The Chant of Savant

Friday 31 December 2010

SALAMU ZA MWAKA MPYA



Nikiwa mpambanaji, kwanza, namshukuru Mungu kuniwezesha kuumaliza mwaka. Pili nawashukuru wasomaji wangu walionipa changamoto mbali mbali. Tatu natoa maazimio yangu ya mwaka tunaouanza.

Nina maazimio na malengo mengi binafsi. Lakini mawili si ya binafsi. Kwanza, nitaendelea kupambana na ufisadi kwa ukali zaidi.
Pili, nitawekeza kwa nguvu, sawa na kwenye ufisadi, kupigania KATIBA MPYA ili kuhakikisha jinai zilizotamalaki hasa ufisadi, uchakachuaji na ubabaishaji vinatoweka na taifa letu kusonga mbele.

Azimio la tatu ni kuhakikisha kazi zangu, yaani miswada, ambazo hazijachapishwa kuwa vitabu, inachapishwa.
Nina viporo kama vile NYUMA YA PAZIA, WAZALENDO WA DANGANYIKA, BUSARA, KILIO CHA MSIKWAO na VISA VYA MPAYUKAJI.

NAWATAKIENI HERI YA MWAKA MPYA KWA NIABA YANGU NA FAMILIA YANGU.
,

Thursday 30 December 2010

ICC Withdrawal: A Great Goof by Kenya



Luis Moreno-Ocampo ICC Prosecutor



The decision by Kenya parliamentarians to pull out of the International criminal Court (ICC) does not do Kenya good in any sense. Sadly, it paints Kenya as an outlaw and rogue state in the making. What makes this a blow is the fact that the MPs who supported the move obviously did it under the tantrums and fears of the international transparent judicial system that knows not the influence or history of the culprit.

A cabal of influential people engineered this simply because a few of theirs were mentioned in the famous Ocampo Six namely: Uhuru Kenyatta (Deputy PM and Finance minister), William Ruto (Former Higher Education Minister), Francis Muthaura), head of the civil service and Secretary to the Cabinet, Henry Kosgey, (Industrialisation Minister), Major General Mohamed Hussein Ali current Poster master and former IGP and Joshua arap Sang (Kalenjin KASS FM presenter of a morning phone-in show, ‘Lene Emet’ (How is the country?)

Looking at the names featuring on ICC chief prosecutor Luis Moreno-Ocampo's list, one notes that, all except Sang, are but big fish. Before the eyes of MPs, these are even better than over 1,000 Kenyans that lost their lives in the post-elections chaos. They are not only big fish, but also, for some, right -hand men of current principals. The fact that Ocampo's scissors cut right in the middle of the coalition government forced the principals as well as their sycophants to devise the method out of this legal quagmire though a bit too late.

No one imagined that Kenya would commit a crime of such magnitude in the first place. One would believe and think that politicians would even feel pity for allowing the 2007 mayhem to happen. Who was behind it if not the same politicians that are today pulling Kenya out of ICC so as to save their skin? This implies how collectively guilty politicians are, though not all. Their acts betray the conspiracy behind the 2007 mayhem. Kenyans should not rally behind double-faced leaders whose agenda is nothing but to save their faces and partners in crime.

What reason does Kenya give to pull out of the Rome statutes apart from impunity and corruption? That the US once did that? Is it fair to compare US with Kenya in the first place? The US is financially and economically independent, sound and free whilst Kenya is, comparably, but just a pauper-cum- beggar. Even if the US did the same, why should we support and emulate criminality even if it is committed by the high and mighty?

It won't shock anybody to hear other African corrupt countries pulling from ICC so that when they rig and steal elections, they should not be brought to book. Kenyans who always have been champions of positive changes should nary consent to this.

The same MPs that shot down two motions that wanted them to form a local tribunal to look into the matter are the same agitating for pulling out of ICC! When did they see light so as to, now, want the same thing they refuted and trashed? Is it because when the tribunal is formed and manned by local appointees of the president or whoever appoints them, it will be easily compromised Kenyan style as it happened in mega scandals such as Goldenberg, Anglo-Leasing, Dr. Robert Ouko, J.M Kariuki, Tom Mboya, G. Pinto and other massacres where culprits have ever been netted?

It disgusts to hear some MPs saying that Kenya is a sovereign country thus it should not allow her people to be tried outside. Why did she support other nationals such as Charles Taylor, Jean Pierre Bemba, Joseph Kony and other to be tried there if what they mean is to be fair? Why didn't those advocating this carnage conceive this concept of sovereign when the mayhem was committed? When Arusha based International Criminal Tribunal for Rwanda (ICTR) was formed to secure the interests of the sovereign and to make sure that all culprits face justice, Rwandan authorities formed Gacaca to act concurrently with ICTR. Rwanda did not pull out of Rome Statute even when its president was implicated by a French judge.

Though Kenya was not referred to as a failed state, the 2007 sacrilege drove it to the verge of a failed state. The same international community it is now shunning is the only that came to their aid at this very trying time. Now she is out of the danger, MPs want it pulled out of ICC!

To pull Kenya out of ICC won't solve the problem. Instead, it will aggravate it thanks to being the work of mania and myopia. This being the case, Kenyans who love their country should not allow MPs on their behalf to commit this suttee. Kenya is more than the Ocampo Six.

Human rights activists should squeeze politicians to see to it that Kenya remains a signatory of Rome Statutes. For pulling out of ICC is nothing but sheer fear of politicians who think ICC might come again to seek other criminals that were not mentioned by Ocampo this time. Again, by pulling out, it means: Kenya aims at committing the same crime in the future. This is not a stance a civilized country like Kenya should take.

Source: African Executive Magazine Dec. 28, 2010.

Baada ya Dowans nani atafuatia kuchuma?

Ingawa si vizuri kupinga amri halali ya mahakama bila kukata rufaa, kuna haja ya kukuna vichwa upya. Inakuwaje taifa lenye kila wataalamu tena bobozi wa sheria kugeuzwa shamba la bibi hivi?

Taarifa kuwa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara imetoa huku kuwa Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) liilipe jumla ya shilingi 106, 000,000,000 licha ya kuwa pigo na aibu kwa taifa ni hujuma na kashfa nyingine ndani ya kashfa.

Kuonyesha kuna namna, hata baada ya kutangazwa hukumu, si serikali wala TANESCO ameonyesha nia ya kukata rufaa zaidi ya watu wenye uchungu na nchi kuhoji kulikoni? Je kuhoji tu bila kuchukua hatua inatosha? Je kama siyo njama, kwanini serikali imepatwa na kigugumizi hata kuzungumzia suala hili nyeti kabisa? Hawa ndiyo wanataka waaminiwe kurejeshewa pesa ya ujambazi wa rada? Je watanzania wataendelea kurudia makosa?

Je hili tuliite makosa halali ya kisheria au njama za kuendelea kuhujumu taifa letu? Nani yuko nyuma ya kadhia hii? Je hawa wataalamu wa sheria na upelelezi waliojaa serikalini wanalipwa kwa ajili gani iwapo kila siku tunaendelea kugeuzwa na mafisadi kichwa cha mwendawazimu?

Kwa kumbukumbu ni kwamba, kisheria, kila kitu kitokanacho na kitu ambacho ni kinyume cha sheria nacho ni kinyume cha sheria. Whatever is done or acquired by unlawaful means is null and void (and illegal) ab initio. Kisheria hata kiakili za kawaida ujio wa Dowan kurithi mkataba wa kampuni ya Richmond LLC iliyothibitika bila shaka lolote kuwa ya kitapeli unaacha maswali mengi zaidi ya majibu. Je hawa walioridhia kampuni hii kuchukua mahali pa kampuni ambayo ni batili si wa kulaumiwa hata kuwajibishwa?

Nani zaidi ya mwanasheria mkuu wa wakati ule anapaswa kubebeshwa mzigo wa hujuma hii? Nani zaidi ya rais ambaye alishindwa kumwajibisha mwanasheria huyu zaidi ya kumkingia kifua hadi wengine wakastaafu na kupewa marupurupu na mafao lukuki hata ambapo kisheria walishachafuka? Nani zaidi ya wananchi wanaoendelea kukubali jinai hii?

Ilikuwaje wahusika wakakubali kuhamisha mkataba toka kampuni iliyothibitika kuwa hewa na kinyume cha sheria bila kuangalia uhalali kisheria kama hii si hujuma ya makusudi?

Kwanini pale Kamati Teule ya Bunge maarufu kama Kamati Teule ya Bunge ya Mwakyembe ilipofumua siri zote nyuma ya pazia na kugundua kuwa licha ya Richmond kuwa kampuni ya kitapeli ilingizwa kinyume cha sheria, Tanzania iliridhia haraka haraka 'haki' zote kurithishwa Dowans ambayo nayo ni ya kutia mashaka? Rejea kugundulika kuwa anwani zake nchini iliionyesha kuwa ile ile ya Richmond na Kagoda-Kipawa?

Kwanini wahalifu wa Richmond waliachiwa waendelee kulihjumu taifa pamoja na ushahidi na wengine kukiri na kuwajibika kisiasa na si kishria? Je ni yale yale ya EPA au EPA nyingine? Huwezi kujadili yai bila kumjadili kuku. Dowans ni yai viza lililotagwa na Richmond.

Tukubaliane. Tunahujumiwa na wale wale tuliowaamini madaraka. Ingawa mzigo wa Richmond alibebeshwa Edward Lowassa, waziri mkuu aliyetimuliwa, kuna haja ya kuchimbua zaidi. Kwa kumbukumbu ni kwamba wakati wa mchakato wa kuleta Richmond ili kuondoa tatizo sugu la umeme amabalo limegeuka kansa, Kikwete aliwahi kuutaarifu umma kuwa anafuatilia mchakato mzima na hupewa briefings na waziri mkuu. Hii maana yake ni kwamba kila alichofanya Lowassa kilikuwa na baraka za bosi wake na ndiyo maana baada ya kutolewa kafara kuokoa serikali ya rafiki na bosi wake hakuchukuliwa hatua zaidi.

Hebu tusome maneno ya mwenyekiti wa CUF profesa Ibrahim Lipumba aliyotoa tarehe 19 Julai 2009.

“Wananchi, leo nawatobolea siri juu ya Kampuni ya Richmond… mhusika mkuu wa ufisadi wa Richmond ni Rais Jakaya Kikwete. Ukiangalia vizuri ripoti iliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe, utaona inamhusisha Rais Kikwete na ufisadi huo.”

Lipumba aliendelea. “Kwa ukweli huo, Lowassa yeye katolewa kafara tu na rafiki yake Kikwete, lakini rais huyu ndiye aliyepaswa na mpaka sasa ndiye anayepaswa kuwajibika kwa taifa. Hatuwezi kufika kwa mtindo huu.”

Kuonyesha maneno ya Lipumba ni ukweli mtupu, si rais Jakaya Kikwete wala wasaidizi wake walikanusha! Na hii haikuwa mara ya kwanza kwa Kikwete kuhusishwa kwenye kashfa ya Richmond pamoja na ile ya EPA na asikanushe wala kujitetea. Namna hii maana yake ni kwamba tuna mkuu wa serikali anayesimamia hujuma kwa nchi.

Muulize Kikwete. Kwanini hakuwahi kukanusha kushiriki na kunufaika kwake na kashfa ya EPA ambayo pesa yake inasemekana ilitumika kumwigiza madarakani? Muulize hata mtangulizi na swahiba wake Benjamin Mkapa ni kwanini hajawahi kukanusha kuasisi wizi wa EPA?

Wako wapi watuhumiwa waliowezesha wizi huu kama Beredy Sospeter Malegesi,Johnson Rwekaza, Kagoda, Peter Noni na wengine waliotajwa wazi wazi na kubainika walitenda jinai ya EPA?

Tufike mahali tuache kulindana na kuogopana. Tumwambie rais awajibike na kuwawajibisha wenzake vinginevyo tumwajibishe kabla hujuma hii haijatupeleka kuzimu. Na hii ndiyo siri ya taifa kuwa maskini kuliko hata vinchi vidogo vilivyotuzunguka visivyo na raslimali hata robo yetu. Na hii ndiyo siri ya watawala wetu kutotaka kuandika katiba mpya kwa kuhofia hatima yao kutokana na uchafu wanaoendelea kufanya.

Kashfa hii mpya ya Dowans itufungue macho na kuchochea hasira zetu kama umma kukikabili kikundi cha wezi kinachotupeleka kuzimu.

Inapaswa wananchi wafahamu kuwa serikali haina pesa yake zaidi ya pesa yao. Hivyo pesa itakayolipwa kwa kampuni hii yenye kutia kila shaka ni yao na si ya serikali. Watapandishiwa bei ya umeme na vitu vingine ili kufidia pengo hili. Kama hawajui wajue.

Je kutokana na nchi yetu kugeuka chaka la walaji, nani atafuatia kuchuma kwenye hili shamba la bibi? Je ni mikataba mingapi iliyosukwa kidowans ili ikivunjika wahusika watajirike haraka kwa pesa ya mataahira na mafisadi?
Chanzo:Mwanahalisi Desemba 28, 2010.

Wednesday 29 December 2010

Hosea unangoja nini TAKUKURU?



Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea hivi karibuni alijikuta matatani. Hii ni baada ya mtandao wa kufichua usiri na ufisadi wa kimataifa wa Wikileaks kufichua alichoongea na mwana diplomasia wa kimarekani, Purnell Delly mnamo Julai 2007.

Kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Uingereza la 19 Desemba 2010 lililofichua haya ni kwamba Hosea hana imani na bosi wake ambaye anamuona kama kikwazo katika kupambana na ufisadi. Anaonyeshwa kama mtu aliyekata tamaa na asiye na uhakika na usalama wake. Pia anaonyesha kama mtu asiye na mamlaka wala heshima zaidi ya kutumika kama kiraka au kikaragosi tu kwa sababu ya kutaka riziki tu.

Kwa maana hiyo, rais Jakaya Kikwete baada ya kujua hili naye hatakuwa na imani na Hosea tena. Hapa kunajengeka kutoaminiana hata kuogopana na kuweza kuhatarishiana ulaji hata maisha. Na katika vuta nikuvute hii mwenye kuathirika zaidi ni Hosea ambaye maongezi yake yanamwonyesha kama mtu asiyejiamini wala asiye na maadili. Maana angekuwa na vitu hivi ama angemkabili bosi wake na kumpa ya moyoni au kuachia ngazi hasa baada ya kuona anatumiwa na kudhalilishwa. Lakini kwa miaka yote ambayo amekuwa TAKUKURU hajafurukuta zaidi ya kuendelea kujirahisi na kukubali kuendelea kutumiwa.

Ingawa Hosea alikanusha yaliyoandikwa na The Guardian, ukweli ni kwamba hana udhu tena wa kuendelea kuwa Mkurugenzi wa TAKUKURU. Pia hata bosi wake, yaani rais Jakaya Kikwete, hana imani naye tena kama ambavyo amekuwa hana imani na Kikwete kiasi cha kunung'unika. Kwa maneno rahisi ni kwamba Kikwete ni kikwazo katika vita dhidi ya ufisadi.

Je yeye Hosea kwa kukubali kuendelea kutumika asifanye lolote alilotegemewa kufanya hajawa kikwazo katika vita hii dhidi ya ufisadi? Je kunung'unika ni jibu? Kwanini asijiuzulu ili umma umuunge mkono yafanyike mabadiliko kama kweli ana nia nzuri na watanzania?

Pamoja na kukanusha, je Hosea kweli bado anapaswa kuendelea kuwa mkurugenzi wa TAKUKURU wakati amethibitisha wazi alivyoshindwa au tuseme kukwamishwa na rais Kikwete ambaye amekuwa akilalamikiwa kwa kuwakingia kifua washirika zake na marafiki na mabosi wake kama vile rais mstaafu Benjamin, mkewe, vivyele vyake na watoto wake. Rejea kauli ya Kikwete aliyoitoa Machi 2007 alipokuwa akiongea na watanzania waishio Sweden pale mmojawapo alipotaka aeleze ambavyo angemshughulikia Mkapa.

Kikwete hakumung'unya maneno wala kuona aibu ya kutetea ufisadi. Alisema wazi wazi kuwa tumuache mzee Mkapa akapumzike vyema baada ya kutuibia mali zetu. Hata hivyo wengi hawakushangaa kutokana na ukweli kuwa bila msaada wa Mkapa hasa kwenye skandali ya EPA, huenda Kikwete asingeshinda urais. Hivyo, aliamua kulipa fadhila kama ambavyo amekuwa akifanya kwa washirika na marafiki zake wengi wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Muulize Hosea. Kesi ya Kiwira imeishia wapi zaidi ya kusingizia kinga kwa Mkapa? Tulipouliza kama washirika wa Mkapa yaani mkewe wakweze na watoto wao nao wana kinga, hakuna aliyejitokeza kujibu. Hata ukiuliza tena si Mkapa wala serikali, wote watakaa kimya ili umma usahau waendelee kupeta. Nijuacho ni kwamba pamoja na Mkapa na washirika wake kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupwa, waliutumia kuibia pesa ambayo nayo ililipwa na serikali toka hazina. Rejea serikali kulipa mabilioni ya shilingi kwa wafanyakazi wa Kiwira utadhani ilikuwa imewaajiri wakati walikuwa wametwaliwa na Mkapa kama mwekezaji.

Muulize Hosea Kagoda ni nani na amemfanya nini zaidi ya kumjua na kumuepuka kwa kumuogopa bosi wake. Muulize Hosea ambaye alitaka kutumiwa kuhalalisha na kubariki Richmond kwa kuutetea uoza wa aliyeipendelea kuiingiza nchini waziri mkuu mtimuliwa Edward Lowassa. Muulize Hosea, kama kweli ni safi, kama ameishataja mali zake zote bila kuficha.

Wengi wanaweza kudanganyika na kuamini kuwa Hosea alizuliwa. Delly angemzuliaje ili iwe nini wakati akijua fika maongezi yao yalikuwa ni siri za kibalozi ambazo kama siyo kuangukia kwenye mikono ya Wikileaks hakuna ambaye angeyajua akiwamo yeye na bosi wake yaani rais Kikwete. Hivyo kukanusha hakumsaidii na kama ni ubovu kwenye mahusiano na bosi wake umeishatokea. Akubaliane na hili ajiuzulu kabla ya hasira za bosi wake kumuumbua kwa kutimuliwa kwa aibu.

Kumekuwa na shutuma nyingi toka kwa wapinzani wakidai kuwa hata kutokamatwa kwa wamilki wa kampuni ya kijambazi ya Kagoda inayodaiwa kumilkiwa na mbunge wa Igunga Rostam Aziz kumesababishwa na Kikwete kumkingia kifua kutokana na kulipa fadhila. Rejea kumteua mtuhumiwa wa kashfa ya EPA, Peter Noni aliyetajwa na mwanasheria aliyesainisha (attestation) baadhi ya nyaraka za kuhamishia pesa za EPA. Bhindika Michael Sanze toka kampuni ya kisheria ya Maregesi chamber, kuwa mkuu wa benki ya raslimali.

Kitu kingine kinachomtoa knockout kiasi cha kumtupa Hosea nje ya ofisi ni ile hali ya kukiuka kiapo cha utii kwa bosi wake na kutunza siri za ofisi. Laiti siri hizi angezimwaga kwa wananchi ambao kimsingi ndiyo waajiri wa bosi wake, lau wangemtetea. Lakini amekwenda kuzimwaga kwa wageni! Sijui kama Kikwete atamvumilia ikizingatia asivyopenda kukosolewa. Rejea yaliyowapata akina Samuel Sitta walipoanzisha vita dhidi ya ufisadi.

Kwa kukiuka kiapo na kulalamika kwa watu wasio wateule wake na kuonyesha hofu ya maisha yake, Hosea amepoteza uaminifu kabisa. Hivi Hosea atakaa ofisini kufanya nini iwapo ameshindwa hata na mibaka na majambazi ya kawaida yaliyoiba mabilioni ya pesa yetu kwenye ununuzi wa rada na dege feki la rais wakati wanajulikana?

Hata hao wafanyakazi wa TAKUKURU ukiwachunguza kula, vaa yao na mali wanazomilki utakuta nao ni wala rushwa wa kawaida tu kiasi cha kuifanya TAKUKURU kuwa chombo cha kulinda na kudumisha rushwa.

Kutokana na hali hizo hapo juu ni ima Hosea ajiuzulu au ang'ang'anie ili Kikwete amtimue. Pia kwa wananchi kujua kuwa hana ubavu wa kushughulikia ufisadi, wanaweza kushinikiza aachie ngazi huku wakitaka TAKUKURU iondolewe chini ya ofisi ya rais. Maana, kimsingi rais anaitumia kulinda ufisadi badala ya kupambana nao.

Mafisadi sasa matumbo moto


NGOJA niimbe rap ya rais M7 nijiliwaze kidogo. Maana ukiimba unajisikia kama rais rais hivi.

Natema Akati kaarara, Kaarara nikaza Igara, Igara owa Ntambiko, Ntambiko yampa akasyo, Akasyo nakaha abagyesi, Abagyesi bampa oruro, Oruro naruha Warukoko, Warukoko yampa ihuri, Ihuri nariha abaana, Abaana bamp'engyeya, Engyeya naagiha omukama, Omukama yampa Kasha, Kasha nagishweza omukazi, Omukazi yanzaarira omwana, Namweeta Mugarura Yaagarura eby'ow'ishe n'ishenkuru.

Mp'enkoni mp'enkoni mp'enkoni, Mp'enkoni engarama ziizire, Ziizire niicund'ebinio, Ebinio bya Rutendegyere, Rutendegyere enkuba emuteere, Emuteerere ahaiguru mpariya, Ahaiguru hariyo orwitiri, Orwitire oruzaarwa n'enkura,Enkura eshoroma etegire, Etegire akaara k'embogo, Ak'embogo karimu omwonyo, Omwonyo guruga, Nsharira Nsharira omunda y'engoma, Y'engoma, y'engoma, y'engoma.

Dowans dowans karibu bongo, Bongo wana dola,
Dola za kugawa, Ukiwa na mzito, Dola unachota,
Unaunda Richmonduli, Richmonduli inakupa dowanis,
Dowanis inakupa dola, Dola za kutesa.

Do you want another rap? lol! We koma. Baada ya rafiki yangu M7 kukumbwa na misukosuko kuwa aachie madaraka na amekaa muda mrefu na kuchusha huku akihudumia familia, ukoo na kabila lake, aliamua kujiliwaza kwa kuimba rap.

Hata pale jamaa ambaye ni mwanafunzi wangu, Julian Assange ambaye jina lake haswa ni Assenga alipoamua kudai anahofia imla wa Libya, Muamar Gadaffi anaweza kumnyotoa roho, aliamua kujiliwaza kwa kuimba rap.

Mwenzenu sina hamu na hawa jamaa wa wikileaks. Wanavyotoboa siri zetu sijui kama walevi wakizinduka tutapona. Sasa tazama kuwaogopa naishia kuwa mlevi!

Yaani wanajua hata hawara wa maris wote! Nani angelijua kuwa wangefichua hawara wa imla wa Libya waliyemuita toto la Kiukraini? Jamaa wanajua hata chupi wanazovaa vigogo. Wanajua hata wale wanaotawaliwa ima na mafisadi, nyumba ndogo hata wake zao.

Wanawajua hata wale walikasimu madaraka yao kwenye chupi au vyumba vya kulala kiasi cha bi wakubwa kuwa marais wasiochaguliwa na wenye vyama vyao vya nyuma ya pazia wakihomola nchi za kitwahuti kama hawana akili nzuri.

Nani angefikiri kuwa hawa weaklick wangeweza kujua siri zangu zote ingawa hawajazianika kutokana na kuogopa mwanafunzi wangu Assange nisimuachie laana?

Turejee kwa walioanikwa. Mnene wa Taasisi ya Kuboresha na Kuneemesha Ufisadi (TAKUKUU) ndiye majeruhi wa kwanza kayani. Jamaa walianika alivyonanga bosi wake ukiachia mbali kumlamba uchogo na kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

Jamaa kweli alimpaka. Yaani haogopi kumuona bosi wake kama kingpin wa mafisadi yarabi? Kweli wanasiasa ni watu wa ajabu ingawa hawana mikia kama nyani. Hata hivyo hawana tofauti na nyani kutokana na kufanya mambo yao kinyani nyani au monkey business.

Hakuna kitu kilinifanya nicheke si kwa furaha bali uchungu kama jamaa yangu Daktari wa Sharia Eddy Oshea kukimbilia kwenye magazeti kukanusha alichosema.

Jamaa kwa kula matapishi yake ili kulinda ulaji wake mie sina hamu. Amenikumbusha jambazi mmoja aitwaye Johansen Mwananyika aliyekuwa akitaka ninyotolewe roho baada ya kueleza ujuha wake naye akakimbia kukanusha na kutaka kufungia gazeti. Yuko wapi zaidi ya kuishi mafichoni kama Tunituni akilindwa na Njaa Kaya?

Wengi hawakujua kuwa kumbe Oshea ni kama kikaragosi kinachotumiwa na Njaa Kaya kufanya usanii wake. Hana tofauti na kikaragosi cha Joyce Wowowo kwa wale wenye kumbukumbu ya kikaragosi hiki maarufu kwenye jiji la Bongo.

Kilichonikuna ni kikaragosi kutumia kikaragosi wakati vyote ni vikaragosi vinavyochezeshwa na akina Ewassa na Rost na Endelea Chenga.

Una habari kuwa Oshea alikiri kuwa hana ubavu wa kuwagusa mafisadi walioteka kaya na kuigeuza shamba lao la bibi? Nasikia hata kwenye huu ujambazi wa Dowanis ni wao walioko nyuma ya pazia. Mwuulize Papa Six atakujuza
Kwa sasa nina mpango wa kumwandikia mwanafunzi wangu Assange afichue uchafu wao wa Kagoda na HEPA baada ya kugusa ule wa mrada na mdege feki wa bwana rahisi.

Jamaa zangu mabwege kweli. Una habari gabacholi aliyewaunganisha na lile shirika la utapeli wa silaha la kwa mama liitwalo BEA alikwapua dola zaidi ya milioni kumi wakati wao waliishia kupewa kimilioni kimoja kama ilivyokuja kubainika kwa mzee wa madafu Chenga ambaye naye ni kigogo anayemnyima usingizi Oshea?

Kwa kuzingatia niliyonyaka kwenye weacklick ni kwamba Oshea ni kama changu kwani ana mabosi wengi kuanzia mkuu mwenyewe na mafisidunia wenzake. Laiti angekuwa mrume kama mimi ashakitoa zamani huku akimwaga tamaa kwa kuku ili kila mtu adonoe aone nani atafaidi na kufaidiwa.

Kwa vile yeye ni bonge la mroho na mlafu achumiaye pakacha lake liitwalo tumbo, hata mshike pabaya, hawezi kuachia ulaji. Kanikumbusha kisa cha Kanji aliyemwacha bi mkubwa wake achukuliwe na aliyempa mtaji ili biashara yake isidode kwa kudaiwa alipe. Watu wanaopenda vitu hawana utu hata kidogo. Ni watu vitu tena vinyama mwitu waitwao watu wakati si watu bali wanyama mwitu wafananao na watu.

Laiti ningeteuliwa mie kuendesha vita dhidi ya ufisadi licha ya kuwakamata hata walioniteua, ningeamuru kila mtu aniletee maelezo ya alivyopata mimali yake. Baada ya hapo ningeikomba mimali yao halafu nikaishia ughaibuni kwenda kutumbua kama wanavyofanya magabacholi baada ya kuwaliza walevi wa walevi wao watawalao.

Nami baada ya kujua kuwa njuluku zangu zitaibiwa kwa mara nyingine kuwalipa Dowanis, naweza nikaamua kuimba rap. Do yo want another rap?

Yeah Sebo. Walevi itikieni.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 29, 2010.

Sunday 26 December 2010

Heshima au udhalilishaji!

Ajabu jamaa wanachekelea utadhani ni jambo jema! Au huyu mama kaingia kwenye siasa kupitia viti maalum kufanya kazi hii maalum-kujidhalilisha yeye na wanawake wote duniani.



Malawi’s Foreign Minister Etta Banda(on her knees, right) welcomes in style, President Jakaya Mrisho Kikwete shortly after he arrived in Blantyre for one day working visit yesterday. On the left is Malawi’s Minister of transport and public infrastructure. President Kikwete later held talks with President Bingu wa Mutharika of Malawi who is also the current chairman of African Union AU. The President returned to Dar es Salaam yesterday evening.

Hii nayo tunasemaje ingawa tukio zima lau ninasema kuliko picha ya kwanza?


Picha kwa hisani ya profesa JL Mbele.

Friday 24 December 2010

Hapa wa kulaumiwa nani? Tusipendelee




An Iraqi man killed his 19-year-old daughter after he discovered al-Qaida had recruited her as a suicide bomber in an area north of Baghdad, a police spokesman said on Friday.

Al-Qaida has been recruiting women for suicide attacks because they can pass police checkpoints easier than men by concealing explosives under an abaya, a loose, black cloak that conservative Muslim women wear. Suicide bombers have been al-Qaida's most lethal weapon in Iraq, killing hundreds of civilians and members of Iraq's security forces.

The killing of the young woman was discovered when security forces, searching for her on suspicion she had ties to al-Qaida, raided her father's home Thursday outside the former Sunni-insurgent stronghold of Baqouba, 35 miles (60 kilometres) northeast of Baghdad, said Maj. Ghalib al-Karkhi, a police spokesman in Diyala province.

The father, Najim al-Anbaky, was detained in the raid. During questioning he told police he had killed his daughter, Shahlaa, a month earlier because he found out she intended to blow herself up in a suicide attack for al-Qaida, al-Karkhi told The Associated Press.

Al-Anbaky showed police what he said was the woman's grave, al-Karkhi said. The father remains in custody and is under investgiation, but no charges have been made yet.

A police official at the interior ministry in Baghdad confirmed the killing. He spoke to the AP on condition of anonymity because he was not authorized to speak to the media.

A female suicide bomber was behind one of the deadliest attack this year in Iraq, after she blew herself up among Shiite pilgrims Baghdad in February, killing 54 people.

In a separate incident Friday, a Shiite militia leader, his wife and three children were killed in a bomb attack on their home south of Baghdad.

The early morning blast levelled the militia leader's home in Haswa, some 30 miles (50 kilometres) south of the capital, Babil province police spokesman Maj. Muthana Khalid said. Four people were also wounded in the blast.

A local policeman, Abdul-Salam al-Maamouri, identified the dead man as a commander in the Mahdi Army, the militia loyal to radical cleric Muqtada al-Sadr. The militia terrorized Sunni neighbourhoods during the height of Iraq's sectarian fighting in 2006 and 2007, and its fighters have been targets of retribution.

Wednesday 22 December 2010

Mkapa, Lowassa wameuona mchezo nje ya uwanja

KUNA usemi maarufu kuwa ukiwa nje ya uwanja unapata fursa ya kuuona mchezo vizuri kuliko wacheza wenyewe. Hivyo ukosoaji au ushauri unapotelewa na mtu aliyeko nje ya uwanja tena aliyewahi kuwa kocha mchezaji, unakuwa lulu na uzito wa aina yake.

Hii imejitokeza hivi karibuni wakati rais mstaafu Benjamin Mkapa na aliyekuwa Waziri Mkuu aliyestaafu, Edward Lowassa pamaoja na mapungufu yao na, lau walitoa mchango ambao ni adimu na adhimu na unaopaswa kupewa kipaumbele kikubwa tu.

Mkapa alikaririwa akisema: “…hatuna Katiba zingine zaidi ya zile ambazo tumezirithi kutoka kwa wakoloni, Katiba ambazo hazina umakini, tunahitaji mpya.”

Maneno ya Mkapa ni kweli. Karibu katiba zote ukiondoa za Afrika Kusini, Kenya na kidogo ya Botswana, zilirithiwa toka kwa wakoloni walioendelea kuzitumia kuweka vibaraka wao madarakani ili kuwatumia kuwanyonya wananchi waliodanganywa kuwa wako huru.

Pale ambapo wakoloni hawakuweza kuweka vibaraka wao, waasisi mfano kama Tanzania, walianzisha chama kimoja na kujiimarisha madarakani hata bila ridhaa ya watawaliwa. Chaguzi viini macho zilifanyika na wahusika kushinda kirahisi. Na hii ndiyo sababu ya vyama vikongwe kama CCM kuendelea kuwa madarakani hata bila ridhaa ya Watanzania.

Na hii ndiyo sababu kuu inayofanya CCM kutokubali kubadilisha katiba. Maana inajua fika kuwa kufanya hivyo inamaanisha kifo chake hasa kutokana na katiba mpya kuziba upenyo ambao imekuwa ikiutumia kusalia madarakani hata bila kufanya lolote.

Huwezi kuwa huru bila kupata haki zote za msingi kama kuwa na nguvu na maamuzi katika kuongoza nchi yako. Bila wananchi kuwa na ubavu wa kuilazimisha (kuiwajibisha) serikali kuwatawala watakavyo, maana ya kuwa na katiba na uhuru hupotea kama ilivyo kwenye nchi nyingi za kiafrika.

Hatuwezi kuendelea kuamini kuwa tuko huru tu kwa sababu tuna bendera na rais. Uhuru ni uchumi, huduma bora za jamii, uwajibikaji na maendeleo.

Katiba huru itokanayo na wananchi huwapa jeuri na namna ya kuiwajibisha serikali na serikali huwajibika vilivyo kwao. Hii ndiyo siri ya nchi zilizoendelea kuwa na serikali zinazowahudumia wananchi zikiwajibika moja kwa moja kwao.

Na hii ndiyo siri ya serikali kwa mfano kwenye nchi za Italia na Japan kubadilishwa (kutimuliwa) mara kwa mara.

Ingawa Mkapa alisifika kwa kiburi na urushi, kwa hili nakubaliana naye na kumpongeza huku nikimpinga mzee Ali Hassan Mwinyi aliyekaririwa hivi karibuni akisema eti hakuna haraka kwenye kuandika katiba bali kurekebisha iliyopo.

Tutarekebisha hadi lini iwapo katiba yetu ni viraka vitupu na balaa kwa maendeleo ya taifa?

Turejee nukuu nyingine ya Mkapa: “Katiba ndiyo moyo wa nchi, moyo wa mwanadamu unaofanya mwili mzima ufanye kazi… hivyo kwa kuangalia mbele tunahitaji kuundwa kwa Katiba na mihimili yote ya nchi, tunahitaji Katiba huru itakayotulinda katika hatari.”

Mkapa alisema hayo katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Wanasheria wa jumuiya uliofanyika mjini Bujumbura nchini Burundi, Novemba mwaka huu.

Bila kuandika katiba upya tutaendelea kutapeliwa na watawala wababaishaji na mafisadi watokanao na uchakachuaji na jinai nyingine kama kuibia taasisi za umma ili kuhonga wapiga kura.

Lazima tuwe na katiba mpya inayotoa kanuni ya kutatua matatizo yetu na jinsi ya kutawaliwa. Tunataka katiba ambayo inatamka wazi kuwa rais wa Tanzania ni binadamu ambaye yuko chini ya sheria akiwajibika vilivyo kwa waliomchagua na wananchi kwa ujumla.

Tunataka katiba itakayoharamisha rais na wenzake kukataa kutaja mali zao au kuwa na mali zenye kutia shaka zisizo na maelezo kama sasa.

Tunataka katiba inayoainisha haki zote za mwananchi kwa usawa kabisa, katiba inayozuia israfu na ujambazi wa kimadaraka ambao kimsingi ndiyo chanzo kikuu cha umaskini wetu.

Tunahitaji katiba iliyokwenda shule kwa kuazima usemi wa vijana.

Kwa ufupisho tu, mambo tunayokosa kutokana na kutokuwa na katiba mpya itokanayo nasi-umma:

Hakika kwa katiba ya sasa ambapo baadhi ya watu wako juu ya sheria tena kikundi cha watu, umma unakosa haki ya kuishi maisha sawa na wao.

Rejea kwa mfano wanasiasa kujilipa mishahara na marupurupu makubwa kwa kutofanya kazi yoyote.

Wananchi wa kawaida hawana na hawapewi heshima hasa kwenye kuendesha nchi yao. Rejea kwa mfano, umma kulalamika watuhumiwa wakuu wa ufisadi kufikishwa mahakani na serikali-kikundi kidogo cha watu isifanye hivyo.

Uwajibikaji na uadilifu, kashfa zilizoingiza taifa kwenye umaskini kama Richmond-Dowan, EPA, IPTL, CIS, TICTS, SUKITA na nyingine nyingi ziliwezeshwa na katiba mbovu isiyohimiza uadilifu na uwajibikaji.

Uraia wa nchi mbili, wazalendo wamekuwa wakinywa na kuhofishwa kuwa na uraia wa nchi mbili huku wakihimizwa kuwekeza ndani. Ajabu tunao tunaodhani ni raia wenzetu wanaotii katazo hili wenye uraia wa nchi nyingi na si mbili tu.

Mfano, watuhumiwa wa ufisadi kama Sailesh Viran na wenzake wenye asili ya kihindi wasingekuwa na uraia wa nchi nyingi wangewezaji kutoroka toka nchini kirahisi?

Mwanya huu umetumiwa na mamluki na wakimbizi wengi wa kiuchumi wanaoshirikiana na watawala wasio waaminifu kutorosha raslimali na hata pesa zetu nyingi za kigeni bila kudhibitiwa wala kushughulikiwa huku tukishuhudia.

Tutafanya nini iwapo hatuna nguvu kikatiba? Hii ikichangiwa na katiba ya sasa kuwapa wanasiasa madarakana na kinga nyingi, ndicho chanzo kikubwa na ufisadi na umaskini wetu kama nchi.

Tumeona nchi jirani ya Kenya ambapo mawaziri wengi wamepukutishwa kutokana na katiba mpya ya Kenya kutamka wazi kuwa kila atakayeshutumiwa lazima achie madaraka ili achunguzwe na kuwajibishwa jambo ambalo hapa kwetu hakuna.

Kufutilia mbali ufisadi na unyanyasaji wa kitaasisi na mtu binafsi.

Hayo yote hapo juu hayahitaji mtu kuwa na shahada ya utawala wala utafiti kujua. Kila mtanzani anajua fika kuwa kikwazo chetu ni kutokuwa na katiba inayotokana na wananchi wenyewe kwa ajili yao.

Na kila mtu anajua nani anaiba nini wapi hata lini. Na hii ndiyo iliwezesha hata wabunge wa upinzani kuweza kuibua kila aina ya ufisadi kabla ya serikali ya sasa kuhakikisha hili halifanikiwi. Maana yake ni kwamba hata hata whistle blowers wakiwapelekea siri, bungeni watakumbana na kisiki tokana na kuondolewa kwa spika Samuel Sitta. Hii leo hapa si mahali pake.

Ingawa Mkapa alichelewa kuanza mchakato alipokuwa madarakani, aliyosema kuhusiana na kuandikwa katiba upya ni ya msingi na yapewe uzito na kufanyiwa kazi.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 22, 2010.

Madaraka hulevya kuliko hata ulabu

MWENZENU nimerudi wiki jana kutoka Ivory Coast au Cote d' Ivoire kwa wale wanaojua Kifaransa yaani nchi ya wale jamaa waliofungwa na vijana wetu juzi juzi tu na kuleta ujiko kwa wasioustahili yaani wanasiasia.

Wanasiasa walidandia ujiko huu wakati wao ndiyo kikwazo kwa ufisadi ujinga na usanii wao! Hayo tuyaache.

Nilikaribishwa kule kwenda kujaribu kusuluhisha mgogoro wa uchakachuaji ambao umeanza kuwa tatizo sugu na kansa ya kisiasa barani humu. Niliitwa kutokana na kaya yetu kuwa na uzoefu au tuseme ukondoo.

Maana kwetu tulipochakachuliwa, kwanza hatukuwa na marais wawili kama kule wala wachovu hawakuingia mitaani kama Cote d' Ivoire. Walevi huwa hawana taimu na mambo kama hayo bali kuuchapa ulevi. Pili tuliyamaliza kivyetu vyetu kiasi cha wenzetu kutamani nao wajue sayansi hii wasijue ni balaa na kiama cha jamii!

Pia nilialikwa kule kutokana na kaya yetu kuwa karimu kiasi cha kuwa inawazawadia hata matapeli njuluku kama ilivyotokea kwa Dowanis. Waivorien walisema wakimaliza aibu yao watakuja kuwekeza huku ili nao wachume na kufaidi pepo hii ya mabwege.

Leo sitaongelea sana mambo ya Ivory Coast kwa sana kutokana na kutimuliwa na waivorien baada ya kuwambia kuwa natokea Bongolala na siyo Bongo kama walivyodhania.

Walinipa laivu kuwa hawataki mtu wa kwenda kuwafundisha ukondoo na ubongolala ili hapa baadaye wachezewe kama tunavyochezewa na gendaeka wachache waliojipenyeza kwenye maulaji yetu. Walisema wazi kuwa hawakuhitaji mtu wa kuwakeketa kiakili wala kuwaingilia na kuharibu!

Sababu ya pili ni kugundulika kwa njama zangu za kutaka kumtetea Laurent Gbagbo kutokana nami kujua nisipomtetea wakati nilichakachukua ukuu wa kijiwe ingekuwa unafiki. Hivyo, jamaa walinistukia wakanizomea na kuniita Gbagbo wa Kijiweni huku Gbagbo akiitwa Jackalent Kikwegbo sorry. Naomba nisitaje jina jingine walilompa huyu mchakachuaji marhuni.

Ila walimpa sifa ya usanii mfu na nyemelezi vitokanavyo na ufisi na mawazo mgando.

Niliondoka pale Felix Houphet Boigny International Airport kwa aibu kabla ya jamaa yangu mmoja kunikaribisha kupitia kwake na kushuhudia maajabu karibu na yale yanayoanza kujipenyeza kwenye kaya yetu.

Kutoka huko nilipata mwaliko kwenda kumfunda jamaa mmoja mpenda madaraka aitwaye
Dk. Dk. Prof, Alhaj, Mtakatifu, Mtukufu, mhe. Mpendwa mnyenyekewa Mlambwa miguu. Kanali na makorokoro mengi, Yahya Jemus Jukung Jammeh. Jamaa pamoja na kujipachika vyeo na heshima zote hizo ni kihiyo kama jamaa yangu.

Nilitua Yundum Airport salama salimini na kuelekea kula mahanjumati na jamaa yangu huyu ambaye wengi humuona kama kihiyo tapeli na mchakachuzi wa aina yake. Nionye. Hii yandum haitokani na ndumu ya vichaa wangu wanayovuta ili waweze kuhimili mateso ya walaji wa Dowanis.

Huyu jamaa wengi humuona kama juha aliyekaa madarakani kitambo na asifanyiwe kweli.

Huyu jamaa ana nafuu kiasi fulani ikilinganishwa na ukihiyo wake. Siyo kama yule mwingine ambaye leo nitamhifadhi. Tena ni juzi tu tapeli mmoja aliyeshindwa maisha ughaibuni alimtungia kitabu cha kumsifu Jammeh wangu. Huu ndiyo huwa nauita usomi nepi mwenzenu.

Huku ndiyo kujikomba mithili ya changudoa au dungaembe. Huku mwenzenu niliona maajabu ya maajabu!

Jamaa kwa kupenda shahada za dezo na vyuo vya huko vilivyokuwa hovyo, kila chuo kinajikomba kiasi cha wasomi wake nao kugeuka vyangu wa kimaadili tena bila aibu ili kupata madili toka kwa bwana mkubwa mpenda makubwa.

Kila anapokatisha anapewa shahada. Kwangu hivi si vyuo bali vyoo vikuu vya maarifa.

Hata hivyo, sikushangaa sana baada ya shahada kugeuka upuuzi kiasi cha wapuuzi na matapeli kuzighushi na kuzitumia kiasi cha kushindwa kutofautisha kati ya wasomi na waganga wa kienyeji wapendao kujiita maprofesa wakati ukweli ni maprosoo watupu.

Jamaa anapenda dezo kama kapushimo la choo! Hebu katupe chochote uone. Angalau hata kapu na shimo la choo hutosheka, maana lau hujaa. Yeye hatosheki! Ni laana na ufisi kiasi gani?

Ila pamoja na tamaa za shahada na ujiko, rafiki yangu si kiruka njia wa kudandia kila tetea apitaye mbele yake kama jamaa yangu. Ana wake zake wawili, wote waarabu na vitoto vyao viwili.

Hana watoto wa kuokota au kubwagiwa mlangoni au wasiojulikana waliletwa lini. Ukimuuliza swali kuhusu familia yake hasiti wala kuona aibu anakupa jibu linaloingia akilini.

Vitoto vyake bado ni vichanga. Havina sifa ya ulevi wala kupenda kudandia madaraka yake navyo vionekane virais vidogo kama wengine. Kwa hili nimemsifu jamaa huyu pamoja na mapungufu yake.

Kitu kingine nilichogundua kuhusiana na jamaa huyu ni kupenda sifa. Kila tapeli humpa tuzo naye hukenua wakati anatumiwa. Si unajua tena NGO zilivyogeuka miradi ya wake wa vigogo. Lol! Ngoja niishie hapa bi mkubwa wangu asijeinyaka akanipa adhabu ya kudeki na kuosha vitoto.

Turejee kwa matapeli wanaozuga na tuzo uchwara. Anyways, wanatumiana. Si unajua matapeli walivyokuwa na urafiki na usuhuba wa mashaka? Usishangae kesho baada ya jamaa fulani kuondokewa na maulaji hata shoga yake Kagoda bin Dowan akampiga teke na kudandia mwingine atakayemweka mkononi. Kwani matapeli hawa wanaaminika?

Baada ya kuona jamaa anapenda tuzo, nimepanga, siku nikipata kurudi kule nimpelekee tuzo za uzembe, matumizi mabovu, ukabila, uchakachuaji, uzururaji, usanii, ufisadi, usiri, visasi na mengineyo.

Madaraka ya jamaa yangu yamempofusha na kumlewesha kiasi cha kutumiwa na kila tapeli na msaka, ngawira, cheo hata ujiko.

Si wasomi, hasa wale nepi na kanyaboya, wala majuha na matepeli wa kawaida. Wote wamemgeuza mradi wa mafisi na majuha na asikengeuke!

Wa kumtunuku shahada za uongo na ukweli, wanamtunuku na wa kumtungia vitabu na kuimba sifa za uongo wanafanya hivyo kwa namna yake na wakati wake na hastuki japo umma wamcheka kwa ulimbukeni na mapenzi ya dezo.

Jamaa hastuki bado! Amegeuka kokoro au tuseme kichwa cha mwendawazimu mchana kweupe! Ama kweli wahenga walinena. Madaraka hulevya kuliko hata ulabu hasa yaangukiapo mikononi mwa juha na limbukeni mufilisi!

Duh! Kumbe leo ni siku ya mgao (mdowan). Acha niwahi kununua mafuta pale nayo sijui kama hayajachakachuliwa kama sisi!
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 22, 2010.

Tuesday 21 December 2010

Fisadi wa rada Tanil Somaiya afanya kufuru IKULU

Je namna hii taifa letu ni huru kweli?


Ilikuwa ni siku ya Desemba 9, 2010. Tanzania ilikuwa inasherekea miaka 49 ya Uhuru wa taifa. Baada ya kukagua gwaride Uwanja wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete alifanya dhifa ya kitaifa Ikulu na kualika viongozi wa serikali, mabalozi, viongozi wa dini na wafanyabiashara wakuu.

Waalikwa wote, walikuwa wanaingia Ikulu kupitia mlango wa nyuma ulio karibu na bahari upande wa ferry. Lango kuu la kuingia Ikulu lilikuwa halitumiki kwa wageni siku hiyo na lilitumiwa na Rais na viongozi wengine wakuu. Magari yote, ikiwemo ya mawaziri na mabalozi yalipaki nje ya Ikulu kwenye uwanja mkubwa ulio karibu na ferry na wageni waalikwa waliingia kwa mguu kwenye viwanja vya Ikulu.

Mmoja wa wageni waalikwa mashuhuri wa Kikwete alikuwa ni Tanil Somaiya, mmiliki wa Shivacom Group of Companies.

Wakati mawaziri na mabalozi waliambiwa na maafisa usalama Ikulu watumie mlango wa nyuma wa kuingia Ikulu na kutembea mpaka kwenye gardens ambako sherehe ilifanyika, Tanil alipewa heshima ya kipekee na kuruhusiwa kutumia main entrance gate.

Tanil aliingia Ikulu na gari la kifahari jekundu (a red FERRARI) na kuipaki gari hiyo kwenye mlango mkuu wa kuingia IKULU ampako huwa gari la Rais ndipo linapaki.

Aliiacha FERRARI hiyo hapo kwenye lango la kuingia Ikulu kwa zaidi ya masaa mawili huku akijimwaga kwenye dhifa.

Mawaziri, mabalozi na vigogo wengine walibaki wamepigwa na butwaa iwaje wageni wote waambiwe waingie Ikulu kupitia mlango wa nyuma kwa mguu na kuacha magari yao nje halafu mfanyabiashara huyu apite main gate na kuweka gari lake kwenye main entrance ya lango kuu la kuingia Ikulu.

Tanil ni rafiki wa karibu na business partner wa Shailesh Vithlani, mfanyabiashara ambaye amekimbia nchi kutokana na kashfa ya rada.

Tanil, ambaye ametajwa kwenye WikiLeaks kuhusu rada, amehusishwa pamoja na Vithlani kwenye kashfa ya rada, military trucks, military choppers, Gulfstream presidential jet na scandal nyingine.

Inaeleweka kuwa Tanil alimchangia pesa nyingi sana Kikwete kwenye uchaguzi wa Rais uliopita na pia alitoa helikopta zake zitumike kwenye kampeni ya CCM, lakini hii ndivyo Ikulu ya Mwalimu Julius Nyerere inavyodharauliwa siku hizi?

Kwa kutumia main entrance na kupaki gari lake mbele ya lango kuu la Ikulu, Tanil alikuwa anataka kuwaonesha wageni wote kuwa yeye yuko karibu sana na Rais wa nchi na Ikulu ni kama nyumbani kwake.

Mbaya zaidi, kufuru hii ilifanywa siku ambayo Tanzania inaadhimisha uhuru wake. Kuna uhuru kamili kweli kama watuhumiwa wakubwa wa ufisadi wanafanya kufuru namna hii mpaka IKULU?

Unatarajia kweli Edward Hoseah wa PCCB anaweza kuondokana na uoga wa kumkamata Tanil kwa ufisadi wa rada wakati Rais wa nchi ni besti wake na Ikulu ni kama playground yake?

Naiweka kama ilivyotumwa na mdau.

Monday 20 December 2010

Je ingekuwa kweli dunia ingekuwaje? Tafakari




Je hayawani huyu kweli angepata bunduki angelipiza kisasi kwa wanaomuweka kwenye orodha ya viumbe walio kwenye hatari ya kutoweka? Je angeitumia kihayawani kama binadamu au kibinadamu kama hayawani? Je angeitumia kibinadamu japo hayawani? Je yawezekana siku moja hayawani akawa na uwezo na akili ya kumudu zana hii? Je ingekuwa kweli dunia ingekuwaje? Hivi huyo jamaa hapo juu na akina Laurent Gbagbo,Robert Mugabe,Saddam Hussein, Omar Bashir na wengine kama hao nani bora?

Saturday 18 December 2010

Gbagbo should nary be allowed to shed innocent blood



Current goings-on in Ivory Coast are painting but a dour picture. Reports are coming out that confrontations have taken place as patience and reasoning escape. Tens are reported killed. Everybody that cares is worried about what will be the end outcomes of all this instability and impasse.

What astonishes beyond imagination is the indifference of world leaders have displayed. They have said a lot but did nothing.

We understand: UN and the United States of America, among big entities recognized president -elect, Allasane Ouattara. But is this enough to dissipate the impasse Ivorian are in? Is this enough in itself or something else needs to be done urgently? What is the logic behind recognizing the person that has no full control over the country he's elected to man?

We heard ECOWAS announcing suspending Ivory Coast's membership whilst UN stood to guard the new government. Is this enough really? Why suspending a country in lieu of suffocating one morose criminal?

While all these braggadocios are going on, the defeated ruler, Laurent Gbagbo is tightening his grip on power asking for talks. No window should be offered for any negotiations otherwise they mean a loophole for Gbagbo to relinquish power.

While feet dragging is going on, Gbagbo is ordering his army to shoot demonstrators. He's assaulting even a few UN units guarding legally elected president! He's illegally running his government. Moreover, he regards himself president despite knowing he lost elections he prepared and manned himself.

When one looks at the responsibility the US has always assign to itself vis a vis defending democracy, one wonders. Why was it possible for it to topple tyrants such as Manuel Antonio Noriega (Panama) and Saddam Hussein (Iraq) but the same fails to do so to Gbagbo? Hither is whither the whole issue of racism comes into the big picture.

Looking at what is going on in Ivory Coast one asks himself or herself. How many innocent people should be butchered in the quest of defending their constitutional rights and the country whilst the 'champions' of democracy sit aside and look? When will the world community act decisively and sensibly?

Why is the international community dragging feet whilst innocent people are suffering and dying in the hand of a self seeker? Is it because it is Africa? Isn't this international racism and indifference altogether?

When Serbian butcher, Slobodan Milosevic started killing innocent people of Kosovo descent , EU under NATO auspice didn't sit and watch. They decisively and timely intervene and neutralized the terror. What's it that is hampering all this to be applied on Ivory Coast? Is it because it is Africa?

Nobody should tell me that African Unity will address and arrest the problem whilst it squarely failed to intervene in Zimbabwe and Sudan where it has always stood by dictators in these country. In other words AU is the part of the problem.

Inverting militarily and otherwise is sine qua non. This becomes even more crucial in order to discourage other potentates that are currently watching closely as they contemplate doing the same in order to cling unto power. Therefore, my shew stone tells me that taking on, and thus, eradicating Gbagbo will send a clear signal to these tads in power.


More so, intervention will avert more bloodshed and more damage on brittle economy of Ivory Coast that resulted from a decade misunderstanding and division.

So too, intervening will minimize or curtail other losses the country is likely to suffer shall this wino be left to execute his nugatory manoeuvres.

More on this, intervention will avert the danger of the crisis to spew in other countries in west Africa and thus destabilize the region. Refer to allegations that Ouattara is allied with Bukinabe he has been branded to be his mother land. This anomaly started with Henri Konan Bedie who in 1999 alleged that Ouattara was a Burkinabe though this was strongly refuted by president Blaise Compaore who was quoted as thus: "For us things are simple: he does not come from Burkina Faso, neither by birth, marriage, or naturalization. This man has been Prime Minister of Côte d'Ivoire."

This bulimia has always been the take of Gbagbo and his people. If Ouattara is not an Ivorian then why did they allow him to hold high office and run for presidency? This is but hogwash so to speak.

Also refer to what is currently going on in East Africa after Somalia was let to fail. Light arms are currently a menace in the region not to mention piracy, human and drug trafficking, money laundering and what not.

Another player that can chip in to help in easing the tension is the International Criminal Court (ICC). Given that some innocent people have already been killed under the order of Gbagbo, it makes more sense for ICC to start indicting Gbagbo. The pressure thereof is likely to shake him off and discourage his machinations and ambitions to cling unto the office of president.

Source: The African Executive Magazine.

Wednesday 15 December 2010

Wikileaks: Wicked or Hallowed?



The world media is currently awash with sensitive, sensationalized and classified information. Many 'unknowns' are now known. Politicians, especially from 'civilized and developed world' and those from 'wicked and doomed world', have though in different taste and manner, their dirty linens in the agora where every eye can see and tongues wag.

Many, especially, from the establishment, are vehemently condemning Wikileaks’ founder and his team. Some suggest that Julian Assange, the founder and boss of Wikileaks, should be treated as a terrorist thanks to his exposing the rot the high and mighty have been committing for long! What all protagonists don't dispute is the truth of what is released.

US Foreign Secretary Hilary Clinton was recently admitting the dirty job ambassadors have been doing thus: "the illegal publication of classified information poses real concerns and even potential damage to our friends and partners around the world." Who is causing this danger between the one reporting the goings-on behind the curtains and the one that commits those dangerous things for the world?

Some say: what Wikileaks is doing is dangerous to world security. They may be right. But again, what Wikileaks does is telling the high and mighty to do their business decently and safely for the world. Others say: what Wikileaks is doing is honorable and decent job that aims at keeping rulers of the world honest. Who is right and who is wrong depends on how one looks at this hidden world of politicos.

In a word, the writings are on the board that when we do dirty things, others will do clean and right thing to expose our rot. Thus, who is to blame in the first place?

Another interesting thing is the fact that the role of ambassadors has been reduced to tittle-tattling and the likes thanks to the contents of what they send back home as they report. True, thanks to the leaks, a new face of ambassadors that was not known to the world is known-they are not emissaries but legalized spies who can spy any aspect of their host countries including trivial matters such as who sleeps with the president. Refer to the voluptuous Ukrainian nurse that Libyan strong man likes to be by his side wherever he goes.

This being the fact, currently, some of us look at ambassadors as menacingly hypocritical creatures in two ways. Likewise, even some of our rulers are as hypocritical and double faced just like their emissaries. Who would think that the Saudi King would hate Iran even more than their sworn-and-made enemy Israel? Who would risk thinking that the US ambassador to Kenya would dress Raila Odinga and Mwai Kibaki down whilst in public these are the guys he has always commended for ushering the new constitution in? Hither the problem is the fact that ambassadors report truth back home as they tell lies to their hosts in order to win them.

What is the upshot of all this? The Swahili have a saying that your arch enemy is the one that you share table with. So, all compliments our rulers hear from lip servicing lips of diplomats and use them boldly to evaluate their successes are but mere mealy-mouthed- daylight lies so to speak. Ambassadors know how corrupt and inept our rulers are. They want this be known home in order to be used to fix them though the same don't help the Wananchi to dispose the same!

Ambassadors, in this respect, are spies as well as burden to our budgets thanks to spending millions just for gossiping, spying or keeping mum especially those from dependent and poor countries. Do such cabal of government machinery hell bent to spy and sting on others deserve the high place they have always enjoyed?

What Wiki-leaks has fed the world of media wolves shows that ambassadors are spies per se. Is this the reason why everything diplomatic is kept secret not to mention preference in our points of entry? We used to hear of some arrests of ambassadors and diplomats involved in some illegal dealings such as arm-dealing, smuggling in some cases and what not but not spying and gossiping.

We heard of what diplomats from the west say and report about our rulers. What of our own counterparts? Does it mean that we differ when it comes to understanding the role of the ambassadors we dispatch to other countries or we have nothing to spy on? I am anxiously waiting to hear what our diplomats report home from Washington, Paris, London, Brussels and what not.

Looking at the tittle-tattle spying Wikileaks unearthed, Africa is more of a prey than a predator. In other simple words, Africa is taken for a ride and still, our rulers cannot underscore this!

What pains beyond comparisons is the fact that the same informers we hold high are the same creatures that laugh and rub shoulders with our high and mighty free and often so as to stab them on the back. Will our rulers come of age by looking at western ambassadors like spies instead of anything more or less in this matter?

Some bad things may have good things with them. At least our rulers that have ignored those that voted for them as they adore the donors can now see how they have always goofed. They can see how other people see them and use them. For this reason, what Wikileaks is doing is a noble job-keeping tabs on politicians.
Source:The African Executive Magazine Dec. 15, 2005.

Hujuma kwa TANESCO ni ukombozi?



WATANZANIA, tofauti na mataifa mengine, tunasifika kwa ujinga ambao watawala huuita upole na kuthamini amani. Watawala huutumia ukondoo huu kujifanyia wanavyotaka kubwa likiwa ni kushiriki kutuibia bila kuchelea lolote. Jingine ni kutumia vibaya muda na pesa yetu bila kuchelea lolote pia.

Wanakwenda mbali hadi kufikia hata kuchakachua kura zetu nasi tusifurukute. Si umma wala upinzani. Nani hajui kuwa matokeo ya uchaguzi uliopita yalipikwa na Tume ya Uchaguzi ikisaidiana na Usalama wa Taifa kama walivyodai CHADEMA.

Serikali haikukanusha. Hii maana yake ni kwamba madai haya ni ya kweli tupu.

Baada ya uchaguzi kuchakachuliwa na kura kuibiwa, wengi walidhani lau watanzania wangeamka na kudai haki yao yaani uamuzi wao kikatiba kuheshimika. Hawakufanya hivyo! Na pale walipotaka kufanya hivyo, wanasiasa waliwashauri vinginevyo kwa kisingizio cha kulinda amani. Amani gani katikati ya dhuluma ya wazi?

Kabla ya muda kupita, ilifumka kashfa nyingine yaani Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) kuamriwa kulipa shilingi 185,000,000,000 kwa kampuni iliyoingia nchini kwa utata mtupu ya Dowans ambayo ni mtoto wa kampuni nyingine tapeli iliyotimuliwa ya Richmond LLC.

Wengi walidhani, kipindi hiki, Watanzania lau wangetoka kwenye lepe lao la usingizi. Kadri mambo yanavyokwenda, hawataamka zaidi ya kuendelea na ‘business as usual’ ya kulalamika bila kuchukua hatua.

Hata hivyo, kuna mabaya yanayoweza kuwa na mema. Kuoza ni kitu kibaya. Lakini bila mbegu kuoza haiwezi kuota na kuchipua. Bila tofali kuchomwa haliwezi kuwa imara. Tunadhani sasa watanzania wataanza kuonja joto ya jiwe la ufisadi wa kimfumo kiasi cha kuanza kufikiri kuamka.

Kwa msingi huo, ni imani yetu kuwa kama wizi huu wa kimfumo utaendelea kubarikiwa na kuendekezwa na kufanikiwa, maumivu yake yatawagusa wananchi kiasi cha kuondokana na usingizi wa pono. Hivyo basi, wanaolitakia taifa hili mema, waombe hawa mafisadi lindwa na shawishi walipwe hadi TANESCO ifilisike na kushindwa kutoa umeme tuona kama watanzania wataweza kuendelea kuvumia kuishi kizani kama mende.

Bahati mbaya sana, watawala wetu walishajenga imani sugu kuwa watanzania hawawezi kuamka kutokana na kushinda jaribio la kuwalazimisha kuishi kizani kwa mwaka na wasichukue hatua. Je watanzania wataendelea kulala wakati mabalaa yanaongezeka? Hili ni swali gumu kujibu.

Kitu kingine kinachosikitisha ni ukweli kuwa, kama alivyosema Spika wa zamani wa Bunge Samuel Sitta, wezi hawa wanatafuta mitaji ya kisiasa. Hii maana yake ni kwamba walioko nyuma ya hujuma hizi wanataka kupata pesa ya kutuhongea sisi wale wale ili waendelee kutula.

Je, tutaendelea kuwa mataahira na panya kiasi hiki? Je tutaendelea kuridhia kuwa kama samaki kwa kulishwa utumbo wetu na kukaangwa kwa mafuta yetu? Samaki ni hayawani. Je twafaa kuwa kama hayawani wakati tu binadamu?

Hakuna ubishi. Amani ni muhimu na lazima. Lakini amani gani inayolinda dhuluma na nakama? Haiingii akilini kulinda amani kwa kujidhuru. Ni mpumbavu gani atafuga wezi nyumbani kwake eti kwa kuogopa kuvunja amani kwa kuwapeleka polisi au mahakamani? Hii si amani ni utaahira. Hii huwa mbaya vitu hivi vinapogeuka mfumo tena hai badala ya kufishwa kwa gharama yoyote hata kwa kuikosa amani lakini haki ikawapo.

Tuombe Mungu watawala wetu wazidi kujiaminisha kuwa wataendelea kuvurunda bila kukamatwa. Mwisho wa jinai hii ni mateso kuuzidi umma nao ukaamka na kujikomboa kwa kuwafurusha toka madarakani.

Hata nchini Romania wakati wa imla Nicolae Causescu hali ilikuwa mbaya kuliko hapa. Mfano wa karibu ni Zaire ya zamani ambapo jambazi Joseph Desire Mobutu aliigeuza nchi kuwa shamba lake la mifugo. Lakini umma ulipochoka kilichotokea inabaki kuwa historia.

Je, hujuma dhidi ya mali na raslimali za taifa inayosababisha umaskini na mateso makubwa kwa jamii inaweza kuwa chemchemi ya kujitambua na kuleta ukombozi wa taifa? Adui yako muombee njaa kwani itamtoa usingizini akahamanike kuondosha njaa.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 15, 2010.

Nimeunda serikali ya ujanja wa kitaifa

Siku hizi nyumbani kwangu kumezuka balaa ambapo kuna dini na vyama tofauti. Hapakaliki wala kulika kitu bila kuonyeshana ubabe na sura za minuno na mibeuo. Kuna Chama Cha Mama (CCM) na cha Concubine Ushered into Family (CUF). CCM ni cha Bi mkubwa wangu na CUF cha Nyumba ndogo. Niwaonye wasomaji kwanza. Msijechanganya hivi vyama vya nyumbani mwangu ni vile vya kaya yenu hata kama vinafanana kwa majina sifa hata majaliwa.

Nimekuwa, kwa kitambo kirefu, nikisikia umbea wa wagombea wakinigombea wapate ulaji. Japo hatukufanya uchaguzi kwa kuogopa kumwagia maji ya moto na michuzi ya chapati, nimeamua kuunda serikali ya ujanja wa kitaifa (familia). Sitaki wala yanikute yatakayowakuta maharamia kama Laurent Gbagbo wa kule nonihino.

Narudia tena kwa herufi kubwa. Vyama hivi havina uhusiano na vyama vya kisiasa vya nchi yoyote juu ya uso wa ardhi na chini ya jua. Na isitoshe hakuna aliye na hati milki ya kutumia vifupisho husika hata vikifanana. Kwa vile mie ni profesa wa sheria, sina shaka na hili na sijavunja sheria ya nchi yoyote. Hata nikivunja sheria, nitakwenda kwa wale wataalamu wa jinai walioghushi vyeti vya kitaaluma na bado wakateuliwa kuula. Hawa wakishindwa nitakwenda kwa wale majambazi wa Downwans wanipe mbinu ya kuchuna buzi bwege kwa kutumia sheria kama walivyowafanyia jamaa wa Mizengwe.

Tuendelee. Ukiangalia sifa za vyama husika, unaweza ukaona ushindani na mikakati ya kumalizana vilivyo vya hali ya juu.

Baada ya kuona mashitaka na lawama haviishi nimekubali yaishe kwa kuweka silaha chini na kukubali kushindwa hasa baada ya mjumbe kutishia kunifikisha kwa mtendaji wa kata.

Kwangu mtendaji wa kata anatisha kama The Hague na ICC yake kwa serikali mbovu za kiswahili. Isitoshe baada ya kuona kule kwa kina madevu wanawekana sawa na serikali za ujanja wa kitaifa kwanini nami nisiige mfano bila kujali kuwa kuna watu watadhulumika na kuudhika? Hapa unachofanya ni kuwapa ulaji viherehere wenye kufikiri kwa kutumia matumbo yao kama jamaa zangu wa kule Zaainzibaa.

Nimeamua kuunda serikali hii haraka. Nafanya hivyo kwa kujua kuwa nikiendelea kuuchuna wale jamaa wa wikileak wanaweza kunivua nguo bure. Isitoshe wakieleza jinsi nilivyolazimishwa na homa na hofu ya The Hague nitakuwa nimeumbuka mzee mzima.

Turejee kwenye serikali ya ujanja wa kitaifa ambayo ni janga kwa bi mkubwa na vitegemezi vyetu.Muathirika wa kwanza ni bi mkubwa mwenyewe mama Kapayukaji almaaruf mama Kidume. Ameathirika sana baada ya mamlaka yake kuyapiga upande na kuwapa nyumba ndogo kama walivyofanya kina Madevu baada ya kusikia kuwa madevu mwenzao aitwaye Mureno Okampo alikuwa akiwanyemelea na kuwapeleka alipompeleka Chaz Teila.

Hii inaitwa umoja wa kitaifa ambapo haramu na halali huwekwa kapu moja. Kwa lugha nyepesi ni kwamba unaharamisha halali na kuhalalisha haramu. Hii haina tofauti na nilivyofanya kwa kuhalalisha nyumba ndogo na kuharamisha uhasama wa nyumba kubwa kwa nyumba ndogo.

Hebu niike hivi. Kama ni kwenye utawala wa kaya, unaandaa uchafuzi na kutumia pesa za walevi. Wanajipendekeza na kuja kwenye vituo vya kupigia kula wengine hawakuti majina yao na wakiyakuta wakapiga kula unachukua unaweka unachakachua waa. Kwani haya hayapo hata kama tunafungana kamba kwa kisingizio cha amani uchwara ya watu wala watu kuwala watu kwa sanaa hii? Soma taratibu bi mkubwa asikusikie akanivisha gagulo. Ukweli ni kwamba mzee mzima nami nimechakachua kinamna.

Wajua ni kwanini naogopa bi mkubwa asikusikie? Siyo tu atanivisha gagulo bali anaweza kunidai fidia ya mabilioni kama wale wezi wa Downwans walivyowaingiza mkenge mabwege fulani. Naogopa madai kama yule mama kachangu na kadungaembe ahubirie maji akanywa mvinyo. Si mnamjua mama huyu tena mbung'o wa kuteuliwa ambaye neno mume wangu kwake ni msamiati mugumu? Hayo tuyaache. Astaghafillullahi nshajitia nuksi kwa kumjadili nuksi huyu. Kwa jina la baba na la mama na la bibi na roho mtakakitu usiamini.

Tuendelee na serikali yangu ya ujanja wa kifamilia sorry taifa langu. Kama hujui ujue. Kutawala na kuwala walevi ni raha na mchezo japo mchafu lakini wa kufurahisha. Ili kuwaweka sawa waathirika wa sanaa zangu ambao ni bi mkubwa na vitegemezi vyetu, nimewafunga kamba kuwa muafaka na kuunda serikali ya ujanja sorry, ya umoja wa kaya ni cheche na chemi chemi ya maendeleo amani na mshikamano. Nao bila hata kufikiria wameshikilia sanaa zangu! Ukitaka kujua nimaanishacho nenda kawaambie ukweli kuwa nimewaingiza mkenge kwa maslahi yangu, watakunyotoa roho bure.

Maskini hawakujua kuwa nimefikia nilipowafikisha kwa sababu kuu mbili yaani kumuogopa Mureno yaani mtendaji wa kata na kulinda ulaji wangu. Ukisikia uchakachuaji wa kisasa na kisasi ndiyo huu.

Zamani kwenye kaya yangu hatukuwa na makamu wangu wala kitu kama hicho. Kwa sasa wako wangapi? Wako wabee au wawili kwa wale wasiojua lugha za kisasa. Baada ya kuwapa ulaji hawa waliokuwa maadui sasa mambo ni mswano.

Siwezi kumaliza stori hii bila kuelezea balaa linaloninyima usingizi. Baada ya kuonja raha na maisha kwa maana ya maisha, sasa eti walevi wa nyumbani kwangu wanataka katiba mpya itakayoninyang'anya ukuu na utukufu wangu. Kwangu niko juu ya sheria jambo ambalo linanifanya niwajibike kwa tumbo langu na nyumba ndogo zangu nyingi. Sasa walevi wangu wamehanikiza kutaka kunitungua kwa kutaka katiba mpya ya kaya. Sina ujanja. Niko kwenye mchakato wa kukubaliana nao kabla siri zangu nyingi hazijafichuka.

Napanga kukubaliana na madai yao. Kwa sababu nikikataa wakaanza kumwagiana mitusi ngumi hata michuzi, Mureno wangu ambaye ni afisa mtendaji wa kata anaweza kunipeleka lupango kwenye ofisi yake ambayo huwa napenda kuiita The Hague. Mie nimeamua kuwa mkweli, kubadilika na kujifunza kusoma alama za nyakati kabla ya kupitwa na wakati hata kama nikiamini katika uchakachuaji. Najua fika. Uchakachuaji si sayansi ya kudumu bali kujidanganya tu. Wenzangu na mie walioko juu mwaambwa. Mkizidi kujifanya mwajua mtaishia pabaya. Mie simo.

Naona wale wana harakati wa kudai katiba mpya wanakuja. Ngoja nijikate kislesi wasijenibana nikajinohino kwenye msuruali wangu. Usimwambie mtu.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 15, 2010.

Tuesday 14 December 2010

Zuma amshitaki mchora vibonzo




Nchini Afrika Kusini hali si shwari. Tuhuma za ubakaji na ufisadi zinazidi kumuandama rais Jacob Zuma. Jinamizi la kashfa za Zuma lilifufuka hivi karibuni Zuma alipoamua kumshitaki mchora vibonzo maarufu nchini mle, Jonathan Shapiro.

Kibonzo cha Shapiro kijulikanacho kama Zapiro hapo juu kilitoka miaka miwili iliyopita kikionyesha jinsi Zuma alivyotumia madaraka na ushawishi wake kuzima haki za mwanamke aliyedaiwa kumbaka.
Je hatua ya Zuma inaimarisha au kudhoofisha uhuru wa vyombo vya habari? Je Zuma ataendelea kuitumia mahakama iliyojaa wateule wake kuendelea kuukimbia mzuka wa jana yake? Hadi lini?

Pamoja na kudaiwa jumla ya $ 731, 000 kama fidia, Shapiro anasema kupitia wakili wake:"Nadhani rais ameshauriwa vibaya. Watakachofanya yeye na timu yake ni kurejesha kesi hii kwenye jicho la umma."

Alikaririwa akisema Eric van der Berg anayemtetea Shapiro na gazeti la Sunday Times. Je Zuma ataendelea kujivua nguo mwenyewe au kunywea? Time will surely tell.

Monday 13 December 2010

Barua kwa rais Jakaya Kikwete




Ndugu rais,

Samahani sitatumia neno mheshimiwa kutokana na kutolipenda ukiachia mbali kuchukia tabia ya kujikuza na kuabudiwa.

Wala sitakuita daktari bali kanali mstaafu kwa vile udaktari wako ni wa heshima tu.

Kwanza, nikupe pole kwa 'kuchaguliwa kwa kishindo' ingawa si cha Tsunami kama ulivyoahidi, bali cha uchakachuaji. NEC imekuangusha hata taifa. Maana uliotuahidi kishindo cha Tsunami, tunaona kama hukutwambia ukweli.
Naomba niwe mkweli kwako kusema yafuatayo:

Kwanza, sikukupigia kura kutokana na kutoridhishwa na ahadi zako nyingi juu ya nyingine lukuki ambazo hukutekeleza hata moja. Wabaya wanasema: maisha bora yamekuwa ni walio karibu nawe tu.

Pili, ni kutokana na kutowahi kusikia ukiongolea sera zako.

Sababu nyingine iliyonikera ni wewe kukacha mdahalo.

Tatu, marafiki zangu wengi hawakupata hata hiyo fursa ya kupiga kura kutokana na kufanyiwa mchezo mchafu na tume ili kushindisha chama chao.

Nne, kwenye jimbo moja anakotokea rafiki yangu, Tume yako ya Uchaguzi ambayo wabaya wako wanaiita tume ya Uchakachuaji ilitangaza mgombea wa CCM kuwa mshindi ingawa alishindwa wazi kabisa. Na haya ndiyo madai ya majimbo mengi nchini. Hii maana yake ni kwamba NEC imewabambikia wawakilishi wananchi. Na hawa licha ya kutokuwa chaguo la wananchi bali tume, hawawezi kuwawakilisha wananchi wala kuleta maendeleo.

Tano, japo mie si mwanachama wa chama chochote , naungana na wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutokutambua kama rais wangu hata kama utaendelea kulazimisha kunitawala-si kuniongoza. Maana viongozi waliondoka zama za Nyerere. Ukitaka niachane na msimamo huu, kaa kwenye meza ya duara uongee na hawa unaowaona kama adui zako ingawa naamini siyo. Shukuru Mungu una bahati sana ndugu rais. Hivi kama wangeingia mitaani ungefanya nini wakati huu Mahakama ya Jinai ya Kimataifa (ICC) Ilipotandaza nyavu zake barani tena pale nchi jirani ya Kenya?

Japo Chadema wamenyamaza, usijidanganye, ni wanasiasa kama wewe. Ukiendelea kuwazungusha, watabadili lugha na mikakati toka ile ya kuwataka wananchi wawe watulivu na kuwaambia wakaichukue haki yao. Hapa ndipo mapambano hayataepukika. Na yakitokea mapambano, amini mtaishia The Hague.

Pia wananchi wanaweza kupuuzia ushauri wa Chadema wa kutulia wakaamua kutafuta haki yao mitaani. Maana kama ni kupigwa mabomu ni wao waliopigwa mabomu na kunyang'anya ushindi wao na isitoshe wao ndiyo wanaathirika sana kuliko hao wanasiasa. Wazungu hupenda kuweka plan B.

Nawe yapasa uwe na plan B kama ambavyo wananchi pia wanaweza kuwa na plan B.

Tusidanganywe na amani tena ya uongo. Amani gani iwapo matokeo yanatangazwa kwa mabomu ya machozi na utata? Hakuna nchi ilisifika barani Afrika kuliko hata Tanzania kama Ivory Coast. Sasa iko wapi? Je kuna haja ya kwenda kule? Tusijidanganye kuwa kuna amani na mshikamano. Mshikamano gani iwapo kuna wabunge na watu wasiomtambua rais ukiachia mbali waliolazimishwa na tume? Mshikamano gani wa kudanganyana na kuchuuzana tena mchana kweupe?

Tano, japo mie si mshauri wako, naomba nikushauri. Juzi nilishuhudia kitu cha kutia aibu na ghadhabu ambacho kilipunguza heshima na uzito wako. Japo ni haki yao kidemokrasia, wabunge wa Chadema, si haba, wamemekudhoofisha hasa ikichukuliwa ulivyoingia kwa mbwembwe na kishindo mwaka 2005.

Nisisitize. Ni aibu na pili ni pigo la aina yake kwa taasisi ya urais. Hauna tena uzito na heshima ya pekee kama ilivyokuwa awali. Ukichanganya na tuhuma za ufisadi ndiyo usiseme.

Sasa ndugu rais nisikucheleweshe. Naomba nikupe somo toka visiwa vya Zanzibar ambapo kwa miongo zaidi ya miwili tulishuhudia mvutano na heka heka hadi damu kumwagika. Chama cha Wananchi (CUF) kilishikilia ngangari dhidi ya ngunguri hadi sasa kinaanza kueleweka hasa baada ya kuingia maridhiano na hofu ya CCM ya kumwaga damu na kupelekwa The Hague.

Je ndugu rais unashindwa nini kukaa meza moja na Chadema na kumaliza tofauti zenu ambazo kimsingi zimesababishwa na wizi wa kura au uchakachuaji ambao Chadema wanasema ndiyo siri na mtaji wa ushindi wako?

Ndugu rais, dunia nzima sasa inajua kuwa rais wa taifa lililosifika kwa amani ametokana na wizi wa kura. Nashangaa sijawahi kusikia ukikanusha. Si wewe, wasaidizi wako wala chama chako! Sijui hawa mabingwa wa propaganda uzushi na uongo tuliowaona kwenye kampeni kipindi hiki wameishia wapi? Na je wanalipwa kwa lipi kama wanashindwa hata kutoa msimamo wa chama au wewe kama taasisi yenye mamlaka nchini?

Ndugu rais nilikusikia juzi Dodoma ukiwashushua Chadema kuwa hawana rais mwingine isipokuwa wewe na hawana mtatuzi wa matatizo yao isipokuwa wewe. Hii ni kweli. Lakini kama utashikilia mipasho kama jamaa yako komandoo wa zamani wa Zanzibar hutafika mbali.

Kwanza, uchumi wa nchi umo kwenye chumba mahututi ukiachia mbali ripoti ya juzi ya umoja wa mataifa ya maendeleo kuanika uoza wa ajabu. Kwa ufupi ni kwamba ripoti tajwa ilizima tambo zote za kuleta maisha bora kwa watanzania. Sana sana, ukisoma kashfa zinazoanza kuibuka kwa mfano za unyakuzi wa ardhi ambazo zinamhusisha mwanao na asikanushe, waliopata maisha bora ni wale wa nyumbani kwako na marafiki zako.

Na hii ndiyo siri ya watanzania kukupa kura kidogo. Hili nalo ni pigo na tusi kwa mtu aliyeingia akijinakidi kama chaguo la Mungu na watu. Hivi kweli bado wewe ni chaguo la Mungu? Je wale wasaka ngawira na waramba viatu walioandika hata vitabu wakijua fika wanakudanganya, wanajidanganya na kudanganya bado wanakufaa?

Hivyo basi, kama ikitokea mkaendelea kuvutana, kuzungukana na kuhadaana, uchumi wetu na wananchi vitaathirika na kuanzisha fujo.

Naomba nimalizie na jambo moja. Bila kutenda haki ikaonekana ikitendeka, mgomo wa Chadema na hatua nyingine zinazoweza kufuata, vitaua dhana nzima ya amani na utulivu ambavyo wahalifu wengi wanapenda kuvitumia kuwatishia watanzania. Bila haki hakuna amani na amani haiji bali kwa kutenda haki tena kwa wote.

Mwisho, nasikia eti kampuni ya Dowans ni yako, Edward Lowassa na Rostam Aziz?
Kila la heri ndugu rais.
Chanzo: Dira ya Mtanzania Desemba 13, 2010.

Sunday 12 December 2010

Nukuu za gwiji je wewe unasemaje?



Gwiji letu leo ni profesa Issa Shivji.

"Tanzania hatuna wanasiasa bali kuna wapenda madaraka kwa kuwa wanapenda madaraka, basi wanakimbilia huko nawashauri wananchi kungalia hilo."



"Siku moja aliulizwa swali moja la nani anafaa kuwa kiongozi bora, Mwalimu Nyerere alijibu kuwa 'kiongozi bora ni yule ambaye hataki kuwa kiongozi, lakini analazimika kuongoza kwa kuwa hataki wapumbavu watawale."

Thursday 9 December 2010

Je ni kweli Makinda amechongwa na kusimikwa na mafisadi?





Kuna tetesi zinazunguka kuwa spika wa Bunge Anne Semamba Makinda ni chaguo na zao la mafisadi. Tetesi hizi zinazidi kupasha kuwa Makinda alipachikwa na mitandao ya CCM ya kifisadi na akajirahisi na kukubali kutumika kulipizia kisasi kwa spika aliyemaliza muda wake Samuel Sitta.

Kimsingi waliolipiza kisasi kwa Sitta hawakufanya hivyo kwa Sitta bali taifa. Maana kama siyo kulenga kulidhoofisha bunge na hoja zinazoiumbua serikali, basi wamelenga kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Hapa bila shaka, hawakutaka mtu anayeweza kuruhusu bunge hata kuridhia uandikwaji katiba mpya ambayo ndiyo nyenzo ya kutupatia serikali makini, safi na yenye visheni. Je mkakati huu utashinda? Je umma unaoathirika na siasa na serikali za majaribio utaendelea kufumbia macho genge hili ukiachia mbali madhira mengi liliyokwisha kuusababishia?

Pia huu ulikuwa mwanya wa pekee wa kupambana na uchakachuaji tulioshuhudia kwenye uchaguzi uliopita. Hivyo basi, hii maana yake ni kwamba 2015, kama mkakati huu utafanikiwa, tutaona mengi ya kuchusha na kukera kiasi cha kujikuta kwenye machafuko. Hapa ndipo waliosuka mkakati huu hawakuona mbali.

Si hayo tu. Shutuma hizi, licha ya kumdhoofisha, zinamuondolea udhu na imani ya wananchi spika Makinda.

Je tetesi hizi ni uongo au za kuweza kufutika chini ya busati au kufanyia kazi? Je tetesi hizi zaweza kujifia hivi hivi? Je tutegemee nini toka kwa mtu wa namna hii?

Kutokana na uzito wa asasi anayoongoza, kuna haja ya Makinda kujitokeza na kuua uvumi huu. Je ni kweli Makinda alipitishwa na waliompitisha ili kumkomesha Sitta? Je kama ni kweli, huu si ushahidi wa udhaifu wake kuwa anaweza kumtumikia kila kafiri ilimradi apate chake? Je kwa nafasi yake nyeti hivi hii inamwacha kwenye hali gani zaidi ya kumpotezea heshima na imani toka kwa umma?

Makinda anaweza kuwa na sifa zote za kuwa spika. Ana uzoefu tokana na kuwa mbunge kwa muda mrefu ukiachia mbali kuwa naibu spika. Anaweza kuwa na nia nzuri na taifa. Lakini yote haya yanamomonyolewa na madai kuwa alichomolewa huko aliko kuwa kuja kutumikia mafisadi katika kuwalinda na kulipiza kisasi kwa wabaya wao. Huu bado ni mchezo mchafu hata ungepewa msamiati mzuri vipi utabakia kuwa mchezo mchafu. Hapa ndipo Makinda anapaswa kuja na kuueleza umma kuwa yeye si chaguo la mafisadi bali CCM katika ufunuo wake mpya wa kuwajali kina mama.

Makinda, kama kweli hajachomolewa alikochomolewa na kutumika kulipiza kisasi, ajitokeze basi ajitetee na kutoa msimamo wake. Na katika kufanya hivi atoe majibu yanayoingia akilini badala ya kupiga siasa kama walivyozoea.

Ingawa umma ulitangaziwa kuwa zamu hii CCM imeamua kuwakumbuka kina mama, hili kidogo linatia shaka. Kwanini sasa na si siku zilizopita? Kwanini Makinda na si wengine wenye udhu na sifa kemkem zaidi yake?

Wengi wanashangazwa na mapenzi ya ghafla ya CCM kwa kina mama. Mbona hawakuwafikiria wanawake kwenye vyeo vingine? Ni mara ngapi tangu zama za Benjamin Mkapa wameshauriwa wateua mwanamke kushika nafasi ya waziri mkuu bila kufanya hivi? Hii maana yake ni kwamba madai kuwa Makinda ametumika kumkomoa Sitta yanaingia akilini. Hii inamwonyesha Makinda ima kama fisadi au mwenye tamaa anayeweza kutumiwa na mtu au kundi lolote akiweka kando maslahi ya taifa.

Kwa madai kama haya, utendaji wake lazima uingie dosari. Je Makinda atautumikia umma au wale waliomuumba na kumuibua? Bila kujibu hoja hizi Makinda ataendelea kuchukuliwa kama mtu rahisi wa kuweza kutumiwa na yoyote tena kwa madhara ya taifa. Je Makinda tunayeambiwa alifinyangwa atakuwa tofauti na kuibua wa kweli? Time will surely tell.

Mtu anayeweza kutumiwa kirahisi na haraka hivi hafai kusimamia mhimili wa dola achia mbali ofisi ndogo. Mtu wa namna hii ni kifaa katika mikono ya wengine. Hafai. Mtu ambaye haoni ubaya wa mafisadi hawezi kuona uzuri wa kuwaandama. Nisingependa spika wangu adhoofike na kudhalilika hivi.

Kitendo cha Makinda kufinyangwa {kama ni kweli na atakaa kimya) na watu wenye harufu mbaya ya ufisadi tena walio karibu na rais Jakaya Kikwete kinaondoa maana nzima ya mgawanyo wa madaraka. Nani asiyejua kuwa watu hawa wana ushawishi mkubwa kwa rais kiasi cha kuonekana kama wao ndiyo wanaongoza nchi? Rejea wengi wao kuwajibishwa na bunge lililopita lakini rais huyu huyu akawapigia debe na wakarejea bungeni. Rejea wosia wa baba wa taifa kuwa CCM imetekwa na mafisadi. Rejea wosia wa aliyewahi kuwa katibu wa CCM, marehemu Horace Kolimba kuwa CCM imepoteza mwelekeo. Tuseme. CCM imegeuka kokoro ambalo huzoa kila uchafu katika kusaka samaki.

Rejea wengi wao kuwa ndiyo wenye funguo za vyanzo vya pesa ya kampeni ya Kikwete mfano EPA ambayo hajawahi kujitenga nayo lau kwa kutoa utetezi au maelezo.

Leo sitasema mengi zaidi ya kumtaka Makinda ajitokeze na kuondoa utata huu uliogubika kuteuliwa na hatimaye kuchaguliwa kwake na CCM kuwa spika. Na asiishie hapo. Kwenye utendaji wake atumie viwango tulivyoshuhudia kwenye bunge lililopita badala ya vile vya mafisadi- awape nafasi wabunge kuja na hoja zenye kulinda maslahi ya taifa na si kuwaminya ili kuwafurahisha na kuwaokoa mafisadi waliomfinyanga.

Makinda, amka ujisemee badala ya kuacha uvumi kuendelea kuzunguka wadhifa wako.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 7, 2010.

Siku ulipokatiliwa ushauri wa kuokoa pesa ya walevi

Mwenzenu juzi nilikuwa nimejichimbia Bwagamoyo. Msianze kupayuka kuwa mzee mzima nimeamua kufuata dini za kishirikina za jamaa zangu. Hizo nimewaachia waganga njaa kama Shehe Njaa Yahya na wanaojiita viongozi wa kondoo wakati ni mbwa mwitu na mafisi ya kawaida yaliyojificha kwenye ngozi ya kondoo.

Niliitwana Mkuu mwenyewe na rafiki yangu mkubwa ingawa mie si mshiriki wake, Njaa Kaya ili kumpa tafu kwenye kuunda kabineti ya ulaji.

Kabla ya kwenda, ilitangazwa bombani kuwa ameniteua kumshauri katika kuendeleza libeneke hili. Baada ya wapenda ulaji kusikia vile, walinisumbua sina mfano. Mara wanipigie simu. Mara waniandikie emails, barua pepe na meme. Walimemetuka kwa kimuhemuhe na kujaa mapepe. Mie niliwaambiwa openly kwamba waende kwa mwanae na mkewe kwani mi si wa hovyo hivyo. Mie si mtu wa kumlamba mtu matako bwana eti anitupie makombo.

Wengi walijikomba hadi wakatapeliwa na wasaka ngawira waliomzunguka bwana mkubwa. Yote juu ya nini? Kupata mwanya wa kuchakachua mipesa ya wanuka jasho wa Danganyika.

Baada ya kufika kule Bwagamoyo, sikuamini macho yangu. Nilikuta umati mkubwa wa wataka ulaji ukijidhalilisha kwa jamaa yangu utadhani mfalme wa nchi ya kiarabu! Watu wazima waligeuka kama vyangu katika kujikomba na kujirahisi ili wapate ulaji wa dezo.

Nikiwa natafakari hili na lile, mara nikakaribishwa ndani tayari kuanza zoezi la kuteua walaji wenu. Baada ya kuamkuana na jamaa huku akinitupia lawama lukuki kwa kumnyima tafu, nilitoa masharti ya kufanya kibarua kile.

Sharti la kwanza ilikuwa ni kuhakikisha wale wote waliotuhumiwa kughushi nyaraka na vyeti vya shahada na digrii anawapiga chini. Mwe! Jamaa alibadilika. Yule Chekacheka tuliyemzoea alitoweka ghafla na kuingia Nunanuna. Bila hili wala lile alianza kunishushia shutuma badala ya wale walioghushi.

Sharti la pili ilikuwa ni kuhakikisha hakuna cha shemeji wala mtoto wa fulani. Hili nalo nusu limpasue jamaa. Hii ikichanganyikana na afya yake yenye ugogoro ndiyo usiseme. Kabla sijatulia hata kunywa mvinyo uliokuwa ukiningoja mezani, jamaa aliamka na kunionyesha mlango.

Nilipokuwa nikitoka akaniita. Kwa vile mie huwa sina dogo na sitetemekei miungu watu, niliamua kujitoa kama sina akili nzuri. Nilipikigiza mlango na kuishia.

Kwa vile jamaa anajua hasira na busara zangu, hakuwambia uhasama wa taifa kunizuia. Maana ningewatia adabu na kuwaletea aibu hakuna mchezo. Ananijua kuwa mie ni gwiji la jet kune doo na wu shuu ambazo zote nina mikanda ya dhahabu na shahada ya juu ya upigaji karate na judo.

Hivyo hakujisumbua na kunizuia hasa ikizingatiwa mwenembago wangu akipanda naweza kumwadhibu yeyote bila kujali ukubwa wala nini.

Nilitoka nje na kumwamrisha dereva wangu anirejeshe kwangu nyumbani.

Nilipofika nyumbani, kinokia changu kikaanza kuhanikiza. Kucheki namba kumbe Njaa Kaya mwenyewe.

Alijitahidi kuniomba msamaha kwa yaliyotokea huku akiahidi kunitumia helkopta nirudi Bwagamoyo au yeye aje kwangu nimsaidie kibarua kile. Nilimwambia wazi wazi kuwa kama hatatimiza masharti yangu mie sitakuwa tayari kujichafua kama yeye kwa kulala kitanda kimoja na wahalifu.

Tukiwa tunaongea, alitaka kujua ni kwanini nilikuwa na masharti na msimamo mkali. Nami bila kujali ukubwa wake wa kupewa kwa vile namwogopa Subhanna pekee, nilipa sababu za kuja na masharti makubwa vile. Nilimkataza kuendeleza ushikaji na kubebana kwa kuangamiza umma hata kama haufurukuti. Nilimuonya kuwa kuna siku umma utaamka na kufanya kitu ambacho kitawashangaza wengi.

Kumkatisha tamaa, nilimkaripia na kutoa sharti jingine ambalo ilikuwa ni kwamba siku akiutangazi umma wa walevi uteuzi wake, nilitaka atangaze sambamba na hili, kuwaweka ndani watuhumiwa wote wa kughushi na wale wa HEPA na Richmonduli.

Hili lilimchanganya hadi nikasikia sauti yake ikianza kukoroma. Ghafla nilitegemea ningesikia aisee mara ntiii. Lakini haikutokea na kama ilitokea basi wambea hawakuipata.

Niliendelea kumpa sababu ni kwanini nilikuwa na masharti ambayo kwangu yalikuwa ni rahisi ingawa yeye aliona magumu.

Kwanza, lengo langu ilikuwa ni kuhakikisha wale wote walioghushi kama kina Emmy Nchimvi, Bill Waling'ombe Lukuvile, Merry Nyago, Makorongo Muhanga na wengine hawarejei. Ingekuwa laana na aibu ya namna yake kama ningeshiriki kwenye kurejesha wahalifu ulajini ilhali wanapaswa kunyea debe kule lupango.

Hakuna kitu kilinitisha kama kusoma CV ya Emmy Manu Nchimvi. Eti anasema alisomea PhD na masters kwa pamoja tena toka kwenye chuo kinachotia kila aina ya shaka. Haijawahi kutokea. Hata Newton, Galileo, Ensteins nami hatukusoma digrii zetu kwa muda mfupi hivi tena kwa pamoja. Kama sisi na ugwiji wetu tulishindwa inakuwaje kilaza mmoja aweze? Hilo utajibu mwenyewe.

Nilipoangalia CV ya Bill ndiyo nilikaribia kupata kichaa. Ukiondoa cheti ya upiga chaki yaliyobaki ni uchakachuaji mtupu. Hivyo kwa ufupi nilikataa kushiriki jinai hii.

Pili nilitaka watu kama Husseinu Muinyi aliyezembea hadi mibomu ikaua watu kule Mbagala nilitaka atemwe bila kujali kuwa ni mtoto wa aliyemtengeza jamaa yangu. Pia nilimweleza kuwa watu kama Hawa wana Ghasia sikumtaka tena kwenye ulaji kwa vile hakuwa na sifa zaidi ya ushemeji wala mkwe wake mzee wa Ruxa. Pia nilimtaja mtu kama Porofwesa J4 Majembe. Huyu alivuruga elimu. Kuna watu kama Joji Mkunjika na Shukuruni Kawa-Mbwa. Hawa waliboa sana kwenye ngwe ya awali.

Kwa vile jamaa ni mugumu wa kuelewa na kujifunza, baada ya kuona anaendelea kutetea uoza nilkata simu na kumuonya asizidi kunipotezea muda. Nilimshauri kuwa kama angetaka ushauri basi angewaalika Bi Mkubwa wake mpenda sifa na rais wa MAWAWA na kitegemezi chake Riziki One Tegemezi.

Kabla sijasahau, siku moja kabla ya kuitwa Bwagamoyo, nilikuwa nimempigia simu Jamaa kumuonya juu ya uteuzi wa Jan Makambale. Nilimuonya baada ya kusikia mgosi Machungi Makambale akijisifu kuwa lazima kitegemezi chake kiule.

Sambamba na la mtoto wa Makambale nilimuonya kuhusu kumrejesha Ewassa kutokana na fununu nilizo kuwa nimezinyaka. Ingawa alijifanya kutumia timu ya familia yake, naona alitumia baadhi ya ushauri wangu.

Pia nilikuwa nimemshauri aunde kijibaraza kidogo tu na siyo genge kuubwa tuliyojaziwa walaji. Kwa vile jamaa yangu ana domo kubwa na hana masikio, ameendelea kuwaumia walevi bure. Hata hivyo hapa wa kulaumiwa ni walevi wanaoendelea kumuendekeza badala ya kumtolea uvivu maana njuluku wanazokwapua hawa jamaa zake si zake bali walevi.

Don't take me seriously. You know what?

I am just dreaming.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 7, 2010.

Wednesday 8 December 2010

Waweza amini haya ni majeneza?







Dunia haiishi vituko. Vituko vingine huchekesha, kufundisha hata kufikirisha wakati vingine humuacha mtu asijue la kushika!
Nchi ya Ghana huwa nayo haiishiwi vituko. Ina makabila yenye majina mafupi kama Ba, Ga, Ma na mengine mengi.

Ni katika taifa hili ambapo kifo uheshimiwa kuliko uhai. Ni katika sehemu hii ya dunia ambapo mamilioni ya fedha hutumika kwenye mazishi badala ya maisha. Hivyo, usishangae kumsikia mghana akidunduliza kwa ajili ya mazishi badala ya mambo mengine.

Kuongeza utamu kwenye hili, waghana huzikwa kwenye majeneza yanayowakilisha kazi, wadhifa na mapenzi ya marehemu. Rubani huzikwa kwenye kaburi mfano wa ndege, dereva, gari, mlevi chupa na mengine kama hayo.
Siachi kujiuliza. Watu kama Casanova, Osama bin Laden, wezi wetu wa EPA na Richmond wangezaliwa nchini Ghana wangezikwa kwenye majeneza ya namna gani?

Na kama wewe ulikuwa mpayukaji, ungezikwa kwenye jeneza mfano wa nini? Tafakarini.


wezi wa epa
bin laden

Tuesday 7 December 2010

Ni watanzania waishio nje au mapandikizi ya CCM?




Kutoka Kushoto ni Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha wa Tawi Boniface Assenga anayefuatia ni Mwenyekiti wa Tawi Dk. Alfred Kamuzora akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Tawi Neema Kengese na anayefuatia ni Salim Mfungahema Katibu wa Siana, Sera na Uenezi wa Tawi (Moscow Urusi)

Kila mara nimekuwa nikisoma habari za 'watanzania' wanaoishi nje kusherehekea uhuru wa Tanzania, kumpongeza Kikwete na mambo mengine mengi ingawa sijawahi kuwasikia wakishinikiza kupata haki ya kupiga kura.
Maarufu ya jumuia ambazo nimeishasoma habari zao hasa katika kumpongeza Kikwete ni zile za Watanzania waishio Urusi, Italia na Japan kwa uchache tu.

Je inakuwaje watanzania waishio nje na jumuia zao ziwe karibu na CCM tu na si vyama vingine? Je hawa ni wawakilishi wa watanzania waishio nje au mapandikizi ya CCM na wale waliofadhiliwa na CCM kuwa nje?
Mabalozi wa nchi za kiswahili hawana utaratibu hata wa kukusanya takwimu za raia wao walioko nje ukiachia mbali mmoja balozi Maajar wakati alipokuwa Uingereza.
Tusaidieni. Kwanini jumuia nyingi za wabongo zilizoko ughaibuni zinaonyesha kujikomba kwa watawala wanaoshiriki na kulea ufisadi? Je nao hawoni kama hao wanaowaabudia?

Monday 6 December 2010

Ya Pinda na kukataa shangingi na hiyo katuni vipi?




Madili ndani ya maadili.

Katuni ni kwa hisani ya IPP Media.



Waziri mkuu Mizengo Pinda huwa haishiwi vituko na mizengwe. Aliwahi kukoromea matumizi mabaya ya raslimali na fedha ya umma bila kuchukua hatua yoyote zaidi ya kulalama.
Aliwahi kutangaza 'umaskini' wake wakati bosi wake na wenzake walikula jiwe.

Juzi kaja na mpya ya kufungia mwaka alipokataa shangingi lenye thamani ya shilingi 280,000,000. Ajabu ya maajabu alikaririwa akisema kuwa hakuhusishwa kwenye mchakato wa kununua dude hili hatari. Hivyo alilikataa kwa madai kuwa alilo nalo bado linadunda mzigo. Je kukataa kukataa tu ni jibu au kutafuta umaarufu? Kama yeye ndiye mwenye dhamana ya kuidhinisha au kutoidhinisha ununuzi wa magari, alizuiliwa na nini kuamuru lirejeshwe huko lilikolanguliwa na kurejesha 'chenji' yetu?
Je anamlalamikia nani iwapo yeye ndiye mwenye mamlaka? Je mamlaka yake ni ya kazi gani?
Je, kwa mantiki haya, Pinda achukuliwe kama shujaa, mzalendo na mwajibikaji au?