The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Thursday, 10 April 2025

‘Niite’ Fyatu Mfyatuzi Nchonga Kambarange Nyerere

 


Juzi nilimsikia tapeli na zwazwa mmoja akijita kitegemezi cha mzee Nchonga (RIP). Ajabu, nasi mafyatu wake tuliufyata tukafyatuliwa utadhani huu si utapeli. Haraka haraka, niliwasiliana na Madaraka mwana mwenyewe wa Nchonga aliyewahi kunikaribisha Mwisenge nikahiji kwenye kaburi la baba wa kaya na kuniahidi kirungu. Ilikuwa ni baada ya kung’aka baada ya tapeli mmoja wa kisiasa aitwaye Washiti kupewa. Kwa busara na unyenyekevu, alinijibu “mwalimu alikuwa baba wa wote.” Kiakili, kifyatu, na kibusara, alinikata kilimilimi nikakubali yaishe. Pamoja na kuwa kitegemezi original wa baba wa taifa, Madaraka, huwa hapendi kujiita au kuitwa Nyerere zaidi ya Madaraka.
            Kwa kuangalia uhalisia na busara za Madaraka, inakuwaje matapeli wa kawaida tena wachovu na wachafu kujivisha ubini wa Nyerere nasi tunaangalia kana kwamba ni jambo dogo na la kawaida. Japo Nchonga ni dingi wa wote, hakuwa muasharati wa kuzaa nje ya ndoa yake. Hivyo, hata kama unampenda na kumheshimu kiasi gani, hupaswi wala huna haki ya kubeba ubini wake. Isipokuwa uwe fyatu kama mimi.
        Kwanza, kama wote tutabeba ubini wake, wabaya wake watasema tunamwabudia kutokana na kutupumbaza kiakili.
        Pili, tutakuwa tunawanyang’anya au kuwanyima vitegemezi vyake wa damu utambuliko na haki zao vya msingi.
        Tatu, watatokea matapeli hata maadui kutaka kumtumia ili wafanya upumbavu wao.
        Nne, tujikumbushe. Dingi wa kaya hakupenda kusifiwa wala kuabudiwa. Kwa wanaokumbuka, alivyowahi kusema kuwa, kidini, yeye aliuwa mwanaharamu kwa vile alikuwa mtoto wa mke wa tano.
 Hata huu utakatifu anaokaribia kupewa, kama angekuwa hai, ima angehoji hata kuukataa kwa heshima kuonyesha ubinadamu na unyenyekevu wake.
 Hivyo, badala ya kubariki iwe kwa kutojua au bahati mbaya utapeli na dharau kwa dingi wa kaya, tusimame imara si kukemea, bali hata kukomesha mara moja. Tusikubali kutumiwa kwa kuwaita matapeli waliojipachika ubini wa Nyerere kwa kuwaita hivyo. Bila kujua, tutakuwa tunaingizwa mkenge na katika kumtukana na kumdhalilisha dingi wa kaya. Vitegemezi vya dingi wa taifa vinajulikana viwe hai au kutangulia mbele ya haki.
            Tano, hakuna mfano wowote wa mafyatu wa kuvaa ubini wa kiongozi wao. Hata wakristo, walipewa ukristo na siyo ubini wa Yesu kwa vile hakuwa na watoto. Walivaa ukristo kama upakwa mafuta. Kuna kipindi maadui wa uislam toka ulaya walianza kuwaita waislam Mohammedans. Waislamu walichachamaa kwa sababu, a) huwa hawamwabudii Mtume Muhammad bali kumheshimu. Pili, wao si watoto wa Muhammad kwa vile Muhammad mwenyewe, kabla ya kufariki, aliwahi kuwaambia wazi kuwa yeye si baba wa yeyote bali baba wa watoto wake.
            Mbali na kuwa uzwazwa na utapeli, kujipachia ubini wa dingi wa kaya, ni ushahidi kuwa wanaofanya hivyo wameishiwa ubunifu. Wanaonyesha, kukopa maneno ya mwanafunzi wa Mwalimu, Benjamin Mkapa, kuwa ni wavivu wa kufikiri. Wanaonyesha wanavyotumia utumbo kufikiri badala ya ubongo. Niliwahi kuandika makala kuwakata watanzania kumuita rais Samia Suluhu Hassan hasa wale ambao wamemzidi umri waliomwitua maza. Hii ni kutokana na ukweli kuwa wanafanya hivyo kumdanganya, kumtukuza, na kutaka kumtumia mbali na kumzeesha. Kila mtu ana dingi na maza yake. Samia ana watoto wake na––––kama ilivyo kwa dingi wa kaya–––hana historia ya kuzaa kabla ya kuolewa au nje ya ndoa.
            Ukiachiwa kuishiwa na kukosa ubunifu mbali na utapeli, wengi wanaojifanya kubeba ubini wa dingi wa kaya, kwanza, hawana hata dalili moja ya kufanana nae mbali na kuigiza sauti yake au kujichora kama yeye. Kiusanii, tunawaruhusu wafanye hivyo. Kiuhalisia, hapana. Haiwezekani, ukamnasifibisha simba na panya. Pia, si vizuri walevi na vichaa kufagilia makaburi ya watakatifu. Ni ujinga wa pamoja, kuwaruhusu wazinzi kufanyia uchafu wao juu ya makaburi au majina ya mafyatu wetu maarufu waliopigania uhuru wetu.
        Juzi, niliona klipu ya mmoja anayejifanya kitegemezi cha dingi wa kaya akishindwa kusoma hata hotuba ya kimombo aliyoandikiwa. Nyerere alikimanya kimombo. Sasa inakuwaje anayemuingiza ni mbumbumbu na kihiyo? Ukimuigiza mtu, lazima ujitahidi ufanane naye ili kuleta maana na kuwasilisha ujumbe juu yake mbali na kuamsha kumbukumbu juu yake. Haiwezekani nune akamuigiza simba. Nune ni mdudu na simba ni mfalme na malkia wa pori. Kupe hata kwa usanii na utani, hawezi kubeba ubini wa tembo wala ng’ombe. Wawili hawa ni tofauti kabisa.
            Nimalizie kwa kuwaasa mafyatu tusikubali uchokozi wa matapeli, vilaza, na vihiyo wanatafuta riziki hata kwa njia chafu kuwachafua mashujaa wetu walioleta uhuru huu tunaofaidi na kuringia. Wote wanaojiita watoto wa Mwalimu Julius Nyerere wakome na kuacha ili kuwaachia watoto na família yao wafaidi haki na utambuliko wao. Japo hili linaweza kuonekana ni jambo dogo, madhara yake ni makubwa. Hivi nimesema naitwa Fyatu Kambaage au Nyerere?
Chanzo: Mwananchi Jana.

Monday, 7 April 2025

Umuhimi wa Wanandoa Kutunza Siri

Kuna busara wakati wa kuwafunda wanawali katika jamii moja nchini Uganda isemayo kuwa wanapoolewa lazima wajifunze kufunga miguu na kufungua macho badala ya kufungua miguu na kufunga macho. Hii hufanyika wakati mwali akijiandaa kwenda kwa mumewe. Wazazi hufanya hivyo kwa kujua kuwa nyumbani kwa mwali huacha kuwa kwao na huko aendako ndiko hugeuka kwake. Hamjasikia kwa Waswahili wakimwimbia bi harusi kuwa ‘sasa wenda kwako, utarudi huku kutembea?’

 Busara hii, licha ya kuzuia vishawishi vya  uasherati, inalenga kuwaambia wanandoa kuwa makini na waliowazunguka kuhusiana na maisha na ndoa zao. Inawahimiza kuchambua mambo na kujua ya kusema na ya kutosema. Siyo kila jambo lazima lisemwe au kuwekwa wazi kwa wasiohusika. Tumeshagusia kwenye kitabu cha kwanza namna mashoga wanavyoweza kuvunja ndoa. Pia, tuligusia juu ya imani au ushauri visivyofanyiwa utafiti vinaweza kuvunja ndoa. Ndoa nyingi zimevunjika na nyingine zitavunjika kwa sababu hizo. Hivyo, kama njia ya kuwafunda vijana, tumeamua kuchagua kisa hiki kufikisha ujumbe na ujuzi kadhalika.

            Kuna kisa cha mama tulichosoma kwenye gazeti moja la nchini Zimbabwe. Kisa hiki ni juu ya mwanandoa mwenye majivuno na asiyetunza siri za ndoa yake. Akiwa amekwenda kusuka nywele kwenye saluni, alizoea kumlaumu mumewe kwa wenzake kuwa alikuwa akimwachia pesa kidogo. Maskini, kayaya huyu hakujua kuwa alichoona kidogo, kilikuwa kikubwa kwa wenzake. Hivyo, baada ya kuwa akijisifu kwa kumsimanga mumewe kwa ‘kutomwachia’ pesa nyingi, walitokea waliotamani wangeolewa naye wakaanza kumuandama hadi ndoa ikavunjika na  mhusika akashangaa kujikuta aliyechukua nafasi yake alikuwa ni  mmojawapo wa mashoga yake aliyezoea kumlalamikia juu ya tabia za mumewe. Kimsingi, huyu mama hakufunga miguu na kufungua macho. Alipaswa afunge mdomo na kufungua masikio. Je ni wangapi wameishashuhudia au kukutwa na haya? Je hapa utamlaumu nani kama siyo wewe mwenyewe? Huwa tunawashauri na kuwahimiza wanandoa kutofanya maisha yao au ndoa zao magazeti au matangazo.

            Je ni wangapi hufunga miguu na kufungua macho au kufanya kinyume? Je hili halina faida kubwa kwao kama watalishika, kulikumbuka na kulitekeleza?   Unaweza kujisikia raha kuwasimulia wenzako juu ya maisha yako bila kujua madhara yake. Hata hivyom si wasikilizaji wako wote hujisikia kama unavyojisikia. Hivyo, si vibaya kushauri na kusisitiza kwa wanandoa kuchambua na kujua ya kusema na kutosema. Tunajua kuwa si wote wanapata bahati au kuwa na desturi, mila, na tamaduni za kufanya hivi hasa wakati huu wa utandawazi ambapo vijana wanaweza kukulia mbali na jamii zao hadi kuoa au kuolewa. Hivyo, kwa kuliibua na kulikumbushia hili, tunalenga kuwasaidia wasio na fursa au walio nayo lakini wasizingatie.    

            Wewe na mwenzi wako ni sawa na kata na mtungi. Siri ya mtungi apaswaye kuijua ni kata tu. Hivyo, unapofungua mdomo ukaziba masikio, utaumia tu taka usitake. Kama hujaumia, ni suala la muda na si kama bali lini utaumia. Pia, ni vizuri kubainisha kuwa unapaswa kujua mambo ambayo ni siri na siyo siri. Kama hujui, acha kuongea kabisa ili usijikute ukivujisha siri ukidhani siyo siri wakati ni siri. Kwani usiposimulia juu ya maisha yako utakosa nini ikilinganishwa na kuyasimulia ukaishia kujuta? Hata habari huwa hatuzipati bure. Ima utanunua chombo cha habari kama gazeti, runinga, au redio ndio uzipate au ulipie kwa wanaozitoa. Mbali na majanga na misiba, hakuna habari za bure duniani hasa wakati huu ambapo kila kitu ni bidhaa inayoweza kutumiwa na baadhi ya watu kutengeneza faida hata kama ni kwa hasara ya au kuwaumiza wengine.

            Turejee tulikoanzia. Mbali na kushauriwa ufunge miguu na kufungua masikio, tuseme wazi. Je unakosa nini usipofichua siri zako? Je unapata nini unapozisambaza? Kwani, lazima kila unachofanya wakijue watu wakati hujui wafanyayo? Hata ukiyajua wafanyayo, kwani lazima uyafahamu kwa kuhatarisha maisha, ndoa, na siri zako? Hivyo, usikubali kuwa habari kwani si kila habari ni nzuri. Waandishi wa habari husema heri upate habari kuliko wewe kugeuka habari.

Chanzo: Mwananchi J'pili.


Saturday, 5 April 2025

Wamefyatuka wanafyatuana mbele ya mafyatu!


Juzi tilishangaa sana. Mwe! Nani angeamini kuwa mafyatu wanene na wanono wangefyatukiana na kufyatuana hadharani? Unene kweli taabu japo una raha ya kula bila kutoa jasho! Si fyatu mmoja aliyekaribu na mwenyewe kapwakia ulaji kiasi cha kuanza kuwapayukia walaji wa chini yake wasio na nasaba na mwenyewe! Fyatu huyu mwenye kutia shaka, inaonekana, hagusiki. Nani anaweza kumgusa Keinerugaby Mwana wa Mu7 pale jirani? Nasikia shemela zake nao wanafyatua ulaji simply because wanashea bedrooms na vitegemezi vya Mu7. Haka kaugonjwa kanaanza kuenea. Ukiachia mbali Mu7, Jake Zoomer wa Bondeni aliwahi kuruhusu kitegemezi chake kiitwacho Insectzane kutumia maulaji yake utadhani ufalme. Pale kwa Nyayo ya zamani, Billy Rootor na vitegemezi vyake ndo usiseme. Vinafyatua kama havina akili nzuri. Hali ilikuwa chafu hadi ikawapo ofisi ya first daughter. Mafyatu wa k ule walishupaa ikafyatuliwa mbali.
                Nchini Equatorial Guinea, kitegemezi cha mdingi ndiye makamu wa dingi yake. Wakati kaya ya jirani karibu na Diarasee, kitegemezi cha mdingi kinafyatua njuluku kama za dingi wake. Kule Gabon, kitegemezi cha king’ang’anizi aliyefyatua na kuibia kaya ile kwa zaidi ya miaka 40 kilifyatua maulaji baada ya dingi kufyatuliwa na Sir God mwenyewe. Hata hivyo, nacho kilifyatuliwa na geshi kikaishia kuuona unene runingani. Kule Tchad na Togo, bado vitegemezi vinatesa baada ya midingi yao kufyatuka na kurejesha namba.

Nirejee kayani. Japo si kwa sana ikizingatiwa kuwa Stone hakuendekeza ujinga huu sawa na Nchonga na Brother Ben Nkapa. Kamchezo ka kupeana ulaji kiukoo kanaanza kugeuka donda ndugu. Ajabu, mafyatu wanachekelea badala ya kufyatuka wakafyatyua hawa wanaowafyatua! Leo sifyatui majina ya mafyatu fyatuzi wanaofyatuana baada ya kuwafyatua mafyatu nikaishia kuchengetwa kama siyo kufyatuliwa au kuzuiwa ili nifyate. Natamani niorodheshe vitegemezi vya wanene vinavyofyatua mafyatu just because of their surnames. Wengine hata hawana surnames nene bali za madingi wa washirika wao wa bedroom kama aliyefyatuka juzi akamfyatukia fyatu mwenzake mbele ya mafyatu jamaa anayesifika kwa kufyatuka na kupayuka bila kichwa kuwasiliana na midomo.

Brother Al Chakumila upo hapo? Nilijisikia vibaya dogo fyatu wa mwenyewe alivyokufyatua mbele ya mafyatu asijue anaweza kuwafyatua wakafyatuka na kufyatua. Je kipindi hiki utapona kweli? Ilikuwajekuwaje ukamgusa pabaya fyatu wa mwenyewe? Umesahau ulivyopayuka ukafyatuliwa na kukaa pembeni hadi mwenye alipokuhurumia akakurejeshea ulaji unaoanza kudodesha? Inaonekana ufyatu umeanza kukuzidi hadi unajifyatua na kuishia kufyatuliwa. Kwanini hujifunzi au huna kumbukumbu? Ungejua namba unazocheza nazo, wala usingejifyatua ukaishia kufyatuliwa ukafyata. Umewapayukia wengine usijue duniani malipo ni hapa hapa. Sasa ona umefyatuliwa tena hadharani na unafyata. Ingekuwa mie, kwa ufyatu na ufyatuzi wangu, mbona nshajifyatua na kuachia ngazi zamani gani.

Kuna kamsemo kuwa madaraka hulevya chakari. Yakishakulevya, unapoteza uwezo wa kufikiri, kujifunza, kukumbuka, hata kuona na kukubali ukweli. Sijui kwanini mafyatu hawataki kujifunza toka kwa mafyatu waliotesa kama akina Nebukanezza, Mchonga, Jiwe, na wengine! Kufyatukiana na kufyatuana hadharani si uongozi bora bali bora uongo na uongozi. Inaboa na kukera my friends. Japo mafyatu waligoma kufyatua, angalieni msifyatuane mkaishia kuwafyatua wakawafyatua bila kutarajia.

Japo brother Moody alipomfyatua na kumfyatukia brother Al, alikuwa na pwenti, kwanini wasikutane faragha wakayamaliza au ni yale ya kutafuta ujiko wasijue wanavifua na kufuana nguo hadharani bila sababu za msingi. Huwezi kuruhusu ndinga zipitie kwenye uwanja wa mapipa hata kama una power. Huu siyo uzembe bali ni hatarishi kwa madebe na ndinga mbali na abiria. Inakuwaje kayani kila fyatu anajifanyia atakavyo kana kwamba hakuna sharia na miongozo? Huwa nashangaa kusikia eti mkuru wa uilaya anazuia say mikutano ya hadhara kwa vile wanaoiitisha ni wapingaji. Kwani wapingaji si wanakaya na wapo kinyume cha katiba? Mnamfyatua nani kwa kujifyatulisha? Mkifyatuliwa, mnaanza kulalama kama vichanga wanapofyatuliwa kutokana na ufyatu wao uchwara.

Sasa ufanye nini? Nakupa ushauri wa dezo. Achana na kufyatukafyatuka na kupayukapayuka hovyo. Utafyatuliwa. Shauri yako. Usijesema sikukuonya. Unene wa kupewa si unene kitu. Wapo wanaoulinda wakilala na kuamka wakiota ni jinsi gani waanzishe kwaya za sifa ili ulaji usiwatoke. Wapo ambao wako hata tayari kukufuru ilmradi waendelee na ulaji.

Hakuna fyatu anayenifurahisha hata kama sifurahi kama yule aliyefulia. Jamaa likifungua domo kufyatuka ni makufuru na sifa. Mara mwenyewe katenda miujiza, mara kavunja rekodi, mara hivi, mara vile ilmradi siku ziende na ulaji na ukamuaji viendelee. Kwa tunaojua haya mambo na dynamics zake usawa huu, unatumia busara ya Kijamaika isemayo play fool to catch wise. Ukijitia kujuajua na kufyatukafyatuka ukapayukapayuka, unafyatuliwa na wengine wanatesa. Nakushauri utafute the 48 laws of power upone. Hivi nshaamka usingizini?

Chanzo: Mwananchi J'tano iliyopita.

Wednesday, 26 March 2025

Tusichachawe, kuchawishwa, tukachawishana

 

