Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Saturday, 26 March 2016

Mlevi astukia 'ugesishaji' kaya

Tangu alipoingia kwenye ulaji baada ya kuchukua ukanda toka kwa Njaa Kaya aliyeonekana kuwa kilaza kiutawala kiasi cha kuigeuza kaya shamba la bibi kama alivyodai rahis hivi karibuni, nilitokezea kumzimikia rahis Dk John Kanywaji Makufuli. Nilichetuliwa na kasi na namna yake ya kuwasaka na kuwatumbua majipu wagonjwa wa ufisadi. Hata hivyo, tangu juzi alipotangaza timu yake ya wakubwa wa mikoa, badala ya kumzimikia, natamani nimuwakie kama si kumbwatukia. Maana, ametoa rungu kwa machizani ili watuumize tena watakavyo ukiachia mbali kuwaangiza watembeze undavandava hata kama ni kwa makosa ilmradi baadaye warekebishe.
Hakuna kauli iliyonkata na kunifanya nivute na kunywa kama sina akili nzuri kama kuwapa ulaji wageshi wastaafu wakati kuna vijana wengi–tena waliobukua mambo ya siasa na ma-political sciences na madude mengine magumu yahusuyo utawala–wanaoweza kutawala hiyo mikoa bila kulazimisha wala kutoa maamuzi bora maamuzi ili warekebishe baadaye kama alivyowaagiza. Kikatiba, wageshi hawapaswi kujiingiza kwenye siasa hata kama wamestaafu isitoshe siasa zenyewe zinapokuwa za majitaka na kupeana fadhila. Hii maana yake ni kwamba hawa jamaa walikuwa na kadi za nambari wani kibindoni jambo ambalo ni kosa la jinai. Ina maana walikuwa wakifanya kazi ya umma na kulipwa njuluku wakati wamevunja sheria ukiachia mbali upendeleo na kupokea amri za kijinga kama kusimamia uchakachuaji wa kura. Ndiyo maana jamaa amewaamini na kuwaachia kila kitu wafanye watakavyo. Nadhani hapa kamchezo kachafu ka kulipana fadhila karudufiwa. Katika kuwafunda na kuwaagiza, rahis Makufuli alisikika akisema ni heri wafanya maamuzi hata kama ni mabaya watarekebisha baadaye kuliko kutofanya maamuzi. Je kinachotakiwa hapa ni kufanya maamuzi au kuchukua maamuzi ya maana? Kwa walevi, heri mtawala asiyefanya maamuzi ya hovyo ili arekebishe baadaye kuliko anayechukua maamuzi ya kijinga na kutegemea kufanya maamuzi mazuri baadaye. Kwani kazi ya ukubwa wa mikoa ni ya majaribio ya kufanya au kuchukua maamuzi au namna ya kuwafundisha wageshi wastaafu mambo ya utawala?
Kama haikutosha, jamaa aliwaambia wakamate walevi na kusweka ndani hasa wale akina sie tunaoshinda vijiweni kutokana na kutokuwa na ajira. Hebu fikiri. Wachizani kama jamaa yangu Po Makondakonda ambaye alishasweka ndani wahishimiwa na watumishi wengine wa halmashauri atatumiaje rungu hili? Kwani kaya yetu ni ya kigeshi au vipi? Tuambizane kabla ya kuchenchiana bwana. Mbona akina Jimmy Rugemalayer, Roastatamu Kagoda, Singansinga Sethii na mzee wa Vijisenti na majambazi wengi waliosababisha umaskini na ukosefu wa ajira hawakamatwi kama hapa siyo usanii wa Ki-SISIEM?
Simuwakii wala kumbwatukia rahis Makufuli. Badala yake nampa ushauri wa bure. Kama anaamini kuwa wageshi ndiyo wanaweza kukomesha matatizo ya kaya bila kufumua mfumo na kuufuma upya anajidanganya ten asana. Mara hii amesahau tulivyoambiwa kuwa Njaa Kaya alikuwa mgeshi. Hivyo angeweza kuinyoosha kaya akaishia kuiharibu hadi kumpa ujiko Makufuli? Kinachotakiwa si ugeshi wala utishi bali kufuata sheria na kubadili mfumo mfu na muovu ulioanzishwa baada ya kung’atuka mzee Mchonga wa Burito. Hata ukitumia bangi na kanywaji, huwezi kutoa amri za kutatua matatizo ya miaka zaidi ya thelathini ndani ya siku 15. It is impossible sir.
Kitu kingine kinachonifanya nitamani kumuwakia Makufuli ni ile kutoa maagizo ya kihasara hasara kama vile kuwaambia wakubwa wa mikoa na wale wa Banki kubwa kuwa wafute majina ya wafanyakazi hewa ili kuanza upya. Tutaanzaje upya bila kuwakamata na kuwashughulikia walioajiri wafanyakazi hewa na kupiga njuluku kwa miaka nenda rudi?
Nijuavyo aina mpya ya utawala unaoanza kuota mizizi wa kumridhisha Dk Kanywaji, wahusika watakwenda kuumiza walevi bila sababu ili kumridhisha bosi wao. Tushawaona wengi hasa kwenye jiji la Bongo ambako jamaa yangu Makondakta alifanya kila vituko kwa kuvunja kila sheria kitabuni kuhakikisha anamuingiza mkenge Makufuli na kuishia kupewa rungu zaidi ili avurunde zaidi. Siku moja ataniambia kama si kukumbuka haya ninayochora hapa. Angajua usanii wa huyu dogo wala asingejivunjia heshima kumpigia debe wazi wazi. Atajuta baadaye baada ya malalamiko kuzidi juu ya tabia yake ya umungumtu itakapoanza kujitokeza na kuumiza wale anaodai analenga kuwaondolea kero. Sijui kama kuruhusu wakubwa wa mikoa kufanya watakavyo kama ni kuwasaidia walevi. Ni kama ametangaza utawala wa kigeshi kwa mlango wa nyuma asijue madhara yake. Walevi tunapinga kukamatwa na kuswekwa ndani au kuburuzwa simply because wahusika wanataka wajijenge na kumfurahisha muungumtu wao aliyewaumba. Huwezi kuendesha kaya kwa amri ya mtu badala ya kanuni zilizotugwa na kukubaliwa na wanakaya wenyewe. Huu ni uimla hata kama tunaambwa una nia nzuri.
Nimalizie kwa kuwamba wahusika warejeshe kaya yetu kwenye utawala wa kiraia badala ya kuigesisha kwa mlango wa nyuma. Hii kaya ni ya walevi wote bila kujali kazi wala vyeo vyao. Natamani nimuwakie jamaa niliyemzimikia sasa anaanza kuniangusha.
Chanzo: Nipashe, Machi 26, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:15

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

I Love My Country Tanzania

I Love My Country Tanzania

The Curse of Salvation

The Curse of Salvation

Gen Z and Internet Revolution

Gen Z and Internet Revolution

I Cry for Ambazonia and Darfur

I Cry for Ambazonia and Darfur

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

The Story of Stories

The Story of Stories

The Chant of Savant

The Chant of Savant

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presid...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the ho...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon where...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete Pea...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaidi....
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (84)
    • ►  December (1)
    • ►  November (11)
    • ►  October (9)
    • ►  September (7)
    • ►  August (12)
    • ►  July (8)
    • ►  June (7)
    • ►  May (5)
    • ►  April (4)
    • ►  March (6)
    • ►  February (8)
    • ►  January (6)
  • ►  2024 (92)
    • ►  December (7)
    • ►  November (4)
    • ►  October (11)
    • ►  September (9)
    • ►  August (7)
    • ►  July (9)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (7)
    • ►  March (6)
    • ►  February (7)
    • ►  January (8)
  • ►  2023 (118)
    • ►  December (10)
    • ►  November (10)
    • ►  October (9)
    • ►  September (2)
    • ►  August (4)
    • ►  July (6)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (18)
    • ►  March (13)
    • ►  February (9)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ▼  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ▼  March (26)
      • Kijiwe chapanga kutembelea Zenj
      • Barua ya wazi kwa waziri mkuu Majaliwa
      • Lukuvi whom are you trying to dupe
      • Mlevi astukia 'ugesishaji' kaya
      • Kwa ndugu zetu mnaoamini kwenye dini za kigeni
      • SHUKRANI YA PUNDA
      • Kijiwe kupinga amri za Dk Kanywaji
      • How do you view and assess this stuff?
      • Makufuli mtumbue jipu Lukuviii
      • Kijiwe chastukia sanaa za Lukuvi
      • Magufuli usitegemee kuombewa uchukue hatua
      • Janga la taifa: Vyuo vikuu vinapoeneza ujinga
      • Leo natoka na Wanda Boys na vimbwanga vyao
      • Wakuu "wapya" wa mikoa, Magufuli achemsha
      • Boozer won’t pray for Mugful
      • Mlevi amtumbulisha jipu Sifui
      • Sijui kama wanaong'ang'ania madaraka walijifunza k...
      • Reunite East Africa instead of integrating it
      • Haya ni maombi au utapeli na ubangaizaji
      • Kijiwe: Makonda acha kudhalilisha walimu
      • Breaking news Sefue chini Ikulu
      • Cronyism, nepotism and nihilism: Hooray Makamba
      • Kwa wanandoa au watarajiwa
      • Mlevi kuwa wakili wa kujitolea kesi za mafisadi
      • Kijiwe chataka Kiquette ajitumbue kwanza
      • AFRICA REUNITE or PERISH chaanza kufundishwa chuoni
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (399)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (33)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (597)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (94)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.