Kuna baadhi ya wanandoa wenye tabia hatarishi, za hovyo na kinyonyaji kwa wenzao hata wao wenyewe. Hii yaweza kuwa jambo ambalo ni la kupanga au hata kutokea tokana na mazoea au ujinga wa aina fulani kama siyo ubinafsi na upofu. Kwa muktadha huu, si jambo geni kusikia kuwa mwanandoa, hasa akina mama, japo si wote, wakiwashinikiza waume zao kuwajengea wazazi wa wao nyumba, kusomesha ndugu zao, na mengine kama haya. Kwa lugha za mitaani hii ni ima chuma ulete au kuchuna buzi. Mambo haya yapo, na kuna baadhi ya makabila nyonyaji na wavivu wameyazoea kiasi cha kugeuza mabinti zao vitega uchumi.
Utawasikia wazazi wakimuulizwa binti wao kazi au vyeo vya mtarajiwa wake. Wengine hujisifu kuwa mabinti zao wameolewa na watu matajiri au wakubwa kana kwamba wao nao ni wakubwa au matajiri. Hii ni aina fulani ua umaskini wa kijamii na kiuchumi ambapo utu wa mja huzidiwa thamani na vitu fedha na mali. Wengine huwambia kabisa kuwa wanataka binti awaletee mchumba wa aina fulani kana kwamba wao ndiyo wanaoolewa. Japo ni haki ya wazazi kutunzwa na watoto wao, wazazi wa aina hii ni vibaka au wezi wa kawaida wanaotumia mabinti zao kwa kuwageuza watumwa wa vitu bila kujali madhara yake.
Kama wanandoa mna uwezo iwe wa kifedha au utashi, si jambo baya kuwajengea wazazi wa pande zote mbili kama hawakubahatika kujijengea. Pia, si vibaya kusomesha wadogo zenu na mengine kama hayo kama yatafanyika kwa faida ya pande zote. Hata hivyo, mfanye tokana na mapenzi na uwezo wenu na si mashinikizo toka kwa wazazi au wenzi wenu.
Muhimu, mnapofanya haya mambo ambayo yaweza kuwa majukumu yenu, msibague au kupendelea au kuutenga upande mmoja. Ajabu, hao wanaotaka wafanyiwe yote hayo, hawakuwafanyia wakwe zao! Hapo ndipo dhana ya jinai ya unyonyaji, uvivu, na wizi inapojengeka. Hata hivyo, hiki kinapaswa kuwa kipaumbele namba moja, yaani kuwajengea wao kabla ya kujijengea au kuwasomeshea watoto wao?
Tuanzie hapa. Kwanza, tunajua. Wapo wazazi, hasa wenye uwezo, wanaowajengea watoto wao nyumba na kuwapa mali mbali mbali. Pia, wapo wanaowapa vyeo tokana na nafasi walizoshika. Hapa, tunaongelea wale ambao wana uwezo wa kawaida, yaani wanaoanza maisha. Je ni haki kuwajengea wazazi wenu hasa wa mke kabla ya kuwa na nyumba yenu wenyewe? Je, ni halali na sahihi kwa mmoja wenu kuweka kipaumbele upande mmoja huku akiuacha upande mwingine?
Pili, kabla ya kutoa jibu au majibu, tuulize maswali tena. Kabla ya kuwajengea wazazi wenu, jiulizeni. Je wao waliwajengea mababu zenu? Kama jibu ni hapana, kwanini? Kama jibu ni ndiyo, je, walifanya hivyo kibaguzi na kwa shinikizo tena la upande mmoja? Kama kipaumbele cha mmoja wenu ni kuwajengea wazazi wake, jiulize. Kwako utajenga lini? Kwanini uanze na kwenu badala ya kwako? Je na mumeo akiamua kujenga kwao, nawe kwa wazazi wako, kwenu mtajenga lini? Je, kwako, ndoa ni kitega Uchumi au mfumo wa maisha tena ya kudumu baina ya watu wawili na jamii zao? Je hakuna namna ya kuwasaidia wazazi wenu bila ya kubaguana, kujiumiza, kuhujumiana, na kutumiana? Hivi, hali kama hii inapotokea, nani waathirika nan ani wanafaa kuwa wanufaika? Wakati mama ukimshinikiza mumeo awajengee nyumba wazazi wako au kuwasomesha wadogo zako, jiulize, hayo yangefanywa na wifi yako kwa wazazi wako ua mkamwana wako kwako, ungejisikiaje na kufanya nini? Hili ni suala na swali muhimu. Kulijibu uzuri, epuka dhana na imani ya mkuki kwa nguruwe. Wahanga wa jinai hii waweza kuonekana kama nguruwe wanaopaswa kupata mkuki bila kujua hawa wanaowachoma hii mikuki wanaweza kuwa nguruwe wa kesho.
Hivi, inawezekana kuishi sehemu mbili au kutumia mabwana wawili kwa wakati mmoja? Je wanapoamua kuanzisha hujuma hii, huwa wahusika wanajiuliza kama wanaotaka kuwahujumu nao wana akili timamu hata kubwa kuliko zao? Jengeni kwenu kwanza kabla ya kwa wengine. Huu ni usia wa leo.
Utawasikia wazazi wakimuulizwa binti wao kazi au vyeo vya mtarajiwa wake. Wengine hujisifu kuwa mabinti zao wameolewa na watu matajiri au wakubwa kana kwamba wao nao ni wakubwa au matajiri. Hii ni aina fulani ua umaskini wa kijamii na kiuchumi ambapo utu wa mja huzidiwa thamani na vitu fedha na mali. Wengine huwambia kabisa kuwa wanataka binti awaletee mchumba wa aina fulani kana kwamba wao ndiyo wanaoolewa. Japo ni haki ya wazazi kutunzwa na watoto wao, wazazi wa aina hii ni vibaka au wezi wa kawaida wanaotumia mabinti zao kwa kuwageuza watumwa wa vitu bila kujali madhara yake.
Kama wanandoa mna uwezo iwe wa kifedha au utashi, si jambo baya kuwajengea wazazi wa pande zote mbili kama hawakubahatika kujijengea. Pia, si vibaya kusomesha wadogo zenu na mengine kama hayo kama yatafanyika kwa faida ya pande zote. Hata hivyo, mfanye tokana na mapenzi na uwezo wenu na si mashinikizo toka kwa wazazi au wenzi wenu.
Muhimu, mnapofanya haya mambo ambayo yaweza kuwa majukumu yenu, msibague au kupendelea au kuutenga upande mmoja. Ajabu, hao wanaotaka wafanyiwe yote hayo, hawakuwafanyia wakwe zao! Hapo ndipo dhana ya jinai ya unyonyaji, uvivu, na wizi inapojengeka. Hata hivyo, hiki kinapaswa kuwa kipaumbele namba moja, yaani kuwajengea wao kabla ya kujijengea au kuwasomeshea watoto wao?
Tuanzie hapa. Kwanza, tunajua. Wapo wazazi, hasa wenye uwezo, wanaowajengea watoto wao nyumba na kuwapa mali mbali mbali. Pia, wapo wanaowapa vyeo tokana na nafasi walizoshika. Hapa, tunaongelea wale ambao wana uwezo wa kawaida, yaani wanaoanza maisha. Je ni haki kuwajengea wazazi wenu hasa wa mke kabla ya kuwa na nyumba yenu wenyewe? Je, ni halali na sahihi kwa mmoja wenu kuweka kipaumbele upande mmoja huku akiuacha upande mwingine?
Pili, kabla ya kutoa jibu au majibu, tuulize maswali tena. Kabla ya kuwajengea wazazi wenu, jiulizeni. Je wao waliwajengea mababu zenu? Kama jibu ni hapana, kwanini? Kama jibu ni ndiyo, je, walifanya hivyo kibaguzi na kwa shinikizo tena la upande mmoja? Kama kipaumbele cha mmoja wenu ni kuwajengea wazazi wake, jiulize. Kwako utajenga lini? Kwanini uanze na kwenu badala ya kwako? Je na mumeo akiamua kujenga kwao, nawe kwa wazazi wako, kwenu mtajenga lini? Je, kwako, ndoa ni kitega Uchumi au mfumo wa maisha tena ya kudumu baina ya watu wawili na jamii zao? Je hakuna namna ya kuwasaidia wazazi wenu bila ya kubaguana, kujiumiza, kuhujumiana, na kutumiana? Hivi, hali kama hii inapotokea, nani waathirika nan ani wanafaa kuwa wanufaika? Wakati mama ukimshinikiza mumeo awajengee nyumba wazazi wako au kuwasomesha wadogo zako, jiulize, hayo yangefanywa na wifi yako kwa wazazi wako ua mkamwana wako kwako, ungejisikiaje na kufanya nini? Hili ni suala na swali muhimu. Kulijibu uzuri, epuka dhana na imani ya mkuki kwa nguruwe. Wahanga wa jinai hii waweza kuonekana kama nguruwe wanaopaswa kupata mkuki bila kujua hawa wanaowachoma hii mikuki wanaweza kuwa nguruwe wa kesho.
Hivi, inawezekana kuishi sehemu mbili au kutumia mabwana wawili kwa wakati mmoja? Je wanapoamua kuanzisha hujuma hii, huwa wahusika wanajiuliza kama wanaotaka kuwahujumu nao wana akili timamu hata kubwa kuliko zao? Jengeni kwenu kwanza kabla ya kwa wengine. Huu ni usia wa leo.
Chanzo: Jpili iliyopita.
No comments:
Post a Comment