The Chant of Savant

Wednesday 30 September 2015

Kamanda Nkuzi alivyosherehekea Birthday yake




Kamanda wetu Nkuzi alitimiza miaka mitano sambamba na kuanza vidudu huku mdogo wake kama Nkwazi Jr akitimiza miaka mitatu wakati dada yao Mkubwa Nthethe alianza chuo kikuu mwezi huo huo. Tulisheherekea tulivyoweza kwa kutoka nje kidogo. 

Tuesday 29 September 2015

Kipindupindu na wagombea urahis

   Baada ya kuona kampeni zikiendelea huku kila mgombea akija na sanaa zake za kuwaahidi wachovu neema wakati mwisho wa siku ni maafa, Kijiwe kimejitoa kimasomaso kuwataka waongelee gonjwa hili la uchafu liitwalo kipindupindu.
            Mijjinga ameingia akiwa na laptop yake leo kuonyesha kuwa mambo anayaweza. Anaiweka mezani, kuamkua na kutoa mpya, “Wazee mna habari kuwa mgombea mmojawapo amekumbwa na kipindupindu kiasi cha kuwa anakatiza hotuba kwenda msalani?”
            Kila mmoja anastuka. Mgosi anasema, “Una maana kipindupindu cha ubongo au? Maana tinaona wagombea wakisema vitu visivyoiinga akiini kiasi cha kuhisi wanakabiiwa na kipindupindu cha ubongo?”
            “Haswa. Kumbe nawe ni mwanafalsa Mgosi,” Anajibu Mijjinga huku akifuta fumbi laptop yake.
            “Hii mpya na kali! Yaani kipindupindu kimekuwa tishio hadi kukabili ubongo!” Mbwamwitu anachomekea.
            Mipawa anakwanyua mic, “Nadhani kuna ukweli usiopingika. Kuna kipindupindu cha ubongo kimekumba kampeni hizi. Maana sisikii wahusika wakiongelea katiba mpya iliyouawa na mafisadi, kupambana na ufisadi na kuondoa uoza unaoachwa na huyu anayeondoka kiasi cha kugeuka kipindupindu.”
            Msomi Mkatatamaa anatia guu, “Nakubaliana nanyi mia kwa mia. Hata kipindupindu chenyewe ambacho ni alama ya uchafu na umaskini hakiongelewi. Badala yake utasikia wasanii wakiongopa kuwa watatoa elimu bure. Kwanini msitoe elimu ya kipindupindu kwanza? Kwanini hawaongelei uchafu uliokithiri tena kwenye lisirikali ambapo wezi wanajiibia watakavyo kana kwamba kaya hii ni shamba la bibi? Nilitegemea majina kama Jimmy Rugemalayer, Singasinga, Ni zero Kadamage, Kisehna, Idd Lion na mengine yakitajwa na jinsi watakavyoyashughulikia.”
             Kapende anampoka Mgosi mic, “Mkuu hapa umewashika pabaya. Ulitegemea CcM waongelee escrow wakati waliianzisha wao na kupunyua uchache kwa ajili ya kampani ya kampeni? Ulitegemea Mr. Richmonduli aongelee uchafu wakati yeye ndiye bingwa wa kuutenda? Sidhani kama kuna mwenye ubavu wa kuongelea masuala nyeti kama vile katiba mpya au kupambana na ufisadi wakati wahusika wanaogelea kwenye uchafu huo. Ziko wapi nyumba za kaya zilizouzwa na Ben Tunituni Makapu wakati Dk Kanywaji alipokuwa waziri mhusika?”
            “Du mzee unapiga huku na kule bila kupindisha!” anachomekea Mchunguliaji.
            Kanji naye anaamua kukamata mic, “Dugu zangu hii pindupindu natisha sana. Sasa kama siasa kuba naharisha hadi nakimbia hotuba sisi vatu dogo takufa.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kutia guu, “Ni kweli Kanji. Sisi wadogo tutaangamia hasa ikizingatiwa kuwa tunakunywa maji ya visima vilivyojaa kinyesi. Hivi unategemea nini wakati visima vyenyewe vimechimbwa jirani na vyoo?  Huko chini maji yanaingiliana na hii ndiyo sababu kubwa ya wengi kuugua kipindupindu. Pia hatuna uwezo wa kwenye Ugabacholini kutibiwa kama wao.”
            Mpemba anashika mic, “Yakhe mie nshangaa hii roho mbaya ya hawa wasanii wetu wallahi. Waongelea vitu vya ndotoni wakati matatizo ya wazi wayaona na kujifanya hawayaoni. Heri hicho kipindupindu kingewakamata si ubongoni pekee hadi kwenye matumbo yao ili waonje joto ya jiwe wallahi.”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anakamua mic, “Dua la kuku halimpati mwehe kaka yangu Mpemba. Nadhani tatizo la kipindupindu ni la wachovu wenyewe. Wanapaswa kuanza kuchukua hatua za usafi ambazo si lazima wafundishwe. Hapa lazima tujilaumu wenyewe kwa kuingiliwa na gonjwa hili.”
            Mgosi Machungi anarejea, “Da Sofia nakuheshimu sana. Kama kuingiiwa si sote bali nyinyi mnaokii kuingiiwa. Nadhani wangeiingiwa wao kwanza ili kuonyesha kuwa viongozi wako mstai wa mbee ingekuwa poa.”
            Mzee Maneno anakula mic, “Waingiliwe mara ngapi wakati wameishaanza kuonyesha jinsi wanavyoharisha majukwaani? Hukumsikia aliyedai ataondoa umaskini kwa njia ya kutenda ufisadi kama ule wa Richmonduli? Hukumsikia mwingine aliyesimamia wizara ya ardhi akisema kuwa lisirikali liligawa ardhi vibaya utadhani yeye hakuwa kwenye lisirikali hilo? Hawa sidhani kama wana jipya zaidi ya kueneza kipindupindu cha kisiasa.”
            “Mzee Maneno una maneno kweli kweli. Umekumbusha habithi anayetembelea mashangingi kusema eti ataondoa mashangingi na kutumia hiyo njuluku kwenye kutoa elimu. Angekuwa serious si angepanda bajaj kam alivyofanya papa Francis kwa Joji Kichaka alikopanda bajaj na kukataa Beast la Obamiza? Wasanii, wanafiki na waongo watupu. Huwezi kuwa ndani ya Nambari Wani au UKAUA ukawa na jipya zaidi ya kipindupindu cha ubongo.” Anachombeza Kapende huku akibofya ki-Sumsung Galaxy 6 chake.
            Mpemba anarejea, “Mie naona walougua kipindupindu cha tumbo na ubongo ni wale waniodanganywa kwa ahadi hewa huku wengi wao wakiwaomba rushua wagombea ulaji. Kwani hatuoni mitaani ambapo nshiko watembezwa? Kama hawa waniodanganywa hawana kipindupindu sehemu zote inakuwaje wakubali hadaa na urongo wa nchana kana kwamba hawana akili?”
            Kanji anakatua mic, “Dugu yangu Pemba mimi penda veve sana. Nasema kweli tupu dugu yangu.”
            “Angalia Kanji. Eti umisema unampenda sana ii iweje dugu yangu? Veve napenda yeye vipi na kwanini. Hebu tieeze tieewe.” Anachomekea Mgosi huku akiangua kicheko.
            Mijjinga anyakua mic, “Tuache utani. Bila kuuondoa huu mfumo wa kifisadi hata aje malaika atatuambukiza kipindupindu cha ubongo kama hawa wanavyofanya. Sioni mstakabali wa kaya kwenye kampeni hizi zinazolenga kuamuliwa kwa kuangalia watu na siyo sera. Wengine wakiongea utadhani wamemeza chura.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si kunguru aliyeugua kipindupindu akatuharishia!
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 30, 2015.

Kumbe Rugemalira ameiweka serikali ya Kikwete mfukoni!


Makama wa rais Dk Gharib Bilal akimpa tuzo mkurugenzi wa Mabibo Spirits James Rugemalira mtuhumiw amkuu wa ufisadi wa escrow. Huu ni ushahidi kuwa kumbe jamaa bado anao ubavu wa kupewa tuzo kwa biashara chafu iliyotokana na fedha za wizi wa mabilioni ya shilingi ya umma. Ndoa hii ya serikali na fisadi ni hatari na ya kukatisha tamaa ukiachia mbali kupaswa kulaaniwa. Badala ya mhalifu huyu kuwa gerezani sasa yuko majukwaani akichangia hata miradi ya serikali hiyo hiyo aliyoifilisi! Ni ujinga au upumbavukuendelea kuwa na serikali inayolala kitanda kimoja na mafisadi?

Monday 28 September 2015

When parties became diapers

          I recently was following what unfold in Australia where former premier Tony Abbot was unseated by Malcom Turnbull after being in power for just two years. Guess what, we attended the same university with this fella. Abbot’s predecessor spent only six months in power while Julia Gillard spent three years like Abbot. To cut a long story short, since Jake Kiquette came to power, Aussie has already seen six PM coming and going minus the incumbent. This informs us that PM (presidents for Tanzania) are changed like diapers. Why?  It is because there’s no longolongo there. You don’t deliver you hit the road whether you like it or not. No zengwes or what. And you can’t turn Aussies into dumbos like in Bongo.
          When it comes to kicking out governments, Greeks are second to none. They have had five elections in 2015. Since, 2012, Greeks have gone to polls ten times. They give no hoot to governments that don’t deliver. I wish Bongolalalanders were like Greeks.
          In a word, in Bongo politicians are changing parties like diapers. They’re fluky. They aren’t changed like diapers as indicated above in Aussie.  After some were ditched in their parties, they moved to others to seek ulaji. I don’t want to list down the bigwigs we saw decamping to the opposition. What I’m concerned with is this new tendency that the opposing side bared recently. It used to make us believe that it was fighting graft and archaic system to end up embracing emissaries from the same anathema they purported to fight!
          Like Aussies, we need to change them like diapers even if they change parties like diapers. You wonder a person like Makorongo Muhanga would decamp from the party that shielded him even when he faced forging allegations. I didn’t wonder to hear that even Mr Kagoda is supporting the opposing side while he got the dosh he’s burning from the laxity of those he is throwing mud at. Again, If Luwasa and Sumuye can attempt to cut the hand that used to feed them, anybody can cut the tree he is on.
          Another thing that begs us to change politicos like diapers is the fact that they monkey with everything and get away with murder. You’ll hear them promise to solve almost every problem while they actually are more a problem than the problems they purportedly want to take on.
          They monkey around on rostra and spread such false information such as bringing changes that was arrested or betrayed by the outfits sponsoring them. They promise a lot of goodies to end up crucifying the same boozers they duped. For those who remember what we are getting out of will agree with me that politicos are selling boozers down the river while they promised goodies. Despite spewing a lot of promises, politicos don’t get it done. What they’re good at is nothing but self-services as we evidenced on the all past regimes except Mchonga’s. When it comes to taking boozers for a ride, politicos and con men are but ying-yang-like, if not, identical-twin cohabitants. How on earth–for example–promise say jobs, factories, increasing pensions without showing how you’re going to do it and fall short of conning those you’re blatantly duping? How can you promise development without showing how you’re going to tackle obstacles to development such as corruption, mega theft, drug trafficking, tax evasion, capital flights and all the like? How can you do that without having a legal mechanism that empowers you to take on criminals that are always pampered simply because they know how to share the loots? As a boozer–though this can be seen as pushing the limits–methinks, nobody will do anything without having the New Constitution that corrupt bigwigs feared it would send to jail due to the crimes they committed in power. This is why I espouse changing politicos like diapers as we’ve seen in Aussie.
          Guess what. When it comes to addressing corruption, there are some politicos –especially those implicated–who don’t want to touch it. Why should they add fuel to the frame? Again, boozers seem not to get it. Instead of tasking those who want to rule them to address graft; they’re talking about personalities instead of issues! Mtaliwa sana!  Agitate for the system that will enable you to change politicos like diapers the way the politicos have shown in changing parties like diapers. Without tweaking the system all promises are but hogwash and hoo-has.
Source: Guardian Spet., 27, 2015.

Saturday 26 September 2015

Matokeo ya uchaguzi yalete mabadiliko


          Hakuna ubishi. Kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba zimetawaliwa na watu na si masuala. Wagombea wanajinadi kwa sifa binafsi na si sera wanazotegemea kutekeleza. Masuala muhimu kwa watanzania yamewekwa kando. Ni bahati mbaya kuwa –kutokana na mfumo mbovu tuliorithi toka chama kimoja –wapiga kura hawana uwezo kisheria kuhoji.
          Si chama tawala wala upinzani, hakuna anayejikita kwenye sera zitakazoondoa matatizo ya watanzania ambayo yamekuwa yakiterekezwa na kila serikali inayoingia. Kwa mfano, watu wanajadili wagombea wenye ushawishi yaani mgombea wa Chama Tawala (CCM) Dk John Pombe Magufuli na mgombea wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Edward Lowassa. Hata ukiangalia hiki kinachoitwa UKAWA kimeondoka kwenye misingi iliyokiunda, yaani kutetea katiba ya wananchi. Wakati mwingine unashangaa kuona wale waliopinga na kuua katiba husika kuwa vinara wa kambi iliyokuwa ikikumbushia na kupigania katiba mpya.
          Kuna mambo mawili ambayo wapiga kura na wanaotaka kuchaguliwa wameyatelekeza au tuseme kuyaua. Mosi, ni katiba mpya. Na pili, ni namna ya kubadili mfumo wa kikale na mgando uliowaweka mateka watanzania kiasi cha mgombea, kwa mfano, wa chama tawala kutaka kubadili hali ukiwa ni ushahidi kuwa serikali ya chama anachowakilisha ilivuruga. Je serikali inayoondoka haikuvuruga? Jibu wanalo wasomaji na wapiga kura kwa ujumla. Kama ingekuwa ilifanya vizuri, basi mgombea wake asingeikosoa.
          Swali linalosumbua wajuzi na wachambuzi wa mambo ni: Je rais ajaye ataweza ku-deliver wakati mfumo wa kutomwajibisha haujaondolewa? Kwa mfano, rais ajaye hawezi kupambana na ufisadi au kutoushiriki wakati mfumo unamlazimisha kufanya hivyo. Kuweka suala hili kwenye picha rahisi, hebu angalia baadhi ya wagombea wanavyotoa ahadi za kuwapa watu vyeo kana kwamba vyeo hivyo ni mali yao binafsi. Wapo wanoona kama hii ni rushwa ya kitaasisi.
          Japo Dk Magufuli amekuwa akisema kuwa atapambana na ufisadi, je sheria au nyenzo inayompa mamlaka yaliyojitenga na utashi wa mtu binafsi viko wapi?  Magufuli amekuwa akiahidi kupambana na ufisadi huku akijua wazi hakuna mfumo sahihi wa kumwajibisha kama hatafanya hivyo kama alivyofanya rais anayeondoka. Kimsingi, ni hatari kutegemea utashi binafsi wa rais badala ya utashi wa kisheria na kimfumo. Jakaya Kikwete alipoingia madarakani, hata hakusumbuka kujiapiza kuwa angepambana na ufisadi. Na kweli hakupambana nao zaidi ya kuupamba kiasi cha mafisadi papa wengi kuwa washirika na marafiki zake. Rejea madai kuwa Kagoda kampuni iliyohusishwa na mshirika wake Rostam Aziz ilikwapua mabilioni ya fedha kwenye fuko la madeni ya nje EPA. Je mtuhumiwa alichukuliwa hatua gani zaidi ya kuamriwa –yeye na wenzake –warejeshe baadhi ya fedha hata bila kuhojiwa na polisi? Je wezi wa wizi wa kutisha wa hivi karibuni –hata kudaiwa walimshinikiza rais kwa njia ya email asiwachukulie hatua bila yeye kunanusha –wamechukuliwa hatua gani? Je rais ajaye ataweza kuwachukulia wahalifu hawa ambao ni serikali ndani ya serikali bila kuwa na nguvu ya kisheria? Hapa ndipo mantiki ya kuwashauri wananchi washinikize wagombea wajadili sera hasa suala zima la katiba mpya ya wananchi unapokuwa muhimu. Wananchi wakiendelea na usingizi huu wa kupumbazwa na ahadi hewa wataishia kulia sana hata baada ya kuwa na serikali mpya ambayo haitakuwa na jipya lolote zaidi ya business as usual.
          Hakuna awezaye kuleta mabadiliko –hata angekuwa malaika –bila kuwa na nyenzo ya kufanya hivyo kama vile sheria na mfumo unaolenga kuleta mabadiliko. Hivyo, kwanza, tuseme kuwa wagombea wanafanya usanii ili kupata madaraka. Na si kwamba hawajui umuhimu wa kujadili masuala badala ya personalities. Wanajua fika sema wanataka wapate madaraka yatakayowawezesha kuwa miungu watu kama hawa wanaotaka kuwarithi. Sidhani kama mtuhumiwa wa ufisadi au mgombea ambaye chama chake kimelea ufisadi anaweza kuongelea ufisadi. Akifanya hivyo, atakuwa anajitia kitanzi kisiasa. Laiti wapiga kura wangeliona hili na kulishupalia. Kama wapiga kura na watanzania kwa ujumla wataendelea kupumbazwa na ahadi lukuki na maneno matupu, wataishia kujilaumu watakapogundua kuwa kumbe walitapeliwa. Wakati muafaka wa kudai mageuzi ya kweli kwa kushinikiza kubadili mfumo ilikuwa sasa. Kama watanzania wangekuwa makini wangegomea hata uchaguzi au kutaka uchaguzi uendane sambamba na mkakati wa kufufua mchakato wa kupatikana katiba mpya iliyouawa kwa hofu ya waliotenda ufisadi wakiwa madarakani kufikishwa mahakamani. Je mtu binafsi tena aliyeteuliwa au kupitishwa au kuenguliwa na watuhumiwa wakuu ataweza kuwachukulia hatua waliomuumba? Kinachofanyika ni kituko kama kitachukuliwa kama harakati za kuleta ukombozi, mapinduzi na mabadiliko ya kweli katika maisha ya mwananchi wa kawaida wa Tanzania.
          Tumalizie kwa kuwaonya watanzania kuwa –kama wataendelea na mfumo huu –wasitegemee mabadiliko yoyote bila kujali nani watamchagua. Kimsingi, ni kama wanachagua baina ya pombe na mvinyo. Vyote ni vilevi na tofauti yake ni majina tu.
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 27, 2015.

Usalama mitaani: Fungeni tunguli si kamera

          Nilimsikia rahis Njaa Kaya akisema ana mpango wa kuhakikisha miji yote mikubwa kayani inafungwa kamera kudhibiti wizi na maafa mengine. Japo napiga mibangi na ulabu, naunga mkono wazo la kuhakikisha walevi wanatanua bila kusumbuliwa na mijambazi, mipaka hata mifisadi.
           Hata hivyo, nina ushauri tofauti. Badala ya kufunga kamera mitaani, kwanza, funga hizo kamera kwenye vituo vya kupigia na kuhesabia kura ili kuepusha uchakachuaji. Kwani, vidokozi si tatizo zaidi ya mfumo.  Wengi wanaamini kuwa tatizo la vibaka si kubwa kama lile la mafwisadi tena wanaolindwa na wazito walioahidi wangewalinda walevi ukiachia mbali kuwapunyua kodi za kutanulia kuiba kama vile ni shamba la bibi.
          Tunadhani tatizo ni wazito hasa mzito na wateule, marafiki na washirika zao kama vile akina Kagoda, escrow, EPA na wengine wengi.  Wakati tuliposikia hii kitu mlevi mmoja alisema eti hiki nacho ni kituko cha jamaa kuondokea. Kwani muda wote alikuwa wapi ukiachia mitaa yetu mingi kujengwa na kupangwa hovyo .  Walevi wanadhani fweza ambayo ingetumiwa kwenye usanii ingeelekezwa kubomoa mijengo iliyojengwa kinyume cha sheria na chini ya viwango kama ule wa uhindini. Au mijengo ya wanene iliyojengwa sehemu zilizokatazwa kama ule mhekalu wa Mchunaji Rwakatarehe na mingine mingi huko Ukwasini.
            Hata hivyo, jamaa pamoja na ulevi na mibangi yake, alikuwa na pwenti. Umeme wenyewe wa kuendeshea hizo kamera uko wapi?  Hivi kweli umeme wa mgao unaweza kuwaahidi ulevi usalama tokana na mikamera hii hewa au ni sanaa kama kawa? Kama kamera hizo ni dili basi fungeni Masaki na kote wanapoishi binadamu na siyo Uswazi wanakoishi wanyamawatu. Mitaa haina hata taa za barabarani wala za pembezoni mwake. Mijumba yenyewe imejengwa kama magugu na haina namba. Hizo Kamera zitafungwa wapi? Heri mfunge tunguli na si kamera wataziiba kama siyo kuzihujumu.
          Walevi tunapinga kwa nguvu zetu kufungiwa kamera mitaani kwetu. Zinaweza kutuchungulia hasa kwenye vyoo vyetu vya uswazi zitatuchungulia tunaoga na kunonihino. Pili, mnaweza kutupandishia kodi jambo ambalo litawanufaisha wezi wazito kwenye lisirikali.
          Tatu zinaweza kusababisha mabalaa mengine hasa wale wanaopenda kusimama mitaani na washikaji zao wa pembeni. Nasikia hata ndata wanalalamika kuwa zikufungwa kamera zinaweza kuwaacha bila nguo hasa wale wanaosindikiza mizigo ya wizi nyakati za usiku.
           Hata wenye gesti bubu nao wanalalamika kuwa kufunga kamera mitaani kunaweza kuharibu biashara yao ya chapchap. Na kama kweli mko serious basi mtavunja ndoa kibao. Mie mwenzenu nshafunga ndoa na ulabu na bangi. Sina wasi wasi wala kizuizi. Ila msinilaumu kama mtapuuza ushauri wangu.
          Kama kuna haja ya kufunga kamera basi zifunge kwenye vituo vya kupigia kura kwenye uwanja wa ndege, mipakani ili kuzuia mibwimbwi, madini na nyara zetu kutoroshwa nje. Tena kama ingewezekana kwenye maeneo nyeti kama haya tungeshauri zifungwe darubini ili tuwabaini wanaotugeuza mabwege. Pia tungeshauri zana hizi zifungwe kwenye ofisi zote za TRA, Bandari, Uhamiaji, Tanesco, TIC, hospitalini ili kuona wanaopunyua rushwa na kufanya kaya yetu iwe ombaomba wakati uchumi inao lakini inaukalia.  Hata Mjengoni kungefaa kufungwa zana hizi ili kubaini waishiwa vilaza na wanaoupiga usingizi ukiachia mbali wengine kuchangamkia posho bila kufanya lolote.
          Kama kweli jamaa ana maanisha basi ningemshauri afanye kitu moja ya nguvu. Yaani, afunge tunguli. Najua vidokozi na majambazi wengi walivyozoea ushirikina na upuuzi mwingine kama huo basi watazigwaya kuliko hata ukoma. Taarifa; Maswihiba zetu Saleh, Omari,na Hussein Assagaf wa Gerezani wamefiwa na dada yao mwezi uliopita. Salamu ziwafikie washikaji wote wa Gerezani, Kidongo Chekundu, Msimbazi na Lumumba. Nasikia mnakamata Nipashe ili kumsoma mshikaji wenu mlevi kama hamna akili nzuri. Msichunguliane. Kila mmoja anunue nakala yake na kufunua.
Chanzo: Nipashe Sept., 26, 2015.

Tuesday 22 September 2015

Kijiwe chadili ahadi za wagombea


  Baada ya baadhi ya wagombea urahis kuwa wanatoa ahadi kama njugu, kijiwe kimestuka kiasi cha kukaa kama kamati ya ukombozi kujadili janja hii.
           Leo Mheshimiwa Mijjinga ndiye analianzisha, “Waheshimiwa wanakijiwe hivi mnaonaje hili changa la macho ambapo wagombeaji urahis hata uishiwa wanamwaga ahadi kama njugu?”
          Kapende anakula mic, “Usikumbushe hii aina mpya ya utapeli kama nilioshuhudia hivi karibuni nilipokuwa Lindi kabla ya kurejea Bongo na kukumbana na kadhia hii. Kweli watu wanamwaga ahadi utadhani wamesahau ya 2005.”
          “Mgosi unashangaa hii ya kutoa ahadi wakati Njaa Kaya anaendeea kumwaga vyeo kwa washikaji zake kama hana akii nzui! Hakuna aiponiacha hoi kama kumteua Amos Makaa kuwa mkuu wa nkoa ukiachia kuteua mabaozi wakati huu wa lala saama ambapo aipaswa kuwa anafunga viago na kuishia,” anajibu Mgosi Machungi huku akibusu kipisi chake cha sigaa kai.
          Msomi Mkatatamaa anaamua kuingia mapema leo, “Nadhani tunapaswa kulaumu mfumo wa kipuuzi unaotoa madaraka makubwa kwa ngurumbili usijue atayafuja. Hii kutoa ahadi si chochote si lolote bali utapeli wa kisiasa ambao unafanywa na wagombea wote tishio. Kimsingi, tusiposhupaa ikarejeshwa katiba mpya, upuuzi kama huu utaendelea kurudiwa kila baada ya miaka mitano au kumi. Yako wapi Maisha Bora kwa Wote Apechealolo (MBWA)? When you have an imperial president you must expect such things become norms.”
          Kabla ya kuendelea mzee Maneno anamuonya Msomi akisema, “Msomi angalia lugha. Maana maneno mengine yanatua nje akina sie.”
          Mpemba anakula mic, “Wallahi hata mie nshangaa mtu kutoa ahadi kwa mfano ya kuwapa vyeo tena vikubwa waloshindwa utadhani vyeo hivyo mali ya mama yake. Wengine wadai watatoe ilmu bure bila kueleza wanivyopanga kutafuta fedha ukiachia wengine kuahidi vitu visivoingia akilini wallahi.”
          Sofia Lion aka Kanungaembe anakwanyua mic, “Kama wanaoahidiwa wanaridhishwa na ahadi husika hakuna haja ya kulaumu watoa ahadi. Kwani wanalazimishwa kuzikubali zaidi ya kushawishiwa wapige kura?”
          Kanji anakamua mic, “Mimi ona kila gombea tongoza piga kura. Kama tafanya kosa natoa basi taumia sana.”
          Mbwamwitu anamchomekea Kanji, “Kanji acha uhuni. Eti wanatongozwa watoe na wakitoa wataumia! Sasa hapa tumlaumu nani zaidi ya kuwa ubwege wa wahusika? Nawashauri wasikubali kutongozwa wala kutoa kura ili wengine wale.”
          Mipawa anakatua mic, “Hapa mrume umenena. Kama watajirahisisha wakatoa kura watamlaumu nani wakati walishaliwa sana tena si mara moja wala mbili? Inaonekana wengi wamesahau ahadi kibao kama kupambana na ufisadi, kufumua mikataba ya uchukuaji unaoitwa uwekezaji, kupambana na wauza bwimbwi vitu ambavyo vinazidi kuhalalishwa huku wakuu wakichukua cha juu. Kimsingi, nakubaliana na Msomi na Mbwamwitu. Kama watajiachia wataliwa tu.”
          Mgosi anaamua kurejea, “Hei waiwe wao wasisababishe kaya yetu kuiwa na kubakwa kama ambavyo imekuwa ikifanyiwa kwa muda muefu. Yaani imefikia hata wanyama wetu wanatooshwa na hakuna anayejai ukiachia mbai kuendeea kufanya usanii eti watapambana na ushwa na ufisadi.”
          “Hivi jamani mmegundua kuwa baadhi ya wagombea hawapendi kuongelea ufisadi kabisa? Wengine wanauongelea kama suala la mtu binafsi wasijue ni suala la kaya nzima. Nashauri muwashauri walio karibu yenu wastukie huu usanii wa kuahidiwa pepo wakaishia kusweka motoni kama ilivyotokea tangu kuahidiwa maisha bora kwa wote yakaishia kuwa mateso makali kwa wote. Ziko wapi ajira, kukuza uchumi na kupambana na ufisadi? Sana sana kilichokuzwa ni deni la kaya na kuzidi kuumka kwa vitendo vya kifisadi na rushwa. Watu wanafikia mahali hata kughushi shahada na bado wanapewa nafasi za juu zinazohitaji maarifa, busara na elimu ya kutosha! Wanatupeleka wapi hawa? Watu wameua hata Katiba kiasi cha kutuacha tukiendeshwa kama kundi la mbuzi tena linalochungwa na fisi na mbwamwitu.” Msomi anashuka kama hana akili nzuri.
          Mbwamwitu anachomekea, “Msomi angalia.”
          Msomi anaendelea, “Simaani mheshimiwa wewe. Hii ndiyo bahati mbaya ya kupeana majina ya wanyama. Nimaanishacho ni kwamba, hali itakuwa mbaya sana baada ya uchakachuaji huu. Yeyote atakayechaguliwa atavuruga kutokana na mfumo kutompa mamlaka na nyenzo za kuondoa kadhia za wachovu. Uongozi ni taasisi na si mtu binafsi hata angekuwa genius kiasi gani. Waulize wanaosifiwa ziko wapi nyumba za wachovu?”
          Kapende anachomekea, “Aulizwe Denjaman Dugong Makapi na baraza lake la mawaziri. Hamkumsikia akituita wote wapumbavu baada ya kutuita wavivu wa kufikiri. Wakati mwingine alikuwa sawa kwa vile jinsi alivyotuibia na hawara yake Ana Tamaa asingekuwa uraiani zaidi ya kuwa lupango. Nashangaa hata waliomruhusu kusimama kwenye majukwaa na kutoa pumba na upupu wake sijui anawasaidiaje! Sioni tofauti yake na Jose Gwajumaa.”
          Mheshimiwa Bwege aliyekuwa akisoma gazeti anakula mic, “Mie nadhani tunapaswa kutahadharisha kuwa huu msimu ni wa kuliwa, kulana na kula.  Wachovu wasipokuwa makini, wataliwa hadi wanaingia makaburini. Nadhani hapa lazima tulaumu ubwege na usahaulifu wa watakaotoa kura ya kula na kujirahisisha kiasi cha kuliwa kila msimu wasistuke wala kuchukia. Sijui washikwe wapi wastuke?”
Kijiwe kikiwa kinanoga si ikapita misafara ya watoa ahadi hewa. Acha tuwazomee!
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 23, 2015.

Saturday 19 September 2015

JK’s send-off dirge






It is obvious that time is up for President Jake Kiquette. I think he’s currently packing up ready to hit the road to oblivion. We indeed will miss his shows which were but a tragicomedy of some sort so to speak. Many will miss him especially the kit and caboodle that benefited under his lasssez-faire watch. Boozers will miss his promises that he seriously wanted to fulfill. I still remember his super promise of Better Life for All (BLA) which benefited All around him especially members of his family, partners, friends and partners. Chaps like Eddie Luwasa, Jimmy Rugemalayer, Singasiga Roat Tamu Aziz, Nizero Kadamage and many more will badly miss his generosity that enabled them to become billionaire in the hunk of dirty paupers. Again, as Jake exits the scene who knows what Dr. Kanywaji will do after taking over?
 I wonder now when I hear chaps like Eddie make rumpus accusing Jake of all messes such as laxity, doing nothing and whatnot.  Why don’t they appreciate that Jake was a good globetrotter that brought fame to the hunk? Had he not been lax–I think–such fellas would have been wailing in Segerea after robbing the hunk. Do they think we’ve forgotten Richmonduli? Hell no! They must remember Dr. Harry Mwakiembe’s warning that they can have a date with a judge anytime shall the powers that be decide to.
Another promise I remember vividly despite being sozzled is about creating jobs. Indeed, the son of man created a lot of jobs for all such as Salmia, riz-wani, Willy maschillings, Amie Makara, Silvia and Mihigie Rweyependekeza who’ll miss his reign dearly. Again, when Jake promised better life for all (BLA) boozers didn’t get it. They didn’t know he meant Better Life for All around him especially courtiers, bootlickers and praise singers. How many ambassadors DCs judges, RCs and whatnot he offered such posh jobs? Had he not been the head do you think kids like Riz-one would have landed parliamentary jobs? What of the first woman who ended up creating a company through which she raked a lot of dosh not to mention being welcomed and treated like president simply because he shares bed with the big man?
 Indeed, Jake created jobs under the doctrine of expanding the size of the govt to create political jobs he awarded to friends and partners. Sometimes, absolute power corrupts absolutely especially when on is an imperial president.   You can gage this under Jake whereby all those alleged to have participated in graft weren’t charged, jailed even interrogated. What a legacy! Jake’s legacy surpasses even mzee Ruxa’s who initiated all this theatre we enjoy today in the upper echelons of power.
Being a guy who’s hyped as kipenzi cha walevi, Jake made sure that everybody did whatever he or she deemed fit. Drug barons will miss him immensely not to forget our animals that ended up boarding planes as they flew to the Gulf.  For the love of his earthlings, Jake made sure that nobody suffers under his watch. Fakers were not put in trouble due to the fact that they gained more diplomas.  How many doctors were made under Jake’s watch? Had it not been for Jake –do you think–literati like Marry Nyagu, Dolorous Kamala, Emmy Nchimvi, Makorongo Mahanga, Didier Makalio, Billy Lukuvie and others would become ones? Remember the founder of this science Cyril Chitalilo? Why then say that he didn’t provide and improve education while people landed PhDs easily and faster? Don’t ask if such degrees are genuine or not.  Dr. School Kawa-dog will too miss the man dearly.
Our shilling that’s always been in the ICU will dearly miss the guy who allowed to it to enjoy a free fall as our external debt swelled astronomically.
What should I say vis-à-vis guys like, thugs EPA, Escrow and Kagoda who made a killing easily and got away with murder? Guess what. If it Jake weren’t a loving person, such people would have rotted behind bars given that he still has the lists of almost every criminal in the hunk.
So, too, school girls who were impregnated will remember him for giving them the best advice ever saying they must stop kiherehere in order to avoid being poked.
          Another thing that boozers will miss is oft-seeing Jake boarding pipa as he globetrotted to see to it he gets dosh for their upkeep. So, too, as his handlers and spin doctors used to tell us, his many trips abroad brought a lot of dosh however our external debt kept on opposing his efforts to make our hunk richer. Those who used to enjoy a ride whenever the man toured the world will miss him dearly too.
          Jake did a lot of things. His legacy is second to none. He loved his paupers dearly. He enjoyed them.  Though, I don’t know if they enjoyed him the same way.
Go Jake go. Go never turn back. Go. Many eaters and joyriders who used to accompany him will miss you though in different styles and manners. All in all, we’ll miss Jake's courage of the mad to see to it that the hunk was on autopilot for ten years of your stewardship.
Source: Guardian Sept., 20, 2015.

Gwajima: mkeo akikupiga utatangaza?


          Sina haja ya kumtetea Dk Wilbrod Slaa katibu wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Ila maneno ya hovyo, kuudhi na yaliyovuka mipaka yaliyotolewa na anayejiita askofu Josephat Gwajima yamenilazimisha kuandika haya ninayoandika.
          Gwajima alikaririwa kwenye mitandao akisema kuwa aliyesababisha Dk Slaa kuachana na Slaa ni mkewe na siyo mapenzi yake. Japo madai kama haya licha ya kuwa ya kizushi na kitoto, yanavuka mipaka.  Hapa Kanada wananchi wana usemi mmoja kuwa the government has no right to know what is done in our bedroom yaani serikali haina mamlaka ya kuingia kwenye vyumba vyetu vya kulala. Wakanada walitoa kauli hii baada ya baadhi ya wanajamii kutaka kujua kila kitu kuhusiana maisha ya raia na wakazi wa hapa.
          Kinachoshangaza ni ile hali ya mtu anayejiita askofu tena mwanandoa kushindwa kujua mipaka yake kama binadamu, kiongozi wa kiroho hata kama anatia shaka na kama mwanandoa. Hapa ndipo najiuliza: Je Gwajima akipigwa na mkewe atatangaza au atapenda mtu yeyote atangaze? Je kufokewa kwa Dk Slaa –kama alivyokutengeneza na kukuzusha Gwajima –kunamsaidia nini mtanzania wa kawaida?
Je Gwajima anamshambulia na kumdhalilisha Dk Slaa kama nani? Kwanini hakujibu madai yaliyotolewa na Dk Slaa kuwa Gwajima ni mshenga wa Edward Lowassa mgombea wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). Je hii mikakati ya kijinga na kizamani anayotumia Gwajima imebarikiwa na Lowassa au tuseme amemtuma? Je kwa alivyovuka mipaka, anadhani anawasaidia UKAWA?
          Tangu Gwajima ajitokeze baada ya kumkosea adabu askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar Es Salaam mhashamu Polycarp Kardinali Pengo, wengi wanashinda kumwelewa kama ni mwanasiasa au mchungaji. Kwa wanaojua sifa na hadhi ya uaskofu, wanaona kama anachofanya Gwajima ni kutukanisha hicho cheo. Hata hivyo, ana hasara gani kama amejipachika chake?
Kitendo cha Gwajima nadhani kimemshushia yeye heshima kuliko mhanga wake ukiachia mbali kuzidi kuivua nguo UKAWA. Inashangaza viongozi wa UKAWA ambao wengi wao wamekwenda shule kuruhusu siasa za matusi na kashfa kama hizi.
          Tunashauri Gwajima –hata kama ni mshenga wa mgombea wa UKAWA–ajitahidi kujua na kukubali kuwa uchaguzi ni suala la muda. Kuna maisha baada ya uchaguzi. Hakuna haja ya kutukana wakunga na uzazi ungalipo au kumtukana mamba kabla hujavuka mpya. Hakuna madai ya kushangaza kama Gwajima kudai kuwa Dk Slaa anatumika. Hii inaweza kujenga dhana kuwa kwa vile Gwajima ameshindwa kukanusha au kukiri kutumiwa na Lowassa, hivyo basi anadhani kila mtu anatumiwa kama anavyotumiwa.
          Kuna vitu vingine hata ukiwaambia ndege watakucheka. Inashangaza mtu kama Gwajima kusimama hadharani akatoa madai kuwa amemwekea walinzi Dk Slaa. Kama nani? Kimsingi, Gwajima anapaswa ajitahidi kuachana na maigizo anayofanya kwenye biashara yake ambapo huwaaminisha watu kuwa ana uwezo wa kufufua. Atofautishe suala la Dk Slaa na madai kama yale aliyotoea kuwa angeweza kumfufua marehemu Amina Chifupa.
          Hata hivyo, kuna haja ya kuilaumu serikali ambayo imeruhusu kila msanii na msakatonge kusema na kufanya atakavyo hata kama anachofanya hakiwezekani au utapeli. Nani anaweza kumfufua hata inzi leo kama tutakuwa wakweli?
          Japo Gwajima anaweza kujiridhisha kuwa amefanya kazi ya wale wanaomtumia waliyomtuma kuifanya, kama Dk Slaa ataamua kushitaki –kama ilivyotokea kwa mhashamu Pengo –anaweza kujikuta pakanga. Kuna haja ya serikali kuanza kuchunguza madai hasa kuhusiana na nyadhifa fulani kujiridhisha kuwa wanaodai kuwa nazo wamezipata kihalali na kwa kufuata tararatibu ukiachia mbali kuchunguza kama wanazimudu. Sikutegemea askofu–kama kweli mhusika ni askofu wa kweli aliyetimiza vigezo–kusema aliyosema tena mbele ya vyombo vya habari.
          Pia tuchukue fursa hii kuwashauri UKAWA kuachana na siasa za kihuni zinazoweza kujenga hata dhana za udini ukiachia mbali kuumizana kuzishiana na kukashifiana. Pia UKAWA wachunguze washenga wao. Sijui inajenga picha gani kwa wapiga kura wanapomuona askofu au shehe akipigia debe chama fulani wakati hapaswi kuwa shabiki wa chama chochote? Je wanakwazwa vipi kusikia kuwa askofu anayepaswa kuwa mshenga wa Yesu anakuwa mshenga wa mwanasiasa tena mwenye kutia shaka?
          Tumalizie kwa kuwashauri wapiga kura kuwaepuka watu wasiojua mipaka ya uhuru wao. Si hao tu, hata hao wanaowatuma wanapaswa kuogopwa kama ukoma hivyo kutopewa kura. Maana wakipata madaraka hawa wataumiza wengi kutokana na upogo na uroho na ubinafsi wao. Je Gwajima, kama mkeo akikupiga utatangaza au kupenda mtu mwingine atangaze? Inadhalilisha sana hasa mambo kama haya ambao licha ya kuwa dhambi na jinai yanapotendwa na mtu anayejiita askofu au kiongozi wa kiroho.
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 20, 2015.

Gwajumaa: Si uunde chama cha kisiasa?

Baada ya mchunaji, sorry, mchungaji mwenye cheo cha kujipa cha askofu Jose Gwajumaa kutawala majukwaa ya siasa, Mlevi ameamua kumtolea uvivu.
          Kila mchovu, mdanganyika na mbongolalalander ana haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa ingawa si wote. Ndata, wasoja na viongozi wa kiroho wasio na uroho wanaweza kuwa na vyama wanavyopenda japo hawapaswi kuonyesha hadharani. Hii ni kutokana na kuepusha kuwagawa na kuwakwaza waumini. Hata hivyo, siku hizi mambo yamebadilika. Wapo viongozi wa kiroho wanaotia shaka wanaounga mkono vyama fulani tena hadhani. Wengine wamegeuka wasemaji wasio rasmi wa vyama husika. Waambiwe wachague moja joho au gwanda.
          Pamoja na bangi na ulevi wangu, huwa nashangaa mantiki ya ngurumbili hawa kufanya wanayofanya wasijue ni kinyume cha sheria na maadili. Inakuwa noma pale anayejiita kiongozi wa kiroho kujiingiza kwenye siasa za majitaka kama vile kuwa “mshenga” wa mgombea fulani kiasi kujiingiza kwenye vita vya kisiasa. Je huyu tumueleweje usawa huu?
          Hivi karibuni, Gwajumaa alisikika “akimvua nguo” Dk Willy Silaha, katibu wa zamani wa Chakudema aliyeachia ngazi baada ya kutokubaliana na chata lake kuweka mfukoni na wale anaowaita mafisadi mapapa tena wa kunuka. Alisikika akitoboa siri za ndani za Dk Silaha kinyume cha sheria na maadili. Je huyu ana mke; na kama anaye atafurahi kusikia mambo ya chumbani kwake kwenye mikutano ya waandishi wa umbea? Ama kweli mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu!
          Gwajumaa aliyetajwa na Dk Silaha kuwa mshenga wa Eddy Luwasa, alipagawa pale Dk Silaha alipoanika siri zake na undumilakuwili wake.   Kujibu mapigo, alinyofoa tuhuma kiduchu kwenye nyingi alizofyatua Dk Silaha. Gwajumaa alidandia lile dai kuwa alimwambia Dk Silaha kuwa Luwasa angechomoka toka Nambari Wani akiwa na waishiwa kibao huku akiungwa nkono na mabishop kama 30 waliokatiwa uchache. Gwajumaa anasema kitendo cha Dk Silaha kuwatuhumu watu wa God ni chakulaaniwa. Tumuulize swali dogo. Je watu wa God hawahongwi? Mbona Yuda Iskarioti alihongwa vipande 30 akamsaliti mwana wa Adamu sawa na viongozi wa kiroho wanavyomsaliti kwa kujiingiza kwenye mambo ya madili na kiuroho badala ya maadili na ya kiroho?
          Swali la nyongeza: Mbona hivi karibuni askofu mmoja wa kweli alikiri kuwekewa njuluku zipatazo milioni 40 kwenye akaunti yake na fisadi wa Escrow Jimmy Rugemalayer?  Je Gwajumaa anawaongelea maaskofu wapi wakati siku hizi wapo wengi wa kweli na wa kujipachika? Anayejipachika cheo kikubwa kama hiki atashindwa nini kuhongwa ukiachia mbali kuwa na maaskofu ni binadamu? Nani angeamini kuwa watu wa God wangewatafuna kondoo wao kama ilivyotokea kwa kanisa moja kubwa ulimwenguni ambapo makasisi wake walipatikana na hatia za kulawiti na kunajisi watoto na waumini wao tena kwa miongo kibao?
          Pamoja na bangi zangu, nakumbuka kuwa Yesu alisema kuwa mbinguni ni kwa maskini na si kwa matajiri. Rejea mfano wa Zakayo. Leo hii kuna wachunaji sorry, wachungaji ni matajiri wa kutisha hadi kununua vyopa au helkopta kwa kimakonde. Namshauri Dk Kanywaji Makomeo awashughulikie wakwasi hawa waeleze walivyoupata.  Pia nawashauri wakwasi hawa wanaowaibia waumini wajinga na wenye matatizo lukuki wasome Matayo 19:24 isemayo, “Heri ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko wakwasi kuingia kwenye ufalme wa Mungu.”
          Kama Gwajumaa na wengine kama yeye wanapenda siasa si wa waunde vyama badala ya kuwa mguu mmoja kwenye dini na mwingine kwenye siasa? Hata hivyo, hawatafanikiwa. Maana ukiwa kiongozi wa kiroho mwenye uroho ukataka kufanya siasa nje ya chama twawala hufiki popote.
Zumbe atogolwe sana na mbarikiweni sana wasomaji wa pumba hizi za mlevi bingwa wa bangi na ulabu. Wachanganya siasa na dini walaaniwe kama wale wachuuzi waliokuwa wamegeuza sinagogi kuwa genge la biashara.
Chanzo: Nipashe Sept., 19, 2015.

Thursday 17 September 2015

My New Book Born with Voice is out!


 Nkwazi Nkuzi Mhango «Born with Voice»
  • Lightning Source UK Ltd
Born with Voice examines the psyche and scrape of the victims of various crimes, especially sexual discrimination-cum-exploitation, rape, and the killing of people with albinism. The author digs deeper into the hearts and minds, and plights of victims to inspire the society to stand with, and support them. The book offers some nuggets such as, understanding the phenomenon, confronting it and stopping wars that cause sufferings such as rape and death. It champions the urgency of voice for all and sundry. It challenges the industries of technologies of crime and violence to rise above selfish self-interest in the interest of human rights and voicing the voiceless victims of their greed.

Wednesday 16 September 2015

Kijiwe chamshauri Gwaijumaa aanzishe chama

          Baada ya mchunaji, sorry, mchungaji wa kujipachia uaskofu aitwaye Jose Gwaijumaa kuwafunika wanasiasa kwenye siasa, kijiwe kinahoji anafanya hivyo kama nani wakati kayani kwetu kuna utaratibu wa kutenganisha siasa na dini au anahubiri duni?
          Mpemba anaingia akiwa anavuta tasbih yake na kusema, “Wallahi mie nshangaa sana hawa UKAUA. Yaani pamoja na kumuua Pumba na Silaha bado waendelea kujiua kwa kuhubiri udini?”
          Mgosi Machungi anamchomekea Mpemba, “Hebu Ami tieeze vizui tikikueewe. Unamaanisha nini unaposema eti UKAUA wanahubii udini?”
          Mpemba anajibu, “Ami hujamsikia huyu nchunaji Jose Gwaijumaa aiyejipachia uaskofu na upupu anaomwaga ukiachia mbali madai ya ajabu aniyotoa?"
          “Ahaa unaongelea huyu msanii na mshenga wa Luwasa siyo! Nadhani anafaa sana kuvaa gwanda na si joho. Sioni tofauti yake na yule kidhabu wa nambari wani aitwaje Livingjiwe Lushindo. Hata hivyo, sishangai, msimu wa kutafunana, kuhadaana, kuuzana, kuchuuzana na kutapeliana ndiyo huu. Kimsingi, huyu Gwaijumaa alipaswa achunguzwe ukwasi wake kabla ya kujitiatia anajua siasa wakati si cha dini wala siasa ajuacho.” Anajibu Msomi Mkatatamaa.
          “Nadhani huyu msakatonge mnamuonea bure. Mshaambiwa ni mshenga. Sasa mnataka afanye kazi gani zaidi ya upambe. Je mnajua analipwa au ameahidiwa kiasi gani?” anajibu Mijjinga huku akibusu kikombe chake cha kahawa.
          Kapende anaamua kutia timu, “Nyie hamumjui huyu. Huyu ni wale wanaotumia majoho kujitajirisha. Yuko tayari kuingia kitandani na yeyote ilmradi mkono uende kinywani. Hata hivyo, siwalaumu hawa wasanii kutokana na kaya yetu kugeuzwa ya wasanii. Huoni anavyomlaumu Dk Silaha kuwa anatumiwa wakati yeye alianza zamani kutumiwa siyo kutumika?”
          Mipawa hataki aachwe nyuma. Anakwanyua mic, “Dokta Kapende nakuunga mkono na mguu. Usemayo yana maana sana. Tokana na mfumo wa kisanii, sasa hivi tuna hata wauza bwibwi wanaojiita wachungaji hata maaskofu. Ama kweli kaya imeingiliwa na mdudu huyu wa ufisadi na ulafi. Gwaijumaa akitumika basi kila mmoja anaona anatumika kama yeye!”
          Sofia Lion aka Kanungaembe anakwanyua mic, “Japo kaka zangu huwa natofautiana nanyi mara nyingi. Kwa hili mmenipata kweli kweli.”
          Kabla ya kuendelea, Mbwamwitu anamchokea Sofi na kusema, “Hebu tueleze vizuri nasi tukupate. Wamekupataje?”
          Huku akiwa anatabasamu Sofi anajibu, “Usipate tabu hata nawe utanipata tu. Kusema ukweli huyu kidhabu anatia kinyaa kiasi cha hata kuamsha hisia za udini. Tuliwaonya siku nyingi kuwatahadhari hawa wapingaji wa kila kitu. Sasa nadhani mnaanza kutuelewa hatimaye. Hawa ni waharibifu wala hawana lolote.”
          “Da Sofi mie nimekupata japo sivyo unavyotegemea. Yapo mambo nakubaliana nawe na yapo mengine sikubaliani nawe katu. Nadhani kama alivyosema Dk Silaha, kinyesi ni kinyesi hata kiwe chooni au chumbani. Hivyo, kwangu huyu mchunaji wala hanishangazi anachofanya. Hivi kweli kiongozi wa kiroho anaweza kuwa yule? Mmewahi kusikia lugha ya wapiga debe anayotumia? Sijui kwanini asingejiendea shule lau kujipatia elimu kuliko kuendekeza njaa! Hata hivyo, tuwalaumu hawa waliotawala kaya miaka yote kwa kulea uoza kama huu ambapo kila tapeli anawatapeli wachovu. Huyu ametumia vyote siasa na dini.”
          Kanji naye anaamua kula mic, “Mimi sangaa sana ona hii chunaji nasema ongo mingi. Mimi ona kwa TV. Eti sema bibi ya Silaa nakataza yeye siasa. Sasa veve mambo ya tandani ya Silaa sisi nahusu nini dugu yangu Jimaa?”
          Msomi anarejea, “Kuna jambo mnapaswa muelewe. Nadhani jamaa wanamng’ang’ania Dk Silaha ili waepushwe kung’ang’aniwa wao. Ukitaka kuwakwepa mbwa watupia mifupa. Kwa watu wasomi na ambao wako serious kutaka kuchukua kaya, wangejikita kuichapa nambari wani. Pia kwa watu waliopiga shule na kujua mikakati ya kisiasa wasingeruhusu wahuni na majuha kusimama majukwaani na kujadili mambo mazito wasiyo nayo ujuzi. Huyu Gwajumaa ana madhambi mengi ambayo yakiwekwa wazi kama si kukimbia kaya anaweza kuishia lupango kama si kujinyonga. Nadhani wanaojenga hisia za udini hawakosei.”
          Mzee Maneno anakula mic, “Nasikia hata hii chopa wanayoita ya Gwaijumaa kumbe si yake bali ya Luwasa anayemtumia huyu mchunaji. Hata hivyo, nawalaumi nambari wani kwa kutengeneza mazingira ya baadhi ya matapeli kuwaibia wachovu kutumia dini wakitangaza kufanya miujiza wakati miujiza yenyewe ni kuwatoa mshiko na si zaidi. Huyu Gwajumaa anapaswa achunguzwe kama kweli ni askofu, ukwasi wake na kama ana sifa anazodai anazo.”
          “Mzee Maneno maneno yako mazito sana. Nimependa pendekezo lako la kuchunguzwa akili na ukwasi wa mhusika. Kwa mtu kama yeye angefanya kama akina Rugemalayer na Singasinga wa escrow, kunyamaza akiomba Mungu itokee miujiza asinyee debe ingawa hili hawataliepuka siku moja iwe ni hapa duniani au mbinguni,” Kapende anazoza.
          “Yakhe mie nshawaambia tuunde chama vinginevyo twaweza kuwa kitu cha kupokezana baina ya matapeli wa kisiasa.” Mpemba anaonya.
          Mgosi hangoji Ami amalize. Anachomekea, “Nadhani hapa wa kuanzisha chama siyo si bai Gwaijumaa ili ahubii vizui siasa badaaa ya dini.”
          Kijiwe kikiwa kinanoga si likapita shangingi la Gwajumaa. Tulilikimbiza likatuacha. Vinginevyo tulitaka tunkamate na kutia adabu halafu tumvue majoho na kumvisha magwanda.
Chanzo: Tanzania Daima Sept., 16, 2015.