The Chant of Savant

Thursday 5 November 2015

Samia Suluhu Hassan ni nani?



Pamoja na kujua kuwa Bi Samia Suluhu Hassan ndiye makamu wetu wa rais na mwanamke wa kwanza nchini kushika wadhifa huu, wengi hatujamfahamu vizuri. Kwa mfano, katika sherehe za kuapishwa kwake na rais John Magufuli tulionyeshwa wana familia ya Magufuli. Ajabu, tangu ateuliwe kuwa mgombea mwenza hadi kuwa makamu wa rais, habari za familia zake ni kama hazipo. Unapokuwa kiongozi wa umma lazima mambo yako mengi yawekwe wazi. Kwa mfano, tunamjua mke wa rais Magufuli kuwa anaitwa Janet. Sambamba naye hatumjui mume wa bi mkubwa huyu. Je ni single, ameachika au vipi? 



4 comments:

Anonymous said...

Tanzania bibi kila kitu Siri
Hata watoto WA magufuli watuwajuwi
Watakuja rundo la wasukuma ikulu Kama Msoga

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon umepiga pale pale nilipotaka kupiga. Kuna wakati napenda viongozi wezi wa Kenya. Kwani hawafichi biashara zao hata nyumba ntobu. Hawa wetu hawana tofauti na panya. Wanaiba na kuficha mashimoni wakijifanya wajamaa na maskini wakati ni wezi wakubwa na matajiri wa kunuka. Sijui huyu anayeingia atajitetea vipi kuhusu kuuza nyumba za umma? Nadhani tukiwa wakweli, tuwalaumu wapinzani kwa kutuletea bomu kuliko Makufuli vinginevyo kama wangecheza karata zao vizuri mwaka huu ulikuwa mwisho wa chama cha mafisadi.

Anonymous said...

hahahaha, kaka mhango ungekuwa karibu tungeongea na kucheka sana na hili swala, lakini basi tu.
Nimeona wasifu wake wikipedia,
https://en.wikipedia.org/wiki/Samia_Suluhu.
Unamaeleze kuhusu familia yake kwa ufupi.
Ukae salama broo

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon nakushukuru sana kwa mchango wako na kunipa link ambayo nitaitembelea japo haitakuwa na la maana kama ya Makufuli mwenyewe. Sijui inakuwaje wikipedia ya rais mzima inakuwa fupi kiasi hiki.