The Chant of Savant

Saturday 30 September 2017

Kujenga uzio ni kumaliza tatizo la 'danganyikanite'....?

Watasha husema kuwa ukiwa na nyundo, kila kitu hugeuka msumari. Hivi karibuni walevi walishangilia sana kabla ya kushangaa na kujishangaa baadaye baada ya wataalamu kutoa maangalizo yao. Hii ni baada ya munene kutangaza kuwa kule kwenye machimbo yam awe aina ya Danganyikanite kuzungushiwe uzio as soon as possible ili kupambana na upigaji.  Japo hii ni strategy poa, je ndiyo jibu au jipu wakati wapigaji wengi wanakuwa ndani ya uzio huo huo wakifanya vitu vyao chini ya mgongo wa kuajiriwa? Nani mara hii amesahau wataalamu tuliowaona mbele ya pilato juzi wakishitakiwa kwa kutumia utaalamu wao kuwasaidia wapigaji wa almas kule Maganzo na Mwadui kwa ndugu zangu akina Nkwingwa na Ngw’adira? Je hapa tatizo ni nini? Kwa vile mimi nimesomea masuala ya intelligentsia na usalama, nitatoa angalizo langu la kitaalam.
            Kwanza, unapojenga uzio kwenye kichwa unaweza kudhani kila tatizo linahitaji uzio na si mifumo huru yenye kuweza kuzuia maovu kama vile Katiba Mpya na sheria nyingine. Ndiyo maana unaweza kuondoa wapigaji aina moja ukaweka wapigaji aina nyingine. In simple parlance, kwani hao ndata si walevi? Je mipaka nayo mtaweka nyuzio?  Unapojenga uzio, ni rahisi kuwapa nafasi maadui bila kujua kuwa unafanya hivyo. Mfano, unapoweka watu wako wasioguswa kama vile kibashiteshite, wakiamua kukutumia, na of course lazima wakutumie, unajikuta pakanga bila kutegemea. Muulize mzee Mchonga. Alipotangaza ujamaa, akadhani waliokuwa wamemzunguka walikuwa wajamaa. Kustuka, kumbe alikuwa amezungukwa mbwa mwitu na fisi pamoja na utaua wake usiopigiwa mfano.
            Pili, tunapopanga kujenga uzio, kuna mambo fulani fulani tunayopaswa kuzingatia. Mfano, je upigaji wote husaidiwa na kutokuwepo uzio au husukiwa kwenye ofisi zetu? Nitatoa mfano mdogo kuhusiana na wizi wa fedha ama benki au zinapokuwa zikipelekwa au kutolewa benki. Wapigaji lazima kwanza wawe na mtu wao wa ndani anayewapa data zote ili wapange ni wapi pa kutekelezea mpango mzima.kwa vile benki kuna uzio na vya moto vingi, huwa wanavizia njiani au kuingia kwenye benki wakati ambapo walinzi hawako chonjo au kuhakikisha wenye funguo za sefu wapo ndani ili wakiingia wawateke na kuwalazimisha kufungua sefu.  Mbali ni hiyo, ukitaka kujua namna uzio usivyo big wala real deal rejea namna wanaharamu fulani wa ndani wakishirikiana na wa kigeni walivyoweza kupitisha twiga uwanja wa ndege tena mchana kweupe.
            Ushahidi kuwa uzio si muarobaini uko kila sehemu. Rejea namna wakora walivyofanikisha kuinigiza vichwa vya treni bandarini mchana kweupe na kutoweka. Hapa hujagusia upigaji uliokuwa umetamalaki bandari ambapo scanners ziligeuzwa mapambo. Rejea jinsi bwimbwi lilivyokuwa likipitishwa hivyo kwa staili hiyo hiyo ya kugeuza scanners scammers. Kwani bandari na viwanja vya ndege havikuzungushiwa nyigo? You know what I mean.
            Je kutokana na ukweli kuwa uzio si jibu wala muarobaini, nini kifanyike? Mlevi anashauri mtunge sheria za kiwajibikaji ambapo kila mlevi atapaswa kueleza namna alivyopata ukwasi wake; na kama akishindwa kutoa maelezo, adakwe na kuswekwa ndani huku ukwasi husika ukitaifishwa. Mzee Mchonga aliweza kujenga mashule, hospitali, zahanati na viwanda walivyoharibu waliomfuatia si kwa miujiza bali kutunga sheria na kuendesha mfumo kama huu.
            Pili, jenga mifumo inayoweza kubaini ufisadi ambapo walevi watapewa jukumu kisheria kuripoti kila ukwasi au ufisadi pale wanapoushuku Rejesha kale ka mchezo ka Mzee Mchonga ka kuchongeana unapohgisi kuna mtu anapiga njuluku za umma. Huwezi kuwa na jamii ambayo inaruhusu mlevi kulala maskini na kuamka tajiri ukazuia ukwasi. Kimsingi, rejesha sheria ya maadili ili ipambane na madili ambapo kila mlevi lazima awe anatangaza kipato chake kila mwaka.
            Kukomesha ubishi na kukata mzizi wa fitina, lisilikali liwe na mamlaka na lihakikishe; linawachunguza wafanyakazi wote waliowahi na wanaofanya kwenye sehemu nyeti za upigaji kama vile TRA, viwanja vya ndege, bandarini, mipakani na wizara husika tena wengi walioajiriwa kidugu.
            Mwisho kabisa, wanene wanaposhughulikia kadhia hii ya upigaji, wahakikishe hakuna kulindana kama ilivyotokea kwa wanene waliobariki upigaji kwa miaka mingi wao wakiwa wanatanua ughaibuni au kujitwalia baadhi ya mali kama vile machimbo ya makaa ya mawe ya kule Kiwila kwa akina Twambombo tununu. Pia epuka upendeleo kama ulioonyeshwa kwa baadhi ya watuhumiwa wa kughushi hadi zoezi zima likauawa kwa sababu ya wahalifu wachache wenye connection na wanene kibashiteshite kiasi cha kutoguswa. Kwa leo naishia hapa. Kama ni msaada nimewapa bure.
Chanzo: Nipashe J'mosi leo J'mosi.

Friday 29 September 2017

Picha ya wiki: Aliyeko juu mngoje chini

Watuhumiwa wa uchotaji wa fedha za umma kwenye akaunti ya Escrow Habinder Singh na James Rugemalira wakirejeshwa korokoroni kungojea upelelezi wa kesi yao ukamilike. Ama kweli aliyekojuu mngoje chini. Baada ya tawala fisadi zilizopita kuwakingia kifua, sasa wanalipia taratibu madhambi yao.

Wednesday 27 September 2017

The s-called Unknown people must be made known


Tanzania, recently, has been grappling with the wave of the fear of the unknown after a faceless gang of terrorists inflicted pangs, twangs and sufferings on some innocent people. The hell broke loose when unknown outlaws made an attempt oft the president of Tanzania Legal Society (TLS) Tundu Lissu who also is the Member of Parliament (MP) for Singida East (CHADEMA) two weeks ago in Dodoma. Lissu was spurted with bullets to end up being deadly injured. He is currently undergoing treatment in Nairobi.
Interestingly, while these delinquents unleashed their terror, the authorities seem to still be in a slumber.  The major question many are asking is: Is it true that these outlaws are not known really? How in the country with all security instruments such as police, army and Tanzania Intelligence and Security Services (TISS) aka Usalama wa Taifa. Although, this can be taken as a normal criminal wave, there is something fishy and giddy so to speak. How come that such cowards and misfits are able to hold a country to ransom for a long time as the authorities stay side and watch? 
The story of the heinous and horrendous acts by these outlaws is disgustingly long; and the list of the victims of this fraidy-cat gang of goons and crooks is very long to include the massacre of Professor Juan Mwaikusa, Dr. Sengondo Mvungi and Ben Saanane whose plight, up until now, has never been known due to the fact that the authorities have always been tightlippped. This gang o unknown yardbirds once abducted Dr. Steven Ulimboka the former chair of Medical Association of Tanzania (MAT) in 2012, Absalom Kibanda, former chair of Tanzania Editors’ Forum (TEF) as he then was in 2013, rapper Emanuel Elibariki aka Ney wa Mitego in 2017 and this gang of cowards and criminals attacked the president of Tanzania Legal Society (TLS) and the MP for Singida East, Tundu Lissu whose car was sprayed with bullets in early September this year.
When it comes to these unknown morons, one thing is known that they are after the critics of the government. So, their aim is clear. Now, when known becomes unknown, there is a very big problem. Again, in this situation, the problem is very small. The unknown is known save that we are not ready to admit. I will tell why the unknown is known though not to all. Firstly, though such predacious criminals are referred to as unknown people, it is the duty of the authorities to make them known so that they can be dealt with and disposed as soon as possible.
Secondly, it doesn’t make any sense even to a common tweeker for a country that has gotten all sorts of security institutions to be cowered and bamboozled by a gang of the so-called unknown sons of bitches.  Why? It is simply because some people, especially their victims know them. This means the authorities know them just because when the victims reported these misfits disclosed who they actually are. Some of the victims reported to the authorities provided the colour and the plate numbers the vehicles these criminals use. This said, therefore, everything is known save that we don’t want to know even if some of us know everything.  We need to arrest this menace before people lose it and take law into their hands shall the authorities keep on losing out on public security.
The other day a friend of mine told me that these criminals are known. For, if you look at their victims, you can easily tell who these criminals are. He wondered what would have happened had say Tundu Lissu been an MP for the ruling party. Fool me once, shame on you. Fool me twice, shame on me. We should not allow a next victim to follow after Lissu. If we do, shame on us. We need to do something toothsome for ourselves as a people.
Source: Citizen Wed., today.

Tuesday 26 September 2017

Miaka miwili bila Mtikila

Image result for photos of mtikila
            Alipofariki mchungaji Christopher Mtikila aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha Democratic Party (DP) sikupata fursa ya kumwandikia wasfu au kumbukizi. Huwa sipendi kuandika wasfu au ombolezo tokana na athari zake kwangu binafsi hasa inapofikia mtu ninayemfahamu. Huchelea kumsifia sana au kumpunja kwenye yale anayostahiki katika maisha yake.  Hata alipotimiza mwaka mmoja tangu afariki, sikufanya hivyo. Mwaka huu nimeamua kuvunja mwiko.  Hakunaubishi kuwa Mtikila alikuwa mwanasiasa wa aina yake linapokuja suala la kupigania haki za wanyonge tena bila kutetereka ukiachia mbali wakati mwingine kusababisha utata.
            Sasa ni miwili tangu nguli Mtikila atuondoke ghafla tokana na ajali ya gari iliyoacha utata iliyotokea Oktoba 4, 2015. Hivyo, tarehe 4 Oktoba Mtikila anatimiza miaka miwili kamili tangu atutoke.  Sikungoja tarehe kamili aliyotutoka Mtikila. Nimeona niandike kumbukizi hili wiki mbili kabla ya tarehe kamili tokana na sababu nyingi. Mojawapo ikiwa ni kushambuliwa na kuumizwa vibaya kwa mheshimiwa Tundu Lissu anayeonekana kuibuka na kuvaa na kutosha viatu vya Mtikila. Kwani, ukiondoa Mtikila, hakuna mwanasiasa anayeisumbua serikali kama Lissu. Pia hakuna mwanasiasa anayakamatwa na kukabiliwa na kesi nyingi zisizo na kichwa wala miguu zaidi ya Lissu.
Hata hivyo, kabla ya mwisho mwa uhai wake kuonekana kama kupunguza makali yake kisiasa kiasi cha baadhi ya watu kujenga dhana kuwa alikuwa amelishwa kitu jambo ambalo sijui kama lina ukweli. Hata hivyo, Mtikila atabaki kwenye historia ya taifa letu kama mtanzania aliyepigania mageuzi si ya kisiasa tu bali hata ya kisheria. Mtikila anakumbukwa kama mwananchi na mwanasiasa aliyefungua kesi nyingi dhidi ya serikali kandamizaji na kuiangusha mara nyingi tu.
            Nilimjua Mtikila mwishoni mwa miaka ya 80 pale kwenye bustani za Mnazi Mmoja alikopenda kupitia na kusikiliza vikundi mbali mbali vya watu waliokuwa wakibishania mambo mbali mbali ya dini, siasa au masuala mengine waliyoona kama yanastahiki mjadala. Mara chache Mtikila alikuwa akichangia kwa utulivu na hoja nzito; na mara nyingine akiiteka midaharo pale. Mara nyingine akiishia kutazama na kusikiliza bila kuchangia. Mbali na hapo, Mtikila alikuwa jirani yangu maneo ya Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko.
            Pamoja na kufahamiana na kuonana mara kwa mara, hatukutokea kuwa marafiki wa karibu kiasi cha kutembeleana au kukutana zaidi ya kukutana kwenye hadhara mara kwa mara. Kuna wakati tulitofautiana hapa na pale bila kujenga ukaribu wala umbali wala uhasama.  Tulibakia kujuana. Mara ya mwisho, nilikutana na Mtikila alipoamua kumvaa waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye akimtuhumu kujitwalia ardhi ya umma. Nilihudhuria mkutano wake na waandishi wa habari wakati nikiwa Habari Corporation; na huo ukawa ndiyo mwisho wa kukutana kwangu naye. Kwani, baadaye niliondoka nchini. Hata hivyo, nakumbuka; ni Mtikila huyu aliyeitisha maandamano makubwa Jangwani ya kupinga magabacholi kukalia taifa letu. Nilishiriki maandamano hayo yakiwa ni ya kwanza na ya mwisho kwangu hasa baada ya kuonja joto la mabomu ya kutoa machozi.
            Tukirejea kwenye mchango mkubwa na usio na kifani kwa Mtikila kwenye mageuzi ya Tanzania, sijui kama ni wengi bado wanamkumbuka na kumuenzi kama  inavyostahiki hasa kutokana na kujitoa kwake mhanga wakati wengi walikuwa wakiigwaya serikali. Mtikila alijigeuza ghafla kutoka kwenye kuwa mchungaji na kuwa  sauti ya wasio na sauti. Tofauti na wachungaji wa aina yake ambao wengi uchungaji au uaskofu wao hakutokana na mifumo iliyozoeleka, Mtikila hakujiingiza kwenye biashara ya neno la Bwana na kuwa tajiri wa kutisha kama wenzake tunaoshuhudia wakinuka ukwasi na kuhubiri siasa nyuma ya madhabahu kwa kuigopa serikali. Yeye alijitokeza moja kwa moja na kusema wazi alivyokuwa mwanasiasa mchungaji na si mchunaji anayejikomba kwa au kutumiwa na wanasiasa kama ilivyo sasa. Pamoja na elimu yake ya kadri, Mtikila hakujipachia vyeo vikubwa vya udaktari pamoja na kuwa na uwezo kiakili wa kuendana na sifa hii. Pi aliogopa kujiita askofu au nabii. Alibakia mchungaji na ariridhika na nafasi hii. Ni bahati mbaya kuwa ni wachache waliofuatilia na kuiga mfano wake hasa wakati huu ambapo dini, sawa na siasa, imegeuka biashara kubwa karibia sawa na mihadarati.
            Hivyo, binafsi naandika waraka huu lau kumuenzi mpiganaji huyu bingwa wa Ukombozi ambaye historia sahihi ya mageuzi Tanzania haiwezi kukamilika bila kubeba jina lake. Hakuwa mwoga wala mtu wa kunyamazishwa kirahisi. Alisema ukweli kama alivyouona bila kujali nani ageudhika au kuufurahia.
            Kwani, naona kama nina deni kwa nguli huu wa kupigania haki za wanyonge bila woga wala kuoneana au kupendeleana.
            Nilimjua kama mtu aliyekuwa na uwezo mkubwa kiakili hasa akiwa bingwa wa kujenga na kubomoa hoja. Nilimjua Mtikila kama mtu asiyepindisha mambo wala kuteteleka pale alipokuwa akisimamia jambo aliloliamini. Unaweza kusema kuwa staili ya upiganiaji haki wa Mtikila ilihitaji kile ambacho baba wa taifa Marehemu Mwl Julius Nyerere aliwahi kukiita moyo wa mwendawazimu au the courage of the mad kitu ambacho ni alama pekee ya mpambanaji asiye mchumia tumbo.
            Sasa imepita miaka miwili tangu Mtikila aondoke. Hatarudi. Japo kimwili ameondoka, mchango wake utakuwa nasi milele. Kumtendea haki Mtikila, tunapaswa kama taifa kutomsahau. Tumuenzi lau kama ishara ya kutambua mchango wake kwa taifa letu hata kama alikuwa upande wa pili.
Chanzo: Tanzania Daima J'tano leo.

Kijiwe chamuunga mkono Dk Kanywaji Magu

Image result for photos of mererani
            Baada ya Kijiwe kurejea toka Nairoberry kumuona Tunduni Lissu ambaye kwa sasa, si haba na alhamdullillahi, anaendelea vizuri, kilifarijika kusikia kuwa lisirikali limeamka usingizini na kuamua kuweka uzio kwenye machimbo ya bongonite kule Mererani.  Pia kijiwe kilifarijika kusikia kuwa lisirikali lina mpango wa kuntibia Tunduni; hata kama ni kwa kusuasua na kuchelewa baada ya kupima upepo wa walalahoi na kugundua wanampenda na kumuona kama shujaa wao baada ya Chris Mtikisa (RIP).
            Mpemba anaingia akiwa na bashasha tofauti na wiki zilizopita alipokuwa akiingia akiwa amenuna na kukasirika tokana na mwanakijwe mwenzetu kumiminiwa mvua ya shaba. Anaamkua na kuoda kahawa yake na kulianzisha “yakhe mwasemaje kuhusiana na hii amri ya kujenga uzio kuzungushia machimbo ya bongonite kule Nrerani?”
            Kabla ya kuendelea Kanji anamkosoa na kusema “veve Pemba kwanini naharibu Swahili kama hindi? Kule naitwa Rerani siyo Nrerani.” Kijiwe hakina mbavu kwa namna anayemkosoa mwenzake anavyokosea tena zaidi.
            Mbwamwitu anaamkua kumkosoa Kanji “duh! Hii kweli kali. Sasa Kanji unachokosoa nini kama nawe unarudia makosa tena zaidi? Nadhani kule kwaitwa Mererani na Rerani. Hiyo Rerani nadhani iko Bobei lakini si Daganyika dugu yangu.”
            Mpemba akiwa anatabasamu anarejea “hakuna alokosea baina yangu na Kanji hasa ikizingatiwa kuwa kila ntu ana lafudhi ya kwao. Mie ndhani sasa tujadili hili la kulinda utajiri na raslimali za taifa badala ya raslimali za lugha na matanshi yake. Basi mie nshauri tudurusu hii amri alotoa rahis ya kuzungushia wigo maeneo yenye madini yetu.”
            Msomi aliyekuwa akisoma jarida moja kubwa la kigeni anaamua kula mic mapema ili kuokoa mjadala usirejeshwe kwenye utani. Anakwea mic “Mpemba una hoja hapa. Ni kitendo cha maana kuzugushia wigo kwenye eneo la Mererani. Hata hivyo, nina angalizo. Je hili ni jibu? Mbona bandari imezungushiwa wigo na mipaka imejaa mageti lakini mali zetu zinapitishwa na taifa linakula hasara? Nadhani badala ya kujengwa wigo kwenye machimbo ambalo ni jambo safi, tungeanza kujenga wigo kwenye vichwa na mioyo ya watumishi wanaoajiriwa kwenye maeneo nyeti kama haya.”
            Kabla ya kuendelea Kapende anamchomekea “duh! Msomi kweli wewe si wa kawaida! Wachovu wengi waliposikia wigo walisherehekea kiasi cha kupofuka wasijue kuna mianya mingine mawe yanaweza kuibiwa.”
            Kabla ya kuendelea Msomi anampoka mic na kuendelea kudema “ni kweli usemayo. Kawaida wengi huwa na kupelekwa na matukio kiasi cha kushindwa kuyaongoza. Sina ugomvi na ujenzi wa wigo ingawa utatumia fedha nyingi ambayo kama tungekuwa na mifumo ya kupambana na wanaotuibia huenda zingetumika vinginevyo kama vile kuweka mitambo isiyochezewa ya kielektroniki au kuongeza magereza ya kuwafunga wanaotuibia. Nadhani tungetunga sheria kali dhidi ya wezi wa namna hii na kuunda mfumo usiochezewa, ingekuwa bora kuliko nyigo hizi.”
            Mijjinga napoka mic na kuronga ‘usemayo Msomi ni ukweli mtupu tena ya maana. Hata mimi nadhani, tungewekeza kwenye usalama kwa kuwaangalia watendaji wetu wa kwenye maeneo ya madini, viwanja vya ndege na mipakani. Tutatejenga ukuta kuzuia wezi. Je tumeimarisha ulinzi kwenye mipaka yetu kupambana na utoroshaji wa madini na uingiaji na utokaji wa hovyo wa wakimbizi wa kiuchumi?”
            Kabla ya kuendelea, Mgoshi Machungi anakula mic “Mijjinga nakubaiana nawe sawa na Msomi. Hatiwezi kutegemea kuta kia sehemu. Hemu fikiia. Kama twiga waisafiishwa mchana tena kupitia airport na si uchochoo wa mpaka, huu wigo kwei utawazuia wanaotiibia mawe yetu? Kwanini tisitunge sheia ya kuwanyonga watakaopatikana na kuiba mawe yetu ii wanaopanga kufanya hivyo waogope au wajue kinachowangoja?”
Da Sofia Lion aka Kanungembe anakula mic “kaka Mgoshi umenikuna kweli kweli.” Kabla ya kuendelea Mchunguliaji anamchomekea Sofi “dada utani huu mbaya. Eti amekukuna? Amekukuna wapi na vipi ili tujue?”
            Sofia naye hamkawizi anajibu “unataka ujue ili iweje. Ili akukuna nawe siyo kaka yangu?”
            Kabla ya kuendelea Mchunguliaji anachomekea haraka “Da Sofi tuheshimiane tafadhali.”
            Sofia anajibu “kweli dawa ya moto moto. Hivyo ndiyo ninavyokuheshimu kulingana na namna ulivyotumia hilo neno lako na kulielewa visivyo.”
Kabla ya kuendelea Mipawa anaamua kuokoa jahazi. Anazoza “jaman utani tuache kwenye mada serious kama hii hata kama tunahitaji kutaniana basi tuvumiliane au siyo jamanini? Ingekuwa bora kumpa fursa dada Sofia naye aelezee anachodhani kifanyike kuboresha ulinzi wa mawe yetu au siyo?”
            Sofia anakamua mic “kaka umenena. Huyu kazoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi na isitoshe mkuki kwa nguruwe. Hayo tuyaache. Mie nadhani sirikali iongeze bidii katika kudhibiti utajiri na vipato vya wafanyakazi wake. Tumeishapiga kelele tukitaka irejeshwe sheria ya maadili ambapo kila mwanakaya anapaswa kujaza fomu ya mapato yake kila mwaka. Baada ya hapo lazima turejesha mfumo wa kupelelezana na kuripotiana. Nadhani hili ni muarobaini kuliko wigo wa mabilioni. Je hao wanageshi tunaowaweka siyo waja wenye udhaifu wa vishawishi au tunajeshisha kaya?”
            Kabla ya kujiwe kuendelea si tawi la mti likakatika tukatawanyika bila kumaliza mada!
Chanzo: Tanzania Daima J'tano leo.

Sunday 24 September 2017

Somo toka shambulizi dhidi ya Lissu


            Kwa wenye busara kila tukio ni darasa. Tukio la kinyama na kishenzi dhidi ya rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mbunge wa Singida Mashariki Mheshimiwa Tundu Lissu, kadhalika, nalo lina somo kwa Tanzania kama taifa na jamii ya watu. Katika makala ya leo, safu hii itadurusu masomo tunayoweza kupata tokana na kitendo hiki cha kipuuzi na kipumbavu.
            Kwanza, hata kama ni kwa kusuasua na kuchelewa, tunapongeza azma na tamko la serikali la hivi karibuni kuwa itamtibia Lissu popote pale duniani kama yatatafsiriwa kwa vitendo. Hata hivyo, umma unahoji, kwanini serikali imechukua muda mrefu kufikia hatua hii muhimu kana kwamba Lissu si mtanzania na kiongozi.  Japo inaweza kuwa si kweli au kweli, wapo wanaoona kama kuwa kuna upendeleo katika kuhudumia viongozi wetu. Wanadhani; kama Lissu angekuwa mbunge wa upande mwingine, huenda serikali isingechukua muda mrefu kufikia msimamo huu mpya. Hata hivyo, tunaipongeza; na kuishauri, ijifunze kutokana na udhaifu huu. Maana, leo ni kwa Lissu. Kesho hatujui litamtokea nani. Tunasema haya kutokana na uzoefu kuonyesha kuwa kuna viongozi wengi ambao wameishatibiwa nje tena kwa haraka na wakiwa hawako kwenye hali ya kutisha kama aliyokuwa nayo Lissu kabla ya kukimbizwa Nairobi anakoendelea na matibabu.
            Pili, tukio hili limechafua sifa ya Tanzania ya kuwa taifa la amani, sifa ambayo tumeijenga kwa gharama kubwa na kwa muda mrefu lakini sasa inaondolewa na wapuuzi na wahalifu wachache.  Tumechafuka mbele ya mataifa. Kitendo hiki cha kinyama kimelaaniwa dunia nzima kiasi cha jumuia ya kimataifa kuanza kuiangalia Tanzania kwa macho tofauti na ilivyokuwa. Gharama ya unyama huu kwa taifa si ndogo. Kwani, wenzetu sasa wanatuona kama taifa lisilo na amani wala usalama; jambo ambalo lina athari zake kijamiim, kisiasa na kiuchumi. Sijui kama kuna mtu nwenye fedha zake na akili zake atataka kuwekeza kwenye taifa ambalo watu wake na viongozi wake hawako salama.
            Tatu, tukiachia mbali mateso na mahangaiko anayopitia Lissu na familia yake,  kitendo hiki kimehujumu jimbo lake na taifa hasa ikizingatiwa kuwa Lissu ni mwakilishi wa jimbo na kiongozi mkubwa wa kisiasa na kisheria nchini.
            Nne, tukio hili limeonyesha udhaifu wa polisi wetu. Rejea ukweli kuwa Lissu alitoa ripoti si mara moja wala mbili kuwa alikuwa akifuatiliwa na watu ambao walikuwa wakitishia uhai na usalama wake. Kuonyesha ukweli wa madai ya Lissu, polisi waliyapuuzia hadi lilipotukia shambulizi. Hali hii inaondoa imani ya umma kwa jeshi lao la polisi jambo ambalo si jema. Kwa wenye kufanya maamuzi ya haraka, wanaona kama linashiriki au kubariki jinai hii.
            Tano, ukiliangalia shambulizi dhidi ya Lissu kiuchumi, unagundua kuwa hawa wauaji wamelisababishia taifa hasara kijamii, kisiasa hata kiuchumi. Mfano, tujiulize, fedha ambayo imeishatumika kumtibia Lissu ingetumika kujenga vyumba vya madarasa au kununua dawa kwenye zahanati zetu zisizo na madawa ingejenga au kunuua dawa kiasi gani?
            Sita, ukiangalia kadhia hii kwa Lissu na familia yake, ni muda na fedha kiasi gani wameishatumia ukiachia mbali kukwamisha maisha na shughuli zao za kawaida. Hapa hatujagusia mateso ya kisaikolojia familia inapitia bila kusahau maumivu na mateso anayokabiliana nayo mgonjwa. Lissu ni binadamu lakini si wa kawaida. Mchango wake kwa taifa na familia yake ni mkubwa tu. Kama baba, ni kiasi gani watoto na mkewe wanateseka ukiachia mbali ndugu na jamaa wanaomtegemea? Kama mbunge, ni huduma kiasi gani jimbo lake linakosa hasa kipindi hiki cha bunge? Kama wakili, ni watu wangapi wanakosa huduma yake? Kama mkereketwa, taifa linapata hasara kiasi gani kwa kukosa ushauri na mawazo yake kama mbunge na mtaalamu wa sheria? Kimsingi, hasara ni nyingi na kubwa kuliko tunavyoweza kufikiria.
            Saba, kama taifa, kitendo cha kinyama alichofanyiwa Lissu kinapaswa kutuzindua toka kwenye usingizi na ulevi wa amani tulivyokuwa navyo kwa muda mrefu. Kwani, hadi sasa, hatujui nani walifanya unyama huu na kwanini. Hivyo, basi, kama taifa, tunapaswa kuwasaka hawa wauaji na kuwashughulikia kwa mujibu wa sheria ili kurejesha imani mbele ya mataifa na watu wetu. Kwa hali ilivyo, na kutokana na mambo yanayofanywa na serikali ya rais John Magufuli ambayo, bila shaka, ina maadui wengi, hasa wale ambao ulaji wao umeingiliwa, kuna uwezekano kitendo hiki kikafanywa na maadui wa taifa ili kuichonganisha serikali na watu wake ukiachia mbali kuichafua kimataifa. Hivyo, nyavu za kutafuta wahalifu hawa zinapaswa kuwa pana sana. Ukiachia mbali maadui wa serikali, pia wapo watu wanaopenda kujipendekeza wanaoweza kufanya kitendo hiki kwa vile wanamuona Lissu kama adui wa serikali. Rejea kilichotokea hivi karibuni ambapo gazeti fulani lilifungiwa kwa miaka miwili kutokana na kutumia maneno ya rais kuelezea kilichotokea. Je waliochukua hatua hii waliangalia upande wa pili na athari za hatua zao?
            Tumalizie kwa kusema tu; shambulizi dhidi ya Lissu ni somo tosha kwa jamii, nchi na watu wenye kufikiri sawasawa hasa kama tutaangalia upande wa pili wa madhara kuliko malengo ya wauaji hawa. Hatutaki kunyosha vidole. Ila serikali isikwepe kuwajibika kutokana na ukweli kuwa jeshi la polisi lilizembea kwenye wajibu wake mkubwa wa kulinda watanzania na mali zao. Tunamtakia Lissu apone haraka; na taifa lijifunze tokana na kilichomsibu.
Chanzo: Tanzania Daima J'pili leo. 

Saturday 23 September 2017

Long live African kings

Mlevi kupambana na watu wasiojulikana

            Baada ya watu wasiojulikana–au tuseme wahalifu wanaojulikana- wakajjficha nyuma ya kutojulikana tokana na ushamba na ujinga–wamekuwa tishio kayani. Kwanza, sidhani kama kuna watu wasiojulikana wanaoweza kuishi kwenye kaya inayojulikana tena yenye kujisifia kwa kuwa na vyombo vya usalama vyenye kuaminika kiasi cha wakubwa kuwahakikishia walevi kuwa wasiwe na wasiwasi juu ya usalama wao kana kwamba hawa wanaoshambuliwa si raia wa kaya hii. Kaya yoyte ikifikia mahali kama hapa ambapo wahalifu wachache, tena wasiojulikana kuiteka, uje kuna tatizo kubwa tu. Sijui usalama wa kaya kama unaweza kutolewa kafara hivi. Je ni kwa faida ya nani na ili iwe nini kama siyo aina nyingine ya ulevi tena mbaya kuliko wa kanywaji? Hawa watu wasiojulikana wanajulikana. Mheshimwa Tunduni Lissu anawajua; n ahata wahishimiwa wabunge waliofuatiliwa nao wanawajua tu.  Hivyo, wanajulikana; na kila kitu kinajulikana hata wale wanaowatuma wanajulikana. Kama hawajulikani basi wao wanajijua.
            Juzi walevi walinisonga na mawazo wakitaka kujua geshi la nini kama wahuni wachache wanaotumia fursa zao vibaya kwa kuwaumiza hata kuwaua wenzao? Je ndata nao ni wa nini kama wanashindwa na wahalifu na washamba wachache tena wasiojulikana? Basi hata dingi hana sababu ya kuwapo akilipiwa kila kitu wakati kila kitu kimekaa ndivyo sivyo kuhusiana na usalama wa walevi. Walevi wanataka usalama wa uhakika; na kuwaumbua hawa wahalifu wanaojifanya hawajulikani.
            Hawa watu wanajulikana; si mazombi, wala popobawa wala maruhanni. Ni wahalifu, ni washamba, ni wauaji, na yote katika yote, ni washenzi wanaopaswa kutokomezwa kama ndui. Hivyo, wasiendelee kujificha kwenye kutojulikana wakati wanajulikanaau kuvimbisha bichwa kuwa wataendelea kutojulikana. Kwani zimepita tawala ngapi kaya hii? Mbona wakati wa mzee Mchonga hatukuwasikia wala waliofuatia hadi juzi tu?  Kwa vile mimi nimesomea usalama, nitahakikisha nawafichua na kuwaumbua ili wale wanaodhani hawajulikani wajue wanajulikana. Mlevi lazima niwasake na kuwafanyia kitu mbaya tena nchana kweupe. Kitu ya kwanza, nitawasaka mama zao kwanza. Pili, nitahakikisha nawaumizia watu wao kama wanavyoumiza wapendwa wa wengine ili wajue na kuona inavyouma. Haiwezekani tukakubali kaya yetu igeuke kaya ya maimla, wasanii na wababaishaji wanaochukia wenzao kwa vile wanajua uovu na ushenzi wao. Tunduni hivi kosa lake nini zaidi ya kuzoza ukweli? Nani anaweza kuua ukweli akafanikiwa. Unaweza kuchelewesha ukweli kujulikana; lakini huwezi kuua ukweli. Ukweli ni kama mada, hauawi wala kuumbwa. Ukweli ni ukweli na utabaki kuwa ukweli iwe ni kwa shari au kwa heri.
            Inashangaza kusema kuwa kuna wahalifu wasiojulikana wakati waliomuonyesha cha moto Nape Mapepe wanajulikana; sema ndata waliogopa kuwakamata kutokana na kutojua nani aliwatuma kutaka kutenda unyama ule.  Walisahau kuwa wale waliomwonyesha cha moto Mapepe wanaunganishwa na yule aliyekuwa akitaka kushuhgulikia jinai yake na yule aliyempuga haraka haraka ili asiweze kumuumbua mshenzi mwenzake. Sasa mimi nasema. Hawa wajalaana wanajulikana na sababu ya kutenda jinai bila kukamatwa zinajulikana. Mbona watu wasiojulikana waliosumbua walevi wa Rufiji walijulikana na kufutiliwa mbali?  Hivi unataka kuniambia hawa jamaa wangekuwa wanatishia maisha ya wenye kaya wangeendelea kutojulikana kweli?
            Hivi waliowateka akina Dk Steve Ulimboka, Absalom Kibanda, Romania Mkatoliki, na wakampoteza Ben Saanane eti bado hawajulikani kweli? Hivi waliomwagia shaba Tunduni hawajulikani kweli? Hivi waliolipua ofisi za wakili anamofanyia kazi wakili wa Tunduni kweli hawajulikani? Kweli waliompoteza Ben Saanane hawajulikani kweli?  Hawa watu wasiojulikana wana lisirikali ndani ya lisirikali au ni siri kali ya lisirikali?  Yaani ndata wetu na uzoefu wao wamezidiwa ujanja na watu tena wachache wasiojulikana au kuna namna kama si nkono wa ntu?
             Kwanini hawa wasiojulikana wanapambana na wale wanaoonekana kuwa mwiba kwa wenye ulaji wanaoonza kuugeuza urithi? Hivi kweli waliovamia Klauds hawafahamiki an wanaowakingia kifua kwa vile wanatumiana hawajulikani kweli? Basi majini. Basi semeni majini na si watu wasiojulikana wakati wanajulikana. Naona yule anatikisa kichwa. Kama unadhani kawaulize akina Tunduni na wahishimiwa wengine waliowahi kufuatiliwa na ndinga hilo la watu wasiojulikana. Mbona wahishimiwa akiwamo Tunduni walishataarifu ndata kila kitu wasichukue hatua tokana na kuwajua wahusika kuwa hawajulikani na wakijulikana lazima uwaite wasiojulikana wakati wanajulikana.
            Nimalizie kwa kuronga; hawa watu wasiojulikana wanajulikana. Kama hawajulikani kwa walevi, kwa Mungu wanajulikana. Pia, kama umma wa walevi tukiamua wajulikane watajulikana tu. Hivyo, tusitishwe na kivuli cha kutojulikana, wanajulikana na watajulikana japo wapo wanaotaka wasijulikane; ila wajue watajulikana kama wanavyojulikana ingawa twaambwa hawajulikani wakati wanajulikana.
Chanzo: Nipashe J'mosi leo.

Wednesday 20 September 2017

Will the world let Qatar be bullied?


           A few days ago, Tanzania had some explanations to make vis-à-vis ties with North Korea.  I think; this is because our country is not an island when it comes to how it functions in the international community. This has forced me to look at another conflict in the Middle East between Qatar and the Quartet of Bahrain, Egypt, Saudi Arabia, and the United Arab Emirates (UAE).  For some past months, a wealthy country of Qatar has been involved in the tussle with its gulf neighbours. Due to this conflict, the quartet severed diplomatic ties with Qatar after accusing it of supporting terrorist groups the allegations Qatar sturdily denies.
          Essentially, the ongoing Qatar-Gulf- Arab-nations conflict is not a good thing for both Qatar and its neighbouring adversaries. So, too, this conflict is likely to negatively impact on other countries in the region and in the world in general. After this conflict simmered; and came to the surface, the quartet issued some conditions to Qatar among which were the closure of an international media outlet, Al Jazeera; suspension of relationship between Qatar and some countries aggrieved countries view as the enemies of the region; and making sure that Qatar is audited by these countries vis-à-vis its compliance with their demands. Those who know and appreciate the freedom of press and the great role the Al Jazeera has played in the modern world in information dissemination, will never understand the rationale of closing it down.
            First of all, the Al Jazeera has not only open Qatar for the world but also the entire region; which is good for all countries in the region.
            Secondly, the Al Jazeera is an independent media group that is supposed to be left alone to do its business peacefully and professionally as it has been doing since its inception.
            And thirdly, there is no way foreign powers can dictate Qatar’s political life so as to choose friends for it not to mention deciding what is wrong or not for it. This is colonialism; even if it committed by neighbouring countries. Qatar is a sovereign country whose sovereignty is sacrosanct under the international laws.
            Luckily however, Qatar decided to stand its ground and resist this bullying behaviour its neighbours are exhibiting. For, many of the conditions set do completely violate the sacrosanctity of Qatar’s sovereignty.
            Apart from severing diplomatic ties with Qatar, the quartet also decided to close their borders, waters and skies for Qatar which is strange and unfeasible in dealing with the conflict positively. As the conflict drags on, it will play in the hands of the enemies of the region. What is obvious is the fact that regional, international competitors and enemies will like to take advantage of the existing impasse.
Fundamentally, there is no winner in this conflict except the enemies of the countries involved in this imbroglio. If there are winners in this conflict are none other than Iran and Turkey whose leverage in Qatar is likely to grow and glow provided that they will stand by their friend, Qatar at the hour of need; which is natural. Geostrategically, these gulf nations need to think out of the box as far as the conflict is concerned.  
The nature of regional realpolitik shows that Qatar will win big provided that many countries will sympathise with it due to the size and nature of demands its adversaries want it to succumb to or comply with. In June, the quartet offered Qatar a period of ten day to meet their demands. Since then, Qatar has never bowed; and it still soldiers on three month down the line. If all parties stand their ground to see to it that their demands are met by either of the side, chances of losing it are high. Qatar will never sacrifice its sovereignty as any country could do. Arguably, the quartet has to tone down their pressure; and abandon some of its demands shall it want to resolve this conflict constructively and positively. There is no reason for neighbours to shun each other and expect to do well in all aspects of their lives.
In a nutshell, parties to this conflict need to understand that the world does not look at; and into the conflict they are into with the same lens and intentions. The US provides a very good example; it refused to side with any of the parties to conflict. This means; the US as well as the international community see some elements of bullying in the conflict. Therefore, my advice to the parties to this conflict is: Sit on a roundtable and iron out your differences; otherwise, the world will never side with any bully in this conflict at hand.
Source: Citizen Wed., today.

Wilaya ya Ilala isiwaonee ombaomba


            Hivi karibuni rafiki yangu alinitumia kipande kilichorekodiwa cha tangazo la wilaya ya Ilala likiwataka wananchi kutotoa fedha kwa ombaomba wala ombaomba kuomba; na watakaokiuka watachukuliwa hatua za kisheria. Tangazo hili, kwanza lilinishangaza; na pili lilinisikitisha kutokana na sababu zifuatazo:
            Mosi, kwanza, hakuna sheria kama hiyo. Nadhani mtoa tangazo ima hajui sheria au anajifanya kutojua sheria hasa anaposema kuwa suala hili litashughulikiwa chini ya sheria ndogo ndogo ambazo hazina nguvu zinaposimama dhidi ya sheria mama yaani katiba ambayo haisemi kuomba kihalali ni kosa.
            Pili, ni ile hali ya baadhi ya watawala wetu kukurupuka na kushupalia mambo madogo wakati makubwa wakiyaacha au kuwashinda. Hivi kweli ombaomba ni tatizo sawa na mafisadi au wahalifu ambao kwa sasa wamepewa cheo cha watu wasiojulikana? Hivi ombaomba ni tatizo kubwa kuliko uchafu, uzembe, ukahaba na ulevi na kadhia nyingine kwa wilaya ya Ilala?
            Tatu, kwanini wilaya ya Ilala imeona ombaomba kama tatizo kubwa kuliko mengine mengi inayokabiliana nayo kama vile uingiaji wa wahamiaji haramu uliotamalaki nchini hadi wengine kufikia kuendesha biashara bila leseni wala vibali ya kufanya kazi wala kuishi nchini?
            Nne, je wilaya ya Ilala ina habari kuwa taifa lao nalo ni ombaomba? Rejea wakati wa utawala uliopita ambapo rais mstaafu Jakaya Kikwete alilalamikiwa sana na kusifiwa kwa kuzunguka dunia akiomba misaada huku serikali yake ikizembea kiasi cha kuacha madini na raslimali nyingine nyingi zenye thamani kubwa kuliko pesa ya kubomu vikiibiwa kila uchao. Rejea kutoroshwa kwa wanyama hai tena mchana kweupe ukiachia mbali madini yetu yenye thamani ya mabilioni. Hapa hatujaongelea viwanda bubu ambavyo vingi vinamilkiwa na wageni au wahamiaji haramu kama alivyowahi kubaini mkuu wa wilaya ya jirani ya Temeke hivi karibuni.
            Tano, hivi wilaya ya Ilala haijui sababu ya kuwa na raia ombaomba nchini? Tumegusia baadhi ya maovu kama vile ufisadi, wizi wa fedha za umma, uzembe, ubinafsi na ulevi wa madaraka. Nadhani ni mlevi wa madaraka anaweza kuona ombaomba kama tatizo kubwa kuliko ufisadi tokana na ukweli kuwa wengi wa ombaomba wetu wamezalishwa na mipango mibovu ya serikali zetu ukiachia mbali ufisadi uliozalisha watendaji wa umma wanaotumikia wezi wa nje na ndani kwa kuwauma watu wetu na raslimali zao. Rejea namna ambayo rais John Magufuli anavyohangaishwa na ufisadi kiasi cha kuogopa hata kusafiri nje. Rejea kufichuka kwa wizi mkubwa wa madini ya dhahabu kwa njia ya makinikia ukiachia mbali wizi wa almas na tanzanite.
            Sita, je wilaya ya Ilala inaendeshwa kwa sera zipi wakati serikali yake inaongoza nchi ombaomba kimataifa? Au ni yale ya nyani haoni nonihino lake au ile ya mwenye shibe hamjui mwenye njaa?
            Saba, ukiachia nchi kuwa ombaomba wakati ina raslimali lukuki, kuomba si kosa kisheria wala kimaadili. Kuomba kunakoharamishwa ni kama vile kuomba rushwa iwe ya fedha au ngono au upendeleo. Je hii jinai ya kuomba rushwa nchi ikoje? Kuomba ni haki ya binadamu hasa anapokuwa na tatizo ambalo hawezi kulitatua. Ndiyo maana watu hufurika makanisani na misikitini kuomba kila siku. Ukiachia mbali kuomba kuwa si kosa kisheria sawa na mengine tuliyoeleza, hata nchi tajiri na zilizoendelea bado zina ombaomba na haziwabughudhi kwa kujua kuwa kuomba si kosa; na baadhi ya ombaomba wanazalishwa na sera mbaya za serikali au nchi.
            Nane, je nini kifanyike?
            Nashauri wilaya ya Ilala na wengine wenye mawazo kama haya, kwanza wajikite kwenye kuokoa, kusimamia na kulinda raslima za umma ili kupunguza umaskini ambao ndiyo mzazi wa ombaomba wanaokimbia maisha magumu vijijini tokana na kutokuwa na elimu, ujuzi wala mitandao ya kuwawezesha kupata kazi na kuishi maisha mazuri. Sijui kama kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kupenda kuomba au kukuonea fahari.  Kama nchi haioni aibu kuombaomba, itakuwaje wananchi wake tena wasio na raslimali sawa nan chi?
            Pili, nashauri wilaya ya Ilala itafute njia za kukuza uchumi kwa kupambana na vipingamizi kama vile wahamiaji haramu, ufisadi, wizi wa fedha za umma, ufujaji wa raslimali na mali za umma.
            Tatu, simamieni ukusanyaji wa mapato ili muwe na kipato cha kutosha kiasi cha kuanzisha miradi ya kupunguza vijana wasio na kazi na wengine wenye uhitaji kwenye eneo lenu badala ya kutoa amri za ajabu ajabu msijue zitawageuka.
            Mwisho, kabla ya kufikiria achia mbali kutangaza kuwafukuza ombaomba, mfikiri mara mbili. Je ombaomba wanatokana na nini? Je nyinyi si sehemu ya tatizo? Je mwaweza kuwa sehemu ya suluhisho? Je kuzuia wananchi kutoa fedha yao kwa wanaowaonea huruma mnadhani kuna nguvu kisheria kama mnavyotishia? Hata nchi yenyewe inapewe misaada na yeyote anayeionea huruma bila kutenda kosa lolote. Sasa kama nchi yenye kujaliwa kila aina ya raslimali ikazivuja ukiachia mbali kuwa na vyanzo vingine inaomba, itakuwaje mwananchi wa kawaida? Fikiri mara mbili.
Chanzo: Tanzania Daima J'tano leo.

Kijjiwe kwenda Nairobi kumjulia hali Lissu

        
            Baada ya mwenzetu kufanyiwa kitu mbaya na mahabithi wanaoitwa watu wasiojulikana wakati wanajulikana, tuna mpango wa kutuma wajumbe kwenda kumjulia hali kama mchango wetu na kuunga mkono jitihada zake za kupigania haki za wachovu.
            Kapende anaingia akiwa na gazeti lenye picha ya Tunduni Lissu.  Anatusomea kichwa cha habari “sasa Tunduni anaanza kupata nafuu na wanaomtakia mabaya yawapate wao na wake zao au waume zao na watoto familia ndugu jamaa na marafiki zao huku yakiwaacha maadui zao.” Hata kabla ya kuendelea anatokwa jasho huku akihema utadhani katoka kwenye nyumba inayoungua moto.
            Kabla ya kuendelea Msomi Mkatatamaa anaamua kuingilia kati huku akitabasamu na kuhoji “mheshimiwa Kapende hebu nipige darasa la bure. Kweli hicho ni kichwa cha habari au ni kichwa chako? Maana sijawahi kuona kichwa cha habari kama hicho.”
            Kapende anatabasamu na kuzoza “Msomi umeninasa.  Ni kichwa cha habari. Sema nimeongeza na yangu ya kichwani. Hivyo, unaweza kusema ni vichwa vya habari. Lakini hata hivyo si ujumbe umefika kuwa nina maya na wanahizaya na wajalaana waliommiminia shaba shujaa yetu?”
            Mgoshi Machungi anachomekea “hata ingekuwa mimi tingeongeza. Maana hii kitu aiyofanyiwa huyu shujaa inanifanya nitamani kumpiga mtu zongo. Hivi hii kaya inakwenda wapi; au tiseme inapeekeshwa wapi wagoshi? Maana tangu shujaa afanyiwe huu unyama, siikai haionyeshi kustuka waa kutaka kutoa maeezo ii tiandastandi na kuchangia kibidi. Je kunani nyuma ya pazia au kwa vie Tundi Issu ni mpingaji?”
            Mjjinga anakamua mic “Mgoshi jibu unalo. Unadhani angekuwa mwishiwa wa chama twawala hawa wasiojulikana, japo wanajulikana, wangekuwa bado mitaani wakitanua na kula walichopewa kufanya unyama huu ambao siku moja utaumbua hata wale ambao hukutegemea?  Huoni hata watajwa kwenye ujambazi wa almas akina Andru Chenga na Bill Ngereza bado wanaengwaengwa badala ya kuonyeshwa mlango. Heri watu wasiojulikana, wangekuwa wazalendo, wangehangaishwa na hawa mafisadi wakubwa na wenye roho mbay. We acha tu. Nina hasira kiasi kwamba nikipata hawa wasiojulikana naweza kuwabaka hadharani, sorry, kuwafanyia kitu mbaya ili wakawaambie mama zao na wake zao kama wao warume kweli.”
            Bi Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kumpinga Mijjinga “kaka sasa unakwenda kubaya. Unadhani kuwanonihino ni suluhu au msaada kwa mhanga? Nadhani tuwabane wahusika wawataje hawa wanaowajua na kuwaita watu wasiojulikana. Sasa kama wahalifu kama hawa tena wajinga, washamba, na wapumbavu wanaweza kufanya unyama wasijulikane, hao wenye mamlaka wanatawala nini? Je wao ni salama? Au wanangoja yawafike kama si wao watu wao. Ukipanda mbigiri, utavuna mbigiri si maua.”
            Mpemba anaamua kula mic “Yakhe acha da Sofia nami nkuchomekee ashakum si matusi; nadhani wanipata.  Kama yupo awezaye kuwapata hawa watu wasiojulikana waniotaka ua wenzao, dawa yao ni kuwaua vivo hivo walivotaka kunnua Tunduni.  Hapa lazima niseme ukweli lazima tufanya haq bin haq. Untoboa mato nkutoboa mato; hiyo ndiyo haki.”
            Kanji anaamua kutia guu “mimi dugu yangu hapana taka shari vala vunja seria. Lakini kama nafikiri juu ya hii vatu vasivojulikana nafanyia Tunduni, kama napata yeye nafanya kitu baya hata kama baka yeye dugu zanguni hapana sikia baya bali raha. Sasa kama navwanga risasi mingi kama naua jini sisi fanya nini? Kama natoboa roho ya Tunduni, vapi baya toboa yeye.”
            Kijiwe hakina mbavu hadi da Sofia mshirika wa Kanji anaziba uso huku akiangua kicheko tokana na Kanji anavyobukanya uswa na kutishia kumwaga radhi.
            Mbwa Mwitu anauliza huku akicheka “Kanji veve iko taka toboa nani na vapi na kvanini dugu yangu kama iko fuata seria?”
            Kanji hajivungi; anajibu ‘Kama Tunduni iko dugu yako va damu navezasema hii neno nasema sasa au tafuta hii vatu vasivojulikana na kufanya kitu baya navo iumie kama Tunduni naumia yeye na family yake?’
            Mheshimiwa Bwege aliyekuwa kimya akiangalia anaamua kutia guu “wakati mwingine kijiwe hiki kinashangaza. Kila anayeongea anatamani. Kwanini msifanye kweli; kama noma na iwe noma? Kila anayeongea anatamani kuwafanyia kitu mbaya hawa malaya wa kisiasa. Mara natamani niwabake; mara niwafanyie kitu mbaya; mara hiki; mara kile. Sasa mimi nasema. Hivi kuua na kubaka ni lipi kosa kubwa zaidi?  Basi kuanzia leo nasema wanakijiwe kuondoa dada yangu Sofia, tuwatafute hawa wahalifu tuwabane ili waweze kuonea aibu ubakaji wa kaya wanaotaka kuutekeleza kwa kutaka kuua watu wasio na hatia. Hapa hakuna kuwaangalia nyani usoni. Hii kaya ni yetu wala siyo  ya mama zao.”
            Kiiwe kikiwa kinanoga si likapita gari jeupe aina ya Nissan! Kama siyo mwenye gari hili kujiwahi na kutoka nje na kusema yeye tumtazame na anajulikana, huenda tungemnyotoa roho tusijue kuwa kumbe ndata walikosea kusakanya ndinga zote zenye rangi sawa na lile la watu wasiojulikana. Sijui kwanini hawakutaka kulifuatilia kwa namba walizopewa na wahanga!
Chanzo: Tanzania Daima, J'tano leo.

Sunday 17 September 2017

Watu wasiojulikana: Barua ya wazi kwa rais Magufuli

Image result for photos of unkown people
            Ndugu rais John Joseph Pombe Magufuli,      
            Naamini u mzima wa afya na unaendelea na majukumu yako ya ujenzi wa taifa kama raia na rais wa Tanzania. Leo, kwa mara nyingine nimeamua kukuandikia waraka mwingine. Si mara yangu ya kwanza wala ya mwisho kufanya hivyo. Leo naomba kwa taadhima nijielekeze kwenye jinamizi lililokumba taifa letu linalosababishwa na wale wanaojulikana kama watu wasiojulikana. Watu wasiojulikana wameliteka taifa kiasi cha kuanza kuwa na sifa mbaya kimataifa. Swali la kwanza, ningependa kujua, nini msimamo wako kuhusiana na kadhia hii ambayo inaonekana kuwachanganya wananchi tokana na kukosekana tamko rasmi la serikali ukiachia mbali kueleza ni mikakati gani inafanywa kuliangamiza kundi hili la washenzi na wauaji wasiojuliana kabla halijaliangamiza taifa kwa kuamsha chuki na hasira zinazoweza kusababisha vurugu kutokana na hisia kuwa kuna ubaguzi, upendeleo na uonevu?
            Ndugu rais, nadhani, kama raia na rais wa nchi, hii mambo ambayo yameishatendwa na wahalifu hawa yako mezani kwako kama siyo kwenye mitandao na vyombo vyako vya dola. Ajabu ya maajabu, hawa wanaoitwa watu wasiojulikana, kuna baadhi ya watu wanawajua lakini hakuna vyombo vya dola vimefanya jitihada za kutaka kwuajua na kuwaweka wazi baada ya kuwafungia korokoroni.  Kuna wahanga ambao wameishatoa taarifa polisi kuhusiana na watu hawa kuwafuatilia lakini hakuna hatua zilizochukuliwa. Wa kwanza kutoa taarifa hizi ni baadhi ya wabunge waliohisi kuna gari lenye watu wasiojulikana waliokuwa wakiwafuata.  Hapa sijaiongelea watu ambao wameishaumizwa kwa kutekwa na kupatikana baada ya kuteswa. Kinachoshangaza na kustua ni ukweli kuwa  kama wabunge wanafuatiliwa na kutishiwa maisha yao na hakuna anayejali, je hao raia wa kawaida walalahoi  na kajamba nani yakiwakuta hali itakuwaje? Je kwanini tunaruhusu hofu ianze kutawala nchi yetu? Ni kwa nini na kwa faida ya nani?
            Ndugu rais, waheshimiwa wabunge waliotoa taarifa kuhusiana na watu wasiojulikana kuwafuatilia walitoa namba za gari lao na hata rangi ya gari. Ajabu ya maajabu, si polisi wala nani alikuwa tayari kuongelea angalau hata kulaani watu hawa wasiojulikana ambao uharifu wao unajulika nchi nzima. Sijui ukimya huu unaisaidiaje serikali? Sijui hata mantiki ya jeshi lenye kila zana, hadi sasa, kushindwa kuwakamata watu tena wachache wasiojulikana. Je ni kweli hawa watu hawajulikani? Kama nchi yenye vyombo vya usalama inaweza kuwa na watu wasiojulikana, hili hakikisho la usalama wetu kama wananchi ni la nini?
            Ndugu rais, kama kiongozi wa nchi, naandika kukutaarifu na kukuomba uchukue hata ili hawa wasiojulikana wasijevuruga nchi na kuufanya uongozi wako uonekane umeshindwa kulinda usalama wa taifa ukiachia mbali kushindwa na genge la wahalifu tena wanaojifanya hawajulikani wakati wanajulikana.
            Pili, umekuwa ukihubiri amani, na upendo nchini ukihimiza utendaji haki bila ubaguzi. Juzi juzi mheshimwa mbunge Tundu Lissu wa CHADEMA alivamiwa na hawa wanaojifanya kutojulikana na kummiminia risasi mchana kweupe. Ajabu ya maajabu, hadi leo, polisi bado wanasuasua. Hatuoni mikakati ya kuwasaka na kuwakamata hawa watu wasiojulikana. Hili llimewashanga na kuwatia shaka na uchungu wengi kuona mwenzao na kiongozi wao anamiminiwa risasi na hakuna anayejali.
            Ndugu rais, wengi tunajiuliza tena kwa mshangao na uchungu: Huku kuwatumikia watanzania bila kujali tofauti zao kuko wapi iwapo inapokuja kwenye kuwakamata akina Lissu, Halima Mdee na Godbless Lema wote wabunge wa upinzani, hatuoni polisi kusuasua. Ajabu ya maajabu na kituko ni kwamba polisi wana muda wa kuwamata watajwa kwa vitu visivyokuwa na kichwa wala miguu lakini wanashindwa kuwasaka watu wasiojulikana. Je hapa kunani? Wapo wanaohoji kama kweli Lissu angekuwa mbunge wa chama tawala, hawa watu wasiojulikana wangefumbiwa macho au kushughulikiwa taratibu kama ilivyo? Wengi wananahoji, huo usawa mbele ya sheria na kupata hifadhi kutoka katika jamii viko wapi au ni maneno ya jukwaani?
            Ndugu rais, yalipotokea mashambulizi na mauaji kule Kibiti, polisi walichakarika kweli kweli na hatimaye kuyakomesha. Je inakuwaje watu wasiojulikana wanaendelea kuchezea nchi kana kwamba wana serikali yao ndani ya serikali wakati watanzania wanajua kuna serikali mbili tu ya Magufuli na ya Zanzibar?
            Ndugu rais, sitaki niseme mengi. Ninachojua ni kwamba mataifa yaliyoishia kwenye machafuko yalianzia huku tuliko. Haiwezekani watu wasiojulikana, iwe ni kwa kutumwa, kujituma au kujipendekeza waendelee kuonea watu wasio na hatia umma unyamaze. Lazima umma utataka kuwajua na kuwatia adabu kama mamlaka zitaonyesha kushindwa kufanya hivi.  Nisingependa taia letu lifike kule kana kwamba lina ombwe la uongozi. Hawa wahuni na mabwana zao wanapaswa kusakwa na kuteketezwa haraka kabla hawajakuchafulia jina. Tuondoe taifa letu mikononi mwa wahalifu wanaojificha nyuma ya kutojulikana. Tuepusha ukatili na mauaji vinavyoanza kuathiri sifa nzuri ya taifa letu ukiachia mbali kutishia mustakabali na usalama wa taifa.  Watanzania wanangoja tamko, uongozi wako na suluhu juu ya kadhia hii itokanayo na ukatili, ushamba na upumbavu wa wote walioko nyuma ya ujambazi huu.
Kila la heri.
Nkwazi Mhango
Chanzo: Tanzania Daima J'pili leo.