The Chant of Savant

Friday 30 July 2010

Mandela Not Eclipsing Other Luminaries







I read Sam Ditshego's article Mandela: Eclipsing Other Luminaries? with mixed feelings. His vitriolic intro: “This crazy thing about celebrating Mandela's birthday” did not augur well with me. It's totally discourteous of Mandela and those that venerate him. What would be his reactions if the celebration were about his father, queen of England or other colonial even religious monsters?

The author may be right about some issues but not all. Mandela is not eclipsing other luminaries as it was wrongly put. He is rightly where he is supposed to be. Even proposed Nkrumah (to be highly regarded as the father of African unification), did not do it alone. Tanzania has the late Mwl. Julius Nyerere the founder of our nation while Kenya has its Dedan Kimathi. They are highly regarded not just because they accomplished much single-handedly. They guided others just like Mandela. The general always gets credit for his army's victory. Giving them credit is not tantamount to eclipsing others.

Mandela is the only one who openly told the judge that he'd topple the apartheid regime. The judge was shocked for Mandela (as lawyer himself) knew the consequences of admitting to have committed such an offence whose sentence was capital punishment.

There is this issue of sell-out. This might be right or wrong altogether. Some South Africans are bitter given since the conditions of the majority blacks are still worse despite being free. But again, this is the reality almost everywhere in Africa. The economies of African countries have always been in the hands of foreigners that were brought by colonial masters. In Tanzania, Kenya and partly Uganda, all commerce is in the hands of Asians while in West Africa the situation is the same. The difference is that in South Africa, the citizenry hates foreigners from Africa whilst it is always in bed with the rest.

Looking at this situation I can concur with those that exhibit their anger against Mandela. But is it his fault or systemic fallacy? Before terming his efforts to reconcile South Africa as a sell-out, one should remember how shabby and complicated the situation - especially the well being of the black people - was at the time. What other alternative was at hand ? It is easier for the spectators to see what is going on in the pitch but more difficult for the players.

Is Mandela a tax evader? How, when the money given to Mandela foundations ends up being donated to the needy? Besides, Mandela does not manage the said foundations. His name is just used to help others. If his former friend and lawyer was right, can anybody tell us why the authorities did not apprehend Mandela?

I did not understand the allegation that intellectually, Nelson Mandela did not match Lembede, the founding President of the ANCYL in 1943; his deputy Mda and PAC founding President Mangaliso Robert Sobukwe. What does high IQ have to do here? Mahatma Gandhi, Mother Theresa of Calcutta and others were not that bright so to speak in terms of regurgitating what they were taught at school. However, they served and changed the society for the better. To the contrary, look at what “bright” butchers such as Rodovan Karadžić, Slobodan Milosevic and Charles Taylor did. Being bright did no good. Warren Buffet, Bill Gate and Carlos Slim may not be all that bright but this does not hamper us from appreciating their contributions to the development of human kind.

Mandela deserves kudos. What he started offers an opportunity for others to learn, go ahead and achieve impossible. He is a mortal being I know. But again, he rose above human languor when it comes to fighting for others. Had Mandela taken a backward stance, South Africa would still be languishing in the dark days the way Palestinians are simply because they cannot accept harmonious and constructive co-existence with Israel.

Boers had what it takes to soldier on killing, maltreating, segregating, exploiting and torturing blacks had Mandela not taken a conciliatory stance. Better half the misery instead of the whole misery. Mandela read the signs of times and thought outside the box. Had he fanatically rejected to reconcile south Africa, he'd have been the one to lose.

If Mandela sold you out, why don't you buy yourself back? South Africa is better than other sub- Saharan countries in almost everything despite the slow pace things are taking. Mandela is not eclipsing anybody. Being a towering-figure-cum icon, he deserves whatever he gets.
Source: The African Executive Magazine July 28, 2010

Thursday 29 July 2010

Ridhiwan Kikwete usikonde tuko nyuma yako




Bwana mdogo,
Naamini u mzima baada ya kuhangaika na kusaka wadhamini wa mzee nchi nzima.Haikuwa kazi nyepesi. Ni heshima na jukumu la pekee kwako na vijana wote wa taifa hili. Wote tuko nyuma yako na mzee.

Kudos kwa kufanya vitu vyako Yanga ambapo wabaya wetu wanasema umevurunda kwa kuweka mtu wako. Wanakuita kiji-rais kidogo simply because mzee ni rais. Wapuuzi hawa. Hawakujui siyo! Wamuulize Yusuf Masauni uliyemshuguhulikia baada ya kutishia ulaji wa mshikaji wetu Benno . Pia wanaweza kumuuliza Kifukwe uliyemnyima ulaji Yanga akaamua kususa na kundi lake ; kama urais wako ni wa kurahsisha hivyo.

Niliwahi kuwasiliana na mama yako wa kufikia kuhusiana na jinsi watu wanavyotusakama kwa kuwafagilieni. Leo nimeona ni bora kuwasiliana nawe wakati nikijiandaa kuwasiliana na mzee hapo baadaye.

Nimetumia njia hii tokana na kujua wazi kuwa ulipokuja kwetu Mbamba Bay kusaka wadhamini wa mzee sikupata nafasi ya kukuamkua na kukupa salama zangu za upendo wa dhati.

Niseme wazi. Mimi ni shabiki wako damu damu kiasi cha kuwa tayari kumwaga damu yangu kupambana na wale wanaokuonea wivu kwa ulaji unaoupata kutokana na kuzaliwa na kijiko cha dhahabu kwenye nasaba ya kifalme na mzee kukupigia vuvuzela ili hapo baadaye uule.

Kuna watu hawajipendi wala kulipenda taifa hili-wanaokusakama. Hawa ni maadui wa mshikamano na amani ambavyo mzee amevidumisha. Wanasema eti wewe na rafiki yako Januari Makamba ambaye pia ni msaidizi wa mzee mnabebwa. Hivi hawa watu wana akili kweli? Kuna ubaya gani wa mwana kubebwa na baba au mwana kumpigia ndogo ndogo mzee hata kuanza kujaribu kuvaa viatu vyake akiwa hai kama mnavyofanya?

Maadui hawa wa taifa wanakwenda mbali wanadai kuwa mama yako naye anatumia mgongo wa mzee kujineemesha! Hivi hawajui kutesa ni kwa zamu na, isitoshe, hakuna biashara inayoweza kufana bila kuwashirikisha wana familia? Wamesahau ahadi ya mzee ya maisha bora kwa wote yaani baba mama wana na maswahiba!

Eti kwa vile wewe ni mwanasheria, wangetaka uende kutoana jasho na mahakimu ukiwatetea wahalifu ilhali kuna ulaji wa dezo kwenye chama cha mzee! Hawa ni wapuuzi. Mwanangu usiwasikilize. Wakiendelea kukuzonga uwatolee uvivu na kuwapa: wawambie wazee wao wagombee urais waone utamu wake.

Mie sioni makosa yako wala ya mzee. Kwanini asifanye kama watangulizi wengine kama vile mzee Abeid Karume, Hassan Mwinyi, John Malecela, John Nchimbi, Yusuf Makamba na wengine ambao wamevitengenezea vitegemezi vyao ulaji wsa chee katika ngazi za juu?

Kwanini hawataki nawe uwe kama Daktari Hussein ambaye anatesa kutokana na mzee kumpa ulaji? Hawajui siku moja akiukwaa ukuu anaweza kukulipa fadhila kama ambavyo mzee alimlipa fadhila baba yake kwa kumtengeneza? Mzee kaona mbali.

Wasioona mbali wanataka awe kama wao. Mzee anajua: huko tuendako ulaji hautategemea uwezo wa mtu bali nasaba yake kama inavyoanza kujengeka. Huu ni mfumo mzuri tuliokopa toka kwa wahindi ambao wametutawala kiuchumi nchini. Bila hiyo wale watoto wa wakubwa waliotuhumiwa hata kughushi na kuanza kampeni mapema wangekuwa wameishachukuliwa hatua. Lakini ni nyani gani anaweza kumsulubu ngedere wakati wote wala mahindi?

Mfano, kuna kosa gani kwako kupewa kiwanja kwenye maeneo tulivu ya bahari kule Masaki au Mikocheni kama wengine? Kuna kosa gani, kwa mfano, kuwapa tafu washikaji zako kwa kumshauri mzee awape ulaji kama wanavyompakazia yule rafiki yako Lau wa Masha... wee koma, wa kampuni la IMMA.

Kabla sijasahau, naomba umpe salamu zangu Bro Miraji ambaye nilimuona juzi akiwa ametinga T-shirt yenye picha ya mzee iliyoandikwa 2010 ikimaanisha mwaka wa utukufu wa mzee, familia na maswahiba zake. Inapendeza sina mfano.

Kuna wajinga wanadhani kuwa wewe kupewa mikoba na mzee ni kutokana na kutoamini wana mitandao yake. Hawa wamenoa kweli kweli. Hawajui kuwa hata familia yaweza kuwa mtandao ukiachia mbali kupeana ujiko wa hapo baadaye! Wajinga kweli kweli.

Hawa hakika ni vipofu. Kwanini msomi aliyekubuhu kama wewe ujivunge ilhali huku mama ambaye elimu yake tuiache anatanua kwa kubuni mradi wa MAWAWA (Maulaji ya Wake za Wakubwa? Hawajui kuwa nawe una majukumu kwa ndugu na wazazi wako hasa bi mkubwa asiyeishi na dingi? Huu ndiyo wakati adhimu wa kuhomola na kutanua. Ukitaka kuona uzuri wa ushauri wangu, waulize watoto wa Che Nkapa hata bi mkubwa wake. Baada ya mzee kuachia ngazi hawasikiki wala kutanua kama walivyokuwa wakitanua wakati mzee akiwa high.

Japo watu wasiojua chess nzima wanamlaumu mzee kwa nepotism. Kwanza, hawajui kiingereza vizuri. Hawajui kuwa nepotism ni mfumo uliokubalika katika taifa letu kiasi cha kulikomboa kwa kuzalisha mashujaa wengi watokanao na damu takatifu. Bila nepotism Yesu kweli angekuja? Alikuja kwa sababu ya nepotism ya binadamu dhidi ya viumbe wengine. Hii tuiache ni falsafa kubwa iitwayo metaphilosophy.

Hata ule mradi wa mama yao wa Fursa kwa First Family and Friends (FFFF) hauna wachangiaji. Nani achangie watu wasio na mamlaka; ili apate nini? Wasio na busara wanaona kama ni upuuzi kwa mzee kuanza kukupa mikoba. Wanasahau kuwa kadri mambo yalivyo hasa kushukiana ufisadi atakapokuwa ameachia ngazi lazima awe na mtu wake jikoni kama alivyofanya mzee Ruxa.
Bila hiyo mizimu kama Loliondo hata IPTL yangemuandama hadi siku ya kufa. Huoni anavyoenziwa na kutanua kwa amani kana kwamba huko nyuma hakuacha waa?

Turejee kwa Mzee. Lazima adhaminiwe kuonyesha alivyo chaguo la Mungu na kipenzi cha watu. Anayebishia hili aangalia mabilioni aliyochangiwa hata na akina Matonya kutokana na kumzimia. Watakataa kumdhamini iwapo amekuza uchumi kiasi cha serikali kuwa tajiri kiasi cha kusamehe mabilioni ya EPA? Anayebishia hili aangalie misamaha ya kodi na pesa inayopotea kwenye ufisadi na serikali isishughulike nayo.

Nchi yetu sasa ni tajiri kiasi cha kushinda nchi zote za kiafrika kwa kununua na kugawa mashangingi. Rejea tukio la hivi karibuni huko Kilimanjaro ambapo afisa tawala wa mkoa huo Hilda Gondwe alijiuzia shangingi lenye thamani ya shilingi 155,000,000 kwa shilingi milioni sita tu. Kama si ishara ya utajiri wa serikali ni nini? Angalia serikali ilivyowagawia nyumba wakuu wake huku ikitenga mabilioni kujenga nyingine. Mifano ni mingi. Hebu jikumbushe jinsi urais wa Bongo ulivyo aghari. Unadhani urais wa 50,000,000,000 ni mchezo? Kama mtu mmoja anatumia kiasi hiki bila kugusia cha wabunge, huo umma una mafweza kiasi gani?

Angalia Dar Es Salaam ilivyopendeza kutokana na ile minara shufaa ya Balali na EPA na msongamano wa migari anayojisifia mzee hata kama inanyonga watu wetu hovyo. Uliza akina Kagoda wameishia wapi zaidi ya kuendelea kutesa na kupewa maulaji mengine.

Bwana mdogo, naona nisikuchoshe. Kaa ukiamini sisi vijana tunakuunga mkono na kukubali kuwa mrithi wa mzee hapo baadaye. Udumu mshikamano wa baba na mwana. Zidumu fikra za mzee kumtawaza mwana mapema. Walatini husema Noli prohicere maccaritas ad porcos yaani usitupe vito kwa nguruwe. Kadhalika nami naamini nimefanya kinyume.

Nifikishie salamu kwa mzee na hata bi mkubwa na swahiba yako Januari. Wambie tunaviona na kuvikubali vitu vyao hasa mafanikio ya MAWAWA na mradi wako wa wadhamini.

Salamu maalum kwa Januari. Mwambie kitabu chake juu ya ushambaa kimetushinda kutokana na kutumia lugha ngumu. Hivyo wapiga kura tuna shaka kama atatuelewa. Maana yeye ni wa wasomi na ikulu kusema ule ukweli.
Wako Kijana mwenzio akuungaye mikono na miguu,

Nkwazi Mhango pacha wa Mpayukaji Msemambovu , aka El Commandate
Mtandasi,
Mbamba Bay.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 28, 2010.

Uchaguzi ukiisha tegemea dikteta si Mkuu

Nawajua walevi. Hawajijui wala hawanijui vizuri. Na hawatajijua hadi yawakute zaidi ya haya ambayo yameishawakuta wasijifunze. Najua walevi watanichagua kwa kishindo wakidhani mambo yatabadilika wasijue ndiyo yanaanza! Nibadilike nini wakati hii ni lala salama? Anyway, nitabadilika na kuwa imla.

Kwa vile ni lala salama, watakapoanza kustuka mie nitakuwa nawaambieni laleni salama na hii ni ngwe ya lala salama.

Kwa vile nawajua walevi, ni wa hovyo. Sikuogopa kuwatahadhalisha baada ya kudharau tahadhali nyingi kuwa nitatoa makucha baada ya kuchaguliwa kwenye ngwe ya lala salama. Nimesema wazi. Nitawafunga wale wote wanaonikosoa achia mbali wanaonikandia na kufuatafuata ulaji wangu.

Wale wambea ambao kwenye kijiwe tunawaita wambea au magazeti wajiandae kukisikia kijiwe. Nitawakomesha ile mbaya. Nitawafungia kuingia na kutoa upuuzi wao kijiweni. Nitaruhusu wale wanaoniunga mkono na kunipigia debe tu huku wakijigonga kwangu.

Na mfahamu. Hii ndiyo fasheni kwa sasa. Hata mkuu wenu wa kaya ameishaonya kuwa akishaukwaa mjue mtakoma. Ule mchekea mliouzoea hasa wale ndugu zangu wa magazeti na wanaojiita wakereketwa wa dini fulani wakae mkao wa kuliwa. Hamkuona makucha yake pale Yanga alipomtumwa mwana kuwakomesha akina Kifukwe? Hamkuwaona akina Masahauni walivyosahaulika baada ya kugusa ulaji wa washikaji wa mwana? Kaeni mkizubaazubaa. Shauri yenu. Tusilaumiane.

Ametangaza rasmi kuwa baada ya uchaguzi yule Chekacheka mliyezoea kumuona atageuka kuwa Nunanuna huku akiwa amevimba kama nune. Wale ndata ambao hawakuwa na kazi ya kufanya kuwakata mitama wakosoaji sasa wakae mkao wa kula. Sipate picha jamaa atakapokuwa ameuvaa utunituni akiukimbia unjaa kaya itakuwaje? Au ndiyo maana amemnonesha bi mkubwa ili kufanya majaribio ya kutuna na kununa? Naona keshaanza kwa kuvaa miwani tinted ili asiwaonee aibu wala huruma wadanganyika watakaojipendekeza na kumpa kula zao wakidhani zitawaletea maisha bora badala ya maisha ya kiimla.

Anayebisha aangalie alivyowaminya wana nambari wahedi wakagwaya hata kumchalenji ukiachia mbali kuwaminya hadi kumchagia mshiko wa kununulia urahisi. Hakuna uimla mbaya zaidi ya huu tena unaofanywa chini ya kivuli cha domoghasia muitayo demokrasia. Kitaalamu huu huitwa uhuni wa kisiasa wenye kisasi cha kihuni.

Watakaotaka kuula waanzishe mkakati mchafu kama ule wa SHIHATAI wa kutaka kumsafisha Ewassa ili hapo baadaye ajaribu kumrithi mkuu. Hamkuona mkakati ulivyoanza kuiva kwa kumwengua daktari wa Kushaini na kumuweka mgonjwa aitwaye Ughaibuni Bilhali? Shauri yenu. Kama hamnielewi basi endeleeni kuingizwa mkengeni kwa mara nyingine.

Wasiishie hapo. Lazima wajipendekeze pendekeze kwa mkuu ukiachia mbali kuishi kwa kutegemea mtandao wa mafisadi wakiongozwa na baba lao.

Nani alijua kuwa fisadi kama Ewassa angepata ithibati ya kuhojiwa na yule jamaa aitwaye Mtindo Mwando ambaye naye ameanza kuishiwa? Ajabu ya maajabu eti akina Mwando na kundi lake wanataka kumfufua maiti? Hata ahojiwe uchi Ewassa hawezi kuwa mkuu wa kaya hata kwa sekunde moja. Anaweza kutuuza na makaburi yetu kwa uroho na ufisi wake.

Bila aibu linasema eti lilionewa wakati liliinea kaya kwa kuchota njuluku. Eti linasema ni clean yaani halina kinyongo. Kwanini halisemi liko clean kwenye ufisadi?

Kaya hii kweli Danganyika ya wadanganyika! Kesho utasikia majambazi mengine kama Roasttamu, Jose Mainji, Jeff Sambodo yule aliyewahonga chakudema pesa ya ufisadi nayo yakija kuhojiwa ili yasafishike. Kusuru wa kusumu.

Kabla ya kuendelea ngoja kwanza niwamegee kituko. Una habari; baada ya kumkaripia Sofi fyatu wa lion kutokana na kuwaambia wake zetu watunyime nonihino wana Sisiemu wamefyatuka hadi gabacholi mmoja kujiamini na kutoa mshiko wa mamilioni kwa Chakudema? Huyu haogopi mke wake kumnyima nonihino kwa sababu mama wa kigabacholi si limbukeni kama wa kiswahili.Haya tuyaache.

Hata hivyo wengi wanasema sasa Chakudema sasa imeanza kudema kwenye nyavu za mafisadi hasa pale itakapoumbiliwa na jamaa kama alivyowafanyia akina Jose Butuka. Inashangaza kuona akina daktari Silaha waliofichua ufisadi wote wasimuulize gabacholi kama mshiko wake ni safi au matokeo ya ufisadi wake na maswahiba zake akina Joseph Mainji na magabacholi wengine walioshikilia uchumi wa kaya!

Sisi wakubwa unajua: si majuha. Tuna sifa kama ya yule mwarabu na ngamia wake tunapokuwa tunasaka ulaji. Huwa warahimu kama ua na wakarimu kama vyangu. Tukishawatwisha mkenge hugeuka kuwa makenge kweli kweli. Ukitaka kujua ubaya wa kenge jaribu kuigiza mambo yake. Yeye akiona mvua inanyesha anatimkia ziwani, mtoni hata baharini kuikwepa mvua. Ukimshambulia anakuumiza na mkia wake bila kujali kuwa naye anaweza kuumia!

Nasi kadhalika. Unapojifanya unajua kutusakama tunakugeuzia kibao. Badala ya sisi kuonekana makosa yetu, wewe unaonekana mchochezi hata kama unacholonga ni ukweli mtupu.

Nimewapania waleta fujo wanaotaka kuvuruga amani kijiweni. Yaani wao wanahanikiza kuzuia watu tusihomole wasijue wanavunja amani ya kijiwe! Nani aliwambia kuwa mali ya umma inauma? Sasa kelele za nini tunapouma pesa ya umma wa walevi? Ukitaka nawe njoo ule. Ni kuamua kujitoa kimasomaso na kugombea ulaji au kujipendekeza kwetu sisi tulio na mamlaka na unakatiwa chochote kitu unatuliza njaa zako badala ya kututilia kitumbua mchanga.

Kama mkuu ngwe hii ya lala salama sitamvumilia mtu hata awe anasimamia ukweli kiasi gani. Najua kipindi kilichopita sikuchukua hatua yeyote kutokana na kuwazunga walevi wauingie mkenge upya kwa kunichagua. Sasa ngoja waukwae halafu watajua kama mimi ni bingwa wa sanaa au longo longo.

Kama mkuu, nitaanza kumpiga mwanangu Kidume vuvuzela ili hapa baadaye agombee ulaji kama Jan wa mgosi Makambale ambeye anawania jimbo la Umbuji.

Bi mkubwa nshamwambie azidishe juhudi kukusanya mshiko kwenye NGO yake ya MAWAWA ili hapo baadaye tusiumbuke wala kulaumiana. Lazima anunue mijumba chekwa kama Anna Tamaa wa Tunituni. Hii ni ngwe ya kukomba si kuhomola tena. Nataka mkuu wa kijiwe ajaye asikute akiba hata chembe. Nataka akianza naye aanze kivyake vyake ingawa wakati mimi naanza nilikuta njuluku jaalo.

Kuhusu mkakati wa kupambana na wanywanywa, kwanza niseme wazi. Ulianza zamani. Kuna watu tuwaitao magazeti kijiweni nshawalambisha kunisifia hata nipaswapo kupigwa mawe. Hamjawasikia? Yupo Tazama bin Rai na wengine wengi wanaofanya kazi hii ambayo wabaya wangu huiita unepi.

Leo sichongi sana. Nakwenda kusoma vitabu vya akina Idd Amin, Mobutu Seseseko, M7, Marcos, Causescu, Suharto na wengine ili kujua siri ya uimla wao.

Naona mindata inakuja. Kwa vile jamaa keshatangaza wazi atatufiligisa kiimla, acha nitimke yasije yakaanza nami.
Kulaleki tumekwisha.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 28, 2010.

Monday 26 July 2010

Lowassa anataka kumdanganya nani?


Hivi karibuni watanzania walishuhudia mbinu mfu za kutaka kumrejesha aliyekuwa waziri mkuu aliyefurushwa na kashfa ya Richmond, Edward Lowassa zikianza kufanya kazi.

Tenda hii chafu ilikabidhiwa kwa Shirika la Habari Tanzania (TBC) chini ya mkuu wake Tido Mhando ambaye alimuandalia kipindi cha kujisifia na kujisafisha asifue dafu .

Pamoja na lengo zima kuwa kumjengea mazingira ya kumrejesha Lowassa kwenye hadhira kiasi cha baadaye kuzoeleka na kushiriki kwenye siasa za kitaifa, walioandaa mkakati huu na Lowassa mwenyewe walikurupuka.

Hata ukiangalia maneno ya Lowassa hayamjengi zaidi ya kumbomoa. Na kazi hiyo akiifanya mwenyewe kwa mbinu na kinywa chake.

Hebu tutoe nukuu hii halafu tuifanyie uchambuzi. “Mimi si mtu wa kukaa ofisini na kungoja nifungue mafaili. Linapokuja suala la kulishughulikia sihofii kufanya makosa ninapoamua ku-push (kulisukuma) jambo.”

Sasa kama Lowassa yuko tayari kufanya makosa ili kusukuma jambo ana jipya gani la kutufanyia zaidi ya kufanya makosa?

Maneno haya ni ushahidi tosha kuwa alipokuwa akisukuma watendaji watekeleze maslahi yake binafsi kwenye kashfa ya Richmond hakuogopa matokeo. Ndiyo maana ilikuwa rahisi kwake kubwaga manyanga baada ya shinikizo la kutaka aachie ngazi kutolewa.

Na kwa maneno haya Lowassa hana haja ya kuilaumu kamati teule ya Bunge iliyompata na hatia eti kwa kumnyima fursa ya kujitetea wakati walitoa taarifa kuwa kila mtuhumiwa anaweza kufika mbele ya kamati wakati wowote na Lowassa hakufanya hivyo kutokana na sababu alizojua mwenyewe. Ajilaumu mwenyewe na ku-push bila kuogopa consequences.

Kitu kingine hasa kilichonisukuma kuandika makala hii ni ile hali ya Lowassa kujigamba kuwa ana rekodi nzuri kikazi mahali pote alipofanya kazi jambo ambalo si kweli. Kama Lowassa angekuwa ni mkweli na ana rekodi nzuri mwaka 1995 baba wa taifa marehemu Mwl. Julius Nyerere asingemzuia kugombea urais.

Tumkumbushe chanzo cha ugomvi wake na mwalimu. Ugomvi wa wawili hawa ulianza pale Lowassa alipokodisha ndege kwenda kuchukua fomu za kugombea urais Dodoma akampa lifti mgombea mwingine wakati ule, Jakaya Kikwete kitendo ambacho kwa mwalimu kilikuwa na tafsiri mbili.

Mosi, kuthibitisha uvumi kuwa Lowassa amejilimbikizia mali nyingi ambayo haina, hajawahi na hayuko tayari kuitolea maelezo. Huu ni ushahidi fika wa ufisadi na kutokuwa muaminifu kama ilivyokuja kuthibitishwa na kashfa ya Richmond anayojitahidi kuikwepa na kuirahisisha.

Pili, jambo hili pia lilitafsiriwa na mwalimu kama utoto kwa Kikwete kujihusisha na mtu wa aina ya Lowassa. Ndiyo maana alisema kuwa Kikwete hakuwa amekomaa kuwa rais kama alivyokuja kuthibitisha hata baada ya kupita miaka kumi. Hapa ndipo urafiki wa Kikwete na Lowassa ulipochimbuka hasa kujulikana kwa umma. Ni urafiki huu huu wa mashaka kama mwalimu alivyoutilia shaka. Na bila kujibu tuhuma hizi Lowassa atamaliza waganga na dawa wala nafuu hatapata. Maana laana ya marehemu huwa si rahisi kuikwepa wala kuifutu hata ajidanganye na urafiki wake na Kikwete ambao umegeuka mzigo kwake, Kikwete na taifa.

Ni vizuri Lowassa akakubaliana na ukweli na hali halisi hata kama ni kidonge kichungu kuwa wakati huu ambapo ufisadi umegeuka sera kiasi cha kuzidi kuwaumiza na kuwachukiza watanzania walio wengi, maneno ya mwalimu yanazidi kupata ithibati kuliko hata wakati ule alipoyatamka akiwa hai.

Na isitoshe kwa kujiuzulu kwa hiari yake ni kukiri kuwa shutuma zilizokuwa zikimkabili zina ukweli. Ingekuwa mahakamani asingeruhusiwa kukata rufaa kama anavyofanya sasa.

Hata kuwa wa kwanza. Akitaka kujua ninachomaanisha, aangalie watu kama John Malecela aliowagomea kuwania urais walivyojaribu na kushindwa hata baada ya mwalimu kutoweka. Na Lowassa ataishia kama Malecela atake asitake. Na dawa ya hili ni kukubaliana na ukweli badala ya kujidanganya na kuudanganya umma.

Watanzania bado wanakumbuka athari za ufisadi wa Richmond ambapo waliwekwa kizani kwa mwaka mzima ili kushinikiza mitambo yake inunuliwe. Wanakumbuka bado jinsi umeme unavyozidi kuwa aghali kutokana na kulanguliwa ili kufidia hasara zitokanazo na uchafu kama Richmond.

Pia madai kuwa chochoko choko zote za kuifukua Richmond yalilenga kumpokonya uwaziri mkuu Lowassa ni uongo. Ingekuwa hivyo basi mawaziri wengine waliojiuzulu na wengine kupanguliwa wasingefanya hivyo maana aliyekuwa akitafutwa ni yeye. Hebu soma maneno yake:“Bado naamini tatizo lilikuwa ni uwaziri mkuu. Waziri Mkuu si mtu wa kusaini mkataba, ni mtu wa kusukuma...ile kamati (teule) ilikuwa na fedha nyingi, sijui ilitumia kiasi gani, kwani walisafiri hadi Marekani kuwahoji watu halafu hawakuja kabisa kunihoji...bado naamini kamati teule ilifanya makosa.”

Lowassa kimsingi anatapatapa. Kama anaamini na aliamini kuwa kamati ile ilifanya makosa basi asingeachia ngazi. Angeionyesha makosa na kutumia ukweli huo kuendelea kuwa madarakani. Anachofanya Lowassa licha ya kutokuwa saizi yake ni kulidhalilisha bunge, kamati yake na kulitukana taifa akitetea maslahi yake binafsi. Aambiwe ukweli kuwa muda wa kujadili kurejea kwake kwa mara ya pili ulikwishapita na hatafanikiwa hata afanyeje.

Na kuonyesha ukweli huu unaweza kurejea maneno ya Lowassa mwenyewe kuonyesha anavyojidanganya na kuwadanganya wengine. Alipoulizwa atafanya nini, alijibu “Nafsini mwangu I’m clean (sina kinyongo) mimi naiacha historia iwahukumu kwa haki.”

Lakini ukirejea maneno ya kuwa hakutendewa haki na tume ilikosea, Lowassa hana kinyongo tu bali hata ngoa na unywanywa. Na kwa kuzingatia haya ndiyo unaona jinsi Lowassa anavyotapatapa na kulipiza visasi. Hasemi yu safi kuhusiana na kashfa bali moyoni. Je uchafu wake wa Richmond mbona hakutaka kuuongelea?

Japo amejitahidi kuwashutumu waandishi wa habari na kuwaonyesha kama watu ambao hawana elimu ya kutosha, bado Lowassa huyu huyu anawatumia waandishi tena makanjanja kuwachafua wenzake hasa wale waliokuwa kwenye tume ya Mwakyembe au waliounga mkono hoja ya kuwajibishwa. Kuna magazeti yanajulikana na waandishi wake tena wasio na hata hicho cheti cha uandishi wa habari kama wale wa Tazama.

Dokezo la mwisho ni kwamba ukiondoa mwl. Nyerere, hakuna waziri mkuu aliyewahi kuwa rais. Hii ni kutokana na kupewa madaraka haya makubwa na kuonyesha utendaji wao kiasi cha kuwaachia wengine nao waongoze. Rejea harakati za kina Joseph Warioba, Cleopa Msuya, Salim Ahmed Salim, John Malecela na Fredrick Sumaye. Lowassa ni nani na ana nini ukiachia mbali kufanya nini zaidi ya kuliingiza taifa kwenye kiza na hasara? Anadhani tumesahau? Thubutu!

Pamoja na wanasiasa wetu kutuchukulia kama watoto hata mataahira, kuna mambo mengine hayawezekani. Haiwezekani kufufua maiti katika karne hii hata kama aliyekufa alikuwa rafiki wa Kaisari. Ni vigumu kwa Lowassa kurejea kwenye uongozi wa juu. Kama inawezekana basi na Liyumba anaweza kuteuliwa kuwa gavana wa benki kuu aliyoihujumu na kuiibia. Je inawezekana? Heri kuota usiku kuliko mchana. Tusipoteze muda kujadili jinsi ya kufufua maiti.
Chanzo: Dira ya Tanzania Julai 26, 2010

Friday 23 July 2010

African has nary been truly independent

With disbelief and shock, I should admit. I read Bill Rolls' views (July 16 Echo). I didn't know Canada, sadly though, still has people like him with such a frozen take of things. His burning anger was obvious. He felt attacked simply because his symbol was touched negatively! Wow! Though everybody is entitled to his belief, freedom of expression and what not, his was archaic and colonial mentality and ignorance about Africa. He impliedly wanted me to show him one country south of the Sahara whose people are better in freedom than they were under colonialism. It is sad, once again, to ask such ridiculous question. For the person that correctly knows the history/situation Africa is in, such a question is irrelevant and a sheer justification of ignorance. Yeah, we acquired 'independence' in the sixties. But was it true independence really?

Mr. Rolls does not get it. Let me open his eyes. When he drinks coffee, he should understand that farmers producing it in Africa are paid just a dime thanks to a conspiracy by rich countries to reap where they did not sow. When he uses his laptop, he should understand people where the parts are mined are killed everyday to make it easier to plunder and sell at a throw-away price whereby the buyers are the western countries.

For your information Africa has never been truly independent thanks to being manned by western nursed black colonialists. Thanks for mentioning Zimbabwe whose tin-pot dictator was cloned by the same Britain that is against him currently after Joshua Nkomo who was supposed to be the first leader declined to protect their rotten interests. Thanks for bringing Nigeria whose thuggish rulers stashed billions of dollar in banks in Switzerland, U.S., Britain and elsewhere in the western world. Even current terrorists like Osama bin Laden are the creation of west. What's more, stinking dictators such as Idd Amin (Uganda), Hastings Kamuzu Banda (Malawi), Ian Smith (Zimbabwe) were supported by the same Britain when they toppled their governments or came to power for the sin of opposing capitalism as they embraced socialism (those whose freedom fighters allied with the east by then).

If Mr. Rolls and the likes do not want to know and appreciate that many tiny European countries are rich thanks to plundering Africa, history is a meaningless thing. Belgium has no minerals. But it is rich thanks to plundering DRC. I'd recommend that Mr. Rolls and the likes get copies of How Europe Underdeveloped Africa by Walter Rodney or No More Lies About Africa by Mussamaali Nangoli among other titles.

I know there are many people with backward thinking of this type almost everywhere in western world. I know they were nursed and mentored under better-than-thou philosophy. If they like to labour under colonialism as individuals, that's their personal business and so be it. The way the son or daughter of colonial master feels is different from those whose countries were colonized.

This is evidenced in the words of Mr. Rolls who lampoons me that if I fled Africa to escape colonial oppression now it is better for me to go back especially to Nigeria and Zimbabwe! Africa has always been under colonial yolk whereby the show is, by proxy, done by African stooges that conspire with rich countries to rob, plunder and ruin Africa. I should remind him what the CIA did in the current DRC-Africa mineral super power. It killed its first leader simply because he was not ready to betray his people by protecting their vested interests. And let me ask, if what I expound is wrong, why do rich countries give African do-nothing governments money to run their business especially their budgets?

I don't want to turn this page into a debating club. I thus should humbly avoid making a missive by submitting that it is better to hide one's ignorance and exhibit his knowledge.

As for the alternative, Canada should become a republic.

In a nutshell, I am here to stay. Canada is my country; the country of immigrants.
Source: The Red River Valley Echo July 23, 2010.

Wednesday 21 July 2010

Al-Shabaab: Museveni Needs Allies

Museveni has vowed to crush al-Shabaab


The recent terrorist attacks in Kampala Uganda have given Ugandan strongman a big boost. It is sad that the Somalia-based terrorist group succeeded once again to make a point in the July 11 twin-attacks in Kyadondo and Kabalagala that claimed over 70 lives.

Given that Museveni for long has always avoided to state when he would step down, he now has something to tell Ugandans. He will ask for more time to thwart Al-Shabaab.

To avoid this abuse of democracy, Africa should devise means to neutralize Al-Shabaab quickly. The war against Al-Shabaab should not be left to Uganda and Burundi alone. The African Union needs support to see to it that Somalia gets a functional government. Instead of sending peace keeping forces, we must send liberation forces and anti-terrorism squads whose mandate should include combating piracy, drug peddling and arms peddling, a hallmark of groups like Al-Qaeda and Taliban.

Somalia is suffering and bleeding to death as far as abuses of human rights are concerned. Refer to the recent edict that all men in the area controlled by Islamic fundamentalists should grow beards within 30 days. Women are not allowed to wear bras. Schools are not allowed to use bells. People were barred from watching the just ended FIFA World Cup matches in South Africa.

Terrorist groups can be stopped. Refer to what happened in 1978 when Tanzania took on Uganda’s Idi Amin. Many at the time thought it was day dreaming to take on such a boisterous dictator. Tanzania did it and left many people relieved.

We should not allow a replay of the 1998 terrorist bombings in Dar es Salaam and Nairobi when Al-Qaeda attacked and got away with it. We must educate our people who support those groups wrongly thinking they are fighting for Islam. True Islam has nothing to do with terrorism.

Given that Burundi, Kenya and Uganda belong to East African Community, when any or one of them is attacked, all the countries in the region are attacked. This means, the war Museveni promised to launch on Al-Shabaab is the war of the whole region so to speak.

All countries in the region must step up efforts to secure their borders. All suspicious persons from Somalia should be kept under surveillance and their business activities scrutinized. Even the movements of people from Somalia should be restricted and highly regulated for the good of the neighbours.

Rich countries and United Nation Security Council should act decisively to empower countries that are ready to take on Al-Shabaab and act with the same seriouness the US and its allies are showing in Afghanistan.

If this war is left to Museveni alone, Ugandans will pay dearly. Museveni will capitalize in the same to remain in power. But if Al-Shabaab is flushed out timely and quickly, Museveni won't have any reason to cheat Ugandans to remain in power as opposed to the constitution he has already tampered with.

What's more, probing all businesses supervised by suspects, sympathizers, conspirators, and agents needs international cooperation. Investigating the sources of incomes for these groups begs for international solidarity and cooperation. Another thing is to see to it that sanctions are applied to all countries, companies supporting these groups.

Rich countries should fully support African countries to amass African peace keeping forces that should also have full mandate to engage directly with those terrorist groups in the front line. For Museveni, his vows are good if the aim is to stamp out Al-Shabaab. This good motive will end up cropper shall Museveni take the whole issue personally and extend his rule. Uganda can still stand and fight even without Museveni. For what is needed to fight Al-Shabaab is not one person but the country's commitment to its security and prosperity.
Source: The African Executive Magazine July 21, 2010.

Karibu soko la pamoja tuchanganyikiwe


RAFIKI zangu kule Karatu walikuwa wanauliza eti soko la pamoja la Afrika Mashariki limejengwa wapi?

Wambie ni kwenye vichwa vyao. Wakisema mbona hawalihisi, wambie watalihisi tu ni suala na muda tu. Wambie wasiwe na haraka neema zake wataziona ambapo watakuwa na watumishi karibu kila aina kutoka Kenya na Rwanda.

Usishangae na genocide na genocide philosophy vikawamo kwenye soko bila kusahau wembule toka kwa M7 ambaye atauza demokrasia ya mwituni na jinsi ya kutawala kifamilia akisaidia kuongeza soko hii ya Njaa kaya.

Poleni sana kwa kuchanganyikana na nyang'au na wanyonya damu. Mtanyolewa bila maji na mjute. Mie simo. Kwani si juha mie ati!

Bila shaka kwenye soko hili lazima bidhaa ya Philip Onyancha yule mnyonya damu maarufu wa dhehebu la waabudu shetani (Devil worshipper's cult) itakuwapo.

Akina dada poa au changu wa Bongo nao wajiandae kwa ushindani. Kutojua Kiingereza kutawatupa nje ya soko la pamoja. Mambo ya look my milk is standing hayana nafasi hapa tena.

Hapa sijagusia washitakiwa kuwa wabongo ikizingatiwa kuwa hivi karibuni walihusishwa kwenye jaribio la kumuua mkuu wa zamani wa majeshi ya Rwanda, Luteni Jenerali Nyamwasa Kayumba kule sauzi.

Hapa bado hujagusia mibomu, bunduki na mashine za kutungulia madege toka Somalia, bila kusahau wawekezaji toka huko ambao wengi watakuwa maharamia bila shaka.

Pale Rwanda wamejiandaa kutuletea ile bidhaa maarufu ya kufungia wanywanywa ukiachia mbali kuwafuata waliokimbilia nje na kuwamiminia risasi kabla ya Burundi kuja mgombea mmoja kwenye uchaguzi.

Tusishangae siku moja kuona ndege ya bwana mkubwa ikitupiwa mawe kama si makombora kutoka Somalia. Hamkuona AL-Shabaab walivyoingiza bidhaa zao Kampala kwenye kilele cha Kombe la Dunia?

Wale wezi wa benki sasa wanaweza kufanya biashara watakavyo, kwani bidhaa yao inahitajika kwenye soko jipya. Walimu feki na wengine hao ndiyo sisemi.

Academia na Internationals zetu zitajaa hadi zifurike huku ujinga ukizidi kufirika vichwani baada ya mifuko kupakuliwa na kubakia mitupu kwa kulipia upuuzi huu.

Kwa wale wabongo ambao biashara yao ya ngozi na mifupa ya zeruzeru ilikuwa imedoda jiandae kusafirisha nje hasa kwa wale wanyonya damu pale Nairoberry.

Unyakuzi wa ardhi nao ndiyo usiseme. Hamkuwaona akina Londi walivyohomola pale? Huu ni mwanzo tu. Ni biashara itakayolipa sana kiasi cha kufanya watu mabilionea ingawa watakuwa si wabongo.

Hapa hujagusia ile sumu hatari iitwayo njonjoison ambayo ilidodesha soko la kwanza lililokufa mwaka 1977.

Wabongo mmeambiwa na wakubwa wenu msikonde. Hili soko ni mali kwenu. Ni kweli. Msishangae kesho mkakalibisha katiba mpya ili kuchukua nafasi ya hii viraka mliyo nayo ukiachia mbali kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa kama Kenya.

Najua mna ardhi mnayokalia bila kutumia. Japo wakubwa zenu wamewatahadharisha kutouza ardhi kwa wageni, mnaweza mkauza tu. Kwani kilichobaki nini iwapo nanyi mmeuzwa kwenye soko la pamoja?

Kwanza, mna bahati. Hamna ongezeko kubwa la watu wala watu wasio na ardhi kama jamaa zangu pale Murang’a na Kibuye bila kusahau kule Ngozi na Bugenyuzi.

Kinachokera ni ukweli kuwa wakati jamaa hawa wasio na ardhi wakimwagwa kwenu, ardhi yao imekaliwa na watu wala wachache na wageni!

Ndugu zangu kina Aterere, Omera na Mulembe pale Kenya mtegemee kununua bidhaa iitwayo EPA, Richmonduli hata Kagoda.

Bahati mbaya sana kwenu ni kwamba wenye jeuri ya kununua bidhaa hizi ni wala watu wenu muwaitao watawala!

Bila shaka hapa mtabadilishana na ile bidhaa maarufu iitwayo Kibaki Toka, yaani kujiapisha usiku baada ya kuiba sorry kuchukua kura za Jaduong Maduong Odinga mwana wa Amoro. Hamjasikia fununu kuwa Zenj imeishaanza maandalizi ya kutumia bidhaa hii kwa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa ulioanzishwa kwa shinikizo la The Hague kwa kina Ocampo? Maendeleo hayo na mema ya soko holela la pamoja.

Japo wabongo wamelazimishwa kuingia kwenye soko hili na kuachwa kwenye mataa, hawana haja ya kuchukia. Watafurahi tu watakaposhuhudia utitiri wa wasasi wa dili baada ya kuchoshwa na wale wa kihindi. Hapa mitandao ya dili itapanuka.

Msishangae kuwaona jamaa zangu wenye mamlaka wakiagiza Goldenberg toka Kenya huku waganda wakituuzia imla wao atawale soko hili.

Bongo mama mkarimu ana mengi ya kutoa. Jamaa zangu kule Kaspul Kabondo, Nyakach, Emuhaya, Ithekahuno, Wajir, Mutito, Matuu hadi Wote bila kusahau Cyangungu, Ruhengeri, Murindi, Rwimpasha hata Bugarama msikonde. Kuna bidhaa iitwayo mauaji ya vikongwe kwa imani za uchawi.

Hata wale jamaa zangu wa Bubanza, Bururi, Bwiza, Ngozi hata Apuk apar, Bunyaruguru, Soroti, Tororo, Lira na Mbale hamtaachwa nyuma.

Hapa bado hatujaongelea madini bwerere ya Bongo kama vile gold, tanzanite, almasi hata uranium kwa kina Kony kuwalipua wabaya wao, ukiachia mbali kutangazwa yanapatikana toka kwenye jamaa zangu wa unyakuzi wa kila kitu yaani man eat man and everything. Hapa bila shaka watapata ushindani mkali toka kwa jamaa zangu wa fisadi eat everything.

Dzipapa! Dzipapa! Lamkani kudzecha. Yaani papa papa amkeni kumekucha! Ndugu zangu wa kule Shika Adabu, udigoni na udurumani kwa ujumla tunaelewana nadhani.

Hakuna cha soko holela wala huria wala la hela kwenye kijiwe cha mzee Mpayukaji chaguo la Mungu na kipenzi cha walevi. Aaamin.

Mpayukaji (El Commandante)
Chanzo: Tanzania Daima Julai 21, 2010.

CHADEMA kuweni makini na akina Sabodo



Wagiriki husema: "Timeo dona ferentis" au “Timeo Danaos et dona ferentes. “waogope wale (wagiriki) hata waje na zawadi.” Kitendo kilichotangazwa na vyombo vya habari, kwa sana, hivi karibuni baada ya mwana CCM Jaffar Sabodo kuipa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) msaada wa shilingi 100,000,000 huku akiwa ni mfadhili na mkereketwa wa CCM, kilinikumbusha wosia huu wa kigiriki.


Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman alikaririwa akimshukuru mfadhili huyu mpya. Kusaidia au kusaidiwa si jambo baya kama anayefanya hivyo ana udhu na anafanya hivyo kwa nia nzuri. Alisema: “Kwa kweli tunashukuru sana hii ni historia mpya katika siasa za vyama vingi nchini, ni wajibu wa wafanyabiashara wakubwa kuona umuhimu wa kusaidia vyama vyote makini nchini bila ubaguzi wala woga, mzee umeonyesha njia naamini itakuwa ni mfano kwa wengine wenye uwezo.”

Ndege kaunasa mtego hapa. Huwezi ukawatumikia mabwana wawili. Wazungu husema either you be grass eater or meat eater in this game.

Kilichonisukuma kujenga shaka juu ya msaada huu ni ukweli kuwa sikusikia sehemu yoyote CHADEMA wakiulizia usafi wa mtoaji ukiachia mbali historia yake kujulikana vilivyo hasa alipowashambuliwa wazee maarufu wa CCM baada ya kumkosoa rais Jakaya Kikwete kuwa hachukui maamuzi magumu. Hii ni baada ya kumuona yuko kitanda kimoja na mafisadi.

Hivyo basi, kwa moyo huu wa mwenyekiti kushukuru na kupokea bila kuuliza, sitashangaa kusikia akina Kagoda nao wakichangia kiasi cha upinzani wa Tanzania kugeuka kama ule wa Kenya kutokana na tamaa ya kuchuma.

Kuepuka kujidhalilisha na kudhalilishwa kwa viongozi na vyama vyao, kuna haja ya serikali kugharimia uendeshaji wa vyama husika. Mbona tuna pesa ya kusamehe kodi ukiachia mbali kuwaacha mafisadi na matapeli waliojificha nyuma ya wakubwa kutoweka na pesa yetu? Mbona tuna pesa ya kuchezea kwenye ziara nje tena zisizo na ulazimu wala tija?

Kwanini watu binafsi, tena wanaobebwa na serikali kupata hizo pesa zao chafu, waweze kuvisaidia vyama na serikali isiviendeshe kifedha kwa mujibu wa sheria?

Tuwakumbushe CHADEMA. Sabodo huyu aliacha kizaazaa alipoishutumu taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) kuwa ilifanyia ubadhilifu pesa aliyoipa kama msaada. Baadaye ilikuja kugundulika vinginevyo na mhusika wala hakukanusha zaidi ya kuficha uso wake na kutokea CHADEMA sasa. Je CHADEMA wamejihakikishia vipi kuwa hatawafanyia mchezo huu kutokana na kuwa karibu sana na uongozi wa sasa ambao CHADEMA pekee kwenye upinzani imeujeruhi sana kwa kufichua uchafu wake mwingi kuanzia EPA, Richmond, Deep Green Finance na mwingine mwingi?

Is CHADEMA going to hell in a handbasket? Smahani kuchanganya kiingereza na kiswahili. Najaribu kufikisha ujumbe na onyo langu.

Kwa wanaojua wafanyabiashara wengi walivyo tegemezi na wafadhili kwa CCM, atashangaa hii jeuri ya Sabodo inatoka wapi bila baraka za chama chake!

Maana si siri. Kama alivyowahi kupayuka (kutokana na kujisahau) waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye kuwa bila kujiunga na CCM, hakuna mfanyabiashara au mtu yeyote angeweza kufanya mambo yake yanyoke. Tumeona wengi waliokuwa wamekaribia kufa kiuchumi kama Thomas Ngawaiya, Augustine Mrema, Masumbuko Lamwai, Warid Kaboro, Tambwe Hiza wakijirejesha huko ili wanusurike ukapa.

Swali analopaswa kujiuliza kila mwenye nazo na mapenzi na CHADEMA, ni kwanini CCM inaweza kumuacha Sabodo awaunge wapinzani wake mkono wakati wao wakiwapatiliza kama hakuna namna?

Kwa faida zaidi, wanaodhani huu ni wasi wasi tu wajiulize ni kwanini mfanyabiashara tena mwenye udhu Bakhresa alipokisaidia chama cha wananachi (CUF), CCM na serikali yake walianza kumhujumu kiasi cha kutaka kuangusha biashara zake? Kama hakuna namna Sabado ni nini ukilinganisha na Said Bakhresa?

Kwa anayejua jinsi mtandao wa wafanyabiashara hasa wale wafananao na Sabodo walivyo watatanishi, atahoji na kutia shaka kama mimi.

Kama Sabodo aliweza kuwageuka watu makini na jasiri kama MNF ikiongozwa na majabali kama Joseph Bukuku na watu safi kama Salim Ahmed Salim ukiachia mbali kuwaingiza kwenye utata lulu kama Joseph Warioba, CHADEMA ni nini? Kuweni makini na ikiwezekana pesa zake arudishiwe.

Kimsingi mtu kama Sabodo si saizi ya CHADEMA bali waganga njaa kama wale mnaowaona wakijigonga na kujigeuza nyumba ndogo ya Kikwete na CCM yake kama mlivyoshuhudia huko Dodoma hivi karibuni ambapo mmoja alijivua nguo si kawaida.

Kuona hatari inayoweza kuikabili CHADEMA, hata ukiangalia staili iliyotumika kukabidhiwa hivyo vipande thelathini vya fedha ni ya kudhalilisha ukiachia mbali kuashiria mengi kwa wenye akili. Kwanini Sabodo awaite nyumbani kwake viongozi wa chama kana kwamba anawapa zawadi binafsi badala ya kukutana nao ofisini kwao hata hotelini?

Hakuna ubishi. CHADEMA si mwiba tu bali mkuki hata mshale kwa CCM. Hivyo lazima ishughulikiwe na wa kufanya hivvyo si wengine bali makada wake kama Sabodo. Kweli penye udhia penyeza rupia. Walisema wahenga.

Hata ukiangalia maneno ya kumshukuru ya kinara wa mapambano dhidi ya ufisadi toka upinzani,Dk Willbroad Slaa unagundua anavyoanza kulainishwa. Alikaririwa akisema : “Natoa mwito kwa vyombo vya dola, kuacha kuwatisha Watanzania wenye mapenzi mema wanaochangia vyama mbadala kama CHADEMA kwani kufanya hivyo ni kuhujumu taifa na kukwamisha maendeleo ya nchi.”

Angekuwa hajawa-cornered even induced, Slaa bila shaka angechomeka neno walio na fedha safi siyo itokanayo na ufisadi au wenye kutia shaka.

Je alisahau au naye ameanza kuishiwa kama tuliowaona Dododma?

Kwa leo sisemi mengi. CHADEMA imefungua ukurasa mpya wa ushirikiano ambao bila shaka kwangu ni ule wa dubu na kudu.

Nimalize na maneno ya Shakespear. “Alas, poor Yorick! I knew him, Horatio.”
Chanzo: Gazeti la Dira la 18 Julai 2010.

Thursday 15 July 2010

Sofi, wakitunyima utatupa ?


Hivi karibuni bi mkubwa wangu alikuja na mpya. Alisema kuwa kuna shoga yake kamwambia kuwa siku hizi yeye na mumewe wana-sleep mzungu four baada ya kugundua kuwa anakisadia chama cha upinzani! Umbea niliounyaka ni kwamba wako akina mama wengi wameanza kutimiza upuuzi huu!


Anasema mama huyu alianza mkakati huu baada ya kuwaidhiwa na mwenyekiti wa kitengo cha akina mama cha Umoja wa Wanamama Tata (UWT) wa Chama chao Cha Maulaji (CCM siyo Chama Cha Mapinduzi) aitwaye Sofia Lion ambaye watani wake wanamuita Mpayukaji Msemahovyo wa kike kayani.

Niseme kwanza. Sina tabia ya kuwazodoa wala kubishana na wakubwa wa kaya hata kijiwe hadi wanichokoze au kugusa maulaji yangu. Hivyo wanapogusa maulaji yangu huwa sina cha msalie mtume wala kumradhi. Huwa natwanga kama sina akili nzuri. Raha jipe mwenyewe ati alijisemea Njaa Kaya ambaye siku hizi amempa raha na ujiko mwanae ambaye licha ya kuwa mweupe alikuwa hata hajulikani. Hayo tuyaache.

Mbona wao wanapowasaliti walevi hawaambiwi wanyimwe uhondo huu wa Mungu? Au ni yale ya mkuki kwa nguruwe. Hivi kama tungetenda haki si jamaa yangu Nkuu angebaka ukiachia mbali kufa kwa kiherehere alichowasakizia wanafunzi?

Huu ni ushahidi kuwa wakubwa, wake zao hata hawara zao wanataka kutawala akili za wake zetu kiasi cha kutudhalilisha na kutudhulumu haki yetu ya ndoa.

Sofi fyatu alipotoa mpya kuwa akina mama watakaoona waume zao wanaisaliti CCM basi wawanyime kitu ya Ngai Mulungu wetu, ukweli mimi sikujali.

Kwanza, sikudhani kungekuwa na wanawake fyatu na taahira kama yeye wakafanya kitu mbaya kama hii. Nilijua; ni mipayuko na kufilisika kimawazo kulikoanza kugeuka sera za wenzetu. Hivyo nilipuuzia; nikijua hili halitawezekana. Kumbe nilikosea! Sikujua kuna wanawake fyatu na hovyo wangeweza kutekeleza upuuzi huu.

Mie nimemwambia bi mkubwa personally kuwa kama siku akihama chama chetu cha familia cha Ugali Nyama na Maharagwe au Ufisadi Nongwa na Mizengwe (UNM) mie sitajivunga nitamuoa huyo Sofi maana nasikia hana mume. Akigoma nitamnyotoa roho nami nijinyotoe kuliko kutoa talaka hili wengine wafaidi.

Heri ya Sofi ambaye neno husband kwake ni msamiati mgumu. Heri yake anaweza kujivinjari na yeyote kwa vile yeye ni open cheque kwa kimombo. Kama atasema namkashifu nitaiomba mahakama atakaponishitaki aje na cheti cha ndoa na huyo mulume wake. Akitimiza masharti haya mawili basi niko tayari kufungwa maisha hata kunyongwa.

Mgosi Machungi ndiye ametoa mpya kwa kusema kuwa kwa vile Sofi ni kanunga fulani, anatumia mkakati huu kutaka wanawake wawasumbue waume zao ili yeye awanase. Maana Mgosi anasema cheo au elimu ya mtu haiondoi upumbavu wake. Hivyo kaa chonjo Sofi ana lake nyuma ya pazia.

Pia nimetoa ushauri kwa wale waliohujumiwa na mama hili, kwanza, waende mahakamani washitaki chama na baada ya hapo wajitoe chamani na kujiunga na UNM tuikomboe kaya inayozidi kuliwa na hawa nyemelezi wa Njaa Kaya.

Mbinu hii chafu na hatari, kama itapata washikaji, inaweza kuleta balaa hasa talaka na ukimwi ukiachia mbali uzinzi kwa pande zote. Hapa hatujaangalia kupungua idadi ya watoto. Huenda kama mbinu hii mfu ina faida basi si nyingine bali kupunguza ongezeko la watu hasa maskini ambao wenye nazo hawawahitaji kutokana na kuwasumbua kutaka wapambana ufisadi na umaskini. Hayo tuyaache.

Hebu fikiria. Piga picha. Mkeo ambaye ulimuoa kwa posa na kila makando kando bila ya chama kukusaidia, anataifishwa na chama hicho hicho ghafla.

Hebu fikiria mkeo kipenzi anakuwa na washauri wasiojua nini maana ya ndoa zaidi ya kuishi kama jiko la mchina. Unategemea nini bibi mkubwa anapotekeleza ushauri wa mashoga wenye akili mgando ambao kwao mume ni ulaji tena wa siku-kwa maana wanaweza kumchuna yeyote mradi wapate chao iwe pesa au cheo.

Nasikia mume wa shoga wa bi mkubwa hakuficha. Ana mpango wa kwenda kumwambia huyo aliyemgomesha mkewe ampe urodi hata kama aliyefanya hivyo ni changu maarufu potelea mbali atavaa silaha.

Je ni wangapi wataiga mfano wa dume hili la mbegu lililoamua kumtokea Sofi? Je hapa ukimwi utaacha kutumaliza hasa ikizingatiwa kuwa unasambazwa na wale tunaowaita viongozi wetu? Je watu wa namna hii wanafaa kuendelea kuwa kwenye ofisi za kaya hata kama wanajuana na waliowateua kutokana na waliyowafanyia?

Natamani ninkamate Sofi na kumfunga Segerea hata nimhamishie Afghanistan au Saudia akione cha moto.

Uchangu mwingine bwana unatia kinyaa. Unachefua hasa pale yule anayeueneza anapolipwa njuluku zetu za kodi. Hata kama sisi ni walevi na wasotaji wa kutisha, tuachieni burdani yetu yaani kitu ya Mungu. Mmeiba ma-EPA na ma-Richmonduli hatukusema. Mmetulangua na kutukatia maumeme mwaka mzima, manywaji na fegi tumenyamaza. Mmechakachua mafuta hadi magari ya dingi yanamgomea hatukusema! Mmepora pesa yote ya kahawa na kashata pale Bunch of Thieves (BoT) tumeuchuna mkaanza kuumbuana wenye .

Kwa vile mmegusa pabaya lazima tuseme tena kwa herufu kubwa. Kwanza nalaani ufisadi huu na uhujumu dhidi ya taasisi adhimu ya ndoa. Naapa kwa miungu yote. Tutatoana roho kabla ya ngoma kututoa roho.

Sofi, chonde chonde, acha nakusihi. Acha kabla ya kuona kiama kabla ya kukata roho. Hujui kitu hii ndiyo starehe pekee iliyobaki kwa walevi ambao ukapa unazidi kuwaadhibu huku wakubwa wakitanua na mibilioni ya kuusaka ulaji wakiwatumia vitegemezi vyao? Kwanini Sofi unafanya uchokozi hivi? Shida yako nini? Hivi kweli una mume au mshikaji tu? Mume anauma usiambiwe Sofi mwanakwetu mtoto wa
Kizaramizi. Wataka tuzaramie kwako na je utatuweza ambao bi wakubwa zetu wametupiga kibuti kutimiza amri yako?

Mie ningekushauri haya mambo ya ngono uachane nayo. Maana licha ya kukuaibisha huwezi kushinda vita hii. Kwanza, nashangaa. Siasa na ngono wapi na wapi? Mbona mke wa rafiki yangu Willy Silaha ni mpinzani wake kisiasa lakini hii haiwi tatizo kwenye ndoa yao na hawalali mzungu wa four?

Kama ni kunyimwa u-house basi wanyimwe wanaofanya na kulea ufisadi na siyo sisi tunaofaidi haki yetu ya kuweza kutumikia na kusaidia chama chochote. Hii ni haki yetu kikatiba. Mbona nasikia Sofi amesoma sharia lakini ni mweupe asiyejua katiba ya kijiwe chetu chakavu? Kuna haja ya kumchunguza. Huenda alipata ndingirii yake kwa kughushi au kutoa chau chau ya ngoni.

Sofi nasisitiza. Tangaza tujue utatupa ili tusifanye maandamano bure. Kwanza, tutajidai na mtu mwenye cheo kuliko sisi walevi. Sipati picha nami kukwea shangingi la wakubwa nikitanua! Ila nakuonya. Siyo tuje tukute mibuzi mikubwa mikubwa mienzio mtufunge bure. Na vitoto vitakavyozaliwa kwenye kitimtim hiki lazima viitwe chama au siasa.

Mara namsikia yule jamaa ambaye bi mkubwa wake amegomeshwa na Sofi akisema : “Acha niwahi nijitia uturi tayari na kuchukua zana zangu salama nienda kujivinjari na bi Sofi ili bi mkubwa wangu aliyenigomea akome.”

Jamani chungeni. Kuna miwaya na haijali cheo wala nini. Mwenzenu mie simo bi mkubwa wangu si mpuuzi wa kusikiliza upuuzi wa wapuuzi waliolewa ulaji.
Swali linaendelea. Sofi wakitunyima wewe utatupa? Nangojea jibu.
Khalas kweisine.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 14, 2010.

Wednesday 7 July 2010

Safari hii sitaki mavuvuzela kijiweni


KWANZA niseme wazi tena mapema na kwa msisitizo. Mwaka huu umekuwa mbaya sana kwangu.

Walatini huita Annus Horribilis. Licha ya mama watoto kunusurika kwenye ajali kule kwa kina ‘Mura’ mie mwenyewe nimenusurika mara nyingi tu.

Pia sikutimiza ahadi hata moja nilizowapa walevi waliponichagua kitsunami zama zile ili kuongoza kijiwe chao ambacho kimegeuka mali yangu binafsi. Mwenzenu naona aibu ingawa najikaza kisabuni.

Kinachosaidia ni kwamba kwenye mchezo wa sanaa msanii hapaswi kuona aibu vinginevyo ningeishaumbuka zamani gani!

Mambo yangu ni tofauti na mkuu wa kaya ya Tanzia kule karibu na Danganyika ambaye alivurunda lakini bado akajisifu kuwa hakuvurunda ndiyo maana genge lake la ulaji la kiama limempa nafasi nyingine ya ulaji wa bure.


Nilikuwapo pale mitaa ya Dom wakati akijigamba alipokuwa akitangaza azma ya kuula tena ingawa picha halisi ni sawa na yangu. Nilimuona akiitangaza familia yake.

Hatua hii ilitusaidia wengine kujua wanafamilia wake ambao walikuwa hawajulikani kutokana na kutoka kwenye nyumba ndogo zake. Nina mpango wa kumshitaki kwa kuiba sera yangu ya ufamilisho, ujikoisho na udugusisho.

Ukitaka kujua nimaanishacho angalia kazi wanayofanya kwa sasa akina Rizi na Mira ambaye wengi hammjui kutokana na utata wa familia yenyewe na nyumba ntobhu.

Hakuna kilichofanya mwaka huu niuone nuksi kama tishio la baadhi ya wazee wa kijiwe kunitaka nisigombee tena ulaji kwenye kijiwe kutokana na kuvurunda na kuonyesha uchanga badala ya ukomavu, ukiachia mbali kuzungukwa na kashfa kibao za kupunyua njuluku za kijiwe.

Nani kasahau nasaha uchwara za kina mzee Kidevu almaaruf Warihaba, Mchunguliaji almaaruf Kareshi Mati na wengine wengi? Si walisema sifai hata kuwa mjumbe wa nyumba kumi achia mbali rais wa kijiwe!

Najua njaa ndiyo ilisababisha mashambulizi yote haya. Maana tangu nikitaifishe kijiwe mimi familia yangu na marafiki zangu, walevi wamekuwa maskini kiasi cha kushindikia kahawa na kashata.

Na hii imesababisha bei ya kashata na kahawa kupanda kiasi cha watu kutamani wazikwe hai. Wengi wananionea wivu ninavyotanua huku wao wakitanuliwa na njaa na ukapa. Mie nshawambia mara nyingi: raha jipeni wenyewe mie siwapi.

Hapa sijaongelea jamaa zangu wa majoho walioanza kuniita mnafiki kwa vile sikutimiza ahadi yangu ya kuwapa uwanja wa kufanya mihadhara kwenye kijiwe.

Nakumbuka nilipowafunga kamba kuwa utawala wangu utawakomboa waende nchi ya maziwa na asali hawakujua nitawanyonya hadi wakonde na kukoma!

Walevi ni watu wa ajabu. Wanauziwa mbuzi kwenye gunia halafu kwa ujinga wao wanalalamika. Nilidhani kipindi hiki wangestuka waninyime kula ya kura. Ila kwa walivyo wepesi wa kusahau na wapenzi wa kuishi kwa matumaini, hata ngwe hii ya lala salama nitapeta.

Hakuna cha maziwa wala asali kuchanganywa kwenye kahawa wala mikate zaidi ya kashata kavu na lugha laini na wakati mwingine mipasho wanaponiudhi kuchokonoa ulaji wangu.

Baada ya kukaa na kutafakari, nimegundua mbinu mpya ya kuendelea na ulaji-nayo ni kuwakwepa wana mitandao yangu ya ulaji na kutumia wana familia yangu ingawa wapo washenzi wanaosema: mtandao ni mtandao hata uwe wa mke na watoto wako.

Hawajui nawapigia debe watoto na wake zangu hata nyumba ndogo ili hapo baadaye nao wagombee nafasi nyeti kijiweni. Hii ndiyo siri ya kumpa mwanangu mikoba kwenda vijiwe vyote kusaka wadhamini wangu mwaka huu. Mwaka huu situmii vuvuzela hata kidogo.

Kwanza walevi wameishawashtukia licha ya kuchoka na longo longo zao. Nikiangalia kiongozi wao mgosi Machungi Makambale alivyochafuliwa na kashfa ya mwanae na wizi wa kashata, sina hamu na vuvuzela hata kidogo.

Si unajua tena. Hawa jamaa zangu wa mitandao wananitumia wakidhani mie bwege. Ingawa wengi wanadhani tunatumiana, kimsingi wananitumia. Kwani kwa kutumia kisingizio cha kuiba pesa ya kijiwe kuwahonga walevi, nao huchota nyingi kuliko hata zile wanazohonga kiasi cha kuniachia mizigo ya kashfa.

Nani mara hii kasahau ile kashfa niliyoita EPA ya HEPA?

Bado kuna ile ya iliyomeremeta wakati mimi nikimetuka. Hapa sijataja kashfa kama MAWAWA ya Bi. Nkubwa ukiachia mbali ile ya kutumia mipesa kibao kutanua na kupaka nkorogo ikuu yangu ambayo wabaya wangu wanaiita pachafu pa pachafu palipokuwa patakatifu pa patakatifu enzi za mtume yule.

Hapa hujagusa matumizi mabaya ya watu wangu hasa wauzaji na wasimamizi wa kahawa. Bado hujagusa matumizi mengine mabovu ya nyumba zangu ndogo na washikaji wangu wengine ambao sitaki wajulikane.

Sitamtangaza mtu hata walamba viatu wangu. Nawatangaza mwanangu na mke wangu ambao nikishindwa ndio watakuwa waathirika wa kwanza na isitoshe baadaye watagombea ulaji.

Maana ujiko na ulaji wa dezo vitakuwa vimeyeyuka. Nimegundua hata hii pesa ya wizi tunayoiba na kina Roasttamu haiwezi kufua dafu bila kubadili mbinu.

Hapa hapendwi mtu bali njuluku. Kadhalika hafagiliwi mtu bali ndugu.

Ulaji hasa ukuu wa kijiwe si mchezo! Unaweza kuamini kuwa kila mwezi wazee wa ukoo wangu wanapokea wanafamilia wapya? Ulaji umeiunganisha familia yangu iliyokuwa haina mpangilio ingawa wengi wanasema kinachofuatwa hapa ni ulaji potelea mbali! wale vyangu niliopasua nao amri ya sita miaka ya sabini wananiletea wanaharamu kila uchao.

Hivyo usishangae kuona sura ngeni kila uchao kwenye safu ya wanafamilia wangu. Naomba Subhana: wale vyangudoa wa kizungu niliojivinjari nao nilipokuwa nje wasije nao wakaleta wanaharamu wa kichotara. Hata hivyo nani atauliza iwapo kila mtu ananizimia na kuniabudia ili nimmegee mabaki? Hayo tuyaache maana nyumba hutunza makubwa.

Pia nina wasi wasi na washikaji wangu kama Mzee Maneno almaaruf kama Sam Sixx ukiachia mbali Msomimkata tamaa almaaruf Mariko Mwanadosha.

Hata huyu Mpemba almaaruf Wakushaini nimeamua akitoe ili akagombee huko ili asinivurugie madili wala kuwa tishio hapa hasa mrithi wa ufalme huu wa kijiweni.

Dunia hii waja tuna dhambi we acha! Msiyeni Mulungu akale Mulungu walijisemea wanyasa.

Naona Riziki na kundi lake wanakuja kusaka wafadhili. Acha nikitoe nisije nikamnasa mtu makofi ndata wakanizoa bure.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 7, 2010.

Sunday 4 July 2010

Challenge to our thievish MPs

While our Members of Parliament are renowned for being corrupt and thuggish, their counterpart in a rich country are earning earnestly.

They are indulged in double jobs whilst ours in double wheel deals and kickbacks.
Borrow a leaf from these patriotic MPs whose job can be seen on their country everywhere.

Whilst hyena-like-Kenyan MPs are increasing their salaries for doing nothing, Canadian MPs are toiling to earn legally by hard work and sound investment. What a shame for begging country whose budgets depend on rich nation to amass wealth gotten by means of embezzlement!

If anything, this is but a challenge. But again, for our fainted-hearted thieves, this does not add up.

Without keeping our rulers on toes vis a vis accountability, this will be as good as playing a guitar for a goat to dance.

What agonizes is the fact that our people ape and envy this filth-coated wealth our thieves in power own!
This is but another root of corruption in Africa,



By Elizabeth Thompson,

Nearly half of Canada's members of Parliament are moonlighting, running businesses or collecting income above and beyond their six-figure salaries.

A review of recent disclosure statements filed with Parliament's ethics commissioner shows that 151 of Canada's 308 MPs are either receiving an outside income or have an ownership stake in an outside business.

The analysis for The Canadian Press found that 103 MPs are owners or part owners of businesses, ranging from fast-food restaurants, a bakery and wilderness tours to holding companies, farms or real-estate investment.

The filings also show that 99 MPs each received more than $10,000 in income from outside sources in the previous year, in addition to their base salaries of $157,731.

Forty-eight MPs collect pensions — most of them from governments. Another 51 listed income ranging from speaking and consulting fees to rental and farm income.

Fifty-one MPs listed both outside income and outside business interests.

Even two of four party leaders in the House of Commons list outside interests.

Liberal Leader Michael Ignatieff collects rent from a property he co-owns in France, as well as fees from public speaking, freelance journalism and book writing — all on top of his annual $233,247 salary.

NDP Leader Jack Layton is the owner of the Green Catalyst Group Inc., has a 25 per cent interest in Layton Holdings Ltd., is a joint owner of an investment property in Toronto and collects a municipal pension.

Neither Prime Minister Stephen Harper nor Bloc Quebecois Leader Gilles Duceppe listed any outside jobs, companies or income.

While there are some restrictions for cabinet ministers, MPs are allowed to hold as many outside jobs and own as many companies as they like.

Unlike the United Kingdom, there is no requirement for MPs to publicly disclose how much they earn from outside interests, just whether they earned more than $10,000. Nor do they have to disclose how many hours they spend on those outside jobs.

The only restriction is that they can't use their parliamentary office or their position as an MP to benefit their private businesses.

Some question the practice, saying MPs are well paid and expected to perform a full-time job. Others suggest it would be hard to attract candidates if MPs had to ditch their professions and businesses, leaving them nothing to fall back on should they lose an election.

Ned Franks, professor emeritus at Queen's University in Kingston, Ont., says outside interests can make MPs more aware of issues in the business community or in society.

"We don't want a Parliament of eunuchs. On the other hand, you don't want a Parliament of rich people looking after their own interest."

Several MPs, such as St. John's East MP Jack Harris, closed down their practices or businesses after they got elected saying they just don't have time. But others successfully juggle both commitments for years, often relying on family or trusted staff.

When Borys Wrzesnewskyj, Liberal MP for Etobicoke Centre, was elected in 2004 he decided to keep his three businesses — Future Bakery, Aunt Irene's and M-C Dairy. While staff handle daily affairs, Wrzesnewskyj gets detailed monthly reports and loves to return to the bakery floor and roll up his sleeves to help prepare special breads for Christmas and Easter.

"There's nothing like a little bit of real work to reconnect with reality," he said.

Independent Quebec MP Andre Arthur regularly slides into the driver's seat of a passenger bus and hits the open road. He also records commercials and has worked extensively in the past in radio and television.

Arthur says driving a bus helps him keep in touch with real people and real issues.

"When I'm on the road, even when I am with people who aren't from my riding, I have the impression it gives me a grounding in reality."

The businesses and side jobs are as varied as the MPs themselves:

— Thunder Bay-Superior North MP Bruce Hyer owns Wild Waters Nature Tours and a wilderness shop.

— MP John Rafferty owns a communications and media recording business.

— Conservative MP Joe Preston owns a Wendy's restaurant and an interest in a Boston Pizza.

— Liberal MPs Justin Trudeau and Kirsty Duncan earn money from speaking engagements.

— Bloc Quebecois MP Daniel Paille lectures at the Ecole des Hautes Etudes Commerciales.

— Liberal MP Gerard Kennedy is a consultant to Toronto-area Alpha Labs.

Some MPs, such as Liberal Derek Lee, practise law but far more are involved in real estate.

British Columbia MP Keith Martin has to practise medicine periodically to keep his credentials.

Conservative MP Terence Young closed his government relations business because he felt it conflicted with his job as an MP. But Young, a former Ontario MPP, said it can be tough for retired politicians to find a job.

"A wise person plans their exit strategy early."

Source: The Canadian Press

Friday 2 July 2010

Tunataka uwajibikaji si wingi wa mikoa ya kulipana fadhila

Baada ya serikali ya rais Jakaya Kikwete kujiingiza kwenye kashfa tele ambazo zimeligharimu taifa wengi walidhani angalau angestuka.

Hata baada ya serikali ya Kikwete kuwa zigo tokana na kutapanya mali na pesa ya umma wengi walidhani angestuka.
Hata pale wafadhili walipoamua kuiminya serikali ya Kikwete kifedha ili ipambane na ufisadi vilivyo badala ya kuushabikia na kuukingia kifua wengi walidhani angestuka.

Nani amesahau kuwa ripoti ya mkaguzi wa mahesabu ya serikali kila mwaka hufichua matumizi mabaya kwenye karibu wizara na serikali zote za wilaya?

Nani haoni kuwa hali hizi zinasababisha maisha magumu kwa umma ulioahidiwa kupelekwa peponi Kanani ukaishia kwenye mazonge?

Kutokana na upogo na upofu huu wachambuzi wengi walimlingansiha Kikwete na bwana Ziro ambaye siwezi kumtaja kwa vile anafahamika na alivyovurunda, kama alivyokuja kukiri mwenyewe.

Hii inanikumbusha kisa cha ndege mmoja mpumbavu ambaye baada ya kumeza punje moja ya hindi alighafirika na kumeza nyingine. Ndege huyu mpumbavu aliishia kukwamwa na punje na kupasukilia mbali huku mbegu zile zikimgeuza mbolea.

Wengi wanashangaa. Wameshangaa mantiki ya Kikwete kuanzisha mikoa mipya mitatu wakati ile ya zamani inamshinda kutokana na mzigo wa kiutawala. Kwanini sasa kuelekea uchaguzi na si alipoingia madarakani? Jibu liko wazi kuwa hiki ni kishawishi wananchi wanaoangukia kwenye mikoa mipya. Hii ni hoja hata sera kwa waramba viatu wa Kikwete kuwahadaa wananchi kuwa “mnaona Kikwete kaanzisha mikoa wilaya na tarafa mpya ili kuleta huduma karibu.” Kwanini hakuianzisha wakati anaanza tukaona ambavyo angeihudumia? Wajinga wengi watasema tumpe kura Kikwete ili akamilishe mema aliyoanzisha. Rais hakuchaguliwa kutenda mema bali kutekeleza ahadi sera na katiba vilivyomuingiza madarakani finish.

Kwa Tanzania kuwa na kata, tarafa, wilaya hata mikoa haisaidii chochote kama watawala wanaposema kuwa wanafanya hivyo kuleta karibu huduma. Kuna huduma gani zaidi ya umaskini wa kutengenezwa na wajinga wachache wenye mamlaka?

Katika kuelekea uchaguzi, leo tuna mikoa mipya mitatu yaani Njeruma, Geita na Simiyu. Wengi wanahoji mantiki ya ufinyangwaji wake ukiachia hata majina yake. Tuna wilaya mpya kadhalika. Hizi ni Mulele Gairo, Nyasa, Chemba, Ikungi, Mkalama, Mbogwe, Nyang’wale, Buhingwe, Kakonko na Ushetu!
Hata majina yenyewe yanatia shaka achilia mbali kinyaa. Kwanini Njeruma si Mkwawa hata Mnyigumba? Kwanini Geita na si Ziwa au Simiyu na si Bariadi hata Nguliati kwa wanaojua historia ya mkoa huu?

Hapa tunaongelea ulaji kwa Kikwete (kura) na ajira (kulipa fadhila) kwa marafiki wa Kikwete ukiachia mbali majisifu yasiyo na maana. Hujaongelea shilingi zaidi ya bilioni 150 zinazodaiwa kwenye sekta ya elimu mwaka 2008. Si Kikwete wala mawaziri wake wanataka hili lijulikane wala kujadiliwa. Pesa inaibiwa wewe unapanua serikali badala ya kuipunguza ili usimamie vizuri. Uchumi gani huu?

Usishangae kusikia baadhi ya makanjanja na walamba viatu wengine wakipewa ukuu wa wilaya hata mkoa na ubaki kuishia kupigwa na butwaa. Maana kwenye balozi zetu nje nafasi zimejaa ukiachia mbali kwenye bodi za mashirika na ulaji mwingine wa kulipana fadhila.
Leo tuna wakuu wa wilaya hata wabunge waliokuwa wauza maandazi na hakuna anayeuliza walivyofika hapo ukiachia mbali vihiyo wengine kwenye taaluma nyingine hata sheria.

Wengi hasa wachumi wanaoona madudu ya serikali ya Kikwete walidhani: kuondokana na matumizi makubwa yasiyoshabihiana na mapato, Kikwete angepunguza serikali yake badala ya kuipanua. Kwa vile mifumo na siasa zetu ni kwa ajili ya kundi dogo la watawala kujihudumia, Kikwete, washauri na maswahiba zake hawakujihangaisha kuuliza nani atagharimia mzigo huu. Watahangaishwa na nini wakati punda kihongwe (mlipa kodi maskini) yupo na halalamiki?

Je ni vigezo gani vimetumika kufinyanga hii mikoa na wilaya zaidi ya ushikaji kisiasa? Sijui kama hata huo mkoa mpya wa Njaruma ni mkubwa kuliko wilaya ya Kahama. Kesho tutaamiwa. Bagamoyo hata Chalinze ni mikoa! Kweli namna hii tutasonga mbele au nyuma? I have no idea.

Benjamin Mkapa ambaye waliokata tamaa wanaanza kumkumbuka alishambuliwa alipogawa mkoa wa rafiki na mtendaji wake mkuu Fredrick Sumaye kuwa mkoa kwa sababu alizojua. Leo “chaguo la Mungu sijui sheta…” naomba nisimalizie, ameamua kuonyesha maneno uchumi na umma yasivyo kwenye kichwa chake sijui tutafanya nini? Je sisi si mateka wa kiumbe tuliyemtengeneza kama jini na kumtoa kwenye chupa akaanza kuturudi?

Je hapa wa kulaumiwa nani kati ya makuli wabeba mzigo na bwana mkubwa mbebeshaji watu mizigo yake? Mmeonya si mara moja wala mbili kuwa mna muung mtu kwenye ofisi yenu kuu lakini mwamgwaya kiasi cha kuwatoa kafara kwa faida zake na marafiki zake mkiona na msifanye kitu? Katika kitabu changu cha Saa ya Ukombozi nilidurusu hali kama hii kwenye nchi ya Mizengwe ambapo umma uliamka na kuondoa kadhia bila kuchelea patilizi na maangamizi. Je nyie mko tayari? Kazi kwenu. Mnata mitume waje na waseme mara ngapi mkengeuke na kuchukua hatua achia mbali kuamini?

Ukionja nyama ya mtu huishia kwenye urahibu. Kikwete alipanua serikali yake na hakupata misukosuko. Sasa anazidi kupanua zaidi wakati dhiki zikipanuka zaidi. Je tufanyeje? Jibu mnalo waathirika wakuu.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 30, 2010.

Long live my kingdom


Mwezi Juni unaingia kwenye vitabu vya kumbukumbu ya himaya ya walevi kuwa ndio wakati uliposimikwa utawala wangu mfalme mkuu wa walevi almaarufu mfalme Mpayukaji Jackal Kimwemwe I ambao wabaya wangu huuita ufisi yaani Ufisadi Siasa-fisidi na Usanii ingawa siyo.

Kuhakikisha ufalme wangu unadumu milele, nimewateua waramba viatu wangu na wanafamilia kuusimamia na kuusimika katika mioyo ya walevi ambao wananipenda kuliko wanavyojipenda.

Wengi wasiojua siri ya maulaji wamenilaumu kuwa nawachelewesha kwenye himaya na neema niliyowaahidi walevi zama zile! Waarabu wana msemo: “ Kul takhira fi’ khira yaani wakati mwingine bora kuchelewa kuliko kuwahi. Hata waswahili wamesema: Pole pole ndiyo mwendo na haraka haraka haina baraka ingawa ngoja ngoja nayo huumiza matumbo. Tuchague lipi? Mtajijeijei na kiherehere chenu. Mkilizwa mnalalamika wakati ni kiherehere chenu na kutaka takrima na kitochi. Sasa mnataka mimi niwafanyeje yarabi?

Mliambiwa mali mnayo lakini mnaikalia. Akili mnazo lakini hamzitumii badala yake mnatumia matumbo na njaa!

Kuhakikisha ujiko na usalama wa ulaji wangu haviguswi, nimemteua kifungua mimba wangu aitwaye Rizikiwani kufungua usanii kwa kuhakikisha naungwa mkono na wanyama, wadudu, mimea, mbingu, bahari, magari na walevi.

Najua walevi wapenda sifa watachangamkia tenda ya kuniunga mkono kwenye vijiwe vyote wakijisifu kuwa wamenidhamini wakati mdhamini wangu mkuu ni pesa na wenye nazo tu.

Ingawa juzi baiskeli ziligoma kunibeba, lazima kila kitu kitii ufalme huu uliotoka kwa Mungu.

Juzi tu alijitokeza bazazi mmoja kutaka ufalme uangushwe na kila mtu aruhusiwe kugombea kuwa kiongozi wa walevi.

Nilimuita mteule wangu mkuu wa makuhani na kumwambia nisisikie upuuzi huu. Japo mimi si mzee wa makuhani wala msomi wa torati, nilimuagiza ahakikishe shauri hili linakufa haraka. Alifanya kweli na kuutangazia umma kuwa ufalme utadumu milele. Sababu? Kwanza, angegomaje wakati nilimteua kwa kumpendelea kutokana naye kutokuwa na udhu wa kuwa mkuu wa mkuhani kama yule mkuu wa usajili wa timu za kupingana Joni Tenda.

Naitangazia dunia kuwa kila kitu kimetiishwa chini yangu. Si wakuu wa makuhani, waandishi, mafarisayo hata kina Zakayo, masadukayo wala watoza ushuru. Masadukayo wameishaonyesha vitu vyao kwa kunichangia maelfu na ndururu kwa ajili ya kusimika ufalme huku waandishi wakiimba sifa zangu na wazee wa makuhani wakipitisha amri zangu bila kujali mie si msomi wa torati.

Hamkusoma katika Marko 12:43,44 juu ya yule mwanamke maskini aliyotoa senti mbili na kuhesabiwa haki? Mie sihesabii maskini haki bali wenye nazo ambao lazima wanichangie kuimarisha ufalme wangu. Wabaya wangu wanasema nitaishi na kuisha kama Nabkadnezza! Niishi na kuisha mara ngapi zaidi ya wao ninaowabebesha mizigo kama vihongwe?


Pili, wanaotaka kubatilisha ufalme na kuleta jamhuri hawana sura nzuri- yaani they are not beautiful enough to become king even president like me -the most beautiful one and the choice of God.

Tatu, hawana fweza za kuwanywesha walevi kwa kuwapa kitochi na kuonyesha ukarimu wao kupitia takrima.

Nne, wao si chaguo la walevi wala hawapendwi na watu kama mimi kiasi cha watu kunichangia wakati nakwanyua kila uchao mimi bi Nkubwa na wenzangu. Kama alivyowahi kusema chizi mmoja baada ya kulewa maulaji kuwa walevi wanaweza kula majani lakini lazima mkuu apate pipa atanue na shortie wake.

Juzi nilicheka niliposikia kuwa wakati watu wanamchangia jamaa yeye anapaka ikuu nkorogo ukiachi ambali kuahidi milaputopu wakati ukweli ni kwamba kwenye ilmu zilishaibiwa bilioni 150! Upo hapo mshrika? Hii usimwambie mtu kuepuka idadi ya wanaojinyonga kuongezeka kutokana na hili. Nichangieni mie mfalme asiye na makuu.

Tano, hawana ahadi nzuri za kuwazingua na kuwachengua walevi. Hawana lugha tamu ya kuwaahidi Kanani pepo na vinono vingine hata vikigeuka kuwa shubiri kwao.

Sita, hawajasomea sanaa wala hawajui kutumbuiza kwa mipasho yenye kupumbaza kama mimi.

One thing must be noted. Naongea kizungu mjue nimebukua hata kama ni kamba. Baada ya mama mmoja toka huko milima ya Pale kuja na mpya kuwa ukintongoza mwannke usintukane, nimejifunza toka kwake. Ukitaka kuibia wale lazima uwatongoze kwa kuwaahidi kila vinono hata kama unajua huna sera na mwisho wa yote wataishia kusaga meno. Mie nimeahidi spiidi zaidi, Mori zaidi na power zaidi ya kuhomola.

Niliwaahidi walevi majembe ili walime kahawa na kuwa mabilionea nikachemsha. Kwa vile wanapenda kutongozwa na kupumbazwa, kipindi hiki nawaahidi kompyuta kila mlevi na GPS ili nikiwa natanua ajue niko mitaa gani kule majuu ili waje tutanue pamoja, je hii inawezekana? Tia akilini.


Sitanii. Kwa vile nina mpango wa kumrithisha mwanangu ufalme wangu, kipindi hiki nitatanua sana kwani ni lala salama ya ufalme wangu. Wale wanaonikamia kuwa watanitoa nohino nikishamaliza ngwe yangu ya mwisho wamenoa. Hawajui kuwa nitahakikisha mrithi wangu anakuwa mtu wangu kama si mwanangu kiasi cha kunilinda kama nilivyowalinda akina MbwaMwitu na Kanji Roast tamu na wengine kama Tunituni na ukoo wake?

Anayebisha aangalie nilivyomtupa nje ami Mpemba kwa kumwamuru agombee ukuu wa kijiwe kule ng’ambo ili kwa msimamo wake wasijempendekeza arithi kiti changu baada ya kung‘atuka. Unadhani usanii wangu wa leo tu? Shauri yako.

Zama zile nikikwea kiti cha ufalme huu niliwakamata walevi kwa ahadi ambazo ziliishia kuwa sanaa. Sasa nimebadili mbinu. Nataka nitawale kwa ndoto. Nina ndoto kubwa hata kama wapinzani wangu wanaziita za mchana. Nataka walevi wote waendeshe VX na kupanda ndege kama mimi na bi nkubwa na watoto wetu ukiachia mbali waramba viatu wangu.
Nataka vitegemezi vya walevi viishi kama watoto wangu kwa kila kitu. Lazima visome kwenye shule za bei mbaya zinazotumia si kompyuta tu bali lapu topu.

Kwa ufupi ngwe hii ni ya kwenda Kanani kwa vitendo sitanii.

Nhh! Mbona yule ni kama ndata! Acha nijikate wasije na viherehere vyao wakanikata mitama.
Hata hivyo, ngoja nipayuke kabla hawajanitia mikononi. Long live my corruption sorry kingdom.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 30, 2010.