The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Wednesday, 18 June 2025

Mnaringia ‘kiinglish’ are you British or Brutish!!


 Juzi nilishuhudia vita ya kikumbaff na kizwazwa ya mafyatu, au niseme uchangudoa wa kimaadili, ushamba wa kiakili, na ulimbuekeni wa kitabia. Si baada ya mafyatu wa haki za mafyatu kutoka kaya jirani kwenda kusikiliza mtiti wa fyatu mwenzao aliyetaka kukinukisha ili wote wanuke. Walizuiliwa kizembe na kuregeshwa makwao wengine wakiwa hai japo hoi. Kwa sababu wanadai walifanyiwa kitu mbaya bila hata kutoa ushahidi. 

                Acha mafyatu wafyatuane na kuvuana nguo hadharani tena mchana kutwa wakati wenye ngoma yao ni wanene. Badala ya kuwafyatua wanene waliowafyatua wenzao, waliingia ntego na kuanza kufyatuana wenyewe kwa wenyewe. Kwanini mnacheza ngoma ya wengine mkidhani yenu nyambaff wakubwa? Mitusi mizito mizito ilianza kurushwa toka upande zote. Watukufu walitukanwa hadi kikanukishwa kifyatu.

            Nani angeamini kuwa na waishiwa toka pande zote wangetia timu kwenye huu ukumbaff? Walipoteza hata muda wa buge kwa ubugeubuge kama huu! Ukiachia mitusi husika kuhuzunisha na kushangaza, hakuna kilichonishangaza hadi nikaamua kufyatua hili onyo na suto tena kwa Kiswahili japo nshafyatua kwa kiinglish wiki mbili zilizopita. Katika kujitahidi kubagazana na kubaguana, mafyatu wa upande wa pili walishikilia uzwazwa mmoja. 

                Kila wakirusha mikombora ya mitusi, utasikia “nyinyi hamujui kiingeredha.” Kwanza, inshu ilikuwa ni nani anakimanya kibritish au kufyatuliwa haki za binadamu za mafyatu kama kuwekwa tunduni na kupiga persona non grata? Je hii ni nini? Rudi darasani ukasome. Kwa tuliowahi kuishi Kenya, wanaowatuhumu wenzao kutokijua kimombo aka kithungu au kithunguri, wao ndiyo usiseme. Hawakijui wala Kiswahili.

  Hapa naongea na akina Kariuki wa Muriuki au mfufuka aka Karish, Njoroge aka Njoro, Shiko, Waruguru, Khalwale, Awori, Sifuna, Wanyonyi, Ocholla, Omoro, Amoro, Maboi, na wengine wengi. Mwenzenu niliishi maeneo ya Valley Arcade kule Lavington kwa wanene. Hivyo, nawajua kuliko hata mnavyowajua wabongo wenzangu.

            Namaanisha akina Onyango Oburu wajiitao Mc Onyango. Hata mujiite Mac Donald bado ni manugu tu. Wengine wanajiita Doug badala ya Douglas. Si mujiite dog au mbwa ijulikane kama siyo ngui. Kwani nyinyi ni waingereza? Wathunguri au wadhungu wakiwadharau mnalaumu. Basi, badilisheni rangi muwe hao wathunguri. 

                Mbona kama ni kiingirish ni mali mbona mwapeleka vitegemezi vyenu kwa Bro M7 na kitegemezi chake the Avenger aka Muhoooooziiii kohooziiiii ziii? Sijui kama na waiingilish wanajivunia Kijaluo, Kikikuyu hata Kikamba ya kana ka mkamba wa Kaneza, Wamuseto na Wakaiti. Eti Wabongo hawajui Kiingereza. Kwani, nyinyi ni wabritish. Kama watawaona kama manyani, mtaanza kulalamika eti mnabaguliwa? Kumbe mfalme Charles ana koloni ambalo amelisahau la Black Brits. Great minds speak bout ideas, avarage minds discuss events, and small minds discuss people.

            Tokana na mitusi hiyo hapo juu, sijui uhuru wenu unamaanisha nini hadi mnajisifia kibritish wakati Wainglish wanawaona nyinyi ni brutish tuu tena weusi wanaobaguliwa na hao mabritish mnaowaramba makalio? Mbona hamli vyakula vya kibritish bali kathubu kanini, kamceri, makande, mutula, mukimo, madodo na kadhalika? Kabla ya kusema Wabongo hawajui kimombo, nenda kawasilikize akina Mvaithe. Utasikia fyatu akisema, nthis is nthe mbrother from my nconsitituency.  Ukija kwa akina Njoro, utasikia this is mokey business au idepedece yaani uhuru. Shame on you! It is time to stop self-dressing down now.

Acheni jamani. Wenye akili wanawacheka mnavyopwakia na kujivunia lugha za watu.

            Nilisikia wakidai kuwa Bongo bila Kenya haiwezi kuishi na pia ni maskini wakati ukweli ni tofauti. Mnamaanisha Kenya na Bongo ipi? Mnadhani hao waTZ hawawajui uzuri siyo? Mmenoeni tena sana. Wajua muishivyo kwa shida mazee. Nenda Kibera halafu urudi bongo ulinganishe na sehemu yoyote Uswekani. Wengi huwa tunasema eti Manzese ni uswekeni. Jamanini, nendeni Kawangware au ngwaro, Kibera aka kibra,  Mukuru kwa Njenga (wao husema Jenga), Kiandutu (cha funza), Korogocho, Muthurwa, nk. Msipigwe chenga la mato. Nendeni muone halafu mjue mnatukanwa na mafyatu gani.

                 Uliona wapi Bongo fyatu anapanga nyumba bila choo huku akiambiwa choo siyo sehemu ya nyumba? Je huwa wanafanyaje? Jikumbushe kipindi fulani pale jamaa zetu toka kule gabacho..rii walivyoanza kutumia kitu ambacho kwa wenzetu hujulikana kama flying toilets. Fyatu zima sijui na mke na watoi linajisikia kwenda kutua mzigo, linafungua mfuko wa plastiki na kumalizia mambo humo na kurusha mtaani. Hawa ndiyo wabrutish wetu wanaokimanya kibritish japo siyo wote.

            Sasa jiulize nani kapuku. Mwaka 2023, hao wajivuni walituuzia bidhaa zisozidi dolari milioni 14 wakati sisi tukiwauzia bidhaa zenye thamani ya dolari miloni 178 nyingi zikiwa vyakula wakati wao walituuzia bidhaa za viwandani. Ukienda mbele, wanachoringia kutuzidi GDP, utakuta mali nyingi inamilikiwa na watasha na magabacholi.

             Japo nasi tuna tatizo hilo, tunawazidi kitu kimoja. Hatuna wapangaji vijijini kama hawa jamaa ambao huishi kwenye reserves kama waanimo tena kwenye nyumba za mabati kama magari. Nyani angeona nonihino lake, bila shaka, asingewacheka wenzake. Ni ajabu nyani kumcheka mbuzi ambaye nonihino lake limefunikwa na mkia japo wote ni waanimo. Du! Hii mibangi!

Chanzo: Mwananchi leo.

No comments: