The Chant of Savant

Monday 30 August 2010

Tuhoji 'mafanikio' ya Kikwete









Taarifa kuwa kuna wabunge wa Chama Cha Mapinduzi zaidi ya kumi wamepita bila kupingwa si za kufurahisha hasa katika kipindi hiki tunapojigamba kukomaza demokrasia.

Hivi karibuni, kabla ya kuanguka akihutubia wafuasi wa chama chake, rais Jakaya Kikwete alijisifu kuwa amefanikiwa kustawisha demokrasia na haki za binadamu. Je ukiangalia hali halisi aliyosema Kikwete ni kweli au siasa na ghilba?

Ni mafanikio gani ambapo, karne ya 21, eti mtu anapita bila kupingwa? Tumejaribu kupitia baadhi ya majimbo na kushangaa. Hebu chukulia kwa mfano, jimbo la Karagwe ambapo mbunge aliyemaliza muda wake licha ya kukabiliwa na tuhuma za rushwa eti amepita bila kupingwa! Inashangaza sana. Je haya ndiyo mafanikio Kikwete anayopigia upata ya kukuza demokrasia? Mbona wale watuhumiwa wa kughushi vyeti vya taaluma wengi wao wamepita? Mbona mbunge Samuel Chitalilo aliyebainika kughushi vyeti na kuwadanganya wapiga kura hata watanzania amepeta bila kufikishwa mahakamani na sasa anastaafu na kupewa kiinua mgongo kwa jinai hii?

Kikwete alikaririwa akisema eti anajivunia kupambana na ufisadi! Hili nalo ni ajabu la maajabu. Kikwete amepambana na ufisadi gani iwapo watuhumiwa wakuu kama Andrew Chenge, Edward Lowassa, Basil Mramba na wengine wakipeta? Huku ndiko kupambana na rushwa kweli?

Yako wapi maisha bora kwa watanzania wote tuliyoahidiwa? Inatisha sana. Wakati Kikwete akijivuna kuwa amekuza demokrasia hasa haki za binadamu na upashanaji na upokeaji habari, siku aliyoanguka, wananchi walifichwa picha ya tukio kiasi cha kuondoa hata zile zilizokuwapo kwenye mitandao kipindi kidogo baada ya kuwekwa.

Kikwete angekuwa mkweli basi angetaja hata kinachomsumbua hivi sasa hadi akaanguka mara kwa mara. Kama alichomaanisha alikimaanisha kweli basi atuondoe kwenye shaka kuhusiana na afya yake ambayo imezua minong'ono mingi.

Tuhoji mafanikio ya Kikwete bila kuogopa mamlaka yake na chama chake. Tuhoji kwa ajili ya faida ya vizazi vijavyo nasi. Maana ni haki yetu na nchi hii ni yetu si ya Kikwete wala CCM. Huwezi kuwandanganya watu mchana kutwa wakakuacha bila kuhoji. Tujalie kuwa Kikwete alimaanisha alichosema. Je hajui kuwa watanzania hawakupata picha kamili ya tukio ukiachia mbali maelezo yanayoingia kichwani?

Je Kikwete ambaye amejizungushia waramba viatu na wapambe waliomgeuza kipofu na kiziwi kuhusu vilio vyetu, haoni watanzania wanavyotaabika ukaichia mbali kungoja kuonja maisha bora kwa miaka mitano bila kitu?

Ingawa ni haki yake kujinadi ili achaguliwe, Kikwete atutendee haki-atwambie ukweli. Akiri pale alipokosea au kulega lega. Bahati mbaya sana, kwenye mikutano yake ya kampeni huwa hakuna fursa ya kuuliza maswali zaidi ya kuhubiriwa. Je huku ndiko kukomaa kwa demokrasia? Amekwepa hata kushiriki midahalo angalau aulizwe maswali. Je huku ndiko kukuza demokrasia na kutekeleza aliyoahidi?

Juzi nilisikia akijitapa kuwa hata ujambazi umepungua! Ebo! Hivi Kikwete alisoma habari za kifo cha Profesa mashuhuri wa sheria marehem Jwan Mwaikusa? Mbona kila siku magazeti yanafurika habari za majambazi 'kutesa' tena kwenye jiji anamoishi Kikwete-Dar es salaam ambayo si bandari salama tena bali bandar nakama?

Siandiki makala hii kwa chuki dhidi ya Kikwete bali upotoshaji uliojitokeza kutokana na tambo zake. Ukitaka kujua ninachomaanisha, kwa wanaoishi Dar, hebu nenda kwenye hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana uone wagonjwa wanavyorundikana. Hebu hoji matumizi yake hasa kwenye ziara zisizo na faida ughaibuni ambako, baada ya kuanguka wengi wanaanza kusema kuwa huenda kujitibia ingawa si imani yangu kuwa ni hivyo.

Ni juzi tumetaarifiwa na mkaguzi mkuu wa pesa ya serikali (CAG) kuwa, kwa mwaka jana tu,

zaidi ya shilingi 1,700,000,000,000 ziliibiwa kwenye idara za serikali. Je haya ndiyo mafanikio ya kujivunia ya Kikwete? Hapa bado hujaangalia mabilioni mengine yaliyoibiwa miaka iliyotangulia. Kama tutafanya hesabu ya kweli ya kutoa na kujumlisha kuhusiana na wizi wa pesa za umma chini ya Kikwete, hatutakuwa na haja ya kumrejesha madarakani. Ametuangusha sana hasa kwenye kudhibiti na kutumia pesa na raslimali zetu.

Nilimsikia akijisifia kuwa amepanua wigo wa mapato kwa kukusanya pesa nyingi karibu mara mbili ya zile zilizokuwa zikikusanywa na mtangulizi wake. Well done. Je amezisimamia vipi kuhakikisha hazichotwi na wezi wachache wateule? Kukusanya pesa nyingi na kufuja nyingi zaidi si mafanikio wala jambo la kujivunia bali la kutia aibu na kukatisha tamaa. Je tutaendelea kudanganywa hadi lini?

Si uzushi. Serikali ya Kikwete, kwa miaka mitano iliyokuwa madarakani, imetuangusha kwa mambo mengi. Ni juzi juzi waziri wa miundombinu, Shukuru Kawambwa alikaririwa hivi karibuni akionyesha mafanikio ya Kikwete kama ifuatavyo: “Ukiangalia utendaji wa bandari za nchi jirani na zetu utakuta za kwetu ziko chini sasa lazima tukae tujiulize kwanini tuwe na viwango duni vya utendaji kuliko wenzetu.”

Alitoa tamko hili baada ya kupata habari kuwa wateja wengi wa bandari ya Dar es salaam wameamua kupitishia mizigo yao nchi jirani kutokana na bandari ya Dar es salaam kukithiri kwa udokozi na wizi wa mizigo na ucheleweshaji unalonga kutengeneza pesa kwa njia ya rushwa. Je haya ndiyo mafanikio anayojivunia Kikwete?

Wako wapi watuhumiwa wa ujambazi wa kutisha wa EPA hasa kampuni la Kagoda linalodaiwa kumilkiwa na mbunge wa Igunga na swahiba mkuu wa Kikwete, Rostam Aziz?

Kuna swali kuu la kupaswa kujiuliza. Hivi Kikwete kweli angekuwa amefanikiwa kama anavyotaka tuamini, angehitaji kuchangiwa shilingi 50,000,000,000 na kusema kuwa takrima haiepukiki? Je huku si kushindwa vibaya sana kunakoitwa mafanikio?

Tuache utani kwenye mambo yasiyohitaji utani. Kikwete hajafanikiwa lolote. Na kwa wanaojua tabia ya binadamu hasa kwa kuzingatia uzoefu wa mtangulizi wake, akishapata ngwe hii ya lala salama, ata-mess zaidi.

Leo sitasema sana zaidi ya kuwataka watanzania hasa wapiga kura kuhoji na kuhoji na kuhoji hiki kitendawili ambacho Kikwete anakiita mafanikio wakati ni maanguko. Je huu ndiyo usanii ambao watani wake wamekuwa wakimtwisha? Mafanikio ya Kikwete hayawezi kupimwa kwa maneno yake bali hali za wananchi. Kwanini afanye mtihani halafu ajisahihishe mwenyewe na kujipa mia kwa mia wakati aliambulia nunge?

Watanzania tuache kuweka maisha yetu rehani kwa kunogewa na maneno na longo longo za wanasiasa wanaotutumia kama punda kubeba mizigo na madhambi yao. Kuna haja ya kufanya mapinduzi na kuchagua mstakabali wetu badala ya ushabiki wa kipumbavu unaoweza kufakamia kila uongo kwa kujali anayesema badala ya kinachosemwa.

Ajabu la maajabu ni ile hali ya kila kitu kusimamiwa na chama kilichotopea kwenye rushwa. Rejea yaliyojiri kwenye mchakato wa kura za kutafuta wagombea wa CCM. Hakika tuna kila sababu za kuhoji na kuhoji bila kukoma 'mafanikio' ya Kikwete ambayo ni mateso na maanguko ya umma.
Chanzo: Dira ya Mtanzania Agosti 30, 2010.

Sunday 29 August 2010

Sababu za watanzania kutoichagua CCM mwaka huu


















Niseme mapema. Mwaka huu sitaichagua CCM. Naamini sababu za kutofanya hivyo zinashawishi. Natoa sababu zifuatazo:

Mosi, ufisadi- CCM na serikali yake, licha ya kushindwa kukabiliana na ufisadi, hazijawahi kukanusha kuhusika na kashfa za Richmond, EPA, CIS na nyingine ambazo zilizamisha mabilioni hata matrilioni ya shilingi za umma. Ni juzi tu mwanasheria maarufu Mabere Marando alidai EPA ni mradi wa CCM ulioanzishwa kupatia pesa ya kumwingiza madarakani rais Jakaya Kikwete ambaye si yeye wala chama chake wamekanusha tuhuma hizi. Na hii si mara ya kwanza tuhuma hizi kutolewa. Hazijawahi kukanushwa. Ijulikane. Tuhuma hizi ni nzito na hazisahauliki wala kufichika hata kuziacha zijifie.

Pili, matumizi mabaya ya fedha za umma. Rejea ziara zisizo na faida za rais na mkewe nje na kuficha majina ya wajumbe wanaoandamana nao. Pia rejea ununuzi wa magari ya bei mbaya (mashangingi) ambapo inadaiwa serikali inamilki zaidi ya mashangingi 6,000 na kujilipa per diem. Pia kuna hili la ujenzi wa nyumba za mabilioni za watendaji wa serikali. Rejea kashfa za BoT na TANESCO.

Tatu, matumizi mabaya ya raslimali za umma. Rejea ubinafsishaji wa kifisi, mgao usio wa lazima wa umeme na nchi kukaa kizani kwa mwaka mzima karne ya 21 huku wezi wachache wakichota mabilioni kwa kutumia Richmond na serikali ikikaa kimya. Hapa hujagusa misamaha ya kodi yenye kila harufu ya rushwa.

Nne, viongozi wakuu wa serikali kutotaja mali zao kama wanavyotakiwa na sheria. Je kama siyo wezi wanaogopa nini? Je wanatoa picha gani kwa wananchi hasa kuhusiana na uwajibikaji wao? Je wana mali kiasi gani?

Sababu ya tano ni uzembe-kuibiwa pesa nyingi kwenye wizara na taasisi za umma ni juzi tu tuliambiwa kuwa mwaka jana kiasi cha shilingi 1,700,000,000 kiliibiwa. Hebu piga picha kwa nchi yenye bajeti ya trilioni 11 na ushei. Hii maana yake ni kwamba kilichoibiwa kwa mwaka mmoja ni sawa na 1/5 ya bajeti ya taifa ambalo hutegemea wafadhili kwa asilimia 40 ya bajeti yake. Je huu ni uzembe kiasi gani? Je kwa miaka mitano ya utawala wa kisanii zimeibiwa trilioni mamia mangapi? Je haya ndiyo maisha bora?

Sita, dhambi ya kujuana. Vyeo vingi hasa vya juu vyenye malipo manono vimekuwa vikigawiwa kwa upendeleo na kujuana. Rejea kwa mfano rais kumteua rafiki yake waziri mkuu mfukuzwa Edward Lowassa aliyeboronga baadaye kuthibitisha ubaya wa hili.

Sababu ya saba ni kutamalaki kwa rushwa. Rejea yaliyojiri hivi karibuni kwenye uchaguzi wa ndani wa kura za maoni wa CCM. Hawawezi kukwepa. Tena wamekamatwa na TAKUKURU yao.

Nane, masimamango. CCM na viongozi wake wamekuwa wakitusimanga kuwa watatuletea maisha bora wakati, kimsingi, wanaposema maisha bora kwa wote wanamaanisha wao, familia zao, marafiki zao na wawekezaji wa kweli na uongo.

Tisa, kutotimiza ahadi hata moja. Mwenyekiti na mgombea wa CCM aliyechangiwa mabilioni alituahidi mambo mengi hasa pepo. Kuna haja gani ya kumchagua kwa kutulipa jehanamu mahali alipoahidi pepo? Yako wapi maisha bora kwa watanzania ukiachia mbali watu wake wa karibu ambao hata wakiiba au kughushi vyeti hawaguswi?

Tisa, ni uongo. Hakuna serikali yenye kusema uongo kama ya CCM. Kila mtu anawahadaa wananchi kuwa ataweka maslahi ya nchi mbele wakati ukweli wanaweka maslahi ya chama na yao binafsi mahali pa maslahi ya taifa. Na hii ndiyo siri ya mafisadi kila aina kutamalaki na kuneemeka chini ya CCM ambayo watani wake huiita Chama Cha Mafisadi. Bahati nzuri Kikwete aliwahi kusema ana orodha ya majambazi, mafisadi, wala rushwa, wauza mihadarati na wengine wengi. Amezifanyia nini hizi orodha?

Kuna hili la ukosefu wa usalama. Rejea mauaji ya vibaka, vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi wakati majambazi na mafisadi yakilindwa.

Sababu nyingine ni kupanua ukubwa wa serikali bila sababu. Rejea kuundwa mikoa mitatu na kugawanya baadhi ya wilaya kwa maslahi binafsi ya kisiasa kichama na makada wake. Tunataka huduma bora si ukubwa wa serikali ya kishikaji.

Kutosimamia uchumi wa nchi vizuri. Rejea kwa nchi yenye tamalaki ya madini kuwa maskini kuliko hata nchi zilizotoka kwenye majanga jana tena ndogo kama Burundi na Rwanda. Je pesa ya raslimali zetu inakwenda wapi na kumnufaisha nani iwapo watu wetu wanazidi kuwa maskini?

Utawala mbovu usio na mipango wala ubunifu. Rejea maisha magum na ukosefu wa mbolea pembejeo na masoko kwa wakulima na kejeli ya kilimo kwanza wakati ni uwekezaji ubinafsishaji na ufisadi kwanza.

Kuua elimu, rejea kuwa na matundu mengi yaitwayo madarasa yasiyo na vifaa wala walimu.

Kuchusha na kuchoka kwa CCM. Rejea maneno ya baadhi ya waliowahi kuwa viongozi wake kuwa CCM haina mwelekeo na imetekwa na wafanyabiashara nyemelezi. Hayakunushwa zaidi ya wahusika kuuawa au kukolimbwa kama ilivyokuja kujulikana baadaye.

Kuna hili la migongano na migawanyiko ndani baina ya makundi ya kimaslahi au mitandao. Makundi haya yanakula muda na pesa nyingi ya umma kwenye kumalizana badala ya kutatua matatizo ya wananchi yaliyofanya wahusika wachaguliwe. Hawa wengi wao ni wabunge wa CCM wanaojiwakilisha kwa kuwahadaa wananchi kuwa wanawawakilisha.

Pia sitaichagua CCM kutokana na kuua demokrasia. Rejea kutokuwapo kwa tume huru ya uchaguzi na msajili wa vyama kutumika kuviua na kuviminya vyama.

Matumizi mabaya ya vyombo vya dola. Rejea polisi kutumika kuwanyanyasa wananchi huku walimu wakitumika kama ajenti wa uchaguzi wa CCM.

Umaskini na maisha duni kwa umma na maisha bora kwa watawala. Rejea kurundikana kwa wagonjwa mahospitalini hadi wanne kitanda kimoja na wanafunzi mia darasa moja huku kikundi cha watu wachache kikiogelea kwenye kila neema ambazo ni mateso ya umma.

Uchakachuaji wa haki na hata mafuta. Hili mmeliona kwenye magari ya ikulu na uchaguzi wa CCM. Kila kitu kwa sasa ni kuchakachua!

Uhujumu wa uchumi. Rejea kikundi cha watu wachache kupeana tenda za ujenzi wa barabara na majengo yasiyofikia viwango hasa mashule na zahanati.

Kuwekeza kwenye siasa badala ya maendeleo ya kiuchumi. Rejea ukweli kuwa CCM iko tayari kuwalinda wanasiasa wake fisidi kwa gharama ya uchumi wa nchi na wananchi. EPA na Richmond ni mifano mwanana.

Chanzo: MwanaHALISI Agosti 23, 2010.

Friday 27 August 2010

The world tallest teen


Elisany Silva is the tallest teen in the world and she is using her height to her advantage. The Brazilian teen, she lives in a small village called Bragança, has her sights set on the runway and her dream is about to come true. Silva will reportedly be making her modeling debut in a Bridal show very soon.

Yes the Brazilian beauty is about to break into the fashion world and what designer in their right mind would not want her to work for them. If you don’t believe me just check out some pictures of Elisany here, sorry the girl in the photo is not her but she is quite intriguing isn’t she?

Back to Silva although her height will certainly help her desire to become a model it also has its drawback, as I am sure we can all imagine. For example Elisany doesn’t go to school because she can’t fit in the school bus, she has trouble walking around her own house and sadly her condition does not allow her to play with her friends. I have to say I feel inspired by this young girl yet sad for her at the same time

So what exactly is the disease or cause of Silva’s usual height? Well that remains to be seen although some doctors have said she may have Giantismo Elisany’s mother has stated that the family does not have the money to find out the root of her daughters tremendous growth rate or the money to fix it. The Silva’s have six other children all of whom are within the normal, whatever that means, height range.

I tell you what Elisany Silva may be the tallest teen in the world and she may not know what is causing her to grow so tall but she isn’t going to let that hold her back. I have a feeling we will all be seeing more of the beautiful aspiring model.

Fidel Castro: Osama bin Laden is a US agent





HAVANA - Fidel Castro says al-Qaida leader Osama bin Laden is a bought-and-paid-for CIA agent who always popped up when former President George W. Bush needed to scare the world, arguing that documents recently posted on the Internet prove it.

"Any time Bush would stir up fear and make a big speech, bin Laden would appear threatening people with a story about what he was going to do," Castro told state media during a meeting with a Lithuanian-born writer known for advancing conspiracy theories about world domination. "Bush never lacked for bin Laden's support. He was a subordinate."

Castro said documents posted on WikiLeaks.org — a website that recently released thousands of pages of classified documents from the Afghan war — "effectively proved he was a CIA agent." He did not elaborate.

The comments, published in the Communist Party daily Granma on Friday, were the latest in a series of provocative statements by the 84-year-old revolutionary, who has emerged from seclusion to warn that the planet is on the brink of nuclear war.

Castro even predicted the global conflict would mean cancellation of the final rounds of the World Cup last month in South Africa. He later apologized for jumping the gun. Last week, he began highlighting the work of Daniel Estulin, who wrote a trilogy of books highlighting the Bilderberg Club, whose prominent members meet once a year behind closed doors.

The secretive nature of the meetings and prominence of some members — including former U.S. Secretary of State Henry Kissinger, senior U.S. and European officials, and major international business and media executives — have led some to speculate that it operates as a kind of global government, controlling not only international politics and economics, but even culture.

During the meeting, Estulin told Castro that the real voice of bin Laden was last heard in late 2001, not long after the Sept. 11 attacks. He said the person heard making warnings about terror attacks after that was a "bad actor."

Castro stepped down due to ill health in 2006 — first temporarily, then permanently — and handed power over to his younger brother Raul. He has remained head of the Cuban Communist party but stayed out of view for four years after falling sick before returning to the spotlight in July.

Castro did take exception with one of Estulin's major theses: that the human race must move to another habitable planet or face extinction.

Castro said it would be better to fix things on Earth then abandon the planet altogether.

"Humanity ought to take care of itself if it wants to live thousands more years," Castro told the writer.
Source: Paul Haven, The Associated Press

Wednesday 25 August 2010

Uraia wetu unauzwa kama njugu



INGAWA mchakato wa kupata vitambulisho vya utaifa bado unaendelea, huku kukiwa na mawazo tofauti kwamba ni mradi mkubwa kwa wakubwa wachache waroho kujipatia mabilioni ya fedha, visipopatikana nchi itatawaliwa na wageni hata magaidi.

Hii ikichangiwa na uhamiaji kugeuka kuwa duka la kulangulia pasi za kusafiria na nyaraka nyingine muhimu, Huko tuendako hali itakuwa mbaya zaidi.

Nani hajui kuwa kuna 'Watanzania' wengi wa kughushi na kununua? Nenda ofisi ya vizazi na vifo uone watu wanavyonunua 'Utanzania' kama njugu. Kwani hili halijulikani? Jiulize. Wale wakimbizi wa kiuchumi wanaoingizwa kwa maelfu kutoka Asia huishia wapi zaidi ya kununua Utanzania na kuwa Watanzania safi? Nani anajali?

Katika eneo zima la Afrika Mashariki, ni uraia wa Tanzania unaoweza kununuliwa na si kununuliwa tu bali kwa bei ya kutupa. Ukimwambia Mkenya, hata awe mroho kiasi gani wa pesa kuwa unaweza kununua pasi ya Kenya, cheti cha kuzaliwa au uraia atakushangaa na kudhani unapaswa kupimwa akili.

Lakini ukija Tanzania, kuuza uraia sawa na haki nyingine ni kitu cha kawaida. Nimekuwa nikionya tabia ya umbwa na upanya unaoendeshwa na ufisi ufanywao na mafisadi wachache ama wenye madaraka au wasio na madaraka lakini makuwadi wa wenye madaraka. Sasa tazama. Tunaipeleka nchi kuzimu.

Matukio ya hivi karibuni yaliyowahusisha waliokuwa wakiwania kuteuliwa kugombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) huko Nzega hivi karibuni, yamefichua udhaifu wa mifumo na nchi yetu. Wagombea wawili wa ubunge Hussein Bashe na Hamis Andrea Kigwangala yanapaswa kutufungua macho.

Hebu fikiria. Mtu ambaye anasemekana si raia anapewa madaraka makubwa nchini bila mamlaka kujua. Tunaambiwa Bashe ni Msomali ingawa anakanusha. Anajaribu kujitetea. Analeta hati za uthibitisho wa uraia wake kwa nyaraka za mwaka jana! Kwa nini uraia wake uthibitishwe mwaka jana na si kabla ya kupewa nyadhifa kubwa sawa na zile alizovuliwa kwenye umoja wa vijana?

Tunaambiwa amefanyiwa fitna na mahasimu wake yaani Benno Malisa makamu mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM- UVCCM, na swahiba wake mkuu Ridhiwan Kikwete mtoto wa mwenyekiti wa CCM na rais wa jamhuri.

Je, kwa nini mahasimu wake watumie kigezo cha uraia kama hakuna ukweli? Je walijua kuwa si raia na kwa vile alikuwa anaweza kulinda maslahi yao, hili halikuwahangaisha hadi alipotishia maslahi yao?

Je, tunao wakubwa wangapi kwenye CCM wenye udhaifu huu unaotumiwa na wenzao kuwatumia? Je, ni kwa nini mtu anapokosana na vigogo wa CCM au watoto wao ndipo anakuwa si raia? Je, wanawapa ulaji watu wasio raia wakijua udhaifu wao ili wawatumie vizuri kwenye kuhujumu nchi? Hili linawezekana.

Rejea kashfa zenye kuhusisha mabilioni ya shilingi kutendwa na wakubwa zetu kwa kushirikiana na mawakala wao wa kigeni hasa wahindi. Tuna mifano mingi mkubwa ukiwa ule wa VG Chavda ya wizi wa mabilioni na ununuzi wa mashamba ya mkonge.

Je, alipogundulika wakubwa zetu waliomtumia walifanyaje ili kuficha nyuso zao? Walimtimua nchini badala ya kumfikisha mahakamani kwa kuhofia angemwaga mtama kwa kuku.

Kinachoshangaza sana ni kile kilichoripotiwa na vyombo vya habari kuwa kuna uwezekano Bashe alijitetea kwa kutumia nyaraka zinazosemekana ni za kughushi. Je amechukuliwa hatua gani? Nani atamshitaki iwapo wengi wanaopaswa kushinikiza nao wamegushi vyeti vya taaluma na hakuna anayewagusa?

Hata ukichunguza kashfa ya Richmond iliyomfurusha waziri mkuu wa zamani na swahiba wa Rais Kikwete, Edward Lowassa, kashfa ya ununuzi wa rada na ndege ya rais. Nyuma ya kashfa hizi kuna wakubwa fulani na kundi la wageni nyemelezi wanaosemekana kumilki uchumi wetu kwa asilimia 99. Je hapa tunaweza kujidai tuko huru? Je hapa watawala wetu si mawakala wa kawaida tu wa mitandao ya kijambazi ya kimataifa?

Kashfa ya Bashe ni ushahidi kuwa tusipoua mitandao ya kibiashara na kisiasa tutakuja kustukia nchi yetu imeuzwa kwa wageni ambao kwa sasa wameelekeza nguvu zao kwenye ubunge ili watunge sheria za kuwalinda na maslahi yao ambavyo ni hatari kwa mstakabali wa taifa.

Chanzo cha hii yote ni kumomonyoka kwa maadili ambako kumechukuliwa na madili ambapo mtu hulala maskini na kuamka bilionea na hakuna mamlaka inayombana aeleze alivyoupata utajiri wa ghafla hivi.

Uhamiaji wanauza pasi za kusafiria. Kigezo cha kufanya hivi ni pesa badala ya sheria. Kuna 'Watanzania' wa kuchongwa wanaopata pasi za kusafiria hata vyeti vya kuzaliwa bila hata kuweka mguu uhamiaji. Watakwendaje iwapo kuna mawakala wa kufanya kazi hii chafu?

Hali ni mbaya sana. Baadhi ya watendaji wa uhamiaji wana watu wao nje ya ofisi zao wanaowakuwadia watu wanaotaka pasi 'chap chap' kwa mshiko wa hali ya juu.

Kimsingi tusipokengeuka na kupambana na ufisadi na utawala wa kifisi na binafsi wa kubabaisha, tutazua vurugu huko tuendako. Hebu fikiria. Mtu anatoka India jana. Kesho anakuwa raia hata bila kujua lugha ya taifa.

Leo nitatoa mfano wa hapa Kanada. Mtu yeyote haruhusiwi kuwa raia wa Kanada hadi aijue historia ya nchi na moja kati ya lugha mbili za taifa yaani Kiingereza na kifaransa. Na muombaji hutahiniwa kuthibitisha hili.

Pia kupata uraia wa Kanada humchukua muombaji miaka mitatu ambayo anapaswa kuishi nchini humu bila kutoka hata siku moja mbali na zaidi ya mwaka wa kungojea matokeo. Maombi ya uraia huchukua muda mrefu. Hii ni kuzipa mamlaka muda wa kutosha kufanya uchunguzi juu ya muombaji ili zisitoe uraia kwa mtu asiyefaa.

Muombaji lazima awe na rekodi safi. Asiwe na kesi ya jinai au kuwahi kuhukumiwa kwa kesi ya jinai. Je, hali nchini mwetu ikoje? Mfuko wako.

Na wanaofanya uchafu huu washukuru ujinga wa raia wa kawaida wa kutojua madhara ya kuchezea uraia wao. Lakini kutokana na kupanuka kwa mawasiliano na matatizo yasababishwayo na wageni, kuna siku watu wetu watajua haki zao na kuzidai saa nyingine kwa njia yenye kuvuruga taifa.

Hivyo wahusika badala ya kutumia vigezo vya nani si raia na nani ni raia kisiasa, wanapaswa kufanya hivyo kisheria tena kwa maslahi ya vizazi vijavyo. Nchi ya Ivory Coast imegawanyika na kufikia karibu na kusambaratika kutokana na kuachia wageni wanaosemekana toka Burkinabe wajiishie na kufanya wasio paswa kufanya hadi wakajiona wana haki kuliko wananchi na kuiingiza nchi kwenye machafuko yanayoendelea kuigharimu chi hii iliyosifika kwa ustawi na utulivu wake.

Leo wananchi wa Darfur nchini Sudan wa makabila ya Fur, Masariti na Zagawa wanauawa na wageni waliowakaribisha yaani makabila ya Bargwu, Dajo Tama na mengine walipokimbia njaa nchini mwao Chad miaka ya 80.

Serikali haramu ya Khartoum inawatumia wageni hawa kuwaua wenyeji wao wakisaidiana na Janjaweed.

Tufupishe mada. Tanzania na watanzania tusipoacha kuangalia vijisenti kidogo vya kukidhi mahitaji binafsi ya kilafi, tutauza nchi yetu kwa wageni ambao hapo baadaye hawatakuwa na huruma nasi.

Kuna haja ya uhamiaji na serikali kwa ujumla kuachana na umachinga wa kitu muhimu kama uraia. Na Watanzania tuachane na tabia ya kuwa watazamaji hasa pale haki zetu zinapoporwa na wezi wachache wenye nafasi.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 25, 2010.








Masha na Makamba wanamdanganya nani?









Hakuna kitu kilichonistua kama majibu ya ajabu ya waziri wa mambo ya ndani Lawrence Masha pale alipotakiwa na waandishi wa habari kuelezea msimamo wake kuhusiana na sakata la mgombea ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Nzega aliyeenguliwa kwa sababu ya kutokuwa raia, Hussein Bashe.

Alipoulizwa nini msimamo wake alijibu kuwa suala la uraia wa Bashe halina utata!

Alikaririwa akisema: “Hakuna utata kwenye uraia wa Bashe. Naweza kusema hivyo.” Jibu hili la ajabu liliwachanganya waandishi wa habari hadi kuzidi kumchimba na kutaka kujua kama Bashe ni raia au si raia alizidi kujichanganya na kuwachanganya wananchi. Alisema : “ Nasema hakuna utata kwenye uraia wa Bashe na siwezi kuzungumzia suala hilo zaidi. Sikilizeni, hili suala halina umuhimu kama mnavyolizungumzia.”

Hayo ndiyo majibu ya mtu anayeitwa waziri tena wa wizara ya mambo ya ndani. Hebu msomaji tufikiri pamoja. Je kwa majibu haya waziri umeelewa nini? Je kwa majibu yalivyo, ulitegemea yatolewe na mtu mwenye dhamana ya waziri? Je kwa majibu hayo, unaelewa nini kama Bashe ni raia au si raia?

Hebu tuendelee kudodosa udhaifu wa waziri tena mwanasheria. Alipoulizwa kuhusu uraia wa aliyechukua nafasi ya Bashe ambaye naye anadaiwa si raia wa Tanzania bali Burundi waziri alikaririwa akisema : “Nimeagiza watu wangu walifuatilie ili waweze kunipa taarifa.”

Wakati waziri akisema suala la uraia wa mgombea wa CCM aliyechukua nafasi ya Bashe unafuatiliwa, Katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba anasema hivi: “"Tunachojua mgombea wetu ni raia." Je hapa nani anasema ukweli na nani anasema uongo? Tumwamini nani kati ya waziri mwenye dhamana na katibu mkuu wa chama chake? Je Makamba anapata jeuri wapi kutolea maelezo jambo ambalo hana mamlaka nalo kisheria? Je haya ndiyo matokeo ya chama kushika hatamu au kuwa juu ya serikali? Tusaidiane. Nchini mwetu kati ya chama na serikali nani mwenye kuwa juu ya mwingine? Haya maswali yanaweza kuonekana ya kichokozi. Lakini tunapaswa kujua nchi yetu na mifumo inayotutawala ili tuweze kuwa tayari kupambana na wale wanaovunja sheria kwa kuingilia mamlaka ya wenzao kiasi cha kuuibia na kuupotosha umma.

Kinachotia shaka na kuvunja moyo ni ile hali kuwa utawala mvurugano wenye kuingiliana umeanza kukubalika kiasi cha wahusika kuwa mamlaka ndani ya mamlaka na kuweza kuamua lolote bila kuchelea lolote. Hebu angalia majibu ya Makamba aliyotoa alipoulizwa kama chama chake hakitaathirika kama mgombea wake atabainika si raia. Alijibu: "Tatizo la nini wakati nimesema yeye ni raia?" Kumbe Makamba akishasema fulani ni raia hata kama si raia anakuwa raia! Je namna hii tutafika? Je bado tunahitaji watendaji kama hawa wasiojua wanachosema na madhara yake ukiachia mbali kutosoma alama za nyakati?

Laiti wangejua kuwa hata kupayuka kuna wenyewe na si wote wanaweza kupayuka wakawa salama!

Makamba amefanya utafiti upi na lini kujua kuwa mgombea wao ni raia iwapo malalamiko yalitolewa baada ya kamati kuu kumaliza kikao chake?

Je huu si ushahidi kuwa serikali yetu inajiendea tu kiasi cha watendaji wake kutojua hata mipaka ya mamlaka yao kiasi cha kuruhusu wakuu wa chama kutolea majibu masuala ya serikali ambayo hawahusiki nayo kama kwenye sakata hili? Je namna hii tutaujua ukweli na kutendewa haki? Je watendaji kama hawa wasiojua hata majukumu yao ukiachia mbali kujisemea wanapaswa kuendelea kuwa kwenye ofisi za umma?

Kama waziri wa mambo ya ndani mwenye kila wapelelezi na taarifa chini yake hajui nini hali ya uraia wa Bashe kweli atajua maadui wa taifa hasa wakati huu wa kukua kwa sayansi na teknolojia?

Sijui kama waziri anajua hata idadi ya watu walioomba uraia wa Tanzania ukiachia mbali idadi ya wahamiaji haramu waliomo nchini?

Je imekuwaje rais akateua mtu anayeonekana kupwaya wazi kwenye nafasi hii nyeti kwa usalama wa taifa hili? Je wako wangapi kama yeye ambao kimsingi wanatuangusha kama taifa? Nadhani hapa ndipo ilipo siri ya uwekezaji wa kijambazi usio na tija kwa taifa. Kadhalika hapa ndipo unaweza kuona madhara ya kujuana, kulindana. Rejea kutoshughulikiwa kwa wale waliotuhumiwa kughushi vyeti vya taaluma wanaoendelea kufaidi matunda ya nafasi ambazo hawana ujuzi nazo. Je tunafanya hivi kumkomoa nani zaidi ya vizazi vijavyo ambavyo tusipoangalia vitakuja kufukua makaburi yetu na kukojolea mabaki yetu kama ishara ya kulipiza kisasi kwa upuuzi unaofanyika sasa hivi.

Leo nimetumia suala la Bashe ambalo, kwa wasfu wa mhusika ni dogo tu, kuonyesha tulivyo kwenye hatari ya kuangamiza taifa letu kutokana na ombwe la uongozi. Bila kubadilika na kuteua watu makini kwenye nafasi nyeti kama wizara ya mambo ya ndani, kuna siku tutajikuta pabaya na tusijue la kufanya.

Kwa yanayoendelea, kama rais Jakaya Kikwete asingekuwa mbali na umma, alipaswa kuchukua hatua na kutatua matatizo sugu kama vile kughushi, ufisadi, uzembe na kadhia nyingine. Lakini hata hivyo tusimuonee. Kama hakuthubutu kushughulika, achia mbali, kutatua matatizo haya kipindi kilichopita, ni miujiza gani itafanyika kipindi anachosaka afanye hivyo wakati ni lala salama? Tuwakumbushe wapiga kura na wananchi. Kipindi cha kwanza cha urais wa rais mstaafu Benjamin Mkapa kilishuhudia mafanikio ya kupigiwa mfano aliyokuja kuyafuja kwenye kipindi cha lala salama.

Hivyo ni kazi kwao kujua nani anapaswa kuaminiwa nchi yao msimu huu kutokana historia kuwa mwalimu na shahidi mzuri. Wakati pekee wa kurekebisha hili ni kwenye uchaguzi angalau kama siyo kubwaga wote kuwapunguza.

Nisiwachoshe kwa hoja. Nimalize kwa kuuliza swali ambalo mnapaswa kujiuliza na kuwauliza wahusika hata wasipojibu ili mjue la kufanya hapo Oktoba. Je Makamba na Masha nani mkweli na wanamdanganya nani na kwa nini?
Chanzo: Dira ya Mtanzania Agosti 21, 2010.

Huwezi kufuturu pesa ya ufisadi, swaumu ikawa safi

Assalaam Alaykum Wallahmatullillahi Wabarakatu mliofunga na ambao hamkufunga.

Baada ya kuwaamkia sasa naomba nieleze somo la leo. Amma badu, Wallahi, natamani jambo ambalo wengi, naamini, wanatamani pia ili kujikomboa na kuutokomeza uzandiki na ubaramaki unaoendelea miongoni mwetu.

Kwanza tukubaliane. Kaya yetu iko pabaya na mikononi mwa wabaya wanaoweza kujifanyia lolote wasichelee kitu kutokana kudhani kila mmoja ni mlevi kama wao wasijue wengine ni waumini wa kweli!

Kutokana hali hii na kujua kuwa mwezi wa Oktoba tuna uchafuzi uitwao uchaguzi au uchakachuaji, najitahidi kusaka majibu kama nabii wa Mungu kwa Wadanganyika.

Mwenzenu natamani mwezi mtukufu wa Ramadhan ungejiri Oktoba badala ya mwenzi huu. Nisijeeleweka vibaya na kufanya baadhi waanze kunuia kuninyofoa shingo.

Natamani hivyo si kwa ajili ya ujuha, jeuri, kufru wala utwahuti. Naamini kwa dhati. Hii ingetuwezesha kuswafi nia zetu na kunuia kupata mahakama ya Kadhi na kupiga teke mfumo mbovu unaotusababishia kuishi kidhambi dhambi unaoongozwa na mafisadi wanaotaka kutufisidi tusipate mahakama yetu ili tujihukumu wa sharia za mola wetu Subhanna wataala.

Kwanini wana nambari wahedi wahukumiane kwa sheria zao za kitakukukuru na waislamu tusihukumiane kwa sheria za Allah Subhanna wataala? Hivi unadhani watu wangenusurika kunyea debe kama sheria za kaya zingetumika?

Mtu anakuja na nyaraka za kughushi badala ya kumpeleka lupango unamwambia nyaraka zako si sahihi! Je, kipofu anapomuongoza kipofu unategemea nini? Je fisadi anaposhika kani unategemea nini?

Hata mtume aliusia kuwa binadamu anapambana na maadui wakuu watatu wanaoweza kumuingiza kwenye ukafiri kirahisi- ufakiri, upenzi wa kuzidi kipimo na ujinga. Situkani.

Hivi vitu vitatu tunavyo na vinazidi kuongeza namba ya makafiri kwenye kaya. Wanakaya wengi ni wajinga kiasi cha kutojua maadui zao wala haki zao za msingi.

Wapo wapo wanaliwa mchana kweupe na hawafanyi kitu kutokana na ujinga na ujuha waliopandikizwa chini ya dhana chafu za uwenzetu na upuuzi mwingine kama huu.

Kutokana na kaya kuendeshwa kifisadi ufakiri unazidi kuumka huku ujinga ukicheza ngoma kwenye vichwa vya wanakaya kutokana na elimu kuwa bidhaa aghali na feki. Ajabu bado wanakaya hawa waathirika wanawapenda watesi wao kupita kiasi hadi kuwapa kula!

Wengine huiita kura ya kuliwa yaani kumpa mamlaka yule anayekuguguna na kukuchuuza kufanya hivyo kisheria. Wale waliosoma fikhi wananielewa vizuri.

Hivi ni ukafiri kiasi gani waumini wazima kudanganywa kuwa mnasonga mbele wakati mnavutwa nyuma kilometa milioni moja nanyi mkaamini huku mkijua ni uongo? Je huu siyo sawa na ulevi wa walevi wa kijiweni kwangu ambao kila mwaka hunipa kura ili niwale?

Kama Ramadhan ingewadia mwezi huu nina hakika: tungetumia swaumu zetu vizuri na vilivyo kuwashikisha adabu vidhabu wanaotuhadaa kutunyonya na kututesa wakati Maulana alituumbia hii dunia tuifaidi wote si wote wao.

Tungeondokana na yale mambo matatu niliyotaja hapo juu na kuwa waumini na wanakaya safi. Nani kakwambia dini na ukombozi vinagomba?

Kwanza, sijui kama wanaharamu hawa hufunga. Kama wanafunga basi wanajifunga na kuchuma dhambi kwa kumhadaa Allah ambaye haadahiki hata kidogo. Maana huwezi kufuturu pesa ya ufisadi au itokanayo na kuiba na kununua kura swaumu yako ikaswhihi. Never. It can't swihi hata kidogo.

Naanini kama Ramadhan ingewadia mwezi wa kumi, hata madhambi yanayotendwa na hawa wanaowania ulaji wa dezo kwa kumwaga pesa chafu na safi yangepungua.

Wananchi wapenda dezo hasa waliofunga, wangejiepusha na wezi hawa wanaowanunua ili wawauze kwa bei mbaya kwa mabwana zao.

Naamini pia hata hawa wanaosia uongo wangepunguza ingawa hawana dini zaidi ya mamlaka na ufisadi. Unakuta jitu linakariri mistari ya Qur'an na Biblia kila liendako. Lakini nyuma ya pazia jitu hili hili gendaeka ndilo fadhili kuu la mafisadi.

Linatumia madaraka yake kupitisha watoto wake na maswahiba zake kwenye kugombea ulaji huku likiwapendekeza mabwana zake wa nyuma ya pazia wagombee ubunge.

Hebu jiulize. Kwanini siku hizi ubunge umekuwa kivutio cha wafanyabiashara mabilionea wenye kutia kila shaka? Jibu ni rahisi. Wananunua kaya kwa matumizi yao machafu hapo baadaye.

Msipoangalia hata Al-Qaeda na Al Shabaab watakuja chomeka watu wao. Mtastukia mnaambiwa kaya yenu iko chini ya makundi haya bila nyinyi kujua. Shauri yenu endeleeni kujiuza kama vyangu. Kwanini kura yako iwe kula ya mtu mwingine? Bila shaka anayefanya hivi anakuona bwege ndiyo maana anakuhadaa na kukuhonga upuuzi.

Pia natamani Kwaresima nayo ingejiri mwezi Oktoba ili jamaa zangu wa ufisadi na kulindana wageuzwe majivu hasa Jumatano ya majivu. Natamani Kwaresima na Ramadhan zingefika mwezi wa kumi ili hawa wanaohonga ulevi na uongo wakose wakuhonga.

Maana walevi wangeadimika na nafasi yao kuchukuliwa na waumini ambao bila shaka kwa nguvu ya imani zao wangepinga dhambi ya kuhongwa kwa nguvu na akili zao zote.

Hata wale wanaopenda kuomba rushwa ya ngono kama yule ticha wa pale nonihino aliyebambwa juzi wangekoma na kukosa wateja kama si kupungua ingawa wanaharamu hawa hawana dini.

Juzi nilicheka nusu kufa ingawa nilikuwa nimeudhika nikafikia kucheka kwa maudhi. Nilimsikia mgosi Machungi wa Makambale akiongopa kuhusu uraia wa Bwashee.

Ukiangalia msijida wake wa kulazimisha na anavyopenda kukwoti vitabu vitakatifu unaweza kuhadaika kuwa ana dini. Kwa taarifa yenu mgosi ni rafiki yangu na mpambe wangu. Hana dini hata kidogo. Dini yake ni ulaji na mamlaka.

Hii ndiyo maana kwa sasa anazunguka kwa wajina wake na swahiba yake Mainjiii kumtoa upepo wa kuhongea wanuka njaa kwa kisingizio cha kufuturisha.

Kesho mtamsikia yule jambazi wa Kagoda naye akifuturisha kabla ya kuhani mkuu baba yao naye kutoa futari. Mie japo nimepigika kiuchumi, kwa imani yangu ya kweli, siwezi kufuturu futari ya wizi hasa itolewayo na hawa sharmutah wal habithi hata kama wanajiona ni watukufu.

Mie najua wazi kuwa aliye bora mbele ya Allah ni yule amuaminiye na kumuogopa Allah. Hata uwe na mipesa kama wauza unga au madaraka kama firauni mie hunitishi na ndiyo maana huwa napayuka bila kujali ukubwa wa kacheo ka mtu.

Hebu jiulize. Wangekuwa waislamu wa kweli kama mimi kweli wangehujumu uchumi hadi futari inapanda bei na wasifanye kitu?

Loh! Kumbe saa ya kufuturu imetimu! Acha niwahi kufuturu halali mie. Wabillahi tawfiq.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 25, 2010.

Saturday 21 August 2010

Kikwete anahitaji msaada wa haraka sana





Kwa wanaofuatilia afya na shughuli za rais Jakaya Kikwete, watakubaliana nasi kuwa si mzima kiafya hata kisiasa. Utawala wake licha ya kuzungukwa na aibu na utata ni tatanishi na legelege kama afya na sera vyake.

Alifungua dimba la kuanguka mwaka 2005 alipoanza kampeni za urais awamu ya kwanza, akafuatia mwaka 2009 na akafuatia mwaka huu kwenye ufunguzi wa kampeni zake za lala salama. Hatujui: ataanguka mara ngapi tena toka hapa. Ila ukiangalia ukaribu wa anguko la mwaka jana na mwaka huu, unaweza kutabiri kuwa atazidi kuanguka muda si mrefu toka sasa. Je hii inatokana na afya yake kuzidi kudhoofika kiasi cha kufichua uharibifu uliokwishafanyika mwilini ingawa madaktari, Kikwete mwenyewe hata chama chake hawataki hili lijulikane?

Kwanini afya ya rais wa nchi -ambaye ni public figure- inafanywa siri kama hamna namna? Kikwete anatukumbusha kinachoendelea nchini Misri ambapo rais Hosni Mubarak anaweza kukata roho wakati wowote kutokana na kuzidi kushambuliwa na kansa ingawa mamlaka nchini humo hazitaki kukubali hili.

Hata kiongozi wa PLO, Yasser Arafat, afya yake ilipodhoofika, ukimya na usiri vilitanda kilio kikaja kufichua na kutibua kila kitu. Hata mwizi wa DRC, Joseph Desire Mobutu, na wapambe wake alificha kudhoofu kwa afya yake hadi yalipomkuta yaliyomkuta na akaitema DRC aliyoichukulia kama shamba lake na ukoo wake na waramba viatu wake.

Marehemu Oumaru Yar'Adua, rais wa zamani wa Nigeria, alikufa kwa mateso makubwa baada ya waliomzunguka kumtesa kwa kuficha ukweli kuhusiana na kudhoofu afya yake. Hata hivyo, uongo huu wa kujidanganya-self deception haukufua dafu kwa kanuni ya maumbile. Mauti yalimfika Yar'Adua na walioficha ukweli wakaumbuka. Je kwanini hatutaki kujifunza kutokana na ukweli huu wa kihistoria? Je tu majuha na wapuuzi kiasi hiki!

Je Kikwete ni mzima kweli kwa maana halisi ya neno? Swali hili muhimu linachanganya sana ingawa unaweza kutumia ushahidi wa mazingira (circumstantial evidence) kupata jibu. Angekuwa mzima, asingeogopa kupima afya yake na kuweka wazi matokeo kabla ya kugombea. Kuna vitu viwili Kikwete hatafanya na hataki akumbushwe kufanya-kupima afya yake na kutaja mali zake.

Hili pia lingemfaa hata mgombea mwenza Dk Gharib Bilal ambaye naye minong'ono imeshaanza kusikika kuwa afya yake si mulua.

Leo tutatoa ushauri wa bure. Kikwete bingwa wa kumtegemea mtabiri wake Shehe Yahya Hussein, anapaswa kurudi kwake na kukubali amwambie ukweli ambao alimpa kinyume pale alipotabiri kuwa atakayempinga atakufa. Je alimaanisha vinginevyo kutokana na lugha zao za sanaa kama ambayo Kikwete aliahidi maisha bora akimaanisha maisha balaa? Maswali ni mengi kuliko majibu. Kilicho wazi, hata hivyo, ni kwamba afya ya Kikwete ni ugogoro mtupu hata ifanywe fumbo vipi. Hata ndege wanajua hili fika.

Je hii inaweza kufumbua fumbo ni kwanini Kikwete hupenda ziara za nje? Ndiyo. Wengi wanadhani huenda kule kutibiwa kisirisiri. Kuondoa utata na imani kama hizi, kuna haja ya Kikwete kupimwa afya yake na matokeo yake kuwekwa hadharani. Vinginevyo mengi yatasemwa hasa yasiyopendeza ukiachia mbali wasi wasi juu ya mshikamano wa taifa.

Somo jingine la Kikwete kama watanzania wataweka maanani ni ishara ya kuanguka kwenye kura kama wizi wa kura hautavumiliwa. Maana, kimsingi, Kikwete hajakidhi matakwa ya watanzania wala kufanya lolote zaidi ya kuwa balaa. Angalia muungano unavyozidi kubomokea mikononi mwake chini ya uongo uitwao maridhiano ambayo kimisngi ni janja ya wazanzibari kurejesha taifa lao kwa mlango wa nyuma. Angalia mafisadi wanavyozidi kuiteka serikali huku wanaowapinga wanapatilizwa kama ilivyotokea kwa Lucas Selelii na Thomas Nyimbo na wengine. Rejea kupeta kwa Rostam Aziz, Edward Lowassa, Andrew Chenge na wengine ambao, kimsingi, ndiyo mihimili ya Kikwete ya ufisadi unaoendesha serikali yake.

Tuombe Mungu atufumbulie fumbo hili. Tumuombe sana afichue hii siri ya afya na sera zenye ugogoro.

Tunachukua fursa hii kumtakia Kikwete apate nafuu mapema. Muhimu, tunamuomba akubaliane na ukweli kuwa ukweli huwa haukimbiwi wala hauwezi kuuawa hata ukicheleweshwa vipi.

Penye kufuka moshi shurti kuwa na moto na mwanzo wa ngoma lele. Kuna siku mtakumbuka ujumbe huu na siku si nyingi. Katika kitabu changu cha SAA YA UKOMBOZI tukio kama hili limeonyeshwa vizuri pale mkuu wa mkoa wa Chelewa Gibbons Likupatile (Kikwete) linapompata na kuanguka na kuzimia jukwaani alipokuwa akijaribu kuwaongopea wananchi wa Mizengwe (Tanzania) kabla ya serikali fisadi ya Mizengwe kuangushwa kutokana na harakati takatifu zilizoasisiwa na kuratibiwa na mkongwe wa ukombozi Mzee Njema Waithaka mhusika mkuu wa riwaya ya SAA YA UKOMBOZI.

Tusiseme mengi. Soma utafahamu mengi.
Yetu macho. Kikwete, hata CCM, wanahitaji msaada na si kutoka kwa Shehe Yahya au mitandao ya kijambazi ya CCM bali watu wenye ithibati na ujasiri kumwambia apumzike. Uzuri ni kwamba hila zao zimegundulika. Si Kikwete wala Yahya. Wanadanganyana na kutumiana. Hakuna anayempenda wala kumsadia mwenzake zaidi ya kudharauliana na kuchuuzana. Angalau hili limejulikana. Enough is enough tuseme na wakiri. Kwani, tuendako, ataumbuka bure.

Hebu angalia wapuuzi wanavyoanza kuondoa picha ya tukio kwenye mitandao wakidhani wataficha ukweli. Ukweli haufichwi milele bali kwa kitambo tena kidogo. Ajabu wakati wakifanya haya wanasahau kuwa maneno ya mwisho ya Kikwete kabla ya kuanguka ilikuwa ni tambo kuwa ameimarisha uhuru na haki za binadamu hasa vyombo vya habari na haki ya kupokea na kutoa habari. Kuhujumu links zenye picha hii si kufichuka kwa unafiki wa kilichokuwa kikisemwa hadi Kikwete kujisifia? Au ni yale yale kuwa Kikwete akisema hili humaanisha lile?

Tulipata habari za kuanguka kwa Kikwete kupitia UGHAIBUNI ya Evarist Chahali na Jamii Forums. Lakini baada ya muda mfupi picha ya tukio iliondolewa kwenye mitandao. Tunadhani hii ni hujuma. Si utashi na mapenzi ya walioiweka ili ulimwengu ujue ukweli. Hata hivyo walikosea. Maana ukweli ulishasambaa na kujulikana.


HAKIKA, KIKWETE NA WALIOMZUNGUKA NA KUMZUGA WANAHITAJI MSAADA WA HARAKA. Mungu wakomboe watanzania.

Wednesday 18 August 2010

TAKUKURU imepata wapi makali haya?





JAPO wengi wanaoshabikia mkumbo wa mambo baada ya kuchoshwa na ufisadi kwa muda mrefu wameipongeza Tume ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kwa kugusa wasioguswa na vigogo wa chama jogoo, mie simo kwenye kundi hili.

Japo wengi wamefurahi angalau kuona mawaziri, wakuu wa wilaya na wakuu wengine wastaafu kufikishwa mahakamani kwa madai ya kutoa rushwa kwenye kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizopita na kusifika kwa kughubikwa na rushwa, bado hairidhishi wala kustahiki kwa TAKUKURU kupongezwa.

Kwa wanaojua uhasama na uroho wa madaraka uliopo baina ya mitandao ya ndani ya CCM, wataungana nami kuhoji- TAKURURU kama kweli ina meno kama inavyotaka tuamaini, ilikuwa wapi ziliporipotiwa rushwa kubwa kama vile Buzwagi, Ununuzi wa rada na ndege ya Rais kwa uchache?

Kwanini waliokamatwa kipindi hiki hatuwaoni wale magwiji wa kwenye kashfa tajwa hapo juu? Kwanini TAKUKURU hii hii haijawahi hata kuchunguza wapi zilipokwenda pesa za ujambazi wa EPA ambazo tunaambiwa ndizo zilimwingiza Rais Jakaya Kikwete madarakani kama ilivyowahi kudaiwa na CHADEMA na wana mageuzi wengine?

Kwa nini TAKUKURU hii haijawahi kuchunguza baadhi ya ajira na vyeo ndani ya serikali ya CCM? Je, inao ubavu wa kuweza kufanya hivi?

Kwa wanaojua jinsi TAKUKURU ilivyovuliwa nguo wakati wa kutaka kutumika kuua kashfa iliyomng'oa waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa, wana wasi wasi na hawa waliodaiwa kukamatwa na TAKUKURU-jibwa la rais lisilo na meno hata mawili.

Tuzidi kujiuliza. TAKUKURU imepata wapi haya makali ya sasa kama siyo kuagizwa na bosi wake kuwapatiliza na kuwakomesha wabaya wake ambao kimsingi waliusumbua utawala wake?

Kwanini TAKUKURU kama kweli inataka kupambana na rushwa, haijachunguza kukusanywa kwa shilingi bilioni 50 kwa ajili ya kumwezesha rais Kikwete kushinda?

Hivi TAKUKURU wanadhani watu wote ni mataahira siyo? Ni miradi mingapi hasa ya ujenzi wa barabara na tenda ina kila harufu ya rushwa na wakubwa zake wanapeta?

Hebu tuipe eneo mojawapo linalonuka na kuishinda hata serikali kulishughulikia kutokana na kuwa na mtu wake. Hili si jingine ni Tanroads. Muulize kila mtanzania anayefuatilia mambo. Anajua fika jinsi mkurugenzi wa sasa wa mamlaka tajwa alivyo serikalini ndani ya serikali.

Hapa hujaenda kwenye mbuga za wanyama ambapo maeneo ya uwindaji yanatolewa kwa rushwa mchana. Bado hujaenda bandarini na mipakani ambapo karibu kila kitengo kinatolewa kwa wahusika kulingana na uzito na kipato cha kitengo kwa upendeleo na rushwa.

Hebu tuchunguzane nani yuko wapi na aliingiaje hasa maeneo yenye ulaji mkubwa. Mbona TAKUKURU haijachunguza ajira za watoto wa vigogo waliojazana BoT?

Bahati mbaya sana, hata mashirika yanayofanya utafiti hayataki kufanya utafiti huku zaidi ya kujikita kwenye siasa kwa vile ni rahisi kupewa chochote kitu na kuja na matokeo ya kumjenga fulani. Nendeni huko muone nchi ilivyooza huku TAKUKURU ikiwa usingizini.

Kuna hili la rushwa ya wengine pasipo na kugusa rushwa yake. Ukichunguza mishahara ya wafanyakazi wa TAKUKURU na aina ya maisha wanayoishi ni vitu viwili tofauti.

Kama alivyodai mkuu mmoja wa Polisi, TAKUKURU nao wanakula rushwa hata kama hakuna wa kuwakamata. Hii inanikumbusha kisa kimoja kilichonitokea Tabora mwaka 1993.

Nikiwa safarini kuelekea Kigali Rwanda nilikamatwa na afisa mkusanya kodi njiani. Kosa langu ni gari langu kupakia mwanamke aliyekuwa anakwenda msibani ambaye hakuwa amelipa kodi.

Kutokana na kugundua ujuha wa ofisa mkusanya kodi aliyetaka nimlipie abiria wangu kodi ndipo aruhusiwe kuendelea na safari yake kwenda matangani, nilimtaka mhusika anipe karatasi yake ya kodi.

Ajabu ya maajabu niligundua kuwa kumbe naye alikuwa hana hiyo karatasi kutokana na ukweli kuwa hakuna ambaye angemkamata kutolipa kodi kutokana naye kuwa ndiye mkamataji wa wakwepa kodi.

Kadhalika na TAKUKURU inapaswa kuundiwa chombo cha kuichunguza. Tusiiamini TAKUKURU ambayo haiaminiki wala haituamini. Tufikie mahali tujenge vitengo vyenye kufuata kanuni za kijasusi vyenye kuchunguzana ili kutenda haki na kuleta uwajibikaji.

Kwa nini jeshi letu la Polisi lisipewe jukumu la kuichunguza TAKUKURU ili muone uoza wake?

Kwa kuwa chini ya ofisi ya rais, licha ya TAKUKURU kuweza kutumiwa kisiasa kama inavyoonyesha kwenye kuingilia mchakato wa kisiasa wa chama, inaonekana kama mwana mtukufu sawa na bosi wake.

Je, TAKUKURU haiajiri wanadamu hasa watanzania ambao wamebobea kwa rushwa kutokana na mfumo wetu kuwa wa kirushwa?

Mbona TAKUKURU haikamati wezi wakubwa waliojazana kwenye mamlaka ya kodi wanaojulikana kwa ukwasi wa kutisha kuliko hata hao mawaziri?

Kazi ya umma haina cha kuaminiana iwe kwa mtu binafsi au taasisi. Yeyote anaweza kutenda kosa. Ndiyo maana nchi zilizoendelea huwa na mashirika mbali mbali yasiyojuana yanayochunguzana ili kuleta ufanisi uliokusudiwa.

Kwa TAKUKURU kuingilia kura za maoni za CCM ni ushahidi kuwa inatumiwa na CCM. Na hapa vyama vya upinzani vikae chonjo. Hii inaweza kuwa ni gia ya kutaka kuwahujumu wagombea wa upinzani ambao ni tishio kwa CCM.

Na hapa ndipo CCM itaua ndege wawili kwa jiwe moja kuwabana viherehere wa ndani na wapinzani hatari kwa mustakabali wake.

Kama rais wetu ni msafi na anayefuata utawala wa sheria, hana haja ya kuweka mamlaka muhimu kama haya chini ya ofisi yake. Anaiweka chini yake ili aifanye nini zaidi ya kuitumia kwa maslahi yake binafsi? Tuulize swali jingine kuu. Kuna wengi tunaolalamikia utendaji wa mashirika yasiyo ya kiserikali ya wake za marais yaani Anna Mkapa na Salma Kikwete ambayo yanaonyesha wazi yalivyo ya ulaji kupitia mgongo wa Ikulu. Mbona TAKUKURU haiendi huko kuchunguza?

Kuna madai mengi ya tabaka dogo la watu tena wageni kumiliki uchumi wa taifa. Ni hawa hawa wanaotajwa kwenye karibu kashfa zote kubwa zinazobomoa uchumi wetu.

Nani anawagusa kutokana na wao kuwa karibu na wakubwa wa serikali wakidhamini mbio zao kuingia madarakani? Wengine wamefikia hata kuwaweka watoto wao kwenye ubunge ili kulinda maslahi yao na TAKUKURU haifanyi kitu.

Ni wabunge wangapi tunao wametokana na utajiri ama wa wazazi wao au jamii zao wasio na hata chembe moja ya mshipa wa siasa?

Kama kuna Taasisi inayoweza kubebeshwa zigo la kulinda rushwa si nyingine bali TAKUKURU ikishirikiana na ofisi ya rais. Ni afadhali kirefu cha TAKUKURU kuwa Taasisi ya Kuzua na Kupamba na Rushwa kuliko ilivyo.

Tukitaka kupambana na rushwa hasa hii inayowahusu wakubwa wetu, tuisuke upya na kuiondoa TAKUKURU chini ya ofisi ya rais. Na tusikubali kuchafuliwa kama inavyofanyiwa sasa kwa kutumiwa kwenye siasa chafu za CCM.

Ningekuwa mkuu wa TAKUKURU, kwa kujua taasisi yangu inavyoonekana yao hovyo na kutumiwa hovyo, ningeachia ngazi na kutafuta kazi nyingine ya heshima.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 18, 2010.

Huu ni msimu wa hongo na uongo

JUZI kwenye runinga yangu tena kwa maninga yangu nilimuona msanii mkuu ambaye si vizuri kumtaja jina kwa vile kila mtu anamjua hata ndege akiwafunga kamba wakulima aliowasahau kwa karne!

Sikushagaa. Maana huu ni msimu wa hongo na uongo mtindo mmoja. Waliokuwa wamekutelekezeni sasa wanajifanya wenzenu tena wanaokupenda nusura ya kukata roho kama hawakuoni. Ni mapenzi ya kweli au ya uongo usiniulize. Tumia bongo lako maana bongo bila bongo utaliwa tu tena ukijiona.

Wakati wa kutumia matumbo badala ya ubongo umepitwa na wakati hasa kipindi hiki kigumu cha kutiwa majaribuni.

Baada ya kushuhudia usanii na hii jinai nilijiuliza swali moja kuu-je kwa miaka yote hii ulikuwa wapi hadi leo uwaone wanafaa kama kweli wanafaa ukiachia mbali wewe kuwafaa? Hata hivyo, nilipata jibu kuwa wakati wa kula kwa kura lazima kila sanaa ifanyike ili ulaji wa dezo upatikane. Hapa mtaimbiwa ngonjera na nyimbo nzuri za maisha safi wakati ukweli hakuna cha maisha safi bali ulaji mchafu wa kiroho wa kujuana na kulipana fadhila.

Kuna kipindi huwa nashangaa dharau hii hasa kwa hawa jamaa zetu waliohukumiwa kifungo cha maisha cha mateso kwenye mashamba yetu. Li-sirikali liliwatelekeza zamani na kufunga ndoa na wachukuaji na wafanyibiashara wenye kutia kila aina ya shaka.

Eti leo kiranja wake anakwenda kuwageuza majuha jamaa zangu hawa kwa kuwapa vijijembe vya kisasi, uongo uitwao Kilimo First wakati ni Uchukuaji na Uwekezaji First. Je, hii si kuwageuza shamba la bibi? Je nao hawana hata akili lau ‘common sense’ kujua wanaliwa? Kwa nini wasipokee upuuzi huu ambao mie naona ni rushwa halafu kura wakatoa kwa wale wanaoona wanafaa kama walivyopania kufanya wafanywakazi wa kaya hii?

Nasema hivi kutokana na Wadanganyika kuwa na tabia ya kulalamikalalamika wanapojikuta wamebanwa mkengeni wasijue jinsi ya kujinasua. Utaiona imetoa mimacho kama panya kwenye mtego.

Mnalalamika nini wakati matatizo mengine mnajitakia kwa ujuha na tamaa zenu. Naona lile limetoa mimacho kwa hasira na kutaka kupasuka. Soma au acha lakini vidoge ntakupa. Maana huu ndiyo wajibu wangu kama mtume wa Mungu.

Kwanza, jamaa mwenyewe alishawatolea nje akisema raha mjipe wenyewe yeye awape karaha? Sasa anawafuatafuata nini kipindi hiki cha kuvuna asipopanda kama kweli nyinyi si majuha anayoweza kuyachezea kila mahepe? Mkiambiwa ukweli mnafura.

Ni kweli acheni ujuha mtaendelea kuliwa. Hivyo vijembe, vicheko na tabasamu bila kusahau kupiga picha za kipuuzi pamoja siyo ‘big deal’ ndugu zanguni. Mwaliwa ati hata kama hamtaki kusikia ukweli huu. Narudia mwaliwa ndugu zanguni kengeukeni msiukwae mkenge tena wa mchakachuaji huyu.

Huwa nashangaa mapenzi ya namna hii ya kibubusa na kushtukiza huchipuka wapi! Hivi hao wanaowapa hongo zitokanazo na mabaki ya chumo la wizi kwa nini msiwaulize waliwafanyia nini iwapo kila siku tunapata taarifa za wizi wa kutisha kama ule wa juzi wa 1,700,000,000.

Unajua haya ni madafu ambayo ni sawa na shilingi ngapi? A cool one point seven trilioni! Sorry nimechukia hadi ung'eng'e ukanitoka. Namaanisha shilingi za madafu trilioni moja nukta saba karibu na mbili.

Hizi ukipewa ‘mkulimwa’ unaweza kutumia shilingi milioni moja kila siku kwa maisha yako yote na zisiishe. Unaambiwa hii pesa imeibiwa ndani ya mwaka mmoja. Je ndani ya miaka mitano zimeibwa ‘zillions’ ngapi?

Hapa kitu muhimu kufanya ni kwa waliwa kuchangamkia hongo wanazopewa kuwaaminisha kuwa wanawajali na kupiga kura yako kwa wengine. Maana siku ya siku ikifika ni wewe Mungu wako na kura yako.

Hii ndiyo njia ya wanjanja kuonyesha ujanja wao na sio ukale na ujuha ambao huwafanya wahusika kuwachukulia waliwa kama waliwa tu na si wana kaya wanaostahili kutendewa haki.

Hakuna haja ya kuogopa. Tulishuhudia waliwa wa nchi ya Nyayo miaka ile wakiwapiga chini kina Kanuu kiasi cha kuwatoa kwenye historia za siasa za taifa lile ambalo hivi karibuni limepiga hatua nyingine mpya kwa kuondokana na Katiba viraka kama ya kaya.

Hawa ndio wanaweza kusema ni wajanja ambao hawako tayari kuchakachuliwa na kuchuliwa kama jamaa zangu wa hapa ambapo wamegeuzwa mtaji na mafisidunia wakubwa na wadogo. Upo hapo mwanangu? Kazi kwako.

Mambo yao ya kuchukua na kuweka waa yanapaswa kuwageukia. Nanyi mnachukua mnalamba na mnatoa kura nje ili tuone kama watakula jeuri na longolongo zao.

Nijuavyo huu ni mchezo wa karata tatu. Mara hii mmesahau kisa cha matapeli pale Migomigo ambapo mwenye dhahabu feki alimuuzia mwenzie aliyemlipa pesa feki mchezo ukaishia pale kila mmoja akiondoka anajiona mjanja wakati si kweli?

Kama muhula huu watu watapigwa chini litakuwa somo kubwa na zuri kwa wale wengine watakaopata ulaji wa kutokana na ‘kura’ zenu. Hapa ndipo mtaachana na mauti ya kuku kulishwa nafaka kavu akazalisha mayai yenye virutubisho lukuki asiyokula.

Kuku hula asichozalisha na kuzalisha asichokula kwa vile ni kuku. Mwajua ni kwa nini? Kuku kanyimwa ubongo. Maskini hayawani huyu! Ubongo wake haujai hata kijiko atawezaje kung'amua mambo kama nyinyi wenye bongo zinazochemka lakini mkatendewa kama kuku nanyi mkajirahisisha?

Juzi nilikumbuka mambo mengi. Nilikuwa napitia album yangu ya kale na kumuona mzee Musa Mchonga akisaidiana na wananchi-enzi zile-kujenga majengo ya shule, dispensari na mambo mengine. Alikuwa akichapa kazi kavu kavu.

Baada ya kuvuka ukurasa huo niliangalia picha za mkuu wetu bin Sharmutah akifanya kama mzee Musa. Ni mbingu na ardhi. Nani angeamini jamaa anashika ‘kurego’ ilhali kapiga magoti kwenye mkeka ili asichafuke?

Ukilinganisha viumbe hawa wawili ni sawa na kuwalinganisha Lusifa na Yesu au Abujahari na Mtume Mohammad. Hayo tuyaache. Kazi kwetu kutumia akili vizuri siyo kama kuku wa kwenye kisa hapo juu.

Muhimu ni kukubali na kuelewa kuwa msimu wa kuliwa tena bila kunawa wala kuomba ndiyo huu na habari ndiyo hiyo. Nasikia harufu ya wizi wa kula.

Du! mbona yule kavalia kama ndata! Acha niishie kabla sijamkata mitama. Maana siku hizi nawaonea kama sina akili nzuri. Ya kweli hayo? Tusichimbuane wala kuchakachuana.

Khalas kweisine.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 18, 2010.

Monday 16 August 2010

Wanaotaka mdaharo na Kikwete hawamtakii mema


Ingawa wengi wamekilaumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoridhia mgombea wake Jakaya Kikwete kushiriki mdaharo wa wagombea urais kama ilivyotakiwa na mgombea wa CHADEMA Dk. Wilbrod Slaa, kuna haja ya kuangalia historia na ukweli.

Nani mara hii amesahau kuwa Kikwete huyu huyu aliyetuonyesha uhalisia wake kwenye ngwe inayoisha alikacha mdaharo mwaka 2005 akiwekeza kwenye ushabiki kibubusa wa watanzania wakati ule baada ya kuuchoka ukale na ubabe wa Mkapa? Sababu? Aseme nini iwapo kila kitu ki wazi? Mtangulizi wake Benjamin Mkapa mwana tasnia ya uandishi wa habari na mahusiano ya kimataifa alipenda sana midaharo na kuimudu. Hapa lazima ukumbuke vitu viwili-taaluma na uwezo binafsi wa mhusika.

Kumbuka. Wakati Mkapa akiingia madarakani tulikuwa hatuna cha kumuuliza kutokana na sababu kuu mbili. Kwanza alikuwa akiashiria mpito toka chama kimoja kwenda vyama vingi. Hapa euphoria niseme kihoro, vilikuwa vimetawala.

Pili Mkapa licha ya kuwa msemaji na msomi aliyebobea, alikuwa ameungwa mkono na gwiji na kipenzi cha watanzania , hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ukiachia mbali kuwa hakuwa akijulikana vilivyo. Lakini pamoja na mapungufu yote haya Mkapa hakuukacha mdaharo kutokana na kujiamini na usomi wake ambao unakubalika licha ya mapungufu aliyoonyesha kwenye utawala wake.

Pia Mkapa hata Mwalimu, alijua umuhimu wa midaharo hasa katika kujenga taswira ya mhusika na kutoa kile anachotarajiwa kufanya. Mkapa pamoja na mapungufu yake, hakuwa mtupu wala mweupe.

Je ni kwanini CCM na Kikwete hawataki kushiriki mdaharo? Hivi mnategemea Kikwete kweli afue dafu mbele ya wasomi kama Dk. Slaa na profesa Ibrahim Lipumba ukiachia mbali Dk. PAul Kyara? Kwanza, ana nini jipya la kuwambia watanzania iwapo wanamjua nje ndani-urahimu na masihara yaandamanayo na kucheka cheka hata wakati wa mambo yanayohitaji kununa? Kimsingi saizi ya Kikwete ni watu kama Augustine Mrema na wengine aina yake lakini si Slaa wala Lipumba.

Hivi mlitaka Kikwete achukue kitanzi na kuweka shingo lake? Kwani hamjui kuwa kashfa ya hivi karibuni iliyoripotiwa-si na wapinzani, bali shirika la umoja wa mataifa ya shilingi trilioni 1.7 ni pigo la mwisho kwa Kikwete kama wapiga kura na watanzania wangekuwa wanajali uongozi bora na uwajibikaji?

Tujalie Kikwete ashiriki mdaharo huru halafu aulizwe sababu za kutotaja mali zake kama sheria anayopaswa kusimamia inavyotaka. Mnategemea atajibu nini zaidi ya kujikaanga.

Hapa hujagusia kashfa inayosemekana kuundwa ili kumpatia mtaji wa kuingilia madarakani ya EPA. Hapa bado hujagusa watu wake kama vile mkewe ambaye anadaiwa kuunda NGO ya kuchumia utajiri baada ya Kikwete kuapishwa. Hapa hujagusa tuhuma kuwa mwanawe anautumia Umoja wa Vijana wa CCM- UVCCM kujinufaisha pamoja na utawala wa baba yake. Bado hujaongelea maswahiba zake wa karibu kuhusika na kashfa mbali mbali zilizoligharimu taifa mabilioni ya shilingi kiasi cha kuzidi kuwafanya watanzania maskini zaidi na zaidi.

Hujagusia shutuma za usanii yaani kuahidi hiki na kutotekeleza. Yako wapi maisha bora kwa watanzania wote ukiachia mbali walio karibu na kiti cha ulaji?

Bado hujagusia rushwa na migongano ya mitandao ndani ya chama. Hii ni mbali na kipaji na elimu ya mhusika japo tuliwahi kuaminishwa na wasaka ulaji kuwa ni chaguo la Mungu wakati si kweli.

Wanaotaka Kikwete ashiriki mdaharo uwe mdogo hata mkubwa hawamtakii mema. Wanamkejeli na kumshakizia auingie moto. Maana ataulizwa maswali ambayo yatamuacha bila nguo.

Hivi mnategemea nini toka kwa mtu anayeamini kuwa msongamano wa magari barabarani ni ishara za maisha bora wakati ni ushahidi wa ombwe la uongozi na mipango madhubuti?

Je mnategemea aseme nini mtu ambaye amekuwa akiongopa kila uchao? Rejea kuwahi kusema kuwa ana orodha ya kila wahalifu.

Kikwete na washauri wake wanajua kuwa kuna maswali na masuala mengi mazito ambayo hawezi kuyatolea majibu yenye mashiko. Hivyo kumuepusha na aibu na pigo wanashikilia kuwa mgombea hawezi kupimwa kwa mdaharo. Na hakika. Wanajua ni kwa kiasi gani wanaongopa na kujiongopea. Maana hata hao wanaodhamini chaguzi zao yaani nchi tajiri huwapima wagombea wao kwa njia hii muafaka na ya kisayansi. Kwa maana nyingine rahisi ni kwamba Kikwete hana cha kuwafanyia na kuwambia wapiga kura zaidi ya mazoea na ukale hasa ikizingatiwa kuwa CCM imekuwa ikikabiliwa na ombwe la uongozi jambo ambalo hawajawahi kukanusha kumaanisha kuwa ni kweli. Na hakika. Kukacha mdaharo ni sehemu mojawapo ya ombwe.

Kimsingi, wapiga kura na watanzania waogope na kujitenga na mgombea anayeongopa kueleza mawazo na mipango yake. Kikwete kwa hili hasingiziwi kuwa hakutimiza ahadi zake. Nitajie ahadi lau moja aliyotekeleza katika makumi aliyoahidi. Hakuna zaidi ya siasa na sanaa kama kawaida. Kikwete amethibitisha kuendeshwa na matukio yanayolenga kuahirisha lakini si kutatua tatizo. Jana aliahidi hiki asitekeleze. Na usishangae kumsikia leo akiahidi kile ambacho kadhali hana mpango wa kutekeleza. Ameshindwa kufanya maamuzi magumu kama alivyowahi kupewa ushauri wa bure na wazee wa chama chake aliowaita wafitini waongo na wenye wivu.

Kama Kikwete ameshindwa kutekeleza ahadi zake na kutobadilika kwa miaka mitano iliyopita, mnategemea ni miujiza gani itafanyika aweza kuiona nuru-to deliver?

Hakuna haja ya kuandika mate ilhali wino upo. Utendaji dhaifu wa Kikwete kwenye awamu iliyopita ni ushahidi tosha kwa hukumu yake-kutochaguliwa kama wapiga kura watakuwa makini na kujua kuitumia silaha yao yaani kura.

Hivyo tufupishe kwa kusisitiza kuwa kumtaka Kikwete ashiriki mdaharo ni kumpa kitanzi ajimalize ingawa ameishakwisha kama tutatumia busara na kuangalia rekodi zake binafsi, waliomzunguka na utawala wake kwa ujumla.

Nashauri mdaharo ufanyike hata kama Kikwete hatashiriki kutokana na mapungufu niliyotaja hapo juu ili umma ujionee wenyewe mbivu na mbichi pumba na nafaka.
Chanzo: Dira ya Mtanzania Agosti 16, 2010.

Tuesday 10 August 2010

Tumtawaze Kikwete Mfalme Wetu


SINA haja ya kumsakama Rais Jakaya Kikwete na waliomzunguka. Naandika makala hii kwa nia ya kumtahadharisha juu ya staili yake ya kutawala kwa faida yake.

Nalalamikia mchezo mchafu unaoanza kuzoeleka ambapo wake na watoto wa wakubwa wanatumia nyadhifa za wakubwa kujineemesha kifedha na kisiasa.

Hivi karibuni yametokea malalamiko dhidi ya watoto maswahiba wa vigogo wawili wa chama na serikali, yaani Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambapo watoto wao Ridhiwan Kikwete na Januari Makamba wametajwa wazi wazi kuwa nyuma ya shinikizo lililosababisha kuachia ngazi mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Hamad Yusuf Masauni kwa tuhuma za kughushi vyeti vya kuzaliwa. Hatuna utetezi na hili ingawa linatia shaka kwa nini achaguliwe kwanza bila kuliona hili?

Januari pia analalamikiwa na Mbunge wa Bumbuli William Shellukindo kwa kuanza kampeni za ubunge mapema akitumia wadhifa wa baba yake.

Pamoja na shutuma hizi kutolewa dhidi ya wawili hawa si Kikwete wala Makamba hata CCM wamejitokeza kutoa maelezo au karipio!

Hapo juu nimeeleza kuwa Kikwete atawazwe kuwa mfalme wetu wa kwanza. Ukiangalia utawala wake wa kishikaji anavyouendesha, utakubaliana nami kuwa kuna tatizo kubwa tu.

Hebu piga picha juu ya unavyomuona mkewe Salma kwenye shughuli mbali mbali sehemu mbali mbali anavyopokelewa kama kiongozi wa nchi. Kwa nini anapokelewa hivyo? Simpo. Ni mke wa rais.

Salma amekuwa na nguvu kuliko hata baadhi ya mawaziri. Anaongozana na misururu mirefu ya magari na kupokelewa kwa mbwembwe zote za kikubwa utadhani ana ukubwa wowote Kikatiba!

Hapa hatujaongelea asasi yake isiyo ya kiserikali japo inaendeshwa kiserikali aliyoianzisha pindi tu mumewe alipoingia Ikulu ya Wanawake na Maendeleo (WAMA).

Wengi wenye akili tulidhani Kikwete hata Salma wangejifunza kutokana na madudu yaliyofanywa na mtangulizi wake Anna Mkapa anayetuhumiwa kujineemesha kwa mgongo wa Ikulu akitumia asasi yake ya EOTF.

Swali ambalo huwa linajirudia vichwani mwa wachambuzi ni kwa nini aanzishe asasi baada ya mumewe kuwa rais kama kweli analenga kufanya anayofanya kwa nia safi?

Nani anajua ripoti ya ukaguzi ya mahesabu ya asasi husika ukiachia mbali kuendeshwa na mtu mmoja kisiasa hasa kumpigia kampeni mumewe?

Isije kuonekana tunamsakama Kikwete na mkewe. Nitajie asasi ya Hilary Clinton alipokuwa mke wa rais au ya Michelle Obama mke wa sasa wa rais wa Marekani. Hazipo. Hawana haja ya kujidhalilisha na tawala za waume zao kujiingiza kwenye biashara ya ubuyu.

Nionyeshe ofisi ambayo amewahi kugombea Chelsea Clinton. Hakuna. Kwake mapambano ya maisha ni suala binafsi linalopaswa kufanyika kwa uhuru na si utegemezi.

Leo Salma, Ridhiwan na Khalfan wamo kwenye safu za juu za CCM na Chipukizi ukiachia mbali wadogo zake Yusuf na Mohamed waliokuwa kwenye orodha ya wagombea wa uwakilish@ � ��� ?��

Kinachotia shaka hapa ni kuvunjika kwa maadili ya demokrasia. Maana hawa wanaobebwa na pakacha la Ikulu hawaoni hata aibu kudhalilika kwa kutegemea migongo ya wazazi au waume zao.

Mobutu Seseseko wa Zaire (sasa DRC) pamoja na uroho wake hakuwapa ulaji watoto wake chamani na serikalini zaidi ya kuwaruhusu wadokoe kwenye hazina za nchi zao.

Sikusikia wake zao wakiwa na asasi za ulaji wala kupenda kufanya shughuli za kisiasa.

Niliwahi kushauri Kikwete afanye kama imla wa Uganda Yoweri Museveni.

Amteue mkewe waziri na kumpa kitengo cha ulinzi hata ushauri mwanae. Akiwapa nafasi hizi angalau tutakuwa na jinsi ya kuwapima hata kutaka wawajibishwe kwa vile tunajua mamlaka ziliwateua.

Lakini kwa sasa inakuwa vigumu kufanya hivyo kutokana na kuwa na mamlaka yasiyo ya kikatiba.

Hivi kweli ilihitaji PhD Kwa Kikwete kujua kuwa kumteua Januari kuwa msaidizi wake kungeleta mgongano si wa kimaslahi ukiachia mbali kujuana?

Sasa kama rais hawezi kuona hili bado ana chembe ya udhu kustahiki kurejea tena Ikulu? Ili afanye nini kwenye ngwe ya lala salama zaidi ya kusimika ufalme wake na familia yake na ulaji wa lala salama?

Hapa hatujagusia marafiki tena wenye kila tuhuma za uoza. Alipomteua swahiba na muwezeshaji wake mkuu Edward Lowassa ambaye baadaye alikuja kumtoa sadaka kunusuru ufalme wake uliokuwa umefanya kufuru, wenye akili tulijua ufalme tuliohofiwa unawadia.

Mna habari kama Lowassa angegoma kujiuzulu angekuwa bado ni Waziri Mkuu?

Hapa hujagusa watu wanaotuhumiwa kuwa nyuma ya wizi wa mabilioni toka kwenye Benki Kuu wakitumia makampuni mengi hewa.

Ukitaka kuliona hili vizuri jikumbushe jinsi rais alivyomuokoa rafiki yake marehemu Ditopile Mzuzuri alipomuua mtu kabla ya mkono wa Mungu kuingilia kati.

Kumbuka, hapa hatujagusia ufisadi unaofanywa na walio karibu na mfalme ukiachia mbali serikali yake kusifika kwa matumizi mabaya ya pesa ya umma huku mfalme akiitalii dunia na mke wake.

Je kwanini ufalme wa Kikwete unazidi kudumu na kufanikiwa? Simpo: woga na mazoea mabaya ya kifisadi wa kimfumo wa Watanzania ambao wanaweza kubeba kila mzigo bila kunung’unika.

Huu ni upunda na umkokoteni na upakacha ambavyo huwa haviulizi aina ya mzigo viubebao. Je hali itaendelea kuwa hivi? Ni mawili. Tumtose au kumtawaza Kikwete mfalme wetu wa kwanza kama tutashindwa kumngo’a kwenye uchaguzi huu aliopanga kununua kwa bilioni hamsini.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 10, 2010.

Ni siku ya kuchakachua na kuchakachuliwa

MWENZENU nimechoka na uhuni unaoendelea kwenye kaya ambapo fisi wanajitahidi eti kuwania kuwasemea kondoo. Sina hamu kwa niliyoshuhudia mwenyewe kwa maninga yangu. Msianze kusonya sonya. Acha niwaeleze kisa.

Si juzi nikajipeleka mwenyewe kwenye rubaa za siasa za gulio la uuzaji wa haki lililopewa jina la kampeni ambazo ziligeuka za uchafuzi na uchakachuzi wa demokrasia, sorry- uchaguzi wa kura za maoni.

Wazungu wangesema the masquerade, some jet-set smoothies call electoral process whilst it is actually monkey biz! Sorry sana waliwa na wadanganyika. Mwenzenu msinihesabu humo. Nipo na kijiwe changu natesa na kupeta. Sina maradhi ya bulimia wala myopia kama nyinyi.

Ndiyo watu walikuwa wanakula kwa kuona na kutoa kura ya kutoona mbele. Sikujua kuwa kumbe kujinyonga si lazima utumie kamba tu. Hata kura yaweza kukunyonga.

Zamani nilikosea kudhani kuwa majambazi ni wale tu wanaotumia bunduki nisijue na kalamu yaweza kuwa silaha hatari hasa ikitumiwa vibaya! Sikujua kuwa kumbe na usomi waweza kuwa ujuha hasa unavyotumika kichwa chini miguu juu!

Nani alijua kuwa majambazi ya wazi kama Endelea Chenga aka Mzee wa Vijisenti, Roasttamu, Bazie Bozo Notimbili, Abdu Kagoda, Eddie Ewassa, Mustafu Mkulu na wengine wangerejeshwa tena bila kupingwa.

Nani alijua kuwa vinyemelezi vya mafisadi kama Janvier Mgosi Makambale, Emmy Nchimvi, na wengine wangerejeshwa?

Nashukuru Mungu matapeli kama Chitaahira wa Chitalilio, Niziro Kadamage na Dororos Camara wametoswa mwongo huu.

Roho iliniuma nilipooana wale madaktari feki walioghushi vyeti wakipeta. Mmewasahau akina Makorongo, Bill Lukuwi, Meli -Nyagu, Chengeni Rafu, Mwambalakaswa na wengine walioghushi mkuu na genge lake wakawakingia kifua kwa vile wanakula pamoja?

Je hawa waliowapitisha hawajapitisha kitanzi chao baadaye? Nyie ngojeni. Wakianza kuwachakachua nisisikie gendaeka akijiliza na kulalamika kama kichanga ambacho hukojoa kitandani kikahanikiza kulaumu na kulia lia.

Hakuna jamii inayopaswa kuhurumiwa kama ile inayojihadaa kwa kugeuza haki bidhaa tena isiyo na thamani kiasi cha kupokwa na majambazi. Niliwaona wengi tena ambao huwezi kuwadhania. Walikuwapo wasomi, wababaishaji hata matapeli tena kwa wingi tu.

Kutokana na jinsi watu walivyomwaga mifweza (chafu na safi), vijisimu, na upuuzi mwingine, nilijifunza kitu kimoja-kumbe kambale wote wana sharubu! Nitaeleza baadaye hasira na mstuko vikipungua siyo kuisha maana haviwezi wakati ndiyo zali linaanza.

Niliona watu na mijitu. Wa mkuu kule wanahonga na wa wadogo nao kule wanahonga kila kinachoweza kufakamiwa na walevi wa danganyika hii. Heri ningejiendea kwenye jamhuri ya pili ya visiwa ambao hawakupoteza muda na uchafuzi bali kura ya maoni ya kuchanganya kondoo na fisi mbuzi na mbwa mwitu. Tuyaache.

Urafiki wa mbuzi na fisi huleta matokeo hatari hasa kwa mbuzi na faraja kwa fisi. Watajuta baadaye baada ya kushindwa kutumiana.

Hakuna kituko kilichoniacha hoi japo hai. Nani angeamini kuwa wale jamaa zetu wa kukuru kakara za kukuza na kudumisha rushwa nao wangeingia na sanaa zao?

Hawakutaka kubaki nyuma katika mechi hii ya kuonyesha ukichaa ufisi na ufisadi wa kila aina. Tukukuru nao wanafunga kamba huku. Kule mitandao ndiyo usiseme hadi kwenye runinga huku rubaa za kimataifa tukimkosa mtalii ambaye kwa sasa amestaafu ili afanye usanii kwa ajili ya muhula mwingine.

Kambale wote wana sharubu kama nilivyodokeza hapo awali. Mdogo anazo, mkubwa na mkubwa sana. Kadhalika kwenye kaya rushwa ni kuanzia chini kwenda juu na juu kuja chini kushoto na kulia. Huyu anajigamba ana bilioni kadhaa.

Rushwa imeshambulia kiwili wili kizima na kukibadili hadi kugeuka kama kansa ya kudumu (chronic cancer) kwenye kiwiliwili ( kaya). Miguu inayobeba mwili mzima (wazalishaji) imeoza. Tumbo (wanaowanyonya wazalishaji) nayo imeoza bila kusahau ubongo (wasomi). Jamii imeoza na kuzidi kuangamia kwa gonjwa hili.

Nani amsaidie nani? Tuliodhani ni madaktari hao ndiyo usiseme. Ni mahututi wa kufa kesho. Baya zaidi tumeridhika na kujiweka tayari kuangamia kwa pamoja kila mmoja kwa siku yake. Tumegeuka mateka wa matendo na mawazo yetu. Anayewatanabahisha wenzake anachukiwa na kuonekana kama kichaa wakati vichaa ni wale wanaopuuzia ushauri.

Tumegeuka kama panya kuguguna kila kitu hata msingi wa kaya! Tumegeuka wa hovyo kuliko hata panya. Maana wao ni hayawani.

Yule ana milioni kadhaa ya kukwapua na kuchangiwa na wezi wenzake hata wasio. Huyu anahonga na kuahidi vyeo kwa wawezeshaji au tuseme walamba viatu. Yule anahonga vinokia, manywaji, makulaji na hata lifti. Ukitaka kuijua hii soma kitabu cha Mpayukaji kitakapotoka kiitwacho NYUMA YA PAZIA.

Utayaona mafisi yanavyosherehekea nyuma ya pazia huku mbele ya hadhira yakijafanya makondoo na njiwa wakati mashetani na minyama mwitu ile ile leo juzi jana na kesho!

Hii ni kansa ambayo imepakwa mafuta na kuitwa mafua ya mauda wakati ni gonjwa tena hatari la kudumu. Vipofu wamegeuzwa waoni wakati ni vipofu. Kwenye kitabu cha SAA YA UKOMBOZI, Nkwazi Mhango ambaye ni pacha wangu anamaliza kitabu kwa swali dogo lakini lenye maana kubwa zuri na zito liulizalo: Je kipofu aweza kumuongoza kipofu?

Mara huyu kakamatwa mara yule kahonga vinokia, mishiko tuliyokuwa tukiwashitakiwa wachora maandishi sasa iko kwa wanuka jasho njaa na ukapuku!

Kila mtu sasa ni mwema na kila kitu ni chema ufalme wa mungu usifike. Mungu mwenyewe siyo Yehova, Allah wala nani bali Mulungula.

Je mungu mulungula anapotawala unategemea nini? Swali la mwisho ni toka katika kitabu cha SAA YA UKOMBOZI. Je kipofu akimuongoza kipofu inakuwaje? Na mwizi akiongoza mwenye mali inakuwaje? Hapa ni sawa na kusema kila kambare ana sharubu CCM
Nasikia harufu ya EPA mpya. Acha niishie kabla ya kulishwa rushwa kwa ajili ya kuniibia kwa miaka mitano.
Chanzo: Tanzania Daima Agosti 10, 2010

Monday 9 August 2010

Tujiandalie serikali ya mseto nchi nzima

Kabla ya kuingia undani wa kile nitakachokiandika, nachukua fursa hii kuwapongeza wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba kwa kuchagua kuwa na serikali ya mseto au ya umoja wa kitaifa hapo Agosti mosi. Kwa matokeo yaliyotoa kibali kuanzishwa serikali hii, si ufanisi kwa zanzibar tu bali hata bara. Wameonyesha njia na uvumilivu na mapambano yasiyoshindwa vya muda mrefu.

Tukirejea kwenye ujumbe wa leo, japo mie si mtabiri, kama tutasimama imara dhidi ya wizi wa kura na unyanyasaji wapiga kura inapotokea kutaka kuzuia wizi, natabiri tutakuwa na serikali mseto au ya umoja wa kitaifa hivi karibuni.

Ukiangalia kuingia kwa silaha ya moto yaani Dk Wilbrod Slaa kwenye mbio za urais zilizokuwa zimeanza kuchosha kutokana na kutawaliwa na ving'ang'anizi walioshindwa mara nyingi huko nyuma, kuja wa Slaa si bure. Licha ya kutoa mbadala, kunaleta kitu kipya ambacho watanzania wanakihitaji-ukweli katika kupambana na ufisadi.

Chama Cha Mapinduzi kinaweza kujigamba kuwa na kila kitu. Ieleweke. Kinakosa kitu kimoja ambacho CHADEMA wanacho-kufanya kazi kwa vitendo badala ya maneno kama CCM. Uko wapi utekelezaji wa ahadi alizotoa rais anayemaliza muda wake na mgombea na mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete? Hakutimiza hata moja. Heri angekiri kama mtangulizi wake Benjamin Mkapa kuwa sera za CCM hazitekelezeki. Je tunahitaji sera zisizotekelezeka ukiachia mbali watu wasio na uwezo wala visheni ya twende wapi kama ilivyojidhihirisha kwenye kipindi kinachoisha?

Kabla ya kudodosa zaidi, naomba niwarejeshe wasomaji wangu kwenye wizi wa kura ulifanywa mwaka 1995 ambapo kwa utafiti wa haraka tokana na kuhoji watu kwenye mikoa ya kati niligundua kuwa mgombea wa NCCR-Mageuzi wakati ule alikuwa ameshinda kutokana na kupmbanishwa na mtu ambaye hakuwa akijulikana wala kuijua nchi. Hivyo CCM waliweka wakachukua wakamtangaza mtu wao.

Kuondokana na hili, mwaka huu tuhakikishe hatukubali kufanyia uhuni huu. Tukisimama imara inalipa. Rejea kilichotokea nchini Zimbabwe na baadaye Kenya na sasa Zanzibar. Kwanini nasi tusisimame tukatetea haki zetu?

Nchini Zimbabwe, pamoja na ukandamizaji mkubwa wa imla Robert Mugabe, MDC walisimama hata kwa kuteswa hadi nchi ikawa haitawaliki kiasi cha Mugabe kulamba matapishi yake sawa na CCM ilivyofanya visiwani. Hivyo basi, matumizi ya mtutu wa bunduki na bandali za pesa hakuwezi kuua dhamira ya kujikomboa ya binadamu anapodhamiria. Nani amesahau mauaji ya mwaka 2001 na mengine yaliyofuatia visiwani lakini bado ithibati ya wazanzibar ikazidi kudhihiri kiasi cha kuiacha CCM ikiwa haina nguo wala la kufanya zaidi ya kufakamia matapishi yake?

Kitendo cha serikali ya CCM kuridhia serikali ya mseto licha ya kuonyesha kuishiwa na kuvuliwa nguo, ni ushahidi kuwa si jasiri kama tunavyoaminishwa. Pia ni ushahidi wa wazi kuwa wanaosema CCM itatawala milele wana matatizo ya akili. Itatawalaje milele wakati kwa upande wa visiwani imeishakwanyuliwa na kunyolewa bila maji?

Kama watanzania tutaacha ujinga na ukondoo na umshumaa, mwaka huu CCM inaweza kupigika pande zote yaani bara na visiwani kutokana na kuwa na wagombea wenye ushwishi mkubwa na rekodi safi dhidi ya wababaishaji na wenye rekodi chafu wa CCM.

Hatuzushi. Kikwete ametekeleza lipi kuhusiana na kupambana na ufisadi hasa ule wa EPA, Richmond, CIS, kuporwa nyumba za umma, kushughulikia wala rushwa, wauza mihadarati, majambazi na wengine ambao Kikwete alikiri kuwa na orodha zao. Muulize amezuiliwa na nani au nini kuwashughulikia? Muulize ahadi zake za maisha bora zimeishiwa wapi? Je kuna maisha bora au uchuro mtupu? Kama atatoa jibu hata moja, basi huna hata sababu ya kupoteza kura yako kuchagua kitu kile kile kilichozidi kukuzamisha kule kule kwenye matatizo na adhabu za umaskini na ukosefu wa kile ulichoahidiwa hadi ukatoa kura yako.

Hakuna haja ya watanzania kuendelea kushikiliwa na genge la mafisadi. Kuna mbadala muhula huu na mbadala huu ni Dk Slaa.

Iwapo watanzania wataamka kitandani walimolala na utawala mchafu na kuupiga chini, basi hawatakuwa tayari kuletawa matokeo ya uchaguzi ya kupikwa ima na tume ya uchaguzi au serikali iliyoiteua ili kuitumia kufua nepi zake. Watasimama imara na kuwa tayari kwa lolote wakijua mwisho wa siku watashinda. Tumeona mifano michache hapo juu ya watu wenye miili midogo lakini mioyo mikubwa walioangusha vigogo na mibuyu tena katili na vichaa kama Zimbabwe. Hata Afrika Kusini haikufikia ilipo kwa lelemama wala mteremko bali kusimama kidete na kupinga jinai ya ubaguzi iliyokuwa ikiumiza sawa na ufisadi.

Kuna haja ya kutumia fursa hii hasa kipindi hiki ambapo CCM licha ya kumeguka na kudhoofika, imeanza kuufyata kama ilivyotokea Zanzibar. CCM kipindi hiki haiwezi kuamrisha serikali yake itumie mtutu kwa kuhofia wakuu wake kujikuta korokoroni huko The Hague. Na hii si propaganda. Ni ukweli kuwa kwa sasa hata madikteta wanaoogopewa kama Yoweri Museveni, Paul Kagame na wengine wamebadili mwelekeo. Badala ya kutumia majeshi na tume feki za uchaguzi kama Tanzania, wanawanyamazisha au kuwaua hata kuwasababisha wapinzani ambao ni tishio kuozea magerezani kama ilivyo sasa kwa Victoire Ingabile huko Rwanda au kuwaua kama ilivyotokea kwa James Kazini Uganda na Andre Kagwa Rwisereka huko Rwanda au Asumani Nzeyimana huko Burundi. Wengine hutishia kuwakamata kiasi cha kukimbia nchi kama ilivyotokea hivi karibuni nchini Burundi ambapo kiongozi wa upinzani Agaton Rwasa alilazimika kuikimbia nchi ili kuokoa maisha yake.

Huu ni ushahidi kuwa kama umma wa wapiga kura utakataa kuibiwa kura zake hakuna nafasi tena ya kutumia ubabe wa polisi na wanajeshi kama ilivyokuwa ikifanyika uko visiwani.

Hivyo nimalize kwa kuwahimiza watanzania hasa upande wa bara kujiandaa kuingiza serikali ya mseto ambayo baadaye itaondoa huu uoza uliopo.

Kula pesa toka CCM. Lakini kura piga kwa CHADEMA. Mwaka huu tuchague maendeleo na mabadiliko si ukale uoza na mazoea.
Chanzo: Dira ya Mtanzania Agosti 9, 2010.

Thursday 5 August 2010

Tumebaki na siasa za uchakachuaji




CHAMA chochote cha siasa kikibinafsishwa na wafanyabiashara na kikajivua jukumu la ukombozi lililolengwa na waasisi wake, basi hugeuka kuwa moja wa maadui wa wananchi.

Ndivyo kilivyotokea kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Hakina tena mwelekeo wa uongozi. Kimsingi kimefisidika. Katika mazingira haya, uchaguzi ama huwa uchakachuaji au uchafuzi wa demokrasia.

Nasema hivi kutokana na uchakachuaji, kama ufisadi, kuanza kuwa sera rasmi ya CCM.

Rejea serikali kushindwa hata kuadabisha wanaojulikana kuchakachua mafuta hadi magari ya ikulu yananyweshwa mafuta machafu.

Hii ni kutokana na kupeana ulaji na tenda kwa misingi ya kujuana, ukiachia mbali kunyima na hivyo kuhujumu taasisi za umma za kushughulikia huduma hizo.

Jogoo aliwafundisha vifaranga kunya ndani. Ndio mtindo wa Rais Jakaya Kikwete na chama chake kuchangiwa shilingi bilioni 50 eti kwa ajili ya uchaguzi.

Fedha zote hizi za nini, kwa mgombea anayemaliza muhula wake wa mwisho, kama siyo za kuwahongea wananchi waliofanywa maskini na serikali hiihii ambayo bado inawachangisha pesa.

Hapa hujaongelea matumizi mabaya ya mali za umma kama vile magari, ndege na hata fedha taslimu – kulipana posho wakati rais akijinadi kwa kisingizio cha kukagua miradi ya maendeleo.

Jogoo aliwafundisha vifaranga kunya ndani. Kama rais anaweza kuchangisha shilingi bilioni 50, safi na chafu, kwa ajili ya 'kushinda', kwanini wabunge nao wasitenge vibilioni vyao walivyovuna kwa kuwauza wananchi kwa wawekezaji na matapeli wengine wa kiuchumi ingawa si wote?

Je, huu si uchakachuaji wa haki? Ukitaka kujua nimaanishacho, rejea kukamatwa kwa kadi bandia ambazo zinalenga, bila shaka kuwachakachua (kurudufu idadi ya wanachama) ili kupata maruhani na misukule ya kupiga kura.

Na huu ni utaratibu uliozoeleka hasa ikizingatiwa kuwa serikali imekuwa ikilipa mabilioni ya shilingi kwa wafanyakazi hewa bila kuchukua hatua, ilhali watu wetu wanazidi kuwa mafukara.

Leo hii tunajua hata thamani ya kura ya Mtanzania. Tunajua kuwa shilingi bilioni 50 ni bei ya jalada ya urais. Je, ubunge nao ni kiasi gani – vinokia, vitenge, fulana, pilau, ulevi?

Chini ya siasa za uchakachuaji CCM imegawanyika sana ingawa kwa juujuu tunaonyeshwa chama kilichoshikamana.

Kuna mitandao hasidi kama ile dhidi ya Samuel Sitta. Rejea kugunduliwa njama za kutaka kuwahujumu “makamanda wa vita dhidi ya ufisadi” kama Dk. Harrison Mwakyembe, Sitta, Lucas Selelii na wengine.

Angalia kutochukuliwa hatua kwa watuhumiwa wa ufisadi mkubwa serikalini; kwa mfano walioshiriki katika ukwapuaji wa mabilioni ya shilingi kuto Benki Kuu (BoT).

Chunga kimya kilichopo juu ya ujambazi wa kuchefua uliofanywa na makampuni kama vile Kagoda, Deep Green Finance na wengine, ambapo vinara wake ni wagombea tena wanaopigiwa upatu na wazito wa chama kama Katibu mkuu Yusuf Makamba.

Rejea kitendo cha waziri mkuu Mizengo Pinda na Makamba kumuomba mbunge wa Igunga, Rostam Aziz aliyetuhumiwa kuwa nyuma ya Kagoda kuendelea kugombea wakati ana mawaa.

Pinda alikaririwa hapo Mei mwaka huu akisema, “Rostam kama wewe ulijiona huna uwezo wenzako wameona...kauli ya wengi ni ya Mungu.”

Makamba alisema ameacha shughuli zake nyingi ili aende Igunga … kwa kutambua mchango wa Rostam kwenye chama cha CCM na uongozi mzuri jimboni kwake, ndiyo maana nimekuja.”

Ajabu, licha ya kuwa na wala na watoa rushwa wanaochakachua haki zetu, utakuta wengine ama ni wale waliotuhumiwa kwenye kashfa nzito za uhujumu wa taifa au walioghushi vyeti.

Anayepinga kuwa hawana ridhaa ya CCM na CCM haina sera ya uchakachuaji ajiulize ni kwanini serikali yake haiwachukulii hatua za kisheria.

Waingereza husema, “Show me your friend I will tell you who you are” – nionyeshe rafiki yako nitakueleza wewe ni mtu wa aina gani.

Wananchi wanapaswa kuvunja ndoa hii haramu na hatari ya wafanyabiashara wezi na CCM.

Je, unawezaje kuwa na uchaguzi huru na haki bila tume huru ya uchaguzi kama si uchakachuaji hata uchafuzi?, CCM inapenda na kulinda Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC).

Ukiangalia jinsi CCM inavyojivua jukumu la ukombozi na kujiingiza kwenye uchakachuaji, kuna kipindi unaweza kudhani wale wote waliokamatwa kwa kutoa rushwa wameonewa kutokana na mtandao waliomo.

Maana kwa mazingira ya sasa, inawezekana asipatikane hata mbunge mmoja wa CCM wa kurejea bila kutoa rushwa.

Rejea maneno ambayo hayakukanushwa na chama wala wabunge ya mbunge aliyeamua kustaafu kwa madai kuwa amechoshwa na kuombwa rushwa, Chrisant Mzindakaya.

Vilevile, kwa historia ya utendaji, CCM na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ni kitu kimoja. TAKUKURU haiminiki na si huru (none bias); na hili lilionekana vema wakati wa kashfa ya Richmond.

Je, wale waliotaka kuitumia TAKUKURU kipindi kile, hawaitumii kwa sasa kulipiza visasi, ikichukuliwa kuwa ni vinara wa mtandao unaodaiwa kuundwa na wale wanaotuhumiwa ufisadi dhidi ya wale wanaopambana nao?

Katika mazingira haya, hata TAKUKURU ikimkamata rais, haiwezi kurejesha heshima na imani yake kwa umma. Dawa ni kuoindoa chini ya rais na kuifanya kuwa tume huru sambamba na tume huru ya uchaguzi.

Uchakachuaji ni balaa na huua nyoyo. Mkuu wa wilaya au waziri mzima anakamatwa kwa kutoa rushwa, lakini si serikali wala chama, kinatoa tamko la angalau kukaripia.

Je, hapa kuna kusonga mbele kwa mwananchi wa kawaida mbebeshwa mizigo kama punda kihongwe?

Huu ni msimu wa uchaguzi. Kitu muhimu kwa wapigakura ni kukiadhibu CCM kwa kuwauza na kuwasaliti ukiachia mbali kuwatelekeza. Hili liwe somo kwa wengine tunaoweza kuwakasimisha madaraka hapo baadaye.

Hakika umefika wakati wa kuzika siasa za uchakachuaji za CCM.
Chanzo: MwanaHALISI Agost 5, 2010.

Bravo Malawi! The Warm Heart of Africa

Malawi picker

Despite the fact that Africa is often left out in competitions especially those that do not touch on athletics or football, we have some countries that can carry our flag and make us proud.

The recent search for the happiest place on the planet by Lonely Travel Guide, came with something interesting and surprising. In this search, the Canadian city of Montreal topped the list of 10 happiest places on the planet followed by Texas a self-proclaimed a city without a frown in US. Other giants with all, big names, economies pomposity and what not such as New York, Rio de Janeiro, London, Paris you name it were surveyed but did not make it to the top.

Who thought: a poor country like Malawi would feature high in the first place? Believe it or not, Malawi, despite being dirt-poor, made it and found herself among the top ten thanks to her welcoming people and green scenery almost everywhere. This tells us how environmental protection pays more dividends than we tend to think. But is it possible without a good and understanding government?

Another thing to note, generosity does, so too, pay. On this, Lonely Travel Guide had this to say: "If it's grins you're after - big, unabashed ones - head to Malawi, dubbed the 'warm heart of Africa'. The country's people are renowned for the effusive welcome they give travellers, despite living in one of the poorest nations."

LTG did not end there. It added: "From the woodcarving markets of capital Lilongwe to the sandy shores of Lake Malawi and the elephant-grazed bush of Liwonde National Park, you’ll be accosted with smiles at every turn."

Though this maybe brushed aside by detractors, the thing is, it is a challenge-cum-lesson to other African countries with vibrant tourism like Tanzania, Kenya and even Uganda. While we struggle to advertise and convince tourists to come to our countries, other countries have a different way of doing it. Currently, our image is not good thanks to some criminal incidents involving tourists. Refer to shootings of Americans in Kenya, robbery-related occasions in Tanzania, corruption, time wasting at our airports and other points of entry not to mention unstable services such as water, electricity and transport for some countries.

We spend a lot of money advertising our attractions. Tanzania recently spent controversial amounts on CNN. In lieu of wasting this money we badly need, we need to spend it educating our people on the importance of tourism to our wellbeing. We should let them know that their behaviour individually and as a society is an asset shall we need to boost our tourism.

Our governments should embark on the rule of law and true fight against poverty and graft. Our people don't get it when they are told our economy depends on tourism among others. How can they whilst they are left out to suffer and die in miserable poverty whilst the cabal of a few individuals with power is living in opulence? How can they get it when it comes to conserve environment whilst the governments are not putting sound and practicable policy in place for this?

What's more, those attacking tourists or asking bribes or delaying them so as to be given some money may think they are making a killing. Importantly, we need to understand. Being poor does not warrant you to be involved in crime. Malawi is among the dirt-poor countries on earth but her people are generous and trustworthy, something that is missing in East Africa. Whilst it is a boo for us, Malawi is all cheers when one visits the country. Borrow a leaf.

Generosity and security are surer impetus in attracting tourists than adverts. Human beings are like satellites. Wherever they go, they report whatever treatments they were accorded.

Bravo and kudos to Malawi the warm heart of Africa! You have proved to truly be the warm heart of Africa. Don't let your mojo be broken or tarnished. Keep it up!
Source: The African Executive Magazine August 4, 2010.