The Chant of Savant

Saturday 28 January 2017

Bongo kuna jaa si njaa


          Kuna mjadala ulioniacha hoi hivi majuzi. Mjadala wenyewe ni juu ya kuwa kama kuna baa la njaa Kayani au la? Upande wa utawala unasema hakuna kitu kama hii wakati upande wa upingaji ukizidi kukoleza moto kudai hali ni mbaya. Baada ya sintofahamu na mparaganyiko utokanao na madai kama haya, Mlevi nimeamua kuingilia kuamua ugomvi usio na tija kwa kaya na walevi wake. Wakati wawili tajwa wakigombea nani mwenye mamlaka ya kutangaza balaa, mie nitajitenga na mjadala huu. Badala yake nitajikita kwenye mambo ya kifalsafa na kilevi lau niwape shule ya bure. Hivyo, naelekea suala hili kwa kuangalia yafuatayo:
            Mosi, je Bongo pamoja na kuwa na ardhi yenye rutuba kiasi ilicho nacho inaweza kukumbwa na baa la njaa au balaa la akili za njaa? Haiingii akilini kwa kaya kama hii kukumbwa na baa la njaa kama itatumia akili za shibe na si za njaa na kuombaomba kama ilivyokuwa chini ya Njaa Kali na watangulizi wake akina Dugong Makapi.
            Pili, inakuwaje kaya yenye walevi milioni zipatazo 50 kukumbwa na baa la njaa wakati wa akili na mikono zana wanazohitaji kuwekeza kwenye ardhi na rutuba yake na kuweza kujilisha na kulisha wengine. Sitegemei walevi kulishwa makapi toka kaya zenye wenye njaa kali kama vile Uchina na Ugabacholi, Sirilanka na kwingineko. Mtalishwa sumu hasa ikizingatiwa jamaa hawa wanavyowabagua weusi.
            Tatu, tukiachana na akili za njaa zenye kuweza kuleta njaa, inakuwaje kaya yenye mito na maziwa kukubwa na njaa wakati ina uwezo wa kulima hata wakati wa ukame? Hapa tatizo si njaa bali jaa la ujinga na kutokutumia upstairs vizuri. Hapa lazima tukubaliane kuwa zama za kutegemea matone ya mvua wakati yamejaa kwenye mito na maziwa umeishapita siku nyingi. Badala ya kuwekeza kwenye siasa majukwaani mkirushiana vijembe na hata wengine kuzua, wekezeni kwenye mipango ya maana inayoweza kukomboa kaya yenu tokana na balaa la njaa kuanzia vichwani, mioyoni hadi matumboni. Naweza kusema wazi kuwa kama kuna njaa inayoweza kusababisha baa la njaa si nyingine bali njaa ya kichwani ambapo wenye kuwa nayo hupiga domo bila kuchapa kazi.
            Juzi kuna mwanasiasa wa upingaji aliniudhi nusu nipasuke. Huyu jamaa anaitwa Mzito Kabwela. Si alidai kuwa rahis anaogopa kutangaza kuwa kaya inakumbwa na balaa na njaa. Kwani rahis ndiye anayetengeneza mvua au njaa kiasi cha kuogopa kuitangaza? Kwani rahis ndiye aliyewapa baadhi ya walevi njaa vichwani hadi aogope kutangaza njaa ya tumboni? Kwanini rahis atangaze kitu ambacho hakipo au cha kujitakia?
            Kama tutakuwa wakweli kwa nafsi na mawazo yetu, lazima tukiri. Tuna tatizo tena kubwa tu. Mfano, tunafyatua vitegemezi vingi kiasi cha kuongeza mzigo bila kusahau tunavyoruhusu wakimbizi wengi wa kiuchumi kuja kula vyakula vyetu kiasi cha kuanza kuhofia njaa. Wakati mwingine huwa nawashangaa waswahili na mapenzi yao ya mshumaa kama si ujinga. Wakati wanafukuzwa majuu na kuonekana kama balaa kwa maendeleo na tamaduni za majuu, kaya zao zinaendelea kukaribisha wakimbizi wa kiuchumi hasa toka Uchinani na Ugabacholini? Ninapoongelea jaa na njaa ya mawazo ninamaanisha hii? Hivi ni mswahili gani anaweza kwenda Ugabacholini akaruhusiwa kukaa  au kutajirika kinyume cha sheria kama ilivyo hapa? Tieni akilini.
            Haiwezekani mkaishi kama wanyama mbugani bila vitambulisho mkawa salama wakati mmezungukwa na kaya zenya njaa na vita. Ni vyakula kiasi gani vinapenyezwa mipakani tokana na kutokuwa na usalama? Leo mnalalamika njaa. Ngoja itakapoanza njaa ya wanyama wetu ndipo mtashika adabu. Ni mara ngapi tunaambiwa kuwa kule akina Nshomile kuna wafugaji toka kaya jirani wamevamia kaya kusaka malisho wakati ndugu zetu akina Ng’wadera wakihaha kusaka malisho hadi kupotelea Selous. Hii ni akili au jaa?
            Kwa vile sijanyaka kanywaji, acha  leo nikomee hapa huku nikishauri wanasiasa waache ugomvi na urongo visivyo na sababu. Waseme ukweli kuwa kayani tuna jaa na njaa ya mawazo lakini si njaa. Waache kusambaza njaa na urongo. Na badala yake kila mmoja aje na mipango yake ya kuonyesha kuwa hana njaa upstairs na mingine ya kupambana na njaa na jaa vinavyonyemelea kaya kwa kujitakia.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.

Thursday 26 January 2017

Kikwete hakustahili kuwa Mkuu wa UDSM

             Baada ya rais John Magufuli kumteua rais mstaafu Luteni Kanali mstaafu, Jakaya Kikwete kuwa mkuu wa chuo kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM) wanaojua namna Kikwete alivyokacha nafasi hiyo walishangaa sana. Inakuwaje mtu aliyekacha nafasi husika akiwa na madaraka afae kwenye nafasi aliyoikacha mwenyewe? Je nini maana ya kustaafu? Je hakuna watu wengine, tena wenye sifa, ambao wangeweza kuteuliwa? Mie naona kuteuliwa kwa Kikwete ni tatizo. Kwanza, kama nilivyosema hapo juu, hana sifa za kuwa mkuu wa chuo kikuu nje ya urais. Uzoefu wake wa kuacha nafasi hiyo unaweza kusema mengi. Pia anapopewa kazi kama hiyo, ina maana anapokea mishahara miwili yaani marupurupu na stahiki za rais mstaafu na mkuu wa chuo. Ukitaka kuona tunachomaanisha kuhusu kutofaa kwa Kikwete kuwa mkuu wa chuo, juzi alifanya kama alivyofanyiwa kwa kumpa mkataba wa mwaka mmoja rafiki yake Profesa Lwekaza Mkandala alipotimiza umri wa kustaafu. Je hapakuwapo na maprofesa wengine wenye siha ya kuweza kushikilia wadhifa huo au ni yale yale ya kutumia ofisi na nafasi za umma kufadhiliana? Kwani lazima Kikwete au Mkandala? Hii si haki. Inakuwa kituko kwenye taasisi ya kisomi kama UDSM kuendeshwa kisiasa kiasi cha watu binafsi kuigeuza kama taasisi isiyo ya kisomi. Nadhani, kwa aina ya taasisi, haikupaswa ku-recycle watu au kuwa na watu ambao ni recycled. Taasisi inayozalishwa wasomi kila siku haiwezi kukosa mtu wa kufaa kuwa mkuu wake hadi aliyestaafu awe-recycled. Kwa maana hiyo, rais afikirie kufuta huu mkataba wa nyongeza aliopewa Mkandala na rafiki yake Kikwete. Pia kwanini Magufuli asiige mfano wa Mwl Julius Nyerere wa kuwa mkuu wa chuo kikuu hiki muhimu na cha kwanza yeye mwenyewe badala ya kuendeleza utamaduni ulioanzishwa na watu waliokuwa wakiogopa kwenda kule kukalishwa kitimoto kushiriki midaharo? Magufuli ni msomi.
            Tokana na mfumo wa chama kimoja, tulizoea, na kusimikwa ufisadi na ubinafsi baadaye, kupeana kazi kwa kujuana na kulindana. Hivi karibuni rais John Magufuli alisikika akisema hakuna mtu atakeruhusiwa kuwa na vyeo viwili kwa wakati mmoja. Hii maana yake ni kwamba mtu anaposhikilia nafasi mbili, licha ya kupokea mishahara zaidi ya mmoja, anawanyima wengine fursa ya kuajiriwa. Hili moja, je hali inakuwaje anapoteuliwa mtu aliyekwisha kufanya kazi na kustaafu huku wakiachwa wale ambao hawajawahi hata kupata fursa hii?
            Tangu aingie madarakani, rais Magufuli amefanya mambo mengi mapya na makubwa. Hata hivyo, inaonekana anaanza kukwamishwa na mazoea kiasi cha kuanza kujipinga kuhusiana na haki za ajira kwa watanzania. Kwani akiwa rais ameishawateua watu waliostaafu tena wasiofaa kuwa wenyeviti au wajumbe wa bodi. Chukulia Anna Abdallah  kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya Makumbusho. Huyu alishashika kila wadhifa kuanzia ubunge hadi uwaziri. Kama ni kuchuma ameishachuma vya kutosha. Mwingine ni spika wa bunge mstaafu, Anna Makinda ambaye aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya NHIF. Huyu kama si tamaa, ameishachuma vya kutosha. Kama Abdallah alishakuwa mbunge, waziri hadi spika. Hata umri wake si wa kuutumikia umma bali kulea wajukuu. Mwingine ni  Augustine Mrema aliyeteuliwa kuwa mwenyekiti wa Parole wakati ima wahusika walishastaafu au wana nafasi nyingine kama Mrema kama siyo kuendeleza ukale na ubinafsi wa chama  kimoja ni nini? Je uenyekiti na ujumbe wa bodi upo kuhifadhiana kwa wanasiasa au kwa minajili ya utendaji bora kwenye mashirika.
            Ukiachia mbali bodi za mashirika, uchochoro mwingine ambao umekuwa ukitumiwa na serikali kufadhiliana ni ofisi za balozi zetu nje.   Unashangaa kuona mtu anastaafu mfano jeshini hapohapo hata kabla ya kufika nyumbani anateuliwa balozi. Unajiuliza; kwani hizi nafasi ni za rais binafsi kiasi cha kuacha vijana wengi waliojaa wizarani na mitaani wenye ujuzi wa kuweza kuwakilisha nchi?  Tunao mabalozi wangapi wazee waliokwishastaafu jeshini au kwingineko lakini wakateuliwa kwenye nafasi kama hiyo inayohitaji watu wenye kuchemka na wenye nguvu? Mfano mwanajeshi na ubalozi wapi na wapi kama tutatukuwa wakweli? Wengine wanastaafu na kuteuliwa wakuu wa mikoa au wilaya. Je hii si kuwanyima kazi watanzania wengine wenye haki na uwezo wa kushika nyadhifa hizi? Kwanini tusibadili sheria na kuweka vipengele vilivyo wazi kuwa watu ambao wameishafanya kazi na kustaafu wasiruhusiwe kuteuliwa kwenye nafasi zozote? Tokana na serikali ya hovyo na goigoi iliyopita, tumejaza watu wa hovyo kwenye ofisi zetu za ubalozi nje. Walioteuliwa kutokana na kujuana.  Hawa nao wanapaswa kutumbuliwa tu ili kuepusha hasara kwa taifa. Kwani, walipewa mamlaka wasiyo na sifa wala uwezo nayo.
            Tumalizie kwa kuwataka rais na wananchi kuhakikisha unapangwa utaratibu wa kuepuka ajira na uteuzi ambao si chochote bali recycled, sina neno la Kiswahili.
Chanzo: Tanzania Daima.

Wednesday 25 January 2017

Wizi ndani ya wizi AUWSA wahusika wawajibike

Image result for photo of ruth koya
             Hivi karibuni, vyombo vya habari vilifichua wizi wa kutisha kwenye Mamlaka ya Maji kule Arusha (AUWSA) ambapo zilitumika jumla ya shilingi 198 milioni kuchunguza ufisadi wa shilingi milioni 18. Mwanzoni nilidhani utani. Kwa vile vyombo vya habari havina utaji na mafisadi, baada ya kusoma habari nzima nilibaki kuchukia na kupigwa na butwaa hasa kipindi hiki ambapo taifa limo kwenye mapito ya kulirejesha kwenye mstari na kupambana na ufisadi na wizi wa mali za umma. Kabla ya kusema mengi, lazima niseme wazi wazi kuwa wahusika wawajibike wenyewe au wawajibishwe mara moja ili kutoa onyo kwa masalia ya mafisadi yasiyosoma alama za nyakati.
Ni akili gani kutumia milioni 198 kuchunguza ufisadi wa milioni 18? Inanikumbusha kisa cha hivi karibuni ambapo dereva wa basi nchini Korea ya Kusini alitimliwa kazi kwa kuiba dola mbili za nauli wakati mkuu wa Samsung Jay Y Lee akidaiwa kumhonga jumla ya dola milioni 36 Choi Soon-Sil mshirika wa rais aliyesimamishwa madaraka Park Geun-hye. Ajabu ya maajabu, pamoja na kuhonga mamilioni ya dola, Lee aliachiwa huru kiasi cha kuonyesha kuwa kuna sheria za walio nazo na wasio nazo. Sidhani kama tanzania tunahitaji kuwa na sheria za namna hii ingawa kuna ushahidi kuwa serikali zilizopita zimewahi  kufanya hivyo hasa tukiangalia kashfa sugu kama vile EPA, Escrow, IPTL, Ndege ya Rais, Rada UDA na nyingine nyingi.
            Tukirejea AUWSA, ukisikia kuuza ng’ombe kwa kesi ya kuku ni huku. Je hii ni akili au matope? Kwanini wahusika hawakufanya mahesabu ya darasa la kwanza na kujua kuwa kiasi walichopanga kutumia kuchunguza ufisadi kilionyesha ufisadi mkubwa kuliko ule uliofanywa? Hii ni sawa na kumpiga mbu risasi huku ukitaka kumpiga kibao tembo kwa dhamira ya kuwaua wote.
            Je wahusika wanangoja nini wakati kila kitu kiko wazi?
Hivi nao wanangoja watumbuliwe na rais John Magufuli au waziri mhusika? Kwanini hawataki kutumia common sense na kuachia ngazi?
            Gazeti moja litolewalo mara moja kwa wiki lilifichukua kuwa wajumbe walioteuliwa na mkurungenzi wa AUWSA, Ruth Koya walikuwa wakilipwa shilingi 800,000 kwa siku fedha ambayo hata wabunge na mawaziri hawajawahi kulipwa kwa siku tena kufanya kazi isiyo na kichwa wala mguu. Ajabu ya maajabu, wahusika eti walikuwa wakilala kwenye mahoteli ya bei mbaya mjini Arusha wakati wao wenyewe ni wakazi wa mji wa Arusha. Haya ndiyo yale aliyowahi  kusema rais John Magufuli kuwa Tanzania ilifikia pabaya ambapo wajumbe wa bodi walifikia makufuru kwa kuweza kufanya vikao vya bodi ughaibuni wakishughulikia masuala ya Tanzania kana kwamba Tanzania hapakuwa na hoteli. Hapa hujagusia nauli za ndege ambazo hata hawa wa Arusha walilipwa.
             Sasa nini kifanywe?
Mosi, mbali na mkurugenzi wa AUWSA, wote waliohusika na ufisadi huu wa kijinga watajwe na kuwajibisha mara moja kama watashindwa kujiwajibisha ili kupisha uchunguzi kama kweli hawakuwa wamedhamiria kufanya ufisadi.
            Pili, wahusika wa kashfa hii hawapaswi kujiwajibisha wala kuwajibishwa tu bali kufikishwa makamani na kurejesha fedha ya umma waliyoiba kwa njia ya kuchunguza kipele wakati wao wakiwa ni majipu tena sugu bali wasimamishwe kazi kwanza kama nafsi zao zitashindwa kuwasuta wakajiwabisha wenyewe. Hawa ni wahalifu wanaposwa kutoonewa huruma hasa ikizingatiwa kuwa wanapofuja na kuiba fedha za umma hivi, hutumia njia za ajabu kama kupandisha bei ya huduma ili kuendelea kupata fedha ya kuiba na kuchezea.
            Tatu, nashauri uchunguzi ufanywe kwenye taasisi za umma ambamo kumetokea kashfa kama hizi na kuchunguzwa ndani kwa ndani. Inawezekana kilichotokea Arusha ni kipele wakati kuna majipu makubwa tu. Hii inapingana na juhudi za rais za kubana matumizi ili fedha itakayookolewa iwafae maskini badala ya kuendelea kufujwa na kuibiwa na matajiri wengi waliokwisha kujineemesha kwa njia hii miaka nenda rudi chini ya tawala za hovyo zilizopita.
            Nne, mtuhumiwa wa kwanza yaani Koya, alipaswa kuwa nje ya ofisi na mahabusu ili kuepuka kuharibu ushahidi kama ilivyozoeleka nchini ambao inapotokea kashfa kama hizi ushahidi hupotezwa hata kwa kuchoma ofisi bila kujali hasara wahusika wanazolitia taifa.
            Tano, uteuzi au uajiri wa Koya unapaswa kuchunguzwa kuona kiwango chake cha elimu na namna alivyoajiriwa hata kupandishwa cheo kufikia alipo kiasi cha kutojua mipaka ya wadhifa wake. Nimekuwa nikipiga kelele kuwa tunao vihiyo, mafisadi na wahalifu wengi kwenye ofisi na taasisi za umma karibu zote bila kusikilizwa. Sasa naamini wahusika watasikia na kuchukua tahadhari kuhusiana na kadhia kama hizi.
            Itoshe kumalizia kwa kutaka wizara husika ichukue hatua mara moja. Na kama itaendelea kusuasua basi rais aingilie kati ili kuepusha fedha ya umma kuendelea kuibiwa ukiachia mbali mzigo utokanao na kadhia kama hizi kutwishwa wananchi maskini wanaotumia huduma za mamlaka kama hizi. Wahusika wachukue hatua za haraka na za makusudi ili kuepuka kuwapa nafasi watuhumiwa kuharibu ushahidi. Tunaomba kutoa hoja kuwa watuhumiwa wa kashfa ya ufisadi ndani ya ufisadi ya AUWSA ima wajibwajibishe au kuwajiishwa mara moja.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.

Mpayukaji arejea toka Gambia kumtimua Jammeh

          Baada ya kuupa tafu upingaji nchini Gambia na kumtupa nje imla wa huko wa siku nyingi Yaya Jammeh akagoma kukitoa, ilibidi nirejee tena kumtimua tena kwa aibu. Hii ni baada ya jamaa kujifanya hamnazo akajipiga ntama na kutaka aendelee kukinajisi ki nchi hiki kiduchu kule Afrika ya Magharibi. Baada ya kuupa mbinu upingaji kuungana na kumteua Adam Baro kuwa mgombea wake na kushinda, nimeamua kuupa tafu upingaji wote barani Afrika ili kuondokana na utawala msonge na wa kikale ili kuleta maendeleo.
            Nilipiga kampeni kwa marafiki zangu wanene kama vile Mahamadu Bahari na Alpha Shamba Konde na bi Nkubwa Helena Salifu kunipa tafu ya ndata kumchakaza na kumnyaka jamaa na kumtupa lupango. Nilipofika kule, nilikwenda kuonana na Yaya na kumkumbusha namna tulivyomfanyia kitu mbaya Idi Amini yule dada wa Uganda tuliyempa kichapo hadi akatimkia kwa Mwamari Kashafi zama zile akiwika asijue naye ataishia pakanga.
            Baada kumbana habithi huyu ambaye alikuwa amekamia kutoacha madaraka kwa kumtishia kichapo toka kwa ndata wa washirika zangu, ilifikiwa uamuzi kuwa aamue kusuka au kunyolewa. Kwa kujua kichapo kilivyo kikali hadi kuweza kusababisha maafa hata kifo, habithi huyu aliamua kumwaga manyanga na kuachia ngazi huku akielekea ukimbizini akingojea kujua kama ICC itampa mwaliko wa kwenda kulala The Hague akishirika karamu na akina Badboy Gbagbo na Chazi Teila.
            Pamoja na kusherehekea ushindi wa demokrasia nilivyochangia kule Gambia, napenda kutoa taarifa kuwa ving’ang’anizi wa madaraka kuanzia Kusini hadi Kaskazini na Mashariki hadi Maghabiri wakae mkao wa kuliwa hasa ikizingatiwa kuwa wachovu sasa wameamua kuwafanyia kweli wezi na maimla wao. Nimegundua siri ndogo ya kuwabwaga madikteta. Ni kwa wapiga kura kujiandikisha kwa wingi huku wapingaji nao wakiungana kimakwelini na kuondoa upuuzi kirahisi tena mara moja. Kuna jamaa yangu aliniacha hoi. Alidai kuwa maimla wengi barani Afrika sasa wanamlaani Jammeh kwa kundaa uchaguzi bila kuwa na namna ya kuchakachua na kuibuka mshindi tenakwa kishindo kama siyo kitsunami. Waduwanzi hawa wanashangaa namna mtu tena mwenye uchu wa madaraka kuweza kuandaa uchaguzi halafu akashindwa kuuchakachua; wasijue kuwa za mwizi ni arobaini na zikifika huwa hakuna ujanja.  Hii ndiyo maana nawaambia wazi wazi kuwa siku zao zikifika iwe ni kwa heri au shari watafurushwa au kunyotolewa roho kama rafiki na baba yao Kashafi alivyofanyiwa.
            Cha mno hasa hapa Bongolalaland ni kwa wapingaji kujipanga upya wakijenga hoja na kuungana na si kuunda ushirikiano. Mtazidi kugalagazwa huku mkilalalamika na kuzua. Kwa mfano, lazima mrejee kwenye hoja yenu ya kupambana na ufisadi badala ya kubabishwa na mafisadi wachache kuwa watawawezesha kuchukua dola.
            Katika kusuluhusiha mgogoro wa Gambia niligundua kitu kimoja cha kustua. Licha ya kuwa kihiyo asiye na elimu yeyote, kumbe Yaya Jamaa alikuwa kichaa hakuna mfano. Aliwakua akitembea na mifimbo, mishanga na kitabu cha dini moja ambayo sitaki kuitaja japo inajulikana akijipachika kila sifa na vyeo wakati sifa kuu aliyo kuwa nayo ni mwehu. Alijiita Alhaj, Daktari kama Njaa Kaya huku akikwepa kutumia cheo chake cha kijeshi cha Luteni Kanali, Profesa, kama wale waganga wa kienyeji huku akijifanya amegundua tiba ya miwaya asijue yeye mwenyewe hana tofauti na miwaya alivyowatesa Wagambia. Mara nyingi vihiyo kama hawa hupenda vyeo vikubwa vya kisomi wakati walikimbia umande. Nani mtu mwenye akili timamu anaweza kujipachika sifa za kisomi kama daktari wakati hajausomea huo udaktari?
            Wapo wengine wanaodai kuwa huenda hakuwa mtoto riziki hasa ikizingatiwa alivyopenda kuvaa magauni na kuwa na mwili mkubwa kuliko wake. Wengine wanadai alikuwa akificha mavazi ya kuzuia shaba. Kwa vile alikuwa akijua angeweza kurambwa shaba wakati wowote tokana na uduwanzi wake. Alijiita shehe na kutangaza Gambia kuwa taifa la kiislamu huku mkewa akishindwa hata kuvaa ushungi wa kawaida! Kuna jamaa alinitonya kuwa jamaa huyu–kama rafiki yake Kashafi ambaye wanae walikuwa wakikata kalaji kama hawan akili nzuri–anakunywa kama hana akili nzuri. Kuna ukweli kwenye madai haya hasa ikizingatiwa kuwa jamaa alikuwa anajifanya kuijua dini kuliko hata watasha wenyewe wenye dini ukiachia mbali baadhi ya kaya zao kutawaliwa kidini. Utawala wa kidini tena dini yenyewe nyemelezi na mswahili wapi na wapi? Angekuwa msomi angeanzisha utawala dini za kiasili za Kiafrika badala ya kupwakia vya wengine asijue vingemuumbua na kumuonyesha kama mnafiki na limbukeni wa kutupwa. Mbona sasa hakukimbilia kwenye kaya za kidini kama kweli alikuwa ni mtawala wa kidini? Usanii mwingine bwana ni wa kishenzi hakuna mfano.  Acha waitwe watumwa tokana na kupwakia vya watu huku wakivitukana na kuvidhalilisha vyao. Hamuwezi kuendelea kwa kuiga vya wengine. Angalia machainizi na Wajep wanavyozidi kupeta tokana na kuheshimu asili zao.
            Kwa vile ndiyo nimeshuka toka kwenye pipa, acha nikitoe niende zangu kujiweni kupata update ya kilichoendelea wakati nilipokuwa nje ya Kaya. Nasikia wapo watu tena wazima wanashindania kutangaza baa la njaa wasijue wao ndiyo baa lenyewe!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
 

Monday 23 January 2017

Barua ya wazi kwa mheshimiwa Godbless Lema

Mpendwa Godbless,
            Naamini hujambo huko uliko kwenye mazonge ya kufungwa bila kuhukumiwa. Najua ni machungu kiasi gani unapitia wewe, familia, marafiki na chama chako bila kusahau wapiga kura wako na watanzania wapenda demokrasia ya kweli na utawala bora nchi nzima.
            Wapenda amani, demokrasia na haki tunajua kinachoendelea; ni kinachokusudiwa kwa kunyimwa dhamana na kufungwa kwa muda mrefu bila maelezo ya kina. Waingereza huiita hii character assassination ambapo zandiki hulenga kukufanya uonekane kama mtu asiye na heshima wala maana kwenye jamii. Pia unaweza kuita kinachoendelea, licha ya kuwa uvunjaji wa sheria na haki za kiraia za kikatiba ni kile waingereza huita breaking someone’s spirit ambayo ni hali ya kumweka mtu kwenye mateso na mazingira ya kumfanya aondoe matumaini na kujiona si chochote si lolote. Wewe nakujua; ni mpiganaji asiyetishwa wala kukatishwa tamaa. Nakujua kupitia vyombo vya habari. sikujui personally. Hata hivyo, licha ya kuwa mwandishi, msomi na mchambuzi, ni mfuatiliaji wa mambo yanayofanyika nyumbani japo naishi ughaibuni.
            Mheshimiwa Lema, niliguswa sana na kinachoendelea nchini ambapo kuna wimbi la ajabu na hovyo la kuwafunga wabunge wa upinzani. Sina maana ya kusema kuwa nyinyi ni malaika. Je kwanini wabunge wa upinzani? Je tuna majambazi tena yanayojulikana mangapi yamejazana bungeni na hayaguswi kwa vile hayapingi wenye mamlaka? Hivi wale waliopewa fedha ya Escrow si majambazi wa kawaida hata kama hawatumii bunduki bali kalamu? Je walioshiriki ujambazi wa ununuzi wa rada na ndege ya rais wakajipatia mabilioni ya shilingi si majambazi hata kama wanaitwa waheshimiwa? Je hapa tunamdanganya na kumkomoa nani na hadi lini wakati ukubwa una mwisho? Wako wapi akina Benjamin Mkapa waliotuita wavivu wa kufikiri? Wako wapi akina Basil Pesambili waliotutaka tule majani ili wafanikishe jinai yao? Wako wapi majambazi wa EPA na Kagoda? Wako wapi waliohujumu UDA na kuitoa kwa wenzao?
            Mheshimwa Lema, najua ukipata waraka huu utafarijika japo kwa siku moja kujua kuwa wapo wanaothamini mchango wako. Ninachoweza kusema ni kwamba wanaweza kuua na kutesa mwili lakini si roho wala mawazo yako. Akina Nelson Mandela walipitia huko. Akina  Walter Sisulu, Oliver Tambo, na wengine wengi walipitia huko. Je walikatishwa tamaa na wakandamizaji wao? Je walisaliti mawazo, misimamu na imani zao? Hasha. Badala ya kuwavunja moyo na kuwafanya wajione hawafai, walizidi kuimarishwa na kusimamia kile walichoamini. They can destroy your corporeal world but not your spiritual one. Sitatafsiri hii. Orodha ya wahanga na mashujaa ni ndefu. Akina Edward Moringe Sokoine, Steve Bantu Biko, Solomon Kalushi Mahlangu, Edwardo Chivambo Modlane, Samora Moise Machel, Josiah Mwangi Kariuki, Pio Gama Pinto, mtemi Mkwawa, Milambo na wengine wengi waliuawa na wakandamizaji. Hata hivyo, bado tunawakumbuka na kuwaenzi kwa kujitoa kwao mhanga kwa ajili ya demokrasia na haki. Bado historia zao zimeandikwa kwa wino wa dhahabu si kwa sababu nyingine bali kupambana na ukandamizaji na kujitoa mhanga kwa ajili ya watu wao. Wako wapi akina Christopher Mtikila, Kassim Hanga, Major Tito Okello na mashujaa wengine? Nani huyu hataonja mauti?
            Mheshimiwa Lema, japo ujumbe huu ni wako, si wako peke yako; ni wako na mkeo, watoto wako, wazazi wako, ndugu zako, wapiga kura wako, marafiki zako na wapenda haki wote nchini na duniani kwa ujumla. Sitajadili kesi unayopambana nayo mahakamani. Ni kinyume cha sheria. Badala yake nakuandikia kama binadamu ambaye hujafa wala hujaumbika. Nani anajua mwisho wake hasa katika safari ya kisiasa? Je mbora kati yetu ni nani kati ya wazandiki, mafisadi, maimla na wababaishaji na wapigania haki?  Najua fika, kuna mambo yasiyo ya maana yanaweza kuwa yanaendelea kisiasa pamoja na kuwa na serikali inayochapa kazi. Nilishangazwa na kifungo chako kisicho cha kawaida na kile cha mwenzio mheshimiwa Peter Lijualikali ambaye naye na familia yake, wapiga kura wake, marafiki zake, ndugu zake na wapenda haki watafarijika na ujumbe huu.
            Shujaa na kipenzi cha dunia Nelson Mandela aliwahi kusema “ bindamu anaponyimwa haki ya kuishi maisha anayoamini, hana chaguo zaidi ya kuwa mhalifu” hata kama kwa kubambikiwa kama ilivyo kuwa kwake alivyoitwa gaidi na magaidi, mhalifu na wahalifu, mtu hatari na viumbe hatari na majina mengine mengi.
            Nichukue fursa hii adimu na adhimu kumuomba rais John Pombe Magufuli asiruhusu washauri wabaya kuichafua serikali yake. Asiruhusu siasa za visasi na ukandamizaji nchini. Asiruhusu siasa za upendeleo na upatilizaji. Sote ni wana wa nchi hii na tuko safarini ambayo mwisho wake hakuna ajuaye. Siasa si vita ya bunduki bali vita ya hoja. Tupingane na kutofautiana bila kukomoana wala kuumizana. Huu ni utamaduni tulioachiwa na baba wa taifa marehemu Julius Kambarage Nyerere ambaye wanyonge humuenzi kila siku bila kukoma hata kama walevi wa madaraka na mafisadi wanamkashfu na kumng’ong’a kwa kutenda tofauti na  haki na usawa wa binadamu visivyojali upinzani wala serikali tawala. Tufikie mahali tukomae kisiasa na kufanya vitu kama watu wazima na wenye akili.
            Mpendwa Lema, leo naishia hapa nikizidi kukuombea ushinde mtihani huu na kuvuka salama huku ukipiga moyo konde. Kwani yote yana mwisho. Haya ni mapito; na kila binadamu anayo mapito yake.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili jana.

Saturday 21 January 2017

Utabiri wa mwaka huu wa mlevi


            Baada ya matapeli wengi kurithi na kuibuka na utapeli uitwao utabiri, nami kwa nguvu ya kanywaji naamua kutabiri hasa ikizingatiwa kuwa hakuna chuo hata kimoja kinachofundisha kitu hii. Atakayedhani navamia ulaji wa wajanja anionyeshe cheti cha utabiri au uchungaji hata ushehe. Siku hizi kila kitu ni akili kichwani. Hamjaona mitume, wachunaji sorry wachungaji, hata manabii wa kujipachika wakiukata wakati nyinyi mnakatwa na ukata siyo? Acha nijitabirie huenda nikapata ujiko na kuwa karibu na wenye ulaji.  Hivyo ufuatao ni utabiri wa mwaka 2017 wa  Dokta, Profesa, Shehe, Alhaj, Mchunaji, Mchungaji, Maulana, Ustaadhi, Gwiji, Nguli Mlevi mwana wa Mchomajani, expert in astrology and astronomy, vitimbwology and blahblahlology.
            Kwanza, natabiri kuwa watabiri wengi wanaowatabiria wenzao mabaya watakufa au kuumbuka hasa ikizingatiwa kuwa waliyotabiri hatatokea au kutokea tofauti.
            Pili, natabiri kuwa rais John Kanywaji Makufuli hatapewa nishani yoyote kutoka nje zaidi ya walevi waliomchagua. Natabiri kuwa rais Kanywaji atazidi kupeta huku wengi wakizidi kumpa tafu kutokana na kuwaridhisha huku wachache wakimchukia kutokana kuwavurugia ulaji. Hata wale wanaojiona kuwa karibu naye, wengine watajikuta wakitupwa nje kama si kutumbuliwa baada ya madhambi yao kuanikwa hadharani.
            Tatu natabiri kuwa maisha yatazidi kuwa magumu huku mianya ya rushwa ikizidi kupunguzwa katika kujenga mazingira ya uimarikaji wa uchumi unaotegemea kazi na si ubabaishaji; pia walevi wengi wataokoka si kwa sababu ya kumcha God bali kukwepa makali ya ukapa na ukata. Pia vitendo vya ufuska, kujiuza na dhuluma vitaongezeka usawa huu na kusababisha mifarakano na kesi nyingi miongoni mwa walevi huku mji mmoja wa katikati ya kaya ukizidi kuchangamka na kupata wakazi wengi wenye njuluku.
            Nne, natabiri kuwa ubabe na undavaundava kwenye siasa za Bongo utaongezeka huku walioko nyuma yake wakizidi kufukuzana, kutumbuana na kupingana kama ilivyotokea kwenye kadhia ya umeme.
            Tano, natabiri kuwa wasanii wengi watazidi kuigiza kila upuuzi kutoka ng’ambo kama vile kutoga masikio, kujichota tattoos, kufuga vijibwa aina ya Chihuahua na upuuzi mwingine huku wengine wakizidi kudorora kisanaa. Wapo watakaopukutishwa na mibwimbwi na misifa huku wengeni wakipotea toka kwenye tasnia.
            Sita, natabiri kuwa litatokea tetemeko kayani litakalosababisha kiama cha mafisadi hata wale ambao hukuwategemea kutokana na uzito wa nyadhifa walizowahi kushika kayani.
            Saba, natabiri kuwa upingaji utazidi kutifuana na kuimarika taratibu ingawa hautaweza kuungana tokana na kushukiana, kuchuuzana hata kutaka kutumiana kama ambavyo imekuwa siku zote. Wale wanaosema baadhi ya vigogo wataramba matapishi yao ni waongo. Wanene waliotabiriwa kurejea wataendelea kung’ang’ania huko kama luba. Cha mno, upingaji utazidi kujipinga kwa kutetea yale uliyokuwa ukipinga hasa kuhusiana na ufisadi.
            Nane, natabiri  kuwa matapeli wa kidini wa ndani na nje ya kaya watazidi kuongezeka na wengi kuumbuka kama vile kukumbwa na kashfa za ulevi, ngono, kuigiza ulemavu na kujifanya wameomba na kupona; hata idadi ya wanaopwakia usanii wao itazidi kupungua huku serikali ikizidi kuwachunguza wengi kwa kujihusisha na biashara haramu ya bwimbwi na wizi wa sadaka. Wapo watakapofikia makufuru ya ajabu kama vile kutoza ada kwa sala ukiachia mbali wengine kujifanya wameparalyse na kujiombea na kupona wakati ni usanii mtupu.
            Tisa, natabiri kuwa biashara ya mihadarati itaongezeka huku wauzaji wakibadili mbinu. Hata hivyo, baadhi yao ima wataacha au kukamatwa ndani ya mwaka huu. Wapo wauza bwimbwi watakaokufa tokana na laana ya biashara hii haramu. Kuna wakubwa wengi wanaotumiwa na wauza bwimbwi wataumbuka na kutumbuliwa.
            Kumi, natabiri kuwa kiongozi mmoja king’ang’anizi na kikongwe kuliko wote atagombea tena urais na kuzidi kusababisha sintofahamu nchini humo au kufa kabla ya kugombea. Na hapa kaya mnene mmoja atatishia magazeti kutokana na kumnyima raha huku mengine yakifilisiwa kinamna kwa kunyimwa matangazo ukiachia mbali kuminywa kwa njuluku kiasi cha wachovu kuacha kununua magazeti. Hapa ndipo waandikaji wengi watajikuta wakitolewa sadaka na wamilkiji wa vyombo husika.
            Kumi na moja, natabiri kiongozi mmoja mkongwe wa upinzani kwenye kaya ya jirani atashinda urahis na kumuondoa mwana wa mfalme aliyeko kwenye ulaji.
 Kumi na mbili na mwisho,  najitabiria kuwa ujiko wangu utaongezeka kutokana na kutabiri mambo yanayotokea na si kujigonga kisiasa wala kurithi toka kwa dingi yangu kama wale wanaosifika kwa urongo na upuuzi.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.

