Wengi tunaamini walishasikia mengi kuhusiana na wanawake wa Kitanga. Tunaposema wanawake wa Kitanga, lazima tukiri kuwa Tanga ina makabila mengi tena tofauti. Hivyo, hatuwezi kusema kwa kujiamini kuwa wanawake wote wa Kitanga wana sifa au tabia zinazofanana au kujumlishwa pamoja. Hata hivyo, tutafuata mjumlisho juu ya wanawake wa Kitanga ili tujibu swali jumla litokanalo na mjumlisho huu.
Leo, tutaongelea wanawake wa kitanga japo si wote. Wasiowajua vizuri na ufundi wao katika mapenzi, hudhani kuwa wanatumia limbwata au dawa ya mapenzi. Hakuna kitu kama hiki. Wanawake wa Kitanga wanasifika kwa uchangamfu, ukarimu, na ufundi wao katika masuala ya mapenzi na ndoa japo si wote.
Mfano, utasikia watu wakisema kuwa kuingia Tanga ni rahisi na kutoka ni vigumu. Je, ni kwanini? Hatuwezi kutoa jibu moja kwa moja au moja tu. Hatujui chanzo cha imani au msemo huu. Hivyo, ngoja tudurusu na kudadavua kidogo kuhusiana na wanawake hawa wa ambao wanasemekana kuwa wanaweza kumuandalia maji ya kuoga mwanamme na kuyachanganya na malashi ili akishaoga anukie vizuri. Je, hili si jambo zuri? Ni wapi tena hufanyika katika nchi yetu? Nani hawezi kuvutiwa na hili? Hebu jifikirie. Mume ni mvuvi. Anarejea zake nyumbani na shombo. Wewe kama mke utamfanyiani ili awezenukia uzuri? Au mme ni mkulima tena Msukuma au Muha. Anarejea nyumbani baada ya kupiga jembe kwa masaa saba na jasho. Utamsaidiaje?
Wengine wanakwenda mbali na kudai, japo hatuna ushahidi kuwa wanawake wa Kitanga wanaweza hata kumbeba mume mgongoni kama mtoto! Lahaula lakuata! Nani hawezi kuvutiwa na ukarimu huu?
Nani anaweza kuchukia kitu hii? Je, hili nalo ni limbwata au usafi? Hamjawahi kusikia kuwa mwanamke ni usafi? Kama ni limbwata, basi kwenye ndoa, linaswihi sana tu. Japo usafi unapaswa kuwa ni suala binafis la wanandoa wote, bado wapo wanandoa wanaosumbuka katika ndoa zao hasa akina mama tokana na kutozingatia suala la usafi wa miili na ndimi zao. Japo usafi ni suala binafsi, kwa wanaotaka kuepuka madhara yake, si chaguo bali wajibu.
Huwezi, kwa mfano, ukaingia kitandani ukiwa mchafu na unatoa harufu mbaya mambo yakaenda. Japo laweza kuonekana jambo geni, kwani, haya hayapo? Je, ni wangapi wanawaambia wenzao kuwa ni wachafu na hivyo wajisafishe? Msioneane aibu. Ambianeni ukweli. Wapo wasiopenda kukosoana kwa maneno bali mwa matendo. Ni heri kulaumiana kwa kuambiana ukweli iwe kwa maneno au matendo kuliko kukwazana, kuogopana, au kutofautiana hata kufarakana kwa kitu kidogo japo muhimu kama usafi. Hapa, mchague kunyamaziana na kuumizana au kukerana mkilinganisha na kuambiana na mkatatua tatizo pamoja.
Kuna baadhi ya jamii ambazo huwa hawapigi mswaki wakati wa kwenda kulala. Mtu anashinda anakula. Halafu anaingia kitandani bila kupiga mswaki. Wengine hata hawaogi wala kujitawaza. Jamani, binadamu si mnyama alale na kuamka mchafu. Hata kuku akikaribia kwenda kulala huoga kwa michanga lau alale msafi.
Tukizingatia hayo juu na kuyahusisha na sifa za wanawake wa Kitanga, huenda tunaweza kupata maana hata bila kuwahoji. Mbali na usafi. Kuna methali moja kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume ni kupitia tumboni. Mwake. Hapa, ndipo umuhimu na ustadi wa mapishi unapoingia. Jieulize ni wanawake wangapi wanajua mapishi ya kumfanya hata mtu achukie hoteli.
Anayebishia au kupinga hili ajiulize. Kwanini biashara ya mahoteli ni moja ya biashara kubwa ulimwenguni. Ni kwa sababu binadamu wote hupenda chakula kizuri. Huwezi kupiga michemsho kila siku ukashindana na bingwa wa kuaangiza. Wapo watu matajiri wasiokula vyakula vizuri si kwa sababu hawana uwezo bali wahusika hawana ujuzi wa mapishi. Pia, wapo maskini wanaokula vizuri tu kwa sababu ya ufundi wa jikoni. Kimsingi, hakuna chakula kibaya wala kizuri. Kinachoweza kukifanya kiwe hivyo ua kisiwe ni mapishi tu.
Mambo ya chumba cha kulala hatugusi. Hata hivyo, kama ilivyo kwenye mambo mengine hapo juu, nako huko kwahitaji juhudi, maandalizi, na ufundi si haba. Leo, tunaishia hapa.
Chanzo: Mwananchi J'pili juzi.
Mfano, utasikia watu wakisema kuwa kuingia Tanga ni rahisi na kutoka ni vigumu. Je, ni kwanini? Hatuwezi kutoa jibu moja kwa moja au moja tu. Hatujui chanzo cha imani au msemo huu. Hivyo, ngoja tudurusu na kudadavua kidogo kuhusiana na wanawake hawa wa ambao wanasemekana kuwa wanaweza kumuandalia maji ya kuoga mwanamme na kuyachanganya na malashi ili akishaoga anukie vizuri. Je, hili si jambo zuri? Ni wapi tena hufanyika katika nchi yetu? Nani hawezi kuvutiwa na hili? Hebu jifikirie. Mume ni mvuvi. Anarejea zake nyumbani na shombo. Wewe kama mke utamfanyiani ili awezenukia uzuri? Au mme ni mkulima tena Msukuma au Muha. Anarejea nyumbani baada ya kupiga jembe kwa masaa saba na jasho. Utamsaidiaje?
Wengine wanakwenda mbali na kudai, japo hatuna ushahidi kuwa wanawake wa Kitanga wanaweza hata kumbeba mume mgongoni kama mtoto! Lahaula lakuata! Nani hawezi kuvutiwa na ukarimu huu?
Nani anaweza kuchukia kitu hii? Je, hili nalo ni limbwata au usafi? Hamjawahi kusikia kuwa mwanamke ni usafi? Kama ni limbwata, basi kwenye ndoa, linaswihi sana tu. Japo usafi unapaswa kuwa ni suala binafis la wanandoa wote, bado wapo wanandoa wanaosumbuka katika ndoa zao hasa akina mama tokana na kutozingatia suala la usafi wa miili na ndimi zao. Japo usafi ni suala binafsi, kwa wanaotaka kuepuka madhara yake, si chaguo bali wajibu.
Huwezi, kwa mfano, ukaingia kitandani ukiwa mchafu na unatoa harufu mbaya mambo yakaenda. Japo laweza kuonekana jambo geni, kwani, haya hayapo? Je, ni wangapi wanawaambia wenzao kuwa ni wachafu na hivyo wajisafishe? Msioneane aibu. Ambianeni ukweli. Wapo wasiopenda kukosoana kwa maneno bali mwa matendo. Ni heri kulaumiana kwa kuambiana ukweli iwe kwa maneno au matendo kuliko kukwazana, kuogopana, au kutofautiana hata kufarakana kwa kitu kidogo japo muhimu kama usafi. Hapa, mchague kunyamaziana na kuumizana au kukerana mkilinganisha na kuambiana na mkatatua tatizo pamoja.
Kuna baadhi ya jamii ambazo huwa hawapigi mswaki wakati wa kwenda kulala. Mtu anashinda anakula. Halafu anaingia kitandani bila kupiga mswaki. Wengine hata hawaogi wala kujitawaza. Jamani, binadamu si mnyama alale na kuamka mchafu. Hata kuku akikaribia kwenda kulala huoga kwa michanga lau alale msafi.
Tukizingatia hayo juu na kuyahusisha na sifa za wanawake wa Kitanga, huenda tunaweza kupata maana hata bila kuwahoji. Mbali na usafi. Kuna methali moja kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume ni kupitia tumboni. Mwake. Hapa, ndipo umuhimu na ustadi wa mapishi unapoingia. Jieulize ni wanawake wangapi wanajua mapishi ya kumfanya hata mtu achukie hoteli.
Anayebishia au kupinga hili ajiulize. Kwanini biashara ya mahoteli ni moja ya biashara kubwa ulimwenguni. Ni kwa sababu binadamu wote hupenda chakula kizuri. Huwezi kupiga michemsho kila siku ukashindana na bingwa wa kuaangiza. Wapo watu matajiri wasiokula vyakula vizuri si kwa sababu hawana uwezo bali wahusika hawana ujuzi wa mapishi. Pia, wapo maskini wanaokula vizuri tu kwa sababu ya ufundi wa jikoni. Kimsingi, hakuna chakula kibaya wala kizuri. Kinachoweza kukifanya kiwe hivyo ua kisiwe ni mapishi tu.
Mambo ya chumba cha kulala hatugusi. Hata hivyo, kama ilivyo kwenye mambo mengine hapo juu, nako huko kwahitaji juhudi, maandalizi, na ufundi si haba. Leo, tunaishia hapa.
Chanzo: Mwananchi J'pili juzi.
No comments:
Post a Comment