The Chant of Savant

Saturday 30 November 2013

Mlevi kumilki bunduki aue kila anayemuudhi

Baada ya kushuhudia walevi wanavyodedishana kwa shaba, mlevi kwa vile nina usongo na maadui zangu wengi, lazima nimiliki bunduki.
Ukiwa na bunduki hata kama ni ‘apeche alolo’ utaonekana unazo, wasijue wengine wanamilki bunduki ili kutengeneza njuluku hata kama ni kwa njia ya jinai. Siku hizi kaya yetu haina tofauti na Sauzi au kwa Joji Kichaka ambako chuma ni sehemu muhimu ya maisha. 
Bunduki zinanikumbusha usemi maarufu wa Sarah Palin aliyesema, “we say keep your change, we'll keep our God, our guns, our constitution.”
 Tofauti ni kwamba, sisi lazima tuseme, “with our guns we’ll take your coin and destroy your doctored constitution. Our guns have become our source of liberation however in an illegal way and sense.”
Nitawaandama wabaya wangu kuanzia ndata hadi wale wanaommendea bi mkubwa au kutaka kuninyanyasa au kunibambikizia kesi uchwara.
Nani anataka kuona anatembezewa undava ndava wakati ana cha moto? Rafiki zangu ndata mkae mkao wa kudedi kwa shaba kwa vile mnajidai sana na vya moto vyenu, msijue nami nitakuwa nacho cha moto ili iwe jino kwa jino.
Na sitaki kusikia mkilalamika kuwa nimetangaza vita ya kudedisha ndata wakati mkiwaacha wenye vya moto mnaokula nao wadedishe watu na wanyama wetu kila uchao bila kuchukua hatua.
Kama hamtachukua hatua mimi nitawachukulia hatua nyinyi bila kujali nini wala nini.Mafisadi wakae mkao wa kuliwa. Hamuwezi kuiba njuluku zetu na kuficha ulaya mkataka sisi tufe njaa.
Kwa vile mnaogopa cha moto, lazima niwe nacho ili siku nikijisikia kuchacha, nije tugawane kabla sijawamiminia risasi. Mie siwaogopi kama hawa wanaowaogopa na kuwafunga. Lazima mrejeshe changu nami niende kupata raha kama nyinyi.

Pia nitahakikisha na bi mkubwa anakuwa na cha moto chake ili kuwaandama wale mamanzi wanaotaka kuniibia na kunigeuza buzi. Kwa hiyo vyangu kaeni mkao wa kudedi kwa shaba za bi mkubwa ambaye anajulikana kwa kutopenda masihara.

Kwa vile nshawatonya, kazi kwenu. Mkiniona mnatimka kama vile mmeona chizi. Mkiendekeza njaa zenu na ujinga wa si mbaya inzi kufia kidondani, shauri yenu. Ili kuongeza njuluku za kupatia kilaji na kujidai, nitakuwa nikikodisha gun yangu kwa majangili ili wakiua tembo na faru tugawane.

Pia nitahakikisha nakodisha gun yangu kwa majambazi ili wakipata kitu kidogo na kikubwa tugawane.
Kwa vile ujambazi, ufisadi na jinai nyingine kwenye kaya vinakubalika na kuruhusiwa, why should I worry? Money by all means. To me the end justifies the means. I have nothing to lose except my uchovu au vipi? Mambo ni kwa gun!
Nitaitumia bunduki yangu kutishia wale wanaojishaua kwenye mabaa. Ukipingana nami nakutolea gun.
Kwa vile mimi hamnazo najua itakuwa shughuli kupata gun. Hata hivyo, kukwepa kikwazo hiki naandaa njuluku zipatazo madafu laki tano kuwahonga wale wanaotoa gun.
Siku hizi murume ni kuwa na gun. Ukipenda mtu halafu mtu mwingine akaingia kwenye anga zako, unamdedisha kwa shaba.
Wale dada zangu kutoka karibu na mlima Nonihino wanaopenda kugonganisha magari, wakae mkao wa kuuawa.
Sitajali ni uncle au broo. nikigundua unatulisha sahani moja, natwanga shaba tu.  Mie siyo kama Kapuyanga anayeepua vitoto vya shule halafu anavitishia kwa SMS.  Ukiniudhi nakushindilia chuma bila kujinyotoa roho. Nikiona vipi najidedisha ili kuepuka kile Wakameruni huita to have a date with the judge au kumuona pilato ili akubabuseya.
Kwa vile mimi sina miwaya si kama Kapuyanga anayeambukiza miwaya na vitisho, wale Njaa Kaya aliosema wanapata vimimba kutokana na kiherehere, waje kwangu. Sana sana licha ya kuwaambukiza kitambi nitawaambukiza ulevi.
Makonda wanaopenda kunyanyasa abiria wakae mkao wa kuliwa. Nikipanda dala dala lako ukaanza kuleta za kuleta nakufyatua. Nisivyopenda nyodo na mitusi yenu ya nguoni lazima nitadedisha wengi.
Manesi na wakunga wanaopenda kuwatukana wagonjwa hasa akina mama wanaokwenda kujifungua pale Ailala, Mwanyamanyala na Meteke mkae kwa kurambwa shaba.
Kama bi mkubwa atakuja pale kujifungua mkamtukana au kumtakisha chochote kitu, mjue sitawapa njuluku bali shaba.
Wauza baa wenye tabia ya kusachi mifuko ya walevi, kaa mkao wa kuliwa shaba. Nikiingia kwenye baa yako kunywa halafu ukanigeuza buzi lazima nikuchune kwa shaba kabla hujanichuna.
 Hata wale waajiri wanaodhulumu wafanyakazi wao wakae mkao wa kuliwa shaba. Ukiniajiri halafu ukaanza kuniletea za kuleta ninapodai ujira wangu, jua sitakwenda kwenye vyama vya wafanyakazi zaidi ya kukurambisha shaba mchana kweupe.
Wenye mbavu za mbwa wajiitao wenye nyumba wenye tabia ya kunyonya na kunyanyasa wapangaji kaeni mkao wa kufa.  Maana nikipanga kwenye ubavu wa mbwa wako ukaanza kutaka kunigeuza buzi, jua umekufa wakati si wako.
Maana kuna mijitu kuwa na nyumba inaona kama ni kuwa na kila kitu. Ukiwa mpangaji unaonekana kama huna future.
Haijui kuwa wengi wenye nyumba ni wapangaji wa jana na wapangaji wa leo ni wenye nyumba wa kesho. Mijitu mingine mijinga na mipumbavu ikiwa na nyumba inasahau kuwa ni biashara kama nyingine.
Lazima uheshimu mpangaji kwa vile mteja ni mfalme. Wenye nyumba na makonda ni watu wa ovyo wanaopaswa kudedishwa kwa shaba.
Naona yule anatikisa kichwa. Simaanishi kila mwenye nyumba lazima apigwe shaba. Namaanisha wale wenye nyumba wanaodhani kuwa na nyumba ni waranti ya kunyonya na kunyanyasa wengine.
Nikiwa na bunduki yangu kila kitu ni shaba. Akikatiza mbwa nafyatua. Akikatiza inzi nafyatua. Hata akikatiza munen… shaabaa tu.
Leo natuma salama na rambirambi kwa rafiki yangu Saleh Saggaf kwa kuondokewa na mama yake. Inshallah Allah atawaimarisha na kuwawezesha kuvuka kwenye kipindi hiki kigumu.

Chanzo: Nipashe Jumamosi Nov., 30, 2013.

No comments: