The Chant of Savant

Friday 11 December 2015

Nimeipenda hii japo Kikwete, Muhongo na Escrow hawamo

2 comments:

Anonymous said...

Muongo nafikiri mtu sahihi kuwa kiongozi(mkurugenzi) wa idara au kurudi chuo kikuu kufundisha maana ndiyo kazi profesa ni mwalimu na siyo mtawala zaidi hiyo katika majibizano yake mengi kuhusiana na uwekezaji katika gesi asilia na mafuta alikuwa ameelekeza maelezo yake zaidi katika muelekeo wa kimasomo zaidi badala ya halisi. Kama alivyopiga stori pale kijiwe chetu cha malipo kwa kupiga porojo kwa sisi wajinga https://www.youtube.com/watch?v=MsR4lEDyXvw

Pia alikuwa akileta zihaka katika hotuba zake kwa watanzania kwamba hawana mitaji katika kuwekeza gesi asilia na mafuta. Nashangaa alishindwa kujitazama yeye mwenyewe kama miongoni watetea Tengeta escrow moneyi. Kagodi, Richmong na zile dili zingine zote. Hiyo pesa ikijumuishwa ilikuwa inatosha kuchimba visima vingapi kwa pesa za walala hoi zilizochukuliwa na washika dhamana ya uongozi na kutumbukiza matumbo yao ambayo wameyageuza ubongo.https://www.youtube.com/watch?v=D9PyJUcd56g

Mwisho naongeza na namheshimu sana Mzee wa kazi tuu isipikuwa kwenye huyu jamaa anayenuka kujiuzulu kwa kashfa za pesa za umma na wale wapiga kura mabingwa kushabikia ukabila na kumrudisha mtu ambaye ofisi ya umma ilikwisha mshinda kuwa mbunga kwa kuchaguliwa na ninyi majuha wa mtazamo wa mwaka arobaini saba katika karne ya 21.


Mwalimu naishia hapa maana nasikia uchungu, hii ni sawa na gome la mbuzi kulindwa na fisi, halafu mbuzi wakipungua tunakwenda kuiga ramli kutamfuta mwizi wa mbuzi wetu. Mwambie Mzee wa bull dozer kutafuta mtaalamu wa taaluma ya ubunifu katika biashara na uwekezaji kwa maendeleo kuwa waziri katika hii wizara na siyo wana-taaluma ya miamba hapo siyo maala pake kuwapo

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon usemayo ni kweli. Tangu wasomi walipovamia siasa ili kuiba kama wanasiasa, usomi wao uliingia matatani. Muongo ni muongo wa kawaida tu anayepaswa kuwa gerezani na si kwenye wizara nyeti kama hiyo.Imezidi imepungua basi wangempa lau uwaziri wa elimu ambayo ndiyo taaluma yake. Hata hivyo, kusasfishwa na kurejeshwa kwa muongo ni ushahidi kuwa kinachoendelea kinaweza kuishia kuwa sanaa sawa na zile za Kikwete na genge lake la wezi. Ni suala la muda Magufuli wa kweli na walaji wenzake watajianika kutokana na makosa wanayoanza kufanya.