The Chant of Savant

Sunday 5 September 2010

Slaa anachumbia mtalaka na huyu wa Kikwete ni nini?

Rahma Al Kharoos mkurugenzi wa kampuni ya mafuta na madini ya RBP Oil anayesemekana kuwa mke wa pili wa rais wenu.
Bila shaka watanzania wengi wanajua kuwa rais wao aliyemali muda wake Jakaya Kikwete ni Toboatoboa au tuseme Chovyachovya kuanzia Makongo Sekondari, Chuo Kikuu cha Dar es salaam,Sinza Kijiweni hadi nje ya nchi.

Ingawa CCM wanaona kama wamegundua silaha ya nyuklia ya kummaliza Dk Wilibrod Slaa kwa sababu aliachana na mama aliyezaa naye, jambo ambalo hafichi, wajue mtu wao, katika hili la ndoa, hana salama.
Tutaanza kuwaletea nyumba zake ndogo na baadaye tutaleta hata vyangudoa wa mitaani ambao amewahi kuparamia.

Tukimaliza hili, tutakuja na mgogoro wa kuanguka ambao ni ushahidi tosha kuwa afya yake ni ugogoro mtupu ingawa yeye na waramba viatu wake wanaficha.

Tuanze na hawara yake Kikwete anayejiweka weka kwenye udhamini wa mambo fulani fulani huku akimuigiza Salma Kikwete kumpigia kampeni mtu wake.

Hata Salma hatanusurika. Waliofundisha naye wako na wana data zake zote hata na alivyokutana na JK kwenye mazingira ya kutia kila shaka. Hapa bado hatujaenda kwao umakondeni na kuja na data nyingine nyingi tu. Hapa bado hatujagusia vimada waliojazwa kwenye ukuu wa wilaya na sehemu nyingine nyeti serikalini. Hapa bado hatujakuletea aliozaa nao na wanaharamu wake. Hapa bado hatujavinjari kila kona inayojulikana. Na CCM wajue. Tunapata data zake sawa na tulivyopata za EPA-wanaomjua wengi wako tayari kujitolea kuanika uchafu wake.
Hapa hatujagusa biashara zake na mambo mengine machafu kuliko hata hayo.
Inzi ana hekima moja kuu. Anasema. Ukijua huu naujua ule.

7 comments:

Anonymous said...

Una uhakika au unasema tu kumchaflia jina raisis wetu mpendwa Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete?? sisi hatutaki majungu tunataka uthibitisho kwamba ni kweli anakimada Makongo mpaka sinza kijiweni, maana kusema ni rahisi tatizo ni kuthibitisha !!
kama Slaaaa amekubali kwamba yeye ni chovya chovyaa tena mtu ambaye ni mtumishi wa mungu-Padre wewe unauhakika gani na utendaji wake wa kazi??
Maadili huanzia nyumbani bwana!!!!!!
mpe mtu ukweliwake ingawa unaumaaaaaaaa--Tukutanae Octoba 31 2010

Anonymous said...

Huyu Rahma Al Kharoosi ni Raia wa Oman na ni kweli ni mke wa pili wa kikwete, Rahma alikuwa ameolewa hapa Muscat na jamaa na akajaaliwa kupata watoto lakini kwa bahati mbaya ndoa yake haikuweza kuishi.Rahma alikuwa Nurse Hospital Hapa Muscat na baada ya kuachika ndio akakuktana na Kikwete wakati akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje na akaolewa na kikwete. Hii biashara anayofanya inawezekana mtaji kapewa na mumewe. kwani Rahma hana ujuzi wa elimu yeyote inayohusiana na utafutaji mafuta,gas wala madini na hajawahi kufanya kampuni yeyote ile hapa Oman inayohusiana na uchimbaji mafuta.Taaluma yake ni nurse. mimi namjua vizuri Rahma na mzazi wake mzee Abdulrahman Kasiga alikuwa anafanya kazi Oman Air na kastaafu na kwa sasa anaishi Tanzania.
Kwa hiyo muacheni ale matunda ya mumewe.Utajiri alionao ni wa kutokana na mumewe.
Rahma anao ndugu na kaka zake wote wana uraia wa Oman na wanafanya kazi huku Oman.Ibrahim and Amrani na wadogo zake wengine.Waswahili wanasema ukikipata kitumie na ukikikosa kijutie.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Nadhani hayo majibu yanatosha. Kama mpendwa Anonymous bado unataka dozi zaidi na zaidi, wenye data watamwanga bila kinyongo. Huyo mmoja bado ukitaka na za wengine zipo bwerere.
Kila la heri.

malkiory said...

Wewe anonymous kuwa macho. Ni heri wangemtafuta mtu mwingine wa kumchafua lakini kwa Dr. Slaa wanatwanga maji kwenye kinu.

Nadhani unamwelewa fika Dr. Slaa kuwa ni mtu makini anayetumia ushahidi na utafiti. Siku atakapokuja na uchafu wa vigogo wa vyama tawala, sijui mtakimbilia jehanamu?

Kumbuka jinsi alivyoitikisa bunge na mafisadi. Dr. Slaa ni mtu makini sana ndiyo maana alizipuuzia tuhuma dhidi yake.

Anonymous said...

tunajua viongozi wa ccm wana2ibia hela zetu, wanafanya anasa kwa kutumia hela zetu na wanajitajirisha vile vile lakini tukirudi kwa slaa nae ni wale wale anataka madaraka na yeye atuibie yeye ni padri na padri haruhusiwi kuwa na mke wala mwanamke je slaa hana?! Na isitoshe tunajua now hayupo tena kwnye uongozi wa dini kwasababu alifukuzwa na na viongozi wake kwa kuiba pesa za kanisa sasa mtu huyo aloiba pesa mali ya mungu je ataacha kutuibia sisi

Anonymous said...

Hah hah haha haaaaaaaaaaaaaaaaa!
tumesubiri data za uhuni wa JK, vyangudoa zake, mahawara, miradi yake ya kifisadi hadi tumechoka. HOVYOOOOOOOOOOOOO, mwanaume wa kiislam mwisho wake wa4, la ajabu kwa Jk nini? Kasheshe huyo Padri Slaa aliekimbia kondoo wa Mungu akaishi na kimada na kuzaa nae kisha kamuacha na kupora mke wa mtu, hilo ndo la ajabu. Mtu wa aina yake kuongoza nchi hawezi sbb ni kigeugeu,popo. Upadre hawezi,mke kamshindwa, anajaribu mke wa wenzie, nae atamshinda sooooo.,nchi ataweza?

Anonymous said...

Anonymous 30 March 2012 07:38 unataka data zipo nyingi,Rizone unamjua mama yake? au unataka data nyingine tukuwekee. Zipo tele uliza zingine tukumwagie,kwani dini haikazi kuoa bali hairuhusu vimada.