The Chant of Savant

Tuesday 4 February 2014

Kweli Jogoo alifundisha vifaranga “kupuu” ndani!

Baada ya kichwa ngumu mkulu mwenyewe kuwashiti akinakiherehere Andalaman Kinamna na Mape Mapepe Ninaye waliowaita wateule wake mizigo, ametoa mpya.  Si amerejesha mizigo na migushi hasa pale alipowapandisha ulaji walaji ambao CVs zao zinaonyesha walivyo vihiyo walioghushi. Hapa ni kama vile matapeli wawili wametosana. Kwanini kuwatumia walevi kupata sifa? Nadhani hawa nao, kama vibinti vya shule za msingi vinavyopachikwa mimba, wameponzwa na kiherehere chao. Hakika kilichotokea ni sawa na kuruka mkojo na kukalia na si kukanyaga manonihino. Ama kweli jogoo aliwafundisha vifaranga kunya ndani! Sijui inaleta picha gani inapotokea yule mliyedhani atalinda maslahi yenu anapokuwa mstari wa mbele, kwa mfano, kuwakingia kifua majambazi, vibaka na waharifu kila aina? Msitu ule ule na nyani wale wale. Kinachogomba ni wale wanaofanya makosa ya kuwaamini wakidhani wana jipya wakati waliishiwa miaka mingi iliyopita tangu aondoke mzee Nchonga.
Kutokana na mlevi kusoma sana somo la Research Methods, aliamua kufanya kile ambacho akina Edward Snowden na Julian Assange huita udukuzi. I decided to bug some new appointed ministers particuluraly Saidia Mkuya Salimu na Naibu wake aitwaye Adam Kigoma Milima. Lolololooooo! Niliyogundua ni makubwa God knows. Bahati nzuri wakati nikifanya ugunduzi na udukuzi huu sikuwa nimevuta wala kupata kanywaji. Nilikuwa mzima na timamu kiakili hata kimwili na kiroho. Ndiyo nilikuwa natoka gymn kutunisha misuli baada ya kutoka kwenye tambiko ambako nako nilikwenda baada ya kuandika article moja kwa ajili ya jarida moja la walevi la ulimwengu kuhusu jinsi wakubwa wanavyoweza kubebana na kufichiana uoza wao.
Kwa vile nilikuwa naandika kuhusu uoza wa wakubwa uchwara, niliamua kutembelea wavuti wa mjengo wa Jamhuri ya Mgongano wa Danganyika na kupata haya madudu. Leo nitacheza na Mkuiya na Milima. Hata hivyo, ifahamike. Wawili hawa ni kile ambacho wakameruni huita typical replica ya kile kinachoendelea kwenye kaya ya Danganyika.  Hakuna kitu kimebarikiwa na kuhalalishwa kama kughushi kwenye kaya hii. Warning, kughushi ni halali kwa vigogo si kwa fito na wachovu. Ukiwa ni kigogo na mzito unaweza kughushi utakavyo hata vitegemezi vyako. Hii ndiyo maana kuna uwezekano wa Milima kughushi na hakuna anayemgusa kwa vile dingi wake alikuwa kizito wa wizara ya njuluku.  Kuna ubaya gani akirithishwa wizara ya baba yake? Laiti wizara hiyo ingebadilishwa jina ikaitwa wizara ya Milima ya Fwedha. Maana kuna kakurithishana fulani. Usishangae dokta Hossein Muinyi siku moja akataka arithishwe ikuu ya dingi wake. Bado mlevi anafanya kazi ya ziada kujua huyu Mkuiya anabebwa na kupaishwa kwenye ulaji kwa sababu ya nini. Hajajua kama ni kitegemezi au kishikaji au kilaji cha kigogo fulani.
Mambo ya vigogo na vishikaji na vilaji na vitegemezi vyao tuyaache. Tuangalie kinachotarajiwa kufuata. Kwa kitaalamu nasema what I am going to do is predict what forgerers and the agents of ruining outfit will do in the ministry of dosh and njuluku.
 Tumeishaonyesha kuwa mkuu wa wizara na naibu wake wa njuluku ni vihiyo. Hivyo, huyu naibu wa sera za ukwapuaji aitwaye Mwehujuu Lameeeki Michemba atakachofanya ni kutumia hawa vihiyo kuchomoa njuluku kwa ajili ya uchakachuaji ujao. Nadhani yote hii itafanyika ili kupatikana kiraka kingine kitakachofunika madhambi ya majamba wazi makubwa yatakayoondoka. Mara hii mmesahau jambazi wa Kiwila na nkewe, vivyele na mashoga zake bila kusahau bi mkubwa Annae Tamaa Makapi wa Makapu? Unadhani waasisi na wanufaika wa HEPA wataepa vipi lupango kama siyo kuwawezesha majambawazi wengine ili wawalinde kama walivyomlinda Tunituni Ben Denjaman Makapu? Are you thither guys? Mnaliwa mnajiona msipoamka. Mliwe hadi wapi na lini ndipo msituke Yarabini?
Hebu twende kwenye mada ya mizigo na migushi. Mizigo ishatua kwenye ulaji na hakuna anayeigusa. Hata wale akina Mapepe walioifichua sasa wanaitetea wakijifanya hawakueleweka kama wakati ule waliposhupalia magamba wakaishia kugeuka magamba wenyewe kama ambavyo wamegeuka mizigo huku mizigo yenyewe ikipeta na kutesa. Hamkumsikia Silvia Rweyependekezamu akisema kuwa tuache kupiga kelele kwa vile bosi wake ameishatimiza wajibu wake wa kutubebesha mizigo? Hamkumsikia akiongea kama vile hana akili nzuri. Ungemwangalia usoni huyu Rweye……mu alivyokuwa akitoa jasho na povu, unagundua kuwa naye haamini alichokuwa akisema. Sema njaa ndiyo ilikuwa ikimsukuma atetee upuuzi na mizigo. Huyo tushamzoea aliyesaliti taaluma yake akageuka nepi ya jamaa.
Niliposoma CVs za hawa vilaza sorry waishiwa sorry wahishimiwa niligundua kitu kimoja. Mkuiya anasema ana masters mbili lakini hana bachela wala haelezei alipozipata hizi mastaz! Ni Bongolalaland pekee ambapo mtu anaweza kunyaka masters wakati hata hiyo bachela hana. Nani angeamini kuwa Milima aliweza kutoka darasa la 12, tena failure, akaweza kufanya masters? Tembelea wavuti wa mjengoni uone utapeli na upuuzi vya kitoto hadi ulewe bila kunywa wala kuvuta. Nimeyaona mengi huko.  Kuna watu wamepewa ulaji wakati hawana chochote zaidi ya kujishebedua kwa wakubwa wenye uchu wa nyuchi na mambo mengine kama hayo.
CV nyingine iliyoniacha hoi ni ya huyu mwingine ambaye nilim-bug, yaani mgosi toka Zenj daktari Hossein Muinyi anayedai ana PhD ya madawa na kukuta kumbe ni mtupu. Maana kwenye maandiko ya kisomi wala hana hata moja zaidi yay ale yanayomnukuu akiwa waziri wa afya. Mpaka leo sijaamini kama kweli mtu mwenye PhD ya kweli asiwe na andiko hata moja la kisomi. Huyu jamaa si ndiye alisababisha milipuko kule Mgongo wa Mboto? Sasa anarejeshwa kwenye ujeshi ili kuua wengine zaidi siyo?  Utapeli mwingine wa kitoto God knows.
Funga kazi ni kuteuliwa kwa kasuku mmoja toka Dodoma aitwaye Ju-ma Mkamiawaandishi na mtuhumiwa wa rushwa toka serikali za mitaa aitwaye Erasto Dhambi. Huyu ana madhambi God knows. Mwenzie waliyekuwa wakiomba rushwa pamoja anasota akingojea hukumu wakati yeye akipewa ulaji! Ama kweli jogoo aliwafunza vifaranga kupuuu ndani!
Chanzo: Nipashe Jumamosi fEB. 1, 2014.

No comments: