The Chant of Savant

Sunday 6 February 2011

Pamoja na neema zote hizi bado tu maskini!







Hizo picha hapo juu zilipigwa na mdau Cyril Akko alipokwenda kujionea uharibifu wa mazingira utakaosababishwa na ujenzi wa barabara mpya kupitia kwenye mbuga ya wanyama ya Serengeti.

Kinachogomba ni ile hali ya watawala wetu kutotueleza kwa kinagaubaga faida na hasara za mradi huu.

Hakuna anayepinga maendeleo. Kinachogomba ni ile hali ya utata kati ya maendeleo na faida binafsi ya wezi wachache watakaochukua mkopo wa mradi huu. Tunasema hivyo kutokana na ushahidi kuwa tuna vivutio na raslimali nyingi ambazo kama zingetumika vizuri zingetuingizia pesa nyingi na kubadili maisha ya watu wetu.

Tuna dhahabu lukuki. Tuna Tanzanite lukuki, tuna wanyama lukuki. Je mtu wa kawaida anafaidakaje na raslimali hizi zaidi ya kuwa laana kwake? Nenda Arusha, Mara, Shinyanga na Mwanza kwa uchache. Madini yameibiwa na yamebaki mashimo na uharibifu mkubwa wa maadili na mazingira.

Cha mno hapa ni uzuri wa nchi yetu unaoharibiwa na roho mbaya na uroho wa wezi wetu walioko madarakani.
Picha kwa hisani ya Cyril Akko wa Arusha.

No comments: