The Chant of Savant

Thursday 22 September 2011

CCM inapoendekeza njaa na hongo


Kitendo cha kuwahonga wapiga kura wali ni cha kulaaniwa. Huu ni ushahidi wa rushwa, ufisadi na kufilisika kisiasa. Aliyebuni na kutenda jinai hii ni hatari kwa usalama na mstakabali wa taifa kuliko hata Ukimwi. Hatuwatukani. Wananchi wetu wamegeuzwa wadudu na hayawani wapwakizi wa kila upuuzi kiasi cha kufikiri kwa matumbo badala ya vichwa. Jinai hii ingetendwa na wapinzani ingekuwa nongwa. Ni kuwadharau wapiga kura kiasi gani kiasi cha kuwapa ubwabwa ili watoe haki yao ya miaka mitano? Kama hali halitoshi, mkuu wa fedha wa CCM Mwigulu Machemba amenogewa kiasi cha kufumaniwa na mke wa mtu. Haya ndiyo matokeo ya siasa za kifisi na kipanya ambapo kila mtu huangalia atakula nini badala ya atapata nini kisera. Kuna haja ya kuishinikiza CCM kuacha mchezo huu mchafu wa kila fisi kujaribu mbinu zake za porini. Ni mawazo mgando kiasi gani kupata kura kwa gharama ya chakula? Utawasikia CCM wakijisifu: tumeweka, tumechukua waaa! Upuuzi mtupu! Hii ni kuua na kudhalilisha dhana nzima ya demokrasia ya vyama vingi. Kuna kila sababu ya kupambana na jinai hii kama kweli tunalenga kulikomboa taifa.

No comments: