The Chant of Savant

Friday 31 July 2009

Kijiwe chataka ianzishwe mahakama ya kadhia

BAADA ya Waislamu nchini kuhanikiza wakitaka, pamoja na mambo mengine, na kama, sore, mahakama ya kadhi mkuu, nasi wana kijiwe tumeamua kupitisha azimio la kuitaka sirikali iridhie tuanzishe mahakama ya kadhia, sambamba na hii ya kadhi kama itairuhusu.

Tuna sababu nuzuhu na nzuri tu kutaka ianzishwe mahakama hii tukufu ya kadhia ambayo, kimsingi, itaikomboa kaya kutoka kwenye meno na makucha ya majizi wachache wanaotumia vibaya mamlaka.

Kwa ufupi lengo la mahakama hii ni kupambana na dhambi kuu iitwayo ufisadi ambayo mara nyingi inatendwa na mafala wanaojiona wajanja wakati ni mafala tu.

Chini ya mahakama yetu, mafisi na mafisadi wote watavuliwa nguo na kuchapwa bakora kabla ya kunyongwa hadharani ili liwe somo kwa wote wenye mawazo finyu na hulka za kifisi na kifisadi.

Pia chini ya mahakama yetu ya kadhia, atakayezini na akabainika amefanya hivyo, kama atakuwa mwanaume, shurti abakwe na mwanamke azibwe sehemu yake ya dhambi ili asirudie kitendo hiki kichafu.

Mwanamume atapigwa picha akifanyiwa ufirauni huu ili zisambazwe ajulikane alivyo cho…wahalifu wengine tutakaoshughulikia ni wale wanaoghushi vyeti na shahada ili wapate ulaji.

Hawa tutawapofua macho ili wasiweze kuona tena na kwa hiyo waanze kuomba omba badala ya kukiibia kijiwe. Pia tutawakata mkono wa kulia ili wasile tena mali ya umma. Ikumbukwe.

Sisi hatuna magereza. Hivyo adhabu zetu nyingi ni kufagia viungo na kunyotoa roho. Unadhani bila magereza kama tutapendekeza vifungo tutawafungia wapi zaidi ya kuadhirika?

Pia chini ya mahakama hii, tutahalalisha pombe na kupiga marufuku ulevi, hasa ule wa madaraka. Wale wote waliokwisha kukumbwa na ugonjwa wa kulewa madaraka, watafungwa maisha ili kuepusha kuiharibu jamii.

Kwa atakaye kunywa pombe akalewa adhabu yake ni kwamba akiingia peponi baada ya kurudisha namba atakunywa soda na maji baridi tu. Maana atakuwa amefanya kosa kubwa, yaani uchoyo na kuvuka kiwango kilichowekwa cha kunywa kwa ajili ya afya.

Wanaume watapaswa wavae ninja, nao waonje joto ya kuivaa hasa sehemu zenye joto kama vile pwani. Pia tutafanya hivyo ili kina mama wasiwatamani.

Atakayegundulika kutembea bila kuvaa ninja atachapwa bakora hamsini na kupigwa marufuku kutoka nje kwa miaka mitano. Dini yetu inahimiza wanaume wavae ninja ili kuleta usawa na suluhisho baina ya jinsia mbili ambazo zimekuwa zikinyonyana na kutumikishana ukiachia kudhalilishana.

Mahakama yetu inatamka wazi kuwa wanaume wengi ni waongo wa kupindukia. Ni mabingwa wa kutoa ahadi lakini wasitekeleze. Ni mabingwa wa usanii na ujambazi mbuzi.

Wanawaahidi kina mama kuwapeleka Kanani, wanaishia kuwapeleka motoni. Waongo wote watakatwa midomo ya juu ili kila wapitapo wajulikane na wananchi wawaepuke na kutowasikiliza.

Pia chini ya mahakama ya kadhia, itakuwa ruksa kuchanganya dini na siasa. Chini ya mahakama hii, watu wa dini watafanya siasa kwa kujificha nyuma ya majoho yao na wanasiasa watatumia nyumba za ibada kueneza siasa zao.

Katika mahakama ya kadhia, dini na siasa vinachanganyikana na haviwaki kama ambavyo matapeli fulani wamekuwa wakiwatisha wanakijiwe ilhali wao wanavichanganya vitu hivi.

Pia mahakama yetu itatoa tangazo la thamani kwa binadamu. Mwanamke mmoja ana thamani sawa na wanaume watatu. Tulifikia ugunduzi huu baada ya kubaini kuwa wanaume wengi ni mafisadi na mafisi kuliko wanawake na wanadanganywa kirahisi na nyumba zao ndogo kama tulivyoona kwa Kingungo Ngumbaru Mwehu pale Ubungo, Benjaa Makapa na Anibeni, Dadi Balallii, Njaa Kaya anavyotumiwa na Salama Hatari kwa sasa na Anna Mgando na wengine wengi. Hivyo hata kwenye mahakama yetu, ushahidi wa mwanamke utakuwa na nguvu kuliko wa wanaume wawili hata watatu.

Pia wanaume wamegundulika kuwa waharibifu kupindukia. Wanawatelekeza hata watoto ukiachia mbali kuwazalisha ovyo kina mama wanaowakimbia na kuwaachia watoto. Pia uchunguzi wetu umegundua kuwa wanaume wengi hupoteza pesa nyingi kwenye nyama choma, manywaji na nyumba ndogo.

Hivyo kuwakomesha ni kuwatungia sheria ngumu ili kuwaadhibu na kuwadhibiti. Pia chini ya mahakama yetu, wanaume watakuwa wakipeleka watoto kliniki na kuwalisha wawapo nyumbani.

Pia mahakama yetu itahalalisha kiti moto ili kupunguza bei ya nyama ya ng’ombe na kuzidi kuuawa kwa viumbe hawa wasio na hatia. Tutafanya hivyo ili kuangalia kama kweli homa ya nguruwe H1N1 ni hatari. Tutawatumia watu wetu kufanyia majaribio kama wanavyotumiwa na mafisadi wa kiutawala kwa sasa.

Mahakama tukufu ya kadhia pia inatamka wazi kuwa imani asilia ndizo zitoe muongozo wa kuendesha kaya badala ya hizi nyemelezi za kikoloni na kimapokeo. Chini ya mahakama hii, majina yote ya kigeni na kishenzi yatafutwa na dini zote zitaomba radhi kwa umma kwa kutuita washenzi, makafiri na wapagani.

Chini ya mahakama hizi, dini zote nyemelezi na za kimapokeo zitatozwa kodi kubwa kutokana na kuchuma mahali ambapo hazikupanda, hasa kwa njia ya sadaka.

Tutapiga marufuku matangazo ya miujiza ya kiwizi ya kuwaibia wanakijiwe huku tukipiga marufuku makelele ya mahubiri na kuitana kwenda kusali.

Chini ya mahakama ya kadhia, rais atapaswa kuwa mtu asiye na dini yoyote ya kimapokeo isipokuwa ya asilia. Na kaya itaendeshwa kwa sheria za mizimu na mababu.

Chini ya mahakama ya kadhia, wafadhili wote watapaswa kutulipa riba wanapotukopesha maana sisi ni watu wa nchi takatifu tupaswao kufaidi utajiri na matunda ya mataifa ya nchi nyingine.

Pia chini ya mahakama ya kadhia, wakoloni weupe wataruhusiwa kurejea ili kuwaondoa hawa weusi ambao wamethibitisha kuwa wezi, walafu na wenye roho mbaya ukiachia mbali upogo na upofu.

Chini ya mahakama ya kadhia, umri wa kuoa au kuolewa ni miaka 30 ili wahusika wawe wameishaanza kujitegemea na kufundwa. Hakuna cha kuonjana au ‘engagements’ ambazo zimeonekana kuwa kichaka cha umalaya.

Pia chini ya mahakama hii tukufu, watuhumiwa wote wa ufisadi hawataruhusiwa kukaribia nyumba za ibada wala kutoa michango na misaada yao huko.

Pia chini ya mahakama hii, wanasiasa watakaogundulika kuwadanganya wananchi, watakatwa midomo na kufungwa ili wasiendelee kuiharibu jamii.

Sheria ya mahakama ya kadhia itatangaza wazi kuwa Bunge, ikulu na sehemu nyingine za usanii zigeuzwe mabaa ili watakaoingia humo wajulikane ni walevi ambao ulafi wao utawakosesha manywaji huko peponi.

Chini ya mahakama ya kadhia, waheshimiwa wote wanaoutumia uheshimiwa kuwaibia walala njaa wataitwa wadharauliwa na watakaogundulika kuendelea kuwaibia wananchi, adhabu yao itakuwa ni kuvishwa magunia na kutandikwa bakora uchi hadi warejeshe pesa yote waliyolipwa kwa kuhadaa umma.

Chini ya mahakama yetu tukufu, wezi wote walioibia kaya watanyongwa bila kujali kama walikuwa wakubwa au wadogo. Kwa mfano baada ya kupitishwa mahakama hii, wezi wenu wa Kiwira, EPA, Kagoda, Richmond, watauawa kwa kuchomwa moto kama vibaka ili liwe somo kwa wengine wanaopanga kufanya makufuru kama haya.

Pia tutafufua makaburi ya wale waliokufa bila kuadhibiwa na kuzichapa bakora maiti kabla ya kuzizika kwenye mashimo ya taka. Kwa wale waliokimbiziwa nje ya nchi, tutatuma mahakimu wetu wawahukumu huko huko na nchi itakayokataa kushirikiana nasi, basi watu wake watakuwa halali yetu tutakapowateka.

Huu ni mwanzo wa madai. Baada ya kupata mahakama ya kadhia, tutadai na kodi ziendeshwe kwa imani ya dini yetu huku tukihanikiza baadhi ya mambo yapigwe marufuku.

Tutapiga marufuku kuongezeka kwa watu wasio wa dini yetu ya asili. Tutawarejesha kwenye kundi ima kwa pesa, ulaghai hata nguvu ili mradi tuwe na wafuasi wengi tuweze kuitawala kaya na hatimaye dunia nzima.
Chanzo: Tanzania Daima Julai, 29.2009.

Thursday 23 July 2009

Kilango, Selelii na wengine someni ya Wilfred Kajeke

IF "I have this mandate to stop this reckless and irresponsible mortgaging of our country and I cannot do it, then there is no reason for me to continue being in this House. That is why I am leaving, not for a UN job, rather, to liberate my conscience.”

Tafsiri: “Kama mamlaka haya niliyo nayo (ya kuwa mbunge) hayawezi kuzuia uchuuzi huu wa nchi yetu, na siwezi, basi sina sababu ya kuendelea kuwa kwenye bunge hili. Na hii ndiyo sababu naondoka, si kwa kupata kazi Umoja wa Mataifa bali kujikomboa.”

Haya ni maneno mazito ya Mbunge Wilfred Kajeke wa Jimbo la Mbale, Uganda baada ya kuchoshwa na tabia ya bunge kugeuzwa muhuri wa kubariki ufisadi wa kimfumo kama ilivyo hapa kwetu.

Alijiuzulu kwa hiari baada ya kukaa bungeni kwa miaka minane na kugundua kuwa anazidi kujiumiza roho kwa kushiriki ujambazi wa kimfumo kama ilivyo hapa kwetu.

Baada ya kusoma tukio hili la kusisimua na somo kuu katika uwajibikaji na uwazi, haraka haraka majina ya mashujaa wetu wa maneno lakini woga wa vitendo kama Anne Kilango Malecela, Lucas Selelii, Fred Mpendazoe na wengine yalinijia haraka.

Nilitumia muda mrefu kufikiria kuandika makala hii kuwakumbusha wahusika kuwa, wanachofanya ni kujidhalilisha hata kama kuna watu wachache wanaoona kama ni ushujaa au ujasiri. Ujasiri si kusema bali kutenda. Wako wapi kina Kajeke wetu?

Mbunge aligundua kuwa anabeba dhambi kubwa kushiriki uharibifu na uchuuzi wa nchi yake, tena akiwa amekalia kiti cha uwakilishi wa umma. Ameona ni heri akose maulaji na ujiko kuliko kuendelea kuwa mnafiki na mtumwa wa tumbo. Ameaamua kutumia kichwa baada ya kuchoka kutumia utumbo.

Je, wabunge wetu waliotuaminisha wangekwamisha, kwa mfano, bajeti ya Mstaafa Mkulo na baadaye wakalamba matapishi yao kwa kuipitisha, wanaposoma au kusikia habari kama hizi wanajiona wa hovyo kiasi gani?

Je, wabunge wa namna hii si watumwa wa hiari? Je, hawa wanaopinga ufisadi kwa midomo na kuubariki kwa kura zao katika kupitisha miswaada si mafisadi kuliko mafisadi wenyewe ambao kimsingi hujikalia kimya ili umma uwajue wao ni nani kuliko hawa mafisadi wanaojifanya wanapinga ufisadi kwa midomo na kuubariki kwa mikono yao?

Lazima uwe moto au baridi lakini si vyote kwa wakati mmoja. Lazima uwe na mimba (fisadi) au usiwe nayo.

Hakika msimamo wa Kejeke ni somo na suto kwa wachumia tumbo wetu wanaojigeuza mbogo dhidi ya ufisadi kila uchaguzi ukaribiapo ili kuwaaminisha wananchi kuwa wanawawakilisha ili baadaye wawachague waendelee kuwabamiza mkenge.

Wamekuwa mabingwa wa kulipua mabomu yasiyoweza kuua hata nzi! Kila siku viapo na chokochoko visivyozaa matunda. Mafisadi wanaendelea kupeta huku wao wakikauka makoo kumbe lao moja.

Kama si moja basi achieni ngazi kama Kajeke. Fanyeni kweli. Tumechoka na longolongo zenu. Kama hamuwezi mnyamaze kuliko kutupigia mikelele wakati nanyi ni mafisadi.

Katika hili, Kajeke ana ushauri: “Either to join the system and fully participate in the looting or say enough is enough. I have chosen the latter and I am leaving.”

Tafsiri: “Ama kujiunga na mfumo (serikali) na kushiriki ujambazi au kusema imetosha. Nimechagua la pili na naondoka.”

Kama mamlaka uliyo nayo hayakusaidii kuepusha nchi yetu kutaifishwa na kina EPA, Richmond, ANBEN, TICTS, Dowans, IPTL na wengine, basi wewe ni mtumwa na roho yako inakusutu. Kuendelea kukaa bungeni ni utumwa wa hiari kwa ajili ya kutumikia tumbo lako. Unahitaji ukombozi kwa kuacha kuchaguliwa ili kina Kajeke waje wawakomboe wananchi baada ya kujikomboa wao.

Je, tunao kina Kajeke wangapi Tanzania? Huwa nashangaa mantiki hata ya wabunge wa upinzani kuondoa shilingi ili bajeti ikwame na rais avunje Bunge kama kisemavyo kifungu cha Katiba cha 90 (2) (b), ambacho Spika wa Bunge, Samuel Sitta, alikitumia hivi karibuni kuwanyamazisha na kupitisha bajeti ambayo kimsingi ni ya maangamizi kwa wale wanaodai kuwawakilisha.

Hapa ndipo ukweli kuwa unaweza kumuamini yeyote lakini si mwanasiasa unajidhihiri. Ingawa tumekuwa tukiwasifu wabunge tunaowaita machachari, ukweli ni kwamba umachachari wao kama hauwezi kuiadabisha serikali ikaacha kutuibia ni sawa na umachachari wa kibonzo au katuni. Hawa wabunge ni sawa na simba wa karatasi asiyeweza hata kumpoka nzi.

Tumalizie kwa maneno ya Kajeke. “Don't let the people of Uganda down. If you do, one day you will encounter them at your gate or on the streets of Kampala, demanding for their share.”

Tafsiri: “Msiwaangushe wananchi wa Uganda. Mkifanya hivyo, siku moja mtapambana nao kwenye geti au mitaani Kampala wakitaka shea yao.”

Nanyi wabunge wetu wapenda sifa na kulipua mabomu, msiwaangushe wananchi wa Tanzania. Kuna siku usaliti huu utawatokea puani. Kwani wamevumilia vya kutosha na sasa wamechoka.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 22, 2009.

Kijiwe chaandaa nishani ya ufisadi kumtuza Njaa Kaya


KWANZA Kijiwe kinaomba msamaha. Ilipita miezi mingi bila kuwasikia akina Mgosi Machungi, Mzee Kidevu, Mbwa Mwitu, Mpemba, Kapende na Mzee Maneno pamoja na wengine bila kumsahau Makengeza au Kenge kwa ufupi.

Tunaye mwanakijiwe mpya Mipawa wa Pawa. Tulikuwa na udhuru mkubwa hasa kushiriki chaguzi kule Biharamulo na Busanda ambapo lafu ilichezwa sina mfano.

Baada ya kuachana na mambo ya siasa, sasa Kijiwe kimerejea kwenye shughuli za kawaida. Kumbuka hiki si kama kile cha Idodomya ambapo kutishana na kuapizana kukwamishiana bajeti ni maigizo ya kawaida.

Sisi tunafanya shughuli za kijiwe vilivyo. Hatupayuki ili wanakijiwe watuchague tuwabamize tena mkenge kama jamaa zetu wa Idodomya ambao, kama vyura, kila mmoja anahanikiza utadhani anawapenda walevi wakati anawaponda! Sisi tunawakilisha wanakijiwe na si matumbo yetu.

Nikiwa nimejiinamia nikimsaka mtu wa kubomu lau nyumbani watoto waende nonihino, mara Mpemba anatuamkua “Assalaam alaykum jamia.”

Muuza kahawa anakuwa wa kwanza kuitikia “Walikuwa waislamu.”

Inaonekana Mpemba ana jambo linamhini. Kwani hata utani wa muuza kahawa hausikii. Anaanza hata bila kungoja kuulizwa ni yaje.

“Mmesikia hawa walafu na mafisadi eti wasema mafuta si saala la muungano? Sie Pemba twaangalia tu. Mbona wao walitumia karafuu yetu kujenga Unguja hatusemi? Sasa washikilia mafuta hata yasovumbuliwa."

Kabla hata ya Mpemba kujibiwa, mara Mgosi Machungi anaingia na gazeti la “Waambie”. Anatusomea habari. “ rofesa Ibueim Ipumba amuipua Njaa Kaya Kikwekwe na kusema ndiye baba wa ufisadi wa EPA na Richmond.”

Kapende anadandia mic. Anasema, “Hii si habari mpya. Sema kwa vile aliyemtaja msanii ni mzito wa chama. Je, walevi watastuka na kumshikisha adabu? Hata kunguru wanajua Njaa Kaya, nkewe na genge lake walivyo EPA na Richmonduli.”

Anakohoa na kubwia kahawa yake kidogo na kuendelea. “Mna habari Njaa Kaya alidhani anaweza kuukimbia ukweli kwa kumtoa kafara Mzee wa Richmonduli Ewassa.”

Mzee Maneno anakwanyua mic. “Ushuzi siku zote huwezi kuuficha kwa kujitia marashi. Inzi lazima watakufuata kama ambavyo Njaa Kaya hataukimbia ukweli. Kila mtu anajua alivyotumia pesa ya EPA na Richmond kutoa takrima na kuibuka kwa ushindi wa Tsunami unaogeuka kuwa Tsunami kweli.”

Mgosi Machungi anadakia. “Ajabu bado anatiaminisha timchague aibe tena. Kama kipindi cha kwanza ametiibia hivi hiyo lala saama itakuwaje; si atatiibia hata wake zetu jamani.”

Mipawa hajivungi; anajibu haraka. “Awaibe mara ngapi? Hamuoni, kama Tunituni na Anna Tamaa, anavyowatumia wake zetu chini ya NGO, lake wizi mtupu? Wake zetu wameishaibiwa taka usitake.”

Mbwa Mwitu anachomekea haraka haraka. “Kuiba au kutowaiba wake zetu mimi haliniangaishi. Kinachonihangaisha ni kuiba mstakabali wa taifa.” Wakati akisema haya Mgosi Machungi anamkata jicho na kusema. “Ina maana wewe huna uchungu na mkeo!”

Mbwa anajibu kwa utani. “Nina uchungu hasa na mkeo.”

Machungi anatahadhalisha. “Mbwa angaia maneno yako. Tinaweza kutoana macho wenyewe kwa wenyewe. Kama una uchungu wa kuipiza kisasa si uende unchukue mke wa Njaa Kaya anayetumia wake zetu ili nae aone uchungu?”

“Loo! Mbwa Mwitu ndiyo unazidi kulikoroga kabisa, eti anawatumia wake zetu!” Anachomekea Makengeza.

“Anatutumia wote. Huko nyuma haikuwa hivyo. Je tumelogwa kiasi cha kujirahisi na kuendelea kuchezewa kuliko huko nyuma.” Alidakia Mchunguliaji aliyekuwa akichungulia vichwa vya habari.

Mara Kapende anadaka mic. "Jamani wabongo kwa matusi sina hamu. Huko nyuma na kuchezewa maana yake nini?" Wakati huo Mzee Maneno ndiyo alikuwa anamalizia kipisi chake cha sigara kali.

Abusu mic. "Njaa Kaya kweli anatuchezea na kujichezea mwenyewe. Maana anafanya mambo kana kwamba hakuna kesho. Nasikia anaumwa ugonjwa wa moyo kutokana na kutaa taa akitafuta jinsi ya kulizima jinamizi la EPA na Richmond. Kwani hata alipomtoa kafara rafiki yake Ewassa bado zimwi linamuandama vilivyo."

Kabla ya kuendelea, Mzee Kidevu anamwingilia na kusema. "Nasikia kweli jamaa anaumwa. Maana akina Kagoda wametishia kumfichua kama atawafichua au kuwafikisha mahakamani. Hivyo anaomba Mungu uchaguzi ufike mwakani apete na ahomole na kukitoa akingojea majaliwa yake kutokana na atakayemrithi."

Machungi anatia timu tena. "Kuna kipindi tinapaswa tijilaumu wenyewe kwa kuendeea kugeuzwa mazuzu. Kwanini tisiandamane hadi ikuu kumwambia akitoe wenye akili wationgoze?"

Mpemba hajivungi. Anakwanyua mic. "Yakhe Ngosi, mie naunga nkono mawazo yako. Kutonkabili Njaa Kaya kwamfanya aone wote wakeze ati. Jamaa ana roho ya paka yule. Hata useme vipi yeye anyamaa na kuendelea vuruga mambo. Umeona alivonywea kwenye sakata la mahakama ya kadhi na chochoko choko cha kujiunga na OIC?"

Anatwaa kombe na kulibusu kidogo na kuendelea. "Sasa kila kitu afanya huyu wa Kupinda ambaye naye apindisha mambo ati. Wajua huyu bwana njinga sana? Wakumbuka alivontetea Nkapa eti si fisadi, ni ncha Mungu wakati jizi na familia yake?"

"Yakhe mwache huyu jamaa. Nilikuwa namheshimu sana. Lakini baada ya kujigeuza dodoki la fisadi Tunituni nimemponda kuliko hata kuku na Njaa Kaya. Sikujua jamaa angetumiwa kufanya uchafu kama huu. Tusilaumu sana. Tunatawaliwa na mafisi na mafisadi." Anachomekea Mbwa Mwitu.

Mzee Mzima naona kama mada itaisha bila kukamua. Naamua kuvamia uga ili nisije nikafulia. "Wazee tuambizane ukweli. Njaa Kaya anapoteza muda. Hata Tunituni alipoonywa kuhusu ufisadi hasa wa mkewe alijigeuza mbogo. Njaa Kaya ameamua kutumia njia ya kunyamaza akidhani atapona. Kila lililo na mwanzo sharti liwe na mwisho."

Nakatua kashata na kuendelea. "Jamaa kaishiwa hakuna mfano. Siku hizi gazeti lake la umbea la Daily Wizi linaonyesha video ya safari yake kwa Obama. Ajabu wanaandika upuuzi eti Obama alimsifia kuwa kiongozi wa kuigwa barani wakati yu habithi!

Kama alimsifia kwanini aliamua kumpiga kibuti na kufanya ziara nchini Ghana badala ya Bongolala? Alijua jamaa lilivyo sanii na fisadi. Wataendelea kuwadanganya wajinga wenzao lakini si kijiwe chetu. Mie naona tungeandaa nishani ya usaliti na ufisadi tumpe Njaa Kaya ajue sisi si wa kuchezea. Nishani ya pili tumpe nkewe na ya tatu tumpe Tunituni na Anatamaa. Mnasemaje wazee?"

Wanakijiwe wanalipuka kwa vicheko na vigelegele huku makelele yakihanikiza kiasi cha kuwavuta wapita njia ambao wanasimama kwa mshangao na mshawawasha. Si mnawajua wadanganyika kwa kupenda kushangaa.

Mie sijali naendelea. "Aibu kuwa na sanii kwenye patakatifu pa patakatifu. Mnaona aibu aliyotuletea kwa kumuunga mkono habithi Humer Shari wa Sudan? Jitu limenyonga watu wake nasi tunaliunga mkono lisikamatwe na mahakama ya kimataifa ya jinai. Mnafahamu yule mwendesha mashitaka wa ICC, Luis Moreno Ocampo tulisoma naye ughaibuni?"

Wanakijiwe wanaonyesha mshangao. Wanajua hizi ni kamba za mzee mzima. Ila ukweli ni kwamba Ocampo ni rafiki yangu na kuna siku nitamkaribisha kuwakamata wauaji wa kwenye migodi kule Musoma wanaoua watu kwa kuchafua mazingira.

Mara Mgosi Machungi anachomekea. "Hata Njaa Kaya na kundi lake wanapaswa kufikishwa Uhoanzi kujibu tuhuma za kuua wadanganyika kutokana na ufisadi wake. Nao wanafanya mauaji ya haaiki kwa kutumia umaskini badala ya bunduki."

Tom anaingilia kati. "You are right Mgosi. Una habari kama kosa la kuuibia umma litatafakariwa vizuri akina Njaa Kaya ni wauaji sawa na wale wanaofanya genocide nchini Sudan? Normally ufisadi huzaa upendeleo na chuki miongoni mwa wanajamii kiasi cha kusababisha umwagaji damu. Tunaelekea huko ingawa wezi wetu hawataki kukubali.

Hebu nieleze. Bunge letu lina maana gani iwapo bajeti za kipumbavu kama ile ya Mstaafu Mkulu inapita huku pesa nyingi ikiibiwa kwenye bajeti iliyopita? Actually, we need to.."

Kabla ya kuendelea mzee Kidevu anaamua kuvamia uga kumtahadharisha Tom apunguze umombo.

Anasema. "Msomi taratibu. Unatuaacha nyuma. Angalia lugha msomi."

Kabla ya Tom kuendelea, naona vimbelembele wawili wakiwa kwenye magwanda yao wakijongelea kijiwe kutokana na zile shamra shamra za kutaka kutoa nishani. Kila mmoja anajikata kisilesi na kumwacha muuza kahawa akitaataa na vyombo vyake tayari naye kutimka.

Tuonane wiki ijayo inshallah.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 22, 2009.

Wednesday 8 July 2009

Omar Bashir Indictment: AU has Betrayed Africa


Bashir: Peacemaker or troublemaker? Photo courtesy

It is disgusting and appalling that African rulers congregating in Sirte (Libya) vowed to stand by Sudanese President, Omar Bashir. African rulers have once again proved to be hypocrites and indifferent altogether as far as human rights are concerned. Sadly, Rwandan strongman, Paul Kagame who claims to have stopped the genocide in Rwanda, too, concurred with this megalomania whilst his country suffered the same genocide as Darfur. It's unfortunate. Africa did not learn from what transpired in Rwanda.

Again, looking at how genocide was committed in Rwanda, who knows? Maybe Kagame has smelt a rat before ICC knocks on the door. The Swahili have a saying that when you see your colleague being shaved without water, rinse your head. African rulers wrongly think ICC is there to foster colonialism and interfere in their affairs thanks to taking on one of theirs. This does not help AU. And if reality is openly faced, chances are, African rulers were manipulated by the current chair of AU, Libyan Muammar Gadaffi.

If Bashir did not commit genocide in Darfur, why is he afraid of facing the ICC? Given that genocide was committed under his watch and order, Bashir can do anything but not to appear before the tribunal. This reminds me of one cartoon showing him driving over thousands of human skulls but still asking: do you have any evidence to prove that my Janjaweeds committed genocide in Darfur?

In its vague bagatelle, AU averred, "The AU member states shall not co-operate... relating to immunities for the arrest and surrender of Sudanese President Omar al-Bashir to the ICC." This betrayal was applauded and received by Sudan as a breakthrough in getting away with genocide Sudan committed to Darfur.

When AU, then OAU, was founded, its aim among others was to unify and ultimately emancipate African countries from the yoke of colonialism and all sorts of humiliation, degradation and inhumanity. But as days go by, AU has proved to be the opposite thanks to Africa being ruled by dictators, thieves and killers. Ironically, black colonialists are on the helm. AU's goals have changed from fighting colonialism to defending it as its members are homegrown colonialists.

One would expect AU to issue a statement with regards to what is going on in Gabon where the son of the former tyrant is bracing himself to replace his father. AU is expected to chart the way for Zimbabwe whose prime minister, Morgan Tsvangirai, recently came back with empty hands after western countries failed to live up to their promise of rebuilding Zimbabwe after embracing the government of national unity.

Many African countries have betrayed Darfur as it bleeds to death. They are adding more insults to injuries by ganging up with Bashir. With such nugatory stance, AU has proved to be a gang of dictators in power as far as emancipation and unification of Africa are concerned. It's totally failed to solve crises in Darfur, Somalia and Zimbabwe. Though noises are made on unification of Africa, looking at how our potentates behave, this is a day dream if AU can conspire with and connive crimes like genocide in Darfur.

AU should have shut up and put up rather than taking side. This won't help begging Africa so to speak. Of all African countries, Botswana and Kenya did the right thing by not consenting to this betrayal and shame. In law, the perpetrator of any offence is criminal and liable as the conspirator. Since genocide in Darfur has all blessings of AU, the AU must be held responsible for it. Even its bagatelle was passed without voting.

Donor countries that strongly support ICC must suspend their aids to all African countries that shamelessly support this perilous stance that butchers its own people it is duty bound to protect. African countries that signed the instrument establishing ICC must be reminded of their obligations.

Despite the fact that African rulers allege that ICC is interfering in their affairs, no sane mind can consent to this. The so-called 'their affairs' ICC is alleged to interfere with are the same that caused genocide in Rwanda. Why do African rulers forget easily? Under Idi Amin, Uganda suffered a lot thanks to the same pretext of not interfering in the affairs of the country. It also happened in Zimbabwe as Robert Mugabe sent the country to purgatory as the same AU stood by him.

AU can wrongly assure itself that it will save and protect Bashir but history will one day persecute him. He has been given visas to travel in the continent without any hitch and fear but time will come when some countries will see the light and take on him as it happened in Liberia. By fully or partially supporting Bashir, indeed, AU has proved how awkward it is.
Source: The African Executive Magazine July 15, 2009

Tunituni na Chekacheka wasameheni waishiwa


Nillinyaka juzi kuwa jamaa wa kupinda kawafunga walevi kamba eti mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwila utatwaliwa na kurejeshwa serikalini. Kwa juu, hii ni habari njema. Lakini ukiangalia tabia ya longolongo na sanaa za jamaa yangu Chekacheka, unhhh, unapata wasi wasi kama kweli wa kupinda anajua anachosema bila kupindisha.

Nao waishiwa, baada ya kulazimishwa kupitisha upuuzi, sorry, bageti ya Mstaafu Mkulu kwa kutumia katiba viraka, nao wamejitutumua! Wanataka kumjadili Tunituni kabla ya kunyang’anywa mgodi. Mlikuwa wapi muda wote huu?

Kusema ukweli, mimi na Chekacheka tusingetaka Tunituni ajadiliwe wala kuchunguzwa. Tunataka tuchukue mgodi ili kufunika kombe wanaharamu wapete. Waishiwa wakitaka tumjadili tutaumbuka wengi. Kwanza, Chekacheka alishasema atamkingia kifua hadi anang’atuka baada naye kunyakua atakochoridhia. Si unajua tena kaya ya ulaji na Bongolala.

Kwa vile waishiwa hata Chekacheka wanakabiliwa na kiminyo mwakani kwenye uchafuzi mwakani, kila mtu ajitutumue ili asikike. Sisi, tumeamua kurejesha mgodi kwanza, ili kumuepusha jamaa yetu Tunituni kwenda lupango kama jamaa yetu pale Zambia. Pili ni kutaka kupata kura za walevi. Maana ukifika wakati wa kampeni hili litageuka dili na sera. Si unajua tena mambo ya kuusaka ulaji wa dezo.

Hakuna haja ya kumchambua Tunituni kama karanga. Kwanza ni mtu safi anayemcha Mungu kweli kweli. Ila kumbukeni. Wacha Mungu tuko wengi. Mie namcha Mungu pesa; wengine Mungu madaraka na wengine Mungu sifa mradi kila mtu ni mcha Mungu. Hata yule jamaa yangu wa Richmonduli ni mcha Mungu kwelikweli. Amewahi kwenda hata Yerusalimu kuhiji baada ya kuona kuwa Mungu wake wa tamaa halipi. Hivyo aliamua kumrejea Mungu wa Israeli.

Kwa walevi wasiojua ulaji unavyolewesha, wanadhani Tunituni alikosea kukwapua alichokwapua. Hivi ulitegemea nini na angefanya nini wakati Bi. Mkubwa, kama alivyo wa Chekacheka, alikuwa akimweka majaribuni kila siku ukiachia mbali shemeji zake.
Kwanza angeogopa nini iwapo na geshi nalo alilipa ulaji tena unaomeremeta kama dhahabu na almasi? Kimsingi, Tunituni, kama Charles Ponzi na Bernard Madoff, ataacha legacy ya upatu. Wakati wachezesha upate wenzake walichukua pesa ya wateja wao, Tunituni alichukua mali za walevi wake.

Ingawa hayajawakuta, hali inavyokwenda, msishangae ya Tunituni mkaona ya Chekacheka. Heri ya Tunituni mvua tano za kwanza alifanya kweli kuliko Chekacheka aliyeshindwa kabla hata ya kuanza kuwatumikia walevi ambao aliamua kuwatumia badala ya kuwatumikia.

Nawaonea huruma waishiwa. Hivi wao wana udhu gani wa kumjadili Tunituni iwapo wamepitisha bageti ya makufuru na matusi? Kama kuna wa kumjadili Tunituni basi si wengine ni wale waheshimiwa wa upinzani lakini si waishiwa wa nambari ziro. Kwanza jamaa hawa ni wanafiki na woga. Juzi niliandika ukurusa mzima kuwasifia kwa kukamia kukwamisha bajeti ya Mkulu halafu wakaipitisha kwa kishindo cha Tsunami! Hawa hawafai na hawana hata maana.

Kwanza nawahurumia. Sijui kama wengi watarudi kutokana rekodi yao ya kupenda kukaa Bongo wakifanya umachinga badala ya kwenda kwenye majimbo kuwahudumia walevi. Wapo ambao wamepata nishani za ububu. Yaani jitu linalipwa mshahara na marupurupu mazito tena linatembelea shangingi halafu linakwenda bungeni kufanya ushangingi!
Nilishangaa kuona mmoja wa mabubu haya anajitutumua kuwataja nyangumi baada ya kumfichua kuwa yeye ni papa. Kwa maslahi ya waliompa kula hana muda wala maneno ya kusema. Ila kwa maslahi yake na Kagoda anachonga kama kasuku! Je huyu naye anapaswa kurudi jamani hata kama anawahonga wapenda nyama nyama?

Hakuna watu nina usongo nao kama wale mawaziri wanaojifanya uwaziri ni mali ya kurithi kiasi cha kuwadharau waishiwa. Hata kama ni waishiwa,si wameishiwa wenyewe lakini si wale waliowatuma. Hivyo, tutaona. Kama kuna watu wenye hati milki za uwaziri tutajua. Hata uwe shemeji yake bosi au mshirika wake, bado si dili kuwadharau waishiwa waliotumwa na walevi wawakilishe shida zao. Ajabu tena bila aibu, wengine walifikia hata kufuru ya kutetea mapapa wakijua kufanya hivyo ni kuwahujumu na kuwasaliti walevi. Hata kama ni walevi jamani watendeeni haki. Kwani hamjasikia? Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kuna kesho.

Turejee kwa Tunituni na Chekacheka na jamaa yetu wa kupinda. Tumeamua kurejesha huo mgodi ili kuepusha kuwasweka rumande jamaa zake hasa Bi Nkubwa na watoto. Baada ya kuona yaliyomfika first lady Regina Chiluba pale Zambia, washauri wetu wametwambia: tukiendelea kulaza damu Anna Tamaa Tunituni na vitegemezi, na vivyele vyake wanaweza kujikuta wakinoniho kwenye debe kule Ukonga alikowahi kusota mshikaji wake wa zamani Pesatatu.

Hivyo kuwaokoa hawa, ni kuchukua godi bila kutoa maelezo kibao ili kuepuka kuwapa wambea faida. Pia kufanya hivi ni kuepusha jamaa zetu kudaiwa fidia kwa muda waliolikamua godi.
Pia tunazuia waishiwa wa nambari ziro kujadili suala hili ambalo baadaye watalipitisha kama bajeti, ili kuepusha kuwapa nafasi wale waheshimiwa wa upingaji kuzidi kutuanika na kustukia madili yetu mengine.

Pamoja na yote, tumeona kuepusha lawama, tumpe wa kupinda alipue bomu. Maana yeye kwa cheo chake cha uwaziri mkubwa anateuliwa si kuchaguliwa kama sisi. Hivyo jamaa lazima afanye kazi ya kusafisha uoza wetu ili walevi watuamini na baadaye watupe kula tuwafungie mzigo kama Tunituni ngwe yetu ikiisha.

Kitu kingine, k ama waishiwa wangekuwa wanawawakilisha walevi kweli na si matumbo yao, wangekuwa na kila sababu ya kumjadili Tunituni. Wengekuwa safi wangefanya hivyo bila shaka. Pia kiama chetu hakiwezi kuruhusu mchezo huu kwa kujichoma kisu mwenyewe ikizingatiwa kuwa ukiruhusu mjadala watakaoumilki ni wapingaji wetu. Hata hivyo kwa mujibu wa sera zetu za chukua chako mapema, Tunituni ni shujaa wa kupigiwa mfano. Ndiyo maana wa kupinda aliamua kummwangia ujiko kibao. Ni muadilifu kuliko Tunituni na waishiwa waliopitisha libajeti lisilo na maana kwa walevi.
Naona simu ya Tunituni. Acha nikaijibu haraka.

Monday 6 July 2009

Vote for me come next elections

My name is Fisadi son of Mbangaizaji. We’re having general elections next year, I better to start campaigning even if the electoral commission hasn’t declared it yet.

Given this is the season for ulaji through ballot box, I’m prepared to serve you. Though I deserve no honour, I still want to be referred to as honorable Fisadi. No way. I can’t let this chance slip by.

I’ve already put strategies in place. Firstly, I’ve already acquired seven college degrees from Commonwealth Nonexistent University , Hazard, and Eden-bug, Open University of the World (OUW), New York and Kuchonga University Bangarole, India .

I also have already talked to Gabacholi and Arab tycoons to sponsor my campaigns so that after I become an MP I see to it they invest in Bongolala. Given that I’m going to become a law maker, I’ll see to it that we enact favourable laws for them to be able to do capital flight business comfortably.

To begin with, I’ll donate money to youth and women clubs and some schools in my constituency.

My Dubai based Arab friend will pour money like crazy to bribe all members of select committee at the tune of 500,000/- per head.i ‘m sure they’ll swallow the bait without any question.

Nonetheless, I was not mentioned in EPA and Richmond Deep Green Finance, Meremeta,, Kagoda and other vampiric scams, I got some cut from them. Don’t tell anybody and when you read this make sure you do it silently. My cut will be employed on bribing sippers and their wives who like free clothes like Khangas, T-shirts, BBQ and other nonsense. Mind you. I’m neither a shark nor a whale though a fisadi.

I’ve already gotten some Kanjanjas that will decorate my name in their newspapers. My slogan is: hither comes God-chosen saviour that will deliver sippers to Canaan in the country of barbeque and wine.

I’m a smart guy. Despite spending centuries without entering God’s buildings, I’ve already teamed up with some churches and mosques that will drum and trumpet my name Hon. Fisadi Mbangaizaji PhD Phil, MA in lies and hypothetical thinking, BSc. Umbea, Dip in Corruption and mafia, Dip. (Mass mobilization), MBA (Masters in Money making), etc, MP for Tumboni Ulaji.

See. All my degrees need a genius especially MA in Lies and Hypocritical Thinking. Only a few fellas have acquired it. Those are, Ben Makapu and Joe Makamba. When it comes to Africa we’re a few including Bob Mugabe, Jack Zuma, Yoweri M7, and Moi Kibaki.

You know what? My strategies are bigger than a mountain. My slogan is new zeal, new love (Zero) and new big things. Surely, sippers will believe in my make-believe stuffs by voting for me for their peril.

To begin with, I’ll start sharing kanywaji with them. I’ll great them by mentioning their names as I embrace each of them to prove I love them.

I’ll also make sure my VX becomes sipper’s town bus. It’ll take them wherever they like.

My memsahib will form an NGO for the defence of their wives. She’ll fight to see to it that men do home chores such as floor mopping, nail doing and washing babies without forgetting to wear skirts.

So too, I’ll form Mbangaizaji Anthropological Society of Thoughts (MAST) to defend all creatures including sharks and whales without forgetting albinos and elderly.

I’ll raise money for supporting students and patients in the constituency. Hither, I’ll buy 500 mosquito nets and 200 desks to support uswekeni primary school and dispensary.

What’s more, I’ll buy some balls and uniforms of which I’ll wear one as I play soccer with the youths I used to fear like HIV.

During this match, my ten thousand buck Rolex will be left home to avoid being snatched by these man-made petty robbers.

I’ve already fixed the tribal elders. I’ll bribe their head. Wonder not when you see me in traditional regalia signifying being an elder of the tribe and a District Youth Commander of the party.

My mistress Hawara d/o Nyumbandogo with who I’ve a boy will be bribed so that she keeps mum. That bastard I disowned will secretly become my darling baby.

To nicely corner her, I’ll find an international school for her son. This will convince her that I’m preparing him for becoming a leader in future. I’ll promise her to send her son to London for advanced studies. Stupid farmers will be promised good price for their produce. I’ll loan a page from Mizengwe Pindu.

Like him, I’ll promise a tractor and hallow for every village. So too, I’ll promise clean and safe water. Hither is where my Dubai Arab comes in. To make off with their votes, I’ll invite students from Water Resource College to survey the whole projects.

Another strategy is defending the chair of our party for whatever nonsense he commits. To convince him, I’ve already threatened to sue whoever opposes him. In so doing, I tremble like a Maasai morani when offended. I swear by all gods real and fake.

Though many will think this is daydreaming, I’ll make it to the Bunge. Firstly, I’m beautiful like Njaa Kaya. And I’m just a boy of 65 years old who smiles even at funeral.

So too, I’m God-chosen. Thirdly I command sweet language on top of being a good perfomer. Fifth, I’m the man of the people. Don’t ask if there’s a man of hyenas.

Sixth, I’ve brought peace in people’s pockets in the constituency.

For more strategies, let’s meet next time.

So long from Uswekeni.

Saturday 4 July 2009

Charade Bailout Tanzania Style!


When the US government discovered big holes in its ailing economy (thanks to underworld business by greedy corporates) it invented bailout. Economists still fiercely differ on this. On the one hand there are those that take it as a smart move aimed at keeping the people in the main street afloat. On the other hand there are those that look at bailout as sinking tax payer’s money to the hole. When one looks at the reasons they offer, they all seem to be right.

But again, logically, one thing makes sense. First of all, the US and other affluent countries have enough financial muscles to take on this. Secondly, the manner in which the bailout is conducted in some areas convinces: there can be romp in soon thanks to the signs the US economy is currently showing. Thirdly US caused this calamity to the rest of the world. Thus it deserves to do something about it even at the world level. Fourthly, greed and selfishness being the engines of capitalism as well as the bombs (as of now), there was no way the US would sit idly by and evidence its children dying of the disease it cultivated. It had to reap the benefits of its system as well as stand by when things go wrong.

So the first thing to do was to take on greedy CEOs who offered credit generously knowingly this irresponsibility would backfire. Their gargantuan emoluments like golden parachutes, salaries and the likes were practically abolished or slashed. To make sure that these crooks do nary get away with it, the government purchases some shares in affected firms so as to ultimately-for some-own them.

Currently AIG and General Motors or Government Motors as it is joked, are under government watch as it becomes the holder of majority shareholder of the restructured company, with 60% of the stock. To make sure the crime is not repeated, White House receives briefings on economy almost everyday among which is the state of the bill of health of bailed out firms. This way, the government is doing business to see to it that taxpayer’s money is not swindled.

Recently, Tanzania ’s government blatantly proposed bailout measures to her all-time-sick economy. This move sounds smart. Nonetheless, it’s already been seen as charade aimed at stealing taxpayer’s money. With rampancy of stinking corruption in the upper echelons of power, one can comfortably predict its end- it’ll end up a cropper as it morosely digs more menacing holes on the already moth-holed economy.

One thing to remember, this is the same government that stupidly nationalized almost everything especially profit-making gung-hos Nyerere found after felling them and proving to be shoddy as far as business is concerned. Sadly by relegating back to business, this means: privatization is a hoax or much bigger mess should be xpected.

Let me prove my point. Tanzania secured a loan of over 1/-tn to bail out her economy. Amazingly, this amount is a debt whose interest rate is 11%. The good government in Dar es Salaam is planning to loan the same to some unspecified companies at the interest of 2%! Reasoning and reality have been given a heave-ho of a sort! Who will pay generously forgiven 9%? Monkey business of course!

If this megalomania is not stopped, Tanzania's economy will be ruined even more under the pretext of bailing it out. How should it stop crumbling if loans are sought to be abused as the case in point? Renowned economist Professor Ibrahim Lipumba and opposition MPs queried this and termed it as flapdoodle that needs a courage and heart of the mad to commit. He said, “I am getting some feelings that this plan is going to be like a crash programme. Normally crash programmes are implemented without adequate preparations.” Lipumba added, “I listened to President Kikwete’s address …. and also read the speech budget. I could not find anywhere where an ordinary farmer is mentioned as far as the stimulus package is concerned.”

Despite warnings from experts, as usual, like a wise monkey that sees, hears and does nothing, Dar is still hell bent to go on with this buffoonery! Before thinking about bailout, it would have been wise to tackle the root cause-graft and lack of fiscal discipline and vision. The same government that’s chest beating is sitting on mega million scandals! Without combating graft, poor and begging countries will be attempting suttee in the name of bailout. For, in the end, the money aimed at bailing economy out will bail out thieves and crooks in power.

For long, Africa ’s economies were marginalized from the rest of the world so as to be nicely exploited. The prices of our produce have been low and there have nary been equal terms in the so-called international trade since in flag independence. Our countries are run by straight-jacket policies tailored abroad and supervised by puppets not to mention strings attached to the prescription vending international agencies such as World Bank and IMF.

What’s more, African economies still largely depend on those of rich countries on top of our governments’ lack of vision and mission. Though this dependence is superficial, it affects them verily. Africa still spends much needed money on unnecessary military undertakings. If African rulers that make us believe: they mean to save our economies were sincere, the first right thing to do would have been to dwindle the size of their armies and governments.

Another sensible thing to do would be embarking on narrow-and-straight fiscal policies. Instead of depending on and loaning from WB and IMF, African experts in this area should be consulted and their expertise be heed and exploited. Will the West allow this? To avoid going on being caught in their nests, Africa needs to embark on home made policies based on African culture, values and aspirations-self respect and abhorring dependence.

What does this mean? Africa is an unregulated free market for the world. Many substandard goods enter Africa everyday. Many unnecessary items such as expensive oil guzzlers are preferred by African crooks in power. Africa’s agricultural sector is forgotten. Efforts are directed towards vending and trading left resources at throw-away prices that makes sense only to ten-percent-charging thieves in power. This forces Africa to import.

In other countries, IMF-WB’s policies have ruined the countries so as to depend on donors even on food. Without feeding oneself, one can not forge ahead. To do away from current economic crises and poverty Africa needs to think about feeding herself as the step towards fully emancipation. Without doing this, all is good for nothing. In such a debacle can we make it without planning and manning ourselves really? The recipe number one to thwart this is tackling graft at all levels and by all means.

Moreover, our good-at-aping rulers tell us: bailout is an in-thing for the rejuvenation of the economy, thanks to American invention. America did not award money to greedy CEOs or dish out money to the loss making companies. Instead it bought stakes in these companies and put them under government watch to see to it that taxpayer’s money is returned. Indeed, wherever there is a clean and sensible government, this is the surest way of combating embezzlement and corruption even aiding economy to recover.

In a nutshell, bailout African style will ruin our ICU-based economies. We need good governance and empowerment of our people in place and responsible governments accountable to their people. Economic crimes especially involving embezzlement of public money should be categorized as crimes against humanity. Otherwise, this charade we saw aimed at economic bailout is yet havoc to the continent.
Source: The African Magazine July 1, 2009.

Pinda, unataka kumdanganya nani?


Nafahamu waziri mkuu Mizengo Pinda ni mwanasheria. Matamshi yake hivi karibuni kwa bunge kuwa atachukua mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira toka mikononi mwa rais mstaafu Benjamin Mkapa, familia yake na marafiki zake yana utata kisheria.

Yanaonekana kuwa ya kisiasa zaidi ya kisheria. Alikaririwa akisema, "Mimi nilichoamua... kama issue ya Kiwira ndio kitu kikubwa, nitahakikisha zile hisa zote zinarudi serikalini, zote,"

Aliendelea, "Nitachukua zote nitazirudisha serikalini tuanze upya ili tuone kuwa hiki tulichoanza nacho, pengine kitatupa tija tunayohitaji." Je hapa Pinda anaamua kama Pinda haoni kama anatoa mwanya kwa akina Mkapa kumshitaki na hatimaye kurejeshwa mgodi na kudai fidia? Anashindwa nini kusema serikali imeamua kama kweli ana nia nzuri ya kuurejesha mgodi huu? Je hajui kama ataamua kama waziri mkuu, kuna bosi wake juu yake ambaye alishasema hana mpango wa kumchunguza Mkapa?

Je kitendo cha Pinda kutaka jinai hii iishe kishikaji si njia ya kuwanusuru wengine wasio na kinga kama Mkapa? Je huu haujawa usanii na kutuhadaa na kutugeuza majuha? Kwanini uzuie bunge kujadili suala hili halafu mtu mmoja asiye na mamlaka yoyote kikatiba ajitwishe kadhia hii kama hakuna namna?

Kinachofanya nitilie shaka mikakati ya Pinda ni kauli zake. Hebu tazama nukuu hii. "Tunapomtaja Mkapa kuwa ni fisadi, tujiulize ufisadi wake upo wapi? Ameweka mabilioni ya fedha nje ya nchi… Naamini mtu huyu ni safi na namfahamu kuwa ni mcha Mungu,"

Ufisadi tafsiri yake si kuweka pesa nyingi nje ya nchi. Ufisadi ni ile hali ya mtu kutumia nafasi yake, ushawishi au vyovyote iwavyo kuuibia umma kama alivyofanya Mkap ana wenzake.

Eti Pinda hajui ufisadi wa Mkapa? Ajabu! Yaani anaona rais kutumia madaraka yake kutwaa mali ya umma ndiyo huo ucha Mungu anaotwambia Pinda? Huwezi kumuita Yuda Iskalioti mcha Mungu kwa kumsaliti Bwana. Kama Mkapa ni mcha Mungu ni kwa Pinda si kwa watanzania ambao hadi sasa wanaishi maisha magumu kutokana na ufisadi wake. Rejea kuiba nyumba za umma na kuzigawa miongoni mwake na mwaziri wake akiwamo Pinda na bosi wake. Reja kuingia mikataba ya kijambazi ya uwekezaji kama ule wa kuleta Net Solution Group kulikofanywa na shemeji zake. Rejea kuiua na kuiuza iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC). Rejea kulihujumu shirika la umeme Tanesco kwa kuingia mikataba kama IPTL. Rejea kuruhusu familia yake hasa mkewe kutumia NGO kujineemesha kwa mgongo wa ofisi ya rais bila kusahau kupata mikopo nafuu na kujitwalia mali za umma kama Kiwira.

Pinda anajikaanga mwenyewe kwa kutoa madai yaliyopinda. Anakiri kuwa Mkapa alishiriki ujambazi wa Kiwira lakini bado anamuita mcha Mungu! Inaelekea ndugu yetu hajui maana ya neno mcha Mungu.

Alikaririwa akikiri. "Tuangalie, inawezekana aliburuzwa kutokana na matatizo ya wakati ule," Kwanini mtu mwenye akili timamu na kila nyenzo ya usalama aburuzwe kama kweli hakuwa na nia ya kujineemesha kwa kutumia madaraka? Mbona Mkapa alishauriwa akawachukia waliofanya hivyo hadi kufikia hata kuwafutia uraia baadhi yao ? Huyu si mtu wa kuburuzwa bali kuburuza kama anavyotaka kutuburuza mtetezi wake Pinda.

Kuna haja ya kustukia na kupinga mbinu za Pinda, Mkapa na wenzake. Inadaiwa kuwa mgodi wa Kiwira unamilikiwa na Nick Mkapa, Foster Mkapa na B. Mahembe ambao wanamiliki kampuni ya Fosnlid wakati kampuni ya Devconsult LTD wamiliki wake ni D.Yona na Danny Yona J.R.

Makampuni mengine ambayo yaliungana na kununua mgodi huo ni Choice Industries, ya Joe Mbuna ambaye ni kivyele cha Mkapa na Goodyeer Francis na kampuni ya Universal Technologies, ambayo inamilikiwa na Willfred Malekia na Evance Mapundi. Wabia hawa ndio waliounda kampuni ya Tanpower Resources Ltd inayomiliki mgodi huo.

Je haoni kwa kunyang’anya mgodi kienyeji ni kuwaepusha wamilki wengine kufikishwa mbele ya sheria na kuwajibika? Je hasara iliyokwisababishwa na kuendelea kumilkiwa kwa mgodi huu kinyume cha sheria anaiweka upande gani? Ni vizuri Pinda akaelezwa ukweli kuwa anachofanya ni usanii na kushirikiana na wahalifu kutaka kuendelea kulihujumu taifa.

Ni vizuri Pinda na wenzake wakajua kuwa watanzania wamekomaa. Hivyo kuwafanyia usanii wa kitoto ni kuwatukana matusi ya nguoni.

Kwanini Pinda asiseme wazi kuwa ametumwa amtetee Mkapa? Ingawa anajitahidi kufanya hivyo hata kwa kuweka kiapo chake rehani, hawezi kumsafisha Mkapa. Kwanini asimwache Mkapa akajitetea hata mawakili wake? Hivi Pinda hajui kuwa analipwa na umma huo huo anaotaka kuudanganya na kuuhujumu na si Mkapa anayemtetea? Kama wanajuana na Mkapa, hili ni suala binafsi. Lisiingizwe kwenye mambo ya taifa. Mkapa si kichanga cha kutetewa na kila anayejihisi kufanya hivyo. Kuendelea kwa watawala walioko madarakani kumtetea Mkapa kunaweza kutoa ishara kuwa ima walishirikiana naye au nao wana mpango wa kufanya kama yeye watakapostaafu kisheria. Namna hii amani uchwara tunayojivunia itatoweka. Maana wananchi wamechoka kugeuzwa nepi na ngazi na kila fisi na fisadi ajae na kujihomolea.

