The Chant of Savant

Tuesday 12 January 2010

Mpayukaji aanza maandalizi ya uchaguzi

Ndugu wapendwa sana wanakijiwe na jamii kwa ujumla,

Huu ni mwaka wa uchaguzi wa kijiwe chetu kitukufu. Hivyo, kama mgombea mtarajiwa, nimesimamisha au kupunguza kuzurura ili kuwa karibu na kijiwe tayari kukibamiza mkenge. Hivyo, leo niko kijiweni tele kama pishi la mchele.

Najua wachovu wengi walionichagua kwa kupenda sura yangu wameishanichoka. Wanasema: wanataka sera siyo sura. Hata wale waliosema mie chaguo la Mungu wameishastukiwa nao kustuka. Wameniruka futi mia!

Tufuatane katika kikao cha leo uone ninavyosulubiwa na kujinasua kabla ya siku ya tatu-uchaguzi.

Namuona mpambe wangu na mropokaji mkuu Mgosi Machungi almaarufu Joe Makambale ametulizana pale akitabasamu baada ya kunideku nikitia timu.

Pia yupo mwezeshaji mkuu gabacholi Kanji almaarufu Roast Tamu. Eddie Ewassa au Mkwapuzi Mbwa Mwitu yupo pia. Kadhalika yupo msomi Mkata tamaa almaarufu Daktari (Lakini si wa kughushi).

Timu leo imekamilika. Namuona Mpemba almaarufu Madevu na mzee Maneno almaarufu Kimdunge Mwehu bila kumsahau mzee Kidevu almaarufu Mtoboa siri.

Naona msomi anaingia akiwa anaimba wimbo wake wa kizungu. Ukiona msomi kaimba ng’eng’e jua mambo si mambo. Huko mbele sijui kama salama.

Anaendelea kujiimbia:

By the rivers of Babylon , there we sat down
ye-eah we wept, when we remembered Zion.

When the wicked
carried us away in captivity
required from us a song

Aaaaa aaaaaaa!

Now how shall we sing the lord's song in a strange land
Let the words of our mouth and the meditations of our heart
be acceptable in thy sight here tonight
Let the words of our mouth and the meditation of our hearts
be acceptable in thy sight here tonight
nnnnnnh nnnnnnh!

By the rivers of Babylon , there we sat down
ye-eah we wept, when we remembered Zion.

By the rivers of Babylon (dark tears of Babylon )
there we sat down (You got to sing a song)
ye-eah we wept, (Sing a song of love)
when we remember Zion . (Yeah yeah yeah yeah yeah)
By the rivers of Babylon (Rough bits of Babylon )
there we sat down (You hear the people cry)
ye-eah we wept, (They need that ???)
When we remember Zion . (Ooh, have the power)

Naanza kujitetea baada ya msomi kuacha kuimba. “Nani kakumbusha farao rafiki yangu?”

Msomi anajibu haraka: “Mwizi, msanii na jambazi yeyote hata awe na sura nzuri hana tofauti na farao. Period.”

Kijiwe kimepigwa na butwaa hasa ikizingatiwa si wote ung’eng’e unapanda.

Machungi anajifanya hii si kitu. Anaanza kwa kunikaribisha kwenye kijiwe. Anasema: Mheshimiwa Mpayukaji. Ingawa ni siku nyingi hatijakutia machoni kutokana na shughui za ujenzi wa kijiwe, keibu kwenye kijiwe chako.” Anabwia kahawa yake huku akijichekesha kama changu na kuendelea: “ Kwanza tipe habai za bi nkubwa ambaye juzi tilimuona kwenye uninga akikufanyia vitu vyake.”

Naweka chini kikombe changu cha tangawizi na kukohoa na kusema: “Mabwana na mabibi, ni furaha iliyoje kuona kijiwe chetu kimeshikamana na kina amani. Sina maneno kuwashukuruni mnavyoelewa mzigo nilio nao kwa ajili yenu.”

Kabla ya kuendelea, lazima niwataarifuni. Tuna mgeni kijiweni. Naye si Mwingine ni bi Sofii Fyatu almaarufu Lioness. Anasifika kwa kubwia ugolo, kuvuta ganja na kupayuka hakuna mchezo!

Kabla ya kuendelea bi Sofii anatia guu kilingeni. Anasema: “Mzee na kiongozi wetu. Hapa tuna ugogoro. Kuna watu wanamuonea wivu Ewassa kwa vile ni kidume cha shoka.”

Kabla ya kuendelea Mpemba anaingilia. “Weye mama tumia lugha ya kistaaarabu ati. Nani waona si kidume weye au kwa vile siye si mumeo?” Jaribu utupe uone kama lugha haitabadirika.”

Mara Mgosi Machungi anadandia kuokoa jahazi. “Jamani, tiwe na adabu. Kia mtu ni kidume cha shoka kwa nkewe bwana. Naomba Sofiii usiseme hivyo tena. Tinaweza kupandwa na hasia tikafanya kitu mbaya hapa.”

Anapokea sigara kali toka kwa Sofii na kuendelea. “Leo tinataka tipange mikakati ya uchaguzi na sio habai za vidume na upuuzi mwingine kama huu.”

Kachokoza nyuki! Mipawa anatia timu bila hata kutoa taarifa. “Hapa hakuna cha kupanga mikakati ya uchaguzi bali ya kumuengua mwenyekiti (yaani mimi).” Ananiangalia kwa jicho la chuki na dharau na kuendelea. “Mwenyekiti amekuwa akizurura muda wote. Mara yuko Nairobi kwa wakora, mara Uganda kwa akina SSebo mara huku mara kule.”

Hapumui. Anaendelea. “Baya zaidi anatumia pesa ya kijiwe na mkewe kwenye haya matanuzi utadhani tulimchagua huyo shorty wake!”

Napandwa na hasira na kutia timu. “Mipawa nakuheshimu. Usirudie kumuita lazizi wangu shorty. Huoni alivyopendeza na kuchana siku hizi?”

Mwe! Nimelikoroga! Msomi anaingilia bila hata kungoja nimpambe bi mkubwa. Anasema: “Mzee kubali umechemsha sana hata kama wapambe zako akina Makambale Mgosi hawaoni.

Huwezi kukiibia kijiwe ukatumia pesa vibaya halafu ukaanza kutufundisha jinsi ya kukueleza matatizo yetu. Mie napendekeza usiruhusiwe hata kugombea mwakani. Maana wewe ni hovyo. Umeacha kijiwe kiendeshwe na akina Mbwa Mwitu na Kanji na Mgosi ilhali sisi hatutendewi haki. Kijiwe kinakabiliwa na ombwe la uongozi.”

Anajiweka vizuri kwenye benchi na kuendelea. “Kwenye kampeni ulituahidi maisha ya raha kwa kutoa kashata na kahawa bure kwa wote tusistuke kumbe wote ni wewe na wapambe zako na shorty wako!’

Anapiga chafya mara mbili na kuendelea. “Ulituhadaa kwa sura yako nzuri wakati ule. Sasa huna sura wala sera. Umenenepeana kama guruwe kwa pesa ya kijiwe. Huyo mkeo ndiyo usiseme. Yaani hata pesa ya mkorogo atumia ya kijiwe!”

Mzee uzalendo unanishinda. Naamua kuamka na kukabiliana naye nisijue daktari wangu alinishauri nipumzike. Nilianguka nikazimika kwa dakika kama mbili hivi kabla ya kuokotwa na wapambe wangu na kuniondoa kwa aibu.

Ukiondoa wapambe wangu, naona wajumbe wote wanatikisa vichwa kuunga mkono yaliyosemwa na msomi.

Wakati wakinizoa zoa msomi anaendela kuzoza. “M tu mwenye keshajiishia! Mwaka huu tunataka matendo si maneno matamu na usanii wa kijinga. Sisi si wajinga tena na tumechoka na kutumiwa kama nepi.

Nasema wazi ingawa wapambe zako wanasema kukukosoa ni kukuchukia-hufai ndugu yangu kitoe uache watu wenye uwezo wafanye vitu vyao. Tumekuchoka tumekuchoka tumekuchoka hakuna mfano.”

Baada ya kumwangiwa maji na kupata nafuu nakaa nikiwa nimejiinamia.

Kabla ya kuendelea kusiliba, Mpemba anaingilia. “Ami usemayo kweli. Lakiini kuna namna ya kuyaongelea ati.”

Hangoji Mpemba amalizie. “Hakuna cha namna wala nini jamaa hafai hata ujumbe wa nyumba kumi achia mbali ukuu wa kijiwe!’

“Loo!” Anatia guu mzee Maneno. “Kwanza Mpayukaji omba radhi sheitwan apite. Pili Msomi hujakosea ingawa umekosea. Tatizo la wengi wetu ni kujifanya wanajua hata kama hakuna wanalojua; kujifanya wanaweza hata kama hakuna waliwezalo. Kusema ukweli mkuu tunakushika faini. Toa tangawizi na kashata ili kikao kiendelee.”

Kwa nyonde nyonde namnong’oneza Kanji anifadhili kuwanunulia walevi tangawizi. Naona nyuso zinaanza kufurahi.

Msomi anasema. “Mie sinywi tangawizi yako. Ni hongo. Mie si panya bwana.” Anaamka na kujikata kislesi!

Nabaki nimepigwa butwaa. Lakini hanitishi huyu. Nitamwambia shehe ubwabwa atabiri kuwa atayakenichukia na kutishia kitumbua changu lazima adedi ghafla. Shauri yenu.

Hayo tuyaache. Vipi mlinionaje juzi nikiwa nimejinoma na Drogba? Eti wapuuzi wanasema nilipaswa kuwa waziri wa michezo kwa sababu mambo yangu ya mchezo mchezo. Hawajui huu ni wakati wa kuwabamiza mkenge vijana na wapenda michezo! Mie hata kwenye misiba naponyoka na kwenda kucheki mechi.

Kabla ya kusahau, nilipewa mwaliko kwenye harusi ya my friend Zuma alipojiponyolea kimwana cha tano. Mie haya siyawezi. Nafanya kwa siri.

Bado mwaliko toka kwa kijogoo mwenzako Mswati wakati wa Umhlanga atakapoponyoa kitu cha 15. Duh mila au uchangupaka mtupu? Tuyaache. Nyumba na ukuu vinaficha mengi na mengine.

Guys I am serious. Mark my words.

Acha nami nikitotoe kabla ndata hawajanifungulia kesi ya uchochezi ingawa ni ukweli!
Chanzo: Tanzania Daima Januari 13, 2006.

No comments: