The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Wednesday, 19 August 2026

Naunda tume tatu kwa mpigo kuchunguza tume

 
Juzi, Mafyatu walinikera sana. Si walidai eti nawachukia ndiyo maana maisha yao yamefyatuka kichwa chini miguu juu kwa shida na tabu. Utafiti niliofanya kwenye kanywaji umenipa matokeo yenye kutekenya akili. Nimegundua kuwa mafyatu wengi hawana raha. Hata wakipata kanywaji hawapati raha bali karaha. Kutokana na kadhia hii, napanga kuunda tume tatu kwa mpigo. Hii ni kusaidia mambo kadhaa. Kwanza, kuwafyatua mafyatu waamini nataka kusuluhisha matatizo yao. Pili, ni kutaka kuhakikisha wao wanajiona kama visababishi vya matatizo, mateso, shida, na taabu na siyo mimi rahis wao.
            Ili kufyatua kisawasawa wasifyatuke wakanifyatua, lazima niwafyatue kabla hawajanifyatua au hata kufyatuka wakajaribu. Tume ninazopanga kuunda zitakuwa ile ya kuchunguza kero, ya pili itakuwa ya kuchunguza tume ya kuchunguza kero, na ya mwisho itakuwa ile ya kuchunguza tume ya tume ya kuchunguza tume ya kunguza tuem ya kuchunguza tume ya kuchunguza tume ya kuchunguza kero. Naona yule anatikisa kichwa akidhani huu ni mkenge. Maana, haijawahi kutokea Fyatuland tume kuchungu tume na tume nyingine kuchunguza tume nyingine. Nikiona mkenge mafyatu hawaukwai huu mkeng, naunda ya nne, yaani, tume ya kuchunguza tume za kuchunguza tume za kuchunguza kero na kuchunguza zile za kuchunguza kero ad infinitum.
            Kwa vile Mafyatu hawaniamini kwa vile siwaamini, nitaarika marafiki zangu toka ughaibuni kuja kuchunguza kadhia zao zisizo na mwisho. Hapa, lazima washikaji wangu hawa wapinge njuluku ndefu ya mafyatu kudadeki! Maana njuluku ya mafyatu haiumi japo wao wanaumwa na kutofyatuka. Mifyatu inajifyatua kujiteka na kujitekesha halafu inalaumu ndata wangu. Mingine inajitoa roho nalaumiwa mimi. Kama wewe unapiga kanywaji hadi kanakufyatua akili nawe unajifyatua uhai kwanini unilaumu? Vitegemezi vipewa njuluku na maadui za Fyatuland wa kigeni vinaingia mtaani eti kunifyatua! Nikivifyatua, mnanilaani! Mlitaka vinivyatue siyo? Hafyatuliwi rahis hapa hasa mwenyewe anapokuwa Fyatu Mfyatuzi bingwa wa kufyatuka na kufyatua. Yeyote atakayejifyatua kunifyatua namfyatua kabla ya kunifyatua kama nilivyofyatua vile vitegemezi fyatu vya mafyatu uchwara.
            Hakuna kitu hunishangaza kama kufyatua mafyatu wasiofyatuka wakakufyatua wakaanza kulalamika na kulaumulaumu bila kufyatuka badala ya kujilaum kwa kutofyatuka wakati nguvu na uwezo wa kukufyatua wanavyosema hawafyatuki na kuvitumia. Hivyo, utawasikia wakilalamika kuwa hakuna njuluku na maisha ni magumu. Maisha magumu vipi wakati kuna njuluku ya kumwaga na kufyatuliwa na mafyatu wachache wanene wakati mafyatu waathirika wakigoma kufyatuka na kufyatua bali kuishia kulaani na kulalamika. Fyatukeni mfyatue muone kama hakuna njuluku tena zinazopigwa kila uchao na wachache wakati nyingi mkifyatuliwa na shida za kujitakia. Hil, nalo nitaulindia tume kulichunguza kujua ni kwanini mafyatu hawafyatuki hata wanapofyatuliwa.
            Utasikia fyatu limejifyatua au kumfyatua mwenzake roho halafu nalaumiwa mimi! Ebo! Kwani, nani alikuzuia kufyatuka na kufyatua wanaokufyatua badala ya kujiua au kuua wenzio? Wengi wa wanaojifyatua na kujitoa roho ni wakumbaff walioshindwa kuelewa inshu kutokana na kukosa ubunifu wa kujua kuwa jibu si kuwafyatua wenzao bali wale wanaowafyatua na kujifanya wanawapenda wakati wanawaponda. Nimesika vilio vingi kuwa maisha ni magumu! Magumu vipi wakati bila kufyatuka na kuwafyatua wanaowafyatua yatazidi kuwa magumu? Maisha ni rahisi na ya raha kwa mafyatu wanaofyatuka na kuwafyatua wanaowafyatua. Unalalamikaje maisha ni magumu wakati mvua zinavyesha, mito inatiririka, ardhi ipo ya kumwaga mbali na amani ya imani? Nenda kalime uone. Japo hii ni fomula, ukilima bila kujua anakula au kununa mazao yako, utanilaumu. Najua wengi wanafanya kazi tena kwa nguvu. Kinachokosekana na ufyatu wa kutojifyatua na kudai haki katika kila kitu kinachofanyika. Wakulima wanalima tena kwa sana lakini ajabu wanaotajirika ni madalali wanaowafyatua. Fyatueni madali muone kama hamtatajirika hata kuliko wao.
            Mafyatu yanachapa mzigo kama hayana akili nzuri lakini yanazidi kuwa makapuku. Guess what. Hata mfanye kazi vipi bila kufyatuka na kudai hata kuipoka haki, mtafyatuliwa muishie kulalamika hata kujiua na kuuana. Ni simpo. Fyatukeni muwafyatue wanaowafyatua muone maisha yatakavyo kuwa mukide kkkk. Na hili, nitaliundia tume ya kulichunguza na nyingine ya kuichunguza hii tume ya kulichunguza ilmradi inichunguze nikaifyatua kuzuia kufyatuliwa na wale ninaowafyatua tokana ufyatu wao wa kutofyatuka na kunifyatua hadi nawafyatua.
            Nadhani wengi wameishachukia kwanini siendi kwenye mada ya kuunda tume za kuchunguzana. Nafanya hivyo makusudi. Yote ni kwa sababu unapowafyatua mafyatu lazima uwazungushe na kuwachosha ili wachoke na kusahau. Kabla ya kuunda tume hizi tatu, mbali na nyingine nitakazounda kama zengwe halifatanikwa, nshaunda tume nyingine za kutaka kuwafyatua mafyatu wasinifyatue au kuamini kuwa niliwafyatua japo niliwafyatua. Hivyo, kuzungusha ndo mujarabu wa kuwapumbaza na kuwafyatua mkenge wasifyatuke. Nataka wafyatuane na kulaumiana badala ya kunifyatua au kunilaumu. Si inapendeza?
       Kwa vile bado nina masuala ya kwenda kundia tume za kuchunguza na kuchunguzana bila kunichunguza mimi, lazima niishie hapa kwanza niende kuunda tume za tume za tume za tume za kuchuuuzana, sorry, kuchunguzana. Tume lazima ichunguze tume na tume ziichunguze.
Kumbe hakujacha!!
Chanzo: Mwananchi J'tano Leo.
Dk. Nkwazi Mhango ni mwana kolumu wa Mwananchi na safu hii hutoka kila Jumatano.

No comments: