The Chant of Savant

Monday 19 June 2017

KUSHITAKIWA WEZI WA ESCROW: Nampongeza Magufuli Japo NI Wajibu Wake


rugemalira.png
Watuhumiwa wakuu wa Escrow Harbinder Singh na James Rugemalira wakiwa mikononi mwa polisi
                   Taarifa tulizo nazo ni kwamba wale watuhumiwa wakuu wa kashfa iliyoliibia taifa mabilioni ya shilingi kupitia mfuko wa ESCROW, James Rugemalira na Harbinder Singh wamefikishwa mahakamani leo. Tunaipongeza serikali kwa kuamua kutoka usingizini na kuanza kufanya kazi. Maana, kashfa hii, licha ya kulitia hasara taifa, ililetea aibu na mateso hasa kwa watumiaji wa umeme.
            Tunampongeza rais John Pombe Magufuli kwa kuthubutu. Tunamsihi hata kwenye kushughulikia marais wastaafu waliofanya ufisadi kama vile Jakaya Kikwete na Benjamin Mkapa aachane na kuwaramba miguu. Maana kufanya hivyo kutamuonyesha kama mtu msafi na mwenye nia ya kupambanan a ufisadi kwa haki na si kwa upendeleo, woga na unafiki.

No comments: