The Chant of Savant

Friday 28 February 2014

Bunge au buge la Katiba na kuiba pesa ya umma?

Ijue sare ya Jeshi la Mafisadi Tanzania(JMT)

Thursday 27 February 2014

Kenyan'll always laugh at us with our Vasco da Gama Kikwete


Looking at president Uhuru Kenyatta's itinerary, for the first time, I wish he're the president of my country. I don't know if what he did not to globe-trot comes from personal conviction or systemic restrictions. If anything, apart from being tired of corruption, Tanzanians are tired of a corrupt and extravagant globetrotter in the office of the president. Since he came to power eight years down the line, President Jakaya Kikwete has toured the world  over 350 trips which is equivalent to approx. 40 trips annually or three trips a month.It means Kenyatta's annual timeline is equal to Kikwete's three-month schedule. What can Tanzania benefit from such a self-serving-and-loss-making president who is blind and greedy not to see the dent he causes the country? Though Kenyatta is the son of the first president who screwed up Kenya a great deal, his restraint against globetrotting is a good thing for the country and for himself. The New Constitution needs to put a stop on megalomaniacs and joyriders who can be elected president like Jakaya Kikwete. For more info, CLICK HERE.

Hii kali:" Papa" anapokutana na "dagaa"!

Wednesday 26 February 2014

Ukweli usiopingika

Je Katuni hii inaweza kuvumbua aina nyingine ya majangili ukiachia wale wa maofisini na maajenti wao mbugani? Je katika wale 40 anaowajua na kuwachunia rais Jakaya Kikwete na huyu yumo? Maswali ni mengi kuliko majibu.

Bob Mugabe@ 90 and Nyerere legacy


          
Zimbabwe’s long serving and first president Robert Mugabe aka Jongwe (cockerel) celebrated his 90th Birthday last week. For a country where life span is almost a half of Mugabe’s age, to reach 90 is not a joke. Again, what lesson do we get from this milestone especially if we look at the person? African sage has it that the cockerel taught the chicks to poop in the nest.
          Mugabe is full of shockers. He spent the celebrations once again to warn Zimbabweans to refrain from talking about succession. For, the Jongwe isn't going anywhere. He’s quoted as saying, “But why should it (succession) be discussed when it is not due? Is it due? As you can see (I am) still fit as a fiddle.” He went on saying that talk about succession is shameful for those whose names are mentioned to succeed him. If anything, the implications were clear that you talk about succeeding Mugabe for your peril be it in his party or outside of it. Mugabe added, “That is what we are fighting against and I am going to fight against this one quite blatantly because that is what is destroying the party.” Two names are mentioned in succession races in Zimbabwe; these are vice president Joyce Mujuru and Emerson Munangagwa (Defence).
          Mugabe used his 90th Birthday to eulogize the late Mwalimu Julius Nyerere the founder of Tanzania for whom he had kind words as he was quoted saying, “I want to say, when all honour has been showered on heroes in Africa, the man who has been humiliated is Mwalimu Julius Nyerere.” Ironically, Nyerere didn't cling unto power like Mugabe and all those who pretend to honour and eulogize him while they preach water and drink wine something Nyerere abhorred. For Nyerere, a million bucks was a huge amount he’d not allow to be spent on dining and wining while children in his country or in any African countries were going to bed with nothing in stomach. Nyerere’d nary stomach such pointless extravagance by all standards. Interestingly, many African dictators whom Nyerere helped to get into power are always praising him when they are cornered. What leaves many shocked is the fact that the same dictators who pretend to honour and remember Nyerere do completely different from what he stood and fought for. There is no ruler that can pretend that he respects Nyerere while he does completely differently from Nyerere used do. If anything, this is hypocrisy of its order.
To prove that Mugabe is out of touch with reality, he's quoted priding himself for soldiering on despite sanctions. He's able to spend a million bucks for just a birthday party. He said, "Those opponents of ours who had imposed sanctions on us were baffled."  Once again, Mugabe was right. It needs the courage of the mad to spend such humongous amount of money in the country like Zimbabwe where unemployment is in double digits. To do this one must be either insane or selfish and indifference altogether.
Although it right and true to say that Nyerere spent much of the resources of his country to see to it that all African countries are becoming independent, he didn't rule but  he led. He didn’t spend his countries monies on his birthday celebrations or rigging elections. Ironically, according to Al Jazeera a million bucks was spent on this birthday.
Zimbabweans especially the new generation seems to be tired of one man show. Those in their early late thirties have only known one president since they were born. They're tired of just the same as far as manning their country's concerned. Many are asking: What new can a nonagenarian like Mugabe offer to their country?  Although Mugabe is credited for having ushered Independence in Zimbabwe, his role as a leader is no longer wanted. Zimbabweans of today are not looking for a freedom fight. Instead, they’re looking for a leader who can redeem their lost glory under Mugabe’s policies. 
As Mugabe celebrated his 90th Birthday, he’s named as the oldest head of state in the world along with Israeli president   Shimon Peres who is ninety as well save that Peres has nary been in power for such long time. Surprise, surprise, Mugabe’s ZANU-PF has already said that he is going to run for presidency come next elections.
In sum, Mugabe at 90 he obviously seem to be frail. Even his birthday party had to be postponed to wait for him to return from Singapore where he underwent eye surgery.  
Source: The African Executive Magazine Feb., 26, 2014.

Kalenga watachagua ukoo au ukombozi?

 

PAMOJA na kuwa na ustaarabu wa miaka mingi, Bara Hindi linasifika kwa mifumo ya kibaguzi chini ya mfumo wa ‘caste’, unyanyasaji wa kina mama na ubaguzi wa watu wengine hasa wasio Wahindi.Pamoja na mfumo huu kuwabagua hata kuwanyanyasa kina mama, una udhaifu mmoja ambao ni kuabudia madaraka na wenye nacho. Hapa ndipo siri ya wanawake kama Indira Gandhi na Sonia Gandhi (India), Benazir Bhutto (Pakistan), Sirimavo na Chandrika Bandaranaike, (Sri Lanka) na Sheikha Hassina bint Mujibur Rahman (Bangladesh) walikuwa maarufu na kuvuka vikwazo wanavyopambana navyo wanawake wengine kwenye Bara Hindi, kwa sababu wazazi wao walikuwa watu maarufu, wenye ushawishi kisiasa na kiuchumi.

Hivyo, kwa kupitia majina makubwa ya baba, waume au wakwe, mabinti hawa walitokea kuwa maarufu.


Tanzania hasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) taratibu kimeingiza nchi kwenye siasa za Kihindi, ukiachia mbali uwekezaji hata ujenzi na biashara za Kihindi.  CCM bila aibu wala kujali malengo ya waanzilishi wake waliolenga kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye unyonge, umaskini, ujinga, ubaguzi, magonjwa na maadui wengine, wameamua kuingiza nchini mfumo huu wa kilafi na baguzi ili waendelee kuhodhi madaraka ya taifa letu.
Ushahidi wa hivi karibuni ni kuteuliwa kwa mtoto wa kiume wa aliyekuwa Waziri wa Fedha na mbunge wa Kalenga marehemu William Mgimwa, aliyefia nchini Afrika Kusini mwanzoni mwa mwaka huu, kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mdogo.
Ukiuliza huyu bwana mdogo ana nini cha mno kisiasa zaidi ya jina la baba yake hakuna jibu linaloingia kichwani.
Walifanya hivyo Arumeru Mashariki alipofariki dunia, Naibu  Waziri wa Fedha, Jeremiah Sumari, kwa kumchagua mwanae Sioi kupeperusha bendera lakini akabwagwa na Joshua Nassari wa CHADEMA, baada ya watu wa Arumeru Mashariki kukataa siasa za kurithishana na majina makubwa badala ya sifa.
Je, tutegemee hili kujirudia Kalenga? Je, wapiga kura wa Kalenga watabariki au kukataa utawala wa kurithishana ambao umezalisha wanasiasa watokanao na majina ya baba zao kama vile Aman Abeid Karume, Ali Karume, Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi, Vita Kawawa, Zainab, Adam Malima, Januari Makamba, Violet Mzindakaya,  Emanuel Nchimbi  na wengine wengi?
Kwa wanaojua majukumu na wajibu wa mbunge kwa wapiga kura, watakubaliana nasi kuwa sifa kubwa anayopaswa kuwa nayo ni kukubalika kwa wapiga kura na kuwa na sifa za kufanya akubarike zaidi ya jina kubwa la baba au mama yake.
Unapochagua mtu kwa kuzingatia ukubwa wa jina la wazazi wake, unakuwa unalirudisha taifa nyuma na kukiuka msingi mmojawapo wa mapambano ya uhuru wa taifa letu ambalo ni kuondoa ubaguzi wa aina yoyote.
Tunasema ubaguzi kutokana na wakubwa wenye majina makubwa walio au wanaotaka kuwarithisha madaraka watoto wao kuwaandaa kwa kuwadhulumu maskini. Kwa mfano, wakubwa hawa wamefanikiwa kuvuruga na kuharibu mfumo wa elimu yetu huku wakisomesha watoto wao nje kwenye elimu bora wanayotumia kama kigezo cha kuwarubuni wapiga kura.
Ni ajabu kwa wazazi au jamaa wa vijana wanaohenyeshwa kwenye mikopo na kusomea kwenye mazingira magumu kuchagua watoto wa wateule waliosoma ughaibuni.  Je, mtu aliyesoma nje tena kwa pesa na kodi za wapiga kura anafanana nao?
Je, wananchi wa kawaida hasa wa mashambani kama Kalenga wanapaswa kumchagua mtu huyu asiyefanana nao? Watakuwa wendawazimu kama watafanya kosa hili hata mgombea husika angetoka chama kinachopendwa vipi.
Mbunge lazima afanane na wale anawawakilisha na si kuwatumia kama mtaji wa kuendeleza jina la baba yake. Mgombea namna hii hatafuti ubunge kuwatumikia wananchi bali kutimiza malengo yake na ukoo wake hasa kuendeleza jina la baba au mama yake na kuendelea kuwatumia wananchi kuchuma utajiri.
Tunaposema mfumo wa kisiasa wa Kihindi tunamaanisha hali hii ya baadhi ya koo kama tulivyoona hapo juu kuwatumia watu maskini tena waliosababishiwa umaskini na koo hizi hizi kuendelea kuwatumia kwa kisingizio cha kuwatawala.
Huu ni ufalme fichi na wa kijanja wa Kihindi, sawa na ufalme na uemir wa Mashariki ya Kati. Tofauti ni kwamba inatumika demokrasia kama vile uchaguzi kuhalalisha ufalme huu wa kinafiki na fichi.
Koo, hizi licha ya kuwaona wapiga kura kama punda wazibebao, zinawachukulia kama watu wasio na akili sawa sawa, ambao wameshindwa kujitambua na kutumia nguvu yao ya kura kuziondosha kwenye ufalme fichi unaoanzia baba kuelekea mwana hadi wajukuu. 
Ukweli huu ulifichuliwa na Katibu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba, aliyesema kuwa hakuna awezaye kumzuia mwanae kuteuliwa waziri.  Kweli baada ya muda mfupi, aliteuliwa na kuwa waziri. Tumeyaona haya kwenye kashfa zilizowahusisha watoto wa wateule kama vile Hussein Mwinyi –  Waziri wa Ulinzi aliyevurunda wizara hii mara mbili na kurejeshwa hata baada ya milipuko ya mabomu kuuwa watu wasio na hatia mara mbili asiwajibishwe.
Tumeyaona kwenye kashfa ya Adam Malima na jinsi ambavyo amekuwa akirejeshwa kwenye baraza la mawaziri si kwa sifa yoyote bali jina lake la ukoo. Je, watu wa Kalenga watabariki jinai hii au kuikataa kama wenzao wa Arumeru Mashariki?
Je, watashabikia ukombozi au umwinyi na ufalme wa Kihindi ambao hautawapeleka popote zaidi ya kuwarejesha kwenye zama za mawe? Je, watajitambua na kutoa somo kama walivyofanya watu wa Arumeru Mashariki ambao wameingia kwenye vitabu vitukufu vya taifa letu kwa kujitambua na kuleta ukombozi kwa kukataa utawala wa koo na majina?
Tumalizie kwa kuwashauri wananchi wa Kalenga wachague ukombozi. Tunaamini historia fupi ya utawala wa kifalme fichi wa Kihindi utawasaidia kuona mwanga na kuuchagua wakikataa kuchagua giza na utawala fichi wa koo na majina makubwa ya makada wa vyama na wakubwa wa serikali ambayo kimsingi inawachukulia kama punda vihongwe wa kubeba koo husika.
Chanzo:Tanzania Daima Feb., 26, 2014.

Katiba mpya: Mgosi kwenda na mkewe

BAADA ya kijiwe kufanyiwa mtima nyongo na kuenguliwa kushiriki Bunge la Katiba, mmoja wetu Mgosi Machungi amejipenyeza kama mzee Kimdunge Ngumaru Mwehu aliyepitia chama cha waganga wa jadi. Mgosi Machungi ametuacha hoi kwa kuingia Bunge la Katiba kupitia chama cha wapiga ramli.

