Mwaka jana, Mkaguaji mkubwa wa njuluku za sirkal aka KAGO alitoa taarifa ya kuchefua baada ya baadhi ya mafyatu kufyatua mafyatu wote waliokataa kufyatuka wakafyatua wapigaji wakaishia kuufyata. Alionya kuwa, kama ufyatuaji unaoendelea usipofyatuliwa, kaya nzima ima itaendelea kufyatuliwa kama inavyofyatuliwa na itakavyofatuliwa kiasi cha kufyatuka na kuanza kuwafyatua wanaoifyatua. Na hapa, itakuwa pata shika na shaka, nguo kuchanika.
Si ubishi wala uchawa kukiri kuwa mwaka ulofyatuka tulifyatuliwa na kuufyata bila kufyatuka. Njuluku zilifyatuliwa na maisha yakaendelea kuwafyatua mafyatu waliogoma kufyatua ima kutokana na ufyatu uchwara au kukosa ufyatu kabisa zaidi ya sifa za kipuuzi. Kazi na sifa ya mafyatu ni kama bomu au upinde. Lazima wafyatuke na kufyatua na si kujikomba na kusifia hata ukumbaff. Ila wasipofyatua wakafyatuliwa wanageuka bomu yaani kitu kisichofaa wala kufyatuka na si bomu linalofyatuka na kufyatua. Hata upinde, lazima ufyatuke. Usipofyatuka, hugeuka upondo.
Sasa turejee na kufyatua inshu ya KAGO na ufyatuaji wa njuluku za mafyatu uliofanywa na mafyatu waliopaswa kufyatuliwa wasifyatuliwe wakaishia kufyatua, bila mafyatu kufyatuka na kuwafyatua hawa mafyatu, watafyatuliwa tena tena hata mwaka huu. Mwaka jana tulifyatuliwa. Mwaka huu tushafutuliwa. Je tutakubali kuendelea kufyatuliwa na wanaotufyatua na kufyatua njuluku zetu au tutawafyatua kabla hawajatufyatua tukafyata na kufyatuliwa kama tulivyofyatuliwa bila kufyatuka bali kufyatuliwa kama tutakavyo fyatuliwa tusivyofyatuka na kufyatua kabla ya kufyatuliwa kwa vile hatufyatuki tukafyatuka? Naona. Hapa nimefyatua hadi mafyatu wanafyatuka kizungumkuti tokana na ufyatu na ufyatuzi wa fyatu mfyatuzi bingwa wa ufyatu na ufyatuzi asiyeufyata wala kufyatuliwa kama mafyatu waufyatao wakafyatuliwa na wale wawafyatuwao wanaopaswa kuwafyatuwa wasiwafyutue.
Pamoja na KAGO kufyatua ripoti ya ufyatuzi kayani mwaka jana, hadi unaisha, sikuona wala kusikia wafyatuaji wakifyatuliwa na wale wanaopaswa kuwafyatua ili kukomesha ufyatuaji wa njuluku za mafyatu fyata. Pia, kwenye salamu za kuukaribisha mwaka, sikusikia mikakati ya kuwafyatua wafyatuaji wa njuluku za mafyatu. Ajabu, pamona na mafyatua wapaswao kuwafyatua mafyatu wanaowafyatua mafyatu kuufyata, sikusikia mafyatu wakifyatuka na kudai hawa wanaowafyatua wafyatuliwe au wawafyatue hawa wanaopaswa kufyatua wawafyatuao wasio wafyatua!
Kwanini mafyatu wanaofyatuliwa hawakuwafyatua mafyatu wanaolipwa njuluku kuhakikisha wanasimamia njuluku za mafyata au kuwafyatua wanaowafyatua hizo njuluku wasiwafyatue? Mwaka jana, nilimsikia mwenyewe kwa masikio yangu mtukuka asiyefananishwa na muungu akisema "sababu dosari zilizotolewa hapa, tutakwenda kukaa tuzifanyie kazi, turekebishe na mwakani pengine hizi hazitajirudia, na tutakuwa tumesogea.” Ajabu ya maajabu, katika hutba yake ya kufunga mwaka uliofyatuka, sikumsikia akikumbushia namna atakavyowafyatua hawa wafyatuaji wa mafyatu waliogoma kufyatuka na kufyatua. Je ni kwanini hakufyatuka lau kiduchu juu ya namna atakavyowafyatua hawa mafyatu wafyatuaji wanaohitaji wafyatuzi ili wakome kufyatua njuluku za mafyatu walioamu kuufyata?
Mwaka jana, tulivyatuliwa matrilioni. Kama wanaopaswa kuwafyatua wanaofyatua mafyatu njuluku wasipowafyatua, sitashangaa KAGO kuja na ripoti kilio cha ufyatuzi wa madafu gizilioni kama siyo quadrilioni. Kwa vile hawa wafyatuaji hawakufyatuliwa na wale wanaopaswa kuwafyatua, sina shaka, watafyatua njuluku za mafyatu tena kama walivyozoea. Kwa kimakunduchi hii huitwa bizinesi ezi usual. Unafyatua hapa na kuhamishiwa pale ili uendelee kufyatua. Kinachoweza kukuzuia kufyatua hapa ni kifo tu. Kama kikufyatua, kila kitu ikiwemo ufyatuzi wa njulu za kaya vinaisha. Ajabu ya maajabu, hata ufyatue vipi, hakuna atakayeondoka na njuluku za mafyatu anazofyatua. Kwa maana nyingine, ni kama unajifyatua kufyatua visivyoweza kukusaidia bwana Godi akikufyatua.
Japo ukisema haya unaonekana chizi au zwazwa, fyatu ana nini juu ya uso wa ardhi? Ana nini kiumbe aliyekuja bure na kuondoka bure? Laiti mafyatu wengi wangejua ukweli huu, wasingedhulumiana, kuibiana, hata kuuana kwa ajili ya vitu wanavyovikuta na kuviacha hapa. Ukisema ni utaahira, mafyatu wengi wanakushangaa na kuchukia kuwa umewatukana wakati ukweli ni kwamba ni mataahira wasioona zaidi ya usawa wa matumbo na pua zao. Wangapi waliwika dunia hii tena kwa madaraka makubwa lakini walishafyatuka na kusahaulika kiasi cha mali na ushaufu wao kuviacha hapahapa hata wengine kuharibika? Nani hakumbuki fyatu jambazi kama Mobutu Nseleko wa Kongwa alivyojenga kwao kwenye kijiji cha porini cha Gabadolite? Ukiangalia kilichosaliwa baada ya kufyatua na kuunguza njuluku za mafyatu, unakubaliana nami kuwa wanaofyatua njuluku na mali za umma, wengine ni machizi watakaoacha kila kitu hapa wakiondoka watupu kama walivyokuja.
Wapo wapi akina Mafarao, Nabukadneza na mashaufu wengi uchwara waliojifyatua kwa kuwafyatua wenzao wakidhani hawatafyatuliwa? Tutankhamun, Farao aliyesifika sana, alikuwa na umri wa miaka chini ya 20. Sasa hawa wanaopiga njuluku za mafyatu na kuwafyatua wataishi milele? Unaweza kuacha mijengo mikubwa, akaunti nono, jua kufa ni kufa tu. Heri kuwaneemesha mafyatu kuliko kuwafyatua hadi inafikia mahali unashindwa kujua ni kwanini tumefyatuliwa, tutafyatuliwa,kama hatutachunga kufyatuliwa tena. Hivi niko wapi?
Si ubishi wala uchawa kukiri kuwa mwaka ulofyatuka tulifyatuliwa na kuufyata bila kufyatuka. Njuluku zilifyatuliwa na maisha yakaendelea kuwafyatua mafyatu waliogoma kufyatua ima kutokana na ufyatu uchwara au kukosa ufyatu kabisa zaidi ya sifa za kipuuzi. Kazi na sifa ya mafyatu ni kama bomu au upinde. Lazima wafyatuke na kufyatua na si kujikomba na kusifia hata ukumbaff. Ila wasipofyatua wakafyatuliwa wanageuka bomu yaani kitu kisichofaa wala kufyatuka na si bomu linalofyatuka na kufyatua. Hata upinde, lazima ufyatuke. Usipofyatuka, hugeuka upondo.
Sasa turejee na kufyatua inshu ya KAGO na ufyatuaji wa njuluku za mafyatu uliofanywa na mafyatu waliopaswa kufyatuliwa wasifyatuliwe wakaishia kufyatua, bila mafyatu kufyatuka na kuwafyatua hawa mafyatu, watafyatuliwa tena tena hata mwaka huu. Mwaka jana tulifyatuliwa. Mwaka huu tushafutuliwa. Je tutakubali kuendelea kufyatuliwa na wanaotufyatua na kufyatua njuluku zetu au tutawafyatua kabla hawajatufyatua tukafyata na kufyatuliwa kama tulivyofyatuliwa bila kufyatuka bali kufyatuliwa kama tutakavyo fyatuliwa tusivyofyatuka na kufyatua kabla ya kufyatuliwa kwa vile hatufyatuki tukafyatuka? Naona. Hapa nimefyatua hadi mafyatu wanafyatuka kizungumkuti tokana na ufyatu na ufyatuzi wa fyatu mfyatuzi bingwa wa ufyatu na ufyatuzi asiyeufyata wala kufyatuliwa kama mafyatu waufyatao wakafyatuliwa na wale wawafyatuwao wanaopaswa kuwafyatuwa wasiwafyutue.
Pamoja na KAGO kufyatua ripoti ya ufyatuzi kayani mwaka jana, hadi unaisha, sikuona wala kusikia wafyatuaji wakifyatuliwa na wale wanaopaswa kuwafyatua ili kukomesha ufyatuaji wa njuluku za mafyatu fyata. Pia, kwenye salamu za kuukaribisha mwaka, sikusikia mikakati ya kuwafyatua wafyatuaji wa njuluku za mafyatu. Ajabu, pamona na mafyatua wapaswao kuwafyatua mafyatu wanaowafyatua mafyatu kuufyata, sikusikia mafyatu wakifyatuka na kudai hawa wanaowafyatua wafyatuliwe au wawafyatue hawa wanaopaswa kufyatua wawafyatuao wasio wafyatua!
Kwanini mafyatu wanaofyatuliwa hawakuwafyatua mafyatu wanaolipwa njuluku kuhakikisha wanasimamia njuluku za mafyata au kuwafyatua wanaowafyatua hizo njuluku wasiwafyatue? Mwaka jana, nilimsikia mwenyewe kwa masikio yangu mtukuka asiyefananishwa na muungu akisema "sababu dosari zilizotolewa hapa, tutakwenda kukaa tuzifanyie kazi, turekebishe na mwakani pengine hizi hazitajirudia, na tutakuwa tumesogea.” Ajabu ya maajabu, katika hutba yake ya kufunga mwaka uliofyatuka, sikumsikia akikumbushia namna atakavyowafyatua hawa wafyatuaji wa mafyatu waliogoma kufyatuka na kufyatua. Je ni kwanini hakufyatuka lau kiduchu juu ya namna atakavyowafyatua hawa mafyatu wafyatuaji wanaohitaji wafyatuzi ili wakome kufyatua njuluku za mafyatu walioamu kuufyata?
Mwaka jana, tulivyatuliwa matrilioni. Kama wanaopaswa kuwafyatua wanaofyatua mafyatu njuluku wasipowafyatua, sitashangaa KAGO kuja na ripoti kilio cha ufyatuzi wa madafu gizilioni kama siyo quadrilioni. Kwa vile hawa wafyatuaji hawakufyatuliwa na wale wanaopaswa kuwafyatua, sina shaka, watafyatua njuluku za mafyatu tena kama walivyozoea. Kwa kimakunduchi hii huitwa bizinesi ezi usual. Unafyatua hapa na kuhamishiwa pale ili uendelee kufyatua. Kinachoweza kukuzuia kufyatua hapa ni kifo tu. Kama kikufyatua, kila kitu ikiwemo ufyatuzi wa njulu za kaya vinaisha. Ajabu ya maajabu, hata ufyatue vipi, hakuna atakayeondoka na njuluku za mafyatu anazofyatua. Kwa maana nyingine, ni kama unajifyatua kufyatua visivyoweza kukusaidia bwana Godi akikufyatua.
Japo ukisema haya unaonekana chizi au zwazwa, fyatu ana nini juu ya uso wa ardhi? Ana nini kiumbe aliyekuja bure na kuondoka bure? Laiti mafyatu wengi wangejua ukweli huu, wasingedhulumiana, kuibiana, hata kuuana kwa ajili ya vitu wanavyovikuta na kuviacha hapa. Ukisema ni utaahira, mafyatu wengi wanakushangaa na kuchukia kuwa umewatukana wakati ukweli ni kwamba ni mataahira wasioona zaidi ya usawa wa matumbo na pua zao. Wangapi waliwika dunia hii tena kwa madaraka makubwa lakini walishafyatuka na kusahaulika kiasi cha mali na ushaufu wao kuviacha hapahapa hata wengine kuharibika? Nani hakumbuki fyatu jambazi kama Mobutu Nseleko wa Kongwa alivyojenga kwao kwenye kijiji cha porini cha Gabadolite? Ukiangalia kilichosaliwa baada ya kufyatua na kuunguza njuluku za mafyatu, unakubaliana nami kuwa wanaofyatua njuluku na mali za umma, wengine ni machizi watakaoacha kila kitu hapa wakiondoka watupu kama walivyokuja.
Wapo wapi akina Mafarao, Nabukadneza na mashaufu wengi uchwara waliojifyatua kwa kuwafyatua wenzao wakidhani hawatafyatuliwa? Tutankhamun, Farao aliyesifika sana, alikuwa na umri wa miaka chini ya 20. Sasa hawa wanaopiga njuluku za mafyatu na kuwafyatua wataishi milele? Unaweza kuacha mijengo mikubwa, akaunti nono, jua kufa ni kufa tu. Heri kuwaneemesha mafyatu kuliko kuwafyatua hadi inafikia mahali unashindwa kujua ni kwanini tumefyatuliwa, tutafyatuliwa,kama hatutachunga kufyatuliwa tena. Hivi niko wapi?
Chanzo: Mwananchi, Machi 24, 2025.
No comments:
Post a Comment