The Chant of Savant

Thursday 8 June 2017

Huu ni Ubinafsi, Ulimbukeni, Upofu au Utukufu?

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, akichoma
Watawala wetu mara nyingi hutuaminisha kuwa tuko sawa na wao. Hutuaminisha kuwa wanatutumikia sisi siyo kututumia. Wanahubiri usawa na kutenda ubaguzi. Picha hiyo hapo juu anaonekana makamu wa rais Samia Suluhu Hassan akichoma nyavu haramu. Hilo ni jambo jema. Ukiangalia walioshuhudia wote hawajafunikwa pua zao. Aliyefunikwa ni makamu wa rais. Je yeye na hao wanaoshuhudia wako sawa? Je ana aleji? Je wanaomshauri Makamu wa rais wamempa ushauri juu ya madhara ya kujionyesha kama binadamu zaidi ya wenzake. Sijui kama bosi wake rais Magufuli angefanya hivyo.

No comments: