuongeza alleles za ugonjwa kiasi cha Carsinoma kubadilika na kuwa Kaposi’s Sarcoma ambayo mara nyingi waganga huiita kansa ya ngozi in vivo. Lakini katika sayansi ya utawala hii Kaposi’s sarcoma tunaiita ufisi kutokana na kutandaa kwenye mwili wa nchi kwa kushambulia huku na kule kama fisi wafanyavyo. Hivyo jinaufisi au ufisadi kwa lugha nyepesi.

Hivyo misaada ikikatwa, kondoo watageuka fisi na kuanza kushambuliana na viini vya Kaposi’s sarcoma. Katika elimu ya chembe chembe za uhai Cellular anology and morphology hii huwa tunaiita killing the formation of malignant neoplasmic Golgi apparatus. haya madudu ni magumu kwa Kiswahili. Hivyo nitaomba niachie hapa nisije nikapasua vichwa vya wasomaji wangu ambao najua hawasomei PhD kama mimi ambaye nililazimika kuyasoma haya madudu ili kuipata na kuwakoga walioghushi na kupewa dezo.

Kwa ufupi ni kwamba mimi ni mtaalamu wa chembechembe za mfumo ndiyo maana ilinibidi kusoma chembe chembe za viumbe hai ili kuweza kulinganisha na mifumo ya dola. Uzuri wa PhD yangu ni kwamba naweza kwenda hospitalini na kutibu au hata kufundisha kwenye vyuo vikuu hasa wanafunzi wanaotaka kubobea kwenye utafiti wa chembe chembe za uhai. Ndiyo maana niligundua kuwa kanywaji kana chembe chembe zinazoamsha ubongo na kufanya kazi kama kompyuta.

Sitaki niseme mengi ili nisionekane najidai na PhD yangu. kwa ufupi ni kwamba ninaposema naitwa Dk. Mlevi Mdanganyika si kwamba naigiza au kutumia ya udaktari wa kughushi au kupewa. la! Nimesotea sana kwa madolari mengi ambayo yalitolewa na rafiki yangu na ndugu yangu Bill Gates na shemeji Mellinda. Ila usimwambie mtu ili Matonya wenu wenye masuti wasijeenda kumghasi kutaka asomeshe vitegemezi vyao visivyo na akili. Hamkuviona vingi vikiondoka na divisheni zero? Angekuwa kitegemezi changu siku hiyo ningemnyonga kama siyo kumkatakata vipande na kuwapa mbwa. Hata hivyo angepata wapi utaahira wakati wazazi wake wote tu vipanga? Hata bi mkubwa wangu anamalizia PhD yake kwenye uwekezaji. Uzuri anasoma majuu ambako hakuna shahada za chupi kama nonihino. Hata hivyo miwaya itawamaliza. Mwakaribishwa wote kwenye mnuso wa kusherehekea kutunukiwa PhD kwa mlevi isipokuwa wale walioghushi.

Chanzo: Dira Machi, 2012.





Thursday, 1 March 2012

Wakati wafadhiliwa wakitanua, wafadhili wanapatilizwa


Rais Nicolas Sarkozy wa Ufaransa amekumbwa na kasheshe za kuzomewa na kutupiwa mayai visa hadi kukimbilia kwenye baa alipojificha kujinusuru na hasira za wananchi wanaochukia utawala wake. Inashangaza hasa kwa watawala wetu ambao ni miungu hasa ikizingatiwa kuwa wanaowafadhili na kuwawezesha kubakia madarakani wanatenzwa kama wasio na cheo. Je inakuwaje wafadhili wafadhaishwe na watu wao lakini wafadhili hao hao wawavumilie watawala wanaofadhaisha wananchi wao ukiachia mbali kuwanyonya na kuwadhalilisha. Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.

Wednesday, 29 February 2012

Africa Needs to Sign a New Social Contract

Jean Russeau wrote in Social Contract, “Man is born free and everywhere he is in chains.” To free himself, Russeau suggests that man must gain security and measure of freedom from action in exchange for surrender of rights and property to the general will. This is not the language of compliance or cowardice but of rebellion.


It is no exaggeration to assert that Africa, politically, socially and economically is in the 14th century. Many African countries are sitting on the vast resources which are abused by a cabal of people in power. While this is happening, the big population is dying in abject destitution.


When philosophers Thomas Donaldson and Thomas W. Dunfee coined a phrase, “Intergrated Social Contract Theory” (ISCT), they stated categorically that every right an individual enjoys also has corresponding duty. In business, this is sharing risk and reward. Whenever there is a risk, change, calamity or needs, the corporate as a big entity benefiting more from the business must help employees - who also benefit from the business but at a less magnitude comparably - in this period of transition.


Running a country is like running a corporation. The difference though is that the corporation employs a person because he/she has some qualities or qualifications the corporation needs to use to make profit and sustain it. When it comes to be a citizen in the corporate known as a state, the citizen qualifies by the right of birth or application for those who apply for citizenship of other countries. When it comes to men and women manning Africa, they enjoy rights of spending poor taxpayers’ money as they deem fit without the corresponding duty of delivering service.


The corporate-government is duty bound to deliver so as to enjoy the right of being a government. This is where the situation in African countries worsens more than even under colonialism in 1960s. If anything, Africa needs a jumping-off point from the 14th century style of management next to Caesars’, to the 21st century of responsible presidents or managers of the corporation known as state. It is high time for Africa to have responsible and accountable leadership championed by our academics.


We need advocates of a new social contract who can decisively interpret and champion ISCT. This will be possible if our academics will stand and take on dirty regimes instead of joining them to plunder the hoi polloi as it currently is in many countries. It is no longer shocking to see African ignorant rulers using academics in their governments to destroy their country as it once happened in the Gambia where President Yahya Jammeh used the minister of health who is a doctor professionally to claim he had discovered a cure for HIV/AIDS. Under the new social contract, this wouldn’t be possible given that presidents would be accountable for their word and deed.


Our rulers are prone and proud of being referred to as Excellencies and other fake homilies. They live in the heaven amidst the hell of miseries of their people. Who is wrong hither between them and the citizens who are in bed with such obnoxious and notorious vices?


Gandhi once remarked, “How can men feel themselves honoured by the humiliation of their fellow-beings?” In the same book by Louis Fischer: Gandhi: His Life and the Message to the World seems to have the answer. He wrote, “Some men loom larger by lifting up others and some by kicking and humiliating others.” If anything, this is the real situation between Africa and the developed world. How can for instance, DRC produce tonnes and tonnes of minerals and Nigeria oil alongside with tonnes and tonnes of poor people? The West, despite having fewer resources, was able to attain their development, among others, thanks to signing and ratifying a new social contract that empowers people and their governments. It through accountability of everybody that made western countries be ahead of us for everything.


Africa cannot forge ahead with the current mediocrity whereby academics are abused without resisting. Our academics should enlighten the hoi polloi so that they can take on their irresponsible rulers. This must be the war between hoity toity and hoi polloi spearheaded by academics. It does not make sense to see our rulers abuse our tax and donor monies while academics scramble to join politics so as to share the loot. Why are our rulers spending our hard-earned taxes on travelling abroad and recruiting private armies while we are dying wantonly? This is the question our academics need to ask and give the answer instead of being in bed with those who arrest the future of our continent and her innocent people.


For Africa to move forward, a new social contract that holds our ruler accountable and responsible for whatever they say and do must be signed. We can draw a lesson from academics such as Martin Luther, Conrad Grebel, Bathsar Hubmaier, Thomas Muetzer, Ulrich Zwingli and others who gave the Roman Church hard time so as to change the world despite being young guys. We need to start asking our rulers what have they have done for us as agreed in elections or constitutions.


We need to start enjoying the fruits of our freedom that turned out to be enjoyed by rulers and their henchmen. Academics must pull Africa from the 14th Century to 21st Century by advocating the signing of a new social contract that makes our rulers accountable.

Source: The African Executive Magazine Feb. 29, 2012.

Kupunguza ujumbe au kuchunguza ziara za Kikwete?

TAHARIRI ya gazeti hili ya tarehe 22 Februari si ya kupuuza. Suala ililolenga na kuliongelea ni muhimu sana kwa mustakabali wa uchumi wa Tanzania na watu wake. Kwa ufupi ni kwamba tahariri tajwa ilibeba kichwa cha “Msafara wa Rais nje upunguzwe.”

Mhariri alimuonea aibu Rais Jakaya Kikwete kwa kutaka msafara wake upunguzwe. Kimsingi, msafara wa rais Kikwete si wa kupunguzwa bali kuchunguzwa na kuwekewa masharti. Kama rais hana nidhamu ya matumizi wa chini yake wataipata wapi? Maana, pesa anayofuja na marafiki zake huko nje si zake bali za mlipa kodi maskini wa nchi hii. Hapa ndipo mzizi wa umaskini wa nchi yetu. Lazima waliomwajiri (walipa kodi) wajue aina ya watu anaoandamana nao na kwanini? Kwa nchi yetu ilivyooza, tusipozuia mchezo huu wa matumizi ya hovyo yasiyoangalia hali halisi ya kiuchumi, tutashtukia tukiwa tunalipia misafara sawa na ile ya akina Mobutu Seseseko iliyojazana marafiki, waramba viatu na wanafamilia ya mwizi huyu wa zamani wa DRC.

Niliwahi kuhoji ni kwanini msafara wa rais siku hizi umekuwa hata siri. ni juzi tu nilijua kuwa aliandamana na watu 40. Mara nyingi idadi ya anaoandamana nao inakuwa siri. Mbona wakati wa mwalimu Julius Nyerere licha ya kufanya ziara chache, ujumbe aliokuwa akiandamana nao ulikuwa ukitangazwa? Rais Kikwete amelalamikiwa mara nyingi ila ameziba masikio. Amefikia kuitwa majina ya ajabu ajabu kama mtalii, Vasco da Gama na mengine mengi kutokana na mapenzi yake ya kusafiri nje hata wakati akihitajika kutoa maelezo na uongozi nchini. Nani mara hii kasahau alivyokwenda kwenye mkutano wa uchumi wa Davos nchini Uswizi wakati wa mgomo wa madaktari uliosababisha vifo vya watu wengi?

Kwanini rais hataki kujua na kukubali kuwa ziara zake nje ni chanzo kimojawapo cha umaskini wa taifa letu na mfadhaiko wa uchumi? Je, ni kwanini rais anajali sana safari za nje badala ya watanzania wenye dhiki nyingi za kutengenezwa na utawala mbovu uliokumbatia ufisadi na matanuzi? Je, rais anafanya hivi kwa faida ya nani? Kwa wanaokumbuka shutuma zilizompata waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye alipotumia zaidi ya shilingi 500,000,000 kwenye ziara yake ya Marekani, wajaribu kufikiri. Je rais anatumia kiasi gani kwa ziara moja ughaibuni iwapo waziri mkuu zama zile wakati mfumko wa bei na gharama za maisha vilikuwa chini anatumia kiasi gani kwa sasa? Kwa mujibu wa taarifa za siri za kiuchunguzi, kufikia tarehe 9/9/2011 rais aliposafiri kwenda Kenya kwa ziara ya kikazi, alikamilisha ya 316 tangu aingie madarakani mwaka 2005! Hii maana yake ni kwamba tangu Rais Kikwete aingie madarakani mwaka 2005, amekwisha kusafiri nje zaidi ya mara 300. Hii ukigawanya kwa miaka sita ambayo amekuwa madarakani ni kwamba kila mwaka amekuwa akisafiri mara 50 sawa na karibia mara mbili kwa mwezi au tuseme kila baada ya siku 20. Je, rais kama huyu anayekaa nje ya ofisi na nchi zaidi ya ofisini anafanya kazi lini?

Mbona marais kama Ian Khama wa Botswana nchi yenye uchumi mzuri Afrika hawasafiri kila siku? Mbona hapa jirani yetu Rais Mwai Kibaki hatumsikii akiruka kila uchao? Kuna nini kwenye biashara hii ya ziara za ughaibuni? Kwanini Kikwete hataki kuona na kuukubali ukweli? Je, hajui kuwa baada ya kuondoka madarakani hiki chaweza kuwa kikwazo kwake? Inashangaza kuona taifa lenye bajeti tegemezi kwa wafadhili kwa kiasi cha 40% kuwa na rais anayesafiri sana kuliko hata wafadhili wake. Ukifuatilia ziara za rais Barack Obama nje au waziri mkuu wa Uingereza na Canada nje, utakuta hazifikii hata hamsini, kwa mfano tangu Obama aingie madarakani, ni kwa utajiri upi Kikwete anatanua hivi? Kufikia tarehe 19/11/ 2009 Rais Obama alikuwa amefanya ziara 24 nje ya nchi tangu aingie madarakani na hili lilipigiwa kelele na Wamarekani. Kwa miaka minne maana yake ni kwamba kila mwaka amefanya ziara nane kwa mwaka wakati Kikwete akifanya mara zaidi ya kumi na mbili ya ziara za Obama! Ziara za Obama si siri; zina hadi Wikipedia yake ili anayetaka kujua aweze kujionea. Huu ndiyo uchumi na uwazi na ukweli na si matanuzi na maangamizi ya fedha za umma.

Kufikia tarehe 23/10/2010 rais mwingine anayeitwa mtalii na watu wake Zuma alikuwa ameishafanya ziara 40 chini ya miaka miwili tangu kuingia madarakani. Hata hivyo, baada ya kupigiwa kelele na wananchi wake, Zuma amepunguza ziara zake nje tofauti na Kikwete anayeendelea kuongeza ziara zake. Kwa wanaojua tabia ya Kikwete hawatashangaa kutokujifunza kwake. Hatabadilika. Maana hata alipoingia madarakani aliahidi kupunguza ukubwa wa serikali hasa baraza la mawaziri. Alifanya nini baadaye? Licha ya kuunda baraza kubwa la mawaziri kuliko la mtangulizi wake, aliongeza idadi ya wilaya na mikoa wakati uchumi ukiendelea kuporomoka kutokana na usimamizi mbaya na ufisadi.

Anachofanya Kikwete sawa na mwenzake wa Uganda ni kutumia pesa nyingi kuliko hata wizara nyeti. Mwaka 2011 kulikuwa na kituko ambapo Ikulu ya Uganda iliomba jumla ya sh za Uganda 5,055,000,000 kwa ajili ya safari za rais kwa miezi saba tu huku Wizara ya Maji na Mazingira ikitengewa sh bilioni 2.44 kwa mwaka 2010 na bilioni 3.228 mwaka 2011 kwa ajili mishahara ya miaka miwili. Wakati Ikulu ikitaka bilioni hizo 5.055 kwa ajili ya matanuzi ya Museveni nje, Ikulu hiyo hiyo iliomba pia Ushs bilioni 3.497 kwa ajili ya matengenezo ya magari ya rais huku mafuta pekee yakigharimu Ushs 120, 000,000! Wachunguzi wa mambo wanasemea kuwa Museveni alitumia jumla ya Ushs bilioni 13.386 ambazo ni zaidi ya mara nne ya bajeti ya Maji na Mazingira. Je, kwa watawala waroho na wabinafsi kama hawa Afrika inaweza kusogea mbele? Je, hawa si chanzo kikuu cha umaskini wa watu wetu? Je, rais kama Museveni au Kikwete wanatumia pesa kiasi gani katika utawala wao wote? Trillions of shillings of course. Kuna haja ya kuchunguza bajeti inayotengwa kwa ajili ya matumizi ya Kikwete. Chanzo: Tanzania Daima Februari 29, 2012.

Wednesday, 22 February 2012

Africa: Are Rip-offs Paying Off?

News from Uganda that two ministers resigned after allegedly misappropriating a cool $ 60,000,000 was shocking. When this sacrilegious theft by the high and mighty was reported, Ugandans as well as other Africans received it just as a normal thing especially for a begging country like Uganda!

The two were Gender Minister, Syda Bbumba who then served as finance minister and Prof. Khiddu Makubuya, a minister in the Office of the Prime Minister, who was attorney general when money was paid as compensation to one Bassajjabalaba by inflating amount of money at the tune of excess $60,000,000. This is according to the Parliamentary Accounts Committee which launched an investigation and unraveled such rip-off.

Those conversant with how Africa is ruined and plundered by her own were not shocked. In neighboring Tanzania in 2005, close to presidential and parliamentary elections, over $ 130,000,000 was stolen from the Bank of Tanzania. The trails directed to the then president Benjamin Mkapa and the then presidential candidate Jakaya Kikwete, the current president. Since then, this country has not jailed any culprit in this connection.

Remember the mother of all theft in East Africa, the ‘Goldenberg’ scandal in 1990 that saw Kenya lose over $ 600,000,000 ? Responsible con-people have never been convicted since then. The Goldenberg scam was estimated to have cost Kenya the equivalent of more than 10% of its annual Gross Domestic Product (GDP).

Many would argue: Where was government? In the two cases of Kenya and Tanzania, such huge amounts of money were stolen directly from the Central Banks of the said countries. The governments were there in the same business of plundering the hoi polloi.

Going back to Uganda, when the two ministers decided to resign, the general public saw it as a victory due to the fact that sacred cows in Africa are nary slaughtered. So for countries where accountability is a foreign vocabulary, people felt like wining against the venal officials without knowing that resigning after causing such a huge hole on the economy is nothing comparably if the law would be utilized reasonably.

When a person robs the public and the punishment meted out on him is resignation, this means many will steal so as to retire rich guys. With such megalomaniacs in power, can we really develop our countries? What agonises is the fact that donor countries are always shouting at the top of their voices that accountability, good governance and democracy are key to a country being aided.

Is it because much of the money stolen is ending up being stashed in western banks or it involves their nationals? It is because this business- plundering Africa- has always benefitted them due to the fact that many fat thieves end up investing there as it happened for Mobutu Sese-seko and other big thieves? In Africa, stealing public monies is not a crime apparently. Challenging or opposing a president is. Africa is in financial anarchy whereby a connected cabal of thieves can rob the public without being made to face the music.

If you want to die earlier in Africa, try to steal small money or chicken. You will be butchered in the daylight even in front of police officer. But when you steal big sums, no son of gun will touch you. Instead, you’ll become mightier so as to dine with the president. For money is always power. Those who remember, Kamlesh Pattni, the architect of Goldenberg, know what I mean. One thing is obvious. Every humungous theft in East Africa used to involve two people -government official and Asian businessmen. Why? Simple, it takes two to tango. However, Uganda’s case is an exception to the general rule. For the receiver was a Ugandan. May be this is revolution in stealing public money. Before this revolutionary theft, who’d trust the guy, who after being cornered, would spill the beans by revealing who is behind this theft by the high and mighty whereas Indian business men can pack and jump onto the plane and vanish to Canada India and UK?

Africa must fight by all means to stop such $ 60,000,000 resignation as the only punishment for such an offence. When one muses on this theft, let us quote one of the reports that implicated these two ministers as quoted by The Daily Monitor, “November 13, 2010. President Museveni writes to Makubuya, Central Bank Governor Tumusiime Mutebile and Ms Bbumba instructing them to oversee a speedy compensation for Haba Group’s claims.” By the way, who’s who in this theft?

Source: The African Executive Magazine Feb.22, 2012.

Ubunge wa viti maalum ni haramu kisheria


Tanzania inaweza kuwa nchi pekee yenye viti vingi vya ubunge utokanao na vitu vyenye kila aina ya ubaguzi hata udhalilishaji chini ya dhana ya viti maalumu-wabunge wasio na kazi yoyote bungeni zaidi ya kungojea posho na sifa ndogo ndogo magazetini.

Kimsingi, hakuna mantiki ya kumpa mtu eti kuwakilisha vijana kwenye bunge, huyu mbunge wa kawaida ambaye jimbo lake lina kila aina ya binadamu atawakilisha nani? Je vijana au wanawake wana nini cha zaidi hadi kuwa na wawakilishi zaidi ya mmoja?

Kimsingi ubunge uwe wa vijana wazazi, wanawake na upuuzi mwingine ni iwizi wa pesa ya mlipa kodi unaofanywa na wanasiasa. Bahati mbaya hata vyama vya upinzani vimeuingia mtego huu na kushiriki dhambi hii. Siku hizi kila sehemu zinasikika nyimbo na ngonjera za demokrasia na usawa baina ya mwanamke na mwanaume. Hivi kweli kumpa mtu kiti kwa kigezo maalum na jina maalumu kama viti maalum si kumtukana na kumdhalilisha? Kwanini, kama tunawapenda na kuwathamini wanawake, tunawatengea viti vichache tu? Kwanini tusijenge mazingira ya ushindani wa haki na uchaguzi huru ili wanawake na wanaume na wanawake wapambane na atakayeshinda awe mbunge? Kwanini kuwadhalilisha na kuwagawana vijana na wanawake ambao kimsingi ni wengi na wakiamua kutumia wingi wao kwa busara hawana haja ya kupewa upuuzi unaoitwa viti maalum.

Umefika wakati wa kuwaambia vijana na wanawake kuwa viti maalum si suluhisho wala ukombozi kwao bali nyenzo ya kuwapumbaza na kuwagawanya ili wasitumie nguvu yao ya wingi kuamua nani awe mbunge hata rais. Hakuna asiyejua kuwa, kwa mfano, wanawake wengi walioteuliwa kwenye viti maalum wengi wanaonekana kwa jicho baya. Wapo wanaowaona kama kupe waliobebwa na watu fulani na kupewa ulaji huku wengine wakifikia hata kuvidhalilisha viti hivyo kwa kuviita viti vya chupi. Tumefikia mahali hata spika wa bunge anachaguliwa kwa jinsi yake badala ya sifa! Huku si kumkomboa mwanamke bali kumdhalilisha.

Ukiachia kudhalilishwa kwa viti hivi maalum, wengi wa wanufaika wa nafasi hizi ni watu ima ambao ni watoto wa wakubwa au wenye kuwa karibu na wakubwa chamani jambo ambalo limeleta malalamiko mengi karibu katika vyama vyote. Wengine wanasemekana kupata nafasi hizi kupitia rushwa na jinai nyingine kama kujuana, ukabila hata ujimbo. Anayebishia hili ajikumbushe majina ya akina mama wengi wabunge wa kuteuliwa ambao waume zao au baba zao wana madaraka atajua tunachomaanisha. Huku si kumkomboa mwanamke bali kumnyonya, kumtumia na kumdhalilisha.

Kwa vijana na wanawake kilichofanyika ni sawa na kuwatupia mbwa mfupa halafu mwizi aliyefanya hivyo akapata upenyo wa kuiba toka kwenye lindo la mbwa hao hao. Kuna haja ya kuwaambia wabunge wa kuteuliwa na viti maalum kuwa wanachofanya licha ya kuwa kazi ya kutumiwa, wanahujumu uchumi wetu. Hawana kazi bungeni zaidi ya kuwakilisha matumbo yao na wale waliowapigia kifua. Kimsingi, hawa si wabunge bali wala vya dezo vya umma. Kuwaambia ukweli ndiyo njia pekee ya kuwakomboa kuliko hawa wanaowatumia na kuendelea kutafuta jinsi ya kuhami jinai hii iliyohalalishwa.

Ukiangalia nchi ombaomba kama Tanzania kuwa na utitiri wa wabunge hata majimbo ya uchaguzi na mikoa unashangaa uwezo wetu wa kufikiri. Badala ya kujibana na kusogeza nchi yetu mbele, tumeruhusu kundi la watu wachache kupeana ulaji tena kwa kulipana kodi zetu! Kimsingi, hata tukiamua kutumia sheria zilizopo hasa katika inayolaani ubaguzi wa aina yoyote na kuhimiza usawa, viti maalum ni haramu na wizi unaohalalishwa kwa vile unatendwa na wanaoitwa waheshimiwa. Kwanini kwa mfano jimbo la Lushoto kuwa na wabunge maalum wakati mbunge wa jimbo anawakilisha aina zote za watu kuanzia wanawake, wanaume, wazee, vijana, watoto na kadhalika?

Kisheria kuwapa watu ubunge au kazi kwa kuangalia umri, jinsi, watokako na kadhalika ni uvunjaji wa katiba na sheria uanopaswa kuwafikisha wahusika gerezani. Je kuwapa wanawake ubunge kwa kuangalia jinsia yao siyo kuwabugua wanaume na hata kuwadhalilisha wanawake wenyewe? Au kwa vile ubunge ni ulaji basi wanawake wameridhika kuhongwa, kudhalilishwa na kubaguliwa katika taasisi za nchi? Kama wao wameridhika na dhihaka na jinai hii sisi kazi yetu kuwastua kuwa wasidhani kwa kupewa viti viwili vitatu vya udhalilishaji wamepata. Badala yake wamepunjwa na kupatikana. Hii yote huenda inatokana na kuwa na malengo madogo na mafupi kisiasa na ile hali ya wenye vyama kuwagaawana na kuwadhoofisha kimawazo.

Kimsingi viti maalumu licha ya kuwa nyenzo za kuibia kodi yetu na kutuwekea viongozi wa kupandikizwa na vikundi vya watu, ni chambo cha kuwaziba midomo mbwa wasiwapigie kelele wezi.

Je kuwapa vijana ubunge kwa kuangalia ujana siyo kuwabagua wazee? Mwanzoni mwa mwaka huu kuliamriwa kesi ya kihistoria iliyotufanya wachambuzi wa mambo tuliangalie upya suala zima la ubaguzi.

Je mnapotoa viti maalumu kwa mfano kwa jumuia ya wazazi. Hii siyo kuwabagua wasiozaa au ambao wameishaacha kuzaa? Wazazi hawahitaji hata kuwa na jumuia maana hata wabunge wa kuchaguliwa ni wazazi au wana wazazi pia na kama ni wanawake na wengine ni wanawake na kama ni vijana na wengine ni vijana.

Chimbuko la viti maalum ni mfumo wa chama kimoja uliowatumia ukiwahadaa kuwa walikuwa viognozi wa kesho. kuepuka changamoto na wingi wa wanawake na vijana ilibidi uundwe uchochoro wa kuwazuga, kuwagawanya ili wasikengeuke na kudai wao ni taifa la leo. mfumo wa chama kimoja uliona hatari ya vijana na wanawake kama wangeachwa bila kupewa kitu cha kuwahangaisha huku wakijenga chuki miongoni mwao kama ilivyo sasa ili kutotishia nafasi za wakubwa ambao mara nyingi waliwatumia vijana kwenye kila aina ya miradi na kampeni zenye faida kwao.

Sababu nyingine ya kuundwa jumuia za vijana ilikuwa ni kuwezesha kuwafuatilia na kuwadhibiti. Ukichunguza, kwa mfano, jumuia za Chama Cha Mapinduzi (CCM), kabla ya kuingia mfumo-zengwe wa vyama vingi vinavyoendeshwa na katiba ya chama kimoja, zilikuwa kama taasisi za ujasusi ya kuchunguzana baina ya vijana kwa vijana ndani ya chama.

Makala moja haitoshi kueleza ubovu na sababu za kuwapo ubunge wa aibu wa kudhalilishana. Tukipata muda siku nyingine tutauchambua tena. Kimsingi, kuna haja ya kubatilisha haraka ubunge huu haramu.
Chanzo: Dira Februari, 2012.

Mlevi aanzisha kampuni ya simu

KAMPUNI hii inaitwa TapelitelCOM. TAPELITEL au kwa urefu Tanzania Affordable and Preferable and Economical long-distance and Internal Telephone ni kampuni mpya iliyoanzishwa na mjasiriamali mie.

Ujasiriamali wangu ni tofauti na wa wale walioamua kujitwalia mali za umma wao wake zao watoto wao hata wakwe zao. Nadhani bado mnawakumbuka ingawa hamkuwapa discipline kwa ujambazi na udokozi huu.

Kwa vile mie si kibaka wala fisadi, nimeamua kuanzisha kampuni halali na ya kisasa isiyo ya kisasi kama ya wale.

Mie siyo kama wale walipopewa ulaji waliamua kugawana hata raslimali za umma. Nenda kwenye miraba ya uwindaji huko maporini utajua nimaanishachoa. karibu kila mahali ni ulaji ulaji ulaji mtupu. Na hii ndiyo maana mafisadi na mafisi hawashughulikiwi kwa vile huwezi kujua nani ni nani. Usijekuta unayetegemea amkamate mwizi ndiye mwizi mwenyewe. hayo tuyaache.

Nilitaka kuita kampuni yangu ya simu WALEtel au World Airphone Longdistance and Abracadabra Telephones baada ya kugundua kuwa kumbe uwekezaji kwenye makampuni ya simu una ulaji usio wa kutoa jasho, Mlevi nimesukuti kuanzisha kampuni ya simu. Ingawa sawa na makampuni ya simu ya ulaji yaliyojazana Danganyika, kampuni ya mlevi imebeba neno tel na com kwa shingo upande.

Maana uzoefu umeonyesha kuwa makampuni yenye majina ya tel mwishoni ni tel kweli kweli. Unajua maana ya tel? Tell Everybody Lies kwa Kiswahili mwambie kila mmoja hasa mteja uongo. Hamjasikia ukipiga simu unaambiwa mara: namba unayopiga haipo, huna salio la kutosha hata kama unapiga kwa dola, mara utasikia: jaribu tena mwaka ujao, namba yako imerongwa, namba unayopiga ni ya mzito na anaogopa kupokea, mara unayempigia yuko chooni na upuuzi mwingine mwingi. Wajua maana ya Com? com imewekwa kuficha ukweli wa neno lenyewe yaani Con or tapeli.

Tapelitel haitakusumbua na nyimbo za dini wala rafu ili kukuibia maana hazitolewi bure. Maana unaburudishwa ili kupumbazwa uibiwe. Pia mchezo wa simu kupokewa na secretary ndani ya gari la bosi unaambiwa bosi katoka nje kamuachia secretary usukani na simu hakuna.

Mambo ya bosi yuko mkutano wakati yuko pembeni mwa secretary ni noma sana. Pia kampuni ya Tapelitel haitaruhusu ukupe wa watu kubeep beep au kupiga haraka na kusema naomba unipigie. Maana uzoefu umeonyesha kuwa wanaobeep au kupiga na kuongea kama machizi kuwa uwapigie huwa na shida zao wanazotaka kukwambia lakini kwa kutumia pesa yako.

Wao wanajiona wajanja huku wakikuona wewe juha. Siku moja mlevi amewahi kupigiwa simu na jamaa akaomba ampigie. Alipompigia alishangaa kusikia kupe huyu akisema alitaka kumbomu fedha! Yaani unibomu halafu kufanikisha kunibomu eti mie ni kupigie? I am not mad and stupid that way. Sorry saana.

Kwa wale wanaishi nje wanajua adhabu wanayopewa kwa kukatwa pesa nyingi kwa kuunganishiwa simu bila kuongea. Yaani inakuwa pale kugundua kuwa mtu anakatwa pesa simply because kusikiliza upuuzi na uongo uliorekodiwa kwenye memory ya kompyuta. Jamaa washenzi kweli. Wanaunganisha simu ukianza kuongea wanakata na kuishia na pesa yako. Utasikia kuwa huna salio mara simu imeugua na upuuzi mwingine.

Kampuni ya TAPELITEL inawaahidi huduma mulua na za kisasa na si za kisasi kama hizi za sasa. Tutahakikisha wenye makampuni yote ya kijambazi na kisanii yanayowaambia upuuzi kila mnapopiga simu yatafunga madudu yake na kurejea huko ushenzini yalikotoka.

Kwa vile taifa linataka mkombozi katika mawasiliano, Tapelitel mkombozi aliyesubiliwa miaka mingi inawaahidi huduma siyo hujuma bora kama ilivyo. Kwanza tutatoza kiwango kidogo cha kuunganisha simu kwa walioko nje. Hawana haja tena ya kupiga simu zao kupitia kaya jirani.

Kwa walio ndani ya kaya, mambo ya kuwa na mitandao elfu katika simu moja sahau. Tutawapa huduma bora karibu na bure. Ila kwa wale wanaotumia simu kusema uongo na kutongozatongoza hovyo wanafunzi, wake na waume za watu wajue ima watapandishiwa gharama au simu zao kukatika hovyo hovyo kama hizi za sasa.

Kadhalika Tapelitel haitawasumbua na matangazo ya kijinga au kampeni za kifisadi kwa kuhongwa pesa na wanasiasa kuwatumia ujumbe wa kipuuzi. Sisi tutahakikisha mnaongea mnavyotaka wakati mnaotaka na kwa mnaowataka mradi msivunje kanuni tulizotoa hapo juu.

Pia Tapelitel haitashiriki kwenye kamari ya jishindie hiki wala kile. Sisi badala ya kuwapa zawadi zitokanazo na kuwaibia tutawapa huduma mnayostahili. Tutalipa kodi ipasavyo na wala hatutabadili jina hovyo hovyo ili kukwepa kodi.

Kitu kingine tutakachofanya tofauti na makampuni mengine ya kijambazi ni kuhakikisha tunaajiri wazawa kwenye kila idara ya kampuni. Tuna shida gani kuajiri wakimbizi wa kiuchumi wakati kaya ina maelfu ya watu wanaomaliza vyuo vikuu ndani na nje?

Kwanini kuajiri watu wa kuja kuiba na kulia kwao huku wakiwaacha walevi wakiadhirika kwa umaskini? Kitu kingine, Tapelitelcom haitaruhusu wakubwa wenye uroho, wake zao au watoto na wapambe zao kuja kununua shea kwenye kampuni hii adhimu.

Kwa ufupi ni kwamba kampuni hii mpya inaahidi kuwakomboa walevi kutoka kwenye makucha ya wezi wanaoitwa wawekaji wakati ni wachukuaji. Tunaahidi mapinduzi ya hali ya juu kuhakikisha kuwa kaya yetu inakuwa mojawapo ya kaya zenye huduma bora za simu. kitu ambacho tunapaswa kuwaambia mapema ni kwamba, sisi hatuna mshikamano na wanasiasa.

Hatuhitaji msaada wa wanasiasa kwa vile hatuna mpango wa kuhujumu uchumi wa kaya kama wao kwa kuwahonga wenye mamlaka ili waendelee kututia umaskini. Kimsingi, Tapelitelcom ni simu ya kila mtu.

Ni simu ya jamii na mali ya jamii. Tuungeni mkono tutokomeze huu ujambazi wa mchana unaofanywa na watu wenye mtindio wa ubongo kwa kukubali kutumiwa kuwahujumu watu wao.

Ngrrrrrrr! ngrrrrrr! Nani huyu kanideep? Ngoja nimtwangie. Pwi,pwi,pwi, ngrrrr ngrrr. “Simu unayopiga ina mafua.” Kwaheri.


Chanzo: Tanzania Daima Februari 22,2012.

Sunday, 19 February 2012

Pesa ya Lowassa na marafiki zake ni safi na halali?


Hakuna shaka kuwa Edward Lowassa waziri mkuu aliyetimka madarakani kutokana na kuingiza kampuni feki ya Richmond iliyoishia kuleta maafa kwa taifa, ni mtu ambaye amegeuka kuwa mkarimu hata kupita kiasi.

Hivi karibuni akiwa Kigoma akichangia shule ya Sekondari ya FPCT Bigabiro, Kigoma, alitoa mchango wa shilingi 60, 500,000 cash ukiwa ni mchango wake na marafiki zake ambao hawatajwi kwa majina. Huu si mchango mnono wa kwanza wa Lowassa hasa baada ya kuondoka madarakani. Wengi wanajiuliza: Kama ana uchungu na taifa hili kiasi cha kulitakia maendeleo na mengine mema, mbona alitumia nafasi yake kujinufaisha kwa kuingiza kampuni feki iliyoliingiza taifa kwenye zahama? Mwaka 2006 alichanga jumla ya shilingi shilingi 60, 000,000 kati ya sh 88,340,000 kwa ajili ya shule ya sekondari ya michezo ya Kigamboni. Hapa bado hatujaorodhesha michango mingine ya kuanzia shilingi 10,000,000 kwenda juu ambazo Lowassa ameishachangia kwa vituo vya yatima, kuzindua album, makanisa na mingine mingi.

Je hii pesa inayochangwa imepatikana kihalali au ni matunda ya tuhuma zake za Richmond na nyingine za zamani za marehemu baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyedai mwaka 1995 kuwa Lowassa amejilimbikizia utajiri mwingi ambao hautokani na kipato halali-asioweza kuutolea maelezo ulivyopatikana. Na kweli, tangu mwalimu alirushe kimondo hicho, si Lowassa wala familia yake walikuwa tayari kuelezea walivyochuma huo utajiri!

Baada ya Lowassa kulazimishwa kuutema uwaziri mkuu, alijikuta akikabiliwa na pigo jingine takatifu. Pigo hili ni pale chama chake Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilipomtuhumu kuwa gamba au mtuhumiwa mkuu wa ufisadi kiasi cha kumtaka aachie hata nyadhifa chache alizokuwa amebakia nazo. Lowassa hakukubali kutupwa nje ya uringo wa siasa hasa ikichukuliwa kuwa anatajwa tajwa kutaka eti kumrithi rais Jakaya Kikwete hapo 2015 jambo ambalo wanaojua alivyochafuka sana wanaona ni kama tusi na kejeli kwa taasisi ya urais na wananchi wa Tanzania kwa ujumla.

Ili kufanikisha azma yake hii, Lowassa, bila kujali kuwa watu wana akili za kuhoji na kuchambua, amekuwa akimwaga pesa kwa njia ya michango ili kujiweka karibu na wapiga kura akiwaaminisha kuwa anaweza kuwafaa wakati nafasi ya kufanya hivyo aliishaipoteza kwa kuitumia vibaya na kuliacha taifa kwenye zahama ya kiza na kulanguliwa umeme.

Je haya mamilioni anayotoa Lowassa yanatokana na malipo ya marupurupu ya ustaafu anayopewa kinyume cha sheria? Maana, Lowassa hakuwahi kustaafu zaidi ya kulazimishwa kuachia ngazi. Wengi wanashangaa ni kwanini Lowassa anaendelea kutanua bila kufikishwa mahakamani. Pia wengi wanashangaa jinsi CCM inavyomgwaya kiasi cha kumtishiatishia bila kumchukulia hatua. Kuko wapi kutekeleza dhana ya kujivua gamba ambako kumekuwa kukiahirishwa baada ya Lowassa kutishia kumwaga mtama? Je Lowassa kwa kukikamata mateka chama chake na serikali yake anaweza vile vile kuwakamata mateka watanzania akaishia kuwa rais wao hata kama ataingia kwenye vitabu vya historia kuwa anaweza kuwa rais mwenye kuchafuka kuliko waliowahi kumtangulia? Je watanzania ni wa hovyo kiasi hiki? Je wanapopokea mamilioni yake wanategemea kumpa kura wakati ukifika au kuyatumia kama ushahidi kutaka aeleze aliko na alivyoyapata huku pia wakimlazimisha atoe maelezo kuhusu shutuma zake?

Wengi pia wangetaka kuwajua hao marafiki wa Lowassa wenye uchungu na taifa letu kiasi cha kumwaga mamilioni kama wameyapata kihalali au ni watu wa kuaminika au kutisha shaka. Lazima kujiridhisha isijekuwa wananchi na michango ya maendeleo vinatumika kusafishia pesa chafu itokayo kwa magenge ya watu wachafu. Hata hivyo, kwa wanaokumbuka adha alizowasababishia Lowassa kwa kubariki na kuingiza kampuni ya Richmond na hatimaye Dowans, hata awape nini hawawezi kumsamehe. Kwa wanaokumbuka ni mabilioni mangapi ya shilingi yaliteketezwa na mradi huu ambao waziri wa zamani wa Nishati na Madini Ibrahim Msabaha aliwahi kusema ni waziri mkuu yaani Lowassa na mhindi wake yaani Rostam Aziz, hawezi kupumbazwa na misaada ya mamilioni wakati wao walichuma mabilioni ukiachia mbali kuendelea kuchuma ya ustaafu wakati Lowassa hakustaafu.

Kama michango yote ambayo Lowassa ameishaitoa ingefanyiwa mahesabu, ni pesa nyingi kuliko hata mishahara yake yote ya utumishi wake serikalini. Kwa mfano mifano miwili hapo juu ya michango ya Lowassa ya shilingi 120,000,000 ni zaidi ya mshahara wa mbunge wa mwaka mzima. Hapa hajala wala kulisha familia yake kuvaa na kufanya mambo mengine. Kama Lowassa akifanyiwa ukaguzi wa kimahasibu tangu aanze kazi na marupurupu yake yote vikalinganishwa na misaada aliyowahi kutoa na mali anazomiliki itagundulika kuwa maneno ya baba wa taifa yalikuwa ya kweli. Na hivyo, yasipuuzwe wala kusahauliwa hasa wakati huu ambapo nchi inahitaji uongozi adilifu na mpya.

Tumalizie kwa kumtaka Lowassa awataje hao marafiki zake na jinsi walivyopata hayo mamilioni. Lazima tujue kama wanafanya biashara au kazi halali, wakilipa kodi na kama ni watumishi wa umma akiwamo naye na Lowassa, je wametaja mali zao kama wanavyotakiwa na sheria? Kujua ukweli kuhusu jinsi wanavyopata pesa hii wanayotoa kwa jina jema la kusaidia jamii ni jambo jema. Lazima kila kitu kieleweke ili kuepuka jamii kugeuzwa kama fisi kulishwa nyama yake nayo ikaifakamia kwa uchoyo. Ni wakati muafaka kuangalia nani anatoa kuliko kuangalia nini kimetolewa. Hapa tuepuke cha baniani mbaya kiatu chake dawa.
Chanzo: Dira Februari, 2012.

Wednesday, 15 February 2012

Rais huyu mstaafu anatufundisha nini kwa anavyoadhirika?

Nani angeamini kuwa baada ya rais kuitumikia nchi kwa miaka minne na kuweka miundo mbinu ya demokrasia bila kuiba hata shilingi moja angejikuta akifadhiliwa na mama
yake kwenye mabanda? Huyu simwingine bali rais mstaafu wa Sierra Leone, Valentine Esegragbo Melvine Strasser aliyetawala tangia mwaka 1992 hadi 1996 baada ya kunyakua madaraka kwa kuangusha Jenerali Joseph Momoh. Je hali hii inatufundisha nini? Je kwanini tunakuwa wepesi kufadhili mafisadi ilhali tukiwasulubu waadilifu? Huyu angekuwa amekwapua asingeteseka. Je nafsi yake ingekuwa huru? Inachanganya na kukera God knows. Kwa habari zaidi,BONYEZA HAPA

CCM ianguke mara ngapi?

KWA wanaofuatilia taarifa za vyombo mbali mbali vya habari walishtuka kusikia Rais Jakaya Kikwete akinakiriwa akisema kuwa kama Chama Cha Mapinduzi ambacho yeye ni mwenyekiti kinaweza kuanguka kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Wengi walishangaa kusikia kuwa kumbe Kikwete hajui kuwa CCM kilianguka miaka mingi iliyopita sema imeinuliwa na mbinu chafu kama vile kuchafuana mingoni mwao kumpata mgombea wa urais kama ilivyotokea mwaka 2005.

Kitu kingine ambacho inaonekana Kikwete amesahau ni ukweli kuwa CCM kama si kuokolewa na tume yake ya uchaguzi kwa kuiruhusu ichakachue uchaguzi na matokeo yake, ingekuwa historia kama UNIP (Zambia), KANU (Kenya), NP (Afrika Kusini) na MCP (Malawi).

Je, ni kwanini rais wa nchi na mwenyekiti wa chama tawala anakosa habari kama hizi kiasi cha kujua kuwa kumbe chama chake kilianguka miaka mingi tangu kilipobinafsishwa kwa mafisadi na wasanii?

Hivi Rais Kikwete hajui kuwa chama anachokiongoza kilianguka tangu siku kilipozika maadili ya uongozi na kupwakia madili?

Hivi Kikwete hajui kuwa chama chake kilianguka siku kilipotoa ahadi lukuki kisitimize hata nusu?

Hivi kwanini Kikwete haambiwi na washauri wake kuwa CCM kilianguka zama zile kiliporidhia kutumia pesa ya wizi kutoka kwenye taasisi za umma kama BoT (ujambazi wa EPA) kuwahonga wapiga kura na kuchakachua matokeo?

Hivi kweli kujua haya kunahitaji shahada ya uzamivu kwenye masuala ya siasa? Je, Kikwete na wenye mawazo kama yake wanaishi nchi na dunia gani?

Ili kujionea rais anavyoishi kwenye dunia ya kufikirika, hebu angalia nukuu hii iliyomnukuu akipokea maadamano ya kuadhimisha miaka 35 ya CCM huko Mwanza.

Alisema: “Haiwezekani tukaendelea kuwa na watu wa hovyo, lazima chama kijipange na kujiweka sawa ili kisipoteze sifa kwa jamii,”

Hao watu wa hovyo zaidi anayewavumilia ni nani? Kwanini Kikwete awaone hao watu wake wa hovyo leo na si jana alipokuwa akitahadharishwa kuwa chama kinamezwa na mafisadi?

Tungeomba Kikwete atutajie hao watu wake wa hovyo kama kweli ameamua kuwa mkweli badala ya kupiga siasa kama kawaida yake.

Hivi kuna mtu wa hovyo kama aliyeahidi maisha bora kwa Watanzania wote akaishia kuwapa dhidi wote? Hivi kuna mtu wa hovyo kama yule aliyesimama jukwaani mchana kweupe kuwapigia kampeni watu wa hovyo kama watuhumiwa mbalimbali wa ufisadi ambao ni wabunge kwa sasa?

Hebu angalia janja ya Kikwete. “Hivi karibuni nikiwa na NEC hapo Dodoma, nilitumia kauli ‘Nyoka Kujivua Gamba’. Usemi huo ulienezwa tofauti kabisa. Kimsingi tulipitisha maazimio mengi, lakini wenzetu wameona azimio moja tu la kujivua gamba.”

Kuna jambo baya kama kauli hii isiyo na hata chembe ya ukweli? Kwanini Kikwete hasemi ukweli kuwa baada ya kuambiwa kuwa naye ni gamba hakuona haja tena ya kujivua gamba kwa maana aliyepaswa kuvuliwa kwanza ni yeye kabla ya kuwaambia wengine wenye magamba mepesi kujivua magamba?

“Wito wa kujivua gamba haujapewa mwitikio mzuri. Tumetupa mpira huo kwa wanachama kuwawajibisha viongozi hao, maana tunawafahamu. Sasa kazi kwetu sote,” anaongeza Kikwete.

Hivi Kikwete anataka kumdanganya nani kwa kuwatupia wanachama mzigo wakati wanachama walisharidhia vikao vya chama viwawajibishe magamba ambayo hayakutaka kujiwajibisha? sasa ni nini mantiki ya kupoteza pesa ya umma kufanya vikao iwapo jukumu lenyewe liliachwa kwa wanachama wasio na mamlaka yoyote kikatiba kuwawajibisha viongozi wao mafisadi?

Je, huku ni kuchanganyikiwa au kuishiwa kiasi cha kusema vitu vinavyopingana kwenye jukwaa moja na kwa wakati mmoja? Je, hapa wa hovyo ni nani? Nikijibu watasema Nkwazi Mhango siku zote ni mchochezi.

Kwa vile lengo la makala hii ni kutaka kuthibitisha kuwa watu wa hovyo ni viongozi wa CCM, tunatoa nukuu ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, ili wasomaji wapime pale alipokuwa akiongelea tuhuma za kujivua gamba.

Alisema: “Hata Waingereza wana tabia moja. Wakiona jambo linawasumbua, wanaunda Royal Commission, jambo hilo litachunguzwa kwa muda mrefu. Wakimaliza, watu wameshasahau.”

Mukama aliongeza: “Kufukuzana si dawa, si unaona jinsi jamii ilivyowageuka NCCR Mageuzi kwa kumfukuza David Kafulila au kufukuzwa kwa Hamad wa CUF? Sisi tumesema, kufukuzana si suluhisho, utakuwa unashughulikia tu dalili wakati ugonjwa wenyewe haujaufikia,”

Kwanza ni vigumu kuamini kuwa Mukama anaweza kujipayukia bila kujua anachosema ni nini na kinaweza kutafsiriwa vipi.

Sasa kama njama ya CCM ni hii ya kufanya mambo kijanjakijanja ili wananchi wasahau, Rais Kikwete analalamika nini au kutoa ushauri wa nini juu ya kufukuzwa watuhumiwa wa ufisadi. Huu si unafiki? Maana kama uongozi wa juu umeunda CCM royal commission ili kuwasahaulisha wananchi halafu mtu anakurupuka na kusema eti wananchi wataamua, wataamua nini iwapo wakubwa wamekwisha kuamua?

Je, hapa kama wananchi tufuate ya nani hasa ikizingatiwa kuwa Kikwete ana tabia ya kujipinga?

Rejea juzi juzi waziri mkuu Mizengo Pinda na Spika wa bunge Anne Makinda waliporipoti kuwa alikuwa ameidhinisha kulipwa nyongeza ya posho lakini baadaye akawageuka.

Kwa wanaoona CCM inavyozidi kuchanganyikiwa wakati ikipitisha hili na kulipinga hana sababu ya kuhofia kuwa haitaanguka kwenye uchaguzi ujao.

Wakati Mukama akisema hivi vigogo wengine wanasema vile. Hebu tumalizie kwa maneno ya waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye aliyesema sambamba na Mukama: “Hatuwezi kuwa na chama imara kama hatukuondoa magamba, mwenyekiti wetu wa chama taifa lazima tuyaondoe magamba yanayokipaka chama matope.”

Kama kuna kitu kitaiachia makovu ya kudumu CCM si kingine ni dhana ya kujivua gamba ambayo iliuawa baada ya rais mwenyewe kutajwa kuwa ni gamba, tena nene, ukiachia mbali magamba mengine kujua udhaifu wake na kugoma kuachia ngazi kama yalivyotakiwa. Je, kwa namna hii CCM ianguke mara ngapi?


Chanzo:Tanzania Daima Februari 15 , 2012.