Wednesday 18 January 2017

Go Jammeh go!




Go Yahya Jammeh go
Go Jammeh go ye Yahya
Go without turning thy head back ever
The game is up and over sir
Go son of hell, a coward in your own right
Go Jammeh go down cowing like a dolt
In flames go down like that
In a shame go even faster
Go, go Jammeh go, go
And others will go
Museveni will go
Obiang will also go
Sassou-Nguesso will go
Kabila will follow
Derby too will pack and go
Kagame will go
Bashir soon will go
I am sure many will go
Mugabe is on the go
However, he’s kept on hanging on
Afwerki will go
I am saying many will go
And, indeed, many will follow
Big trees will fall
And Africa will glow
Go Jammeh go


Go the way Compaore went
Mubarak was kicked out
Ben Ali is now the past
Go please; don’t lament
Go for this is your feat
Go leave the worst legacy back
Go like a goon and a stooge
Go the ignoble way go.
Go Jammeh go

Go Jammeh go
Go the world will remember you
Just as a symbol of megalomania
Please peacefully leave Gambia
History will record you
Just like a letdown extraordinaire
You are reaping what you sowed
This  is the rule
Go like a fool
Who abused the power of the presidency
Go with your decadency 
Organically as it will always be
He who live by the sword
He will die by the sword
Go dictator go
Go Jammeh go
It is time to go
Never look back go
Go Jammeh go
It is time to go.
Go from thy man-made no-go
Go go it’s time to go
Go go go go


Don’t turn back, just go!
Those that you treated like rats
They have used their votes
Even when threatened with bullets
History has it now intact
You treated Gambians like braggarts
Now you are but a rat
On a trap that it has been caught
Gambians have spoken
Jammeh you need to hearken
Wait your future in the prison
You wrongly thought you’re smart
My friend you are connered
Go Jammeh go.

Go Jammeh go
Don't go Idi Amin way
Do you want to go Gaddafi way?
I cn bet you are going the Gbagbo way
This means you will end up in jail
It depends on if you survive
You better be brave
Just make a  meaningful and peaceful move
Never wait for such a style
Go your friends will follow
Welcome Adama Barrow
As for Jammeh
Where will you go?
To the jail or to exile
Whatever you chose just do
Go Jammeh go
It is only to Zimbabwe you can go
Go Jammeh go
Go Jammeh go
Go go go!


Do you want to leave power in a coffin?
Why should you ignore the signs of time?
Will this give you a win?
Never waste any time
Jammeh your time is up
The game is over
Just pack up 
Pack up and jump
Hit the road my friend
Now way you can win this time
Go Jammeh go
It is your time to go
Go go and go

I congratulate Gambians
On your victory I salute you
For your courage I emulate you
For your unity I hail you
I challenge all Africans
Let’s take on our ruffians
Now Gambians have spoken
Their prison has been broken
Everybody needs to listen
Yes, we all need to learn
There a big lesson to be taken
The rest of Africa needs to learn
Let dictators pack and go
The way Jammeh is going
Unceremoniously he is going
Youths need to stand
They must take a strand
They need to emancipate their continent
The precedent Gambians have set
Indeed, will liberate our continent
Go join the Burkinabe
Let there peace be
And blessed be
Let there development be
Let the country move
Go rebuild your country
You have it back
Stand together as one