Leo Pinda kaja na Kiwira kwa usanii ule ule. Kesho atakuja na Richmond ambayo nayo inawahusisha wakubwa wenzake bila kusahau Kagoda na EPA ambavyo vimegeuka serikali ndani ya serikali.

Hivyo basi wabunge wana haki ya kujadili jinsi ya kurejesha Kiwira na hatua za kuwachukulia wahusika. Sheria za nchi ziko wazi hasa zile za uhujumu uchumi. Hapa kinachopaswa kuangaliwa sana sana ni kinga uchwara ya rais ambayo matumizi na tafsiri yake inaanza kutumia kifisadi. Pinda, tell it to the birds. Unachofanya ni uhujumu na kulindana.
Chanzo: Tanzania Daima, Julai 1, 2009.

Mene mene Tekel u-Pharsin



JAMANI mnaosoma unabii huu mjue ni wa serikali ya kifisadi ya ndotoni ya Mtukufu Mpayukaji Msemahovyo - chaguo la Mungu. Hivyo msije mkafanya makosa mkanichukia bure, kuwa nimewakwaza mkidhani nisemayo yanaihusu serikali yenu tukufu ya KISHIPA yaani Kikwete, Shein na Pinda.

Leo, nazungumzia tulivyopitisha bajeti ‘ngwengwe’ baada ya kuwatandika bao la kisigino wabunge wa Bunge letu la ndotoni. Wengi wa wanakijiwe walikuwa wamepania kuikwamisha eti kwa sababu ni ya kujipendelea na uchaguzi wa kijiwe mwakani.

Ingawa tunawajua walivyo hovyo, tulizinyaka toka kwa mashushu wetu. Hivyo hatukufanya ajizi. Tulijiandaa kuwatia adabu hasa kwa kuwatisha kuwa kama wasingeipitisha bajeti mishahara yao licha ya kuifyeka, tusingewalipa kwa vile pasingekuwa na pesa ya kufanya hivyo.

Kutokana na ufisi, ufisadi na ubinafsi wa wabunge wetu wa kijiwe, wale viherehere wote waliokuwa wamejiaibisha kwa kuapa wangeikwamisha bajeti mbona walifyata mikia na kufakamia matapishi yao kama mbwa!

Penye udhia penyeza rupia walisema wahenga. Hii ilifanya kazi kweli kweli hasa ikizingatiwa kuwa jamaa zangu wako bungeni kujineemesha kwa kuwaongopea wanuka jasho kuwa wanawawakilisha wasijue wanawakilisha matumbo yao!

Basi, bila ajizi tulimbonyeza spika wa kijiwe, mheshimiwa Six Meno Sam awatishe wabunge. Kwa kuwa letu moja, aliamua kuwasomea katiba viraka ya kijiwe isemayo Mheshimiwa Mpayukaji anaweza kuvunja bunge la ulaji iwapo wabunge wangemkosea adabu kwa kutaka kuingilia ulaji wake.

Kifungo cha 20 (7) (c) cha katiba yetu kinasema wazi kuwa wakati wowote Mpayukaji atavunja Bunge na kuwalamba bakora wabunge hata kuwafunga watakapokataa kutia muhuri makufuru yake.

Mpayukaji ana mamlaka ya kuyatumia vibaya mamlaka (power to abuse power). Yeye ni Mungu hapa duniani awatawalaye walevi na asifanywe kitu. Yeye na nyumba yake na marafiki zake wametukuka na hawakosei hata wakikosea si kosa. Hivyo, wabunge nao kwa kujua uhovyo wao, walifyata mikia na kuanza kuisifia ili wapewa ulaji wao.

Kuonyesha tulivyo wajanja, wapo waliojipendekeza hata kutumia misahafu kutulaani kwa kukwamisha mambo. Ajabu ukiwaona kina Mbwa Mwitu ambaye tunamtania kuwa ni Mzindikakaya, wanaofanya hivyo walivyo na harufu ya ufisadi unakosa maana ya misahafu!

Hata hivyo, tusiwalaumu sana. Ni wangapi wanashika misahafu kuapa kuitumia nchi kwa kuwahadaa waliwa eti wataitumikia nchi? Hamkumsikia yule jamaa aliyepinda kwa mizengwe akisema eti Tunituni Makapi ni mcha Mungu wakati ni kibaka wa kawaida?

Siku hizi viapo havina maana kama zamani. Mtu anaweza kuapa tena mbele za watu akatenda kile alichoapa kutotenda na walevi wakaendelea kumuamini. Hamjamsikia Njaa Kaya anavyowabamiza mkenge kweupe nao wakiendelea kukalia matumaini kama waathirika?

Ni wangapi wanaapa altareni au kwa shehe kuwa watakuwa kitu kimoja katika shida na raha lakini umaskini au mabalaa yanapopiga hodi wanaachana? Ni wangapi wanavunja amri ya sita wakati wameoa au kuolewa? Nenda Idodomya ujionee.

Huu ndiyo ujanja. Unatumia misahafu kuhalalisha dhambi zako kama Belshazzar wa Nabkadnezza. Ingawa maandishi ya Mene mene Tekel u-Pharsin tayari yako ukutani. Sisi hatujali. Walevi wakija kushtuka tutakuwa tunakunja jamvi na kuwaachia mkangafu wao baada ya kurarua kama tumbusi na fisi. Tutakuwa tumeishauozesha kama inzi.

Pia ifahamike. Maandishi haya yanatulenga sote. Maana siku gharika likija hakuna atakayenusirika. Tutazamishwa wote. Kwani tumeiharibu ardhi takatifu wote. Kila mmoja ukiondoa vichaa watoto na wanyama, ana mchango katika kufuru hii.

Kaya ya walevi kwa vituko hakuna mfano duniani mna habari? Kuna watu wa majoho eti walitaka tulaaniwe kwa kuingilia ulaji wao! Mbona wao wanakula sadaka ya Bwana na hakuna anayewalaani?

Eti wengine wanasema waziri wa fedha na kuchuma aachie ngazi kwa sababu waligundua alilambishwa akasamehe kodi kwa baadhi ya sekta. Hivi wanataka ale polisi siyo? Katika nchi ya walevi kujiuzulu ni dhambi isiyosameheka na kuwajibishana ni matusi ya nguoni.

Kwanza nani amuwajibishe mwenzake iwapo wote tunanuka? Nani huyu awe wa kwanza kutupa jiwe iwapo kila mtu ana ka-ulaji wake na ka-serikali kake kama Kagoda na Richmonduli katika nchi ya Ahaha?

Tatizo ni kwamba walevi wengi hawajui serikali inavyofanya kazi. Wanashikilia kuwa tuliwaahidi kwenda Kanani. Ebo! Kanani nyinyi ni Wayahudi? Hatuwezi kufanya kosa hili. Maana tukiwapeleka kule mtaichafua nchi takatifu kiasi cha kulaanika kama nyinyi.

Hivi kuna nchi takatifu kama yenu iliyozungukwa maziwa, mito , vilima huku ikiwa imejaa vito kuliko yoyote? Hapa tuambizane ukweli. Haikulaaniwa ardhi yenu bali nyinyi na nafsi zenu.

Mlilaanika pale mlipoanza kutumia matumbo na makalio kufikiri badala ya ubongo. Mlilaanika mlipoanza kujifikiria badala ya jamii. Mlilaanika na mtalaanika kwa kuwa woga na wanafiki tena kwa nafsi na maisha yenu.

Mnataka muambiwe mara ngapi? Mbona maandishi ya Mene mene yako ukutani miaka kibao. Mnayasoma na kuyaacha pale pale? Hii inakumbusha kisa cha mbuzi. Akivamia shamba kula mahindi akirushiwa jiwe anadhani msamalia mwema kamrushia mahindi zaidi!

Hadi yamkute ndipo anatia akilini. ‘Too late’. Jilaumuni badala ya kutulaumu sisi. Yamekaa ukutani hadi yanaanza kuliwa na mchwa! Ajabu kila fala anajifanya mjuaji na kila mjuaji anageuzwa fala na bado watu wanadai mambo yako sawa!

Bwana wee, ngoja nitimke kwenda kufaidi chai na mahanjumati ya bilioni 19 za brother Mstaafu Mkulu.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 1, 2009.