The Chant of Savant

Monday 31 March 2008

EPA: This is white washing, witch hunting and ping pong

The East African March 17, 2008 has it that the government of Tanzania has issued an international prohibitory notice stopping the sale and transfer of properties bought by Tanzanian firms and individuals suspected to have obtained money fraudulently from the external payment arrears (EPA) account of the central bank. Kudos and bravo with all bravadoes shall you mean the biz.

Looking at it at the face value, one would think: now the government is at last at work! come on folks. What must be done is not to issue this prohibitory notice or whatever it is but to arraign the culprits in the first place shall the government be serious and genuine in this.

I thought. What would come first, shall common sense be employed, would be the arrest of the culprits who are still sashaying in our streets driving their oil-guzzlers as they head for their King-size mansions.

They are still dining and wining in our expensive hotels. Indeed they are but still free bin-Adams amidst us. What is the government waiting for? Arrest them first and others will follow if indeed you are serious.

This braggadocio reminds me of the fanfaronades during the Chavda saga. We were told: Chavda would end up in the gaol. Did he go there? Thubutu. He was given his carte Blanche and hit the road to Bombay to enjoy his loot.

Show me anyone behind the bars I shall give you the cow that I inherited from my father. Who is sullying who and who are these bloody thieves who seem to be the government with another? Why is the government catching a cold foot when it comes to arrest these mega thieves?

Is the government waiting to witness what happened in Urambo whereby the offended Wananchi torched the houses of corrupt officials? Though this may be regarded as an unthinkable reminiscent to big thieves in upper echelons of powers, times are changing. People, tired of this dirty game, may wake up and punish the culprits extemporaneously. So shall we invoke common sense, for the security of culprits and our money, culprits need to be behind the bars as soon as possible.

I know this is difficult. For in our country, mega thieves are rewarded thanks to their big brains that enable them to rake billions whilst the Mlalanjaa is dying in penury unnecessarily.

If I were JK, I would have no mercy with anyone who is implicated in wrong doings. I still can’t understand why the government is lax and is ready to take heat for the crimes committed by others! How does it benefit from these scams so as to become a sacrificial lamb of mega thieves?

The so called international prohibitory notice may end up being taken and used as a loop for the culprits to salvage their loots and get away with it. What will the government tell us shall this happen? Let the government be warned. Letting the culprits free is but regarded as abetting with them to commit even bigger crimes as far as money changing hands and destroying exhibits are concerned.

If at all the names of the culprits are known even to a dove, then what are we waiting for? Are we waiting for roman soldiers who arrested Jesus to come and help us? Guys stop fooling us. Arrest these big freebooters as soon as possible before we burst with angers.

By the way, how far has the government gone as far as bringing back the chief architect of EPA profligacy, Daud Ballali? The last I heard of the saga was to the effect that the US authorities were waiting for the formal application from the government of Tanzania to effect the arrest of the bum. Good job for keeping mum but…

Another point, white washing is not the venue of the government that has all sorts of investigation's organs under its disposal.

Wizi EPA ni mkubwa kuliko tunavyoambiwa

GAZETI la ‘The East African’ la Machi 17, 2008 lilifichua kuwa serikali ilitoa waraka maalumu wa kuwatahadharisha na kuwazuia watu kununua mali za watuhumiwa na wanufaika wawili - Johson Lukaza na Beredy Sospeter Maregesi - wa wizi wa fedha kutoka kwenye mfuko wa madeni ya nje (EPA).

Bahati mbaya taarifa hizi hazikueleza kama watuhumiwa wamekamatwa au la.

Inavyoonekana watuhumiwa hawa wanaotambulika hawajakamatwa kwa sababu taarifa hii ya serikali inaonekana kuwa kimya, kuhusiana na kukamatwa kwa watuhumiwa hawa. Sababu? Serikali pekee na wao ndiyo wanaojua!

Hapa ndipo utata wa ‘seriousness’ ya serikali unapozidi kujitokeza. Je, hawa nao ni serikali ndani ya serikali au ni serikali sirini? Kuna nini hapa?

Kama kuna jambo linangojewa na Watanzania wenye mali, basi si jingine bali kuwaona wahalifu hawa wakiwa mbele ya vyombo vya sheria ili haki itendeke na ukweli ujulikane.

Taarifa zilizotolewa zilibainisha wazi kuwa watuhumiwa wana mali zenye thamani ya fedha zipatazo dola 20,000,000 nchini.

Kama Lukaza na Maregesi wana mali za dola 20,000,000, je, hao mabosi wanaofichwa waliowatumia kutenda jinai hii kwa taifa wana utajiri kiasi gani?

Na kama wameweza kuwekeza kiasi cha dola 20,000,000 je, wamefuja au kuficha kiasi gani? Maana, kuna uvumi kuwa mmoja wao amewahi kuagiza gari la thamani ya dola 200,000 kutoka Uingereza na kulipakiza kwenye ndege kutoka London hadi Dar.

Huyu hawezi kutumia shilingi mbili kwa siku. Lazima atakuwa ni mtu wa matanuzi na hatari kwa pesa. Pamoja na muda aliokaa bila kubainika, si bure pesa nyingi itakuwa imeshafujwa, kiasi cha kuwezesha mhusika kuozea gerezani kama haki itatendeka na kuonekana ikitendeka.

Je, ni kwa nini serikali imekamata mali za watu wawili tu kati ya wengi?

Dola 20,000,000 ni asilimia 15.037 ya pesa zilizoripotiwa kuibwa kwenye fuko la EPA, nashindwa kukubaliana na takwimu zinazotolewa.

Haiwezekani watuhumiwa, tena wadogo wawili, wawe na utajiri mkubwa kiasi hiki. Hii maana yake ni kwamba kama vidagaa waliotumiwa na wakubwa kuiba wana utajiri wa dola 20,000,000 basi waliowatumia wanaweza kuwa na hata mara kumi yao.

Hapa ndipo madai kuwa pesa iliyoibwa inaweza kufikia hata dola 800,000,000 na pengine zaidi ya hapo unapoanza kuwa na mashiko.

Kuna haja ya kujua idadi ya watuhumiwa na pesa waliyochukua kila mmoja, ndipo ukweli uwekwe wazi.

Hata ukizigawanya pesa hizi dola 133,000,000 tulizoambiwa kuwa ndizo zilizoibwa kwa makampuni uchwara yaliyotajwa 22 unazidi kupata shaka.

Je, wana mali kiasi gani zilizo nje ya nchi au ambazo hazijafichuka? Je, ni mali kiasi gani zimo mikononi mwa ndugu zao? Kuna maswali mengi yasiyokuwa na majibu. Wahusika si wapumbavu. Hizi mali zilizofichuka zaweza kuwa ‘tip of an iceberg.’

Kama watu wadogo kiasi hiki wana utajiri wa kutisha kiasi hivi, hawa kina Meremeta, Deep Green Finance na wengine wanao husishwa na vigogo walikwapua kiasi gani?

Kukadiria ni kiasi gani, rejea pesa iliyotumika kwenye takrima nchi nzima kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 unaohusishwa na wizi huu.

Kama watu wageni wa pesa kama hawa wana utajiri kiasi hicho, hawa wenye Kagoda wana utajiri kiasi gani? Na Jeetu Patel atakuwa na utajiri kiasi gani?

Bado hawa si wezi wenyewe, bali vyambo vilivyotumika kuvua mabilioni haya kwa ajali ya mpango maalumu wa watu maalumu. Nadhani hapa ndipo serikali inaposhikwa na kigugumizi kusema ukweli ni upi na walioko nyuma ya wizi huu ni kina nani.

Wakati Rais Ali Hassan Mwinyi akiondoka madarakani mwaka 1995, dola moja ya Kimarekani ilibadilishwa kwa takriban sh 520 za Kitanzania. Angalia Mkapa anaondoka ameiacha wapi? Ilikuwa imezama kwa takriban asilimia 50.

Je, kwa serikali iliyokuwa inajisifu kuleta nidhamu ya matumizi na makusanyo, kwa nini iliporomosha shilingi yetu badala ya kuipa thamani zaidi ya iliyoikuta nayo? Hapa ndipo sanaa ya kutoa taarifa safi kwenye makabrasha wakati nyuma ya pazia mambo ni tofauti, inapowafumba macho wananchi wasijue ukweli na kuchukua hatua madhubuti.

Hapa ndipo Rais mstaafu Benjamin Mkapa anapopaswa kubanwa atoe maelezo ya ‘tambo’ zake za kufufua uchumi na kubana mfumko wa bei. Kama alifanikiwa kubana mfumko, alifanya hivyo si kwa kuzalisha bali kubana mzunguko wa pesa. Huu nao ni usanii.

Kashfa ya Goldenberg nchini Kenya ilikula takriban dola 200,000,000 na nchi ilinusurika kidogo kufilisika. Ikumbukwe Kenya ilikuwa na uchumi imara na mkubwa kuliko wetu. Sasa kama Tanzania haijafilisika inaendeshwa kwa muujiza upi?

Baya zaidi, tunaambiwa uchumi umeimarika. Lakini wakati tukiambiwa hivyo, tumeonywa: hali za maisha zitakuwa mbaya. Sasa nini ishara na faida za kukua kwa uchumi kama si kuboresha hali za wananchi? Hiki nacho ni kitendawili kinachotaka kutenguliwa na wachumi ili umma uelewe sanaa unazotembezewa.

Tanzania ina kila sababu za kuwa muflis. Taarifa zisizo rasmi ni kwamba serikali inamiliki mashangingi zaidi ya 6,000 yenye thamani ya zaidi ya dola 30,000 kila moja. Haya ni magari yanayokula mafuta sana (gas guzzlers).

Gharama ya kulitunza shangingi moja kwa mwaka nayo si haba. Kulitengeneza na kulilisha mafuta si mchezo. Bado hatujaja kwenye kufuja rasilimali za nchi kama nishati, simu na fedha maofisini ambako kumegeuka vijiwe vya kupigia stori na soga na serikali isifanye kitu.

Bado hatujaangalia posho na malipo kwa watu wanaokwenda kazini kupiga siasa au soga waliotamalaki nchi nzima. Bado hapa hatujaingiza matumizi ya matanuzi ya watawala ndani na nje ya nchi. Bado hujagusa kashfa nyingine kubwa zinazohusisha pesa nyingi kama Richmond, Independence Power Tanzania Limited (IPTL) na nyingine nyingi tu.

Tujiulize, kwa nini serikali inapata kigugumizi kuwataja watuhumiwa wote wa ufisadi tata wa EPA? Kwa nini serikali haiwasilishi ombi rasmi kwa mamlaka za Marekani kumrejesha Dk. Daud Ballali, gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mwasisi na mtuhumiwa nambari wani wa kadhia hii? Je, wanaomzunguka Dk. Ballali kama mkewe waliotajwa kuhusika na kadhia hii wako wapi na mbona serikali haielezi kinachoendelea?

Je, hapa mchawi wetu si huyu tuliyempa mtoto alee ilhali tukijua atamnyonga na kumla kama ambavyo inajionyesha kwenye kashfa ya EPA?

Siku zote serikali inasema ipo madarakani kwa ajili ya umma. Hata katiba yetu viraka inasema hivyo. Mbona linapokuja suala la kutwambia ukweli inatuficha? Huku kuwajibika kwa wananchi ni kupi na kutaanza lini?

Wapo wanaomhusisha Rais Jakaya Kikwete na uchafu huu kutokana na kuwa mnufaika na aliyekuwamo kwenye serikali chafu ya Mkapa. Bahati mbaya naye ameshikwa na kigugumizi. Amebakia kuja na ahadi za nitawakamata wapi kama na yeye anahusishwa?

Rejea ile ‘List of Shame’ iliyotolewa na wapinzani mwaka jana na ikabainika kuwa kweli baada ya serikali kujaribu kuua madai yao bila mafanikio.

Pia kuna jambo linashangaza. Kwa mfano, kwa nini Gray Mgonja, mtuhumiwa kwenye wizi wa EPA, bado yumo madarakani huku watuhumiwa wengine kama Johnson Mwanyika, Mwanasheria Mkuu wa Serikali; na Edward Hosea, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru); nao wakiendelea kushughulikia suala ambalo wana maslahi nalo?

Hapa si siri, kinachochezewa ni sisi na rasilimali zetu. Ajabu, nasi tumeendelea kumuunga mkono Rais awashughulikie watuhumiwa wakati naye ni mtuhumiwa. Kwa nini hatoi utetezi wala maelezo kama kweli si mtuhumiwa au hakushiriki?

Kimsingi kadhia nzima ya EPA ukweli bado haujajulikana. Hivyo ni jukumu letu wananchi kuusaka ukweli hadi tuupate utuweke huru.

Source: Tanzania Daima Machi 30, 2008


Maoni ya Wasomaji

nashangaa sana kuona watz tumekaa tu hatuandamani kuuliza ya hapo juu wakati maisha yetu ni magumu ile mbaya

na k - 30.03.08 @ 09:36 | #4116

mpayukaji kaweka mambo yote hadharani kazi kwetu watanzania,kila mara nasema wakati wa kuongea umeshapita,na sasa kilichobaki ni vitendo,mana hawa mafisadi wanafurahi na kuzidi kutuibia baada ya kuona hatusemi lolote,siku zote madarasani tunaanza na theory halafu practical,sasa watanzania wakati wa theory umepita tuanze practical ili wale wote wanaoiba waone ya kua watu wameamka,ila cha ajabu ambacho hadi leo sijapata jibu ni kwamba,2010 watakuja hawa mafisadi kwa maneno matamu na watapewa tena nchi,sasa sijapata jibu ya kua fulana na kofia na wali kwenye kampeni ndio vinawachanganya watu ama ni ushabiki tu,mana wengine ukiwauliza wanakupa majibu ya kipuuzi sana,kwamba kikwete ndio anafaa na hakuna mwingine anaeweza kuongoza,siku zote mtu km hapewi nafasi tutabakia kusema hawafai mpk mwisho wa dunia,na mwingine akasema kikwete anafaa sababu ni handsome huyu dada alinipa wakati mgumu sana kuamua nilie ama nicheke,ila mwishoni nikasema MUNGU atusaidie watanzania,ila tusikate tamaa tuendelee kuwasomesha ndugu zetu km hawa ili wasituletee viongozi km hawa tena,naamini hata MUNGU atakua anajisikia vibaya sana,kwani katuma akili na nguvu ila tunashindwa kuvitumia na kubaki kumsingizia na kumalaumu kua ndio kaleta umaskini wetu wakati tunaona na kujua kabisa wanaoleta umaskini wa watz ni watu wachache tena tunaowajua,sasa mtu ana utajiri wote huo wkt sumve huko hakuna zahanati,na wkt huohuo tunamkamua mwananchi ambae anaishi chini ya dola 1 kwa siku achangishe shule,jamani hii inakaaje.

na mstari wa mbele, calif/usa, - 30.03.08 @ 10:05 | #4124

sasa ni nani wa kulianzisha maana sisi tunasubiri mtu wa kuanzisha tu halafu nasi tuliendeleze nyie mnaoandika siyo mtuandikie tu,tuelelezeni na mahala pa kupata silaha sisi kwa sasa tuko tayari maana kama ni kufa tulishauawa sasa tutachoogopa ni nini tumechoka na longo za serikali

na mulokozi, tanzania, - 30.03.08 @ 11:55 | #4156

mimi ni koplo kwa cheo ila kwa habari zinazoandikwa na mambo tunayoyashuhudia sasa imefika mahala hatutasikiliza habari ya nani maana sasa mambo yanayofanywa na serikali yanatukatisha tamaa na hata kama sisi ndiwo walinzi wa amani pia hatuhitaji amani ya kutufanya sisi wajinga na hatuwezi kukubali kama hivi serikali inamuachia mtu mmoja tu tena mgeni huyu anayeitwa azizi amechukua hicho kiasi cha pesa bilion 200 halafu sisi tunateseka na watoto wetu pa kulala hakuna elimu ya watoto wetu ni duni sasa tunacholinda hapa tanzania ni nini?MUDA SIYO MREFU TUTALIANZISHA NA BAADA YA HAPO NDIPO TUTAHESHIMIANA

na koplo john, tanzania, - 30.03.08 @ 12:04 | #4158

serikali isitufanye wajinga tunachosubiri sasa hivi ni mtu wa kuazisha tu na baada ya hapo hawa mafisadi wote watakiona maana serikali imeshindwa kuwatia adabu kwa hiyo ni muda sasa warudishe mastaka kwa wenye nchi yao ambao ndiyo sisi wananchi hasira tuliyo nayo kwa sasa ni kubwa iliyovuka mipaka VIONGOZI GANI HAWA WANAKULA HAWASHIBI?!!!!

na chacha, tanzania, - 30.03.08 @ 12:12 | #4159

Naamini njia muafaka ya kuiwajibisha serikali kwanza ni kwa kura kwa kipindi kijacho cha 2010. Ila kwa sasa njia ya haraka ili hali isifikie katika vita kati ya uongozi wa serikali wakitumia vyombo vya dola dhidi ya wanachi wenye machungu, nivyema kama wapo wanasheria wazalendo wenye uchungu pia swala hili likachukua mkondo wa kisheria,maandamano ya amani, migomo ya nchi nzima na mashinikizo kwa kupitia vyama vya upinzani taasisi huru za kijamii,taasisi na mashirika ya kidini na wafadhili wa nje na mabalozi. Naamini kwa kutumia massmovement ya namna hii tunauwezo wa kuishinikiza serikali hii ambayo wengi wetu tumeiweka madarakani kuachia ngazi mara moja! La basi tuko radhi kutoa uhai wetu kwa kizazi kijacho kama ikibidi kua hivyo...Mungu aepushe hilo kwa mapeozi yake.

na Mtz pure, Hillbrow. Joberg. RSA, - 30.03.08 @ 13:01 | #4161

SIKU INAKUJA.........., nayo ipo!!!,chezeni tu

na imani - 30.03.08 @ 14:32 | #4178

Big up mulokozi, mesema sahihi, wewe koplo nakuunga mkono, silah atatupa huyo koplo hapo juu inaonekana yuko tayari na yuko upande wetu.

nchi hii tupigane kidogo baada ya hapo heshima itakuja , MAANA HATA SASA WATU WANAKUFA SANA HILA SIO KWA VITA, NA TUSPICHUKUA HATUA WATAENDELEA KUFA, AFADHALI TUPIGANE KIDOGO TUZUIE VIFO VYA KUDUMU MAHOSPITALINI, JELA, MASHULENI, WAMACHINGA nk....................Afande ebu weka e-mail yako hata kama si ya jina lako sahihi tuanze vuguvugu hili.

na yoooooooo - 30.03.08 @ 14:53 | #4182

Sasa naona pameanza pambazuka nchi hii. Kwa mawazo haya naona Tz yenye neema ya kweli iko malangoni. Makala zenye kuibua hisia mwanana na za kiukombozi namna hii zidumu luliko Chama Cha Mafisadi (CCM). Tuwafundishe watz ukweli huu kwa nguvu zetu zote ili kwanza waichukie CCM na serekali yake alafu tuone kama kuna mtz atauliza afanye nini. Tukisema tungoje 2010 hawa mafisadi na tume yao ya ubaguzi watajihalalisha tena kuendeleza sera zao za kutufisadi kiakili, kiuchumi na kiutamaduni, sisi na vizazi vyetu.

na emmanuel, songea, - 30.03.08 @ 15:40 | #4188

Kwanza ningependa kujua kama Prof Semboja, Prof Matamballya, kama wachumi, Prof. Haroub O, Prof Kabudi, wanasoma haya maandishi? Mimi sioni jumuiya ya wasomi inafanya chochote kuamsha na kuipa jamii uelewa wa kutosha kuhusu fani walizoshikiria. Ninavyofahamu Jumuiya za Wasomi ndizo zinzoendesha mabadiliko katika nchi zinazoendelea. Inakuwaje Profesa unakaa kimya mwaka mzima hujazungumzia chochote kinachotokea ndani ya nchi yako kiuchumi, kisiasa na kisheria? Hawa wananchi wa kawaida wasiopata nafasi ya kuingia madarasani watapataje mwamko na uelewa wa kinachojiri katika ardhi yao? Wasomi wanaiangusha sana jamii. Haya yote yanayotokea katika nchi zetu za kimaskini ni kwa sababu wasomi wameshindwa kuiamsha jamii. Nini tofauti yao na wale wananchi walioko vijijini huko makwao? Tunao wachumi waliobobea lakini tunamjua huyu Semboja, Matamballya, wanasheria kibao, tunamsikia Kabudi, Shivji na sengondo, elimu ya siasa Baregu na ukuchungulia hawa ni kwa maslahi fulani, au siasa au wameitwa kwa ajili ya kuhojiwa, vinginevyo wanapumzika tu pale Mimani. Aibu. Fanyeni (siyo kutimiza) wajibu wenu. Hawa walioko katika siasa tunawaona jinsi wanavyoendekeza njaa, hawana msaada. Hakuna hata Prof mmoja aliyekuja na mpango mbadala unaoleta tofauti katika taasisi na idara wanazoongoza. Magufuli ni bora kuliko Msolla, Maghembe, Kapuya, aaah basi bwana.

na Christopher , Dar Tanzania, - 30.03.08 @ 17:22 | #4198

Watanzania kwa muda mrefu sana wamekuwa kimya wahesabiwa kama wapole au wajinga,mtajaza wenyewe.Imefikia mahali wamechoka na wanalalamikia hali halisi inavyokwenda.Tamko la ajabu na la kuvunja moyo toka kwa Rais wetu ni kuwa,kelele za wapinzani hazimnyimi usingizi.Hii si nchi ya wapinzani wala ccm,kwani rais hajui kuwa wapiganapo fahari nyasi ndo huumia? Kwa kusikia hizo kelele ni ishara kuwa hazitabakia kelele,wakati unakuja ambapo itakuwa ni zaidi ya kelele.Hatasikia kelele ila ataona yatokanayo na kelele.Sikio la kufa halisikii dawa.Haoni waliojidai kutawala kwa ubabe leo hii hawana hata kauli kwa kisingizio kuwa wameacha siasa,huo ni woga na aibu.Ataongea nini aeleweke na anajua watu si wa enzi zile.Watu wanabadilika.OLOE WENU WEZI NINYI,DAWA YENU IKO TAYARI.NI KIASI CHA KUINYWA TU.

na KERO, TZ, - 30.03.08 @ 17:37 | #4202

ndugu zangu tukisema tunamsubiri wa kulianzisha,anaweza kua hayupo au akaja ila akawa amechelewa,sasa kikubwa ni kujua hata mimi,wewe na yule tunaweza kulianzisha,ila kikubwa ni kwamba tuanze kwanza kuwapa somo ndugu zetu hasa wa vijijini ambao habari hawazipati au wanazipata zikiwa zimepitwa na wakati,ingawa sipendi tuanze huko mana muda umeshaenda sana ndio mana nasema tukisubiri wa kulianzisha tutakaa maisha yote na asije wa kulianzisha,km swala ni silaha sio ishu sana mana zipo nyingi sana kwenye black market ambazo wengi tulio huku tulipo tunajua wakina nani wanauza silaha kongo,swala ni kujuana km kweli wote tuna lengo 1 au wengine wametumwa na ccm,hapo ndio watu wengi hatuna uhakika,kuna watu wengi tu ambao wanafanya balaa huko kongo wanasema wapo tayari kutusaidia tukishajipanga bado hatujapata watu wa kuwaamini,mana isije tukafanya kitu halafu kikaishia kua aibu na tukaonekana wapumbavu badala ya wakombozi,kwa hiyo tujipange tu na tukiwa tayari mtaona tu kinaumana km kenya walivyofanya,na ilikua kidogo tu nchi ile iingie vitani watu walishajipanga haikua ajali tu,MUNGU tupe nguvu na ujasiri watz ili tuokoe nchi yetu kutoka mikononi mwa wajanja wachache,na kinachouma zaidi hawa watu wa nje wakina rostam ambao kwa dili 1 wanakula pesa ambayo ingetusaidia watz kwa miaka mingi sana mbele,sielewi kikwete anamkumbatia vp rostam ama nae kikwete sio mbongo ndio mana hawasikilizi wabongo wenzake,leo hii naamini kikwete yupo tayari kuona mbongo akifa,ila hayupo tayari kuona mtt ama ndugu wa rostam ama dewji wakifa sasa tumuweke pembeni mtu km huyu na kuweka watu wa kazi ambao watajali watu wao na maliasili zao na tukisema siku inakuja tunajidanganya kwa nini hiyo siku isiwe leo,ifikie wakati tuishi km makonda kwamba wanatafuta cha leo na cha kesho watajua kesho,sasa watz tufanye mapinduzi leo ya kesho au siku kuja tutajua siku hiyo itakapokuja,ila linalowezekana leo lifanywe leo.

na mstari wa mbele, calif/usa, - 30.03.08 @ 20:47 | #4219

ENOUGH IS ENOUGH , NAWAOMBA NDUGU ZANGO WOTE WA KITANZANIA MNAO ISHI NJE YA TANZANIA KIPINDI CHA KUSOMA MAGAZETINA KUTOA MAONI KWENYE INTERNET HAISAIDII HATA KIDOGO ,MIMI NAAMINI TUNAWEZA KUFANYA MABADILIKO.TUKI UNGANA NA KUIPA SHINIKIZO SERIKALI PAMOJA NA WAPINZANI WALIOKO TZ ,NINA IMANI MABADILIKO YANAEWZA KUTOKEA.WEWE NA MIMI NDUGU ZETU WAKIENDA HOSPITAL HATA PANADOL WANAKOSA LAKINI SPIKA WA BUNGE ANADAI DAWA ZA 2MILIONI INATIA HASIRA SANA SPEKA WA BUNGE LA TANZANIA AMETENGEWA MAGARI MAWILI WAKATI SPIKA WA BUNGE SIDHANI KAMA ANA GARI 2

Wednesday 26 March 2008

Ignorance Costing Africa Heavily



Jane Goodall is a renowned naturalist. Her work,at Gombe Baboons’ National Park, Kigoma, Tanzania, gave her a unique credit. She spent all of her youth there researching on apes.

The other day, I came across her book Wildebeest Family at one hospital here in Canada. The book has all rights reserved. No copying, photocopying, recording and all that goes with one’s rights to his or her work. I don’t know the number of such books by Goodall and other swindlers. Goodall has a series of books about African animals.

Goodhall is selling the pictures of our beasts the world over, making a fortune and name from our natural resources. Are the authorities in Tanzania or Kenya aware of this theft of her resources?

I know Godall personally. I met her at Kinondoni secondary school when she was giving us a lecture on preserving apes. I know her as an ape specialist but not a specialist on other wild beasts like Jacko and the little calf from the hibernating beasts of the Serengeti I saw in her book. Even Dr. Louis Leakey who conducted his research in Olduvai Gorge did not do this macabre business.

After perusing the said book, I start thinking. When did Godall become an expert and a photojournalist in the first place? When did she take the photos; she is strictly selling the world over? Did she obtain our consent or just took the snaps and disguised under her renowned title of a naturalist to rob us of our resources? One may wonder where I am driving to. But it should be underscored: our resources are our heritage meant to be used for our benefit not Goodall’s.

Sadly, many foreign countries send their emissaries to Africa where they take photos which they sell the world over and make billions of dollars. What does Africa get from this lucrative business? Why are our authorities getting cold feet when it comes to thwart this illegal business by the so called expatriates and researchers such as Goodall?

What aggrieves even much is the fact that Goodall does not offer any attribution- even a word of thanks to the place or country she stole those photos from! How many likes of Goodall are in the world? How much money are we losing thanks to this machination?

Africa has been losing a lot thanks to this naivety and ignorance. Many thieves are coming in the name of promoting our attractions. We are welcoming them little knowing they are after looting- not advertising or making our attractions known as they sully us! Some have teamed up with ‘investors’ and have turned our national parks into theirs! Kenya knows this too well. How many so-called investors are running Kenya’s national parks? How much do they pay to the government? Why should they pay if at all they are well connected with some corrupt officials in the upper echelons of power?

This, since colonial times, has been the practice. In Tanzania, even the skull of the Hehe Chief, Mkwawa and the longest lizard ever discovered were detained in Germany and England respectively! When the authorities agitated, I did not hear of the redress for being used and spent for such a long time! How many Africa’s symbols are still in Europe since pre-independence era? How much does Europe make out of these items? The answer partly, can be found in Walter Rodney’s How Europe Underdeveloped Africa. Think twice Africa and Africans!




By Nkwazi Mhango
Mhango is a Tanzanian living in Canada. He is a Journalist, Teacher, Poet, Human Rights activist and member of the Writers' Alliance of New Foundland and Labrador (WANL)

Source: The African Executive Magazine No 153

Mpayukaji nakwenda Butiama kumwambia Mwalimu hivi


MAMA Kidume jana kanipa taabu kweli. Analalamika nafuja pesa ya familia ipatikanayo kwa dhiki kukamilisha mpango wangu kabambe. Nakuibia kidogo. Ngoja niseme kwa sauti ya chini CCM wasinisikie wakadhani nakwenda kuwachongea kwa Mwalimu. Baada ya kuibiwa nyuzi kuwa CCM watakutana Butiama kufanya vikao vya Halmashauri Kubwa na Kamati Kubwa, nimeamua niende huko huko ili kijulikane. Siendi kuwachongea kwa wapenzi wa chama kama kina Butuku. Wanajua madudu yote yanayofanyika. Wamesema hadi makoo yamewakauka. Sijui watafanya nini kuona mpendwa wetu na wao marehemu Baba wa Taifa anafanyiwa unyama huu? Nilipanga kujinyonga nikagundua siyo jibu. Kimsingi nakwenda kuwaambia waheshimiwa wasio heshima: wamwambie Mwalimu yafuatayo. Nataka nisisikie gazetini wala kuona radioni. Nataka nishuhudie mwenyewe ili nije niwajuze wana Kijiwe chetu. Kwanza wamwambie Mwalimu kuwa kazi yao ya kuyafufua yote mema aliyopigania na kuyafia imekaribia kukamilika. Najua Mwalimu ni mwelewa atawakubalia hasa wakimpa sababu zenye mashiko. Naenda kuwatambulisha wafanyabiashara maarufu wanaopenda chama chake ambao wako tayari kukichangia hata kwenye uchaguzi kinapoonekana kuelemewa na wapingaji hasa kwa njia ya takrima. Nimeishawasiliana na mgosi wa Nk’oogwe amkaribishe Mjasiriamali, mkewe mama pochi, mwanae anayeonekana kurithi damu ya ujasiriamali ya baba na mama na rafiki yao mkubwa Jona. Nakwenda kuzitambulisha rasmi kwa Mwalimu ANBEN, Tanpower, Fosnik, Kagoda na Deep Green Finance. Nakwenda kumuonyesha Mwalimu kuwa uchumi wa nchi yake umekua kiasi cha kuwa na mashangingi kwa kila mjumbe mkubwa na mdogo. Pia nakwenda kutoa taarifa rasmi kuwa hata wafanyabiashara sasa wanakipenda chama chake kiasi cha kukipaisha kama dege la Lowassa. Pia nakwenda kuwasilisha ripoti ya kazi nzuri iliyofanywa na Benki Kuu chini ya mpango wa EPA au Economic Profligacy for Authorized-corsairs, ambapo karibu madeni yote ya nje ya benki na sheria yamelipwa bila wasi wasi. Pia sitasahau kumpa taarifa jinsi rafiki yake toka umasaini Ole Mmeru Ewassa, aliyemshauri asipoteze muda kujipaka uchafu kuwania uongozi alivyochafuka na kupigwa kibuti, tena kwa aibu na kibuhuti huku Bi mkubwa wake akimwaga michozi utadhani darling wake alikuwa ndiyo ananyotoka roho! Hapa lazima nimshike mkono Daktari Mwakiembe na kumtambulisha kwa Mwalimu. Najua atafurahi na kumpa nasaha moja, mbili. Sitaacha kumpa taarifa, hata kama ni za aibu, kuwa kile kizee kilichojidanganya kingevaa viatu vyake chamani kiliboa na kuanza kuropoka na kupayuka kama mimi kiasi cha umma kukizomea. Nitamueleza jinsi zile mvi za kile kibabu zilivyoishia kuwa hovyo. Hayo tuyaache. Ni yangu na Mwalimu. Pia nitautambulisha rasmi ule mradi wa bi mkubwa wa hiki kibabu pale Ubungo kituo kikuu cha mabasi. Pia nitampa Mwalimu habari njema kuwa kwa sasa nchi yake inajiandaa kutoa mabilionea kwenye jarida maarufu la Forbes watakaopambana na akina Warren G Buffet Carlos Salem na Bill Gates. Kwa mara ya kwanza Bongo itatoa bilionea wa kwanza mwanamke, Bi Nonihino Clean Ben wa Makapi. Kitu kingine nitamjulisha Mwalimu kuwa maadili ya uongozi siku hizi yamerejerewa vilivyo. Viongozi wana maadili na madili kweli kweli. Wakifanya uchafu wanasafishwa na TAKUKURU ili wasichafuke na kukiuka miiko ya uongozi. Hapa nitampa salamu za rafiki yake Ole Mmeru Ewassa na yaliyomfika alipopuuza ushauri na utabiri wake. Kadhalika nitampa taarifa ya mafanikio ya Net Group ambapo tumefanikiwa kupandisha bei ya umeme kwa zaidi ya asilimia 240 ili kuondoa tabia ya watu kupenda starehe za kutumia umeme hovyo. Pia nitamtaarifu Mwalimu kuwa chama chake kimeanzisha utaratibu wa kisayansi na kiteknolojia wa kutumia mitandao badala ya matawi ya chama ambayo ni rahisi kukatika hasa kutokana na ukame. Nitawatambulisha wabunifu wa mitandao ya kisasa katika chama ambayo imeanza kuleta matunda kwa kushindana kiasi cha kukipaisha chama. Kitu kingine nitakachomwambia Mwalimu ni suala zima la muafaka kule visiwani. Nitamtaarifu: ule muafaka aliodhani ungekuwa ni baina ya vyama umeboreka kiasi cha kugeuka kuwa suala la viongozi wa vyama. Juzi nilimuona jamaa mwenye midevu kama Osa… sorry Mpayukaji akicheka na mjomba’ake Mgosi tuliyedhani walikuwa maadui kumbe wa ubani! Pia nitampa taarifa Mwalimu kuwa siku hizi chama kimeanza kuzingatia urithi hasa wa nasaba. Kimegundua kuwa kumbe alikosea kuwazuia watoto wake na mkewe kushika nyadhifa chamani. Kufanya hivyo kulikinyima chama damu safi kama yake. Hivyo siku hizi ruksa kwa yeyote kugombea na kushika madaraka chamani bila kujali ni mke au mtoto wa mwenyekiti au rais. Hihuu! Atafurahi najua akisikia hili. Kitu kingine nitakachomwambia Mwalimu ni kuzuka kwa imani ndani ya nchi na chama, hasa ya kuabudiwa pesa na walio nazo. Kwani wataalamu chini ya ugonjwa uitwao metastasis kitaalamu, wamegundua kuwa bila pesa hakuna madaraka na bila madaraka hakuna pesa. Hivyo kuepuka nchi kusikinika, tumeanzisha ibada za namna hii ili kukuza uchumi na kuwa na viongozi wajasiriamali. Pia nitamfahamisha kuwa siku hizi, ili kukuza uchumi, ni lazima kufanyia biashara Ikulu. Hii ni kutaka uchumi uendeshe nchi badala ya siasa. Nitamkosoa kwa kushindwa kuchukua mikopo ya mamilioni ya dola alivyokuwa madarakani. Maana kutofanya hivyo kumefanya aonekane mchovu ilhali kijana wake sasa ana majumba na miradi minono. Ahitaji kujengewa kibanda kama cha Mwalimu na jeshi wala polisi. Akitaka anaweza kupigwa tafu na mkewe au wafanyabiashara marafiki zake. Pia nitamwambia jinsi wachonga maneno na peni walivyozibuka. Nitamwambia walivyoshika bango eti kijana wake Ben afikishwe kwa pilato wasijue ujasiriamali ndiyo siasa za kisasa za kimataifa! Walipozidi mkuu aliwaonya waache umbea na kutishia amani na mshikamano wa taifa kwa kutaka kuwabughudhi wakubwa wanapokuwa wanafaidi matunda ya kustaafu. Enhee! Kitu kingine. Nitamwambia Mwalimu jinsi watawala wetu wanavyojua kuchapa kazi na kuchangamkia tenda. Nitampa kisa cha lijamaa Nshomile lilivyochangamkia tenda hata kwenye hoteli kule kwa Kwini. Jamaa lilikuwa shapu na tayari kuwafuata wawekezaji hata kule Calgary, London na hotelini! Mwisho nitamfahamisha Mwalimu jinsi yale madini aliyokuwa ametunza kwa ajili ya vizazi vijavyo yanavyoingiza mabilioni baada ya vizazi vijavyo kuja kwa kasi mpya ari mpya na nguvu mpya. Madini haya yameifanya nchi kuwa na matajiri wa kutosha na kutisha hata kuchusha kiasi cha kuita hata wengine waje kutoka India wakiwa maskini lakini wayatumie kuwa mabilionia na kuiletea nchi sifa. Naamini atafurahia mafanikio tuliyopata kwenye EPA na miradi mingine kabambe. Na mwisho nitampa hongera kwa kuona mbali hasa pale aliposema tunapochagua rais tusifanye hivyo kama tunachagua mchumba. Tumeishaona na kuelewa alichomaanisha. Sasa bila kuwachosha, ni kwamba mama Kidume hataki kusikia nasafiri. Kwanza anahofia nitapata fursa ya kutanua na ‘nyumba ntobhu’ zangu ukiachia mbali kufuja pesa. Mwanamke kidhabu huyu! Yaani anajua pesa ya kusafiria nimepewa hisani na rafiki yangu Kanji lakini bado anashupalia utadhani nimechomoa kwenye akiba yake ya chakula! Inaonekana mama huyu hajui jinsi siasa za kisasa zinavyofanywa. Anataka kila siku nikae Bongo kwenye joto na tishio la migawo mwishowe mandata wanitokee wanikate mitama. Ashindwe na washindwe na kulegea. Naona kichaa mwenyewe mshirika wa bedroom, Mama Kidume, anakuja akiwa amekunja uso. Wacha nikitoe asije akanivisha gagulo na kunipigisha deki.

mpayukaji@yahoo.com


source:Tanzania Daima, Machi 25, 2008

Wednesday 19 March 2008

Chiligati alivyovuruga kijiwe chetu

JUZI katibu wa umbea wa Chama cha Chui Chatu na Mafisi (CCM - si Chama cha Mapinduzi), Yohana Chilingamiti, alichokoza kijiwe chetu.

Alisema eti kijiwe chetu kinamshambulia bosi wa chama chake. Tamko lake lilikuja sanjari na lile la Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, akidai wapinzani wanatumia kashfa ya EPA kumchafua Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete! Kwa hiyo wanaodaiwa kushambuliwa ni Mpayukaji Msemahovyo na Jakaya Kikwete. Kwa vile chama cha Chui Chatu na Mafisi si maarufu kama nambari wani, basi tutazama kwenye hili la pili.

Leo baada ya kumlaani katibu wa umbea wa CCM, mpinzani wa Kijiwe, tutajadili tamko la Chiligati wa CCM ya Tanzania. Pia Kijiwe kimepata mwanachama mpya aitwaye Tumbwelizeni. Sisi tunapenda kumuita Tumbomlizeni au Mchumia Tumbo. Huyu ni mpenzi, mwanachama na shabiki wa CCM. Inasemekana zamani alikuwa Kanjanja na alikunywa na kuchanjia maji ya bendera. Hivyo ni kichaa wa chama chake.

Mgosi Machungi analianzisha. “Wgoshi imesikia matusi ya John Chiigati eti wapinzani wananchafua Jakaya? Kweli amejua kutitukana waahi. Hivi nani anaweza kukojoa bahaini akasema ameongeza maji?”

Mchumia Tumbo hangoji. Anaamua kuhami chama lake. “Mgosi tutakosana. Huna hata heshima. Kwanza Chilgati si mtu mdogo kama wewe. Hivi mnataka mfanyiwe nini ndiyo mridhike?”

Mgosi sasa kaguswa pabaya. “Jamani timuhuumie ndugu yetu mgonjwa ah soe, Mchumia Tumbo. Hivi huoni wapi Chiigati ametukana!” Anakwanyua kombe lake la kahawa na kupiga tama mbili, tatu na kuendelea.

“Anasema wapinzani wanataka kumchafua rais! Hivi nani anaweza kuchafua kitu kilichochafuka miaka mia iiyopita? Kwa vie yeye anaipwa na kuteuliwa na rais, basi wote anaona tina makengeza kama yake. Timwambie pasonae:rais anajichafua mwenyewe na wapambe na marafiki zake.”

Mchumia hangoji Mgosi amalize. Anaivaa mic. “Kwanza ni Chiligati siyo Chiigati. Pia yuko right. Nani haoni maenedeleo tuliyofikia kama taifa? Tunaongoza kwa uwekezaji barani. Nchi ina amani. Tumesuluhisha hata ugomvi wa majirani zetu.”

Kabla ya kumalizia, Mzee Maneno anadandia mic. “Kijana mgeni wetu umesema vyema. Kwanza sijui umetokea mkoa gani?”

Mbwa mwitu anaongezea. “Nchi yetu inapaa kama dege la Lowasha. Tunaongoza kwa kuwa na serikali tajiri yenye mashangingi mengi na Wahindi wengi mamilionea.”

Mchumia anajiwahi kujibu swali la mzee Maneno akipuuza kijembe cha Mbwa mwitu. “Suala hapa si mtu anakotoka wala katoka lini bali hoja yenye mashiko mzee wangu.”

Mzee Maneno anasema: “Umenena vyema. Kweli CCM yako imeleta maendeleo. Ni kweli nchi yetu imefufua uchumi kiasi cha kuweza kuzalisha mamilionea kama kina Jeetu Patel, Balaliii, Magerezi, Kagoda na wengine. Kweli tunaona makampuni ya kitapeli yanavyozalisha pesa bila kufanya lolote."

Kabla ya kuendelea Mchunguliaji anadandia mic. “Mzee wangu umesahau. CCM kweli imeleta amani. Huoni wamachinga wa kibongo wanavyofukuzwa ili wamachinga wa Kichina na Kihindi wapate amani? Huoni pale EPA, Richmond, Dowans, IPTL na watukufu wengine wanavyotengeneza pesa kwa amani?”

“Mchunguliaji umesahau. Ndiyo maana Chiligati ameamua kuwakumbusha wapingaji kuacha mchezo mchafu wa kumchafua rais msafi na kipenzi cha watu. Na walaaniwe.” Anachomekea Mkurupukaji.

Kijiwe hakina mbavu jinsi Mshamba anavyoingizwa mjini. Naye anaanza kushtuka kuona anasifiwa ujinga.

Mzee Ndomo anatia guu akiwa anakenua meno yake yaliyoharibiwa na pombe za kienyeji. “Kijana tukusaidie. Huyo mtukufu wako unayeona kachafuliwa ana usafi gani wa halisi zaidi ya sifa za wapuuzi wachache? Kwa maneno jamaa ni msafi. Lakini kivitendo nnnh…huko usiende. Ila watakucheka kijana angalia.”

Msomi leo hangojei. “Mie huyo jamaa namfahamu sana. Tulikuwa wote JKT. Kwa vile kilikuwa hakikupanda aliamua kuzamia huko huko. Si mnajua wakati ule? Hata ukiangalia yanayosemwa yanaonyesha ukihiyo wa mhusika, kwani siri?"

Anakamua kombe lake na kuendelea. “Kama ni ugomvi wa mgeni ndugu yetu Mchumia Tumbo sina ugomvi nchi imepiga hatua. Nadhani ni nchi pekee duniani unapoweza kutumia ofisi ya umma unavyotaka na usipate taabu wala adhabu. Ni nchi ambako kuwajibika ni upuuzi na upumbavu wa hali ya juu!

“Nani anataka mambo ya Kizungu wakati sisi ni Waafrika? Nani anataka viongozi wanaofuatwa fuatwa na wanuka jasho wakati ni viongozi wao? Sisi kweli tumepiga hatua kweli kweli. Tunawapenda watu kuliko watu wowote. Hamkuona juzi rais wetu kipenzi cha watu alivyowapatanisha Wakenya ingawa pale Unguja kidogo atamaliza.”

Mchumia kapata upenyo. Anadandia. “We kweli msomi! Wapo wanaodhani ameshindwa Pemba ilhali anataka kushughulikia kwa makini ili kusiwe na ubishi na hatari kama Kenya.”

“Hiloo! Umesifiwa kunya unaanza kuharisha! Hivi unaelewa anachosema msomi au ndiyo huko kupayuka?” Anapayuka Mchumia tumbo.

Msomi anaamua kumuokoa Mchumia tumbo. “Huyu msimuonee. Kama viongozi wake ni hivyo yeye mnategemea nini? Hujui jogoo aliwafundisha vifaranga kunanihii ndani!”

Anajikakamua na kubwia kahawa kidogo na kuendelea. “Mchumia nakusifu sana kwa welewa wako mkubwa wa mambo. Inaonekana una welewa mkubwa kama viongozi wako hata chama chako. Hakuna kitu kinafanya niwapende CCM kama kutoficha ukweli wao. Nimesikia Mgosi akisema eti rais si msafi. Mzee wangu.”

Anamgeukia Machungi na kuendelea. “Tukubaliane. Rais karithi usafi wa Bwana Msafi, Clean Benjamin Mkapa. Huoni wanavyofanana na kuheshimiana. Hata pale wapuuzi walipomsingizia Mkapa na mkewe kuwa aliiba, rais hakuwaamini.

Na kwa kuwakomesha aliwaambia Mkapa, mkewe, rafiki wala mwanawe hawaguswi na yeyote. Wana kinga hawa. Kwanza hawawezi kuiba. Wana shida gani? Hawa si wavivu wa kufikiri kama wapingaji wanaotapatapa. Upo hapo Mchumia.” Anamgeukia Mchumia anayeonekana kutabasamu lakini kwa mashaka na mshangao asijue kinachomaanishwa.

“Kitu kingine ambapo Chiligati kapatia kiasi cha kumpongeza ni kusema wanataka kumkatisha tamaa rais na kujipatia mitaji ya kisiasa."

Anaendelea Msomi. “Inaonekana wapingaji hawajui dhana nzima ya maendeleo. Hawajui rais ameleta maendeleo sana? Sisi ni nchi pekee yenye kuweza kumgharimia gavana wake wa zamani wa Benki Kuu kuishi kwenye mahoteli makubwa huko Marekani. Hii si sifa kidogo. Sisi ni nchi pekee duniani inayoweza kugawana madini yake na wageni vizuri ili kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.”

Wakati Msomi akiendelea kumchamba Mchumia, Mzee Kidevu anaonekana kukerwa kiasi cha kumnong’oneza Kapende sikioni. “Mbona Msomi simuelewi! Au kaishahongwa pesa ya EPA?”

Kapende. “Siyo hivyo mzee wangu. Inaonekana leo kaamua kutumia vijembe akiwaambia walioko chini ili wa juu waelewe. Anafunga nyama.”

Msomi anaendelea: “Hawa hawaoni rais wetu alivyoteuliwa na waziri mkuu wa Finland kuwa mkurugenzi kwenye ulaji fulani huko?”

Kabla ya kumaliza, Mkurupukaji ambaye ndiyo anaingia anakurupukia mic. “Msomi leo umechemsha. Yaani unafurahia rais wako kudhalilishwa kwa kuteuliwa na waziri mkuu kama wake hata kama ni Mzungu!

Huu ni ukoloni na kufilisika jamani. Hii njaa itatumaliza.”

Akiwa anajiandaa kumjibu, askari wa city walituvamia tukatimka!

Source: Tanzania Daima Machi 19, 2008

Why Canada Has No Gates and Walls



A Nigerian friend was shocked. He shocked me too. This happened when he arrived in Canada. He found that there are no gates, guards and walls surrounding houses as in many Africa cities.

To this friend, gates, guards and high walls are the symbol of affluence!After understanding his problem, I decided to tell him why such features don’t exist around Canadian houses.

This friend did not know that the gates, high walls and the guards be they Maasai with their simis or mgambo like group so and so are the sign of corruption and selfishness! He did not know that corruption begets the society of fear! Worse enough, this fear is among the same citizens!

Canada has nothing like that. How can it have this if at all the government and the citizenry fulfill their duties to each other? Every able Canadian pays tax to the government. The government in turn fulfills all agreed duties. If anything, Canada has a very strong social security system that can not be found anywhere on earth thanks to a strong and responsible tax collection system.

If one peeped into the tax world most people we see in Africa priding themselves of being tycoons, he would die of shock to discover they are criminals for evading tax and stealing as happened in the Richmond scam in Tanzania.

Canadians are living like one family. They are not angels. But again when it comes to worthy life, Canada is second to none. I shall adduce the reasons: Generally every Canadian is entitled to all essential amenities of life such as shelter, food and medication. To make sure this works, if one’s annual income is below C$ 30,000, he is categorized as poor. Thus he is entitled to some tax exemptions and support from the government. Every Canadian has his or her health covered under Medical Care Program (MCP). This differs from one province to another. Every teen is entitled to free education up to grade twelve. Every Canadian is entitled to family care.

Whilst in Tanzania, for example, the national housing houses are used by the-well-to-do bureaucrats, in Canada, government houses are the venue of families especially those with lower income. Rent paid for these houses depend on the income of the person and the category one is in.

Every general rule has an exception to it. Looking at the goodies of Canadian system one may think there are no hitches. Though Canadians are entitled to essential amenities, there are those who mismanage the assistance (such as social service money) that is offered monthly to the jobless. Some of the beneficiaries of this money squander it so as to become panhandlers on the streets. However their number is smaller.

If anything, this is the source of tranquility and maximum security in Canadian cities. One does not need a guard or a wall. What for if at all everybody gets his daily bread? Canadian system does not build walls and gates to do away from crimes. Instead it builds human lives based on equal and reasonable distribution and provision of services. Nobody fears anybody. We fear weather. We fear blizzards, cold, tornadoes, snow and other related natural agents but not human beings.

Dar es salaam or Mombasa like damsels and women have all right and room to enjoy donning on their regalia from gems such as gold earrings, bracelets, chains and what not to all wares as they are pleased. No threat of your vipuli or ear being snatched.

Recently scientists discovered that stonewalled houses we are prone of in Africa are the good source of asthmatic problems. For the ventilation is really poor.So my friends in Masaki, Muthaiga, Lavington, Oyesterbay, Mbezi and Karen in Dar and Nairobi respectively, beware! What you think is the symbol of affluence is nothing but the symbol of decadence so to speak.


By Nkwazi Mhango
Mhango is a Tanzanian living in Canada. He is a Journalist, Teacher, Human Rights activist and member of the Writers' Alliance of New Foundland and Labrador (WANL)


Source: The African Executive Magazine

Monday 17 March 2008

Post-colonial Education and Chaos in Africa


I still gape how a highly educated society like Kenyan could cascade into anarchy and carnage. Referring to the on going impasse in Kenya, one can see what I mean.

Kenya is among highly educated countries in Africa. Nigeria too is a highly educated nation in Africa. But looking at the history of carnage and corruption in these two African nations, one doubts the importance of Post-colonial African education. I once mused on this some days ago. When I look at how African elites robbed and cankered Africa, my heart breaks so as to see a grim future as shall we fail to trace a missing link.

Robert Mugabe in Zimbabwe is an educated person by all standards. But what has he offered to his nation? Goukoun Weddeye of Chad was professor. What did he offer to his country? Remember professor Paschal Lesouba of Central Africa? He left tribal wars behind after failing to govern. Professor Amos Sawyer, Bacchus Marchus and others helped Samuel Doe to butcher Liberians.

Currently in Kenya professors George Saitoti and Sam Ongeri are helping Kibaki to lead Kenya to the purgatory. One still wonders: why a savant and economist like Kibaki would rig elections so as to cause mayhem in which sense destabilizes economy. Where is the logic for Kibaki being elite?

Before embossing what I will call the missing link, remind yourself of professor Yusuf Lule of Uganda, Drs. Hastings Kamuzu Banda (Malawi), Milton Obote (Uganda), Koffi Busia (Ghana), Theodore Sindikubwabo (Rwanda) and others. Go a mile ahead and assess their contributions to their countries. Compare the above elites to semi-literates like King Sobhuza, King Moshweshwe and Sam Nujoma, who united their countries. All those above elites proved to be a loss and shame to Africa.

In Kenya, Professor George Saitoti was hoodwinked by illiterates, Daniel arap Moi and Kamlesh Pattni so as to loot and ruin the country. What is happening in Kenya is the result of their bulimia.

In the neighboring Tanzania Dr. Daudi Ballali, former Governor of Bank of Tanzania was diddled by goons like Jeetu Patel and other Indian con men to rob the country of billions of shillings. Also elite, Benjamin Mkapa was cheated by Indian con men so as to tarnish his image on top of stealing from the public.

Looking at these few examples, one may comfortably ask: what is wrong with our education system that sires irresponsible, myopic and selfish elites like those above?

I think: we are made to swallow many unnecessary things in the name of education in lieu of pursuing practical education suited to our environment. To me this is academia-bulimia.

Colonial education is making us dependent on our former colonial masters at the peril of our own people. I like citing example from my grand father. This guy was not educated. He did not know how to write and read. Yet he forced his children to go to school. When they completed and started using English in everything they called professional, he started equating them to a White man’s dog that knows English but still it is a dog!

In my grandfather’s point of view, moral corruption and unfaithfulness went tete a tete with education he used to look at as modernity. This is true. The more educated the more the residents of the area the more the moral corruption. Compare Nairobi to other areas in Kenya. Even the level of corruption in Swaziland is lower compared to that of Ghana.

There is a Tanzanian doyen writer Shaaban Robert. This --standard four leaver-- wrote many books. Many of them are used at the university level. Many students of linguistic read and use Robert’s books in order to qualify and able to be awarded their degrees. I still ask myself: who is really educated between Robert and those copying and quoting his books? Why was Robert able to write whilst our graduates can not do so? Does it mean our education creates lack of self-confidence?

I stand to be braved. This missing link makes my heard go into circlets. I can’t espy any sense in, say, a professor who shied away from his name Kinuthia to take George knowingly the later is a colonial thing aimed at distorting and stealing his identity; or the one that was used by illiterates to abuse his office and trust.

The missing link so sought seems to be lack of practical education system made in Africa for Africa. This becomes evident due to the fact that the education system we inherited from colonial regimes was meant to produce a cohort of stooges who could be used to entrench colonialism even after the exit of the colonizers themselves as it happened in Africa.

That is why Africa has never even been able to use an African language in its business abroad just like Chinese, Japanese, Arabs and others. That is why Africa became a witness of the demise of her "justicious" religions and culture.

Kenyan renowned elite, Ali Mazrui in 1964 was jeered at when he suggested Swahili be used in the business of the then Organization of African Unity.As to date, there has been going on a kafuffle between Franco-phone and Anglo-phone countries. This used to go far deeper so as to affect even the post of secretary-general of OAU! Africa needs practical education made in Africa. This will emancipate Africans from being used by imperialists to sabotage Africa.

Last killer point, presently a Tanzanian from Monduli (Maasai) asks a passport from a Kenyan Maasai from Kajiado not knowing that those folks used to live in one country known as Africa before 1884 during the Berlin conference! If the said Maasai possesses no passport, he is shown the door in his own country by his own brother! Are these two folks really educated? Education is a tool by which to solve one's problems as he becomes more human than anything else.

A Kenyan Gikuyu is torching the house of a Kenyan Luo just because they belong to different political and tribal outfits. But at the end of the day these folks are Kenyans just like other Africans who have never accepted to be Africans in principle as they are over occupied by the colonial demarcated weak nations that hamper the re-unification of Africa!

Had African elites really received worthy education, they’d have re-united Africa after they acquired their independence. That is why it becomes logical to aver that Africa has never become independent. How could it if at all what is going on is the prolongation of colonialism? Here is where the missing link sits.



By Nkwazi Mhango
Mhango is a Tanzanian living in Canada. He is a Journalist, Teacher, Human Rights activist and member of the Writers' Alliance of New Foundland and Labrador (WANL)

Source: The African Executive Magazine and The Citizen

Thursday 13 March 2008

Taifa linakwenda wapi?

KAMA kuna sifa Tanzania imebaki nayo si nyingine bali kuparaganyikiwa na kutekwa na mafisi watu na mafisadi karibu katika kila nyanja, kuanzia nyumbani hadi Ikulu.

Nitatoa mifano. Leo tunaletewa habari kuwa mafisadi wanarejesha pesa waliyokuwa wameiba. Ajabu na serikali inapokea bila hata kuchelea kuvunja sheria ilizochaguliwa kuzihami. Je, kwa kufanya hivi serikali inajitofautishaje na mafisadi? Kwanini isiwakamate na kuwapeleka kunakowafaa? Kuonyesha nchi imeharibika kiasi gani, serikali inapokea pesa kwa mlango wa nyuma na kuficha majina ya wezi hawa!

Leo tuna wabunge wanaojulikana kughushi vyeti. Raia wema wamekwenda hadi mahakamani kutaka wahalifu hawa waadhibiwe bila mafanikio. Kisa? Serikali na chama tawala wameamua kupindisha sheria ili kuwanusuru wahalifu hawa. Je, serikali na chama si magenge ya kihalifu yaliyojificha nyuma ya madaraka?

Tuna wabunge wanaojulikana kukamatwa wakitoa rushwa. Ajabu bado wako bungeni wakiitwa waheshimiwa wakati ni wala na watoa rushwa. Je, serikali inayoweza kuwavumilia wabunge watoa rushwa na kuendelea kuwalipa pesa ya wananchi si serikali inayokula rushwa kwa njia ya kusaidia kutendeka kwa jinai hii? Je, chama chenye wabunge watoa rushwa kinanusurika na kuwa mshirika wa jinai hii?

Leo tuna utitiri wa wachungaji matapeli hadi bungeni. Mbona tuliambiwa siasa na dini havichanganyikani? Je, wabunge wachungaji si makada wa chama wanaotumia ushawishi wao kuwaumiza waumini wao kwa kuwalisha siasa chafu? Je, chama chenye uchafu na hila kama hizi si cha kidini ingawa kila uchao kinasema wananchi wasichanganye dini na siasa? Je, huu si usanii na utapeli wa kichama na kitaasisi?

Leo tuna waganga wa kienyeji wanaotumia vyeo vya uprofesa na udaktari ilhali ni mbumbumbu wasio na elimu hata ya kidato cha sita!

Leo tuna matapeli waliovamia majoho na kujiita wachungaji wakitumia luninga na redio kutangaza uongo kwa kumsingizia hata Mungu! Ajabu nasi kama hadhira, tunameza uchafu wao kwa vile tuna shida. Au ni kwa vile tu wajinga?

Ajabu ya maajabu, hata serikali inayopaswa iwe mkombozi wa wananchi, inatoa baraka kwa utapeli na jinai hii kwa kutoa leseni kwa matapeli hawa. Niulize haya unayapata wapi? Nitakujibu. Wapo wengi ninawajua nawe unawajua nao wanajijua. Mtu anakurupuka na kuanza kutangaza anafanya miujiza ya kuponya. Matapeli wenzake wanajitokeza kwenye luninga na kutoa ushuhuda wameponywa! Ebo! Kama unaponya kwanini usiende Muhimbili ukawaponya wagonjwa waliojazana Moi?

Mojawapo ya jukumu la serikali ni kuhakikisha wananchi wanalishwa huduma safi na stahiki. Je, serikali inayovumilia jinai hii si mshirika wa jinai yenyewe? Je, kwa serikali ya namna hii hata viwango vya huduma tunazopata kuanzia vyakula, madawa, elimu hata huduma za kiroho vilivyo chini ya kiwango si kosa lake? Je, serikali kama hii si ya kitapeli na kisanii?

Wapo wanaowaita watu wawape utajiri ilhali wanakwenda kuibiwa. Kama unatoa utajiri kwanini usiipe serikali yetu inayokesha na kushinda ikiombaomba na kukopakopa? Kwanini usiwasaidie watoto wetu wanaopigwa kalenda kila uchao wa elimu ya juu kuhusu mikopo?

Leo watu wanasema pesa iliyotembezwa wakati wa uchaguzi iliibwa serikalini na ndiyo hizi kashfa tunazoshuhudia kila uchao. Si chama wala serikali waliojitokeza kutoa maelezo! Je, hapa hatujawa na serikali na chama tawala vya kihalifu?

Anayebishia hili ajiulize ni kwanini kumekuwa na kelele za ufisadi, lakini hakamatwi wala kutangazwa mtu? Je, hapa tunamuuliza mwizi amtaje mwizi? Nani atamkamata nani iwapo lao ni moja? Nani atamtangaza nani iwapo wote ni wahalifu?

Kuna malalamiko kuwa mkurugenzi mmoja Ikulu ni fisadi kutokana na jinsi alivyotumiwa kwenye mchakato wa kuelekea uchaguzi. Huyu anajulikana alivyotumia kalamu yake vibaya kuudanganya umma. Ajabu ya maajabu anaendeleza ufisadi wake huu na kulipwa pesa ya kodi ya wale aliowadanganya. Je, nchi haijawa ya hovyo?

Mwaka juzi tuliambiwa kuwa serikali ilikuwa na mpango wa kupunguza mashangingi baada ya vyombo vya habari kufichua uwepo wa magari mengi ya bei mbaya yasiyoendana na uwezo na uchumi wetu. Iulize serikali. Imefikia wapi kwenye mkakati huu? Sana sana utakuta imeongeza magari haya. Je, kwa kuwa na serikali inayosema hili na kesho ikajipinga, hatujawa nchi ya wasanii na matapeli?

Gazeti hili limeishaandika tahariri zaidi ya kumi likikumbushia ahadi ya rais kurejesha nyumba zetu zilizoporwa na serikali iliyotangulia. Sasa ni mwaka wa tatu tangu ahadi hii itolewe na hakuna kilichofanyika. Je, kwa kuwa na serikali na viongozi wasiofuatilia wanayosema nchi haijawa ya wasanii na matapeli na waganga njaa?

Leo tuna mgogoro wa kulanguliwa huduma ya umeme ambapo imegundulika kuwa pesa tunayolanguliwa inaishia kuwalipa kina Richmond na IPTL. Ajabu wananchi tunaumizwa tumeshindwa kuchukua hatua. Je, sisi si jamii ya matapeli na wasanii?

Kinacholea upuuzi huu ni ile hali ya kuwa na jamii ya watu vidokozi. Anaibiwa huku naye anakwenda kudokoa kule ilimradi liende. Niliwahi kuonya kuhusu jamii ya ‘pesa ya kula’. Tumekuwa wa hovyo kiasi cha hata salamu zetu kuwa za hovyo. Utamsikia mtu anasema naenda kubangaiza, akimaanisha anakwenda kazini. Anasema bila aibu anatafuta pesa ya kula. Je, ya kuolea, kustarehe, kusomea na kutibiwa ataitafuta lini?

Hapa ndipo hatari ya kuwa na jamii na taifa lenye malengo mafupi inapojitokeza. Huwezi ukaishi kutafuta pesa ya kula tu. Mbona kunguru wasio na akili wanaishi bila wasiwasi ilihali wewe mwanadamu unajigeuza hayawani wa kutumikia tumbo kiasi cha baadhi yetu kuanza kutumia utumbo kufikiri badala ya ubongo.

Ukiangalia malipo waliyopewa mafisadi kuanzia wa EPA hadi Richmond na mambo waliyofanya utaona ukweli wa ninalosema. Ni wa hovyo hawa. Wamepewa pesa ya hovyo wakafanya vitu vya hovyo na kuipeleka nchi kwa hovyo.

Hupenda kuwaita vyangudoa hawa. Hawana tofauti na vyangudoa ambao hujivua nguo na kuuweka peupe utupu wao ili wapate pesa ambayo hatima yake itaishia kuliwa.

Hata ukiangalia kashfa kama ANBEN, Fosnik, Tanpower ukalinganisha na uzito na thamani ya dhima waliyokuwa wamepewa wahusika, utagundua upogo huu. Nyerere anaheshimika na kuogopeka dunia nzima kiasi cha kuwaangusha walio hai akiwa marehemu kutokana na kutokuwa na malengo ya hovyo na mafupi kama ya sasa.

Hakuna kitu chenye thamani kama sifa njema ambayo ni bora kuliko hata uturi. Leo wavitaka vyote uchafu na uturi utaweza? Mfano, rais alitahadharishwa kuhusu mkewe kuwa na NGO kama za wake wa marais waliopita. Nani anajua wafadhili wake na kiasi cha fedha inazopokea na kutumia bila kukaguliwa kimahesabu. Rais amekuwa haoni jinsi EOTFL ilivyomchafua Mkapa? Hakika tumekuwa taifa la hovyo.



Source: Tanzania Daima Machi 13, 2008.

Stop dilly-dallying arrest EPA's thieves

IF anything, small droughts read revelations of nonsensical and suicidal deals that thieves behind economic profligacy by so-called thieves are returning the External-Payment-Account loots to the Bank of Tanzania.

It is said:they are doing it secretly, the mighty power-that-be, this should lead the central bank, is receiving the money returned silently! Surely, such action is shameful, to say the least.

It is a cardinal sin in the first place! Some are saying. But may I ask you folks: Do you want the power-that-be to burn their own fingers? I say nay, nobody is ready to kill his own kids.

One person has sarcastically said ’’ Under any law under the sun this is but bloody theft even if it is committed by the high and mighty. How can the power-that-be commit such a financial sacrilege so to speak? I have heard that they have suspended the chief architects of this scam. But they have not hauled them to court!

Today I am not saying much. After gulping some liquor I have the temerity to say: ’’What adds up to this abracadabra is the fact that even the names of the thieves behind this crime are being concealed? So too is the amount and the dates of return of the cash! Gosh!

"If this is the murky way we are doing things, time will come when the culprits will iron out things with their victims! If not they too will be suspended in lieu of being brought to book! This looks like jungle justice per excellence!’’

Who are those being concealed? One is tempted to ask: Are they a government within a government? JK told us point blank: His is a government purely made by him. No allies. No shareholders, even us, the stakeholders.’’

"If what JK said was right, and we have no reason to doubt him for, after all he is at the helm of our country. Then where does this returned loot come from? Was it hidden under various mattresses or pots, awaiting things to cool down before it was taken back to the bank in Tanzania or in off-shore banks?

Another Bongoman says ’’The braggarts behind the curtains are big men and women with big influence in the power-that-be circles. But let’s face it single-handedly: How long will this deceit last if at all we want to know everything?’’

Let me put it point blank. I am not supporting these EPA undertakings altogether. Phew! Stop dilly-dallying and arrest those who are returning our money soonest.’’

Today things are hotter. Bettie the liquor seller says: ’’Return our money. Those implicated must face the music along with forfeiture of their ill-gotten property. Because they have committed a sin.

Bettie, the liquor seller, keeps saying: ’’We still need Ballali, the ex-BoT governor, to face the music as well. We shall never stop making loud noises so that he lands in the cooler once proven guilty.’’

She adds point blank. ’’If I got it right, I remember. The president has been asking us to help him by producing the names of the corrupt fellows in our midst. Now those behind EPA scam are known, what else is the president waiting for?’’

As Bettie pauses to quaff a little bit, Vyombo adds: ’’Does he philosophically mean we should go and attack them wherever they are in our republic? It can’t be!’’

Such behaviour would only create chaos in our country that is famous for keeping law and order.

As our meeting was about to delve deeper into EPA’s looting, the police stormed in to arrest us for drinking bootleg liquor instead of pursuing EPA’s looters using techniques they learned from Scotland Yard or the Federal Bureau of Investigation!

Source: Thisday March 13, 2008

Wednesday 12 March 2008

Go to Butiama and tell Mwalimu Nyerere


Many critics are wondering. Why? In a word, reasons for CCM to flock in Butiama. Some say: they’re in Butiama to be booted out by those that still love the founder of CCM, Mwl.JK Nyerere.

I, for one, I am saying: keep in on Folks. Go and tell Mwalimu how you are in the verge of finishing the job of rejuvenating all-he-fought-and-died-for pillars. Go and tell him as you give him the reasons. I know he’ll agree.


Go with you expensive oil guzzlers-Mashangingi. Go along with your business blossom friends who have been supporting the party he found. Go show him them. And don’t forget to remember to tell him. The biz people love the party too.


Before you go, make sure you invite the Mjasiriamali and his biz oriented wife of ANBEN. Don’t forget his son who also seems to inherit the blood of entrepreneurship-Nick of Fosnik.
Also when you go there, brief him about the nice job some of you did with regards to EPA or Economic Profligacy for Authorized-corsairs. Folks don’t ever forget. Tell him also how his best friend -he advised not to waste time running for the office- was unceremoniously booted out by the select committee.


Also do me a favor. Tell Mwl: that old man who wrongly thought; would wear his shoes in the party, proved to be a let down. His mvi meant nothing! He started blabbing like a mad person until recently he was told to retire and enjoy the money his wife makes at a Ubungo bus station. She owns a lucrative biz there thanks to ethics-less regime we are in.
If you can guys, tell him how some of you are competing in the fortune Magazine of Forbes. Mwalimu must know. Soon his party and country will produce a billionaire the size of Warren G Buffet Carlos Salem, Bill Gates etc.


So too, all so-called leadership ethics are now history. The so called party branches are no longer vital like mitandao or network.
Another thing you should not forget to brief Mwl. on is the whole issue of muafaka. Tell him please. The muafaka he thought would result into agreements between CUF and CCM meant to be inter alia individuals we see blossoming with those we used to think they’re their sworn enemies. Tell him. The other day I saw the man with bush like beads laughing heartily with his uncle- a firebrand sort of comedian guy.
Another thing, tell mwl. Nowadays it is ruxa for the whole family to run and hold high party positions regardless whether it is the family of president, chairman or else.
While he did not like to see his kids vying for top posts in the party, presently this is an in-thing. Woo-hoo!
Another crucial thing to tell Mwl., what was then regarded as metastasis with regard to the love and worship of money has currently mimed his people. No money, no power and power mean money or means of making money. In a nut shell tell him. Money is the means to the end.
Before I forget, tell Mwl please that his student he left in "the holy of the holy" defecated there. He made millions of dollars he loaned from the banks. He is currently among super rich Tanzanians tell him.
Lucubrate too that some tongue wagers wanted him brought to books. But the president said: such charges were nonsensical and a dangerous to the integrity of the nation. He said: big people should not be perturbed when they are enjoying their heavy pecks of retirement.
Let me wrap up. But I must remind you to tell Mwalimu: the many minerals he protected for the future is currently bringing billions of dollars. This has made our country to have super rich officials who know how to do business. These guys are sharp. They are ready to even follow the investor wherever he his be it London or Calgary or at sea. One of them, one time followed a Canadian investor in the hotel in London and sealed a deal just in the hotel.


The last thing, tell him. He was right. He said: when choosing a leader, we should not act as if we looking for a bride. Now we know this too well. Otherwise say hi to Mwl.
Tempus fugit, I thus have to call it a day.

Chiligati jichunguzeni msiweweseke na kutapatapa

Kwenye kitabu chao "The heart of the soul", Gary Zukav na Linda Francis wanasema "....safari ndefu katika maisha utakayofanya ni kutoka kichwani mwako hadi moyoni mwako" (Tafsiri yangu).
Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Waziri na mbunge John Chiligati alikaririwa hivi karibuni akiupotosha umma kwa kudai wanasiasa wanapotosha umma na kutumia kashfa ya wizi katika akaunti ya madeni ya nje (EPA).
Aliendelea kudai kuwa wanafanya hivyo ili kumdhoofisha rais Jakaya Kikwete ambaye kimsingi anajidhoofisha mwenyewe!
Kinachotisha na kutisha ni ile hali ya Chiligati kuamua kupotosha huku akiona wenzie ndio wanapotosha! Alichofanya ni kama kumzuia mtu asivute sigara wewe ukavuta bangi!

Hebu angalia maneno yake:"Katika hali hii, CCM tunayo kila sababu ya kuamini kwamba kashfa ya EPA imeanza kutumiwa kwa malengo ya kisiasa, ya kudhoofisha kazi nzuri inayofanywa na rais katika kushughulikia ufisadi na mafisadi… na kumdhoofisha rais aonekane hajafanya jambo lolote la maana. Njama hizi siyo za kiungwana na ni mchezo mchafu," John Chiligati.

Hivi Chiligati anaishi Tanzania kweli? Je anajua anachosema na anaowaambia? Hata kama ni kutetea kitumbua, huku siyo bali kujivua nguo kiasi cha kuwafanya watu wenye akili kushuku hata uelewa wa huyu Bwana. Kama na rais Jakaya Kikwete na Chama chake, nao wataufakamia upuuzi huu, basi huku ni kufilisika alikowahi kuonya Marehemu Horrace Kolimba; aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho.

Chiligati anasema: kashfa ya EPA inatumika kutimiza malengo ya kisiasa. Ebo! Ukiishi kwa upanga utakufa kwa upanga. Kwani pesa iliyochotwa BoT kwenye fuko la EPA ilitumika kufanya nini zaidi ya kukamilisha malengo ya kisiasa ya Kikwete na chama chake? Kwao kuuibia umma na kufanikisha malengo yao kisiasa ni halali lakini haramu kusema :walifanya hivyo! Hiyo ndiyo kazi nzuri ya CCM na Kikwete anayotaka watanzania tujivunie na kushangilia kama yeye anayenufaika nayo?

Nani hajui kuwa CCM ni mtuhumiwa mkuu katika jinai hii ambapo kampuni lake la Deep Green Finance linatajwa sana? Yaani Chiligati bado hajui kuwa watanzania wanajua mchezo mzima na anayecheza mchezo mchafu na safi? Ajiulize kwanini serikali yenye kila zana na nyenzo za kupambana na uharifu imeshindwa kuwanasa wezi walioko nyuma ya EPA. Jibu ni rahisi. Hawakamatiki wezi wa EPA kwa sababu wao ndiyo wakamataji. Kama Chiligati atanipa sababu hata moja ya serikali na chama kusua sua na kushindwa ktk sakata la kuwakamata watuhumiwa wa EPA, niko tayari kuachana na kazi ya uchambuzi. Chiligati angekuwa anajua anachosema,angewalaumu hata wana-CCM kama akina Joseph Butiku wanaokemea kila uchao hadi kufikia kusema nchi sasa ina ombwe la uongozi na ukosefu wa watu wenye visheni na ithibati.

Yaani Chiligati anadhani watu bado ni mbumbumbu kiasi hiki! Hebu angalia maneno yake mengine:"Ni lazima wananchi wakatae njama na hila hizi zinazoendeshwa na baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani," alisisitiza Chiligati.
Upuuzi. Hivi akina Butiku nao ni wapinzani? Hata yeye Chiligati kama siyo tumbo, haamini anayosema. Huu ndio uoza na ufisadi mkubwa wa CCM-kuhadaana na kujihadaa.

Kunya anye kuku asingiziwe bata! Chiligati anasema wapinzani wanataka kumkatisha tamaa na kukwamisha kazi nzuri anayofanya Kikwete! Kazi gani nzuri? Kuachia fedha na raslimali vya umma vikiibiwa na mafisi kila uchao! Namtaka Chiligati anionyeshe kazi nzuri aliyofanya Kikwete, nitamuomba msamaha Kikwete hata yeye Chiligati tena ukurasa wa mbele.Wakati akifanya hivyo ajikumbushe ahadi alizotoa bosi wake zikafanya tumchafue.

Anasema CCM wanaamini kinachofanyika ni njama ya wanasiasa na vyama vyao kumchafua Kikwete! Hakuna aliyemchafua Kikwete kama Kikwete mwenyewe na chama chake na wapambe wake. Kikwete hana usafi hata chembe. Alichafuka zamani kiasi cha kunuka. Chiligati inabidi aukubali ukweli huu hata kama ni shubiri kumeza.

Kinachochekesha sana ni ile hali ya Chiligati eti kuonya wanasiasa waache mchezo huu mchafu. Anayepaswa kuonywa na kukemewa ni yeye Chiligati na chama chake kwa kuhadaa umma na kulinda uchafu. Kinachopaswa kufanywa na CCM na Kikwete hata Chiligati siyo kuonya wala kutishana bali kujisafisha haraka iwezekanavyo.Wana bahati wananchi hawajawatokea mitaani kudai haki zao zinazochezewa chini ya Chama kilichofilisika kwa kila namna.
Tumpe marejeo Chiligati. Anaweza kuueleza umma ni kwanini rais Kikwete hajawahi kukanusha wala kutolea maelezo ya shutuma kuwa ni fisadi mkubwa yaliyotolewa na wapinzani mwaka jana chini ya kinachojulikana kama List of Shame.

Si Kikwete peke yake. Hata CCM imekuwa ikizigeuza zile shutuma-- zinazoanza kuonekana kuwa kweli-- kuwa suala la kisiasa badala ya kisheria! Hivi Chiligati anaweza kunipa sababu za ni kwanini CCM imeshindwa hata kuwafukuza au kuwaadhibu hata wabunge wake na makada wake wanaokabiliwa na tuhuma chafu kama kughushi vyeti, kutoa rushwa, kuiba pesa ya umma. Hebu nimpe majina. Edward Lowassa, Nazir Karamagi, Ibrahim Msabaha, Rostam Aziz, Gray Mgonja na wengine ni makada wazuri wa CCM. Wameguswa wazi wazi kwenye kashfa ya Richmond hadi wakafukuzwa kwenye cabinet. Je CCM na Kikwete kama siyo washirika wao wamewachukulia hatua gani wahusika kichama?

Samuel Mchele Chitaliro (Busega-CCM), Gozibert Begumisa Blandes (Karagwe-CCM), Michael Lekule Laizer ( Longido-CCM) na Elisa David Mollel ( Arumeru Magharibi-CCM). Hawa wabunge pamoja na kubainika kwa jinai waliyotenda, bado wako bungeni tena wakilindwa na chama! Kinachofanyika ni kupiga dana dana ili muda uende wamalize ngwe zao au umma usahau. Kuna uchafu kama huu?

Makala hii haiwezi bila kumtaja mwenyekiti mstaafu wa chama, rais mstaafu, Benjamin Mkapa na mkewe na watoto hata marafiki wanaotuhumiwa kujipatia mabilioni ya shilingi kiharifu kwa kutumia ofisi ya rais. Wana makampuni. Ni ANBEN, Tanpower, na Fosnik kwa uchache. CCM ingekuwa na mwelekeo na udhu angalau ingewaonya hata kuwashughulikia. Ndiyo kila uchao wanampongeza na kuzidi kumlamba miguu! Chiligati tueleze CCM na Kikwete wamewachukulia hatua gani waharifu hawa wanaojificha nyuma ya madaraka? Kuna uchafu kama huu? Kuna ufisadi na jinai kama hii ndugu Chiligati? Yaani tunaanza kubariki na kukubali hata ufisadi wa kimawazo! Jamii iliyoharibikiwa ni ile ambayo hutumia tumbo kufikiri badala ya ubongo. Hii ni jamii ya hayawani wakiongozwa na kuku.

Tumalizie na kituko cha Chiligati na CCM yake. Eti wanasema mafisadi walaaniwe na kurejesha pesa waliyoiba EPA! Wakati kidole chao kimoja cha shahada kikiwasota mafisadi, vinne vyote vilivyobakia hata vya miguuni vinaielekea CCM na Kikwete na Chiligati. Ni mafisadi walaaniwe na kurejesha au mlaaniwe na mrejeshe? Naomba kutoa hoja nikiamini Chiligati na CCM hata Kikwete watanipa maelezo kama wanataka umma uwaelewe. Hakika darasa analoweza kufanya na kutoa Chiligati hata Kikwete na CCM ni safari ya kuanzia vichwani mwao hadi nyoyoni mwao.

Kenya watushangaa! Twahami kwao kwetu kukiungua

Juzi baada ya wakenya kumwagana damu wakiwagombea mafisadi wao, nilidhani nisingerejea Nairobi kutia stori na washikaji zangu kwenye kijiwe chetu maarufu mitaa ya Kimathi, Ghana, Rivaroli (River road) Ngala na mingineyo.

Nilikwenda kusuluhisha vijiwe vya huko baada ya kuchenjiana.Baada ya hali kutulia, nilijimwaga zangu Moa nikaingia Mombasa raha nikijifanya Mduruma. Nilichukua jina la Nyae Mduruma. Huyo zangu Mombasa sehemu za Miritini na Chuda!

Nimelazimika kuingia kwa njia hii ya mazabe kuogopa kuchukua pasi ya Tanzania. Maana tangu jeshi letu lilipowanyonga majambazi wa Kenya askari wa kule waliamua kutulipishia sisi kisasi utadhani sisi ndiyo tuliowatuma au kuwanyonga! Isitoshe pasi za bongo si mali kitu baada ya wasomali, waethiopia, wanyarwanda na warundi kuzichangamkia kuzamia zao majuu.

Pale Mombasa nilitia stori kidogo nikasikia malalamiko ya wapwani dhidi ya wabara na vita kwenye pori la Murungunipa huyo sikufurahishwa nikaamua kuingia zangu Nairobi au Nyairofi kama wenyewe wanavyopaita.

Zamu hii nilikuwa na washirika zangu akina Mureithi, Ndamu, Kinyanjui, Njema, Jadwong, Mukami, Boit na Vaite Kiraitu.Nikiwa natafuna miraa (mirungi). Huku ni halali.

Mara namuona Muthamaki Njema anatia guu. Ananiamukua. "Mu-TZ umekunjanga lini Kenya hii? Huongopi kuona tunanyongana!"

Akiwa anashangaa Mureithi anaingilia. "Wewe hjuangi wa-TZ. Hii iko akili mingi. Don’t you remember wamezoea vita ya kutengeneza marais ya nchi nyingine Afrika?"

Jadwong naona hakupendezwa na maongezi juu ya hili. Anaingilia. "Omera I like prezo (Rais) yenu. Amesaidia Kenya to reach to the agreement na Kibaki."

Kabla Jadwong hajaendelea, Ndamu anaingilia. "Wewe napenda prezzo ya TZ juu ya nini? Kama najua kutongorya (Kuongoza) bona ile conflict ya Zanzibar nashinda yeye? Aache mabo ya Kenya kwa Kenyans."

Kabla Ndamu hajamaliza,Mutiso anaingilia. "Mwana wa Kaneza nasikia kibeti (mke) ya Prezzo yenu najua biasara. Eti nauda NGO inamtengezea chapaa sana."

Mambo yamekuwa mambo. Boit anaingilia. "Your prezzo ni hypocrite. Mbona hakamati ile mafisadi tena wengi Indians? Bona kuna MTZ alini-tell kuwa iko sirika na ile wevi yote naibia TZ?. Nasema ile gavana ya central banki naiba na kwenda America. Sisi yetu najaribu nafuta yeye na kupeleka yeye kortini."Njuguna anaingilia. "

Boit sidaganye MTZ. Bona ile Kalenjin Kotut naiba na Moi naache yeye. Kitu moja nasapoti wewe. Prezzo yote wevi kama Moi."

Mukami anaingilia na kumuunga mkono Boit. "Hapa watu nataka kukwepa issues. Mimi haikoona tofauti ya prezzo ya TZ na Moi au Kenyatta. Moi alizoea kwenda Church na kupozi kama born again lakini wajua ni machafu gapi Moi nafanyia Kenya? Prezzo ya TZ ni politician. Yeye kama twilight girls wa Koinange street. Naweza tembea na bwana yoyote mradi chapaa."

Anageuka na kuniangalia na kuendelea. Washenzi wamezibuka hawana akili nzuri!"

Nasikia nyinyi iko nayo street naitwa Ohio. Yes. Politicians ni kama hao girls. Leo wale nakuwa napinga Kibaki kuogea na Raila iko bele kusema nataka reconcialiation!"

Mvaite Kiraitu anaingilia. "Hii kitu kawaida. Huoni Moi nakuwa rafiki na Kibaki. Hata nasikie prezzo ya TZ imefuta kesi yote ya former prezzo iliyoiba pesa mingi na bibi yake na watoto yake."

Kuona wamezidi kunishindilia naamua kuingilia kidogo. "Naona waheshimiwa mmepatia. Kwanza nakubaliana nanyi ni unafiki kusuluhisha mgogo wa nchi kubwa kama yenu tukashindwa wa visiwa vidogo tena karibu na nchi moja."

Kabla ya kuendelea naona Wakashohi anamnong’oneza Njoroge. Anasema. "Unasikia Swahili yake ilivyo poa?"Wakashohi anasema. "Swahili poa lakini English bovu."

"Goof not my friends. What is unique with English in the first place? Do you want puritans in English as if we are British. Even Britons sometimes, make mistake. That’s why they came up with common mistakes?"

niliamua kujibu mapigo kiasi cha kuwaacha hoi wasijue wamechokoza mtu anayeongea ung’eng’e wa malkia tena wa London.

Mureithi kaona tunavuka mipaka. Anaamua kuokoa jahazi. "Wajameni. Sisi iko dugu. Kwanza wote nateswa na politicians. Tanzania haiko na chapaa na Kenyans haikuo na land. Tanzania juzi nafukuza premier Kenyans na-contain Kibaki."

Kabla ya kuendelea na busara yake mara Kinyanjui anaingilia. "Eti capital city yenu haiko na jumba kubwa kama yetu Kenya? Nasikia Nyerere alikuwa kisema kwanini kweda London while Nairobi iko!""Pia nasikia Indians naiba pesa mingi TZ? Sisi Kenya politicians ndiyo naiba pesa mingi. Naona ile jumba refu ghorofa thalathini along Kenyatta avenue? Ile ni mali ya Githunguri. Ile mingine ni ya Kanyottu na mingine kule ni ya Waithaka Waititu."

Anageuka na kuniangalia. "Eti nyinyi politicians yenu naficha pesa yote ije? Kwanini nakuwa na tabia kama panya?" Alijigamba Njuguna.

Jadwong kasikia jina la Mwalimu. Naona anatabasamu. "Mimi napenda sana Nyerere. Ilikuwa friend ya Jadwong Oginga Odinga. Leo naongelea politicians fisi na fisadi. Nyerere na Oginga haikuiba mali ya wanaichi. Hata hakuacha na bibi yake wala watoto na mali mingi kama yetu hapa inaacha land sawa na province yote."" Zamani TZ likuwa naita sisi nyang’au. Leo iko na nyang’au mingi kuliko yetu hata kama nasuluhisha sisi.

Kijiwe hakina mbavu jinsi wanavyowachambua wanasiasa. Mei kiroho kinaniuma kuona mifano inatolewa kwa mtu wetu lakini nani anajali? Siku hizi hakuna cha kujuana bali kutimiza malengo kwa umma bwana.

Mukami anaamua kubadili mada baada ya kuona tunaanza kunyambuana ilhali wote ni walalahoi. Anasema. "Sisi Africans tuko na problems. Naangalia watu ya siasa nasahau watu ya dini. Bona haisemi Revered Muiru iliyogombania uprezzo na kuchaganya mafuta na maji? Bona naogopa kushakiza (kutoa changamoto) kwa raiaa iliyokubali kuuana kulida watu ya siasa chafu? Sisi Kenya na TZ napaswa raiaa kuugana na kutosha watu chafu yote."

Jaduong anaamuunga mkono. "Sisi raiaa iko na makosa kubwa. Leo nasherehekea coalition yetu kati ya ODM na PNU. Lakini hapana jali ile ya Ugunja!"

Nami namkusoa na kusema Unguja siyo Ugunja ya Mombasa.Anaendelea. "Mimi sisifu prezzo ya TZ. Kwanini nakuja okoa Kenya naacha nchi yake kwa moto?"

Mureithi kapata upenyo. Analonga. "Hii coalition siyo muzuri. Inaangalia personalities badala ya issues na nchi. Kama yenyewe naugana wapi naweka vyama nyingine ya opposition? Nao inyongane diyo ipewe powers?"

Kijiwe kikiwa ndiyo kinaanza kunoga mara karau (polisi) walitutokea wakitaka chapaa. Mie sikujivunga nilianza kuangusha ung’eng’e wakadhani ni Mjamaica hivyo hawakunitoa chapaa.

Baada ya mandata kuishia mara lilikuja gari la mpambe wa Raila likiwa linatoa matangazo juu ya mkutano wa usuluhishi pale Kamkunji stadium. Hivyo Kijiwe nacho kwa nyonde nyonde kilihamia baa kucheza mwomboko na mwihiguro kusherehekea ushindi wa Jadwong Raila Ajuma Oginga Odinga dhidi ya Muthamaki Mutongorya Stanley Emilio Githinji wa Moi mwana wa Othaya.

Mara wimbo ulianza kutumbuiza. Jambo? Jambo Bwana Kenya yetu hakuna matata. Wageni mwakaribishwa Kenya yetu hakuna matata.Nilikumbuka jinsi tulivyokaribisha wageni wa kihindi wakatutia kwenye matata ingawa leo tunasifiwa kusuluhisha ya wenzetu Kenya wakati Pemba imegeuka kuwa fupa lililomshinda chifu Emeka Anyauko na Commonwealth ya Malkia Elizabert mke wa Philip Mountabaten!

Ama kweli hakuna unafiki kama kuhami kwa mwenzio ilhali kwako kunateketea. Kama ni mapenzi basi ni ya mshumaa.Tukutane kijiwe kijacho. Mpayukaji toka Nairobi Kenya kulikoungua shoka ukabakia mpini alioudandia Kikwekwe.

Source: Tanzania Daima Machi 12, 2008.

Kenyans hailed for solving stalemate

The imbroglio Kenya was in meant a lot to the region and the world. I remember a friend --here in Canada—asking me what my take on it was. Atrociously, I told him that it meant a lot to the world. I pondered on how the economy and peace in the whole region would be negatively affected. Though I am not Kenyan, I am East African and any shame on an African country is for all Africans. I congratulate all Kenyans for taking a bold step to put behind their differences and envisage on the future.


It should however be noted that no more blood should be spilled again. A single drop of a citizen's blood suffices to cause grief, shame and concerns for the whole nation. He who is stung twice in the same hole is a fool. Kenyans should employ what happened as a lesson.


Currently in Kenya, a new nation is in the making. The supremos should not let this synergy and chance slip away thanks to "gonzo politics" and myopic politicking. Though we are jubilating over a new dawn in Kenya, we need to see to it that the newly born baby is not suffocated.


I have reasons for my worries: First, it is upon Kenyans to save Kenya. Neighbors can come to help if you are ready. But if you are not, nothing can work.

Second, reconciliation is what many African countries long for. The resilience and spirit of engaging in dialogue, at last, have saved the country that was cascading into anarchy. If there is a winner, it is none other than Kenyans who openheartedly and readily acclaimed the agreement to form a coalition government.


What happened is but forgone shall we aim at forging ahead. Kenyans have been living for over forty years without knowing who they truly are. Now we truly know each other. Let us match ahead thumbs up.

Another sine quo non is the formation of justice truth and reconciliation commission to come up with the recipes for averting overflowing back.


Important too is the need of changing the land policy in Kenya. It is not a pun: many Kenyans are landless. This makes them desperate and vulnerable to being used by protagonists of tawdry and turgid politics. Refer to the carnage by Mungiki which also needs to be addressed. Land policy should clearly state that every Kenyan deserves to own land. Tanzania, on the next door, is a good school as far as land policy is concerned.

When human beings have nothing to own, they tend to become suicidal and chaotic. Hither is where the whole issue of land reforms becomes thorny and contentious altogether.


Eradication of corruption is another issue. People implicated in embezzling should return the loot, to empower desperate citizenry.Kenyans would like to see all corrupt officials implicated before the court. How will the Kibaki-Raila regime effectively address this?


Another issue is the new constitution. The current constitution is indeed another heck for the nation. Any wino can come and use it to devour the nation. Here is where the need to establish a sufficient and self-running system is inevitable.

The agreement of coalition provides for and was entered by two parties. What of the rest? The new constitution can fill this lacuna.


What we are celebrating today came into being thanks to the efforts of individuals supported by hoi polloi. Looking at how difficult and cadaverous it has been, it is high time for the coalition government, among others; to see to it the new constitution is delivered urgently.

Kenya has somewhere to commence: the draft constitution that was suffocated by tawdry politics is still logical and around. Go back to Bomas in a new and good spirit of building the nation.


To Raila Odinga and Mwai Kibaki: Kenyans want their Kenya back in one piece. Don’t let them down. Why shouldn't the coalition regime work as transitional government preparing an election that will enable Kenyans to have a legal government?


I know. Under euphoria, many crucial points may be ignored. But again, politics like business is a tricky game that needs much more care than jubilation.

To cut the story short, I would suggest: Kenyans go back to searching for a new constitution. What happened showed them the need of having a new constitution and how the lack of it can send a country to purgatory.


What a dangerous stance to be in when the constitution of the country fails to address its problems! The citizenry is gaspingly filing behind their leaders in licking the wounds of post-election bulimia. Let them sashay as we give them their prize-peace and tranquility.


OFF THE CUFFS: There is one thing I don't understand. Why should such highly educated Kenyan society fall in the trap of tribal and lunatic politics? Analysts need to do something about this. If anything, there is a missing link in the menu of our education.Otherwise thanks folks for reaching this milestone.

By Nkwazi Mhango Mhango is a Tanzanian living in Canada. He is a Journalist, Teacher,Poet, Human Rights activist and member of the Writers' Alliance of New Foundland and Labrador (WANL)

Source The African Executive Magazine-Nairobi.

Monday 10 March 2008

Hoseya kitoe. What are you waiting for?

Some people are mincing words. They fall short of telling the head of PCCB or Promoting and Condoning Corruption Body, Dr. Eddie Hoseya to pack and hit the road.

I wonder: what this chief suspect, among others, is waiting! Why should everything reminiscent to toto accountability and responsibility, wait for the select committee? How many committees are we to form to knock sense into the heads of some goons?

Folk , use your common sense to sense the embarrassment you are causing the nation even the president.

First of all, we’re tired of self-seekers who pose as hard workers. We know. In principle, these freebooters are but criminals in suits and high offices of the public.

Guy, didn’t you read the story of the wife of the King? Why if Mwl. Julius K Nyerere used to refer to it quite often? It was like this. When the wife of the King was suspected of being unfaithful in her marriage with the king, she did not keep mum like you. She mounted a defense that she was innocent. You know what? The King told the queen: for my wife even suspicions are themselves an offense let alone committing the alleged offense.


We saw many. We saw Dr. Ballaa of "Bunch of Thieves" self-deceiving as he averred that his morale was high whilst, in essence, he’d a stomach full of butterflies!

There came this guy fallen from grace recently, Eddie Luwasha. You know him. If you don’t, well, he is your name sake. Where is he despite being the best pal of the biggie of biggies? He clung unto premium. We formed a commission of Kyembeson that showed him the door. He is gone. He is waiting for being crucified legally shall Jackie understand what good governance really is.

Even my friend, Mulangira son of Mustapha Ka-damage was adamant when he was told to hit the road. Even Bangusilo Ibra M7ha became a stone when he was told the same. Where are these guys?

Guy, are you waiting for Jackie to cascade on you like an eagle? I insist point blank. Use your bloody common sense not bulimia and self-deception. Do you think the waliwa do not know what you did behind the curtains? Refer to your report exonerating your name sake whom we showed the door recently. Unang’ang’ania ofisi ni ya mama yako? if you think you loved to remain in that office why then did you involve yourself in dirty deeds? Being obscurantist does not pay you. It is not even an answer. If it does, indeed it is just the matter of time. You days are numbered.

Believe ye me son of so and so. Soon you’ll be booted out. Then you will head for before the Pilate to award you your reward.Your firm is stinking with corruption. Deny it. Can you truly declare your wealth? Thubutu yako?

Ask Ben son of Makapu the husband of Anna and the father to Nic what happened when he white-washed with his hocus pocus? He told us. He’d then had one Mkweche and ubavu wa dog in Chingaland. This is when he was ascending to powers.When he stood down, he left silently like hunger! I have already sent him my gospel.

Let me surmise Eddie. Park and jump into the water before we flash you under the bridge. All of your dirty linens are on the agora. You know it: we know it. PCCB, don’t mistake this with Prevention and Combating Corruption Bureau of Tanzania, is but a lame duck even a dirty goose. It is but a napkin every bed wetter can use.

Guy Devil with you in lieu of God bye you. Importantly, mark and hark my words as you hit the road now before we bundle and shove you out.

One last piece of mind. The real man stands alone and faces whatever consequences in lieu of pretending he does not comprehend. Hossie kitoe: timka umechemsha. What are you waiting for?