The Chant of Savant

Monday 12 December 2011

Kwetu wanapeana na kulilia nishani Chinua anazikataa!


Katika kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, rais Jakaya Kikwete aliwatunukia watu mbali mbali wakiwamo wanaofaa na wasiofaa nishani, nchini Nigeria gwiji wa fasihi Chinua Achebe amekataa nishani kama hiyo.

Wakati kwetu watu wanahoji kwanini kwa mfano Spika wa bunge la sasa Anna Makinda amepewa nishani wakati hafai, nchini Nigeria mambo ni tofauti. Achebe alikataa nishani ya Commander of the Federal Republic award-nishani ya rais kwa madai kuwa mhusika hajashughulikia mambo muhimu ambayo Achebe ameataka yatekelezwe ambayo ni kupambana na ufisadi, umaskini na vurugu havijashughulikiwa. Achebe alitoa changamoto mwaka 2004 alipokataa nishani kama hii. Je ni nani ana ubavu wa kukataa nishani Tanzania ambapo nishani, shahada za kupewa na kughushi, kujuana katika ulaji na udugu ni madhambi yaliyohalalishwa. Waulize waliotoa na waliopokea nishani kama kuna mwenye udhu na ubavu wa kuhoji kama Achebe. Je Kikwete aliyeingia madarakani kupitia wizi wa EPA na Richmond ana udhu wa kuweza kutoa nishani yenye kuweza kuitwa nishani na kuheshimika? Kama anao basi anaweza kutoa nishani si kwa maana ya nishani bali kituko.

Kwa Achebe kitu muhimu si nishani bali matendo. Kwake rais mharifu ni mharifu sawa na kibaka. Tieni akilini na mtafakuri kwa kina. Je waliopewa nishani wamepewa nishani na mamlaka yenye udhu au wamepewa dharau na aibu? Inashangaza ni kwanini Rostam Aziz na Andrew Chenge hawakupewa nishani hizi zenye maana kinyume na tunavyoelezwa. Aibu ni kwamba marehemu Mwalimu Julius Nyerere amepewa nishani hii chafu na mikono michafu iliyoitoa! Kweli simba akifariki ngozi yake yaweza kugugunwa na panya. Imetokea tena Tanzania.Kwa habari zaidi, BONYEZA HAPA

No comments: