The Chant of Savant

Saturday 15 October 2011

Tanzania inapoathimisha zoezi la kunawa mikono bila maji!

Salma Kikwete akiongoza watanzania kunawa mikono kwa maji yasiyokuwepo!

Tumeona picha nyingi zikiwaonyesha watanzania wakiadhimisha siku ya kunawa mikono duniani. Ni jambo bora kiafya kunawa mikono kila wakati. Je watanzania wangapi wananawa mikono kila mahali wakati maji ni tatizo?

Bahati mbaya sana, nchi zetu huwa zinadandia kila jambo bila hata kutafakari. Huwezi kuadhimisha siku ya kunawa mikono kwa kunawa maji yasiyokuwepo. Mie nadhani maadhimisho haya yangeelekezwa kutoa maji kwa watanzania wote. Hivi jijini Dar es salaam, kwa mfano,ambalo ndilo uso wa nchi ni wangapi wana maji ya uhakika? Ni ajabu kwa nchi inayoruhusu hata watu kufungua biashara bila kuwa na vyoo kuwa na jeuri ya kusherehekea siku ya kunawa mikono.
Kuna haja ya kuelekeza vipaumbele vyetu kwenye matatizo ya kweli badala ya kuwa wadandizi wa kila kitu hata kile kinachotusuta.

No comments: