The Chant of Savant

Tuesday 29 November 2011

Siku kanisa lilipomuasi bwana na kudondokea mfukoni


Edward Lowassa mtuhumiwa mkuu wa ufisadi chamani mwake, amebadili mbinu ya kuusaka urais. Ameamua kuwatumia viongozi waroho na vipofu wa kidini walioishiwa roho mtakatifu na kujaa roho mtakakitu.
Kama kondoo, wanaswagwa kwenda wasikojua isipokuwa matumbo yao. Bahati mbaya sana, mbwamwitu hawa wanataka na kuwaburuza kondoo huko kwa mafisi? Je anachofanya Lowassa si udini wa wazi wazi? Mbona hatumuoni akichangia misikiti? Je makanisa yamefilisika kiakili na kiuchumi kiasi cha kujengwa kwa kutegemea pesa chafu? Tunaipeleka wapi jamii iwapo wanaodhaniwa kuwa viongozi wa kiroho wamegeuka kuwa viongozi wa uroho? Kesho Kikwete akianza kumwaga pesa misikitini maaskofu waanze kumshambulia wakati wako kitanda kimoja na udini na ufisadi vinavyonuka hakuna mfano?

No comments: