Baada ya mafyatu wa upingaji kuanza kufyatuka, kufyatua, na kukinukisha, Chambo cha Maulaji (CcM) tumeamua kuanza kuwafyatua wapika kura ya kula kwa ajili ya uchakachuzi ujao. Tokana na wingi wao tumeanza kufyatua wakulimaji. Kuwafyatua ili mwakani wawe wamesahau kero zetu, tumeamua kuondoa tozos kuanzia talafa, wiraya, hata nkoa. Juzi mlimisikia waziwazi Husheni Bwashee akifyatuka mjengoni kuwa mambo sasa mmatana kwa wapigwaji wafyatuliwao na ngwamba wakizalisha ili tufyatue njuluku kupitia tozos.
Wasiojua tozos, it is simple. Tozos meaning tabuz on ze organisms and servants. Naona yule anadhani nimechapia asijue mie ni profesa emeritus mwenye shahada ya juu ya uchumi na utozaji tozo duniani niliyoipata toka kwenye chuo kikuu cha CcM Kivushani. We koma!
Uzuri wa mafyatu, huwa hawahoji kwanini tuone mwanga sasa kama kweli tumeuona na si kamba za kuwafyatua tufyatue kura za kula mwakani. Je hizi njuluku zilizokuwa zikifyatulilwa kila mwaka kwa miaka nenda rudi zitarejeshwa? Ni kiasi gani? waliozifyatua nao watafyatuliwa lau wakanyeeee debe? Je hiyo njuluku iliyokuwa ikipigwa toka kwa walimaji ilifyatuliwa au ilifanyiwa nini? Je watapata hakikisho gani kuwa baada ya uchakachuzi tozos hazitarejea kama kawa? Je wanaweza kuwachukulia hatua za kuwafyatua hawa waliowafyatua na kufyatua njuluku zao? Je wahusika wakuu walikuwa wapi?
Tuna bahati sana. Mafyatu wangeuliza hata nusu au robo ya maswali hayo hapo juu, mbona wangetufyatua. Tunashukuru. Hawaulizi kwanini hatukufuta tozos zote hadi ya kimataifa. Walitaka tule nini? Ngoja nizoze kichinichini mafyatu wasininyake nikawafyatua wakafyatuka na kutufyatua maswali ya kifyatu ambayo hata maprofedheha wetu chamani hawana uwezo kujibu mbali na kugomea kura. Anyway, kwa sababu sisi ngazi ya kimataifa lazima tufyatue, tumewatoa kafara hawa wadogowadogo hapo juu ili kuwafyatua mafyatu tufyatue kura za kula.
Mbali na kuondosha tozos ambazo tutazitoza kwa njia nyingine, tutaanzisha fuko la kulinda mafyatu wote kuanzia Januari ili Oktoba watupe kura tuwale baadaye kwa kurejesha upigaji kama kawa. Wapika gongo tutawaacha kwanza ili wapike kure tutajuana baadaye. Tutahakikisha hata anayetaka kwenda kununua gongo au lijisigara kubwa tunampiga tafu ili alainike atupe kura ya kula baadaye tumfyatue asiwe na la kufanya. Tutaangiza hata ndata wasiwanyake vibaka ili wasiwaudhi wakatunyima kura ya kula na kufyatua njuluku zao tukaendelea kunenepa na kuwa wanene.
Tangu sasa, tutaongea lugha za kusubsidize. Siyo kwa sababu tunataka kufanya hivyo bali kuvutia kura ya kula. Twenty twenty-six, kila kitu kitarejea kama kawa. Tutatoza na kutoza hadi kutozana. Chawa watarejeshewa mirija wanyonye. Kwa tulivyo na usongo wa kuendelea kufyatua ulaji, hata kama mawe yangekuwa yanapika kura ya kula tungeyapenda na kuyasikiliza ili yatuwezeshe kupiga juluku ya fatu vote na pata kula raha sisi vote janja ya kaya.
Baada ya ‘ku-subsidize,’ tutaanza hata kulialia mjengoni. Tutaondoa hata kikokotoo ili tukokotoe na kukomba kura halafu tukirejeshe baada ya kupata kura. Tuna mkakati wa kuhakikisha kila mwishiwa wetu njengoni analia, kugaragara, hata kutaka kujinyotoa au kunyotoa fyatu wanene wenzake roho kwa sababu ya kuwalove kuwadefend mafyatu. Huu sio wakati wa kuwatoza tozos au kuwaponda mafyatu kama tulivyozoea. Ili kufanikisha hili, hata chawa atakamuliwa damu lau mafyatu wasahau waachie. Huu ni wakati wa kuwaonyesha mapenzi mafyatu hadi wayafaidi na kulewaga. Kwenye CcM tuna mkakati wa kuhakikisha wale ambao hawaonyeshi usongo na sanaa kwa mafyatu hatutawapa tiketi ya kugombea ulaji mwakani.
Baada ya kuwalewesha mafyatu kwa ganzi na mapenzi fake ili waachie vitu, tutaanza hata kutoa mbolea bure ili mafyatu watoe kura kwa wingi. Tutawajaza mbolea ili waweze kuzalisha kura nyingi. Huwezi kutegemea kuzalisha sana bila kutumia mbolea. Hii tunayopanga kutoa si mbolea ya mimea tu bali ya kura za kula. Juzi mazeri kaamuru bei ya gasi ishuswe japo haikushushwa. Yote nini? Sisi wanene huwa hatuli vyakula kwanza. Tunakula kura ya kula kwanza. Huku ndiko kunaitwa kufyatua kisayansi kwa kupiga ganzi kila kitu. Hukumuona yule mwishiwa aliyetoa shangingi lake kwa bibi mmoja eti kuendea nyaraka na namna anavyotatua matatizo ya udongo papo kwa papo. Ngoja apite uishiwa uone atakavyoadimika kama nkojo wa kuku. Kwa sasa, waliwa na walaji wote wanafaidi usawa hadi zikishatoka kura za kula.
Usiseme tunawahonga kama wale. Hapana, tunawahongoa kama siyo kuwaongeza shime watupe kura ya kula tuwale kama chata twawala. Are you there? Kaa Chonjo Saa Mbaya!
Wasiojua tozos, it is simple. Tozos meaning tabuz on ze organisms and servants. Naona yule anadhani nimechapia asijue mie ni profesa emeritus mwenye shahada ya juu ya uchumi na utozaji tozo duniani niliyoipata toka kwenye chuo kikuu cha CcM Kivushani. We koma!
Uzuri wa mafyatu, huwa hawahoji kwanini tuone mwanga sasa kama kweli tumeuona na si kamba za kuwafyatua tufyatue kura za kula mwakani. Je hizi njuluku zilizokuwa zikifyatulilwa kila mwaka kwa miaka nenda rudi zitarejeshwa? Ni kiasi gani? waliozifyatua nao watafyatuliwa lau wakanyeeee debe? Je hiyo njuluku iliyokuwa ikipigwa toka kwa walimaji ilifyatuliwa au ilifanyiwa nini? Je watapata hakikisho gani kuwa baada ya uchakachuzi tozos hazitarejea kama kawa? Je wanaweza kuwachukulia hatua za kuwafyatua hawa waliowafyatua na kufyatua njuluku zao? Je wahusika wakuu walikuwa wapi?
Tuna bahati sana. Mafyatu wangeuliza hata nusu au robo ya maswali hayo hapo juu, mbona wangetufyatua. Tunashukuru. Hawaulizi kwanini hatukufuta tozos zote hadi ya kimataifa. Walitaka tule nini? Ngoja nizoze kichinichini mafyatu wasininyake nikawafyatua wakafyatuka na kutufyatua maswali ya kifyatu ambayo hata maprofedheha wetu chamani hawana uwezo kujibu mbali na kugomea kura. Anyway, kwa sababu sisi ngazi ya kimataifa lazima tufyatue, tumewatoa kafara hawa wadogowadogo hapo juu ili kuwafyatua mafyatu tufyatue kura za kula.
Mbali na kuondosha tozos ambazo tutazitoza kwa njia nyingine, tutaanzisha fuko la kulinda mafyatu wote kuanzia Januari ili Oktoba watupe kura tuwale baadaye kwa kurejesha upigaji kama kawa. Wapika gongo tutawaacha kwanza ili wapike kure tutajuana baadaye. Tutahakikisha hata anayetaka kwenda kununua gongo au lijisigara kubwa tunampiga tafu ili alainike atupe kura ya kula baadaye tumfyatue asiwe na la kufanya. Tutaangiza hata ndata wasiwanyake vibaka ili wasiwaudhi wakatunyima kura ya kula na kufyatua njuluku zao tukaendelea kunenepa na kuwa wanene.
Tangu sasa, tutaongea lugha za kusubsidize. Siyo kwa sababu tunataka kufanya hivyo bali kuvutia kura ya kula. Twenty twenty-six, kila kitu kitarejea kama kawa. Tutatoza na kutoza hadi kutozana. Chawa watarejeshewa mirija wanyonye. Kwa tulivyo na usongo wa kuendelea kufyatua ulaji, hata kama mawe yangekuwa yanapika kura ya kula tungeyapenda na kuyasikiliza ili yatuwezeshe kupiga juluku ya fatu vote na pata kula raha sisi vote janja ya kaya.
Baada ya ‘ku-subsidize,’ tutaanza hata kulialia mjengoni. Tutaondoa hata kikokotoo ili tukokotoe na kukomba kura halafu tukirejeshe baada ya kupata kura. Tuna mkakati wa kuhakikisha kila mwishiwa wetu njengoni analia, kugaragara, hata kutaka kujinyotoa au kunyotoa fyatu wanene wenzake roho kwa sababu ya kuwalove kuwadefend mafyatu. Huu sio wakati wa kuwatoza tozos au kuwaponda mafyatu kama tulivyozoea. Ili kufanikisha hili, hata chawa atakamuliwa damu lau mafyatu wasahau waachie. Huu ni wakati wa kuwaonyesha mapenzi mafyatu hadi wayafaidi na kulewaga. Kwenye CcM tuna mkakati wa kuhakikisha wale ambao hawaonyeshi usongo na sanaa kwa mafyatu hatutawapa tiketi ya kugombea ulaji mwakani.
Baada ya kuwalewesha mafyatu kwa ganzi na mapenzi fake ili waachie vitu, tutaanza hata kutoa mbolea bure ili mafyatu watoe kura kwa wingi. Tutawajaza mbolea ili waweze kuzalisha kura nyingi. Huwezi kutegemea kuzalisha sana bila kutumia mbolea. Hii tunayopanga kutoa si mbolea ya mimea tu bali ya kura za kula. Juzi mazeri kaamuru bei ya gasi ishuswe japo haikushushwa. Yote nini? Sisi wanene huwa hatuli vyakula kwanza. Tunakula kura ya kula kwanza. Huku ndiko kunaitwa kufyatua kisayansi kwa kupiga ganzi kila kitu. Hukumuona yule mwishiwa aliyetoa shangingi lake kwa bibi mmoja eti kuendea nyaraka na namna anavyotatua matatizo ya udongo papo kwa papo. Ngoja apite uishiwa uone atakavyoadimika kama nkojo wa kuku. Kwa sasa, waliwa na walaji wote wanafaidi usawa hadi zikishatoka kura za kula.
Usiseme tunawahonga kama wale. Hapana, tunawahongoa kama siyo kuwaongeza shime watupe kura ya kula tuwale kama chata twawala. Are you there? Kaa Chonjo Saa Mbaya!
Mwishiwa Bwashee Bashee alisema kuwa hata kuku wataacha kutozwatozwa tozo. Hivyo, wanaofyatua wanapaswa kupunguza kuwatoza tozos kwa kuwaibia mayai yao. Hata wachungaji tunashauri wapunguze kuwatoza tozo ng’ombe hadi tumalize uchakachuaji tuwakamue hata damu. Pia, wachunaji wapunguze kutoza sadaka na zaka. Wafugao chawa, lazima muwambie waache kutoza tozo za damu. Hapa lazima chawa na machawa wakonde kidogo lau tusiwastue wale wanaowafyatua kwa kuwakondesha, kuwaambukiza maradhi kiasi cha kustuka na kubania kura ya kula.
Chanzo: Mwananchi J'tano.
No comments:
Post a Comment