Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Wednesday, 30 November 2016

Makonda na Sirro wachunguzwe wote

            Kwanza niombe msamaha kwa kutowataarifu wasomaji kuwa nilikuwa na mpango wa kuendeleza makala ya wiki jana juu ya tuhuma za ulaji rushwa wa wazito wa mkoa wa Dar Es Salaam. Vyombo vya habari viliripoti kuwa Kamishina wa kipolisi, Simon Sirro, wa Jiji la Dar Es Salaam na RPC wa  Kinondoni, Susan Kaganda wanachunguzwa tokana na tuhuma zilizotolewa dhidi yao na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda. Hili ni jambo ambalo ni jema–japo kuchunguzwa watuhumiwa bila kumchunguza Makonda itakuwa si kuwatendea haki makamanda hawa–ukiachia mbaliku kujenga mazingira kuwa kuna watu wasiogusika (untouchables) nchini. Tunasema; Makonda naye achunguzwe. Kwani, alionyesha uzembe na, unaweza kusema, ubabaishaji na kukwepa wajibu wake kama kiongozi wa ngazi ya juu na raia kwa kutoripoti makosa ya jinai yaliyokuwa yakitaka kutendeka kwa kumhushisha. Makonda, kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa, kwanini–kama hakuwa na maslahi kwenye kadhia hii–hakuchukua hatua kama vile kuripoti kwa waziri mkuu hata rais na badala yake akaishia kulalamika kama hapakuwa na namna au mvutano? Hili swali linajirudia kuliko mengine ili  kumpa picha msomaji afanye tathmini hata hitimisho lake.
            Pili, Makonda anapaswa abanwe awataje wahusika ili washughulikiwe na kueleza kwanini hakuwataja awali. Na hapa lazima tuwe wazi. Tusizugwe na watuhumiwa walioripotiwa na vyombo vya habari kukamatwa siku moja tu baada ya vyombo vya habari kuja juu. Kwanini wakamatwe siku moja baada ya tuhuma hizi kufichuliwa kama hakuna namna? Je mamlaka zilikuwa wapi siku zote hizi? Je hapa nani anatuchezea mahepe kati ya Makonda, Sirro na Kaganda? Hii maana yake ni kwamba watatu hawa, kwa sababu wajuazo wenyewe, walikuwa wanawaachia wauza shisha. Je, kama hakuna namna, ilikuwaje wawajibike sasa na si kabla? Maana, vyombo vya habari vimeripoti hivi karibuni kuwa watu watatu wamekamatwa kwa makosa yahusianayo na uuzaji shisha.
            Ukiachia maswali hayo mama, kuna mengine:
            Mosi, je tutaendelea kufanya kazi kwa namna ya kuzamia na kuchomeana hadi lini?
            Pili, je hawa watatu tu waliokamatwa wanatosha; au wahusika wanatafuta kutuliza hasira na shuku za wananchi ili waendelee na business as usual kama ilivyokuwa kabla ya kuchomeana utambi?
            Tatu, baada ya Makonda kumshutumu Sirro na mwenzake, je wao wanajitetea vipi lau wananchi wapime na kujua mbivu na mbichi ni ipi?
            Nne, je wawili hawa watakwenda mbele ya vyombo vya sheria ili kupata stahiki yao au watanyamaza na kuacha yapite ilhali kunyamaza kunaweza kutafsiriwa kama ukweli wa madai?
            Tano, je watatumia njia mbadala za ndani ya serikali na kuutangazia umma kilichofikiwa?
            Sita, kwa upande wa mamlaka zilizowateua, zitafanya kama ilivyokuwa kwa marehemu Wilson Kabwe? Yaani kuwawajibisha wahusika bila kusikiliza upande wa pili jambo ambalo litamfanya Makonda aonekane bora kuliko wenzake (better than thou) jambo ambalo si jema kwenye utumishi wa umma ambapo kila mtu ni sawa. Kama wawili hawa watatoa utetezi au maelezo yao, itakuwa vigumu kwa umma na hata wakubwa wao kubaini nani mkweli na nani muongo, nani mtafuta sifa na nani mchapakazi.
            Saba, je kuna mengine mengi yaliyofichwa nyuma ya utata huu unaoonekana kukiuka kanuni za utawala hata uongozi kwa kufanya mambo hovyo hovyo bila kufuata taratibu zilizowekwa na zinazojulikana? Hivi karibuni, mwandishi mmoja alishuku mbinu ya Makonda ya kumchafua Sirro kama njama ya kumzuia asiteuliwa IGP. Lisemwalo lipo; kama halipo laja. Hili nalo lapaswa kuchunguzwa.
             Nane, je kitendo cha Makonda kumuumbua Sirro na Kaganda hadharani si ushahidi kuwa baadhi ya watendaji wa serikali ya awamu ya tano, ima hawajui mipaka ya madaraka yao au hawajui hata wanachofanya kiasi cha kulimana hadharani tokana na wengine kupewa madaraka makubwa kuliko uwezo wao?
            Tisa, je huu si ushahidi kuwa serikali ya awamu ya tano haikushikamana (incohesive) sifa ambayo si nzuri kwa serikali ilijionyesha kuwa makini? Sijui kama akina Makonda wanalijua na kuliona hili hasa wakati huu ambapo wafanyakazi wanalalamikia kunyanyaswa na wateule wa rais.
            Kumi, tokana na tabia ya Makonda kuwa kujifanyia mambo atakavyo hata kwa kukiuka kanuni, wapo wanaodhani amepewa madaraka makubwa kuliko uwezo wake. Mfano, hivi karibuni, alionekana akiwadhalilisha baadhi ya watendaji kwa kudai wanaamini ushirikina badala ya kufanya kazi bila ushahidi. Kama haitoshi, alimkalisha kiti moto DMO wa Kigamboni mbele ya umma kana kwamba hakuna mechanisms za kushughulikia tatizo kama hili.
            Tuhitimishe kwa kuvitaka vyombo vya dola visimuongope yeyote tokana na cheo au ushawishi wake. Chunguzeni wote; ili ukweli na mengine ambayo yanaweza kuwa yamefichwa vijulikane. Kwani wahusika, licha ya kuwa viongozi wa ngazi ya juu, bado ni wanadamu wenye kila aina ya udhaifu ukiwemo uwezekano wa kushawishika kupokea rushwa hata kukomoana.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:29 No comments:

Kijiwe chamuunga mkono askofu Mokiwa

 
             Baada ya kuzidi kuongezeka kwa matapeli na wapigaji wanaotumia majoho, askofu Zaky Mokiwa ameamua kuwatolea uvivu. Ameripotiwa akitaka mamlaka kuwachunguza hasa aina ya mahubiri wanayotoa. Uzuri hili limetoka kwenye kinywa cha mwenzao ambaye hata hivyo siyo wa kujipachika wala kanjanja kama wale alishauri washughulikiwe.
            Mipawa ndiye anaanzisha mada baada ya kutua gazeti la Rongaronga mezani ambalo Mchunguliaji analidaka na kuanza kulibukua. Anauliza “wazee mnalisemeaje hili la kutaka wachungaji, wachunaji na wapigaji wanaotumia neno la Mungu kutuvuruga, kutunyonya, kutudanganya, kutuibia hata kutudhalilisha ambalo limetolewa na askofu wa kweli Zaky Mokiwa?”
            Kapende anakula mic “hili halina njadala. Lazima wajanja hawa wanaowarubuni na kuwaibia wajinga wetu wachunguzwe ndani na nje bila ya cha nsalie Ntume. Haiwezekeni kama kaya tukaendelea na aina hii ya ufisadi wa kiroho ulioshamiri uroho.”
            Mpemba anampoka mic Kapende na kuronga “hata mimi nakubaliana na pendekezo hili hasa wakati huu wa “Hapa Kazi Tu”. Kwani, waliachiwa na kujitajirisha huku wakiwasikinisha wajinga wengi walioharibikiwa maisha kutokana na elimu haba. Wanachofanya baadhi ya wachunaji waliojivisha majoho ni ufisadi, ujambazi na wizi wa wazi wazi. Lazima mahubiri yao yachunguzwe na wanaokiuka maadili, sheria na taratibu washughulikiwe mojawapo ikiwa ni kuwapiga marufuku hata kuwatupa lupango.”
            Msomi Mkatatamaa anakula mic “ushauri huu umekuja kwa wakati wake. Kwanini tuwawajibishe watumishi wa umma kama vile vihiyo, watumishi na wanafunzi hewa wakati tuna wachungaji wanaohubiri mahubiri hewa na hasi? Napendekeza wachunguze mapato kama ni ya kweli na kama sadaka zinatumika vizuri na si kupigia ulabu kama ilivyotokea  kwa mzee wa mipako  hadi akapayuka na kupakwa kinomi.’
            Anakohoa na kuendelea “wachunguze tabia binafsi maana wapo walevi, mafisadi, wazinzi na kila aina ya matapeli. Wachunguzwe elimu zao kubaini vilaza na vihiyo. Wachunguzwe biashara zao wapo wauza bwimbwi na utumiaji misamaha ya kodi kujineemesha kwa kupitisha bidhaa za wafanyabiashara wezi wanaowatumia. Wachunguzwe historia zao maana wengine hata si wana kaya bali wakimbizi wa kiuchumi toka kaya jirani. Hapa ni kuchunguzana ili kuepuka kuchuuzana kama ilivyokuwa chini ya tawala zandiki zillizopita ambazo nazo zinapaswa kuchunguzwa na kutumbuliwa bila huruma wala kulindana.”
            Mgoshi Machungi anakatua mic “ningependa nimchomekee askofu Mokiwa kwa kupanua wigo wa uchunguzi. Hapa lazima tiwachunguze hata maisha yao binafsi ikiwezekana tiwatoze kodi na kukagua shuhui zao. Napendekeza wakaguzi wa fedha za umma wawe wanawakagua hawa jamaa ii kuepuka kuendeea kuwabia wachovu watu na kutajiika wakati sisi tikipigika kwa ukapa. Niseme wazi. Nakubaiana na wae wanaoita huu kuwa aina mpya ya ufisadi na ujambazi wa kumtumia Mungu.”
            Kanji hajivungi. Anakwanyua mic “mimi iko sangaa sana. Naona chungaji hubiri lakini hapana nafanya kazi. At the end nakuwa tajir sana. Nazidi hata ile nafanya biasara. Sana napata wapi juluku? Iko uuza neno na kupata juluku au iko biasara nafanya sirini?”
            Mpemba anakamua “yakhe hapa unkuna kweli kweli. Hata mie nshangaa kuona watu wasiofanya kazi yoyote isipokuwa kupiga kelele kuishi kwenye mahekalu, kununua hata madege na kuishi maisha ya kikwasi. Hapa lazimu iwepo biashara waniyofanya nyuma ya pazia wallahi.”
            Da Sofia Lion aka Kanungaembe anampoka Mpemba mic na kudema “kumbe hamjui! Baada ya dokta Kanywaji kuwabana wapigaji, sasa dili limebakia kuwa kuanzisha madhehebu ya dini. Hapa ndipo hitajio la kuchunguza maisha yao binafsi linakuwa muhimu. Lazima wataje vyanzo vya mapato na matumizi yao hasa wakieleza zinapokwenda sadaka. Hamkuona mmoja alivyofikishwa kwa pilato akidaiwa kuiba bilioni 15 za waumini? Kimsingi, hawa hawana tofauti na waganga wa kienyeji. Hawahubiri kuchapa kazi, uadilifu wala ukweli bali uponyaji utadhani kaya nzima ni ya wagonjwa. Wapo matapeli wanaojifanya kuombea ndoa, biashara hata elimu bila kujua kuwa ufanisi wa mambo haya hutegemea juhudi na si maombi.”
            Kabla ya kuendelea Mbwamwitu anamchomekea da Sofi na kusema “wao wenyewe wanapaswa kuombewa kwa ushirikina na uganga wa kienyeji na uganga njaa wanavyofanya. Na niseme hapa.  Kama kweli kuna pepo, hawa hawataingia. Wataingiaje wakati wametengeneza pepo zao hapa duniani? Kama pepo hii ipo sitaingia kama nitwakuta hawa wezi wa majoho kusema ule ukweli.”
            Mheshimwa Bwege anapoka mic “msemayo ni kweli. Nakubaliana nawe Mbwamwitu. Hawa wezi walishajitengenezea pepo zao hapa hapa duniani kwa kuwaibia wachovu. Angalia migari, mijumba na wengine midege wanayoangusha wakati Yesu wanayemhubiri alikuwa kapuku wa kutupwa. Je wanamhubiri Yesu yupi zaidi ya farao tajiri mwenzao? Biashara ya kuchuna inalipa. Unajenga duka na kuliita nyumba ya ibada. Unaweka mabenchi na wajinga wanafurika kulipa kodi wakidhani ni sadaka. Miaka nenda rudi wanamchangia Mungu. Mungu gani maskini asiyejajirika pamoja na kupewa sadaka miaka yote hii. Je yeye atatoa lini? Haiwezekani Mungu akageuzwa pakacha lisiloshiba wakati ukweli Mungu mwenyewe ni hao hao wanaowanyonya wachovu wa kaya hii. Ama kweli wachovu hawa wanahitaji ulinzi wa lisirikali hata kama wanaibiwa kwa ujinga wao na kutojiamini.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita mzee wa Upayuko akiwa amelewa chakari akitukana na kumwaga radhi! Acha tumtokee na kudai arejeshe chetu!
Chanzo: Tanzania Jumatano leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:07 No comments:

Sunday, 27 November 2016

Nchi ya viwanda Escrow, UDA, NSSF nk wapi na wapi?

          Baada ya rais John Pombe Magufuli kuingia madarakani na kukuta madudu na mdororor wa uchumi, alikuja na mipango ya kuifanya Tanzania nchi ya viwanda. Magufuli, pamoja na mengini, alilenga kutengeneza ajira, kufufua uchumi, kuwezesha watanzania kupata huduma safi na kufaidi raslimali za nchi yao na kuboroesha maisha ya watanzania.
            Pamoja na mipango na nia nzuri vya rais, kuna mambo yanapaswa kuwekwa wazi kabla ya kuendelea kujiaminisha kuwa tunaweza kujenga Tanzania ya Viwanda bila kuyakabili bila simile. Yafuatayo ni mambo yanayopaswa kuzingatiwa katika safari yetu ya kwenda nchi ya viwanda:
            Mosi, kwanza tuunde sera ya kitaifa ya viwanda bila kutegemea sera ya chama kinachotawala. Hapa lazima tubadili katiba na kutamka wapi Tanzania inapokwenda na itafanya hivyo vipi. Kwani, kwa sasa, sera ya viwanda ni ya kisiasa na si ya kiuchumi. Mpaka sasa si rahisi kuelezea Tanzania inatumia mfumo na sera zipi zaidi ya ujamaa unaoendelea kubakia kwenye katiba wakati haupo tena.
            Pili, lazima tuliandae taifa kwenda kwenye nchi ya viwanda. Mfano, tueleze tutakavyovuna nguvu kazi iliyopo na kutengeneza wataalamu wa kutufikisha kule. Hata nchi ya Ulaya zilipoamua kufanya mapinduzi ya viwanda (industrial revolution), pamoja na kutumia nguvu kazi ya bure ya watumwa, zilijiandaa kupata na kuvuna nguvu kazi hiyo. Kwa sasa utumwa haupo tena. Tuna watu wetu; tuwaandae na kuwatumia vilivyo. Kwani mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe. Je tumewaandaa wananchi wetu kwa kuijenga nchi ya viwanda au tutategemea wawekezaji wasioaminika na ambao wanaweza kuondoka wakati wowote maslahi yao yanapoguswa?
 Tatu, lazima tupambane na ufisadi kwa maana ya kupambana bila kubagua, kubangaiza, kuonea wala kupendelea.
            Nne, tuangalie kama sheria zetu zinapambana na ufisadi na wizi wa mali za umma na makosa yatokanayo na hayo. Kama hazifai tuzibadili au kutunga mpya na kufuta nyingine.
            Tano, tumifunze toka kwa nchi zilizotoka kwenye mazingira kama yetu. Kwani, nchi ya viwanda kama China haijengwi kwa woga na matamanio bali mipango madhubuti na ya makusudi.  Huwezi kujenga nchi ya viwanda wakati huandai maisha ya kuzalisha na kukusanya kodi vilivyo. Tunapaswa kuwashughulikia wote wanaotukwamisha na waliotukwamisha bila huruma. Hapa lazima wahusika wafilisiwe na watanzania wawe na mfumo wa kila mmoja kutoa taarifa za kodi na mapato kila mwaka ili kubaini wanaotuibia na kutukwamisha. Huwezi ukajenga nchi ya viwanda katikati ya kashfa kama EPA, Escrow, NSSF, UDA na nyingine nyingi ambazo karibu tawala zote zimeonyesha kuzigwaya au kuzivumilia kwa sababu wajuazo wahusika.    
            Sita, nchi ya viwanda inahitaji mtaji ambao nao unaibiwa na tunaangalia au kusuasua kushughulikia majizi yanayojulikana kwa sura na majina. Hivi kashfa tajwa hapo juu zilisababisha taifa hsara ya mabilioni mangapi? Je fedha hiyo ingejenga viwanda vingapi au kusaidia kuweka msingi wa viwanda nchini kama ingesimamiwa vizuri au kuwakamata wahusika wakairejesha?
             Saba, je tunahofia nini na tunamdanganya nani kwa kutaka kujenga nchi ya viwanda bila sera ya kitaifa iliyowekwa kwenye katiba ya nchi? Haiwezekani tukashughulikia kashfa ya NSSF kwa kuchagua. Inakuwaje, kwa mfano, aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa NSSF ateuliwe balozi badala ya kuchunguzwa kusikia ana ushahidi na utetezi upi kuhusiana na kashfa iliyotendeka chini ya uangalizi wake?
            Nane, kama ilivyodokezwa hapo juu, China imepiga hatua kwa kasi ya ajabu kiuchumi kutokana na kasi ya ajabu katika kushughulikia ufisadi na wizi wa mali ya umma. Imeishafunga vigogo zaidi ya milioni moja tangu idhamirie kubadili mwelekeo wa maendeleo yake. Zamani nchini China ukiwa kwenye chama tawala basi umeula na huguswi sawa na ambavyo ilivyo nchini ambapo baadhi ya wazito wanatuhumiwa hata kusafirisha nyara za taifa ughaibuni na bado wako ofisini ukiachia wale waliotuhumiwa wazi wazi kujihusisha na mihadarati.
             Kwa mujibu  wa Kamati kuu ya Ukaguzi wa Nidhani ya China (CCDI), serikali ya China  imeanzisha kampeni tangu rais Xi Jinping  achukue usukani wa  Chama  Kikomunisti cha China (CCP) mwishoni mwa mwaka 2012, maafisa wa ngazi za juu 414,000 wameishawajibishwa na chama kwa ufisadi; na maafisa wapatao 201,600 walishashitakiwa. Mfano kwenye mkoa wa Shanxi, mmoja wa mikoa fisadimaaafisa wapatao 15,450 walipatikana na hatia mwaka jana ambalo ni ongezeko la aslimia 30 ikilinganishwa na mwaka 2013.  Kauli mbiu ya inaelezea hatua hii kama kuua chui na kupunga inzi.
            Tisa, ukiangalia maendeleo ya kupiga vita ufisadi iliyofikia China, kwetu ni kinyume. Tunaua inzi na kupunga mapapa. Vinginevyo walioko nyuma ya kashfa tajwa hapo juu wangekuwa wameishauwa na si kupungwa.
            Kumi, na mwisho, tunasisitiza kuwa lazima tubadili katiba na kuja na katiba mpya ya uwajibikaji na uchapa kazi badala ya kutegemea nguvu ya kisiasa chama au mtu mmoja. Nchi ya viwanja inajengwa na wananchi wote wanapotambua na kujua wanachotaka na wanachotaka kufanya.
Nashauri tuanzie kwa haya machache, pamoja na mengine, kuiandaa Tanzania kwenda kwenye nchi ya viwanda.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:35 No comments:

Saturday, 26 November 2016

Miaka mitatu bila Dk Sengondo Mvungi

 
            Leo ni miaka mitatu na siku chache tangu Dk Sengodo Mvungi afariki dunia.  Kwanza, niwatahadharishe wasomaji wa safu hii. Makala hii nimeiandika nikiwa soba kabisa bila kupata kitu chochote. Hivyo, msishangae mkidhani nimedesa kwa mtu. Hii inaonyesha sura yangu ya pili ambayo wengi hawaijui. Hayo tuyaache.
            Japo Mvungi alizikwa, kuombolezwa hata kupendwa na wengi, sijui kama bado wengi hao wanamkumbuka. Sijui kama wanakumbuka yale mema yote aliyosimamia na kutenda.  Sijui kama wanamkumbuka kama moja wa watu waliosukuma taifa mbele taifa. Sijui kama kama ndani ya kipindi kifupi tu cha miaka mitatu aliyotoweka angesahaulika kirahisi hivi hasa kwa wale walioangusha kazi pevu aliyofanya. Kusema ukweli; kitendo kilichofanywa cha kuzika Katiba Mpya ni dharau ya aina yake kwa marehemu Dk Mvungi. Kwa utamaduni wa kiafrika, mja anapoaga dunia, waliosalia hupenda kuyaenzi yale aliyoyatenda hasa katika mwisho wa uhai wake.  Hata hivyo, tokana na dhuluma na dharau hii, sijui kama hao watukufu bado wana hamu naye kwa namna wanadamu tulivyo wasahaulifu kana kwamba kuna watakaoishi milele.  Dk Mvungi aliyefia nchini Afrika Kusini mnamo 21 Novemba, 2013 wakati akifanyiwa matibabu baada ya kushambuliwa na majambazi nyumbani kwake. Heri wangemwimbia wakamwachia uhai wake ili aendelee kulitumikia taifa lake na watu wake bila kinyongo wala kuchoka katika nafasi zote alizotumika nchini. 
            Kwa tunaomfahamu na kumkumbuka, Mvungi alikuwa msomi mbobezi wa sheria, mchangamfu, asiye na makuu ambaye angeweza kujichanganya na makapuku bila kujali hadhi yao kimaisha, mwanasiasa na mtetezi wa haki za binadamu wa kupigiwa mfano. Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC) wanalifahamu hili na ni mashahidi tosha wa umahiri wa Mvungi katika kutetea haki za wanyongo. Mbali na hiyo, mchango wake katika kuandika Katiba Mpya iliyouawa na mafisadi haumithiliki ingawa umesahaulika kutokana na kuzikwa kwa katiba husika na majahiri wasiojua kuwa siku yao nao ipo. Wale waliofanya kazi naye kwenye tume hii wanajua umahiri na kujitoa mhanga kwake kwa niaba ya wenzake. Wale waliobahatika kukutana naye iwe ni kikazi au nje ya kazi, ni mashahidi tosha wanaoweza kumweleza marehemu Mvungi alivyokuwa mtu wa watu. Kwa maana hiyo, wengi walidhani; wenye mamlaka walilomteua kuwa mjumbe wa kamati ya kukusanya maoni ya wananchi ya Katiba Mpya wangeipitisha tena bila kuichafua na kuichakachua kama njia mojawapo ya kumuenzi mzalendo huyu mtoto wa taifa hili aliyelipenda bila shaka yoyote. Hata hivyo, hii haikuwa. Ni kiburi na kujilisha pepo kiasi gani? Kwani, wao wataishi au kudhulumu milele? Binadamu ni nini zaidi ya kuwa mavumbi yanayongoja kutawanyishwa na upepo na wadudu?
            Dhumuni ya kuandika waraka huu–licha ya kumkumbuka Mvungi angalau iwe faraja kwake, familia yake, marafiki zake na wapendwa wake–nalenda kumrejesha kwenye hadhira lau kutafakari urathi alioacha kama mwadamu muadilifu na mpenda na mtetea haki. Najua hawezi kujibu waraka wangu; lakini anaona. Kwani walichoua ni mwili si roho ya marehemu. Katika kumbukumbu yangu ya Dk Mvungi, licha ya kuongea na wasomaji, naongea na wenye madaraka watende haki kama sehemu ya kumuenzi Dk Mvungi aliyekuwa mpigania haki mahiri na asiyechoka.
            Pili, tupambane na ujambazi na kila aina ya jinai vilivyotamalaki nchini mwetu. Kwani, kilichomuua Mvungi si kingine bali ujambazi huu huu ambao utawala uliopita ulionekana kuridhika nao kiasi cha kuulea kutokana na serikali kuwa goigoi na iliyokuwa ikijiendesha bila uongozi imara na wenye visheni. Sasa mambo yamebadilika. Tuna serikali mpya yenye makali angalau. Tunawaomba wenye mamlaka waliopo kulifanyia kazi hili ili tusipoteze Dk Mvungi wengine ambao taifa linawahitaji. Hatutaongelea waliomuua Dk Mvungi kwa vile kesi iko mahakamani.
            Tatu, tupambane na ufisadi na ulafi wa kimfumo unaohamasisha wahalifu kutafuta utajiri wa haraka hata kwa kuwaua wenzao. Ningependa siku moja kila mtanzania aeleze alivyochuma mali zake ili wanaopata utajiri kwa njia haramu wataifishwe na kuwajibishwa kisheria jambo ambalo bila shaka litaondoa motisha wa baadhi ya wenzetu kutenda maovu kama, kuwadhuru, kuwaua na kuwaibia wenzao.
            Nne, katika kutenda haki kwa watanzania wote, tunapaswa kurejesha kanuni na maadili ya utumishi wa umma. Maana bila kanuni hizi tutapoteza muda kwa kutegemea ukereketwa wa viongozi wachache.
            Mwisho, napenda kuiomba jamii ya watanzania popote ilipo, imuenzi marehemu Mvungi kwa kupigania na kutenda haki; vitu ambavyo vilimtambulisha ulimwenguni. Pia tunaipa mkono wa rambirambi familia ya marehemu katika kuadhimisha miaka mitatu ya kifo cha Mvungi. Najua wao huadhimisha maisha ya marehemu kila sekunde, kila dakika, kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka. Nawaombea faraja katika safari hii ngumu yenye kila majaribu na kukatisha tamaa. Faraja kubwa ni moja kuwa yeye alitangulia, sie tuko nyuma yake. Kwa wale waliozoea ulevi naomba wanisamehe. Huu ni msiba. Auhitaji utani hasa ikizingatiwa kuwa kila nafsi itaonja mauti.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 09:20 No comments:

Wednesday, 23 November 2016

Kijiwe chashangaa wanaoshupalia njuluku ya tetemeko


         
            Wiki jana baada ya vyombo vya umbea kusheheni malalamiko ya wahanga wa tetemeko kule kwa akina Nshomile, Kijiwe kimeamua kuingilia kati lau kutoa elimu na ushauri vya bure.
            Leo anayeanzisha mada ni Mipawa tokana na baadhi ya marafiki zake aliokwenda nao shule kukumbwa na tetemeko ikiwemo shule alikosomea kidato cha tano na sita kabla ya kwenda Ng’ambo kunyaka shahada zake nyingine. Anaonyesha gazeti la Rongorongo lenye kichwa cha habari “Wahanga wa Tetemeko waijia juu Lisirikali.”
            Anatongoa “mmeona hii kasheshe kati ya wahanga na akina Nshomile baada ya lisirikali kusema kuwa njuluku iliyokusanywa itaelekezwa kwenye ujenzi wa miundombinu badala ya mbavu za mbwa binafsi? Jamaa wanapokoma kama hawana akili nzuri.”
            “Kwa lisirikali la sasa watalia sana na wamechemsha. Si rahis keshasema kuwa si kazi ya lisirikali kunjengea mchovu; sasa wanadhani malalamiko yatasaidia,” anachomekea Mbwamwitu.
            Msomi Mkatatamaa anakula mic “hapa nakubaliana na lisirikali. Kwani miundombinu ni muhimu kuliko wachovu binafsi. Nadhani wanaolalamika–pamoja na kuwa ni haki yao kufanya hivyo–wanapaswa kujiuliza baadhi ya maswali hata kama si ya kufurahisha. Mfano, mbona mbavu zao za mbwa zilipopukutishwa na tetemeko, wengi licha ya kulilalamikia na kupata misaada toka kwa lisirikali hilo hilo wanaloliaani sasa walitegemea miundombinu hiyo hiyo hiyo kama vile mashule, barabara, kliniki na mahospitali kupata huduma za kwanza, kujihifadhi na hata baada ya hapo? Mnyonge mnyongeni; lakini haki yake mpeni jamani.”
             Kabla ya kuendelea Mgoshi Machungi anamchomekea na kusema “Kwei Mgoshi, shue ni bora kuiko ubavu wa mbwa wa mchovu binafsi.  Nadhani badaa ya kulaamika, waathiika wanapaswa kukaa na seikai na kuangalia namna ya kusaidiana akini siyo kuazimishana na kutoa laana bue.”
            Kapende aliyekuwa ndiyo anamaliza kusoma gazeti la Rongorongo anakatua mic, “nasikia lisirikali lilikusanya madafu kama bilioni 15 na ushei. Kwa wachovu maskini wanadhani hii njuluku ni kubwa na lukuki wasijue gharama ya miundombinu usipite. Hebu fikiria mfano kujenga barabara moja yenye urefu wa kilometa kumi toka njini Bukoba kwenda huko kwa waathirika ni bei gani?”
            Kabla ya kuendelea, Da Sofia Lion aka Kanungaembe anadakia “hapa hujaongelea shule, hospitali, zahanati, na miundombinu mingine. Hapa wajanja hawajapiga chao hasa ikizingatiwa kuwa kaya yetu ina ugonjwa wa kuwa na vitu hewa.”
            Leo inaonekana ni kuchomekea mtindo mmoja. Kwani kabla ya da Sofi kumaliza si Mchunguliaji anamchomekea akisema “sitashangaa kusikia kuna wahanga hewa, na madai hewa bila kusahau, misaada hewa. Mara hii wahanga wamesahau wapigaji waliokuwa wameishafungua akaunti kujipatia njuluku za dezo! Ama kweli kufa kufaana. Lazima na serikali iboreshe miundombiu yake hata kama ilikuwa imeishabomoka hata kabla ya tetemeko kuimalizia au vipi?”
            Kanji anaamua kula mic “Sahili iko penda sana lalamika sana. Sasa dugu yangu tetemeko naangusa jumbani yako veve lau sirkali diyo naangusa? Je kama sirkali haikotangaza tetemeko, hiyo saada veve iko weza pata bila sirkali tangaza na kusimamia ili janja chache isiibe saada?”
            Mpemba aliyekuwa kimya akisikiliza anaamua kula mic “mie ndhani watu wafanye tathmini kwanza. Pia waangalie kipi cha kupata kipaumbele kwanza yakhe. Huwezi jenga nyumba ya Shaame au Makame kabla ya kujenga shule wala hospitali ati. Hivi kama tetemeko likirejea, hawa wanaolalamika watanlalamikia nani kutaka nsaada kama siyo hiyo hiyo sirikali waniyoilaumu sasa? Hapa zahitajika busara na subra vinginevyo twaweza shikana uchawi na hilo siyo jibu ati.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kula mic “mie silaumu wahanga wala lisirikali. Naweza kusema tu kwa ufupi kuwa usawa huu wa kuadimika njuluku, kila mmoja analalamika hata wale waliozoea za kupiga na wavivu. Je kama hawa wanaolalamika hawajakumbwa na janga lolote zaidi ya kukatwa mirija yao, hawa wahanga wa tetemeko usawa huu unategemea wafanye nini? Nadhani lisirikali lingeacha ung’ang’anizi. Kama wahanga wataona kuwa mbavu zao za mbwa kwao ni muhimu kuliko miundombinu, basi ikae nao na kuwaelimisha juu ya nini kinahitajika kwanza badala ya kuwaacha Solemba wakilalamika. Nadhani hapa hakuna kilichoharibika zaidi ya mawasiliano haba. Kama wakubwa wa lisirikali watakutana na wahanga na kuwapa sababu za kutoa kipaumbele kwa miundombinu wataelewa na kukubali yaishe huku wakijipa matumaini na kungoja zamu yao au vipi?”
            Mgoshi Machungi anarejea na kukatua mic “hapa azima isiikai iseme ukwei vinginevyo wahanga watazani imekula ushwa kama yue bwana mdogo Makondakonda aiyewahifadhi wahaifu akijidai kakataa ushwa bila kueeza namda aivotaka kuhongwa njuuku iii aluhushu shisha.”
            Msomi aliyekuwa akibofya kisimu chake anamchomekea Mgoshi “sasa Mgoshi hili la dogo Makondakonda kuchemsha na kuramba mlungula linaingiaje au umechanganya madawa au vipi?”
            Mgosi anagundua alivyochemsha na kuamua kujitetea “kwei kaka nimechemsha. Unajua wakati mkizoza niikuwa namtumia meseji bi mkubwa Nesaa ujumbe kuwa aniandaie ie mboga ya kishambaa iitwayo kinyeto. Shamahani ndugu zangu kwa kuchemsha. Hizi simu nazo!”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si ikapiga radi! Acha tutoke mkuku tukidhani ni tetemeko jingine!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 08:17 No comments:

Saturday, 19 November 2016

Magufuli unangoja nini kumtumbua Makonda?

         Mheshimiwa rais John Pombe Magufuli,
                 Najua unajua kuwa hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makond alitoa mpya ya kufungia mwaka. Makonda alikaririwa na vyombo vya habari akidai kuna wafanyabiashara wa shisha (kumradhi sijui maana yake) wapatao 10 waliomwendea na kutaka kumhonga shilingi 5,000,000 kila mwezi kila mmoja akakataa.  Madai haya, licha ya kushangaza, yamezua maswali mengi kuliko majibu. Je ni kweli kuwa Makonda alikataa rushwa hii au inaweza kujenga dhana kuwa alisema haya ili aonekane safi na kupata sifa kirahisi?  Mosi, tokana na uzito wa shutuma hizi, basi wengi wangetaka Makonda awataje hadharani wahusika ili sheria ichukue mkondo wake. Pia ingekuwa vyema Makonda aeleze ni kwanini hakuwawekea mtego wakakamatwa?
Pili, Makonda, awaombe radhi aliowatuhumu bila ushahidi wala sababu za msingi zaidi ya kile kinachoweza kutafsiriwa kama kutaka kujijengea umaarufu kwa kuwachafua wengine. Maana kufanya hivyo kunawaonyesha kama wala rushwa na mawakala wa shisha bila sababu na ushahidi vya kutosha. Nitashangaa kama wahanga hawatamchukulia hatua za kisheria Makonda. Wasipofanya hivyo, watakuwa wanathibitisha ukweli wa madai ya Makonda.
Tatu, je kwanini Makonda, kama hakuwa na maslahi na biashara hiyo aliamua kuwaficha wahusika wakati akijua kuwa ni wajibu wa kila mtanzania kulipoti kosa la jinai anaposhuhudia ima likitendeka au likiwa katika harakati za kutendeka?
Nne, je kama mkuu wa mkoa kama Makonda analalamika lalamika, hao wa chini–ambao wengi wao ni waathirika wa jinai hii–wafanye nini?
Tano, je Makonda huwa anajitahidi kuruhusu kinywa na ubongo viwasiliane kabla ya kunena; au ndiyo hayo hayo ya kujisemea kila kinachotoka ima kujijenga, kujifurahisha na kuifurahisha hadhira yake?
Sita, kama Makonda atashindwa kuwataja wahusika, basi awajibishwe mara moja ima kwa kuwaficha wahalifu au kutaka kuuongopea umma kwa faida binafsi. Hatuwezi kuendelea na kuuzoea mchezo huu ambao madhara yake yanaweza kuwa makubwa huko tuendako. Kwa kauli kama hizi, umma unaweza kuishiwa imani na serikali, jambo ambalo si jema kwa nchi.
Saba, hata hivyo, Makonda ana bahati kuwa aliyemweleza, yaani waziri mkuu Kassim Majaliwa alichukulia tuhuma zake kimzahamzaha kama si kumuonea huruma na kumuepusha na aibu. Vinginevyo, Waziri Mkuu–kama naye angeamua kuwajibika kwa wadhifa wake–bila shaka alipaswa kumtaka awataje wahusika au kutoa kueleza ni kwanini hakuvitaarifu vyombo husika ili viwashughulikie.  Hapa napo Waziri Mkuu alionyesha udhaifu mkubwa kiutendaji.  Nadhani aliyosema Makonda, kama angeyasema mbele yako, ungemtaka awataje pale pale vinginevyo atumbuliwe; vinginevyo angetumbuliwa yeye. Rejea ulivyokataa taarifa, tena kwenye msiba, kuwa meya wa zamani wa jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi alikuwa na mke mmoja wakati alikuwa nao wengi tu.
Nane, je fungate ya Makonda inaanza kuisha kiasi cha kuanza kufichua kilichoko nyuma ya pazia ya Makonda waliyezoea kumuona watanzania? Maana madai ya Makonda; na namna alivyoshughulikia hii rushwa ni ya ajabu na ushahidi kuwa kuna tatizo tena kubwa tu.
Tisa, ikumbukwe. Hii si mara ya kwanza Makonda kulalamika bila kufuata hata utaratibu. Nani amesahau namna alivyomchomea utambi Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam wa zamani marehemu Wilson Kabwe badala ya kufuata utaratibu? Nani amesahau Makonda alivyowahi kuwaweka ndani watumishi wa Manispaa ya Kinondoni?
Kumi, mchezo wa kujisemea na kutoa madai ya ajabu si jambo jipya kwa baadhi ya watendaji wa juu wa serikali ya awamu ya tano. Rejea hapo mnamo mwezi Machi mwaka huu waziri wa Ardhi, William Lukuvi, kama Makonda, alikuja na madai kuwa kuna wafanyabiashara wawili walanguzi wa ardhi walitaka kumhonga shilingi bilioni tano akazikataa bila kuwawekea mtego wakamatwe wala kuwa tayari kuwataja majina.
Hivi kweli Makonda hajui kuwa kumshawishi mtu tena kiongozi wa juu kama yeye kupokea rushwa ni kosa la jinai?  Je hapa Makonda haoni kuwa alitenda kosa la jinai kwa njia ya kutochukua hatua (omission) kama raia na kiongozi? Usomi wake sasa ni wa nini kama hajui vitu rahisi kama hivi? Tokana na ukali na kutenda haki vilivyoonyeshwa na serikali ya awamu ya tano, nakushauari umtumbue Makonda mara moja ili liwe somo kwa wengine wanaodhani vyeo ni sehemu ya kuchezea na kujifanyia mambo watakavyo hata kwa kukiuka wazi sheria. 
Nimalizie kwa kumtaka Makonda auambie umma ukweli na kwanini hakuchukua hatua kama si mnufaika wa jinai aliyoieleza. Hakuna haja ya kuwang’ang’ania viongozi wa aina hii hasa ikizingatiwa kuwa kuna watanzania wengi wenye sifa tosha. Huu hakika ni mtihani kwako hasa ikizingatiwa kuwa ulimtumbua Mkuu wa zamani wa Mkoa wa Shinyanga Anna Kilango Malecela kwa kueleza umma uongo. Itashangaza kama utamvumilia Makonda. Maana, hii itaonyesha kuwa kuna wasioguswa katika serikali ya awamu ya tano jambo ambalo si zuri na linaloweza kuchafua sifa nzuri ya seriakali husika katika kuwatumikia na kuwakomboa watanzania toka kwenye uovu na uoza uliokuwa umeanza kuzoeleka.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 16:19 No comments:

Je Tanzania inao wageni wanaohodhi ardhi wangapi?


 
            Hakuna ubishi. Chini ya utawala rais mstaafu Benjamin Mkapa, Tanzania ilipwakia uwekezaji bila maandalizi wala ujuzi wa kile ulichokuwa ukiingia. Mkapa atabaki kwenye vitabu vya historia ya Tanzania kama rais aliyeuza nchi kwa wawekezaji. Hili unaweza kuliona kwenye kashfa zilizohusisha uwekezaji zilizofumka wakati wa utawala wake. Jikumbushe iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) iliyouzwa kwa ABSA Group ya Afrika Kusini kwa bei ya kutupwa na kifisadi. Rejea mdororo wa Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) lililowekwa chini ya uendeshaji wa kampuni ya Afrika Kusini. Rejea kuuzwa kwa viwanda vingi vilivyoishia kuwa mabohari na vingine kunyofolowa vifaa hadi juzi tu rais John Magufuli alipoamuru wenye kuvifuja kuviendeleza kabla hajavitwaa.
            Kwa ufupi, uwekezaji chini ya Mkapa ulikuwa ni wa kijambazi na kifisadi uliotokana na rushwa ambao uliliingiza taifa kwenye mdororo wa kiuchumi jambo ambalo baadaye Mkapa alijutia. Alilwahi kukaririwa akisema “kwenye uongozi wangu kitu ambacho mpaka sasa ninajuitia ni kuanzisha sera ya ubinafsishaji na kushindwa kuweka mfumo au chombo cha kuudhibiti.”  Kwa kushindwa kuudhibiti uwekezaji, Mkapa alijenga tabia chafu ya kuabudia wageni ambao kwao wanasifika kuwabagua watu weusi.
            Mbali na Mkapa, utawala wa Jakaya Kikwete ndiyo ulivuruga kila kitu. Kwani, Kikwete alipokuwa akifanya kampeni, aliahidi kurekebisha mikataba ya uwekezaji. Hata hivyo, baada ya kuingia madarakani wala hakufanya hivyo. Badala yake alianzisha utawala wa hovyo ambao wengi waliuona kama uholela ambao uliiweka nchi kwenye autopilot kwa miaka yote kumi aliyokuwa madarakani akisifika kwa kuizunguka dunia akiandamana na marafiki na wapambe wasio na umuhimu kiasi cha kutunisha deni la taifa.
            Tukiacha na tawala zilizopita ambazo hazina lolote la maana kwa sasa, tuangalia hali ilivyo kwa sasa.
            Mosi, chini ya kivuli cha uwekezaji, kumekuwapo na tabia ya kuendekeza njaa kiasi cha maafisa wa serikali kugeuka makuwadi na vijakazi wa wawekezaji. Wamekuwa wakiwasaidia kukwepa kodi na kuingia mikataba ya kipumbavu kama mkataba wa TICTS ambao rais Magufuli alitaka ubadilishwe hivi karibuni badala ya kuubatilisha na kuwachukulia sheria walioingia mkataba huu wa hovyo.
            Pili, tumeendelea kuwa na mfumo mbovu wa udhibiti wa mali za umma. Mfano wa hivi karibuni ni kufutwa hati za umilki ardhi kwa Hamant Patel ambaye alighushi vyeti vya kuzaliwa na kujitwalia ardhi kinyume cha sheria. Je huyu Patel, hata kama angekuwa mtanzania wa kuzaliwa, aliruhusiwaje kuhodhi ardhi kila mahali? Je tunao patel wangapi walioodhi ardhi yetu na kuifanyia biashara huku wakiishi nje wakati hakuna mswahili anaweza kupata hata inchi moja huko watokako?
            Kumekuwapo na ukurupukaji katika kushughulia kadhia zinazotokana na uwekezaji na wizi mwingine wa mali na raslimali za umma. Mfano, tunaambiwa Patel amefutia hati. Je alikamatwa na kujibu tuhuma? Je waliomwezesha wamebainiwa, kukamatwa na kushughulikiwa?
            Nne, je nini kifanyike? Fanyeni ukaguzi mpya wa ardhi na raslimali zote ambazo majambazi wa kigeni wamezoea kuzitumia kukopea na kuishi ughaibuni kwa starehe. Ni bahati mbaya kuwa taifa letu lina tatizo la kusahau na kutojifunza kutokana na historia na makosa yake. Uozefu unaonyesha; hatukujifunza tokana na kashfa na hujuma ya Chavda aliyemilkishwa mashamba ya mkonge akaishia kuyatumia kujipatia mikopo na kutoroka nchi.
            Tano, tujibu maswali makuuu yafuatayo:
            Mosi, ilikuwaje huyu Patel hakuitwa na kukamatwa kwa makosa ya kujipatia ardhi na nyaraka kinyume cha sheria ili lau aonje joto ya jiwe na liwe somo kwa wahalifu wengine?  Bila kuwa na kuwaadhibu wahalifu waliokwishathibitika, tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu.
            Pili, je tunao majambazi kama hawa kiasi gani nchini wakichezea mali zetu wakati watu wetu wanaendelea kuangamia kwa ujinga na umaskini?
            Tatu, je ni nani hao waliompatia nyaraka na kumpa umilki wa ardhi? Haya ni maswali ambayo yalipaswa kujibiwa kabla ya kumstua mhalifu huyu. Je waliochukua hatua hii ya pupa na hasara kwa taifa hawakujua vitu rahisi kama hivi; au kuna namna kama siyo watu wasio na sifa na ujuzi kupewa nyadhifa nyeti kama hizi?
            Nne, je tutaendelea kuwa shamba la bibi hadi lini? Inashangaza kuona taifa lililojaliwa raslimali lukuki kuzidiwa hata na viinchi vidogo na visivyo na raslimali hata nusu yetu.
            Tano, je nini kifanyike? Kagueni hati zote za kuzaliwa za watanzania. Mchezo wa wageni hasa wahindi kuja kununua vyeti vya kuzaliwa nchini ukiachia mbali paspoti ni biashara inayojulikana kuwapo muda mrefu tena wakisaidiwa na watanzania wenzetu waroho umezidi kuzoeleka kiasi cha kuwa janga la kitaifa. Nadhani tunapaswa kupambana na genge hili na kulitokomeza kwa kuwafunga walioko nyuma yake vifungo vya maisha ili liwe somo kwa wengine.
            Sita, tungeni sheria kali ya kuhakikisha wanaokamatwa na mawakala wao wanafia gerezani. Bila kuwa na sheria kali za kupambana na jinai hii, hata hii amani tunayojivunia itatokea. Wananchi watakapojua kinachoendelea, watajichukulia sheria mkononi. Tumeishasikia wengi wakivamia mashamba na kujitwalia baada ya kugundua yalichukuliwa kifisadi.
Je namna hii twaweza kusonga mbele kiuchumi wakati ardhi na mali zetu zinatwaliwa na mahalifu wa kigeni na kuacha watu wetu wakiendelea kuteketea kwa umaskini? Je tunao akina Patel wangapi?
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 16:17 No comments:

Mlevi afuta safari kwenda kutibiwa Ughaibuni


 
            Baada ya rais Joni Kanywaji Makufuli kuonekana kwenye hospitali ya kaya ya Muhimbiza akimjulia hali mshirika wake wa bedroom, Bi mkubwa Jane, mlevi ambaye bi mkubwa wangu alikuwa akitarajiwa kuondoka kayani kwenda kutibiwa ughaibuni nilijihisi kushushuka na kuona aibu. Nilipiga moyo kondo na kujisuta; ndipo nilipoamua kumkabili Bi Mkubwa wangu Mama Domokubwa kumpasha kuwa hatakwenda kutibiwa ughaibuni.  Kama kawaida yake, aliamka na kunikaba shati kuuliza kulikoni naongea kama hamnazo. Alidhani wazo hili lilisababishwa na mma na yale majani ninayovuta. Baada ya kuninusa na kukuta sina harufu ya zali lolote ilibidi aniachie. Alijifunga kibwebwe na kushika kiuno. Aliuliza tena “we baba Shikaadabu, unayosema ni kweli au umeanza kunitania siku hizi?” nilimjibu kwa kumpa gazeti la Sema Nao la siku ile lililobeba picha ya Bi Nkubwa Jane akiwa kwenye lango la kutokea la  wodi ya Sewa al Haji. Stori ni ndefu  na ina mivutano na misutano kibao.
            Kwa ufupi, tokana na somo nililopata tokana na kitendo cha Bi Nkubwa Jane kupiga mbonji kwenye Hospitali uchwara, rasmi na wazi wazi, natangaza rasmi kwa walevi wote. Mshirika wangu wa bedroom hatakwenda ughaibuni kutibiwa wala kuchekiwa afya yake baadaye. Badala yake atakwenda kutibiwa Muhimbiza; na siku zote zijazo, atakuwa akichekiwa afya yake pale. Nadhani hii licha ya kuwa kuunga mkono spirit ya rahis, ni kutaka kuwaaminisha walevi ninaowaongoza kuwa ninasema ninayotenda na kutenda ninayosema kuhusiana na uzalendo na kuacha ulimbukeni na kujitukuza kana kwamba hakuna atakayenyotoka roho. Wangapi tumeshuhudia wakienda kutibiwa ughaibuni na kurejea kwenye jeneza? Hakuna kusiko na kifo.
            Kitendo hiki ninachopanga kufanya kitashangaza wengi wapenzi na wabaya wangu. Ukiachia bi mkubwa kwenda kutibiwa Muhimbiza, kuanzia sasa nitaagiza walevi wote wawe wakubwa au wadogo kuchekiwa afya zao kayani na si ughaibuni. Nadhani hii itawasaidia wanaohujumu huduma za jamii kuacha kufanya hivyo; kwa vile watakuwa wakijiumiza wenyewe baada ya kuziba uchochoro wa kuzihujumu na kukimbilia ughaibuni kuunguza kodi za walevi. Mbali na hilo, nitaamuru walevi wote kuacha kupwakia vitu vya nje; na badala yake nitawaamuru watumie vya kayani ili kukuza uchumi wetu.
            Pili, msishangae kusikia nikitoa amri kuwa hata vitegemezi vya walevi wote visomee kayani badala ya kupelekwa ughaibuni na kurejea na kufanya kazi kayani. Kama kuna wazazi wanaoogopa vigegemezi vyao kusomea kayani, kwanini waviamini kufanya kazi kayani? Nadhani na hii itasaidia kuwapa somo wale wanaohujumu elimu kwa kutegemea kutumia njuluku wanazopiga kupeleka vitegemezi vyao ughaibuni. Mbona biggie wetu wote waliosomea hapa kayani na wameweza kuukata wakati wengi wa waliosomea ughaibuni wengine tunawaona wakisuasua kisiasa?
            Tatu, tokana na mfano wa rahis ambao bila shaka alidesa toka kwa walevi kama sisi ambao hujinywea mataputapu ya hapa kaya badala ya kunywa wine, whisk na vinywaji vya kigeni, nina imani kuwa hata mahoteli yetu yanayoitwa ya kitalii yatajifunza hili toka kwetu. Kwa walevi ulevi ni ulevi. Unywe mimaa ya kigeni au ya kienyeji mwisho wa siku wote mtalewa na kuangusha magari, simple and clear au vipi?
            Nne, lazima tukubaliane hata kama hatutaki. Wakati wa wanene kwenda kuchekiwa mafua ughaibuni lazima ugeuke historia. Kuna mlevi mmoja alituacha hoi; alipodai kuwa kuna wakubwa walifikia makufuru hata ya kupeleka mbwa na paka wao ughaibuni kuchekiwa afya kwa kufuja kodi za walevi waliopigika ile mbaya. Hawa wangekuwa chini ya utawala wangu wangekula shaba kama siyo kutimuliwa kibarua ili wakarejee huko madongo poromoka walikotokea.
            Tano, naona hata wakati wa kupunguza mashangingi ya wanene umefika. Kwani, haiigii akilini kwa kaya ya wachovu kuendelea kununua mishangingi hata ya kupelekea mbwa kliniki na vitegemezi vya wanene shuleni. Tunamkomoa nani zaidi ya sisi wenyewe?
            Naona mhariri anaanza kusonya na kupiga kipenga cha kuniondoa dimbani. Acha niwaageni kwa kuwaomba mzingatie aya hizi nilizotoa mimi mtume wa walevi wa kaya hii. Achene ulimbukeni, ubinafsi na roho mbaya ya kufuja mali na njuluku za walevi kwenda kuchekiwa ughaibuni. 
Chanzo: Nipahe Jumamosi leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 02:33 No comments:

Thursday, 17 November 2016

Exiting the ICC: This is Lovely

source: Daily Nation (17 November 2016).
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 04:59 No comments:

Wednesday, 16 November 2016

How the West Depends on Africa but not vice versa


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 17:12 No comments:

Kama Magufuli hataki kuchimbua makaburi anyamaze


 Image result for photos of mafisadi tanzania
          Hivi karibuni, rais John Pombe Magufuli alikutana na waandishi wa habari katika siku ya kuadhimisha mwaka mmoja wa kuwepo kwake madarakani. Baada ya kuongea na waandishi wa habari, rais aliulizwa swali kuhusiana na mategemeo yake alipoingia madarakani. Akijibu swali aliloulizwa na mwandishi wa habari aitwaye Anna Kwambaza kuhusu mambo aliyoyakuta ikulu kama yalikuwa sawa na mategemeo yake, rais Magufuli, pamoja na majibu marefu, alikaririwa na akisema “nimeshughulikia changamoto mbalimbali lakini siwezi kuyafukuwa makaburi yote; kwa sababu kuna mengine nitashindwa kuyafunika, sikuja kufukua makaburi nataka kuanza na yale niliyoyakuta ili tujenge Tanzania yetu.” Hapa alimaanisha madudu aliyoyakuta Ikulu kama yalivyotendwa ima na watangulizi wake au yalivyovumiliwa kama kashfa mbali mbali ambazo zimelitikisa taifa kwa muda mrefu. Aliendelea mbele kutoa mfano kuwa ilifikia mahali ambapo meli zipatazo 60 zilitia nanga bandarini na kutoweka bila kulipa ushuru wala kuingizwa kwenye kumbukumbu yoyote. Hii ina maana kuwa nchi ilikuwa ikichezewa hakuna mfano. Je kama anachukizwa na uhujumu huu wa taifa, anashindwa nini kuunda tume ya kuchunguza kashfa hii na kuwabaini walioutenda na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria hata kukamata mali zao? Je waliotenda uovu huu hawajulikani? Je hili nalo ni kaburi analoweza kulifukua akashindwa kulifukia?
            Kwa wanaojua namna Magufuli anavyojitahidi kuelezea uovu alioukuta kwenye serikali,  wapo wanaosema kuwa makaburi anayomaanisha Magufuli, ima unaweza kuwa uchafu wa watangulizi wake au hata wao wenyewe hasa ikizingatiwa kuwa ikulu kunaishi watu . Pia wapo wanaodhani kuwa rais anamaanisha kuwa mtangulizi wake alifuja madaraka kiasi cha nchi kufikia kujiendea kama vile hapakuwa na serikali wala kiongozi wa serikali. Hii inaweza kuwa kweli au vinginevyo. Yote inategemea namna unavyoliangalia suala hili na namna unavyotafsiri na kutathmini utendaji wa tawala zilizotangulia.  Maana, kama utaangalia ukweli wa mambo kwa kuzingatia ukweli na hali halisi vitokanavyo na utawala uliopita, utapata jibu kuwa hapa kuna tatizo tena kubwa. Kinachogomba hapa ni ukweli kuwa ni kwanini Magufuli alikuwa wa kwanza kumtetea mtangulizi wake na wenzake hata wale wanaojulikana kubariki uhujumu wa taifa kwa muda mrefu ukiachia mbali ufujaji wa fedha na mali za umma kama kweli anaamisha kuweka nchi kwenye mstari kama ambavyo amekaririwa mara nyingi akisema? Je kama rais mwenye vyombo vyote vya dola analalamika na kuishia kukiri kushindwa, amechaguliwa kufanya nini? Je hao wananchi wa kawaida ambao ndiyo waathirika wakubwa wasemeje au kufanya nini? wapo wanaodhani kuwa ima rais ayafukue makaburi na wananchi watamsaidia kuyafukia au ajinyamazie na kuchapa kazi pale anapoweza badala ya kutumikia mabwana wawili; yaani wananchi na hao wakubwa wa hovyo anaowalinda kwa kugopa kufukua makaburi wakati yanajulikana yamejaa uoza unaonuka?
            Bila kupambana na ufisadi bila kuwa na simile, Magufuli atajipiga mtama mwenyewe. Kwa vile amekiri kuwa amekuwa serikalini kwa zaidi ya miaka 20, anajua kila kitu na vipi kila kitu kiliharibika. Mfano, kuna kashfa zinazojulikana kama Escrow, UDA, TICTS, na nyingine nyingi tu zinazojulikana.
            Japo hataki kuchimbua makaburi kwa kushindwa kuyafukia, inakuwaje anaruhusu makaburi yaendelee kuwatesa wasio na hatia? Tuna makaburi ambayo yanachimbuka na kufikika hasa kama atawashirikisha wananchi na taasisi zake. Kwanini, kwa mfano, tusichimbue makaburi kama NBC, Richmond, SUKITA, Meremeta, Kagoda, UDA, DART, EPA, Escrow na mengine mengi ili kuepusha vifo vya watanzania wasio na hatia ukiachia mbali waliokwishafishwa na hayo makaburi? Je kama rais mwenye kila taasisi anaogopa makaburi, ataweza kuwakabili mafisadi wenyewe wachimba makaburi ya kufichia mali zetu? Kama Magufuli ameshindwa kuchimbua makaburi, basi ajitoe na kuwaachia wenye ujasiri wa kuweza kuyachimbua makaburi na kuyafunika. Je kwanini anaogopa makaburi? Atawezaje walio hai kama vile wauza unga, majangili, mafisadi kila aina wenye kuendelea kushikilia mitandao yao ya kihalifu?
            Alipoulizwa kuhusiana na kurejea mchakato wa Katiba Mpya, Magufuli aliogopa tena kugusa kaburi kwa kusema “tutengeneze nchi kwanza, nimezunguka nchi nzima wakati wa kampeni sikuzungumzia Katiba Mpya; kwa hiyo katiba zinaweza kuwa nyingi tu lakini kwa sasa mniachwe ninyooshe nchi kwanza.” Hapa nilishindwa kumwelewa Magufuli hasa ikizingatiwa kuwa Katiba Mpya iliyofishwa na mafisadi ililenga kupambana na ufisadi na kujenga taifa la uwajibikaji. Magufuli anapaswa kufahamu kuwa nchi si mali yake binafsi. Hawezi kuinyoosha kwa mapenzi yake bila kuwa na sheria inayomsaidia kufanya hivyo. Kama kweli anamaanisha anayosema, hana budi kurejesha mchakato wa Katiba Mpya kama watanzania walio wengi wanavyotaka badala ya kutoa visingizio. Lazima tujenge nchi kikatiba na si kwa kutegemea usongo wa mtu mmoja yaani rais badala ya Katiba Mpya ambayo ililenga kujenga taasisi zenye nguvu badala ya watu wenye nguvu katika kuendesha nchi. rais wa Marekani Barack Obama aliwahi kusema kuwa Afrika ahitaji mabwana au strong men bali taasisi imara yaani strong institutions. Na Tanzania kadhalika, inahitaji Katiba Mpya yenye nguvu badala ya rais mwenye nguvu na utashi wa kufanya atakavyo. Kama rais anaogopa kuchimbua makaburi kwa vile hawezi kuyafunika, awaachie wananchi wamasaidi kayafunika au ajinyamazie tu.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 05:33 No comments:
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Comments (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

I Love My Country Tanzania

I Love My Country Tanzania

The Curse of Salvation

The Curse of Salvation

Gen Z and Internet Revolution

Gen Z and Internet Revolution

I Cry for Ambazonia and Darfur

I Cry for Ambazonia and Darfur

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

The Story of Stories

The Story of Stories

The Chant of Savant

The Chant of Savant

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presid...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the ho...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon where...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete Pea...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaidi....
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (84)
    • ►  December (1)
    • ►  November (11)
    • ►  October (9)
    • ►  September (7)
    • ►  August (12)
    • ►  July (8)
    • ►  June (7)
    • ►  May (5)
    • ►  April (4)
    • ►  March (6)
    • ►  February (8)
    • ►  January (6)
  • ►  2024 (92)
    • ►  December (7)
    • ►  November (4)
    • ►  October (11)
    • ►  September (9)
    • ►  August (7)
    • ►  July (9)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (7)
    • ►  March (6)
    • ►  February (7)
    • ►  January (8)
  • ►  2023 (118)
    • ►  December (10)
    • ►  November (10)
    • ►  October (9)
    • ►  September (2)
    • ►  August (4)
    • ►  July (6)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (18)
    • ►  March (13)
    • ►  February (9)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ▼  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ▼  November (21)
      • Makonda na Sirro wachunguzwe wote
      • Kijiwe chamuunga mkono askofu Mokiwa
      • Nchi ya viwanda Escrow, UDA, NSSF nk wapi na wapi?
      • Miaka mitatu bila Dk Sengondo Mvungi
      • Kijiwe chashangaa wanaoshupalia njuluku ya tetemeko
      • Magufuli unangoja nini kumtumbua Makonda?
      • Je Tanzania inao wageni wanaohodhi ardhi wangapi?
      • Mlevi afuta safari kwenda kutibiwa Ughaibuni
      • Exiting the ICC: This is Lovely
      • How the West Depends on Africa but not vice versa
      • Kama Magufuli hataki kuchimbua makaburi anyamaze
      • Kijiwe champongeza Dk Kanywaji na mkewe
      • Bila kufukua ‘makaburi’ tutakufa kwa uoza
      • Kijiwe chashangaa Makufuli kuogopa ‘makaburi’
      • If Clinton loses it Michelle Obama Should Warm up ...
      • If Clinton trumps Trump Tomorrow
      • Mihadarati: Kwanini Kikwete hamsaidii Magufuli?
      • Mpayukaji aitwa kwa Joji Kichaka kupiga tafu kampeni
      • Kwa Hili, Naingia Bongolalaland Kuwekeza Ardhini
      • Magufuli aache kulalamikia maovu atumbue
      • Onyo na Ushauri: Mlioghushi Msingonje Kifo Kiwafichue
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (399)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (33)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (597)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (94)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.