Kwa vile Mgosi Machungi anaenda kwenye neema ameishaanza kudengua hata kuotesha kifriji. Anaingia akitembea kama anayecheza kidembwa kama si mdumange.
Haamkui wala nini zaidi ya kuagiza kahawa na kujifanya yuko bize akisoma mnyuzipepa wake wa Danganyana Daima. Si unajua Mswahili akiangukia!
Akiwa amekula jiwe na kujifanya mbukuzi, Mbwa Mwitu anamchokoza akisema: “Mgosi sasa hii kashfa. Yaani unatukuta waheshimiwa kama sisi unajikausha hata huamkui!”
Mgosi anajibu: “Sasa unyonge basi. Ukiendeea kutifatafata titakutoa mpaka tikubindize kabua ya kutoboa mimacho ili kujibu mapigo. Siku hizi sina mchezo. Ukinikera naamuisha wahuni wenzangu. Titakufanyia kitu mbaya kama si ku-Mwangosi au hata ku-Ulimboka.”
Mbwa Mwitu na wanakijiwe hatuna mbavu. Anasema: “Kumbe umekuja na mawazo mfu ya Njaa Kaya kichwani! Ujibu mapigo kwa lipi na unyonge upi wakati sote hapa tunaheshimiana wala hatuibiani wala kuchakachuana kama Njaa Kaya na genge lake dhidi ya wapingaji wake?”
“Usanii sasa basi. Lazima tupate Katiba mpya itakayowabana wezi wakubwa ambao wanaotuibia na kututumia watakavyo. Kila anayekuja anatajirisha ukoo wake na hata waramba makalio yake. Ushenzi na ujambazi huu hadi lini?”  Anachomekea Kapende huku akibwia tangawizi yake kwa madaha. Leo zimemtembelea.  Hanywi kahawa chungu. Hata alivyouramba kwa kuchomekea utadhani limbukeni aitwaye Pedejee!
“Hakuna cha Katiba mpya wala nini.  Ni ulaji kwenda mbele. Mambo yalivyo, wachovu wasipoingia mitaani, wataingizwa mkenge kwa Katiba mbovu kuliko iliyopo kama alivyosema fyatu Living stone Ushindwe hivi karibuni kuwa genge lake limejiandaa kuichakachua Katiba kulinda masilahi yake.” Anazoza mzee Maneno.
Msomi aliyekuwa akibofya ki ipad anakula mic. “Hakuna waliponiacha hoi kutaka eti kumpigia debe fisadi Endelea Chenga kuwa spika wa Bunge la Katiba.  This is nonsense crap and malicious! Hivi ukishakuwa na spika jambazi unategemea uwe na Katiba ya kuweza kuzuia ujambazi, bwimbwi na ujangili wakati mtu wao ndiye ameshika patamu? Hapa naona unafiki na kigeugeu cha Njaa Kaya. Amewaingiza mkenge wachovu kuwa anataka kuwapatia Katiba mpya wakati si kweli.”
Kanji anakwanyua mic na kusoza: “Somi sasa changanya sisi. Tukufu iko taka kuwa na constution zuri. Lazima shukuru yeye hata kama napinga yeye.”
“Wapashe wamezidi hawa.” Anachomekea Sofia Lion aka Kanungaembe.
“Sofia acha kumchomekea Kanji au kwa vile ni mshikaji wako?” anatania Mbwa Mwitu.
Msomi anapuuzia utani na kuamua kujibu mapingo. Anasema: “Tuwe makini tunapowahukumu wengine.  Simhukumu Njaa Kaya bila ushahidi. Hivi kama Kanji anavyodai kuwa alitaka kutupatia katiba bora, iweje ateuwe zaidi ya 75% makada wa genge lake badala ya watu wasio na upande ili haki itendeke? Kwani Katiba ni ya mama yake au genge lake?”
“Du! Hapa umemshika pabaya Njaa Kaya! Kweli haya maigizo. Hukusikia jamaa aliyeteuliwa yeye na mkewe kwenda kufaidi njuluku zetu?” Anachomekea Mchunguliaji.
Mpemba aliyekuwa kimya anaamua kuchangia: “Mie hakuna kitu kilintisha kama watu kujadili jambo moja, yaani Muuungano. Nadhani kama twataka songa mbele basi tuunganishe kaya iwe moja badala ya kuwa na sirikali tatu zitazozidi tuongezea nzigo ati au mwasemaje jamani? Hili la nke mbona kawaida hata Njengoni?”
Mijjinga anaamua kutia guu kwa vile alichelewa kufika kiasi cha kukuta mada ishaanza hivyo akalazimika kuifuatilia kabla ya kutia guu. Anasema: “Ami unfurahisha sana leo wallahi. Ila haya usemayo usiende yasema kule kwenye visiwa. Hujakosea. Watu wawezapeleka hata hawara zao mjengoni na hakuna ubaya.” Anaongea akimuigiza Mpemba ambaye anacheka tu.
Mipawa anachomekea na kusema: “Actuare hapa umeongeaga pwenti. Watu wamekuwa wakijadili muungano hadi wanasahau maulaji ya rahisi, mfumo wa kifisadi, kurejesha maadili, kuondosha madili, kupunguza utitiri wa wilaya na mikoa na madudu mengine kama vile rahisi na wakubwa kutolipa kodi na kutumia vibaya njuluku za wachovu.”
Wakati wengi wakichangia kuhusu Katiba hawakuwa na habari kuwa Mgosi Machungi alishaukwaa ubunge wa Katiba. Hivyo, naye kwa kutambua hili anaamua kutamba. Anasema: “Tisikiizane. Hapa tinapoongea mjue minaongea na mheshimiwa Mgosi Machungi Shemtwashua wa Kiango mbuge asimi wa Bunge la Katiba. Kwanza, nipigieni makofi.”  Kila mtu anapigwa na butwaa. Wengine wanadhani ni utani.
Sofi Kanungaembe anamzodoa: “Mgosi acha ulimbukeni utapigwa makofi. Uchaguliwe Bunge la Katiba una sura, dola au sera. Halo halo!”
“Kwei duniani kuna watu na viatu. Pigeni makofi siyo mnipige makofi, hujui Kiswahiii nini? Niko nafanya mpango na mke wangu Mama Andallah naye ateuliwe ili tule kuku kama yue Mkaidi aliyependekeza jina la mkewe.” Anachomoa kitambulisho chake huku akimpa Sofi ajionee mwenyewe.
Sofi anapigwa bumbuwazi na kusema: “Mwenzetu kumbe umo kwenye ulaji!  Nijuavyo, wengi hamuendi kupoteza muda kutoa mapovu kuchangia bali kufaidi posho au vipi mshikaji.”
“Sofia tiheshimiane. Hivi mama Andallah akimisikia unadhani ataacha kukupiga zongo? Tinaende kue kutetea haki zenu waa sina njaa kama chama chenu. Tinaenda kue kubomoa mfumo huu wa kifisadi ambao umeticheesha kimaisha na kumaiza rasiimali zetu.”
Mipawa anachomekea: “Kweli muendage kututetea badala ya kwenda kutafuta vidosho kama waishiwa ambao juzi juzi walifichua kuwa kila mmoja ana wake mjengoni. Je, utampa fisadi mzee wa Vijesenti au Sam Sixx?”
“Hayo matusi sasa.” Anang’aka Mgosi. “Namaanisha kura,” Anajitetea Mipawa. “Yue hata kigombea na mbwa nitamchagua mbwa kuiko yeye.” Anajibu Mgosi huku akitoa oda ya kahawa kwa wanakijiwe wote ili wafaidi neema iliyomtembelea.
Msomi kapata upenyo. Anazoza: “Tuache utani. Kama fisadi wa vijisenti atasimikwa mjue hakuna Katiba. Hapa unafiki wa Njaa Kaya ndipo utakapofichuka. Kama wachovu hawatakuwa tayari kuingia mitaani kupinga Katiba mchakachuo kama mikakati ya sasa ya mafisadi kupenyeza watu wengi itafanikiwa, mjue mtakuwa mmeliwa mara mbili, yaani mtaikosa Katiba na mtaliwa njuluku bure.”
Kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga si tawi la mwembe likakatika.  Tulidhani mabomu ya ndata au al Shubbub!
Chanzo: Tanzania Daima Feb., 26, 2014.

When a clone meets he who cloned it


Ally Hassan Mwinyi, the professor of political embryology is welcomed by his clone, Adam Malima. Mwinyi is credited for having cloned guys like Jakaya Kikwete, Adam Malima, Yusuf Makamba whose son was later cloned by Kikwete and many more suspicious characters in the ulaji in the hunk.

I Love This Stuff

Tuesday 25 February 2014

Ukuaji wa uchumi unapokuza umaskini

 
          Juzi nilifurahi sambamba na kuchukia. Ni pale runinga ya Afrika Kusini ilipoonyesha kuwa uchumi wa Tanzania utakuwa kwa kasi kuliko chumi zote duniani miaka michache ijayo. Baada ya kuona hili nilianza kuangalia uzuri na ubaya wa kukua uchumi kwa kasi kwenye taifa linaloongozwa kifisadi. Je uchumi wetu utakapokuwa nani atafaidi kati ya wananchi na makuwadi wa wawekezaji ambao wamehakikisha kila kitu kinawanufaisha wao na mabwana zao? Rejea kugundulia utitiri wa madini ambao matokeo yake ni utitiri wa mashimo na kashfa kiasi cha kuwaacha watu wetu maskini na wakimbizi kwenye nchi yao. Nani amesahau mauaji ya watu wasio na hatia kule Mara kwa kosa la kukatisha kwenye mgodi? Nani amesahau magonjwa ya hatari yanayowasumbua wakazi wa huko huko Mara ambao kemikali zimenyiririshwa kwenye vyanzo vyao vya maji?
          Je kuna haya ya walalahoi kushangilia habari hii au kuomboleza kwani kukua kwa uchumi wa Tanzania kwao ni chachu ya kukua kwa umaskini? Hivi unategemea nini toka kwenye nchi inayogawa raslimali zake bure au kuharibu mali za umma kama vile kuuza mashirika ya umma kwa bei ya kutupwa kama ilivyotokea kwenye uuzaji wa iliyo kuwa Kampuni ya Usafiri Dar es salaam (UDA), NBC na mashirika mengi?
           Taarifa za ukuaji wa uchumi wa Tanzania zilizotolewa mwaka 2012 na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Morrice Oyuke zilionyesha kuwa uchumi wa Tanzania ungekuwa kwa asilimia 7.1. Hili ni jambo la kujivunia. Kinachogomba ni kwamba huyu mtakwimu hakueleza ni kiasi gani umaskini utakuwa. Wapo waliosema kuwa umaskini ungeongezeka kwa asilimia 5 na ushei sambamba na ukuaji huu. Je hii inatoa picha gani? Wapo wanaoona kama takwimu tunazoletewa ni za ungo wa kawaida. Na hii inaweza kuwa kweli hasa tukizingatia jinsi takwimu zinavyoweza kuficha ukweli kama alivyowahi kusema, Joel Best kwenye kitabu chake cha Damned lies and statistics, “Mujumuisho ni hatua muhimu katika kufikiri kitakwimu. Mara chache twaweza kuhesabu matukio haya yote ya kijamii. Badala yake, tunakusanya baadhi ya ushahidi kutokana na sampli na kutoa hitimisho la jumla,” (uk.6). Sambamba na hili Benjamin Disraeli (1804–1881) waziri mkuu wa Uingiereza aliwahi kusema, “There are three kinds of lies: lies, damned lies, and statistics.” Hatuna tafsiri ya nukuu hii.  Pamoja na kwamba si takwimu zote zinaficha uongo, kuna haja ya kuwa makini na takwimu hasa katika kuzilinganisha na ukweli halisi.  Kwa wanaojua udhaifu wa takwimu, wanajua ninachoongelea hapa. Takwimu zinaweza kuonyesha picha tofauti na hali halisi kama ilivyo kwenye suala la kukua uchumi wa taifa. Ukitaka kujua uongo wa takwimu hebu nenda vijiji uangalie aina ya maisha wananchi wanayoishi. Huwezi kukuza uchumi kwa takwimu bali uzalishaji na matumizi bora na nidhamu ya pesa na raslimali za umma jambo ambalo ni msamiati mgeni nchini.  Huwezi kukuza uchumi kwa midomo au kisiasa au kwa kupika takwimu. Mwandishi wa makala hii ni muumini wa dhana tofauti na takwimu. Anaamini kuwa ukuaji wa kweli wa uchumi hauelezeki kwa takwimu tu bali unaweza kuelezewa vizuri na wakati maskini wa vijijini au mabandani mijini. Hali za maisha ya makundi haya ya wasio nacho zinaweza kutupa picha nzuri na ya kweli kuhusiana na kukua kwa uchumi. je wanapata huduma bora? Je wanaridhika na mambo yanavyokwenda? je wanashirikishwa kikamilifu? Je wanawezeshwa? je wanapewa taarifa muhimu? je wana welewa wa taarifa husika kiasi cha kuzichambua na kuzifanyia kazi ikiwamo na kuzikubali au kuzikataa? Haya ndiyo mambo ya kuzingatia katika kutoa tafsiri ya kukua kwa uchumi. Je waliotoa taarifa za ukuaji wa uchumi wetu wameyazingatia haya? Jibu ni hapana tena kubwa tu.
          Kwa wanaojua udhaifu wa uwekezaji nchini, bila shaka wanategemea ongezeko la wamachinga wanaojiita wawekezaji toka India, Pakstani, Bangladesh, China na kwingineko. Pia wanategemea utoroshaji wa mtaji na raslimali kuongezeka kutokana na mamlaka zilizopo kupoteza muda kwenye kusaka rushwa badili ya kukusanya mapato na kubana mianya ya kutorosha mitaji na mali za umma. Uliza madini kama Tanzanite yameisaidia nini Tanzania zaidi ya kuwa laana na msaada kwa nchi jirani ya Kenya na India?
          Je uchumi wetu utakuwa kiuchumi au kisiasa? Kwa wanaojua ukuaji wa uchumi wa kisiasa ambao ulielezewa na rais Jakaya Kikwete aliposema kuwa ukiona mitaa yetu finyu imejaa misongamano ujue uchumi umekuwa kiasi cha watanzania wengi kuwa na mikangafu. Tofauti, ukuaji wa kisayansi ni ule unaowezesha nchi kuongeza pato lake na kupunguza utegemezi katika misaada au kuagiza zaidi ya unavyouza. Je Tanzania nchi iliyojaa bidhaa zilizo chini ya viwango kutoka India na China kweli inaweza kuwa na ukuaji wa kujivunia kwa watanzania?
Tujalie kuwa uchumi wetu kweli utakua, je utafua dafu kwenye matumizi mabaya ya kisiasa ambapo tumezalisha mikoa na wilaya nyingi kukidhi mahitaji ya kisiasa badala ya matakwa ya wananchi?  Je ukuaji huu uliotabiriwa utaondoa au kupunguza uombaomba wa nchi yetu ambapo bajeti yetu hutegemea michango ya wafadhili kana kwamba hatukujaliwa raslimali?
Tukifie mahali tuuangalie ukweli kama ulivyo kwa kujitenga na kujipigia debe kisiasa ili wahusika wachaguliwe tena wafanya madudu tena. Swali linalopaswa kuulizwa na kujibia kwa utuo ni: Je uchumi wa Tanzania unapimwa na nani na nini katika ukuaji wake? Je ukuaji, kama upo, unamnufaisha nani na vipi?
Ukuaji wa uchumi unaowaacha nje maskini ambao wanaona umaskini na uduni wa huduma vikiongezeka hauna maana. Watawala wetu wanapaswa kufikiri kabla ya kutuletea takwimu za ajabu ajabu zilizokaa kikampeni zaidi ya sayansi. Je inakuwaje uchumi wa Tanzania unakuwa sambamba na umaskini?
Chanzo: Dira Feb., 2014.

Kufungwa mtoto wa rais faida ya kuchagua upinzani

Taarifa za kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili kwa mwana wa aliyekuwa rais wa Zambia Rupiah Banda aitwaye Andrew (53) ni faraja kwa wanaochukia ufisadi na utawala wa kifamilia ambapo madaraka ya mtu mmoja hutegemewa na kutumiwa na ukoo mzima.
Andrew Banda alifungwa kwa kosa la kutumia madaraka ya baba yake na kujipatia rushwa ya mamilioni ya shilingi toka kwenye kampuni moja ya ujenzi ya kitaliano. Je kwanini tukio lililotokea Zambia livute hisia za wengine nje ya nchi? Jibu ni rahisi kuwa kutokana na utawala wa kifisadi kutamalaki ambapo watoto au wake wa marais nao hugeuka marais wadogo na kujipatia utajiri wa haraka kwa njia haramu, kusikia kuwa mmoja wao hata kama ni kutoka nchi nyingine ni ushindi wa aina yake.
Zambia imekuwa mbele kwenye suala la utawala bora na demokrasia. ni nchini Zambia ambako mke wa rais amewahi kuhukumiwa kifungo na akafungwa kweli. Hii ilitokea mnamo Machi 3, 2009 ambapo Regina Chiluba mke wa rais wa zamani Fredrick Chiluba alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu na nusu kutokana na kutumia madaraka ya mumewe kujipatia mali kinyume cha sheria. Je Afrika inao akina Andrew na Regina wangapi ambao hawajafikishwa mbele ya haki? Tunawaona wakituibia au kutumia ofisi zetu kujipatia utajiri kupitia NGO na biashara za ajabu ajabu kama kuwatumia makuwadi wao kununua mashirika ya umma kwa bei ya kutupwa kama ilivyotokea hivi karibuni kwenye kashfa ya uuzaji wa kutupwa wa UDA ambao nyuma yake  kuna mtoto wa mkubwa fulani ambaye ikifika wakati wa kumtaja tutamuanika. Kinachokera ni kushuhudia wezi hawa na makuwadi wao wakitukoga hata wakati mwingine kutunyanyasa, na kutudhulumu hata baada ya kutuibia kama umma.
Wakati Andrew Banda akifungwa kwa kujipatia $ 63,000, Regina alikuwa amejipatia dola 300,000. Hii ni rushwa moja. Je ni rushwa kiasi gani ambayo haikufichuka?
Kitu kinachovutia na cha kuigwa mfano ni namna mamlaka zilivyogundua ufisadi wa Andrew. Alikutwa akiwa na dola 63,000 kwenye akaunti yake. Alipotakiwa aeleze alivyozipata alishindwa na hivyo mahakama kuhitimisha kuwa alizipata kihalifu. Hivyo, ikaamua kumkuta na hatia. Je watoto na wake wa watawala wa nchi kama yetu inayosifika kwa uwekezaji wa kijambazi wana akaunti nono kiasi gani? Je tunaweza kuwakamata vipi? Jibu ni rahisi. Chagua upinzani kila kitu kitafichuka. Zambia haikupiga hatua hii ya kupigiwa mfano kwa ujanja zaidi ya kuwa na serikali ya upinzani madarakani. Tumeyaona kama haya nchini Malawi hata kama hayakufikia ukubwa wa Zambia.
Hivyo, njia rahisi kwa watanzania kupambana na kizazi cha kijambazi kitokanacho na ndugu na jamaa wa wakubwa kutumia nafasi zao kuibia umma ni kuondoa chama tawala madarakani ili kila kitu kifumuliwe upya. Tumekuwa tukilalamikia kashfa kama EPA, Richmond, Kiwira na nyingine nyingi. Uking’atua CCM kila kitu kinakuwa wazi na wale waliojiona hawawezi kunyea debe wanajikuta gerezani. Najua watanzania wengi wanakasirishwa na wizi wa kilafi na kiroho mbaya ambapo wengi wa wanaoiba hawaibii shida bali roho mbaya na tabia mbaya.   Haiwezekani umaskini uendelee kuongezeka huku genge la majambazi likiwashika matake taifa na kusiwepo na harakati za kukomesha jinai hii. Sasa ni juu ya watanzania kujilaumu kutokana na kutopenda mabadiliko. Bila kubadilika na kubadili utawala uliopo wengi watazidi kuumia. Tukichagua upinzani kashfa zote kama zile za kuficha fedha nje, mihadarati, mikataba ya kijambazi na uwekezaji wa kiwizi vyote vinafumliwa na haki inatendeka. lakini kama tutaendelea kuchagua status quo pro quo itakuwa ni kuteseka sana na sana huku wahalifu na mafala waliopata ukwasi si kwa ujanja wao bali vyeo vya baba zao au waume na jamaa zao wataendelea kututambia kwa chumo la wizi utokanao na pesa yetu wenyewe. Mafala watatugeuza mafala kiasi cha wao kuonekana wajanja wakati ni wahalifu wa kawaida tu.
Andrew kabla ya kukutwa na hatia alikuwa anatumbua na kuonekana mjanja wakati ni mhalifu wa kawaida.kabla ya Regina kupatikana na hatia alikuwa akiabudiwa kama first lady wakati ni mwizi wa kawaida tu. Tutaendelea na utawala wa kijambazi hadi lini? Tumezidiwa na wakoloni ambapo mke wa gavana wa kikoloni wala wanae hawakuwa magavana wadogo wala wabia wa wahalifu waliowatumia kama makuwadi wao!
Kwa umri wa Andrew ni aibu kumtegemea baba yake wakati ni mtu mzima mwenye akili anayepaswa kujitegemea. Wenzetu ni wa kweli kwao binafsi na wale wanaowaongoza. Mfano mwingine ni wa Hilary Clinton. Alipokuwa first lady wala hakutumia madaraka ya mumewe ingawa alikuwa akipenda madaraka. Baada ya muwe kumaliza muda wake, Hilary aliamua kujaribu kugombea urais na kushindwa. Hata hivyo, alijijengea heshima kuwa hakutumia madaraka ya mumewe kutimiza malengo yake ya kisiasa kama wanavyofanya wake za watawala dhalimu na fisadi. Hilary hakuiba hata dime moja ya wamarekani. Hakuanzisha NGO wala binti yao Chalsea hakutanua na kuiba kwa jina la baba wala mama sawa na wengi tunaoshuhdia.
Tumalizie kwa kuwahimiza watanzania kuchagua mageuzi ili kuondoa mfumo mbovu uliotamalaki wa kuhudumiana ambapo utawala unageuka mali ya ukoo ambao nao unageuza taifa kuwa shamba la bibi. Tukichagua upinzani tutaweza kuwakomesha akina Andrew na Regina wetu kiasi cha kurejesha heshima na maadili katika utumishi wa umma. Hatuwezi kuendelea na mazoea mabovu yaliyopo ambapo wachache wananufaika kwa kuuibia umma. Lazima tuwajibishane na wakati wenyewe ni huu.
Chanzo: Dira Feb., 2014.

Monday 24 February 2014

Hold your horses Jake Kiquette

RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KUFUATIA KIFO CHA PADRI MUSHI ...

           I evidenced Presider Jake Kiquette who always smiles and laughs even at the time one’d not dare to, being turned into a spitfire. During opening the National Executive Committee of his outfit in Dom the guy shocked many especially the message he put across. Wrinkles on his face, speaking in tongues and parables, he moaned, “Unyonge basi.” His displeasure sated by hard times ahead for his outfit, Chama cha Mapi (CcM) plus being blooded by one Brit paper that enjoined him with poachers alleging are his friends, the man had all reasons to breathe embers. His first step’s to paint opponents with the same brush accusing them of being quarrelsome.
 Vomiting vile or saliva’s one’s choice. Again, when it comes to fabricating things, nobody’s at liberty to do it. For, it hurts others. The good man said that the opponents are belligerent and chaotic while actually this might mean opposite.  Although Kiquette’s regime has always wanted to level the opponents off, it needs to use scientific and reasonable means instead of lies and far-fetched things such as calling them names.
The great man’s quoted as saying, “Let’s us not be afraid…let you journalists leave all the news, but say this…we won’t be cowed…patience has its end. “Wow! Did he mean that boozers’ patience of evidencing all messes aka madudu his outfit’s always made should come to a grinding halt? If this is what he meant, kudos.  Did he mean that boozers shouldn't be afraid to task him to come clean on allegations by a Brit paper that said he’s in bed with poachers? Does it mean that when he went to London to campaign for  the "abolition" of ivory trade he’s shedding cloc’s tears? Such damning allegations forced one fyatu Silvia Rweyemaaamu to surface and mount weak and skinny defense  that left us in shock especially when he pointlessly said that allegations that the doctor who cloned him has a soft spot in fighting poaching is “none sense, crap and malicious” without knowing that he’s trying to jump a smoking gun. He very well knows. Media especially international ones don’t jump on drawing conclusion without having all fact  rightly abreast. What he ended up doing’s just paint the wind and please his boss who’s not a savvy as far as media is concerned. This Nshomile who happen to be a scribe that betrayed the trade uses massaburis to think more than anything. I’m not trying to belittle him. Since he devoured his own vomits for the sake of being where he’s, I've nary forgiven him. Such ethical prostitution will piss off anybody who cares about ethics so to speak.
If I were present at that face-the-media pub, I’d have asked him how he feels to be used like a diaper. I’d have added to ask if he reads the articles he wrote before he became a tool in somebody’s hands.
Again, if Jake meant to order cops to kill like they did in Arusha, this is unacceptable. If he means to unleash death squad which butchered Daud Mwangosi, it is sad and megalomaniac. Who wants to see Mike Kamuhanda being promoted just for felling other boozers?
After CcM became a grotesque caricature of its giant and energetic former self, it seems, it’s decided to die with others. Who’d think that such old outfit would become so bankrupt that it relies on archaic and bush tricks such as using cops to humiliate, kill and demonize opponents so as to carry the day? While this goes on chakachuazation, tops up in the game. Is this that Kiquette wants boozers to be tired of? If this is what he meant, he said the right thing. But if he meant his sycophants, ala Rweyemaamu, should go and attack opponents, he’s but bankrupt as he once accused others of.
 One thing boozers are asking themselves is: Suppose you’re given gold on the silver platter, will you take the gold and throw the platter away or keep both? Some stupid beings will take the platter and throw the gold away. Now that Jake told us not to be afraid, why should we? We need to question everybody and everything in our hunk even if we’re not the members or sycophants of his outfit. We need to not be afraid even if it means to turn tables against the man himself.
When Jake spat embers boozers met at their swallowing joint to discuss his move. One fyatu wondered why Jake’s nary been as furious as he was when evil things such as smuggling our animals are done. He went on questioning Jake’s silence about many things such as EPA, Richmonduli, Meremeta, Mwananchi Gold and other stinking scams. While we mused about this challenge one boozer decided to give us an answer. He said that Jake has nary taken on those who committed this sacrilege.  After all, those scams mentioned were conceived and executed simply because those behind them were untouchable that nobody should touch.
Jake was right. Boozers won’t be cowed. So too, they’re not afraid of taking on those robbing them just like those who are afraid of them so as to complain.
Source: ThisDay Feb., 24, 2014.

Sunday 23 February 2014

Be serious this time Prof Tiba-Ijuka?












          























I’m sure Prof Ann Kajuamlo Tiba-ijuka, minister of Hekalus, Mbavu za Dog, Lands and Heavens  knows me. I know. You read my stuff not once or twice. I’m also sure. You know that boozers and I take seriously whatever you say. So too, you verily know that we love you so much so that we offer you our free nuggets of wisdom whenever you need them.
Good prof, you said recently that you’re going to demolish all buildings in open spaces and other grabbed lands.  Tawile! Well done big girl shall you live up to your words. If you don’t bring down those mijengos, beware. I’ll commit suicide. Given that you love and value me, you’ll live up to your words to save my precious life even if I'm a boozer.
You said that you’ll take on land grabbers mercilessly. Boozers are waiting anxiously to see how you’ll take on bigwigs such as Gettie Rwakaterehe and others with villas and castles in posh areas such Masaki, Upanga, Mikocheni, Msasani, Mbezi Beach and elsewhere. Guess what. When you fulfill your promise, true, we’ll invite you for kanywaji so as to show the world that you’re not done politically. We’ll shame your detractors who think you’re but a political cadaver if not a casualty.
Given that I've been reminding you to bring down the uhindini ghorofa to no avail, now hopefully, you’ll bring this killer building down just soon. Given that you've discovered how fat land grabbers use our courts to frustrate your efforts, we encourage you to stand your ground and see to it that no bin-Adam is stopping you however big or powerful that person is. I know. You know. Our hunk is now a laughing stock almost in everything. Did you hear how poachers killed our elephants and rhinos while those supposed to apprehend them end up complaining?  You know how our airports have become harbours of illegal trades in drugs, ivory, minerals and whatnot. I know you. You've nary become a person that complains. I also know that you know what transpired when a good Dr. Harry Mwakiembe boasted that he’d take on drug barons who ended up taking him down shamelessly as he vanished shamefully.
Good prof, you’re quoted recently as saying that you erected billboards notifying people who built in open areas to demolish their houses to no avail.  You went ahead chest beating saying that you’ll demolish those buildings and those who said you’re done politically should take a note that you’re not done yet. Bravo big girl.
You added “We will demolish houses I've seen in Mbezi areas and others without looking at the face of a person. We won’t waste time with those with fake title deeds. Instead we will  meet with before the court after demolishing.”
Such words are bold and encouraging if you'll live up to your promises. After all, boozers are tired of empty promises. They’d like to see you swing into actions.
Great prof, I need to warn you. Before you swing into actions make sure that the cops you’re going to use are not beating people up. If they do, your operation will end up a cropper just like Operesheni Tukuza Ujangili. You know what befell four ministers. Some gossipers in boozing circles are saying that the bigwigs were booted out not just because they violated Bin-Adam’s rights. Nay! The gossipers say that the guys were shown the door for trying to take on untouchable who happen to be connected. As one paper in the land of Brits put it, poachers are protected by powerful people who also happen to be their conspirators and biz partners. I don't mean your boss. Spare me.
So big girl, when you start taking on those land thieves aka land grabbers try to avoid all traps aimed at halting your noble cause for our hunk if you mean what you said and said what you mean. Again, though you broke my heart when you swore to bring down the ugabacholini building and failed, I still trust you. I understand. There are general elections next year. Watch your steps. Some party bigwigs could descend on you saying that if you demolish those buildings those owning them won’t give your outfit votes. Yeah! This once happened a few years ago when matching guys and those who live in  informal dwellings especially in Jangwani  marshlands were supposed to be moved forcefully. Again, given that such a move was to take place close to general elections, those who wanted to purge mabondeni dwellers were stopped for the same reasons, votes for Numero Uno. You know what I mean.
Great profwessor, thank your lucky stars I heard another minister who answers to the name Bin Lithmus Mahenge saying that he, too, will expel all top dogs who erected their infamous hekalus on our beaches. Team up with him and show those sons and daughter of the hell the heck. Usikubali kuingiliwa dear.
Source: The Guardian Feb., 23, 2014.

Saturday 22 February 2014

Ukraine: Nguvu ya umma yamng'oa rais

... Tymoshenko – Letter to Ukranian President Viktor Yanukovych | News
Sasa si gumzo wala majungu. Viktor Yanukovych's aliyekuwa rais wa Ukraine ameangushwa na umma. Hii ni baada ya kukumbwa na maandamano ya zaidi ya miezi mitatu. Yanukovych alipatwa na yaliyomkuta baada ya kupinga juhudi za Ukraine kujiunga na jumuia ya Ulaya (EU). Pamoja na msimamo wake mkali akiungwa mkono na Urusi, Yanukovych alijikuta akipinguduliwa kutokana na mapigo mawili moja likiwa ni bunge kupiga kura ya kumuondoa madarakani na pili waandamanaji kuendelea kukaa mitaani pamoja na baridi kali kwa zaidi ya miezi mitatu. Msumari wa mwisho kwenye geneza la Yanukovych kisiasa ulipigwa baada ya kuachiwa kwa hasimu wake mkuu waziri mkuu wa zamani Yulia Tymoshenko aliyewashukuru wananachi kwa kuleta mabadiliko na kuomba wasiondoke mitaani hadi kieleweke zaidi.

Mlevi kuanzisha jeshi la kupambana na Jinai

Seriously, nilikuwa nchini Mexico juzi ambapo nilialikwa na rais wa nchi hiyo kumpa ushauri kuhusiana na jinsi ya kuboresha jeshi lake la Sungusungu la kupambana na wauza bwimbwi. Je ni kwanini aliamua kuniita? Alisema ni kwa sababu baada ya kusoma mojawapo ya vitu vyangu alipata wazo la kunialika hasa baada ya kuambiwa na mmoja wa waanzilishi wa Sungusungu wa kupambana na wauza bwimbwi kusema alipata wazo hilo toka kwenye makala yangu mojawapo.
Huwezi kuamini kuwa nilikuwa nimeishasahau kutokana na kuwa na mitikasi mingi ya kufanya. Si unajua tena mashine kubwa lazima ifikiri na kuchemka kama haina akili nzuri. Hata hivyo, nilifarijika kugundua kuwa kuna watu wanafuatilia ushauri wangu hata kama walengwa wangu wa Bongolalaland wanasoma na kusonya huku wakiendelea na business ya kuuza bwimbwi as usual. Hata hivyo, wakae wakijua kuwa kiama chao kinakuja kama walevi watanielewa na kuamua kujikomboa.
Hali ilikuwa mbaya sana hasa katika jimbo la Michoacan ambako nilishuhudia wakuu wa magenge ya kijinai wakikamatwa na kunyotelewa roho mchana kweupe. Hata ndata waliokuwa wakila nao baada ya kugundua kuwa walevi wanaweza kuwachenchia kibao, walilazimika kujiunga na sungusungu hawa waliozaliwa na wazo langu. Maana kushuhudia watu wakiuawa kupigwa au kutozwa pesa ili kuendesha maisha yao ya kawaida kulikokuwa kukifanywa na magenge ya wauza unga ilikuwa jambo la kawaida. Baada ya wananchi kuchoshwa na uonevu na unyama huu, waliamua kufuata ushauri wangu. Hivyo, hata walevi kujikomboa kutokana na kutenzwa kinyama na magenge ya kiharifu kama vile ndata, wauza bwimbwi, sirikali na manyang’au wengine lazima kukomeshwa mara moja.
Baada ya kutoa muhtasari wa kwanini nataka kuanzisha Jeshi la Kupambana na Jinai kwa kikameruni Force Against Crimes in Tanzia (FACT). Tofauti na wenzetu wa Mexico, sisi tutapanua wigo na kupambana na wauza bwimbwi, mafisadi, walioghushi, wala rushwa, vyangudoa wa kila aina kuanzia wa kimaadili hadi wa siasa.
Kwa vile wanaouza bwimbwi, kupokea rushwa, mafisadi, walioghushi na hata wanaofanya usharmuta wa kila aina wanajulikana, FACT itakuwa ikivamia makazi yao na kuwakamata na kuwapa kichapo kabla ya kupitisha hukumu ya umma kama wanavyofanya kule Mexico.
Najua wengi wanaweza kuchukulia wazo hili kama la kilevi na lisilowezekana.  Kwa vile kwetu wameshindwa hivyo lazima tuwasaidie. Tuna hakika tutafanikiwa kwenye vita hii ya kuikomboa na kuigomboa kaya toka kwenye mikono ya waovu hata kama baadhi yao wana maulaji na mamlaka. Sisi hatutabakisha kitu. Tutapambana na yeyote kumuonyesha kuwa kaya hii ni ya walevi na si ya watenda jinai.
Je unajua ni kwanini watendaji wako wameshindwa? Rushwa rushwa ndugu zanguni. Mijitu imehongwa kiasi cha kukamatwa mateka. Hamkusikia wale waliojitapa kuwa wana orodha ya watenda jinai wote kuanzia wauza bwimbwi, mafisadi, wala rushwa na hata majambazi lakini wakashindwa kuwashughulikia? Sasa tunasema bila kumung’unya maneno kuwa naye tutamwendea atupe sababu nuzuhu za kutowashughulikia hao waharifu kama si wenzake. Hatutaangalia mtu usoni wala kujali cheo na hadhi ya mtu. Lazima kuikomboa kaya toka kwenye mikono michafu ya magenge ya kijambazi.
Najua mtauliza: Je wanafaidika vipi? Si wanakatiwa na kukatiana vitu na uchache huku wakiuacha umma wa walevi uteketee huku wao wakipeta na kuwa mabilionea bin vuu. Sasa muda wa kuendelea kutumiana, kulana na kuuza umekwisha. Lazima walevi wachukue hatua mujarabu.
Kwa vile wale walioaminiwa madaraka wameyachezea au kufanya kile ambacho wakameruni huita to sleep on the wheel, walevi kujichukua hatamu na kukomboa kaya yao. Lazima kuondoa huu wendawazimu ambapo kaya imechafuliwa kiasi cha kukosa hata maana. Hebu fikiria, kwa mfano, washenzi wanaua elimu kwa vile wanasomesha vitegemezi vyao nje na kujenga taifa la wajinga. Je namna hii tutafika? Heri walevi tuingilie kati maana ulevi ni bora kuliko ujinga ingawa na ulevi wenyewe unategemea. Hatuwezi kuendelea kushuhudia elimu yetu ikizama huku sirikali yetu ikijaa vihiyo walioghushi wanaotuuza kwa wachukuaji. Lazima tufanye kitu na kitu chenyewe ni kupitia harakati za FACT kuwanasa na kuwapatiliza wote walioleta balaa na zahma hii.
Hatuwezi kuvumilia kuona mijitu vihiyo mafala na majambazi ikitukoga kwa utajiri ambao ni matokeo ya jinai tena dhidi ya walevi. No. It can’t be us. We’ll fight too see to it that we emancipate ourselves so as to see true manumission of Bin-Adam even if we are boozers. In fact, FACT is there to bring about some real and desired changes in Danganyika. I promise. FACT’ll take thugs’ crown away just soon.
Hatuwezi kuacha mambo kuendelea kienyeji na kijambazi kama yalivyo. Hakuna kilichoniacha hoi kama juzi tu kikundi cha vitoto kiitwacho Mbwa Mwitu kuwatoa jasho. Tukio jingine ni lile la muuaji wa halaiki wa kule kwa akina Mura Mwita aliyenyotoa roho walevi zaidi ya kumi bila kudedishwa. Angekuwa amepambana na FACT angeishakuwa past tense zamani gani. Tunataka kuwaonyesha hawa wapuuzi wanaochezea ulaji jinsi warume tunavyofikiri na kutenda. Tunataka tuwaonyeshe tusivyofikiri kwa massaburi kama wao. Sisi ni vichwa wala si massaburi kama wao. We’ll show them what it means to be thinkers who use kanywaji to warm their brains up. Leo jamani tuvumiliane kwa kuongea sana ukameruni. Ni kutokana na hangover niliyoipata pale Heathrow wakati nikirejea zangu toka Mexico. Hamuoni wale wanaorejea na hangovers kutoka Jersey, Uswisi na nchi nyingine wanakoficha njuluku wanavyoiba zaidi na zaidi kiasi cha kaya kuanza kuwa na mabilionea wezi watupu? Hivi kweli mbunge Kwa mfano, anaweza kuwa bilionea bila kuiba kwa kutumia uishiwa wake? Waulize akina Roast Tamu La Aziz na Mooooo Dewiiiiji. Wanaitwa mabilionea wakati ukweli siyo bali wasanii wanaotumia mfumo wetu mbovu na uongozi mfu na uchwara ambao lazima FACT iukomeshe. Moody Madabidabi uko na utapeli wako wa kuuza ARvS feki?
Habari ndiyo hiyo washikaji.
Chanzo:Nipashe Jumamosi Feb., 22, 2014.

Friday 21 February 2014

Choose Berlin-sired States or EAC

  1. ... Collection Galleries World Map App Garden Camera Finder Flickr Blog
East African Community’s currently undergoing many changes such as monetary union, infrastructural upgrading and attracting new members such as South Sudan. Undergoing some changes is a very good thing if basics and reality are faced. Again, looking at a slow pace "True" change is taking, it is obvious that members seem not to be serious about the whole exercise of ushering True change which mean in this case, true and whole unification of the region. EAC's like an active volcano. Sometimes, it is heard rumbling so as to hear its tremors.  This is a time EAC is on the news. Sometimes, it is quite as if nothing's going on. However, this can be taken as a natural phenomenon for everything; the truth tells a different story.
Many east "Africans" are ready for a full-fledged union will it truly mean union not political hanky- panky as it currently is whereby every member's scheming for securing its interests. For instance, when Tanzanians were asked what they’d like about the union, they said categorically that they’d like a slow-but-sure union in which their interests are assured and protected. This, to me, didn't't’t augur well after noticing that in this union every country's trying to safeguard and protect what it calls its interests however short or long time, overt or covert and elusive they might be. Wow! Is there any marriage with separate interests?
When it comes to “safeguarding” interests, the concept of equality, union and sometimes fairness vanishes. For instance, Tanzanians want their country to be recognized as a pillar of EAC simply because she's much to offer in terms of resources and land compared to others.  If anything, considering the size of the country helps what colonial dividers wanted to achieve when they created such tiny countries like Burundi and Rwanda. I wonder. Why’d we have smaller countries the size of some districts in bigger countries whereby we can have one solid and big country? And surely, such a move will eventuate in a very healthy and solidified country in which nobody fears that another will steal and invest in his or her country.  If you want to slay and destroy the US, for instance, divide it into small states or countries like Africa is. Put it this way. If the US were to be divided like Africa, her economic clout would be history. For, it'd spend a lot on military to feed its fear of the neighbour who are now in the same territory known as the USA.
Further, by having their individual interests, EAC members prove that they’d like to use each other instead of working together for a common goal. This can’t work.  Sticking on their interests encourages division among the people based on who’s what and what size. And this is logical. Who wants to lose to another? This is why Tanzania’s always been seen as an obstacle to the union.
I, for one, have been a staunch advocate for a single unitary entity that‘s EAC. I say. Demolish the borders and abolish the presidency. I’d like to see the current presidents hit the road to give room for one president of united East Africa. Without unifying the region to the tune of what it was at the time prior to 1884, all we are trying to do is like feeding a black hole. Why’s it difficult to think as one nation instead of thinking like colonial-sired small states we currently have and cling unto? Aren't we serving our colonial masters’ ploy-cum-agenda of weakening us by dividing us into tiny, and now independent, states so as to easily rule or exploit us?  Why can’t we see that the perceived insecurity between and among states is the result of this division?  Such fear helps arms-producing countries which are mostly the same that colonized us to sell even more arms to us so that we either butcher one another or waste a lot of time and money on feeding our pseudo fears. If Africa were a single country, the money that’s been spent on arms and wars since independence would boost its economy a great deal more. How many armies does Africa have currently? How much money do African countries spend on arms for the mere fear of their neighbouring Africans?
It is sad to note that our rulers encourage us to think like or as Tanzanians, Ugandans, Kenyans and whatnot so that they can keep their presidency while we actually lose a lot. To add salt to injuries, the same rulers are ruining our countries by blessing and embracing corruption and other vices. The Swahili sage has it, “Mficha uchi hazai,” which can be translated as “One who hides private parts won’t get a child or reproduce.”
Although it may seem as being cynical to say that our rulers are acting like colonial masters to us simply because they’re using our borders to maintain their presidency, if our people need to be united why’d our rulers refuse them to do so by clinging unto power? This is why I always know there are two conflictual forces as far as EAC is concerned namely the people who want to unite and the rulers who don’t.
Ironically, whenever we talk about union we trust the same guys who go there to make sure that their power is not touched.
Time to tell our rulers that we’re tired of their manipulations is now. I once said that I don’t see any logic for Kenyan Masai to carry a passport when visiting another Masai in Tanzania. This is worse than how it was under colonial masters due to the fact that they didn't allow us to think as one. They wanted us divided so that they can easily rule and exploit us.  Now that we’re independent, why are we still feeding on the same anathema of divide and rule?
In sum, if we want a baby which is a True union, we’d all remove our clothes namely the borders and the presidency.  Failure to do so for fear of exposing our nudity should not be allowed to waste the precious time and resources for our people. Let’s everybody go solo under whatever entity be it CoW, GOAT (Great Overall Autonomous Territory) or whatever. Are our rulers ready to remove their dresses?
Verily, it is time to demolish Berlin-sired States in Africa. And this time's now.
Source: Business Times Feb., 21, 2014.