Kuna usemi wa hovyo. Kila nikiusikia, natamani nifyatuke na kuwafyua wadudu hawa wawe ni wadudu au ngurumbili waliofilisika kimawazo hadi kuwa hivyo walivyo hovyo. Msemo unaonichachefua na kunifyatua si mwingine bali ule wa chawa na uchawa ambapo chawa wenyewe ni mafyatu. Mwanzoni, nilidhani chawa wamepata miujiza kiasi cha kufyatuka kama mafyatu na kugeuka mafyatu lakini si mafyatu kufyatuliwa hadi wakajigeuza au kugeuzwa chawa. 
Kwanza, siamini wala kukubali kuwa fyatu mzima na akili zake anaweza ima kujifanya, kufanywa, kujiita, kuitwa, kugeuzwa au kujigeuza chawa. Chawa na fyatu wapi na wapi na katika nini na lini na iwe nini kwa ajili ya nini na nani? Fyatu mwenye akili timamu hawezi kuvumilia achia mbali kufuga chawa. Sijui kama chawa wana akili au ubongo hata uwe kiduchu kiasi gani. Sijui hata kama wana utashi au utambuzi wa kujua wafanyacho zaidi ya kusukumwa na silika kama hayawani wengine kama wao.
Chawa anapoitwa fyatu ni poromosheni na fyatu anapoitwa chawa si dharau na matusi tu bali demosheni. Kwanza, sijui. Inakuwaje fyatu mzima akubali kuitwa au kuita wenzake chawa asione aibu wala kuhofia kuonekana hayawani na zwazwa. Inabidi nirejee kwenye kabrasha langu la mabuku ya saikolojia nijikumbushe kitu hii.
Tofauti na chawa, kazi ya mafyatu ni kufyatua kila kitu, fyatu, na chawa bila kujali ukubwa wala unene wao. Hivyo, siamini hata kidogo kuwa fyatu mwenye akili timamu anaweza kuchawawishwa na kuchachawizwa hadi akakubali kuwa au kugeuzwa chawa. Ili iweje? Ili apate nini? Hata kama mie ni fyatu, lazima niseme tena bila kufyatuka. Hakuna binadamu anaweza kuwa chawa wala chawa kuwa binadamu. 
Kuwa, kufanywa, au kuitwa, kugeuzwa hata kuihisiwa kuwa chawa ni kufuru na maudhi kwa mwenyezi Mungu mwenyewe na mafyatu hata wadudu. Ni hayawani na vichaa pekee wanaweza kunyonywa na chawa kwa vile ni hayawani. Hawana uchaguzi wala uwezo kama mafyatu. Sitaki kufikiri. Sijui inahisika au kuwa vipi kwa fyatu kujilinganisha au kugeuzwa hayawani kama mdudu chawa. Sitaki kujua wala ku-imagine.
Kwa wale waliokua na kwenda shule wakati wa Ujamaa, tuliozoea kuwaita wanyonyaji kupe, si kwa sababu ya ufyatu wao bali hatari, madhara, uchafu, udhalili, na uhovyo wao. Tofauti ni kwamba, mafyatu wanyonyaji walipoitwa makupe, hawakupenda tusi hili. Nasi, tuliwaita vile si kwa kuwasifu wala kutaka watusifu bali kuwakatisha tamaa waache ukupe au unyonyaji. 
Kuna tofauti gani kati ya uchawa na ukupe? Kama wahusika wanamaanisha chawa kwa sababu ya unyonyaji na uchafu wao, hapa sina neno. Nijuacho, hakuna kupe waliojitangaza kuwa makupe au sisi tuliowaita makupe kuwavumilia na kuwafanya sehemu ya maisha au harakati zetu. Tuliwachukia. Walituchukia. Tulichukiana. Je kwa chawa hali ikoje? Mie si chawa. Sijui chawa wanajiteteaje kama wanao utetezi kutegemea na uteuzi wao.
Je ni kwanini tuliwachukia kupe? Nani anapenda kunyonywa? Nani anapenda kufuga viumbe visivyo na faida bali hasara na hatari? Wale watunzao wadudu wanyonyaji hufaidikaje nao? Je kunyonywa kuna raha au karaha? Nani anaweza kufuga maradhi kilio kisimfichue? Ni mpumbavu gani huyo anayengoja kufichuliwa na kilio badala ya kutibu ndwele? Wanyama kama ng’ombe, nyati, tembo na wengine hunyonywa na kunguni. Kwanza, ni kwa sababu wao ni wanyama. Pili, hawana dawa na nyenzo nyingine za kuwaangamiza japo wana utashi. Tatu, wana damu nyingi kuliko mafyatu. Nne, pamoja na kutokuwa na dawa na nyenzo, hawawapendi kupe.
Turejee kwenye chawa au machawa kama wasemavyo watoto wa njini siku hizi. Nina swali. Je chawa anaweza kuishi bila ya kuwanyonya awanyonyao? Je anayenyonywa anaweza kunyonywa bila kuwa na damu na uchafu, bila kusahau ujinga au kukosa uwezo kabisa wa kuwateketeza wadudu kama wanyama hapo juu? Je sasa nani hawa wanafuga machawa na kwa nini ili iwe nini? Je chawa wanaweza kuwapo bila damu na uchafu? Je nani hawa wachafu wanaofuga chawa na ili iweje? Kuna haja ya kuwasaidia ima kuwaosha wawe safi na kuachana na mateso ya kunyonywa na aibu ya kuitwa wafuga chawa au kuwapulizia dawa ya kuua wadudu kama tufanyavyo kwa mbuzi na ng’ombe ambao huwa tunawapelekea joshoni mara kwa mara.
Kimsingi, fyatu anayekubali kunyonywa na chawa bila kuwaua au kujisafisha, anahitaji msaada sawa na chawa wanaomnyonya. Unachoweza kufanya hapa, ni kuua machawa ima kwa kumuosha mhusika, kusafisha nyumba yake huku mkimfundisha faida za kuwa safi na madhara ya kufuga chawa au kupulizia dawa za kufyatua wadudu. Je anayefuga chawa na chawa nani mjanja? Je kati yao, nani anahitaji ukombozi? Kumbe nililewa na kulala kwenye mtaro!
Chanzo: Mwananchi leo.

Monday, 24 March 2025

Shemeji, huwezi kumpiga mke wangu


Kisa hiki kinamhusu rafiki yetu. Siku moja, rafiki yetu alisimulia kuwa kulikuwa na mabishano juu ya suala la kifamilia baina ya mkewe na kaka zake wawili ambao ni mashemeji zake. Katika ubishi huu, mke wa jamaa aliwapinga kaka zake juu ya jambo fulani kiasi cha kuwaudhi. Mmojawapo wa wale makaka ambaye ni mkubwa kwa kufuatana na mke wa jamaa alimtishia dada yake kuwa angeweza kumpiga. Kwanza, alisahau kuwa, pamoja na kuwa dada yake, alikuwa mke wa mtu. Pili, alisahau kuwa jukumu walilomkabidhi shemeji mtu alipomuoa dada yao ilikuwa ni kumlinda na kumtunza dhidi ya hatari au tishio lolote. Tatu, hakujua au alijua lakini akasahau kuwa shemeji yake alimpenda na kumheshimu sana mkewe kiasi cha kutoweza kuvumilia kuwa shahidi wa udhalilishaji au utesaji wake.
            Kaka mtu alipomtishia dada yake kuwa angempiga, shemeji mtu aliamka kwenye kiti pembeni ya mkutano wa ndugu na kumwambia shemeji yake “huwezi kumpiga mke wangu nami nikuache. Tutapigana liwalo na liwe.” Kwa vile wale wakaka hawakutegemea kitu hiki, walishangaa na kuogopa kiasi cha kuwataka radhi dada yao na mumewe na ugomvi kuishia hapo. Baada ya tukio hili, kaka mtu walimheshimu dada yao kiasi cha kuwa wakisimulia kisa kile mara kwa mara kwa kuangua vicheko.
            Kwa mujibu wa mtoa taarifa, kaka mtu walizoea kusema kuwa mumewe alikuwa amemfundisha kuwa na roho ngumu, yaani ugaidi. Kwani, hawakutegemea kuwa shemeji yao angeonyesha hasira na kuamua kuingilia ugomvi wa kifamilia. Badala ya kukuta ndugu wakigombana na kuchukua jembe akalime kama wahenga watuhusiavyo, mume mtu aliamua kuingilia kati akimkingia kifua mkewe. Jambo hili liliwapa somo kubwa wahusika. Kadhalika, jambo hili linatoa funzo kwa wengine kuwa, kama utamlinda mwenzio, hakuna atakayehatarisha maisha yake kwa kuwa tayari kumdhuru. Isitoshe, kama mke au mume ni mwili mmoja, kama mmoja atadhalilishwa au kupigwa, na mwingine, kadhalika atakuwa amedhalilishwa na kupigwa.
            Jamaa alitwambia kuwa baada ya mkasa kusuluhishwa hivyo, mashemeji zake walizoea kumuuliza ni kwanini aliamua kuingilia ugomvi wa ndugu badala ya kuchukua jembe akalime? Aliwajibu kuwa, kama angelaza damu na mkewe akadhalilishwa au kupigwa, angeenda kulipia nyumbani mbali na kushindwa kumlinda na kumheshimisha mkewe. Hivyo, alizoea kuwajibu kuwa walipompa dada yao amuoe, walikoma kuwa na mamlaka juu yake. Kwa maana nyingine, wahusika siyo walitaka kuwadhalilisha na kuwaumiza hawa wawili tu bali kupora madaraka ya shemeji yao. Je ni wangapi wanaliona hili hivi kiasi cha kumhami wenzi wao kama alivyofanya jamaa huyu? Ni wangapi wangechukua majembe na kwenda kulima wakati wakiacha mambo ya familia kama yalivyo japo aliyekuwa akiumizwa ni mke mtu? Je wewe ungefanya nini katika hali hii? Je hili limewatokea wangapi na walichukua hatua gani? Si vibaya kumlinda na kumhami umpendaye hasa anapokuwa mke au mumeo. Tuna wajibu kwa wenzetu kama walivyo nao kwetu pia.
            Hivyo, unapokutana na changamoto au tishio kama hili, wala usisite wala kuona aibu kumhami mwenzio. Kwani, kumhami ni wajibu wako na kutomhami ni kushindwa kutekeleza wajibu wako kwake na kwako. Hisani, siku zote, huanzia nyumbani. Kupenda siyo kuambizana nakupenda bali kuonyesha upendo kwa matendo. Hata sheria nyingi ziko wazi kiasi cha kuzuia mke kuwa shahidi dhidi ya mumewe. Chini ya kile kinachoitwa spousal testimonial privilege au haki ya ushahidi wa mwanandoa dhidi ya mwenzake, mwanandoa ana haki ya kukataa kutoa ushahidi dhidi ya mwenzie. Hata hivyo, sheria hii humpa haki haki hii mwanandoa kwa makosa yaliyodaiwa kutendeka wakati wakiwa katika ndoa si kabla au baada ya kuachana. Sheria, mara nyingi, ni kipofu na haina huruma. Ila katika kuleta amani katika ndoa, inatoa haki hii kwa wanandoa. Hivyo, wanandoa wasiojua sheria wasilazimishwe kutoa ushahidi dhidi ya wenzi wao kwa vile jukumu lao ni kulindana na kuhamiana katika kila hali. Pia, kumhami au kumlinda mwenzi wako si hisani kwake bali wajibu wako kwake.
Chanzo: Mwananchi, Machi 16, 2025.

Tulifyatuliwa, tunafyatuliwa, tutafyatuliwe tena

Mwaka jana, Mkaguaji mkubwa wa njuluku za sirkal aka KAGO alitoa taarifa ya kuchefua baada ya baadhi ya mafyatu kufyatua mafyatu wote waliokataa kufyatuka wakafyatua wapigaji wakaishia kuufyata. Alionya kuwa, kama ufyatuaji unaoendelea usipofyatuliwa, kaya nzima ima itaendelea kufyatuliwa kama inavyofyatuliwa na itakavyofatuliwa kiasi cha kufyatuka na kuanza kuwafyatua wanaoifyatua. Na hapa, itakuwa pata shika na shaka, nguo kuchanika.
            Si ubishi wala uchawa kukiri kuwa mwaka ulofyatuka tulifyatuliwa na kuufyata bila kufyatuka. Njuluku zilifyatuliwa na maisha yakaendelea kuwafyatua mafyatu waliogoma kufyatua ima kutokana na ufyatu uchwara au kukosa ufyatu kabisa zaidi ya sifa za kipuuzi. Kazi na sifa ya mafyatu ni kama bomu au upinde. Lazima wafyatuke na kufyatua na si kujikomba na kusifia hata ukumbaff. Ila wasipofyatua wakafyatuliwa wanageuka bomu yaani kitu kisichofaa wala kufyatuka na si bomu linalofyatuka na kufyatua. Hata upinde, lazima ufyatuke. Usipofyatuka, hugeuka upondo.
            Sasa turejee na kufyatua inshu ya KAGO na ufyatuaji wa njuluku za mafyatu uliofanywa na mafyatu waliopaswa kufyatuliwa wasifyatuliwe wakaishia kufyatua, bila mafyatu kufyatuka na kuwafyatua hawa mafyatu, watafyatuliwa tena tena hata mwaka huu. Mwaka jana tulifyatuliwa. Mwaka huu tushafutuliwa. Je tutakubali kuendelea kufyatuliwa na wanaotufyatua na kufyatua njuluku zetu au tutawafyatua kabla hawajatufyatua tukafyata na kufyatuliwa kama tulivyofyatuliwa bila kufyatuka bali kufyatuliwa kama tutakavyo fyatuliwa tusivyofyatuka na kufyatua kabla ya kufyatuliwa kwa vile hatufyatuki tukafyatuka? Naona. Hapa nimefyatua hadi mafyatu wanafyatuka kizungumkuti tokana na ufyatu na ufyatuzi wa fyatu mfyatuzi bingwa wa ufyatu na ufyatuzi asiyeufyata wala kufyatuliwa kama mafyatu waufyatao wakafyatuliwa na wale wawafyatuwao wanaopaswa kuwafyatuwa wasiwafyutue.
            Pamoja na KAGO kufyatua ripoti ya ufyatuzi kayani mwaka jana, hadi unaisha, sikuona wala kusikia wafyatuaji wakifyatuliwa na wale wanaopaswa kuwafyatua ili kukomesha ufyatuaji wa njuluku za mafyatu fyata. Pia, kwenye salamu za kuukaribisha mwaka, sikusikia mikakati ya kuwafyatua wafyatuaji wa njuluku za mafyatu. Ajabu, pamona na mafyatua wapaswao kuwafyatua mafyatu wanaowafyatua mafyatu kuufyata, sikusikia mafyatu wakifyatuka na kudai hawa wanaowafyatua wafyatuliwe au wawafyatue hawa wanaopaswa kufyatua wawafyatuao wasio wafyatua!
            Kwanini mafyatu wanaofyatuliwa hawakuwafyatua mafyatu wanaolipwa njuluku kuhakikisha wanasimamia njuluku za mafyata au kuwafyatua wanaowafyatua hizo njuluku wasiwafyatue? Mwaka jana, nilimsikia mwenyewe kwa masikio yangu mtukuka asiyefananishwa na muungu akisema "sababu dosari zilizotolewa hapa, tutakwenda kukaa tuzifanyie kazi, turekebishe na mwakani pengine hizi hazitajirudia, na tutakuwa tumesogea.” Ajabu ya maajabu, katika hutba yake ya kufunga mwaka uliofyatuka, sikumsikia akikumbushia namna atakavyowafyatua hawa wafyatuaji wa mafyatu waliogoma kufyatuka na kufyatua. Je ni kwanini hakufyatuka lau kiduchu juu ya namna atakavyowafyatua hawa mafyatu wafyatuaji wanaohitaji wafyatuzi ili wakome kufyatua njuluku za mafyatu walioamu kuufyata?
            Mwaka jana, tulivyatuliwa matrilioni. Kama wanaopaswa kuwafyatua wanaofyatua mafyatu njuluku wasipowafyatua, sitashangaa KAGO kuja na ripoti kilio cha ufyatuzi wa madafu gizilioni kama siyo quadrilioni. Kwa vile hawa wafyatuaji hawakufyatuliwa na wale wanaopaswa kuwafyatua, sina shaka, watafyatua njuluku za mafyatu tena kama walivyozoea. Kwa kimakunduchi hii huitwa bizinesi ezi usual. Unafyatua hapa na kuhamishiwa pale ili uendelee kufyatua. Kinachoweza kukuzuia kufyatua hapa ni kifo tu. Kama kikufyatua, kila kitu ikiwemo ufyatuzi wa njulu za kaya vinaisha. Ajabu ya maajabu, hata ufyatue vipi, hakuna atakayeondoka na njuluku za mafyatu anazofyatua. Kwa maana nyingine, ni kama unajifyatua kufyatua visivyoweza kukusaidia bwana Godi akikufyatua.
            Japo ukisema haya unaonekana chizi au zwazwa, fyatu ana nini juu ya uso wa ardhi? Ana nini kiumbe aliyekuja bure na kuondoka bure? Laiti mafyatu wengi wangejua ukweli huu, wasingedhulumiana, kuibiana, hata kuuana kwa ajili ya vitu wanavyovikuta na kuviacha hapa. Ukisema ni utaahira, mafyatu wengi wanakushangaa na kuchukia kuwa umewatukana wakati ukweli ni kwamba ni mataahira wasioona zaidi ya usawa wa matumbo na pua zao. Wangapi waliwika dunia hii tena kwa madaraka makubwa lakini walishafyatuka na kusahaulika kiasi cha mali na ushaufu wao kuviacha hapahapa hata wengine kuharibika? Nani hakumbuki fyatu jambazi kama Mobutu Nseleko wa Kongwa alivyojenga kwao kwenye kijiji cha porini cha Gabadolite? Ukiangalia kilichosaliwa baada ya kufyatua na kuunguza njuluku za mafyatu, unakubaliana nami kuwa wanaofyatua njuluku na mali za umma, wengine ni machizi watakaoacha kila kitu hapa wakiondoka watupu kama walivyokuja.
            Wapo wapi akina Mafarao, Nabukadneza na mashaufu wengi uchwara waliojifyatua kwa kuwafyatua wenzao wakidhani hawatafyatuliwa? Tutankhamun, Farao aliyesifika sana, alikuwa na umri wa miaka chini ya 20. Sasa hawa wanaopiga njuluku za mafyatu na kuwafyatua wataishi milele? Unaweza kuacha mijengo mikubwa, akaunti nono, jua kufa ni kufa tu. Heri kuwaneemesha mafyatu kuliko kuwafyatua hadi inafikia mahali unashindwa kujua ni kwanini tumefyatuliwa, tutafyatuliwa,kama hatutachunga kufyatuliwa tena. Hivi niko wapi?
Chanzo: Mwananchi, Machi 24, 2025.

Tunashangaa, Tunashangazwa, na Kushangaza

 

Huwa nashangaa. Sijui kama nawe hushangaa kushangaza? Kama hushangai, unashangaza. Kama unashangaa, pia, unashangaza. Hata nami nashangaza kwa kushangaashangaa bila kufyatua. Huwa nashangaa kwa ninayosikia bila kuona ukiachia mbali ninayoona bila kuyasikia. Katika kaya yetu ya kushangaza, kuna vitu vinashangaza. Kila siku nasikia mafyatu wakilalamikia ukapuku wa kutengenezwa wakati kuna wanene waliofyatua njuluku hadi wanakufuru. Hawa hunishangaa kama nishangaavyo. Tunashangaana, kushangazwa, na kushangaza. Hapa, sijaongelea upigaji wa kutisha kila siku. Unashangaza. Unashangaa kwanini tunapigwa tukaendelea kushangaa hadi tunashangaza. Kwa kushangaa kwetu, tunashangaza na kushangazana. Ukinishangaa, nakushangaa. Usiponishangaa kwa kushangaa, nakushangaa kiasi cha kushangaza kwa kushangaana na kushangazana.

            Siachi kushangaa. Hushangaa kusikia mapambio, mashairi, ngonjera, na sifa tena vya kushangaza. Waimbaji ni mafyatu, wanyama, hata wadudu tena wanaoshangaza. Mfano, wapo waishio kwenye ukwasi wanaoshangaza wanaowashangaa waishio kwenye uchochole wa kushangaza. Licha ya kushangaana, wote wanashangaza. Wapo wanaoshangaa. Wanashaangana na kushangazana. Inakuwaje fyatu awe kapuku kwenye kaya inayosifika kutenda miujiza karibu katika kila jambo? Inashangaza. Wakati wenye njuluku wakiwashangaa wasio nazo, nao wanawashangaa namna walivyozipata wakati wao wakikosa. Inashangaza. Wanashangaa na kushangaza.

Hakuna kitu hunishangaza kama taarifa ya Mkaguzi mkuu wa njuluku za kaya (KAGO). Je huwa kweli anazikagua au zinamkagua? Inashangaza. Kwanza, hizo njuluku ziko wapi na ni kiasi gani? Inashangaza. Pili, kwa zinavyopigwa, sijui kama kweli zipo za kukagua. Inashangaza.  Kwanini asikague hata njuluku za wenye nazo waliozipiga toka kwa mafyatu wnaoashangaa na kushangaza? Nashangaa. Kago anashangaza kiasi cha kumshangaa. Sijui kama naye anajishangaa kwa taarifa atoazo za kushangaza. Je huwa anatushangaa? Kila mwaka, huwa anaripoti upigaji na madudu kibao udhani kazi yake ni kufyatua habari mbaya kwa mafyatu. Inashangaza. Kingine kinachoshangaza ni ile hali ya waliofyatua tena njuluku ndefu kuhamishwa vituo kwenda vingine badala ya kupelekwa lupango. Inashangaza.

 Wakati nikishangaa hili, huwa nashangaa namna Mwendesha Makesi wa Kaya (Dipipii) anavyoweza kukukamatisha, ukapozwa hata kusahaulika lupango halafu anajitoa welewa na kusema eti amekufutia mashtaka. Inanishangaza. Huwa namshangaa na vitu kama hivi vya kushangaza. Je huu muda fyatu wapotezao lupango unalipwa na nani? Inashangaza. Huwa nashangaa kama hii nayo ni haki, sheria, na utawala bora. Juzi, nilimuona mzee Silaha, akiwa amechakaa. Nilishangaa. Alikaa lupango kwa mwezi na ushei. Inashangaza. Ukiuliza nini mbaya alifanya? Unashangaa. Unashangaa ni kwanini ndata walimnyaka na kumsweka lupango bila kupeleka kwa pilato! Unamshangaa yeye kuswekwa lupango bila kosa. Unawashangaa ndata hawashangai hili. Pia, unawashangaa wanene wanaoshangaza kwa kudai kuwa wameleta maendeleo na ustawi. Inashangaza. Hivi vinaweza kupatikanaje bila haki? Inashangaza!

Wakati nikiwashangaa Kago, Dipipii, na ndata wa kushangaza pia, humshangaa munene anayeshughulikia njuluku asifikaye kwa kutoa misamaha ya kodi kwa wenye nazo huku akizidi kuwakamua wasio nazo kwa njia mbali mbali kama vile maokoto, tozos, na madude mengine ya ajabu ajabu na kushangaza. Inashangaza. Kabla ya kumaliza kumshangaa jamaa wa njuluku, huwa nashangaa kusikia kuwa kaya imefunguliwa. Inashangaza. Kwani, nani alikuwa ameifunga na kwanini na ili iweje? Inashangaza.

Hakuna kitu nashangaa kama kukatikakatika kwa umeme. Inshangaza sana kwa namna tunavyoahidiwa kuwa migao ingegeuka historia wakati wowote. Inashangaza namna ambavyo mambo ya kushangaza hutokea na ahadi za kumaliza migao kugeuka donda ndugu. Inashangaza ni kwanini hawa wanaotoa ahadi za kushangaza hawajishangai pamoja na kushangaza! Inashangaza na waathirika wasivyowafyatua. Inashangaza sana kwanini wanaofeli katika kutoa huduma nyeti kama hii kutoachia ngazi ili wenye uwezo waingie na kurejesha heshima ya kaya. Huwa nashangaa. Nashangaa sana kuona kuwa wale wale wanaotudanganya, wanafanya hivyo si mara moja wala mbili. Inashangaza.

Ngoja nifyatue mfano japo mmoja wa kushangaza mjue kwanini nashangaa na kushangazwa.Waziri mkubwa alikaririwa mwaka jana akisema “kwanini Muentertain wizi? Watu wanaiba mara ya kwanza, mara ya pili mmeshindwa kuchukua hatua za kuwadhibiti wasirudie tena?” Inashangaza. Nasikia mafyatu wanafyatua hata pesa ya wagonjwa. Je nini kimefanyika badala ya kulalamika? Inashangaza. Waziri mkubwa, pamoja na mamlaka yake, anashangaa. Inashangaza kweli kweli.

Naendelea kushangaa haya mambo ya kushangaza. Mfano, rahis, akihutubia buge, mwaka 2021 alisema “naomba kutumia jukwaa hili la Bunge lako Tukufu kuwaonya wale wote wanaodhani kuwa usimamizi wa mali ya umma kwa maslahi ya wananchi, kukataa ukwepaji wa kodi, wizi, na kukemea uzembe vitasimama kwa sababu tu Rais Magufuli hayupo.” Inashangaza.

Kwa ufupi ninashangaa, inashangaza, nawashangaa japo mnanishangaa kiasi cha kushangaza na kushangazana kama siyo kushangazwa. Wakati mwingine natamani tuitwe washangaaji kama siyo washangazaji. It’s too much. I wonder.

Ninashangaa kwanini nashangaa! Je wewe unashangaa au unashangaza? Hakika. Tunashangaa, kushangaana, na kushangaza. Mafyatu itikieni ‘kweli inashangaza na mseme amina.

Chanzo: Mwananchi, Machi 12, 2025.

Sunday, 9 March 2025

Sasa Kanji nafyatuka nageuka fyatu dugu yangu!


Juzi natoka Bombei ona mama na toto. Iko furahi kuba sana. Naacha toto moja. Nakuta mama nakwisazaa toto sita. Yote faida. Nakaa Bombei. Woo! heva iko chafu veve hapana ona. Sikia tu. Nalala naota Tanjania. Baada ya peleka faida, sasa narudi tafuta faida nyingine.
        Napanda dege. Nafika hapa. Swahili moja fyatu nataka fyatua mimi. Nalalamika kama toto eti fyatu fyatuzi iko nafyatua mimi hadi nafyatuka! Swahili nakuta mimi iko soma gazetini. Nauliza kwanini juluku naibiva kila siku? Nasikia hii iko chava. Kama nasema baya sirkal, nachukia veve. Kwanja, naanja. “Hii hindi iko chafu nachanganya Swahili sana. Napenda sana siasa na iko na multiple citizenship.” Nalalamika eti hapana piga kura lakini kama ongozi nachaguliwa, yeye nakaribisa na kuwa karibu nayo. Naongeza kuva Kanji nafanya ongozi sahau ile nachagua yeye. Sasa iko kosa ya yangu au ongozi? 
        Hii jinga naita mimi choli! Lini swahilihindi nakuwa safi dugu yangu? Kama nafyatua hindi nachanganya na Swahili nafanya juli sana. Naondoa baguzi ya luga na rangi dugu yangu. Sasa kosa nini veve nataka fyatua mimi dugu yangu? Mimi iko penda veve sana na juluku yako naleta dukani yangu nunua witu. Vote napata faida. Veve chukua witu. Mimi chukuva juluku. Hapana pendeja hiyo dugu yangu?
Nafika jumbani. Nakuta Swahili nalalamika sana. Nauliza “iko nini veve nalalamika owo kama toto dogo? Swahili iko sangaa kama paka naona juluku! Nauliza tena. Veve napata sida gani nasangaa hiwi? Nasema eti mimi hapana ongea Swahili juli. Nasangaa hadi nataka fyatua Swahili. Nauliza yeye “kwani Swahili iko ongea hindi juli? Sasa Swahili nataka fyatua kila kitu. Nataka hata kuoa totoz ya hindi! Kwanini nakuwa chokoji? Veve iko ona hindi naona totos ya Swahili? Sasa kama siyo nafyatuka, kwanini taka oa totos ya hindi veve Swahili choli?
        Swahili iko tabu mingi sana. Maisha iko gumu au fyatu iko gumu fyatuka na kufyatua ile nafyatua yeye? Naona vatu ikolalamika maisha iko gumu kama jiwe. Kwani, swahili siyo gumu? Swahili nalalamika kama toto dogo. Hindi nalalamika kama vatu kuba. Kama maisha nakuva gumu, kwanini hapana fyatua ile nafanya maisha kuwa gumu? Sasa lalamika nageuka sera ya vatu vote kwa kayani. Hindi nalalamika. Sirkal nalalamika. Tajir na sikini yote lalamika! Kama sirkal nalalamika, nan tasaidia nani? 
            Maisha iko gumu. Sasa hindi nafatyatuka nageuka fyatuzi dugu yangu. Sasa nauliza polepole. Juluku kayani nakvenda vapi? Mbona ile kuba naishi peponi? Kama Swahili napata juluku, naoa vake mingi. Hii hapana lalamika! Natumia juluku mingi fanye serehe. Juzi nakwenda Bembei. Kule jimboni yangu India, vaziri moja ya koa nasamehe juluku rupia laki moza nafukujwa kaji. Hapa vaziri nasamehe, trilioni napandishwa choo! Sasa hapa laumu nani na nini dugu yangu? Kvanini hapana fyatuka ikafyatua ile nafyatua veve dugu yangu?
Svahili iko tabu sana. Nakwenda sule. Napata digrii mingi. Hapana fanya biasara. Naogopa hasara lakini naishi kwa hasara. 
        Swahili iko penda faida. Vapi tapata faida kama hapana biasara? Au nataka kwenda kwa sirkal na kuibia chofu na fyatu juluku? Ile nasoma nayo howo kabisa. Napata digrii ya chumi nakuja chuma chovu na fyatu! Ile napata kazi kwa sirkal nageuka fisadi kuba. Kama hindi nasindva kwepa kodi, hapana lalamika. Hapa svahili nalalamika. Nasema hindi fisadi kuba. Kwani, hindi dio naongoza kayani?
         Sasa sirkal kama nalalamika hapana juluku, kvanini nasamehe kodi ile fanyabiasara kuba kuba? Hapana ona nafyatua na kuumija vatu yake? Nasikia kwa bungeni vaziri naulizwa kwanini nasamehe kodi bila kufuata sharia. Yeye nanyamaza kama jusi nabanwa na lango au chura kuba!
Sasa fyatu vote nakaa kimya hapana fyatukia vaziri lakini nafyatua kelele tu! Napiga kelele mingi kama chura ya bawani. Chura iko imba “yangu yangu.” Kama naokota jive napiga yeye, nakimbia! Natoka bawani hapana guo ya mvilini. Mingine naita chava. Naitwa chava nafurahi! Chava iko dudu chafu. Iko dogo na howyo sana dugu yangu. Je Swahili natofautina na chava guoni na chura bawani? 
        Kama nataka pata juluku, napasa kwenda fyatua ile fyatu kuba nafyatua juluku yao. Napasa zuia choli na mizi kuba. Kama naiba juluku na fyatu naomba yeye saada, sasa taacha kuiba juluku? Hapana nunua gari mingi ya sirkal. Naharibu kusudi. Nanunua vatu kuba kuba. Nakaa jumbani kuba kuba. Naoatesa tumbo kuba kuba. Naitwa kuba. Kila kitu ya kuba, kuba tu. Sasa dogo naishi vapi na wipi? Hapana tumia gari ya sirkal sereheni. Hapana nasafiri sana. Hapana fanya sanii na babaisaji mingi mingi. 
Kama nafanya mambo kuba na veve iko dogo na akili dogo, hapana ona naleta balaa na fyatu mingi nakosa juluku hadi nafyatuka nataka kufyatua veve kwa sababu ya jinga yako na akili dogo? Du! Kumbe naota!!
Chanzo: Mwananchi Alhamis iliyopita.

Chunga yasikukute ya Aziz na ndoa ya majuu

Aziz ni kijana wa miaka 24 wa Kipalestina aliyekimbia udhalilishaji kwao akaishia kudhalilika majuu. Kisa cha Aziz kinafikirisha, kusikitisha, na kufundisha. Wapo wengi kama Aziz walioharibikiwa maisha baada ya kuolewa wakidhani wameoa majuu. Kijana huyu, akiwa hajui hata Kiingereza, alijikuta akijiingiza kwenye ndoa ya mateso. Nkwazi alimjua Aziz. Alikuwa rafiki wa kaka yake aliyemlalamikia kuwa mdogo wake alikuwa akipoteza mwelekeo.
Tokana na kuwajua wote wawili, Nkwazi aliamua kuingilia kati kumsaidia Aziz. Kaka mtu aliwakutanisha Aziz na Nkwazi nyumbani kwetu walikozoea kuja kupoteza muda na kufundishwa Kiingereza. 
        Baada ya kaka mtu kueleza kisa kizima mbele ya mdogo wake, kama marafiki na walezi, tulimuuonya Aziz asijiingize kwenye uhusiano ambao ungemletea majuto baadaye. La kufa halisikii dawa. Azizi alichukia hadi kutwambia “hii ni Kanada nchi huru ambapo kila mmoja anaweza kufanya atakavyo.” Kwa maneno mengine, alitaka tusimuingilie katika maisha na uhuru wake hasa ikizingatiwa kuwa Kanada, vijana huweza kuamua kufunga ndoa hata bila kuwahusisha wazazi na ndugu japo si wote. Ghafla, Aziz aliacha kuja kwetu. Tulijua sababu. Aziz alikuwa kwenye mapenzi na mama aliyemzidi umri tutakayemuita Meg japo si jina lake aliyetaka wafunge ndoa. 
Pamoja na kumuonya asisikie wala kujali,  tulijua ni haki yake kufanya hivyo japo tulimtahadharisha juu ya tofauti za mila na dini. Mfano, tulimjua Meg kama mama aliyekuwa amempenda akipanga kufunga naye ndoa, alipenda sana kuongelea mbwa wake ambaye alikuwa akisema kuwa hata hula na hulala naye wakati mwingine. 
        Si ajabu huku kwa baadhi ya watu kula na mbwa kwa sababu kwao, mbwa ni sehemu ya familia. Hivyo, tuliona hatari itokanayo na kutofautiana kidini na kimila ambavyo vingemkwaza Aziz japo hakusikia. Baada ya kugundua kuwa Aziz alianza kutuchukia mbali na Meg ambaye alikuwa ameambiwa juu ya ushauri wetu, tulimuacha. Maana, yalikuwa ni maamuzi na maisha yake.
Hakika, Aziz na mama wa Kizungu walifunga safari kwenda kwenye visiwa vya Saint Lucia na kufunga ndoa na Meg.doa ilifungwa. Ndoa ilifungwa na fungate ikafanyika. Aziz na Meg walirejea Kanada wakiwa mke na mume. Baada ya muda mfupi, tuliamua kuhama mkoa tuliokuwa tunaishi na kusahau mambo ya Aziz na Meg.
Siku moja, Nesaa alikwama kwenye theluji usiku akitoka shule. Alijitokeza baba mmoja wa Kiarabu aliyekuwa na familia yake akamsaidia kwa kujaribu kukwamua gari asifanikiwe. Hivyo, alishauri ampe lift hadi nyumbani. Yule baba alimfikisha Nesaa nyumbani. Tuligundua kuwa kumbe aliishi mtaa wa pili toka kwetu. Alimsaidia Nkwazi kukwamua gari na tangu siku hiyo wakawa marafiki.
Baada ya miezi kupita, yule Mwarabu alikuja kutuaga kuwa alikuwa anahamia Toronto. Tulifurahi sana na kusikitika. Hata hivyo, alituuliza kama tunamjua Aziz toka kule tulikokuwa tukiishi mwanzo. Alituelezea namna Aziz alivyomuomba atuombe msamaha kwa kudharau ushauri wetu.             Tulimuuliza yule Mwarabu sababu za Aziz kukimbia na kujutia ndoa yake. Alitwambia kuwa Meg hakuwa tayari kubadili dini wala kuheshimu mila ya Aziz mbali na kutokuwa tayari kuacha kufuga mbwa wake kipenzi pamoja na mambo mengine binafsi kama nani mwenye madaraka zaidi ya mwingine kati yake na mkewe. 
        Kwa ufupi, Aziz alijikuta kwenye ndoa ya mateso hadi akakimbilia Toronto kuepuka ndoa ya mateso. Tulifurahi kusikia kuwa Aziz alikuwa amegundua makosa yake na mchango wetu na kujutia. Hata hivyo, maji yalikuwa yameishamwagika. Aziz, licha ya kuonja mateso na kuumia, alipoteza malengo na muda wake. Kwani, tulimshauri akasome kwanza akaghairi. 
Sasa tujiulize. Kisa hiki kinafundisha nini? Mosi, usilolijua litakusumbua hata kukuuumiza. Pili, asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Tatu, vijana waepuke kujiingiza kwenye makubaliano ya ndoa bila uzoefu wala ushauri.
        Nne, tofauti za dini hata mila ni muhimu katika kufikia maamuzi ya kufunga ndoa. Mfano, Aziz, muislam, asingeweza kuishi na hata kuchangia kitanda na vyombo na mbwa.
        Tano, umri katika ndoa ni muhimu. Japo hatukatazi waliozidiana umri kuoana, kuna haja ya kulidurusu na kulijadili hili kabla ya kujifunga kwenye ndoa. 
        Sita, si kila ving’aravyo ni dhahabu.
saba, ingawa haya yanaweza kuchukuliwa kama masuala binafsi, yana somo kubwa kwa vijana wanaofikiri kuwa kuoa majuu ni kuukata. Wakati mwingi na mwingine, kufanya hivyo si kuukata bali kukatwa kama ilivyo kwa Aziz na wengine kama yeye.
Chanzo: Mwananchi Leo J'pili.

Wednesday, 26 February 2025

No reforms, no elections ilhali tushageuzwa na kuchakachuliwa!!

 

Mjini hakuna stori ya no reforms no elections, kwa kisambaa, hakuna mageuzi, hakuna uchaguzi. Kwanza, sijui kama mafyatu waliofyatuliwa na shida wanaweza kufyatuka wakawafyatua wawafyatuao. Wapo wanaosema eti mafyatu watinge mitaani na kukinukisha! Loo! Mbona mwaota mchana! Mnategemea mafyatu waliofyatuliwa wakafyata wafyatuke watekwe na kupotezwa? Nani afyatuke afyatuliwe shaba kama Tunda Lishe? Waliokwishatekwa, kuteswa, na kupotezwa watoshe. Nasikia ngebe za mageuzi kutaka uchaguzi huru na wa haki. Nani kawambia duniani kuna haki au uhuru hasa kwa mafyatu wafyatuliwa? Hamjaambwa kuwa haki hupokwa na iko peponi au motoni? Acheni ufyatu. Mkikomaa, nateka na kupoteza mkapate haki huko mtakakoharakishiwa. Siwatishi au kufyatuka kifyatu. Wangapi weshatekwa na kupotezwa? Nini kimefanyika?
            Tukiwa wakweli, lini mliwahi kuwa na uchaguzi huru na wa haki au mnaita uchakachuaji uchaguzi? Mnataka kumfyatua nani? Uchaguzi ni dhana tata. Unaweza kuchagua hata kuchakachua ukajiaminisha umechagua. Waweza kutochagua ukapitisha bila kupingwa ukajiridhisha umechagua japo hukuchagua. Mnataka mageuzi. Nani anataka kugeuzwa kama pweza kikaangoni ilhali walaji weshajiandaa kumfyatua hata bila kumpika au kumgeuza?  Kubalini yaishe. Baada ya wenye kaya kufyatua na kupitisha ‘mpendeka na mkubalika’ bila kupingwa hata walipotaka kumpinga, wapingaji wamefyatuka. Wanataka wamfyatue kupitia mageuzi. Wanafyatuka eti watasusa uchakachuaji. Ebo! Mkisusa, wachakachuaji watachakachua, kufyatua, na kula. Mmesahau mazoea au mwajitoa akili? Mnakuwa kama hamjui inshu mafyatu wangu! Kwa taarifa yenu, hata muwange uchi, hakuna cha haki wala mageuzi.
            Mafyatu wangu mlofyatuka na kutaka kufyatua, mnataka kujifanya hamjui manufaa ya kupitisha bila kupingwa kwa kaya na mafyatu waliofyatuliwa wakagoma kufyatuka na kufyatua!? Nazoza na mafyatu mliofyatuka mkatishia kususa uchakachuaji. Kwani hamjui kuwa mpakwa mafuta aliyepitishwa bila kupingwa lazima apite, apete, na kutesa hata mkisusa? Nyie mafyatu msiofyatuka hadi mkafyatuliwa nani aliwaroga kudhani kuwa mageuzi yanaweza kuleta mageuzi ilhali gegezi? Mkitaka mageuzi, jigeuzeni mfyatuke muache kufyatuliwa. Haki haiombwi, hupokwa. Hivyo, kususa ni kusuasua na kufyatuliwa. Badala ya kusema no reforms no elections mseme we must fyatuka and fyatua them to grab our rights. Period.
            Tukubaliane hata kwa kupingana. Mnapingaje mteule wa Mungu mwenye maono na ndoto visivyo vya kifyatu? Hamjui kuwa wateule wa Mungu hupaswa kutawala milele kama Ngwazi wa kwa akina Bwinobwino? Hamuoni maajabu yalotendwa kama ‘kufungua’ kaya iliyomkuwa imefungwa kwa makufuli japo ‘mfunguaji’ alikuwa na walioifunga, kama kweli ilikuwa imefungwa? Sasa kaya ‘imefunguliwa.’ Mnataka nini kama siyo ufyatu uchwara unaowafyatua? Mnapingana na kazi ya Mungu iliyomuondoa Jiwe. Eti mwataka kitabu, sijui katibua, sijui katiba! Mshaambwa kitabu mnachotaka kibadilishwe ni makaratasi yasiyoweza kuzuia mteule kupeta hata kwa goli la mkono.
            Kwa vile kimeishaumana, ishajulikana. Mafyatu weshafyatuliwa wakafyata wasifyatuke. Napendekeza tuokoe njuluku za mafyatu. Tusifanye uchakachuaji, sorry uchaguzi. Isitoshe, tukipitisha mpakwa mafuta tena bila kupingwa na kupingana, tutaondoa hatari za kutekana na kupotezana. Kwa vile ‘anakubalika’ kwa kila kiumbe, mafyatu, ndege, hata wadudu kama chawa na kunguni waliotamalaki siku hizi tokana na maajabu na miujiza, nasema kwa kinywa kipana tena kwa herufi kubwa HAKUNA MAGEUZI. No chakachuaization. Si inampendeza?
            Wasusaji, chonde chonde. Msituvurugie amani kupinga visivyopingwa au kutaka kugeuza visivyogeuzwa. Mnadhani waliofyatuliwa wakapitisha hawakufanya mageuzi? Unaweza kufanya mageuzi bila mageuzi na yote ni mageuzi. Kama mligeuzana na kupinduana, hayo hatutaki. Mnadhani mlivyochafuana na kuvuana nguo, mngekuwa na dola, si mngetekana na kupotezana? Shukuruni hamna dola. Mafyatu tunataka mapinduzi si mageuzi. Mapinduzi huleta amani. Mageuzi huleta machafuko. Nani anataka shari? Kawaulize wenzenu wa kaya ya jirani waliofanya mageuzi. Kila siku, wanageuzana hadi inakera. Wamegeuzana hadi wakawageuka mafyatu. Najua wapingaji hamjakaribishwa kufyatua keki ya kaya. Hivyo, mwawaonea maya tu. Kwa anayetaka mageuzi, anapaswa kupoka haki ndo aje na lugha ‘isiyokubalika’ ya mageuzi. Mnageuza nini wakati tulishageuzwa tangu zama za zidumu fikra za mkiti? Anayebisha aniambie. Lini tulifanya uchaguzi zaidi ya uchakachuaji na uchaguzi?
         Mcheke, mnune, mfyatuke, mfyate, mzoze, mzuzuke hata kuzomea, lazima mpakwa mafuta apite kama alivyoingia. Sasa mnafyatukafyatu ili iweje? Ufyateni na kukubali kufyatuliwa au mfyatuke mfyatue tujue. Kwanini kutaka kugeuza ‘mageuzi’ makubwa ya kidemokrasia yaliyokwishafanyika? Nani haoni haya mageuzi na maendeleo? Kama mnayaona, basi yakubalini tuendelee kutesa pasina kutesana au kuteseka na mageuzi. Kama hamuyaoni, jifanyeni mnayaona. Kama hayapo, jifanyeni yapo, na kama hayafai, jifanye yanawafaa hata kama hayawafai. Mwataka tuwakaubalie mgeuze mipango iliyopitishwa bila kupingwa? Machawa, sorry mafyatu weshasema liwalo na liwe.
Lazima mpakwa mafuta wao apite. No fyatuka, no fyatuliwa. Nisisiteze. Unaweza kuchagua kwa kutochagua na kutochagua kwa kuchagua. Yote ni uchaguzi na uchaguzi ni demokrasia hata kama ghasia. Wanaotaka mageuzi, wangoje hadi Yesu arudi. Hivi leo nimekunywa ngapi?
Chanzo: Mwananchi Leo.

Chunga usiolewe majuu ukidhani umeoa!


Kisa cha jamaa yetu toka tena kwetu Tanzania (mji hatutaji) kinafikirisha na kufundisha kwa wale ambao hawajaingia mkenge kama huyu bwana. Akiwa amesikia mazuri mengi juu ya kuukata kwa kwenda majuu, jamaa alianza mipango ya kwenda majuu kwa njia yoyote ili mradi mambo yake yamnyokee. Alitaka kuukata asijue unaweza kumkata yakamkuta ya kumkuta kama yalivyomkuta. Sawa na vijana wetu wengi, baada ya mambo kuwa magumu na kuwepo misifa mingi juu ya majuu, kijana aliamua kuingia mawindoni kusaka fursa za kumwezesha kukamilisha mipango yake ya kuukata. Kwanza tukiri. Huyu jamaa alifanya utafiti japo si kwa makini. Hakuwe peke yake. Vijana wetu wamejikuta kwenye hatari mbali mbali kama vile kuingia kwenye mataifa ya watu kinyume cha sheria na kuishia kurudishwa hata kufungwa huku wakishuhudia ndoto zao zikiyeyeuka.
        Zamani walikuwa wakizamia kwenye meli. Siku hizi hii njia ni kama imezibwa. Wapo wanaoamua kuomba vyuo ng’ambo ili waweze kuingia kule. Wakishaingia, hukimbia vyuo na kutafuta vibarua lau wajikimu na kuanza pilika za kupata makaratasi ya kuwawezesha kuishi kule kihalali. Wengine huamua kuoa hata kuolewa ili waweze kuishi kule. Kutokana na hii, vijana wetu wengi wanaolewa na wanawake wa Kizungu ili iwe passport ya kupandia majuu. Katika kisa hiki, picha hii inajitokeza kama tutakavyoidurusu.
        Tupo kwenye supermarket na jamaa toka Sudani.  Bila hili wala lile, anatuijia mama Kizungu akiwa na watoto machotara wa Kiafrika na Kizungu.   Kwa kuona hivyo, tunajua huyu mama kaolewa na Mswahili mwenzetu. Tunajipa moyo kuwa yupo sehemu akifanhya manunuzi, hivyo, akimaliza, atatokea japo tujuane. Wakati tukiwaza hili, yule mama wa Kizungu atujongelea na kutusalimia kwa uchangamfu kana kwamba tunajua. Hatushangai. Ni shemeji yetu hata kama hatujui atokako mumewe. Maana, huwezi kujua. Anaweza kuwa mweusi lakini siyo Mwafrika hasa kama anatokea Caribbean au Amerika ya Kati. Baada ya kutumakua kwa Kiingereza, nasi, bila ajizi wala hatujivungi. Tunajibu salamu zake. Anatuuliza “nyie mnatokea Afrika?” Tunamjibu kwa bashasha “haswa.”
            Mama wa Kizungu anatuuliza swali ambalo si Wazungu wengi huuliza kwa vile, kama ilivyo kwa Waswahili kuwa kila Mzungu anatokea Ulaya, nao wanadhani kuwa kila mtu mweusi anatokea Afrika bila kujali nchi walizotengeneza wao. Anauliza “mnatoka nchi gani Afrika?” Swali lake linanishangaza na kunifikirisha. Nami nauliza “umewahi kwenda Afrika? Anajibu “ndiyo, naijua Tanzania ambako ndiko anakotokea mume wangu ambaye bahati mbaya nilimzuia kuja nasi ili akae na watoto.” 
Msudani mmoja anadakia huku akionyesha kidole kwangu “huyu jamaa anatokea Tanzania.” Mama anatabasamu. Napigwa na mshangao tokana na Wazungu wengi kudhani Afrika ni nchi moja. Hivyo, wengi hawajui kuwa Afrika ina nchi zaidi ya hamsini walizotengeneza japo sasa wanaziunganisha. Namuuliza “ni wapi unajua Tanzania?” Anajibu “Arusha, Zanzibar, na Darasalam.”
            Baada ya maongezi mafupi, nawataka radhi tuondoke. Yule mama anatuaga kwa furaha akisema “kama mnaishi hapa, tutakutana tena na mtaongea na mume wangu.” Nami namjibu, “hatuishi hapa. Tunaishi mpakani na Marekani kama kilometa 40 toka hapo japo huwa tunakuja mara nyingi hapa kununua bidhaa.”
            Baada ya kuachana na yule mama, Msudani mmoja anasema “wallahi huyu mama kanifurahisha. Anaipenda Afrika.” Namkatalia. Namuuliza “umesikia alivyosema kuwa anasikitika alimzuia mumewe kuandamana nao ili akae na watoto?” Naongeza “huoni kuwa mwenzetu kaolewa?” Jamaa anastuka. Namwambia “huyu Kawajia yaani mama wa Kizungu hafai.” Tunaachia maongezi hapo na kwenda zetu. Nilipofika nyumbani, nilimpa Nesaa kisa kizima yakaishia hapo.
            Baada ya kama mwezi mmoja, tulirejea na familia kununua mahitaji kawaida. Bila hili wala lile, mwanetu mmoja anasema “naona Waafrika wale.” Kugeuka, tunamuona yule mama wa Kizungu na mumewe Mwafrika wakitujongelea. Mama wa Kizungu ananisalimia kwa bashasha. Anamwambia mumewe “ni yule jamaa niliyekwambia.” Tunapeana mikono jambo ambalo Wazungu wengi huwa hawafanyi. Namgeukia Nesaa na kumwambia “huyu ndiyo yule mama niliyekwambia.”
            Familia mbili zinachangamkiana wazazi na watoto. Mume wa Mzungu ananiuliza kwa kiswahili fasaha na mshangao “hii ndiyo familia yako?” Namjibu “naam.” Anajibu kwa kunyong’onyea “heri wewe umekuja na mkeo.” Nilimuuliza “mwenzetu Tanzania unatokea wapi na ilikuwaje ukawa huku?” Jamaa alitaja atokako Tanzania na namna alivyokuwa akifanya kazi kwenye utalii walopokutana na mkewe wa Kizungu wakaamua kufunga ndoa. Japo hakusema, lengo la kufanya hivyo ilikuwa ni kuukata kwa kuja majuu ambako uliishia kumkata. 
    Japo si wote, wengi wa vijana waliojiingiza kwenye ndoa hizi huishia kuolewa na kutumikishwa mbali na kutumiwa kuzaa watoto ambao kwa nchi zenye upungufu wa watu ni mali, huyu jamaa unaweza kumuweka kwenye kundi hili. Isitoshe, si yeye tu. Wapo wengi ambao, mara nyingi, hujutia uamuzi wao pale wanapojikuta wakimilkiwa na kutumikishwa kama mashini za ngono na watumwa wa mapenzi.
            Kufupisha kisa kirefu, yule bwana, pamoja na kunituchangamkia, hakuonyesha nia ya kutaka tumjue lau kutukaribisha siku moja tutembeleane. Hakutoa namba yake ya simu. Nami, kadhalika, sikutoa namba yangu ya simu. Kwa lugha ya mwili, hakuwa tayari kuwa karibu nasi. Nami nilifahamu ni kwanini. Angependaje tuwe karibu tuone anavyoishi? Pia, tunadhani alijua tunajua waume wa namna hii wanavyoishi kama tutakavyobaini kwenye kisa kingine cha Mfilipino aliyeolewa na mama wa Kizungu.
Chanzo: Mwananchi J'pili.

Wednesday, 19 February 2025

Barua kwa waliofyatuliwa na Tarampu


Kwanza, nawasalimia kabla kuwafyatua lau mfyatuke muwafyatue waliofyatua hadi mkakufyatuliwa na shida mkakimbilia kwa Tarampu aliyefyatuka na kuwafyatua. Nilimwandikia barua. Hajanijibu. Pili, niwajuze. Fyatu niko poa. Najua. Wengi wameniandikia barua mapepe kwa mapepe wakinisikitikia kuwa nitarejea na pingu miguuni na mikononi baada ya Tarampu kufyatuka na kufyatua. Wapo pia wanaoomba nirejeshwe lau wanikoge hasa wale walionibomu nikawachunia. Kadhalika, wapo wanaonionea huruma kuwa nikifyatuliwa na kutua na nitafyatuliwa na ukapuku na mifupo jizi nisiyozoea. Hawa ni nilikuwa nikiwatumia njuluku kidogo mbali na kuwapa moyo kuwa kuna siku ningewasukia waje majuu kutesa wasijue unaweza kuja ukaishia kuteseka.
       Tatu, wapo niliowafyatua hasa wanene wanaotamani nishuke kwenye pipa na pingu nao wanifyatue kuelekea lupango. Hafyatuliwi fyatu vinginevyo nitake. Kwanza, siishi kwa Joji Kichaka mbali na kuwa, hata nikipewa green card, nitaichana. Nani aishi kwenye kaya inayofyatuliwa na kichaa mbaguzi japo ana pwenti?
Nije kwenye inshu. Kwanza, nawashauri watakaofyatuliwa na kurejeshwa na pingu wasikonde na kusononeka. Afrika ina fursa bwererere. Kwa yeyote aliyeishi ughaibuni, kama hazioni, ajue anajifyatua au kujifyatulisha mwenyewe. Najua mifumo yetu ya kikale na kirushwa. Ukikomaa unatoboa. Hivyo, nendeni mkachafyatukie fursa ilmradi msijiingize kwenye siasa za majitaka mkaambiwa mna uraia pacha japo hamna. Pili, nawashauri. Mkishafyatuliwa na kurejea home, fyatueni wanaowafyatua. Anzeni mandingo kuonyesha namna exposure yenu ilivyowakomaza hadi mkang’ang’ania ughaibuni.
Tatu, nawashauri msirudie kosa kudhani kuwa ughaibuni kuna barabara za dhahabu na pepo. Nne, mbali na ubaguzi aliionyesha Tarampu na wengine kama yeye wanaozidi kuchepuka huko Ulaya, mjue adui yenu yuko home siyo ughaibuni. 
Tano, mjiulize hasa wale waliokimbia ukapuku, ilikuwaje mfyatuliwa na kugeuka makapuku kwenye bara lenye utajiri chekwa? Je tatizo ni wanaowafyatua mlowatengeza wenyewe mkashindwa kuwafyatua au nyinyi? Je mmejipanga vipi kuwaelimisha mafyatu juu ya kuwafyatua mafyatu wanene wanaofyatua hadi ukapuku ukawafyatua mkakimbilia ughaibuni bila kuwafyatua?
Sita, hakuna kitu hunichanganya kama sirkal kuhangaika na namna ya kufyatua njuluku toka ughaibuni wakati haina mpango wowote wa kuwasaidia mnapofyatuliwa kama kaya nyingine zilivyofanya kwa mafyatu wao waliofyatuliwa na Tarampu. Sijui hata kama wanajua idadi yenu na mahali mlipo. 
Saba, mjue, njuluku zinazotafutwa na sirkal husaidia mafyatu wezi wanene kuzifyatua na kupoza machungu yenu kiasi cha kushindwa kuwafyatua. Hivyo, husaidia wawafyatue kirahisi. Sasa Tarampu kafyatuka na kufyatua. Mafyatu fyatukeni mfyatue na kudai haki zenu badala ya kutegemea kukimbilia ughaibuni. Hisani huanzia home mafyatu wangu. Hata Tarampu angewajaza madolari na kumkatuma home, wezi wanene wangeyafyatua mkaendelea kuwa makapuku pamoja na kubeba moboksi usiku na mchana.
Kwa wale kama mimi wasio na wasi wasi wa kufyatuliwa wala kulazimika kuchukua uraia kwa sababu uraia pacha ni dhambi kayani, nendeni shule mkafyatue mambo ya maana ili mkirejea lau muwe na nyenzo za kufyatua njuluku kihalali. Mnadhani nisingefyatua shule ningepewa na kuaminiwa uga wa kufyatua ninayo fyatua tena kifyatu bila kuogopa hata mhariri wangu. Sorry. Nimesemaje? Mezea hiyo kama nimekukwaza  bosi wangu. Nilizidisha kanywaji na chigala kubwa.
Najua. Wengi hawatapenda ufyatuzi huu hasa wale wanaowafyatua mafyatu waliogoma kuwafyatuka na kuwafyatua. Kimsingi, Tarampu anatufundisha somo la kujitegemea, kufyatuana, kutokuwa wavivu, kujiheshimu, kutenda na kutendeana haki, na uwajibikaji wa pamoja kama mafyatu tuwe wakubwa hata wadogo. Kwa wanaomkumbuka jembe Joni Kanywaji, alitufundisha kuwa tukifyatuka na kuamua kufyatua mambo, tunaweza. Japo fyatu huyu alikuwa na madhaifu yake, angalau alikuwa na uthubutu wa kifyatu.
Hivyo, badala ya kumchukia na kumshutumu Tarampu, tumshukuru kwa kutukumbusha kuwa mikono na vichwa vyetu si mapambo. Licha ya kutufundisha kwa masimango, Tarampu ameonyesha asivyo mnafiki wala muongo kama wengi waliomtangulia waliokuwa wakitumia misaada ya kuacha mafyatu wetu ughaibuni kama njia ya kutufyatua ili tuwe tegemezi na kufyatuliwa. Ametufundisha kufagia nyumba zetu ili tuwe wasafi japo kiuchumi.
Mnajua siri ya ughaibuni kutuzidi katika kila kitu? Simpo. Kila fyatu huku ni fyatu kweli kweli anayefyatuka na kufyatua bila kuruhusu kufyatuliwa na fyatu yoyote awe na madaraka au la. Huku, mfano, huwezi kufunga rodi kupisha walaji wengi wao wasiolipa kodi bali kuifyatua mbali na kaya kapuku kutoa misaada ukiachia mbali kuingia uwekezaji uliogeuka uchukuaji na ufyatuaji mali na njuluku za mafyatu.
Mwisho, kwa mafyatu walionusurika kufyatuliwa, popote mlipo, gomeni kutuma njuluku hadi mjue haki zenu home. Mfano, muwambie wanaotaka kufyatua au kutegemea njuluku zenu wajenge mazingira yaliyowezesha kaya kama pale kwa jirani kuingiza mabilioni ya dolari. Lazima mjue mna usalama gani mkiwekeza badala ya kufyatuliwa na hadhi sijui maalumu. Nimesemaje? Ngoja nikajifiche wasininyake wakanitia pingu na kunipakiza kwenye pipa bure!
Chanzo: Mwananchi leo.

Monday, 17 February 2025

Ndoa yako imejengwa kwa nguzo ngapi?

Ndoa inaweza kuwa nzuri au mbaya. Pia, ndoa inaweza kujengwa au kubomolewa. Wajenzi na wabomozi wa ndoa ni wanandoa. Ndoa, kama taasisi yoyote ina changamoto zake. Kuna kufanya makosa kwa sababu, kama binadamu wowote, wanafanya makosa. Pia, yanapofanyika makosa lazima kuwepo na suluhu na namna ya kufikia suluhu. Leo tutaongelea ulazima na umuhimu wa wanandoa kkuwa kama daraja au uwili usiotenganishwa wala kuyumbishwa. Daraja, huwa ima na nguzo mbili ingawa kutokana na kukua kwa teknolojia, kuna madaraja yana nguzo moja. Pamoja na kuwa na nguzo moja, madaraja yote huwa na sehemu kuu mbili yaani sehemu ya kuingilia na kutokea.

            Katika kufanya daraja kufaa, kuwa na nguvu, kuhimili mikiki, na kutumika, lazima nguzo mbili zisimame pamoja na kutegemeana ili kufanikisha umuhimu wa kuwapo daraja. Mfano, upande mmoja wa daraja lazima ujue na kukubaliana au kujenga mazingira wezeshi kwa upande wa pili na wa pili kadhalika kwa upande wa kwanza. Mfano, kama upande wa kuingilia utaruhusu magari au wavukaji wengi, upande wapili utashindwa na daraja litayumba au kushindwa kufanya kazi yake ya kuvusha watu na vitu.

            Udaraja katika ndoa unajengwa kwa njia mbalimbali zikiwemo:

Mosi, kukubaliana. Kila kinachoingia au kutoka lazima kipitie sehemu mbili na kubebwa na nguzo mbili au nguzo moja ambayo katika ndoa ni ushirika na wawili. Hapa lazima tukazie. Tunaongelea ndoa ya mke na mume mmoja. Kwa ndoa za mitala, udaraja unawezekana japo kwa taabu. Huko hatutaenda.

Katika dhana ya kulindana, lazima wawili wawe kama nyuki au siafu wanapojilinda au kulinda mzinga au shimo lau. Ukiangalia uhohehahe na utepetevu wa wadudu tajwa, utagundua kuwa bila kushirikiana na kuhamiana, si chochote si lolote. Na wanandoa kadhalika. Mkshikamana, kulilindana, na kuhamiana, wengine watawaogopa. Mkibomoana inakuwa rahisi maadui ambao ni wengi kumalizia. Katika kulindana, lazima kuwa kulihali. Mpendane, mheshimiane, mshirikiane, mhifadhiane, na kuaminiana. Mfano, mkianza kuitana viatu na majina mengine mabaya, wengine watawaita hata makanyagio. Kila kitu mnacho na mna uwezo kubomoa au kujenga, kusuka au kunyoa. Tutatoa visa viwili vinavyotuhusu. Cha kwanza, Nkwazi alitembelea rafiki yake mmoja aishie Kanada. Siku ya kwanza kufika tu, baba alimkaribisha Nkwazi kwa shangwe. Kitu kimoja kilitibua kila kitu. Jamaa alikuwa akimfokea mkewe mbele ya mgeni kama mtoto mtoto mdogo. Hata mtoto mdogo huwezi kumfokea na kumdhalilisha hivyo. Jambo hili lilimuudhi Nkwazi kiasi cha kumwambia mwenyeji wake kuwa asingerudi katika nyumba yake. Mwenyeji alishangaa na kustuka na kuuliza “kwanini.” Nkwazi alimjibu kuwa hakupenda anavyomdhalilisha mkewe hata mbele ya mgeni kitu ambacho kwa Waswahili ni dharau hata kwa mgeni. Jamaa aliahidi kujirekebisha na mambo yakaisha.

Cha pili, kabla ya Nesaa kuja Kanada, marafiki zake Nkwazi walizoea kuuliza ana mke wa aina gani. Aliwajibu kuwa madam huwa ni mtu wa kupenda amani. Ajabu ya maajabu, marafiki zake karibu wote, walianza kumuita Nesaa Madam jina ambalo lilimkaa hadi tunahama mkoa ule tulikofikia. Hata kwenye mapokezi yake uwanja wa ndege, marafiki walionyesha wazi heshima na aina fulani ya woga kulingana na Nkwazi alivyokuwa amemjenga Nesaa ambaye kiumri alikuwa mdogo kuliko marafiki wa Nkwazi.

Mafunzo

Kwanini rafiki wa Nkwazi aliyemkaripia mkewe mbele ya mgeni aliamua kuachana na tabia hiyo? Jibu ni rahisi kuwa mwenzake alimfundisha tabia ya kumjali na kumheshimu mkewe.

            Kwanini marafiki wa Nkwazi, kwa pamoja, walimuita Nesaa Madam kama ishara ya heshima? Ni kwa sababu Nkwazi alimjenga badala ya kumbomoa. Somo kubwa hapa ni kwamba mwanandoa anao uwezo wa kumjenga, kumbomoa, kumheshimisha au kumdharaulisha mwenzake.

Mwisho, kila mwanandoa anao uwezo huu. Hivyo, ili mheshimike, lazima mjiheshimu na kuheshimiana. Kufanya hivyo, lazima kuwa na tabia za haki, usawa, upendo kulindana, kuhamiana, na kutegemeana. Akitukanwa au kudharauliwa mwenzio, nawe kadhalika unatukanwa au kudharauliwa. Kadhalika, akiheshimiwa mwenzio nawe kadhalika unaheshimika. Hapa kuna faida bila hasara. Hivyo, wanandoa, wajue ni daraja lililojengwa na nguzo mbili yaani mke na mume.

Chanzo: Mwananchi Jpili jana.