Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Sunday 2 June 2024

Waishiwa Wasiwe Madoktari au Wabukuzi

Kaya yetu si ya watata wala aihitaji utata,  kuringa, na kuringishiana ujuha. Ni kaya ya mafyatu. Hii inatosha. Siku hizi, kila fyatu anataka aitwe ima doktari au profedheha hata kama hajui kusoma na kuandika ilmradi tu ujiko na kujimwambafy. Hawajui wanavyotusononesha sie tusiobahatika kuwa madoktari wala maprofedheha ingawa ukiwauliza wamefanya nini cha mno, wote ngoma droo. Leo nitafyatua hii tabia hatari katika kutawala. Nitadurusu tabia chafu ya kuringa, kuringishiana, na kutishiana usalama na ulaji kayani na njengoni.
            Pili, ukiwa na waishiwa wasomi, watahoji upigaji wa wanene kiasi cha kuwanyima raha na kuwatia presha wakidai wagawane vinginevyo hakieleweki. Kama chawa wanashibishwa, kwanini wao wasishibishwe?
            Tatu, ukiwa na watawala wabukuzi watabukua kila kitu tofauti na mbumbumbu watakaobungabunga kila kitu na mambo yakaenda.  Haiwezekani wanene wasomeshe vitegemezi vyao ughaibuni halafu waje kushindana na wabukuzi mjengoni au kwenye sirkal. Ili kaya iendelee, tunahitaji mabingwa wa kusema ndiyo,kusifu na kupongeza bila kusahau kuimba mapambio. Haiwezekani maza awe doktari halafu mruhusu madoktari wengine kuja kushindana naye. Doktari anapaswa kuwa mmoja tu kayani.
            Ili kunogesha mambo, tokana na kasheshe, vimbwanga, na vituko nionavyo njengoni, napendekeza sifa mojawapo ya kuwa muishiwa iwe ni kuwa bingwa wa kupiga kanywaji na mmea ili akienda huko vimbwanga, vimbweka, na vituko viongezeke kuwaburudisha mafyatu wasifyatuke wakawafyatua.
            Nne, kushusha viwango vya elimu vitafanya tuzalishe wanene wengi na kugeuka kaya ya wanene tuondolewe kwenye orodha ya kaya kapuku. Tukiondoa ulazima wa kula mabuku, tutaondoa ulalamishi wa waliobukua wakakosa ajira. Wabukuzi ni walalamishi utadhani warugu, wee koma. Si mnamuona Mwambukuzi anavyolalamika? Angekuwa hajabukuwa taabu ingekuwa wapi? Wabukuzi hawafai. Kwanza, si woga. Pili, ni mafyatu wanaoweza  hata kuhoji uraia wa rahis na mgongano wetu mtukutu, sorry, mtukufu.
            Tano, tutaondoa presha na mikikimikiki ya kughushi, kuficha, au kuumbuliwa siri zinapofichuka. Hii inawapa taabu sana mafyatu wetu kiasi cha wengine kufyatuliwa na ugonjwa wa presha ya moyo. Nani anataka kupoteza mafyatu wake wanaowanenepesha wanene kwa kulipa kodi na tozos? Tukiondoa ulazima wa kuwa na shahada za vyoo, sorry jalala, sorry, vyuo vikuu, tutakuwa tumeondoa na kishawishi cha kughushi, urongo, na kujimbwafy na kuwakoga mafyatu mbali na kuokoa njuluku zinazopoteza kuzalisha modktari ambao kazi yao ni kuongea mineno migumu na mambo ya kufikilika na kutufanya tuchukie kutazama kipindi cha runinga njengoni.
            Sita, wabukuzi wanajidai sana. Wanaongea kiswanglish kigumu kiasi cha mafyatu kutonyaka wasemacho njengoni. Wanatunga sharia mbovu, sorry, ngumu kwa mafyatu na zinazowahudumia na kuwalinda wao. Juzi, kuna aliyeniudhi nusu nipige teke runinga yetu. Alisema eti yeye ni doktari wa Philo na Sofia! Yaani, bila aibu unatwambia kuwa una nyumba ndogo? Kama unawatibu hao akina Philo na Sofia wako, sisi inatuhusu au kutusaidia nini? Mwingine naye aliniacha hoi alipodai eti yeye ana bachela sijui ya madudu gani. Yaani, umri wote huo bado wewe ni bachela tu? Mwingine naye eti ana masta. Hivi masta kwa kisambaa siyo bwana? Nani anataka ubwana njengoni?
Kwa kuangalia wale wajimwabafaio kuwa ni madoktari wa Philo na Sofia, nagundua kuwa kaya inawapa njuluku ndefu bila sababu kiasi cha kuwa na nyumba ndogo. Bila hivyo, nani angesomea kuwatibu akina Philo na Sofia? Kesho, tutawasikia wengine wakijidai wao ni madoktari wa Halima na Husna. Mwingine eti doktari wa akina mama! Wako wapi wa akina baba? Tunataka wabukuzi madoktari wa Mafyatu siyo vimwana jamanini. Hii maana yake ni kwamba tupunguze mishiko na marupurupu ya waishiwa ili waonje tunavyofyatuliwa na dhiki zitokanazo na unene na vimbwanga njengoni.
            Saba, tukiwa na waishiwa darasa la saba au ngumbaru tutakuza lugha ya kaya na kuweza kuwasiliana na mafyatu kirahisi. Tutaua lugha za kikoloni zinazozidi kuua waishiwa wetu. Hamjawaona wakibukanya kiswanglish wanavyotoka jasho kiasi cha kupandisha presha ya shinikizo la moyo?
            Nane, tutapunguza idadi ya waishiwa wanaouchapa njengoni tokana na kuboreka kwa kiswanglish na mineno mingine migumu inayowatia usingizi hadi wanauchapa njengoni. Juzi kuna doktari mmoja alikuwa akiwasilisha na kujisifu sijui yeye alimaliza udoktari wake na extinction ya akili yake asifikaye kwa upigaji na kujidai hata kwenye uzwazwa. Kitegemezi changu si kiliniuliza nini maana ya extinction. Bila kujivunga nilikiambia kuwa yule jamaa alikuwa bingwa wa kuzima moto chooni, sorry, chuoni. Vitegemezi vya siku hizi vijanja kama simu janja. Kesho yake si kilikwenda kikamuuliza ticha wake akaniumbua bila kujua!
            Chonde chonde, njengo ujao, tuhakikishe tunachagua ngumbaru na kuachana na madoktari wa akina Philo, Sofia. Nimesemaje  eti nami ni doktari?
Kwanza, elimu yetu yenyewe Iko Chumba cha Umauti (ICCU). Hivyo, hatutaki waishiwa wabukuzi kama Mwambukuzi. Wataleta ubukuzi na kuzuia panyabuku kubukua wabukuavyo.
Chanzo: Mwananchi j'tano iliyopita.


No comments: