The Chant of Savant

Saturday 10 December 2011

Havuliwi mtu nguo wala gamba hapa

Let me sing ye a song Lord
Let me glofy ye Lord
Kumbaya
Oh Lord Kumbaya
Let me sing ye a song Lord
Let me show ye’re that great Lord
Greater than any one in the world
The world is thy Lord
Everything is thine Lord
Oh lord my Lord
Kumbaya
Kumbaya

Nisameheni jamani. Nimekumbuka zama zile nafundisha chuo kikuu cha Havard ambapo niliwafundisha watu kama Joji Kichaka (alikuwa kibonde sana), Toni Big Liar (alikuwa kipanga huyu), na wengine mashuhuri. Hayo tuyaache.

Anyway, jana nilikunywa ulabu toka Uingereza nikiwa najipongeza kunusurika kuvuliwa gamba na nguo ukiachia mbali kuchomwa moto. Hivyo, kila saa naongea kiingereza. Najua wambea weshaanza kusema mashauzi na kujipa ujiko. Kwani kosa? Raha jipe mwenyewe na gamba uvae mwenyewe. Wanadhani naongea broken kama jamaa wa mjengoni. No, believe ye me. Nimepiga shule hadi nikakuta kibao kisemacho no more class, go home and drink coffee, dude.

Kwa taarifa yenu niko serious. Hebu tuwe serious kidogo. Kwa haya mauzauza yaliyotokea juzi kwenye kijiwe ambapo mwenyekiti nilivishwa gamba na Ewassa mbwamwitu sijui kama wanywa kahawa wangekuwa na common sense wasingenyotoa roho tena kwa kunichoma moto au kunitia madole kama Kashafi kule Libiya.

Najua kina mzee Machungi wakisoma hapa wataanza kuapa kwa miungu ya kisambaa wakijua wataninyotoa roho. Hapa utasikia miungu ya Zumbe Kimwei, Shekuza, Shehoza, Sheshatani na mazaga zaga mengine.

Wajua walevi walikuwa wamepania kumvua gamba Mbwamwitu. Kilichomsaidia si alinitaja kuwa ule wizi wa pesa ya makaa al maaruf Richmonduli uliasisiwa nami kupata pesa ya kuwahonga wanichague. Nilipoona jamaa kataka kumwanga mboga baada ya kutaka kummwagia ugali, ikabidi nimlinde ili wote tunusurike japo roho inauma.

Jamaa alinichefua na kunichafua sina mfano. Hata hivyo, nilistuka japo sikuongopa kutokana na kujua wapinzani wangu nao njaa tupu. Kosa walilofanya ni kutojua kuwa kambale wote wana sharubu. Laiti wangejua hili wasingepoteza imani na muda kudhani mwenyekiti - gamba nene na kuu- ningemvua gamba mwenzangu. Walipoteza muda mwingi kumtafuta mchawi wakati mchawi anayewamaliza ni mimi. Walitaka kumsaka na kumchoma moto mwizi wasijue mwizi mwenyewe ni mimi niliyeshika kibiriti!

Kuondoa udhia, kabla ya kufanya kigwena chetu kilichofanyika Idodomya muhula huu, nilimtwangia simu Mbwamwitu na kupanga jinsi ya kuwatosa vidomodomo kina Mchunguliaji, maarufu Mapepe Ninaye na shoga yake Joni Chill. Tuliamua kuwa ili kuwakomesha wasichezee ulaji wetu tena, tuwageuzie kibao. Ili wasijue, tulikubaliana niue hoja ya kujivua gamba japo Mbwamwitu aliamua kunigeuzie kibao. Hata kama ni noma, sina mpango wa kugombea tena uenyekiti wa kijiwe.

Kwa vile tunawajua walevi walivyopigika kiasi cha kuwa majuha, wangekubaliana na sanaa zetu bila kikwazo. Na kweli ndivyo ilivyotokea. Hata hivyo Mbwamwitu ameniumbua. Bahati nzuri, hata wale wapinzani wetu kijiweni, hawakukusikika wakitoa lau karipio na tamko la kulaani zaidi ya kuufyata. Isitoshe, tofauti ya vyama vyetu ni majina maana chama changu cha Nyama Ugali na Maharagwe (UNM), hakina tofauti na Chama cha wapinzani wangu kijiweni cha MT yaani Misheni Town au Mshiko Tosha.

Vyama vyote ni vya ulaji. Na isitoshe wote ni wanachama wangu sema hupiga kelele njaa ikizidi. Ukiwamwagia kahawa na kashata wanaachia kila kitu na unajifaidia.

Wanywa kahawa ni watu wa ajabu sana. Juzi ungewasikia wakihanikiza kuwa mie mwenyekiti wa kijiwe mzee mzima Mpayukaji wa Msemahovyo wa Waambie wa Watieakilini eti ningewatosa washikaji zangu wawili yaani Mbwamwitu al-maarufu Ewassa na Mkwapuaji maarufu Endelea Chenga, ungedhani walikuwa na hoja.

Nakumbuka majina mengi yalitajwa kuwa nyuma ya msukumo wa kuwavua gamba jamaa zangu. Nilisikia majina kama Msomimkatatamaa maarufu Sam Sixx na mengine makubwa kijiweni. Walichonga we wasijue mie mwenyekiti ni bingwa wa sanaa kuliko hata Njaa Kaya.

Msianze kuchanganyikiwa bure na kuchanganyana kusema maneno ya nabii Mpayukaji ya kinabii sana kiasi cha kujaa mafumbo na lugha za kitume. Siku hizi kijiweni tunavuana gamba kama chama twawala chenye magamba mazito na manene.

Acha niwamegee mikakati yetu ya kuhakikisha havuliwa mtu nguo wala gamba. Kwanza, ili kuwapata walevi, tuliazimia kwenye vikao vyetu vya siri kuwa lazima tutengeneze adui ambaye atawachanganya kiasi cha kutotushughulikia. Adui tuliyemtengeneza ni kudai kuwa kijiwe chetu kinakabiliwa na upinzani mkubwa toka kwa wanywanywa wetu.

Hivyo, badala ya kushughulikia ufisi, tulikuja na sanaa ya kudai mshikamano. Na hili lilipita bila kupingwa. Maana kama walevi wangejua tulivyokuwa tunawachezea mahepe, baada ya kugundua kuwa kumbe mimi mwenyekiti ndiye gamba kuu, wangeazimia kunitimua tena kwa kunivua gamba na nguo na kunizomea hata kunichoma moto kama kibaka.

Mana kwa niliyowafanyia sina tofauti na kibaka. Walivyo wa hovyo, hata Mbwamwitu aliposema kuwa nilikuwa nyuma ya ujambazi wa Richmonduli, hawakutaka kujua zaidi zaidi ya kutoa toa mimacho kama kunguru aliyenaswa na mtego! Hawa kweli wazima?

Leo stori ni fupi sana. Kigwena chetu kiliisha kwa kuwafunga kamba walevi kuwa tutavuana magamba kupitia utaratibu wa kijiwe. Hakuna kitu kama hicho. Sana sana tutalipana pesa zaidi ya kahawa kujiandaa kumtawaza Mbwamwitu Ewassa kuwa mwenyekiti wa kijiwe baada ya mie kuachia ngazi hapo baadaye. Hivyo, kwa taarifa yenu ni kwamba walevi mtaendelea kuliwa na sisi wale wale.

Kwa vile mimi ni bonge ya mjanja, ngoja nimtwangie Mbwamwitu simu aje tuzidi kukamata manywaji tukijipongeza kwa kuwaingiza walevi mkengeni kwa mara nyingine.

Sappy tearjecker may be a creep or spooky drama; it all depends on you guys. What a tug-along that this thing is! Mizengwe sure.

Kina Mapepe Ninaye, Sam Sixx, Braza Joni Chill na mashambenga wote mkome. Sisi chata la Mizengwe nambari wani ati! Kulaleki ninasepa! Mungu ibariki Danganyika wazidi kudanganyika. Kafu mshirika upo hapo? Nasema havuliwi mtu gamba wala nguo.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 7, 2011.

3 comments:

Anonymous said...

Duuh!Kaaz kwer kwer!

Evarist Chahali said...

Bwana Mhango,nimejibu shutuma zao dhidi yangu (kwamba nimepokea hongo kutochapisha shairi lako) katika post hii http://www.chahali.com/2011/12/bloga-nkwazi-mhango-anituhumu-kuwa.html

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Bwana Chahali, nimeshangaa kusikia hili. Yawezekana kuwa watu wanataka kutugonganisha ili wapate publicity. And I assume hii imetokea JF ambako kuna watu wanatumia majina yangu kwa sababu wanazojua. Unafahamu ukiwa maarufu kuna madhara na faida zake. Therefore my brother, discredit those bogus allegations in the first place.
Otherwise I am fine and sound.