The Chant of Savant

Sunday 29 January 2012

Nimemkumbuka mzee Yusuf Makamba


Ingawa tulijua kuna siku moja ataachia ngazi, wengi tulipenda katibu mkuu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mzee Yusuf Makamba (Mpayukaji) aendelee kuwa katibu mkuu ili aendelee kuvurunga na kuidhoofisha zaidi CCM. Tutamkumbuka Makamba, katibu mkuu aliyeondolewa madarakani kwa aibu kama mtu aliyekitia aibu CCM. Makamba atakumbukwa kwa kupwaya kwake kiasi cha kuonyesha udhaifu wa kuteuana kwa ushabiki urafiki. Makamba anakumbukwa kwa kutumia sanaa badala ya sera na taratibu katika utendaji wake akilalia sana kusoma na kuitafsiri vibaya biblia ima kutokana na kisomo kidogo au ajenga zake za siri za kisiasa.

Kwanini tumemkumbuka Makamba wakati tukijua hakalii tena kiti muhimu cha mtendaji mkuu wa chama? Tunamkumbuka kwa sababu aliyemrithi, licha ya kufunikwa na kunywea anaonekana kuwa ataleta madhara makubwa kwa chama zaidi ya hata mzee Makamba na vituko na udhaifu wake.
Si uzushi. Katibu mkuu wa sasa wa CCM, Wilson Mukama, aliingia kwa mbwembwe sana madarakani akipania kuwashikisha adabu watuhumiwa wa ufisadi almaarufu magamba. Hawa si wengine bali Edward Lowassa, waziri mkuu wa zamani aliyefurushwa na kashfa ya Richmond, mwanasheria na waziri wa zamani Andrew Chenge almaarufu mzee wa Vijisenti na Rostam Aziz aliyejitoa mwenyewe baada ya kuona ukweli wa shutuma zilizokuwa zikimkabili. Akiwa na siku chache tangu kuteuliwa, Mukama alilihakikishia taifa na dunia akishirikiana na kinara wa vita dhidi ya magamba wakati ule Katibu wa itikadi Nape Nnauye kabla ya kuzimwa, kuwa angewashikisha adabu wahusika. Muulize leo kama amaewashikisha adabu watuhumiwa au kashikishwa adabu yeye. Je Mukama alilazimishwa kujiapiza kuwashughulikia wahusika au alizimwa? Kama alizimwa alizimwa na nani na kwa nini? Je Mukama alitoa kauli hizi ili kutafuta umaarufu kirahisi rahisi au hakujua aina ya maji aliyokuwa akiyavulia nguo? Ni bahati mbaya kuwa sasa CCM imetekwa zaidi na mafisadi hasa magamba kiasi cha kujifanya hamnazo na kutokumbuka kuwa iliwaahidi watanzania kujivua gamba. Chini ya Mukama sawa na Makamba, magamba yanazidi kutuna na kutuna na kutuna na kutuna zaidi hadi kukimeza chama na nchi kwa ujumla.

Ingawa Mukama aliikuta CCM pabaya, sasa anaipeleka pabaya zaidi ya alipoikuta mikononi mwa Makamba hasa kutokana ima na ukimya wake au kuramba matapishi yake kwa kushindwa kushinikiza watuhumiwa wa ufisadi wawajibike kwa kuachia nyadhifa zao kama walivyotakiwa na vikao vya juu vya chama anachoongoza Mukama. Kama Makamba asingekuwa na maslahi na jamaa hawa, nimjuavyo angewabutikia angalau kulinda hadhi yake. Mukama hili limemtoa knockout maskini!

Jaribio rahisi lililoonyesha kuwa CCM ilikuwa pabaya wakati Mukama akiingia ni ile hali ya kuona aibu kumwangukia Philip Mangula katibu wa zamani wa CCM aliyekiimarisha chama, kwenye uchaguzi wa Igunga ambapo CCM iishinda kwa mbinde.

Wengi wanaojua mikiki mikiki na nafasi ya katibu mkuu wa chama tawala wanashangaa ukimya na kupwaya kwa Mukama kiasi cha kumkumbuka Makamba pamoja na udhaifu wake wa kufanya mambo kienyeji na kukurupuka. Je CCM inangoja nini kutafuta mtu mwingine wa kumrithi Mukama ambaye ameonyesha kupwaya tena kwa muda mfupi hasa wakati huu ambapo chama kinahitaji uongozi dhabiti? Kwa wapenzi wa mageuzi, hata hivyo, kama ilivyokuwa kwa Makamba, wanaomba Mungu Mukama aendelee kukalia kiti cha katibu mkuu wa CCM ili avuruge zaidi. Hii itarahisishia upinzani kunyakua dola kwenye uchaguzi ujao.
Wengi wanashangaa. Yule Mukama wa jiji la Dar es salaam aliyeteuliwa na Charles Keenja ametimkia wapi? Je ni yale yale ya siasa na umaarufu wa msimu kama wa akina Augustine Lyatonga Mrema, maalim Seif Shariff Hamad na Keenja mwenyewe? Je Mukama amezibwa mdomo baada ya kuwagusa wasioguswa au amelainishwa kama alivyosema hivi karibuni mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuwa wapambanaji dhidi ya ufisadi wamenyamazishwa kiasi cha kutosikika? Yuko wapi Mukama atupatie japo jibu au maelezo? Amezidiwa na Nape ambaye pamoja na kujitoa kimasomaso kwenye vita yake dhidi ya ufisadi angalau amekuwa akijitokeza mara chache kutoa ufafanuzi juu ya mambo muhimu! Ningekuwa Mukama ningejitokeza na kuondoa kiwingu hiki. Maana ukiachia mbali kuonekana juzi akiwa nchini Ujerumani, Mukama kwa sasa ni sawa na hayupo. Hii si kawaida ya mtendaji mkuu wa chama kilichoko madarakani ambaye lazima mara kwa mara atoe ufafanuzi kuhusiana na sera na mipango ya chama chake na serikali yake.

Mukama amepwaya sana kiasi cha kuzidiwa hata baadhi ya wenyeviti wa CCM wa mikoa ambao siku za hivi karibuni walifikia kukipasua chama wakiwapigia debe “mabwana” zao yaani watuhumiwa wa ufisadi. Ajabu Mukama hakujitokeza kuwashikisha adabu. Angewashikishaje adabu iwapo amewashindwa watu wao ambao hawana hata mamlaka zaidi kwa sasa ikilinganishwa na wenyeviti hawa?

Ingawa Makamba alisifika kwa vitu vidogo kama vituko na mambo mengine ambayo hayakuwa muhimu kwa nafasi yake, kwa udhaifu wa Mukama, tuna kila sababu ya kumkumbuka komredi Mgosi Yusuf Makamba almaarufu mzee wa biblia.
Chanzo; Dira Januari 2012.

Saturday 28 January 2012

Neema toka Davos


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Bill and Melinda Gates Foundation Bw. Bill Gates wakati wa Kongamano la Uchumi Duniani mjini Davos, Switzerland

Thursday 26 January 2012

Kumbe maisha bora Tanzania yanawezekana!



Kibonzo hicho cha Kipanya nadhani kinaweza kuwa na tafsiri nying. Sijui wewe unakitafsirije? Tafsiri yangu ni kwamba watawala wetu wanajali raha zao badala ya maisha yetu- hawatupendi na wanatudharau sana. Yanayotukuta hayawashughulishi na kama yanawashughulisha basi ni kwa kuombea misaada ya kutanulia zaidi na zaidi kwa gharama yetu na vizazi vijavyo. Je kwa mtaji huu kuna haja ya kuwa na watawala wanaokula watu badala ya kuwatumikia?

Wednesday 25 January 2012

Is Libya Safe Under Mustapha A. Jalil?


When former Libya tyrant, Muammar Gaddafi was toppled and later summarily felled, the world went frenzy crazy with the sigh of relief. Dictators in western countries who pretend to be the tutors of democracy congratulated each other for getting rid of undemocratic dictator. Was it right or wrong? Time will surely tell. Now that months have lapsed and news is breaking those rebels who toppled Gaddafi had different aims and agendas altogether. Mistrust and confusion are high. This secret was revealed by the capture of Seif al Islam, who is believed that he was groomed by Gaddafi to take over had anything happened as it was the case in Syria, Togo, DRC, Gabon and North Korea where sons of former presidents took over after their fathers died.

Mistrusts and division forced donor countries to not give frozen Libya’s money to the new regime as it was recently revealed. "The Libyan money is not yet liquid and useable. The donors don't want to give more. Are we going to wait three months to deal with these emergencies?" Georg Charpentier, UN Humanitarian Coordinator, posited at a meeting of heads of agencies in Tripoli in November.

Many Libyans are concerned and they don’t know what is going on. "We're now selling over a million barrels a day - that's $100m (£64m) a day," says Sami Zaptia, the managing director of consultancy firm Know Libya. He adds, "It's a question of where is the money going? Is Libya paying off some debts? Are we paying NATO? What's happening? It's big money."

Since this secret of animosity and division among the rebels came to the agora, the west has kept mum thanks to the doubt this situation create. Will Libya end up becoming another Iraq or Afghanistan? Who knows? Before concluding or passing verdict, we need to examine the current dictator who is running Libya. This is none other than former Prosecutor and minister for justice who is currently the head of National Transition Council, Mustapha Abdul Jalil.

Abdul Jalil was born in 1952 and he is a lawyer by trade. From 2007 to 2011, Abdul Jalil was Minister of Justice or officially, the Secretary of the General People's Committee of Justice under Colonel Muammar Gaddafi. In a simple language, Abdul Jalil was doing Gaddafi’s laundry when it came to apply law. Therefore, his hands are dirty full of filth and the so-called nasty past that shaped Gaddafi and his notorious regime as it is defined by western notorious regimes. In other words if you hate Gaddafi, you must, so too, hate his laundryman Abdul Jalil. What a type that is Abdul Jalil who used his profession to amuse the person he blackmail and now calls dictator? What hypocrisy for such a laundryman to stand on the agora and start throwing stones at his master? This is a very question many thinkers are asking with regard to the future of Libya. Will Libyans overlook this dirty and stinking legacy of their current leader? If they do, what next after the euphoria of getting rid of Gaddafi is over? Will they turn all stones or ignore the reality for their peril?

Like current Egyptian strongman, Field Marshall, Mohamed Hussein Tantawi, will Abdul Jalil get away with it and save his skin or being booted out like Mohamed Ganouchi in Tunisia? If Gaddafi was a butcher, Abdul Jalil was his henchman.

Like abul Jalil who dogedly serving Gaddafi, Tantawi obstinately served Mubarak and Ghanouchi, Zine El Abidine Ben Ali.

More on Abdul Jalil, before even toppling Gaddafi, he had already proved how he was going to follow the trend of the person he was demonizing. He killed Major General Abdul Fattah Younus former Gaddafi Minister of Interior who goofed and defected to join rebels who later killed him. Up to this moment, Abdul Jalil has nary bothered to provide any explanations regarding the death of such a senior person in his struggles! Even the death of Gaddaffi speaks volumes about the man in Tripoli. Will he get away with it? Will Libyans turn tables against him as Egyptians are currently trying to against Marshall Tantawi?

Is Abdul Jalil a new crop of coup d’ etats in Africa? Those who remember how many African junta leaders came to power, are aware that they were created and supported by western countries who found that democratic or the regimes they toppled did not safeguard their vested interests. Likewise, the big question with regards to Abdul Jalil is, did west create him to safeguard their interests that Gaddafi endangered? If not, why then don’t western powers talk about dealing with all those that helped Gaddaffi to commit alleged atrocities? Is Abdul Jalil a good boy before west and therefore a traitor against Libyans? Britain helped Idd Amin to topple a democratically elected government so as to stage dictatorship that would safeguard Britain’s interest. Will Abdul Jalil accomplish this or turn inot a mad dog like Idd
Amin?
Source: The African Executive Magazine Jan. 25, 2012.

Maskini CUF, fupa la CCM limeisambaratisha!

Kwa mtu anayejua tabia za mbwa, hatapingana nasi kuwa, hata awe mjanja, mwenye nidhamu na mafunzo kiasi gani, mbwa akitupiwa fupa usahau kila kitu. Ukitaka kumuibia mbwa hasa anapokuwa kwenye lindo, njoo na fupa.

Hivyo, ndivyo ilipotokea kwa Chama Cha Wananchi (CUF) mbacho kilichozolea umaarufu mkubwa kwa kuitikisa serikali na nchi kutokana na harakati zake za kudai haki hasa kwa upande wa visiwani. Kwa wanaokumbuka historia ya chama hiki watakubaliana nasi kuwa, licha ya historia yake chafu ya kufukuzana, kilileta changamoto ya kutosha kuanzia miaka ya 1992 ulipoingia mfumo wa vyama vingi nchini.

Ingawa tangu kuanzishwa kwake, CUF ilionyesha wazi kimatendo na kimkakati ilivyokuwa imeegemea upande mmoja, si haba ilileta changamoto kwa nchi nzima. Sasa hii imebakia historia baada ya Katibu wake mkuu Seif Sharriff Hamad kupewa umakamu wa kwanza wa rais. Ingawa wengi wanachukulia mvurugano unaondelea kwenye chama cha CUF kama suala la ndani, ukweli ni kwamba mchawi ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichobuni njia rahisi ya kuepuka madhara makubwa visiwani baada na kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Baada ya CCM kugundua kuwa isingeweza kushinda kihalali na CUF wasingekubali matokeo ya kupikwa, kilikumbuka kitu kimoja-CUF imejengwa kwenye jina la mtu na si sera wala mikakati. Na mtu huy si mwingine bali Seif ambaye kimsingi ndiye CUF na CUF ni yeye. Kwa kujua alivyoachwa nje kwa muda mrefu na kuanza kuishiwa kulhali, CCM walimzuga na kumwingiza kwenye mazungumzo yaliyokuwa yamekwama kwa miaka mingi. Kwa kujua kuwa Seif alikuwa anakabiliwa na shinikizo la wanachama kumuona kama hafanikiwi, hakuwa na jinsi bali kukidakia chambo ili aweze kufaidi lau binafsi hata kama ni kwa kukiua chama.

Baada ya Seif kuingia ubia au tuseme kufunga ndoa ya mkeka na CCM, kuna baadhi ya wana CUF waliona kama wanasalitiwa hata kuuzwa kwa ajili ya maslahi ya mtu mmoja. Huu ni upande mmoja. Upande wa pili ni pale Seif alipokikabidhi chama mikononi mwa mtu mwingine ili aweze kutumikia nafasi yake mpya. Hili lilisababisha kuibuka maswali mengi kuhusu utendaji wa Seif. Seif kuona hivi akaamua kuwa mkali na kumshughulikia yoyote aliyehoji ndoa yake na CCM au kukasimu chama mikononi mwa watu wake wa karibu. Kimsingi hiki ndicho chanzo kizuri cha kuvurugana na kufukuzana kwa CUF ambako bila shaka utakidhoofisha chama.
Kitu kingine kilichomtia motisha Seif kufunga ndoa na CCM ni ile hali ya kudhani kuwa anaweza kujaribu tena akashinda urais wa Zanzibar iwapo rais wa sasa atapendekezwa kugombea kiti cha muungano kama mambo yasiyo ya kikatiba ya zamu za pande za muungano yataruhusiwa badala ya vyama kuteua wagombea wanaofaa.

Kwa mahesabu ya haraka, kama rais wa sasa wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein atasimama kwenye uchaguzi wa muungano CCM haitakuwa na mtu mwenye kuweza kushinda urais wa Zanzibar kama mmojawapo atapitishwa na CCM. Hebu fikiria watu kama Dk Hussein Mwinyi ambaye baba yake alishakuwa rais wa Zanzibar na muungano, nani anaweza kuruhusu utawala wa kurithishana na kufuata majina? Maana ni juzi tu mtoto wa rais wa kwanza wa Zanzibar Aman Karume amemaliza kipindi cha miaka kumi. Wengine wanaotajwa na Shamsi Vuai Nahodha ambaye alikuwa waziri kiongozi kwa miaka kumi. Huyu hana ubavu visiwani ingawa aliwahi kushika nafasi ya juu. Mwingine ambaye bila shaka anaweza kuingia kwenye kinyang’anyiro na kutoa upinzani mkubwa wa Seif hata kumshinda ni makamu wa pili wa sasa balozi Idd Seif ambaye chati yake inapanda kwa kasi ya ajabu.

Sababu nyingine iliyosababisha mvurugano ni kuchokwa kwa Seif ambaye amekuwa akigombea miaka mingi bila kufanikiwa ukiachia mbali kuongoza kwa staili moja ya muungu mtu. Zama za chama kumtegemea mtu zimepitwa na wakati.
Kitu kingine ambacho tumeishakiongelea ni ile hali ya CUF kuwa CCM B. Hili limeelezwa wazi wazi na waliofukuzwa na jinsi lilivyowakera. Shoka Khamis ambaye alikuwa Mbunge wa Micheweni, Kaskazini Pemba alikririwa akisema, “Nimejifundisha mengi sana CUF mazuri na mabaya, lakini leo kwa sababu wamenifukuza ngoja niseme mabaya, CUF sisi ni CCM B kama wanavyosema wenzetu. Chama kina sifa mbaya ya kufukuza watu, lakini anayefukuza wenzake, Seif Sharif Hamad yeye anajiona kama mungu hafanyi makosa,”

Sababu ya mwisho ni historia chafu ya kufukuzana au kujenga mazingira ya kuwalazimisha wasiotakiwa kwa kukosoa uongozi wa juu kuhama chama kama ilivyotokea kwa James Mapalala mwanzilishi wa CUF, Maiko Nyaluba, Slivesta Kasulumbai (mbunge), Geoge Shambwe, Shaibu Akwilombwe, Richard Hiza Tambwe,Wilfred Lwakatare, Othman Dunga, Asha Ngende,Khamisi Katuga na Ashura Amazi ambao wallifukuzwa kutoka upande wa bara wakati upande wa visiwani waliotimuliwa au kujiondoa baada ya kuhoji ulaji wa wakubwa au kutofautiana nao kimwazo ni pamoja na Naila Jidawi,Fatuma Magimbi,Juma Othuman, Salumu Msabaha na Hamad Rashid.

Je watafukuzwa au kunyamazishwa wangapi na lini? Hakuna anayeweza kutabiri ingawa hali inaonyesha kuwa ushindi wa Seif ni wa muda. Maana unaweza kuwadanganya watu wote kwa wakati fulani. Pia unaweza kuwadanganya watu fulani kwa wakati wote lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati wote. Kuna haja ya kuwashauri wana-CUF kubadilika na kuanza kupigania maslahi ya chama badala ya kulinda maslahi uchwara ya watu binafsi wanaowatumia kama nyenzo za kushibisha matumbo yao.

Chanzo: Dira Januari 2012.

Mpayukaji kuhamia Kenya

ZAMANI ungeniambia kuhamia nchi kama Kenya ningekufikisha mahakamani kama si kukunyotoa roho. Hata hivyo, nikiri. Imani na mawazo uchawara ya namna hiyo sina tena. Wazungu husema to make a U-turn. Nami nimefanya hivyo. Nimejipiga mtama kweli kweli baada ya kuchoshwa na ujambazi na upuuzi ninaoshuhudia kila siku na kila mahali kwenye kaya.

Ingawa zamani tuliwaita ndugu zetu wa Kenya wakora, nyang’au na majina mengine mengi tusijue sisi ndiyo manyang’au, kwa sasa wana nafuu kimaisha kuliko sisi. Mzee Mchonga mwana Musa alizoea kuwaita man eats man bila kujua atarithiwa na man eats everybody and everything.

Hakujua kuwa kutazaliwa Kiwila thieves na EPA thugs! Uliza: sasa tuko wapi zaidi ya kuwa na manyang'au squred? Wakati sisi tukipiga mbio kwenda nyuma wao wanapaa kwenda mbele. Wana uwezo wa ku-export hata wafanyakazi uchwara kuja kwetu kufanya kazi nzuri na kuondoka na mshiko wa haja wakati sisi tukiangalia.

Wajua siri yao nini? Kujituma, ubunifu na Kiingereza chao cha I dhink mbus has many more passangers than its capacity. Hamkumsikia jamaa kutoka huko ambaye alinyakwa Manyara akifanya kazi ya kupaka rangi milango na madirisha ilhali aliingia nchini kama TX? Mpo hapo waliwa? Hayo tuyaache.

Mwenzenu nimeamua kuhamia Kenya kutokana na sababu za maana sana hasa kushindwa kuishi kwa kubangaiza au kudokoa toka kwa umma. Siko tayari kuishi maisha ya shilingi milioni moja wakati mshahara wangu ni laki mbili. Siko tayari kuishi kwa kutegemea jinai au kubomu kama lisirikali lenu.

Nahama kwa sababu Kenya: Umeme ni bei nafuu si kama hapa ambapo kundi la majambazi limeamua kwenda nje na kuleta wachukuaji na kuwaita wawekezaji halafu linawatumia kutuibia pesa yetu na kutupandishia umeme kila siku.

Mie siyo taahira kuendelea kununua hata kiza tena kwa bei ya kulanguliwa. Inatisha sana kuona nchi yenye vyanzo vingi vya maji kulangua umeme wakati Kenya ambayo inanunua umeme kutoka Uganda inauza umeme huo huo wa kununua kwa bei nafuu kuliko wetu wa kuzalisha wenyewe.

Sababu nyingine inayonihamishia Kenya ni kuepuka kulanguliwa mafuta wakati Kenya ni bei nafuu. Huwa nashangaa. Je, Kenya wananunua mafuta wapi ambapo sisi hatujui kiasi cha kuendelea kuchezeana namna hii? Sina uhakika hata gesi itakuwa bei mbaya ingawa tunaichimbua wenyewe huko Songosongombingo.

Je, ni wangapi wanajiuliza swali kama hili? Kenya hawana WEKULA kama shirika la kudhibiti bei ambalo hapa kwetu kazi yake si kudhibiti bei bali kuzipandisha hovyo hovyo. Sababu nyingine inayonipeleka Kenya ni ile hali ya uchumi wao kukua huku wetu hapa tunaukalia tu.

Kivutio kingine ni kwamba Kenya wana katiba mpya inayohimiza haki na usawa. Wakati wao wakivuna na kufaidi kuwa na katiba mpya sisi tunaendelea kuzungushana na usanii wa kipumbavu kutetea masilahi uchwara na ya kipuuzi ya kikundi cha wezi wachache wasiosoma alama za nyakati.

Kutokana na katiba ya Kenya kuweka usawa, nahamasika kuhamia huko. Naamini nitatendewa haki kiasi cha kuwa na uhakika wa maisha. Hivyo nikiugua sitaambiwa kwenda kwenye mahospitali yasiyo na dawa wakati wao wakihudumiwa kifalme huko Apollo India. Isitoshe hospitali yao ya rufaa ya Kinyatamanyata iko fiti kichizi.

Kivutio kingine kinachonikimbizia Kenya ni ile hali ya rais kutokuwa juu ya katiba. Nakumbuka. Hata baba Dave hawaruhusu kina Dave na wenzake kuibia Kenya kwa kisingizio kuwa dingi wao ni mdosi na mkubwa wa goverinoma. Noma kuibia Wakenya. Hawana mchezo, hata uwe mkubwa kama tembo watakugadafi hata kabla hujatanua pesa yao. Hamuoni pesa yao inavyopaa wakati madafu yakizama utadhani yamefungiwa nanga?

Kutokana na Rahisi kutokuwa juu ya katiba, hata haja ya kuwa na FFU hakuna. Hivyo hakuna wanyanyasaji na wauaji watumiao virungu wanapoamrishwa na wauaji wenzao kuua wale wanaowaonyesha kweli ili iwaweke huru. Kwa nilivyo na kidomodomo, nimeona nijihamie mapema kabla ya wanoko hawa kunishukia kama walivyowashukia Chakudema kule AR mwaka juu na kunyonga watu kama hawana akili nzuri.

Pia nahamia Kenya ambapo majaji wanaheshimiwa na kutenda haki. Ni juzi tu rafiki yangu Jaji mkuu msaidizi Nansi Barasa alijikuta kitanzini baada ya kukataa kupigwa sachi na mlinzi kiasi cha kuudhika na kumvuta pua ambayo sasa imesababishwa naye avutwe ukuu!

Pia napenda sana majaji wa Kenya ambao huchaguliwa na si kuteuliwa na mtu mmoja tena asiyejua sheria ambaye mara nyingi anaweza kuathirika na ushawishi kiasi cha kuendekeza udini, ukabilia na ushoga.

Pia nahamia Kenya ili siku moja niteuliwe kuwa balozi ughaibuni nami nijisikie kinoma. Maana mabalozi wa Kenya umangani si kama wa Danganyika ambao wengi ni re-cycled ukiachia mbali balozi zetu kujaa watoto wa vigogo na magogo.

Anayebishia tuhuma hizi aiulize serikali orodha ya wafanyakazi wa balozi zenu muone kama hamtapasuka kwa presha. Mie hainihusu! Kazi yangu ni kuronga na kuwafumbua macho. Sasa kama mtaridhia kuendelea kuliwa hiyo ni shauri yenu. Narudia, tumieni akili badala ya masaburi.

Kitu kingine kilichonivutia kuhamia kwenye nchi ya nyayo, ni ile hali ya uchumi, sarafu na mambo kufanyika kitaalamu kuliko hapa ambao mambo si mambo bali mambo hovyo hovyo. Cha mno nakwenda kuwekeza Kenya kwenye Kayanite na kuutangaza Mlima Kimaranjaro maana vyote viko huko.

Hivyo, msijedhani nimeishiwa na uzalendo. Hasha! Kenya ni wazalendo kuliko nyinyi kwa sababu wameweza kuimarisha hata mabenki yao kiasi cha kuweza kuja kuwekeza humu wakati yenu mmeyachinjilia mbali na EPA zenu.

Hivyo nikiwekeza Kenya nitakuwa na uhakika wa biashara yangu. Hii ikichangiwa na gharama nafuu za umeme na bei ya kuingia kichwani ya wese, ndiyo usiseme. Huenda one day nitakuja kuwekeza huku baada ya kaya kukombolewa.

Nimalizie kwa kuwapa nyuzi. You know what? Kumbe ule mradi wa Kiwila umeishauzwa tena kwa Tunituni na rafiki yake Dani son of Jonah wake zao na watoto zao bila kusahau hata wakwe wa kike, kiume na jinsia zote.

Ama kweli wabongo ndiyo waliwao! Habari nilizo nazo toka FBI ni kwamba dili hili likikamilika wezi hawa wakubwa wataiibia kaya zaidi ya madafu 1, 0000, 0000, 0000 na ushei.

Acha niwahi kwenye mazishi ya kaya.
Chanzo: Tanzania Daima Januari 25, 2012.

Monday 23 January 2012

Hatimaye ICC yathibitisha kesi dhidi ya vigogo wa Kenya!





Wakenya wana msemo, "kimeumana" wakimaanisha hatari au mgongano. Kwa takribani mwaka na ushei, dunia imekuwa ikishuhudia mikiki na vituko kuhisiana na na kesi dhidi ya watuhumiwa wa mauaji ya kinyama ya baada ya uchaguzi nchini Kenya mnamo mwaka 2007-2008. Sambamba na kipute hiki, kulikuwa na mikiki ya kujipanga kugombea urais wa Kenya baada ya rais Mwai Kibaki kumaliza muda wake kikatiba mwaka huu. Hili lilifanya kesi hii kuwa na mvuto zaidi hasa ikichukuliwa kuwa vigogo wawili waliothibitishiwa tuhuma yaani Uhuru Kenyatta na William Ruto walikuwa mstari wa mbele kutaka kuwania urais.
Mbali na watajwa hapo juu, kigogo mwingine aliyethibitishiwa mashtaka ni Katibu mkuu kiongozi Francis Kirimi Muthaura na mwandishi wa habari Joshua arap Sang.
Katika mashitaka hayo yaliyohusishwa watuhumiwa sita, wawili hawakukutwa na hatia baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthitibisha kwa ushahidi wa kutosha. Hawa ni aliyekuwa mkuu wa polisi wa zamani (PIG), Maj Gen Hussein Mohamed Ali na waziri wa zamani Henry Kosgei ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Orange Democratic Movement cha waziri mkuu wa sasa Raila Odinga. Kwa wachambuzi wa mambo, kunusurika kwa Kosgey ni ushindi kwa Odinga ambaye anategemea kumrithi Kibaki.
Kwa habari zaidi, BONYEZA HAPA.

Wednesday 18 January 2012

Uganda LRA: Who is Fooling Who?


Although atrocities and barbarities Lord Resistance Army (LRA) and government forces commited cannot be condoned, something needs to be done a tad differently and urgently. A gory and cataclysmic war between LRA and the government has take long and caused a lot of mayhem in northen Uganda. Those who have been keen to dig into this unremunating war will agree with us that something urgent needs to be done.

When we look at the history of crises in Africa, there have been other atrocities with even higher magnitude than the one going on in Uganda. Conflicts in Mozambique and South Africa, for instance, claimed many more lives than the conflict in Uganda. Brutality, if compared, for instance, between Boer South Africa and Joseph Kony’s megalomania, chances are that tha latter shed more blood and committed many atrocities than the former. Taliban in Afghanistan also brutalized and killed many.

But again, the conflicants found that power of arms did not work. They decided to sit down and talk it out and brought stability and tranquility in their country. Afghanistan government is currently talking to Talibans despite all. So far as Uganda is concerned, the problem is that gross power hunger and power play are worsening the situation. Another problem is tha fact that Uganda, just like other bellicose states, groups, persons and whatnot, is the enemy within, but not without. So to solve the problem and do away from impasse and mayhem Uganda and the region have been in is look within but not outside. Somewhat, gross power greed and abuses should be vectored above everything. No violent person or warmonger can surely expect the realization of peace if at all what he does is war. How can he if at all he kills his kith and kin that he says he is fighting for? Is the situation different from this anology? No death can result into life except under religious dogma. We’re mortal human beings who must think likewise whether obversely or reversely. Gandhi said that means to be means must always be within our reach. The means of war and manipulation Uganda is using is not means even if it goofs to think this means can justy the end which by all account is going to be problematic given that it does not follow proper procedures. What has Uganda attained by means of war and this behindhandedness?

What is obvious is that even if Ugandan authorities for long used top-to-toe-armed units, it did not and won’t attain anything worthy mentioning except creating more calamities. What do you expect when two madmen confront each other? Like blind horse making circles, they’ll deceive themselves thinking they are making development while they actually are but stranded. Let us face it; conflicants in Uganda are stranded between Scylla and Charybdis. They need to be helped out. If the protagonists had a gist of love for their country and people, they surely would embark on dialogue. Mahatma Gandhi once said; Force of love and pity is infinitely greater than force of arms.

Again, why was it possible for Mozambique and South Africa to forgive forge ahead; but the same-unfortunately though, is impossible to Uganda? Somewhat, there is power play in this conflict whereby the government is using the conflict to cling to power. For Museveni, Northern Uganda conflict is but an extravaganza bonanza. Those who know how bellicose rulers use wars, pretexts and threats as it is in this case, have an inkling of what the upshot is.

So, to solve the conflict in northen Uganda won’t come by the way of the barrel of gun or political machinations that are going on causing mayhem or conjuring up Philip. Instead, through peaceful inititives, this conflict can be put to rest shall the protagonists act seriously and committedly instead of politics. I understand. Joseph Kony is a wanted person after being indicted by the International Criminal Court after president Museveni wanted to. But again, why listening did ICC work exparte in the first place instead of pilloring Museveni by ordering nonbias investigation into the conflict? Why favoring the explanations of one conflicant against another instead of listening to both or devising another mechanism to rid Uganda of the quangmire it has been in for longtime? Does it mean that Museveni did not commit atrocities in Northen Uganda prior and after coming to power? Who wants to bring this to the international séances dealing with the conflict in northen Uganda?

If anything, Uganda needs to form a true Truth and Reconciliation Commission (TRC) as it was the case in South Africa if it really wants to forge ahead. What should be underscored is the fact that means used to attain something decided the results. Peace reached by force is as good as violence because it will create a good breeding groud for violence and revenge.

Conflict in Northen Uganda has become a sort of gismo Museveni has always depended on to gain popularity and legality to foster his illegal regime over Ugandans the same Kony uses it to stay afloat in his criminality and barbarity. It is an open secret that there in no democracy in Uganda. Human rights are violated openly and nobody is taking Museveni to task. Instead Ugandans have been kept at tenterhooks when it comes to when they will be free.

So we need to stalwartly demand that the parties to conflict in Uganda come to the round table and solve their problems instead of hanging on destructive means that have always destroyed the lives of innocent and poor people in the region. Refer to the overflow of the conflict to DRC and CAR. We need to chop the hydra heads of atrocities in the region by facing the truth instead of subscribing to political machinantions.

In sum, the protagonists must be reminded to consider the problems their standpoints are causing to the economy and security of the region instead of their grip on power. They rust for power deos not even help them. It time for Ugandans to deal with their demons.
Source: The African Executive Magazine Jan. 18, 2012.

Kibanda anaongelea Mwalimu Seif yupi?


INGAWA mwandishi Absalom Kibanda, kwa sababu anazojua mwenyewe pamoja aliyempamba, makala yake imenivutia kwa kunitoa mafichoni.

Makala hiyo ilitoka kwenye gazeti la Tanzania Daima Jumatano la Januari 11, 2012 ikiwa na kichwa, “ Zama za Maalim hazijakoma Zanzibar.”

Nampongeza kwa hili ingawa sikubaliani na alichoandika kuhusiana na rafiki yake mpya, Seif Sharrif Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Japokuwa hoja za Kibanda si nyingi kiasi cha kushughulisha akili sana, amefanikiwa kumpamba “mtu” wake kiasi cha kusahau ukweli.

Kwanza, si kweli kuwa Maalim Seif ni mwanasiasa ambaye amefanya mengi kuliko yeyote aliyewahi kutokea visiwani. Hii ni kumkosea heshima hata kumchukia, kwa mfano, aliyewahi kuwa rais wa Zanzibar na muungano mzee Ali Hassan Mwinyi ambao viatu vyake vyaweza kummeza maalim Seif ukiachia mbali mentor wake, mzee Aboud Jumbe.

Pili, sijui Kibanda kama alisoma historia. Na kama aliisoma basi huenda hakusoma ya Tanzania na kama alisoma historia ya Tanzania basi alisoma iliyokuwa imepotoshwa kwa makusudi sawa na ile ya kina Rebman, Carl Peters, Mungo Park, Bathromew Diaz na wengine.

Kama amesoma historia ya kweli ya Tanzania basi hakuielewa na kama aliielewa basi ameamua kuipotosha kwa sababu anazojua mwenyewe.

Katika makala hii sitapoteza muda wala mwelekeo kumlinganisha Seif na mzee Mwinyi kwa vile hana hata chembe moja ya sifa wala uzito kukaribia hata nusu yao acha kuwa sawa nae. Ingawa kusifia au kutosifia mtu ni haki ya mtu binafsi, kuna haja ya kuepuka kupindisha ukweli.

Leo makala hii itaaangalia upande wa maanguko na kupwaya kwa Seif. Tunafanya hivyo kutokana na Kibanda kumaliza kazi ya kupamba na kuficha haya tutakayodurusu bila kupendelea wala kuonea.

Huwezi kumlinganisha Seif kwa mfano, na Mwinyi hata kwa chembe kwani Mwinyi hajawahi kuuza chama chake na kuingia mikataba ya siri kwa kutaka maslahi binafsi yaani kupewa uongozi kama ilivyotokea kwa Seif.

Cha mno Seif ametumia chama kutafuta riziki binafsi bila kujali sera na malengo ya chama kiasi cha kuamsha ari ya uasi unaokiandama chama kwa sasa.

Anajiona yu bora kuliko chama na wanachama wake kiasi cha kuwafukuza wanaomkosoa na kumtaka arudi kwenye mstari. Hii siyo sifa nzuri kwa kiongozi hasa wakati huu wa demokrasia na mabadiliko makubwa kisiasa.

Kiongonzi wa kupigiwa mfano, kwa mfano, hawezi kufanya mambo hovyo hovyo hadi kufikia hata kudharau amri ya mahakama na mawazo tofauti na yake. Kibanda aliogopa kulisema hili.

CUF, kwa madudu iliyoifanya juzi, imejiondoa hadhi ya kuwa chama cha wananchi zaidi na kugeuzwa nyenzo ya viongozi wawili yaani Katibu wake mkuu Maalim Seif Shariff Hamad ambaye kimsingi ndiye CUF na CUF ni yeye kwa sasa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kuusaka ulaji hata kwa kusaliti malengo na dira vya chama.

Madudu aliyotenda Seif kwa kuwafukuza wakosoaji amefuta mpaka baina yake na viongozi waliokwishaonyesha wazi wasivyo madarakani kwa ajili ya chama bali wao kuendelea kuongoza kama James Mbatia, Augustine Mrema na John Cheyo kutaja kwa uchache. Kiongozi wa namna hii hana cha mno cha kutoa kwa jamii hata tumpende na kumpamba vipi.

Ukiachia mbali watajwa hapo juu kutumia chama kama NGO na kampuni yao, wamekaa kwenye madaraka muda mrefu.

Chukulia mfano Hamad, amekuwa akigombea urais wa Zanzibar tangu mwaka 1995 hadi sasa huku Lipumba akigombea nafasi hiyo sambamba kwa upande wa bara huku wote wawili wakibwagwa na CCM.

Wale waliogombea nao toka CCM walishakaa madarakani na kustaafu wakati wawili hawa wakiendelea kung’ang’ania usukani wa chama. Seif kwa kulijua hili vilivyo aliamua kupwakia umakamu wa rais ili angalau asiondoke mikono mitupu.

Kibanda ameliona hili ingawa amelipindisha. Hebu angalia nukuu hii: “Ingawa ndani CCM na hata akiwa CUF hajapata kutawazwa kuwa Rais wa Zanzibar kwa sababu za kufitiniwa kisiasa, Maalim Seif ameendelea kuwa mwanasiasa mwenye mvuto mkubwa na wa kipekee kisiasa na kiuongozi ndani na nje ya visiwa hivyo.”

Kama alifitiniwa bila shaka na CCM, imekuwaje akajirejesha huko huko na baada ya kuzawadiwa cheo? Je, alifitiniwa au wenzake wa CCM walimjua alivyo na tamaa ya madaraka kiasi cha kumhonga madaraka kirahisi na akaachia kile alichokuwa akidai?

Ziko wapi ahadi zake kuwa kama kura zake zingeibiwa Zanzibar kusingekalika? Hii maana yake ni kwamba hakuna kura iliyoibiwa kiasi cha Seif kukosa pa kushika na kisingizio akaridhia kupewa umakamu wa rais wakati alikuwa akiutaka urais.

Hebu tuangalie nukuu nyingine ya Kibanda, “Heshima aliyojijengea kama kiongozi wa watu aliye na ushawishi na nguvu kubwa kwanza katika Kisiwa cha Pemba na kisha Unguja ndiyo ambayo kwa upande mwingine imemfanya ajikute akizalisha maadui wengi wa kisiasa.”

Je, kama Seif ni kiongozi wa watu tena mwenye nguvu kama Kibanda anavyosema, ni kwanini hajawahi kuchaguliwa kuwa rais wa watu?

Najua atasema ushindi wake umekuwa ukiibiwa. Kama kweli umekuwa ukiibiwa, hao watu wake wanaompenda na kumheshimu walifanya nini kuondoa dhuluma hii kama kweli ipo zaidi ya kuwa sanaa za CCM na Seif mwenyewe?

Kawaida unapoongoza chama kuelekea kwenye uchaguzi, unaposhindwa unawaachia wengine waingie na mawazo na mipango mipya ya kuwezesha chama chako kunyakua madaraka.

Ukiwauliza wawili tajwa hapo juu hili sana sana, kwa upande wa Hamad, amefanikiwa kuingia madarakani si kwa nguvu za chama wala wananchi bali kukiweka chama rehani. Maana ukiuliza mantiki ya kuteuliwa kuwa makamu wa rais wa Zanzibar zaidi ya ulaji binafsi hana jibu la maana.

Kwa wale wanaokumbuka wale waliopoteza maisha wakipigania haki ya Wazanzibari hasa wapemba, wanashangaa alikopata mshipa na jeuri kukalia kiti hicho akikitosa chama kwa maslahi binafsi.

Hii maana yake ni kwamba damu ya ndugu zao ilimwagika kwa ajili ya kupalilia ulaji binafsi wa Hamad. Kwa msingi huo, baadhi ya wanachama wa CUF wameona mbali kiasi cha kustukia usaliti uliofanywa na viongozi wao na kupanga kuwaengua ili kuepuka kuua chama.

Vurugu na umwagaji damu vilivyoshuhudiwa hivi karibuni kule Manzese vinaonyesha ni kwa kiasi gani viongozi husika walivyoishiwa kwa kila hali chamani mwao. Je, wanangoja nini? Je hawa wanaweza kuleta demokrasia kitaifa wakati wameshindwa kuitekeleza chamani mwao?

Kwa vile makala husika ilikuwa wimbo wa sifa, leo tunaachia hapa kwa kushauri mhusika afikiri upya upande wa pili wa wimbo wake wa sifa.

Chanzo: Tanzania Daima Januari 18, 2012.

Kumbe na vyama vya upingaji vinatuogopa!

SISI pamoja na kujadili mada zetu chini ya uhuru wa kaya wa kila mwanakaya kuwa na haki ya kusema atakalo ilimradi asivunje sheria, hatukujua kuwa kumbe mada zetu zinavilaza baadhi ya vyama vya upingaji bila usingizi.

Nasikia hata lisirikali huwa halipati usingizi hasa likisoma haya ninayoandika toka kijiweni kutokana na kuwa ukweli mtupu. Naona yule anaguna. Kamuulize Njaa Kaya kama hanijui wala kunijadili kwenye vikao vyao.

Siku moja alitaka tukutane anilipe fadhila nikamtolea nje. Mie sibabaishwi na pesa ya wizi wala madaraka yatokanayo na uchakachuaji na kuchafuana. Anyway, hapa leo si pake.

Ngoja nijongee kwenye mada ya rero. Leo sitaki kuzungusha kwa vile na wao hawakuzungusha. Nani alijua kuwa kumbe vijiwe vyetu vya kahawa vinakisumbua chama cha calf au ndama ambacho wengi hupenda kukiita CCM namba mbili yaani Chama Cha Magamba B? ukweli sasa umefichuliwa na vyombo vya habari kuwa kumbe kijiwe chetu siyo moto kwa Njaa Kaya peke.

Ni umeme kwa vyama vya upingaji hasa calf ambayo imeamua kuwafungulia baadhi ya vigogo wake mashitaka ya kuongelea mambo ya chama kwenye vijiwe vya kahawa.

Maskini ng’ombe hawa hawakujua kuwa nasi ni chama tosha hata kama hatuna usajili. Tofauti yetu na Kaf ni kwamba mimi mzee Dk, Profesa, Al Haj Mchungaji Mtume Mpayukaji Msemahovyo wa Mpakazaji siyo changu kama made… wao.

Sitishwi na vi-ofa uchwara iwe vya urahisi au hata umakamo. Mie siyo ngangala wala ngungule bali msomi wa Harvard University. Mie ni kijigoo na si changu kama mtu wao hata kama ana kichaka cha made...

Sina haja ya kumuandama changu huyu aliyewekwa kinyumba na Chata la Mafisadi wa magamba. Nimuandame wa nini wakati mwisho wake umeishakaribia hasa baada ya mjumbe machachari toka Ginigi na Wawe ameishafanya kazi hiyo? Nimuandame wanini wakati aibu aliyojiingiza inamtosha? Nyie ngojeni muone maajabu ya Mwajabu kukosa adabu bila sababu hasa pale made… atakapofuliwa kama Kafulia ingawa alitaka kuwambatia wenzake.

Tatizo la siasa za matumbo ni kila mmoja kutaka kumnyotoa mwenzie roho ili ale yeye. Mtakapoendelea na upuuzi huu hawa walevi wetu watatetewa na nani? Ajabu na walevi walivyo wa hovyo wezi wakitimuana wanakwenda kwao na kuwaongopea nao wanaiingia mkenge kuwatetea kama ilivyotokea kwa Dave Kafulia.

Hamkusikia walevi wa kule mwisho wa reli wakisema eti watahama naye wasijue jamaa hawawakilishi wao bali tumbo lake? Ya Kafulia kufulia tuyaache maana alishaonyesha asivyo na maana pale alipolialia na kumshika miguu Ku-Mbatia akimwaga michozi hadharani kama kichanga.

Ingawa calf wamechemsha na kujivua nguo, tunakubaliana nao kuwa vijiwe vya kahawa vinatisha. Badala ya wao kuangalia wapi wamejikwaa wanakazania kushutumu waliokoangukia!

Nani alijua kuwa ni vijiwe vya kahawa vilivyofichua nyumba ndogo za watawala hata akiwamo mkuu? Nani anabisha kuwa vijiwe vya kahawa ndiyo vimevichua yaliyokuwako nyuma ya pazia kuhusiana na jamaa wa mabondeni ambao hawataki kuhama kwa sababu ya kulinda biashara yao haramu ya gongo na unga?

Hata Richmonduli, kwa taarifa yenu, ilifichuliwa toka kwenye vijiwe vya kahawa amini usiamini.

Hawa jamaa badala ya kushughulikia matatizo yao wanabaki kuviandama vijiwe. Hivi kweli, kwa mfano, kuna mantiki na haja ya kuvilaumu vijiwe kwa uroho na upuuzi unaofanywa na vyama kama calf?

Watu wanaiba mali za chama halafu wakisemwa kijiweni wanaanza kugeuza hili kuwa kosa la jinai kuliko wizi wanaofanya! Watu wanaanzisha vyama bila sera halafu wakinangwa wanaanza kunung’unika! Kuna kipindi nashindwa kutofautisha vyama vya upingaji na chama twawala. Maana wanapingana huku wakiwala wanachama.

Juzi mwanakijiwe wetu tuliyekuwa tumempandikiza kwenye chama cha Calf, Amri Kirungu alituletea taarifa kuwa ameshitakiwa mbele ya kamati ya nidhamu feki iliyoundwa kumdhibiti Hamada wasijue itawakotea puani kuwa anazungumza mambo ya chama kwenye vijiwe vya kahawa! Ebo! Walitaka aongelee mambo ya calf kitandani au chooni? Stupid all of those who accuse other for what they actually do more than those they accuse.

Samahani. Nimepandisha Mwenembago hadi kuongea kisodoma! Ingawa wametutupia lawama kwa kufichua mambo yao ya aibu, wangoje sasa wakione cha moto kwa kuchezea hata mahakama baada ya kuwapiga stopu wao wakaendelea na ujinga ujinga wasijue zao zinahesabika.

Kumbatia alimfulila Kafulia sorry, Mariam Sefu Sahaulifu anataka kumnyotoa roho jamaa wa Ginigi na Wawe eti kwa vile alikuwa akija kijiweni kwetu na kumwaga siri za ulaji wake na wezi wengine waliotamalaki kwenye vyama vya ulaji viitwavyo vya upingaji.

Hata Rushid Amadi akitimuliwa na ile nyumba ndogo ya chama cha mafisadi na siri za kufanywa nyumba ndogo kwa chama cha Calf zimeishamwagwa tena kwenye vijiwe vyetu vya kahawa na sasa tunamwaga kwenye vijiwe vyetu vya magazeti.

Wao wamewafukuza nasi tumewapokea kijweni kwetu. Kwa sasa Hamada na Kafulia ni wanakijiwe wetu wapya wanaotupa hata siri za mjengoni na jinsi yule mama wa kucheza makidamakida anavyowaburuza na kuwatisha kiasi cha mjengo kugeuka genge la kutetea ujambazi na ufisadi.

Mimi kama rais na mwenyekiti wa vijiwe vya kahawa, natoa mwaliko kwa wanasiasa wote watakaofukuzwa waje vijiweni wamwage stori ili tuzisambaze kwa walevi na wanywa kahawa tuone hawa wanaojiandaa kugombea ukuu kama watapata kura.

Hata hawa jamaa wanaolangua umeme na wese tumeishapata taarifa zao na tunapanga kuwatokea siku moja na kuwagadafi kama siyo kuwamubaraka siku moja. Tuna mpango kamambe wa kuhakikisha tunawaleta walevi toka vijiwe vya jirani hasa kule kwa wakora Nairobbery waje waeleze ni kwanini kwao bei ya umeme na wese viko chini wakati sisi viko juu kama hakuna mkono wa watu wanaoleta wachukuaji wao kama yule Richmond na Downs wanaolipana nyuma ya pazia kwa kuwaibia walevi maskini. Shame on them! Hii kaya imeharibika kiasi cha kustahili kukameroniwa.

Chanzo: Tanzania Daima Januari 18, 2012

Monday 16 January 2012

Kuna harufu ya kujuana kwenye balozi zetu


Mindi Kasiga aliteuliwa hivi karibuni kwenda kwenye ubalozi wetu Washington. Huyu anasadikiwa kuwa na uhusiana na Rahma Kharoos Kasiga anayedaiwa kuwa nyumba ndogo ya bwana mkubwa na mkurugenzi wa kampuni ya mafuta iliyoibuka baada ya bwana mkubwa kuwa madarakani. Wengine wanasema ni mtoto wa dada yake Anna Mkapa. Mindi anaonekana akiwa na wadau wake mmojawapo akiwa Adam Gile. Hatujui kama huyu Gile ana uhusiano na Gile wa Richmond.
Kwa sasa tatizo la ajira nchini ni kubwa kuliko wakati wowote katika historia ya nchi yetu. Sambamba na hili ni kutamalaki kwa vitendo vya rushwa, kughushi, kujuana na kubebana katika ajira hasa zile nono. Kuna maeneo yanayopigiwa kelele na wananchi wa kawaida kwa sababu wao hawahusishwi katika ajira nono kwenye maeneo haya. Miaka mitatu iliyopita kuliibuliwa uoza wa kutishwa kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Kuligundulika majina mengi ya watoto au jamaa wa karibu au watoto wa marafiki wa vigogo kwenye ajira ya BoT kiasic ha kuliamsha taifa kuanza kujiuliza wahusika waliajiriwaje kule kwa wingi vile. Katika majina ya vigogo ambao watoto wao wameajiriwa BoT yalikuwamo majina kama Mwinyi, Lowassa, Mungai na mengine mengi tu. Hata hivyo, sijui ni kutokana na uzito wa majina na nafasi za wazazi wa waajiriwa kwenye jamii, suala hili liliachwa lijifie huku wahusika wakiendelea kuhomola. Hata ukienda kwenye taasisi nyingine zinazolipa vizuri au kuwa na nafasi nzuri ya rushwa kama vile Mamlaka ya Mapato, Uhamiaji, Utalii na madini, mbuga za wanyama, na kwingineko, utakuta mchezo ni ule ule. Watu wachache wenye majina wamepandikiza watoto wao kwenye maeneo haya huku watoto wa maskini wakiendelea kuteseka bila ajira.

Eneo jingine ambalo halikuwa likijulikana kuwa kichaka cha ajira za watoto wa wakubwa ni kwenye balozi zetu nje ya nchi. Ajira za nje zimekuwa siri kubwa ambayo si rahisi kwa mwananchi wa kawaida kujua au hata kufikiria. Hapa hatujaongelea nafasi mbali mbali yaani scholarship zinazotolewa na nchi marafiki ambapo wanufaika wengi ni wale wale-watoto wa vigogo, watoto wa marafiki wa vigogo na hata vigogo wenyewe.

Katika pita pita yangu kwenye vyombo vya habari mbali mbali nilikuta na kitu kilichonistua kidogo kiasi cha kusumbua akili yangu na kujenga dhana hata shaka na ajira za watanzania walioko kwenye balozi zetu nchi mbali mbali. Katika matukio mawili matatu kwenye habari, nilikutana na majina makubwa matatu haraka haraka. Hii ilinifanya nijiulize: je wapo watoto wa ngapi wa vigogo au hata vigogo wenyewe kwenye balozi zetu nje ambapo bila shaka wanalipwa vizuri? Je wameteuliwa au kuajiriwa kwa sifa za kitaaluma au kujuana au vyote? Je watanzania wamejulishwa na kuridhika na hili lililonistua au nao watastuka kama mimi?

Majina makubwa matatu niliyopambana nayo ni kwenye balozi mbili, yaani ule wa Umoja wa Mataifa na ubalozi wa Tanzania nchini Kanada. Majina haya ni ya Rose Mkapa afisa utawala wa ubalozi New York. Mkapa jina la familia ya rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Kwenye ubalozi wa Ottawa Canada, nilikutana na majina kama Richard Tibandebage ambaye ni afisa ubalozi. Kwa wenye kumbukumbuku, marehemu Andrew KajunguTibandebage alikuwa Balozi wa zamani wa Tanzania nje kwa muda mrefu chini ya awamu ya kwanza.

Joseph Sokoine, ni naibu balozi wa Tanzania nchini Kanada. Je huyu ni mtoto wa aliyekuwa waziri mkuu katika awamu ya kwanza, Edward Sokoine?

Yupo mwingine mwenye jina kubwa; naye ni Salome Sijaona balozi wa Tanzania nchini Japan. Je huyu ana uhusiano na Lawi Nangwanda Sijaona alikuwa mmojawapo wa mawaziri wa mwanzo?
Majina mengine ya vigogo ni ya Jaka Mwambi balozi Urusi ambaye alikuwa mkuu wa mikoa mbali mbali na naibu katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) bara na Adadi Rajab ni balozi Zimbabwe kamishina wa makosa ya jinai wa zamani.

Jina jingine kubwa ni la Maura W. Mwingira ni afisa ubalozi New York. Je huyu Mwingira ana uhusiano na kigogo mwingine, Augustine Mwingira mmojawapo wa mawaziri kwenye serikali ya awamu ya kwanza na mkuu wa mkoa kwenye serikali ya awamu ya pili.

Pia yupo Mindi Kasiga afisa habari wizara ya mambo ya nchi za nje. Kasiga ni jina linalohusiana na Rahma Kharoos Kasiga ambaye wengi wamemjua alipoibuka baada ya rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani.

Orodha haikamiliki bila jina Msekwa. Jacob Msekwa ni naibu balozi wa Tanzania nchini Sweden. Je huyu ana uhusiano na Pius Msekwa ni makamu mwenyekiti wa CCM. Jacob hayuko peke yake. Wapo Msekwa wengine ambao ni Erick Msekwa na marehemu Julius Msekwa. Msekwa wawili walio hai bado wanaishi ulaya.

Kigogo mwingine ni Ali Karume balozi wa Tanzania nchini Italia. Huyu anajulikana kuwa mtoto wa rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani Karume Pia Ali ni mdogo wa rais mwingine wa zamani wa Zanzibar Amani Abeid Karume.

Radhia Msuya balozi Afrika Kusini analo jina kubwa la Msuya. Hata hivyo, hatuna uhakika kama Msuya huyu na Cleopa David Msuya waziri mkuu wa zamani wana uhusiano. Uchunguzi mwingine unaonyesha kuwa Radhia Msuya ni mdogo wake Asha Rose Migiro ambaye kabla hajawa balozi kamili alikuwa London kwenye ubalozi wetu akiwa afisa ubalozi msaidizi. Inasemekana Radhia Msuya ana ndugu yake mwingine Fatma Mtengeti ambaye anafanya kazi kwenye ubalozi wetu huko Uingereza.

Mwingine ni Joyce Kafanabo ubalozi wa Tanzania Marekani. Kwa kumbukumbu ni kwamba Peter Kafanabo alikuwa kigogo wa CCM aliyewahi kuwa mkuu wa mikoa mbali mbali nchini. Pia yupo mama Mnanka kwenye ubalozi wa Tanzania nchini Marekani. Je huyu ana uhusiano na Bhoke Mnanka ambaye alikuwa mmoja wa mwaziri wa kwanza wa Tanzania huru.

Kwa ufupi, maswali ni mengi kuliko majibu. Hivyo tungeshauri wahusika lau wajibu huku wananchi wa kawaida hasa waathirika wenye habari kuhusiana na mchezo huu wazianike angalau umma ujue kinachoendelea. Kinachopaswa kupigwa vita ni kuhakikisha huu mchezo wa kujihudumia na kurithishana madaraka unakufa. Leo tumeongelea walioko nje ubalozini. Bado wale waliomo kwenye ngazi za uwaziri kama vile Hussein Mwinyi na Adam Malima.

Chanzo: Dira Januari 2012

Wednesday 11 January 2012

Boko Haram: What Must Nigeria Do?


Jama'atu ahlis Sunna lidda'awati wal-jihad or Boko Haram in Hausa is but haram in Arabic as its name denotes. Haram in Arabic means something illegal even dirty. I don’t know the meaning of Boko in any language that can show it as something illegal or otherwise. Again, Boko Haram can be translated as “Western education is sacrilege in Hausa.” Is it real western education sacrilege or Wild education in the name of Islam? If western education is sacrilegious as Boko Haram and the like-minded cronies think, what is an altenative education to it? Is it Arabic or Quranic one? Methinks, those saying western education is sacrilegious either do not know the meaning of education or, if they know, they have but a hidden agenda so to speak. Such assertion is not only horrible but it is horribly wrong and misleading. It is ludicrous and ridiculous. Again, why do Islamic academics allow their faith to be easily and cheaply abused by stooges such as Boko Haram with all ruckus and rumpus? Though in law silence does not plea of guilty, in a layman interpretation it means the contrary.

More on Boko Haram, by all standards including Nigerian laws, Boko Haram is illegal. Therefore, wiping it out of the surface of earth is legal. Many analysts ask: how was Nigerian government be able to vanguish groups such as The Movement for the Survival of the Ogoni People (MOSSOP) and Niger Delta People Salvation Front (NDPSF) but fail to eradicate terrost group Boko Haram?

Though it is against human rights to punish a person or persons without being heard or being tried by the court, when it comes to terrorist groups such Boko Haram, this prerequisite is not available. For they are not ready to follow proper channels put in place. For Boko Haram and the likes such as al Shabaab, all legal channels that are not put in place or being manned by them or likeminded, regard them as illegal entities. Therefore, such standpoint makes it difficult to consider such terrorist groups under the prerequisite of human rights where things such as natural justice, the right to be heard before being judged, presumption of innoncent and the like apply. How can you presume a person innocent while he is saying loudly and openly that he committed this and that just to fulfill the requirements of his religion? If anything, this is a challenge to human rights lawyers and the whole legal profession without forgetting even the parliaments the world over. In essence, what Boko Haram and the likes do by priding themselves that they committed atrocities like that that was committed on Christmas Eve whereby over 40 innocent people were felled, is self-inculpating. Therefore, such assertions and pleas wave the right to be heard or presumed innocent until the court of law decides otherwise or altogether.

Another precedent can be drawn from how Osama bin Laden was summarily killed by the US. Though the US has been criticized for killing bin Laden without bringing him to justice, what he used to do and say were nothing but self-inculpatory save that the US goofed by not condemning him to death before attacking his hidden posh residence in Abbotabad in Pakistan. It was simple. Charge him in absentia before the court of law and make sure you secure a death sentence then take on him and kill him legally. So, what Nigeria authorities even Kenyan can do now with regards to Boko Haram and al Shabaab respectively, is firstly, declare them legally to be terrorist groups under the law. Secondly, they must obtain the names of the ringleaders and charge them legally and officially and let the court, using already availabele pleas of committing atrocies alleged to have been committed by them as evidence to convict them. This is possible given that the jurisdiction of courts have expanded especially in dealing with atrocities and terrorism internationally. We therefore need to be nippy and steadfast; and thereafter, it will be legal, under all laws and presumpitions, to hunt down these terrorists and kill them without facing the wraths or allegations of violating human rights activists as it was in the case of bin Laden.

Another important thing to do is keep an eye on the source of income for Boko Haram. Where do they get money from? Who are their financiers? It is clear and obvious that such ragtag group cannot survive without being financed especially by foreign entities whose agenda is always what it carries out just like al Shabaab in Somalia.

Although Boko Haram, just like al Shabaab, has been priding itself to fight for Islam, this shebang shouldn't be subscribed to. The truth is: they are but copycats thanks to ignorance, dogma, brainwash and poverty.

As for Nigerian public, people should take on Boko Haram instead of waiting for the government while they are perishing unnecessarily. To do this, in areas where they suspect Boko Haram has sympathizers or agents hiding among them, they should apprehend them and hand them over to the government. Public eye, in this situation, is powerful and can have a corner in everything on the market as far as suffocating and stamping Boko Haram out is concerned. Again, Nigerians should not be fooled and be taken for the ride by Boko Haram’s razzmatazz and circus to believe that war against Boko Haram is war against Islam. It is war against terrorists who want to destabilize the country.

As for Nigerian government, it seems to sleep on the wheel. Otherwise, Boko Haram would have been history.
Source: The African Executive Magazine Jan. 11, 2012.

Utabiri wa mwaka 2012

Salaam aleikum waarahmatullahi wabarakatuhu. Alhamdulilah Wasalatu Wasalaam Ala Rasulullah Wa-ala-alihi Wa-as-habihi Ajmain.
Wapendwa wasomaji walevi na wanywa kahawa wote duniani na hasa nchini Daganyika bin Bongolalaland, mnajimu wenu mkuu Shehe Mpayukaji Msemavyo Mpakazaji wa Waambie anawaletea utabiri wa mwaka 2012 kama unavyoonyeshwa na nyota.

Kwanza, niweke wazi; sitabirii njaa wala umaarufu uchwara. Nimesomea haya madudu kuanzia Clairvoyance, poltegeistry, vampireology, psychometry, thouthtography, astronomy, astrology, cosmology, astrophysics, stigmata, dogmata, doppelganger, bilocation na madude mengine mengi ya kutisha ambayo nikiyaorodhesha yanatosha kuwa makala.

Kinyota, mwaka mpya unaonekana utakuwa mwaka wa ongezeko la matatizo.

Hii ni kutokana na nyota kuonyesha kuwa matatizo yatazidi ilhali wanaopaswa kuyatatua wakigeuka kuwa tatizo kubwa.

Nyota iliyotawala mwaka huu ni nge ikiuma kila kitu kuanzia maisha ya mtu binafsi hadi jamii kwa ujumla.

Kama nge, wenye mamlaka watawala wasio na mamlaka kiasi cha waliwa kuanza kujitambua na kujaribu kupinga uliwaji huu unaofanywa na hawa majahir murakhab.

Kadhalika, nyota zinaonyesha kutakuwa na ongezeko la vimbunga na mafuriko mbali mbali kuanzia maofisini hadi baharini.

Vimbunga hivi vitawakumba baadhi ya waliomo maofisini kiasi cha kujikuta kwenye hali ambazo hawakutegemea.

Kadhalika, ufisadi utaongezeka kutokana na ile hali ya kila mtu kujifanyia atakavyo na muda mwingi kupotezwa kwenye kusaka ngawira badala ya kuhudumia wahudumiwa. Mahospitalini, mahakamani, vituo vya polisi hata kwenye ofisi za ajira kutaongezeka rushwa kiasi cha kutisha.

Itafikia mahali, mwaka huu, haki kuuzwa kama njugu kutokana na mkanganyiko na mvurugano huu wa kinyota.

Kuongezeka kwa ufisadi kutasababisha ughali wa maisha na umaskini vitu ambavyo, kama vitatumika vizuri, kinyota, vinaweza kuleta ukombozi wa walio wengi.

Hii itategemea na wahusika watakavyojitambua na kutambua matatizo yao ya kweli ambayo ni watu na mfumo wanaousimamia kujitajirisha kwenye migongo ya maskini walio wengi.

Kuongeza chumvi kwenye kidonda, mwaka huu utashuhudia makapi mengi kuzidi kurudufiwa (recycling) ambapo wanasiasa waliokataliwa na wapiga kura majimboni mwao, watapewa ulaji kiasi cha kuwaacha waliowakataa vinywa wazi kwa hasira na mshangao na mfadhaiko.

Nyota pia zinaonyesha kuwa kukuwapo na ongezeko la vita ya mitandao ya ulaji na kumalizana katika kuusaka ukuu ambao siku hizi umegeuka dili hasa kutokana na kuwa nyenzo ya wanaoukwaa kula wao ndugu zao, familia zao hata wapambe zao hata bila kunawa.

Siku hizi ukuu si utumishi bali utumikishaji ambapo mwenye kuwa nao ni muungu mtu hapa duniani kutegemea na watakaomrithi.

Kama akiwa na bahati mbaya akarithiwa na watu wenye usongo na kaya yao basi humsweka lupango hata kumnyotoa roho kutokana na madhambi yake ya ukuuni.

Kama akipata vibaraka au marafiki zake basi hutanua maisha yeye na ukoo wake. Hamjaona wakuu wa zama zile ambao watoto wao nao wanatesa kiasi cha kuota hata kuwarithi wakuu wengine? Leo siwataji kwa majina ingawa hata kuku anawajua.

Sambamba na kuongezeka kwa mitandao, usanii pia utaongezeka kiasi cha kuongezeka kwa viongozi wa kiuroho wenye uroho wakisingizia Mungu wakifanya miujiza hata kufikia kukufuru kuiombea kaya badala ya kuiambia ukweli.

Hamkuwasikia wale nilio waonya kwao kuwa ni mbwa kwenye ngozi ya kondoo? Narudia, shauri yenu mtaliwa mwajiona.

Natabiri kuwa ataibuka mzee mwingine sawa na yule wa Loliyondo awalize wengi wenye kutaka mafanikio bila kutoa jasho ua kuficha magonjwa wanayougua kwa kuogopa kuambiwa ukweli kuwa wengine wameikwaa miwaya.

Atatokea mkoa gani? Atatokea katika mkoa mmoja kati ya pande za mashariki, magharibi, Kaskazini, Kusini na Kati. Atatokea muda gani toka sasa? Atatokea wakati ujao.

Pia natabiri kuwa vigogo watano watakufa mwaka huu. Kwa vile sitaki kuwatisha, sitataja majina yao wala vyeo vyao leo.

Ila watarudisha namba kati ya mwezi wa tatu hadi wa 11. Pia, wengine wataaanguka anguka hovyo mara kwa mara. Ingawa mvua zimenyesha na kusababisha mafuriko, mgao wa umeme utaongezeka sambamba na bei za umeme na nauli.

Pia natabiri kuwa ndoa ya chama cha Convention of Unreasonable Fellas (CUF siyo Chama cha Wananachi) na Convention of Conmen and Mafioso (CCM-siyo Chama cha Mapinduzi) itakuwa hatarini kiasi cha kugeukana kwa kushuku kutuhumiana kufikia malengo fichi.

Wawili hawa watashikana uchawi na kushutumiana kutapeliana.

Pia nyota zinaonyesha kuwa kutakuwa na poromoka zaidi la uchumi na thamani ya madafu.

Hii itatokana na kuongezeka kwa wezi wa madafu karibu kila mahali.

Nyota zinaonyesha kuwa pamoja na pigo hili kiuchumi, wakuu wataendelea kujisifia kuleta maendeleo huku wakiongezeana ulaji kuanzia kupandisha mishahara yao na kuongeza walaji hasa makapi, wana familia marafiki na waramba viatu.

Kutakuwa na ongezeko la wanachama wenye kidomo wanaopinga ulaji wa wakuu wa Vyama vya unoko na ulaji na hawa watatimuliwa.

Misiba midogo itaongezeka kiasi cha mkuu kupata fursa nyingi za kwenda matangani kuliko hata safari za kwenda ughaibuni ambazo nazo zitaongezeka chini ya visingizio mbali mbali.

Kadhalika ajali za barabarani zitaongezeka kutokana na kuongezeka kwa haraka za kutafuta njuluku kufidia kulanguliwa mafuta.

Mwisho kabisa kuna marais wanne wa muda mrefu wataangushwa kwa aibu kwa sababu nyota zao wote ni mizani.

Mizani itaanza kuelekea upande wa umma huku ikiwaacha wakiporomoka kama masuke.

Watawala hawa watakaoanguka nchi zao ziko upande wa kaskazini mwa nchi yetu.

Kwa upande wa kusini, rais mmoja bishololo mpenda mabibi ataumbuka na kuwa kwenye mgogoro mzito na waliomweka madarakani hasa vijana.

Pia katika nchi jirani na rais huyu bishololo mfalme mpenda kuoaoa ataingia kwenye matatizo ya kiuchumi kutokana na kuzidisha mabibi na matumizi huku wananchi wake wakiendelea kuwa maskini.

Kwa ufupi huo ndiyo utabiri wa mwaka mpya 2012. Kuhusu utabiri wa kijiwe, hii ni chiri yangu.
Chanzo: Tanzania Daima Januari 11, 2012.

Sunday 8 January 2012

Likitokea la kutokea tuseme kazi ya Mungu hapa?


Picha kwa hisani ya Michuzi blog.
Ingawa watu wetu ni maskini, tukubaliane kuwa umaskini wa kichwani ndiyo unaanza kutawala. Maana picha hii inatisha hata kuangalia acha kutokea lolote? Je wahusika hapa likitokea la kutokea, tuanze kumlaumu Mungu kweli au njaa zetu vichwani na ujinga wa kupita kiasi? Je watawala wetu waliotuahidi maisha bora wanajifunza nini hapa? Je hapa wa kulaumiwa si wote? Du jamaa wanavyojiamini utadhani wanateka maji!

Friday 6 January 2012

What a year that 2011 was!”

December is a time when writers, editors, analysts and all who make news what it is, are busy researching on what to write to wind up the year. Likewise, all media houses and outlets are busy hunting for a sound summary of the year. This is what this article is all about today.

Truly, the year 2011 was a year that empowered hoi polloi against hoit toity in many countries, especially in Africa. Time Magazine named “The Protester” as its Person of the Year. Indeed, thanks to tireless efforts and fearless heart of the protester, we evidenced strong men cascading like a cardhouse. It all started in Tunisia where on 14 January 2011, when a desperate young man Mohamed Bouazizi set himself on fire after being fed up with police harrasments. Just two weeks of the commencement of the year, Zine Abdeen Ben Ali was forced to flee to Saudi Arabia after demonstrators toppled his government under what was later known as Jasmine Revolution.

The Jasmine Revolution became a political meme. It did not end up in Tunisia. A month thereafter, it swept Egypt where a longtime strong man, Field Marshal Mohamad Hosni Mubarak became another casualty. On 25 January 2011 all major Egyptian cities caught on fire of revolution that culminated on 11 February when Mubarak stepped down after noting that the wind of changes was not on his favour.

While new development was registering on Maghreb, Africa south of Sahara was not spared. One of its democrat-turned-dictator president Laurent Gbagbo was at it with his arch foe, current president, Allasane Ouattra who defeated him in polls. The capture of Laurent Gbagbo on 6 April 2011 and handing him over to The Hague on 29 November to face the music was something that marked some changes in SSA, which has defied logic by not being gutted down by Jasmine Revolution. It remains as the place with many stinking dictators that are still safer thanks to lacking enlightened population.

Going back to the year and some of its breakthrough, on 2 May 2011 the world was awaked by the news that the head of al Qaida Osama bin Laden was killed by American seals. The saying “Jeronimo EKIA” or “Jeronimo the Enemy Killed in Action” as it was coined by the Seals, became a hit of its own.

Before long, the wind of change was still blowing in Maghreb. For on 15 February 2011, it started pounding Libya as demonstration commenced in Benghazi. Ever since fierce fighting ensued between the soldiers of the government of the long time ruler Muammar Gaddafi. Gaddafi coined the saying “zanga zanga”, namely surround them everywhere and kill them and the rebels in Benghazi. It took months to bring down the regime in Tripoli. On 20 October Gaddafi along with his son and chief of security were summarily killed as they were trying to escape after their convoy being attacked by NATO jets.

The year 2011 had another side of loss and gains in other circles. For it is in the same year on 25 September 2011 Kenya lost her beloved iconic daughter Nobel Laurete Wangari Maathai, who bravery fought cancer and later succumbed. That was a loss. The gains for Kenya in 2011 were immense.

The ruling about arresting Sudanese strong man, Omar Bashir, should he set foot on Kenya soil by a Kenyan judge, Nichola Ombija on Nov. 28, 2011, brought reliefs to Human Rights activists the world over, so as to uplift Kenya’s name internationally. Also the response of the judiciary to stick to its guns was a breakthrough.

2011 also saw Kenya entering Somalia to flush out al Shabaab. This occurred after thugs from Somalia entered Kenya and abducted three people, two Britons and a French woman who later died in the hands of her captors. This provoked Kenya so as to decide to take on al Shabaab under operation Linda Nchi or Protect the Country.

South of Kenya, it was all jubilations in Zambia, when on 23 September 2011 the opposition swept an incumbent president out of power. This was the second time for this nation to do so.

North of Kenya, in the Middle East, things were not so good. For the former president of Israel, Moshe Katsav was found guilt of rape and on 6 Dec 2011 he started to serve his seven year jail term in Maasiyahu prison. A week thereafter, former French president Jaques Rene Chirac (Bulldozier) was bulldozed before the court and found guilt thence, convicted for misappropriation of public funds save that, different from Katsav, he received a two years suspended sentence. Despite all, this was slap on the face.

The year wound up with the death of North Korean strong man Kim Jong Il on December 17th, 2011 at the age of 69 like Gaddafi. A day after, on 18 December 2011 the world lost a great son Vaclav Havel the former president of Czechoslovakia (1989–19920 and Slovak (1993-2003).

Economically, the year 2011 evidenced turmoil in the Eurozone whereby three countries were on the verge of collapsing economically. These are Italy, Greece and Spain.

Tanzania wound the year with very heavy and brutal floods that claimed the lives of over 40 lives.

As for Uganda, it was relatively calm save that there were some sparks regarding gay rights and the death of Rwandan exiled Journalist Charles Ingabire, who was gunned down on November 30, 2011.

In sum, generally speaking, the year 2011 was intaglioed with many imbroglios and scenarios for my crystal ball. It was but a potpourri. It was not easy to define so to speak.

Source: AfroSpear

Wednesday 4 January 2012

Tumemaliza mwaka kwa kumalizwa

INGAWA kila mmoja, kwa wale waliobahatika kuumaliza mwaka 2011, ana furaha kuumaliza, ukweli ni kwamba: tumeumaliza kwa kumalizwa hasa kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Dk. Al Haj, Profesa and what not true and false, Mpayukaji nilikuwa na mpango wa kwenda kijijini kuhiji. Lakini nilishindwa kutokana na ughali wa maisha hasa kupanda kwa wese kiasi cha kuwapa kisingizio fisi watu wetu kupandisha nauli kiasi cha kutisha. Kilichonishangaza ni ile hali ya wenye madaraka kuwa bize na ulaji wao badala ya kushughulikia jinai hii ambapo wauza wese waliunda serikali ya kijambazi ndani ya kaya.

Ukiachia mbali ughali na ulanguzi wa wese uliotusababishia mateso makubwa akina yakhe kwa kuishi kwenye nchi yetu kama wapangaji na wakimbizi, kulikuwa na tatizo jingine kubwa tu.

Badala ya kutatua matatizo ya walevi, wahusika walipoteza pesa nyingi kujinoma na sherehe za miaka 500 ya udhuru walioupachika jina la uhuru. Mabilioni ya madafu yaliliwa kwa kisingizio cha adhimisho hili la aibu. Unawezaje kuadhimisha aibu ukajisifu kuwa nawe si mtoto riziki?

Kitu kingine kilichoupamba mwaka uliokwisha ni mafuriko ya kujitakia kutokana na uvunjaji wa sheria na miundo mbinu mbovu na kichwa ngumu nayo yaliongeza pigo kwa walevi. Wengi walisombwa na kuuawa na maji huku wengine wengi akiwamo mgosi Machungi kuishia kwenye makambi ya wakimbizi wa mafuriko wakipokea misaada utadhani waliistahiki.

Ajabu eti wajanja hawa wameisharejea mabaondeni tena wakidai kuwa hawako tayari kuhama! Yaani wao wanataka kila mwaka tupoteze pesa na muda kushughulikia matatizo ya kujitakia siyo? Iko wapi nguvu ya serikali hapa? Nenda kule kamata weka ndani na ikiwezekana tupa rupango wale wote watakaojifanya hawataki kuhama ili kulinda biashara zao za gongo na bwimbwi. Nini hasira nao hawa jamaa. Na bahati yao mie serikali yangu ni ya kijiweni tu.

Kwa vile nafasi haitoshi, sitachonga sana. Mwaka 2011 ulishuhudia vituko vya wakubwa hasa pale marafiki wa damu walipogeuziana kibao na kuvalishana magamba baada ya kuvuana nguo mchana kweupe. Jikumbushe kipute baina ya Ewassa na Njaa Kaya kule kwenye kamati ya NECK au shingo la chama kilichogeuka kiama.

Mwaka 2011 pia kujuana kulizidi kiasi cha makapi yaliyosusiwa na wapiga kula ya kura kudufiwa na kupewa ulaji kwenye vijiwe vya nje. Nani mara hii kawasahau akina Bat (Popo)ilda Kwaherini, Phil Mammal, Dolorous Kamaliza, Mwanatunu Mainzi, Stela Ma-tomatoes na makapi mengine mengi? Kuna watu wamekosa aibu. Yaani unawapelekea watu makapi halafu unajisifu!

Katika mwaka 2011 wakuu walizurura sana duniani kiasi cha kuitwa Vasco da Gama wa kizazi hiki. Wakati wenzenu wakizurura tena kwa kutumia njuluku zenu, mwenzenu nilisafiri kikazi kwenda Tunisia, Masri, Libya, Cote de Voire, Syria na Yemen kushuhudia maimla walivyokuwa wakifurushwa na kuadhibiwa kama vibaka kama ilivyotokea kwa Kashafi baada ya kumshauri akaniona hamnazo kama hawa ninao washauri kila siku wao wakaishia kunichukia na kutaka hata kunibambikizia kesi za uchochezi na uhaini. Mie sitaacha kusema.

Ufisiahadi ndiyo usiseme. Mwaka 2011, kama kawa, njuluku ziliendelea kuibiwa huku wahusika wakijifanya hamnazo wala hayawahusu. Nani mara hii kasahau ujambazi wa UDAR ambapo wahusika wanajulikana na bado wako kwenye ofisi za kijiwe wakitanua wakati walipaswa kwenda rupango?

Kama siyo kufikiri kwa masaburi wahusika wangeishafikishwa kwa pilato na kukatiwa mvua zao mchana kweupe. Lakini nani amfikishe nani kwa pilato wakati wote ni akina Yuda Iskarioti? Hivi kweli ni halali nyani kumuadhibu ngedere wakati wote mchezo wao ni uleule? Je, hawa wajinga wanaowafuga nyani nao kweli si nyani maradufu?

Mwaka 2011 haukuishiwa vituko. Huko mjengoni nako kulikera baada ya wezi waitwao wadharauliwa kujiongezea madafu ya makalio ilhali wakiwaacha walalanjaa wakihaha kufukuzia njuluku ili wasukume muda. Nani anawajali wananchi iwapo wananchi wanaowakilishwa na ngulu mbili hawa ni matumbo yao na nyumba zao ndogo? Nani awajali wafu wasiojijali? Je, hapa mwenye kosa ni nyani au hata wale wamleao kwa kumuengaenga wakati walipaswa kumfanyia kweli bila kumuangalia usoni kama walivyofanya walibya kwa Kashafi?

Tukija kijiweni, uchumi wa kijiwe ulizidi kuporomoka kutokana na kutokuwa na uongozi makini na wenye akili zaidi ya uroho na roho mbaya. Ila good news kwa waroho wenye uongo ngozi ni kwamba kipato chao kiliongezeka kutokana na kuwageuza walevi shamba la bibi nao wasifurukute.

Kwa taarifa za kijasusi nilizopata ni kwamba kaya ilizidisha umatonya kiasi cha kutaka kugeuzwa shoga na hao wanaotupa sarafu kwenye bakuli. Nasikia baada ya kwa Mulla Omar na Iraki, tunafuatia sisi kwa kumwagiwa njuluku ingawa hakuna la maana tunalofanyia hiyo pesa zaidi ya kurejeshwa ughaibuni kwa mlango wa nyuma kutokana na ujuha wetu.

Pia mwaka 2011 ulishuhudia watasha wakitaka kutu-cameron. Ingawa tulifaragua kukataa ushoga, je, sisi si mashoga kiuchumi? Maana, hiyo misaada tunayopewa inatokana na kodi za hao hao mashoga. Unakula pesa ya kiti moto halafu unasema huli kiti moto siyo? Ni utoto na ujuha kiasi gani? Mie nshasema. Mtu hata awe mtasha au nani akinijia na hoja zake za ushoga nachomoa panga langu na kumkatilia mbali kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili. Hata hivyo tujisute. Inakuwaje kaya yenye kila rasilimali kuwa kapuku kiasi cha mkuu wake kujisifia ujuha na uhodari wa kutembeza bakuli? Acha jamaa watudhalilishe. Maana tunajidhalilisha wenyewe.

Kuna kipindi najikuta ni kicheka kwa huzuni kutokana na kushuhudia ushoga wa kisiasa tunaofanya. Nani mara hii kasahau kwa mfano Madevu kuwekwa kule Zaainzibaa baada ya kumwaga damu za wafuasi wengi waliodhani anawapigania kumbe wasijue alikuwa anawatumia kufukuzia ulaji? Je, hawa nao si mashoga wa kisiasa kama yeye?

Lo! Kumbe ni mwaka mpya! Herini ya mwaka mpya wa bundi. Sii yuu.

Chanzo: Tanzania Daima Januari 4, 2012.

Sunday 1 January 2012

Jaji Bomani: Wageni wanaimaliza nchi

MWENYEKITI wa Tume ya Kufuatilia Kampuni za Madini Serikalini (TEITI), Jaji Mark Bomani alikaririwa hivi karibuni akiishauri serikali kubadilisha sheria za madini ili kuepusha utoroshaji wa fedha na madini unaofanywa na wageni waitwao wawekezaji. Ingawa asemayo jaji Bomani ni kweli, wa kulaumiwa si wageni bali watawala wetu vibaka waliotanguliza matumbo badala ya uzalendo na uwajibikaji bila kuwasahau wananchi wanaovumilia au kufumbia macho upuuzi huu.
Tujiulize maswali rahisi: kama wahusika ndiyo hao hao walioasisi na kutekeleza ujambazi kama Richmond, IPTL, Dowans, EPA, CIC, TICT na mwingine mwingi ambapo pesa iliyokwisha kutengenezwa tena ikiwa kwenye benki kuu iliibiwa na hakuna aliyewajibishwa, watahangaika na madini ambayo yanawaletea ten percent bila kutoa jasho? Huwezi kutawaliwa na watu ombaomba tena wakijisifu kwa uhodari wa kuomba ukategemea haya yasitokee. Tatizo siyo sheria mbaya bali wanaozisimamia na kuzitunga kupitia chama chako ambapo hoja hupitishwa kwa kuunga mkono chama badala ya sheria na hoja.
“Hakuna mfanyabiashara anayeweza kusema ukweli juu ya faida gani anayoipata kutokana na kuchimba madini, haiwezekani Tanzania tuendelee kuwa masikini wakati madini yetu yanayotoka yangeweza kusukuma mbele maendeleo yetu,” alisema Bomani. Hii pia ni kweli na ahitaji kuwa jaji au profesa wa uchumi au sheria kujua kuwa huu ni wizi uliohalalishwa. Je wahusika wanafanya hivyo kutokana na ujinga au wanajua sema matumbo yao hayawaruhusu kuona ukweli huu. Hawa si wajinga: wengi ni wasomi tena wenye PhD lakini ni wa hovyo na waroho.
Je wageni wanaoimaliza nchi yetu ni wawekezaji tu hata wengine? Je mchezo huu mchafu ulianza jana au umekuwapo kwa miongo mingi hasa bada ya awamu ya kwanza iliyojitahidi kuziba kila miayanya ya udokozi na ujambazi wa wazi wazi? Baada ya kuondoka kwa awamu ya kwanza, wizi ulibarikiwa wazi wazi. Wakati huu tulikuwa na wahindi wakifanya udukawallah ulioficha madhambi mengi kama uhujumu wa uchumi, ulanguzi wa bidhaa, ukwepaji kodi na utoroshaji wa fedha za kigeni. Nani wamekuwa wanawasaidia kukwepa kodi, kupata vibali feki na kuingia na kuishi kinyemela ukiachia mbali kutorosha pesa yetu?
Nani hajui kuwa mabohari mengi ya wahindi siku hizi yameficha wageni haramu toka India ukiachia mbali ubaguzi katika ajira ambapo wahindi huletwa kufanya kazi za hovyo wakijidai ni wataalamu. Kwani hili halijulikani? Rejea kashfa maarufu kama vile Chavda, Somaia, vithlani na wengine wengi waliohujumu nchi hii kupitia ujuambazi mbali mbali wakishirikiana na wakubwa wetu lakini hawakufikishwa mahakamani. Je tatizo ni wao au walikuwa makuwadi tu? Idd Simba waziri wa zamani wa biashara aliwahi kudai kuwa uchumi wa Tanzania umo mikononi mwa wahindi wapatao 10. Nani alihoji au kustuka? Nani angestuka wakati wahusika wanajua ukweli kuwa wao ndiyo wanufaika wa zahama hii kwa taifa na watu wake?
Nani hajui kuwa kuna wageni wanaokuja Tanzania wakijidai wataalamu toka nchi jirani wakati si wataalamu kitu? Je wanaingizwa na kuajiriwa na nani kama si watanzania wenyewe ambao wamejigeuza shamba la bibi kutokana na ufisi na ubinafsi?
Wageni wanaopata uraia wetu kinyemela hadi wanakuwa hata viongozi waandamizi kama ilivyogundulika miaka michache iliyopita huko Kagera ambapo mwenyekiti wa CCM wa mkoa aligundulika kutokuwa mtanzania. Mpaka leo, CCM haitaki kueleza ni kwanini mtu ambaye si raia alikubaliwa chamani na kufikia kuwa kiongozi mkubwa bila mamlaka kustuka. Hapa hakuna cha kuficha wala kuzungusha. Wageni hawa haramu walitumia uroho na upogo wa CCM kujipatia uraia hata uongozi tena wa juu.
Sababu nyingine itakayoimaliza Tanzania ni kuwa na mipaka iliyo wazi ikisimamiwa na watu waroho wanaoitumia kama duka lao la kutengenezea pesa kwa kuwatoza rushwa wageni na kuwaruhusu waingie nchini na kufanya watakavyo. Kwani hili halijulikani? Anayetilia shaka hili aende mipakani aone maafisa uhamiaji wanavyokusanya pesa kama makondakta wa daladala na kutokea kuwa matajiri wasijue wanachezea maisha ya vizazi vijavyo. Kwa ufupi ni kwamba mipaka yetu haina ulinzi wala udhibiti wa kutosha. Tarehe 22 Desemba 2011, nchini Kenya kwenye bandari ya Mombasa mamlaka ya bandari ilikamata pembe za ndovu zaidi ya mia moja na zote zilitokea Tanzania kutokana na viroba vilivyokuwa vimehifadhi pembe hizo kuwa na nembo ya Kilombero Sugar. Na hii haikuwa shehena ya kwanza. Ukiachia hilo, nani hajui kuwa soko la madini ya Tanzanite ambayo yanapatikana Tanzania pekee duniani liko Kenya na Afrika ya Kusini? Lakini ajabu nchi bado inajisifia kwa uombaomba ikielezwa kuwa nchi ya tatu baada ya Irak kupokea misaada mingi duniani lakini pia ikiwa mkiani kiuchumi!
Kitu kingine kitakachoimaliza Tanzania ni ile hali ya watanzania kutokuwa na vitambulisho vya uraia. Ajabu ni miaka sasa tangu serikali itoe pesa ya kutengeneza hivyo vitambulisho. Wahusika wametia pesa mfukoni na vitambulisho havionekani zaidi ya kupiga kalenda kila uchao. Nani anahoji au kujali iwapo kila mtu ameshika lake? Viongozi wanafukuzia ten percent wakati wananchi wanafukuzia pesa ya kula. Njaa ya ubongo na tumbo vimechanganyikana kiasi cha kuiacha nchi iibiwe kana kwamba wakazi wake ima ni mataahira au wanyama na hayawani wasio na akili.
Pia kuna tatizo la kuajiriana na kuteuana kwa kuangalia uanachama, urafiki, kujuana na mambo mengine kama hayo ambapo wahusika hujifanyia madudu bila kuchukuliwa hatua kutokana na wanaopaswa kuwashughulikia kuwa jamaa zao.
Tumalizie kwa kusema kuwa tatizo la Tanzania kwa sasa si wageni bali watanzania wenyewe hasa viongozi makuwadi wa wageni wanaowatumia kama mawakala wao. Haiwezekani nchi yenye kila idara na nyenzo za kiserikali isijue kinachoendelea. Wahusika wanajua kila kitu lakini kwa vile wao ndiyo wanufaika, hata hizo sheria tunazosema wabadili wanazitunga wao na hawatazibadili. Maana kufanya hivyo ni kuharibu ulaji wao haramu.
Chanzo: Dira Desemba, 2011.