The Chant of Savant

Friday 22 June 2018

Picha ya wiki


Za zile wakiwa huru, watuhumiwa hawa wa ufisadi wa IPTL, Habinder Singh na James Rugemalira walikuwa watu wa kutisha na kuogopewa ukiacha mbali kupendwa kwa mishiko yao ya wiz. Walinawiri kweli kweli wakivaa mavazi nadhifu na kuficha uzee wao. Tangu utawala wa awamu ya tano uwatolee uvivu, unaweza ukaona kuwa mshahara wa ufisadi ni nini. Waliokuwa wakionekana kama miamba isiyoguswa na tawala zote zilizopita ukiondoa ule wa mwalimu Nyerere sasa ni mbendembende. Ama kweli duniani hujafa hujaumbika!

No comments: