The Chant of Savant

Wednesday 24 July 2013

Bila mkalimani hawa wamama wanaelewa kweli?


Mke wa rais Salma Kikwete akimsikiliza mke wa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Cherrie Blair huko Hoyoyo. Kwa walioona picha ya kuwasili kwa rais Obama na mkewe jinsi Salma alivyosimama kama mpambe huku Michelle akilazimika kuongea na Kikwete na mumewe kutokana na mwenyeji wake kutokiweza kimombo watajiuliza swali lile lile.Ni bahati mbaya kuwa Salma akishauriwa asipoteze muda kwenye usasi wa ngawira kupitia NGO yake ya WAMA na badala yake akajiendeleze,anaona wanaofanya hivyo kama wanamchukia au kumdharau wakati siyo. Je hawa wawili wanaelewanaje bila mkalimani?

6 comments:

Anonymous said...

Hahaha LUGHA GONGANA!!! Niliona kuna picha moja ya yeye na Michelle Obama yaani ilikuwa inaonyesha kabisa kuwa hawaelewani. Anahitaji kujifunza oops kurudi darasani sasa sijui ataanza level gani???

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Asiogope kwani elimu haina mwisho. Ni bahati mbaya kuwa tunatawaliwa na vihiyo. Ingekuwa nchi za wenzetu angelazimishwa kurudi class. Natoa ofa ya kumfundisha bure ili kuondoa aibu kwa taifa letu so to speak. Hata hivyo tusimlaumu sana. Iwapo mume wake yuko in bed with forgers like Emanuel Nchimbi, William Lukuvi, Makongoro Mahanga, Didace Masaburi, Diodorus Kamala na wengine nani amkumbushe nani umuhimu wa ilm?

Jaribu said...

Mume wake mwenyewe naye ni kihiyo. Ungetegea "dakta" mzima angekuwa anamsaidia mkewe kwa kumfundisha. Shida ni kwamba hata na yeye mwenyewe Kikwete anahitaji tuition.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Jaribu uliadimika. Karibu tena ndugu yangu. Sasa namngojea Mtwagio. Maana nyinyi si wasomaji tu bali marafiki wa kweli.

Jaribu said...

Ahsante na pongezi kwa kukamilisha miaka 16 ya ndoa. Shughuli nyingi lakini kila ninapopata muda najitosa hapa.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Shukrani kwa kututakia heri katika ndoa na pole kwa mihangaiko. Najua ndiyo maisha muhimu afya na uzima.
Kila heri,