The Chant of Savant

Sunday 11 March 2012

Nilivyoshehekea Siku yangu ya kuzaliwa




Ingawa sikufanya sherehe kubwa zaidi ya kukusanyika na familia yangu, Siku ya kuzaliwa kwangu ilifana si haba.  Ilifanyika wapi?  Altona MB, Kanada.

10 comments:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Hongera Mwalimu. Hakuna haja ya kuwa na sherehe kubwa. Mungu Akubariki ili usherehekee tena na tena sherehe kama hii. Hongera kwa familia yote. Kale kapayukaji ketu kadogo kako wapi?

(Mimi mwaka jana binti yangu mkubwa - miaka 10 - alini-surprise kwa kunipikia ugali kwa mara ya kwanza kama zawadi yangu. Afadhali yako naona unabugia KEKI !!!)

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Nashukuru bwana Matondo. Kwa vile umemkumbuka rafiki yako Kapayukaji ngoja naye nimuongeze umuone alivyokua. Yeye zawadi yake ni kupiga mateke. Heri yako ulipikiwa ugali na unajua msukuma bila ugali hakuna maisha. Kila la heri.

Yasinta Ngonyani said...

Nategemea sijachelewa kukupa hongera za siku ya kuzaliwa kwako. HONGERA SANA NA MUNGU AKUBARIKI UZIDI KUSHEREKEA TENA NA TENA.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Da Yacinta huwa huna kawaida ya kuchelewa. Nashukuru kwa maombi yako na moyo wa upendo. Kila la heri na asante sana ndugu yangu.

Jaribu said...

Happy Birthday Mhango! Uendelee kupata nyingine tele tele!

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Jaribu nakushukuru sana si kwa salamu tu bali hata kunitembelea mara kwa mara na kuacha unyayo kwenye uga wangu. Mungu akuongezee umri na mafanikio hasa uchungu wa kulikomboa taifa letu toka kwenye makucha ya manyang'au na mafisadi.

Anonymous said...

Hii imetulia mkuu! Hongera sana. Naona Kapayukaji ketu kanaonyesha kako ngangari.. :-)

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Dear Anonymous,
Kapayukaji ni hatari. Kameanza kutupayukia ukiachia mbali kuharibu kila kitu kuanzia TV hadi kitanda chake. Ni hatari usiambiwe. The boy is everywhere everytime.
Thanks for your remarks.

Miss K. said...

Ohhh nimechelewa??? Bado naweza kukutakia heri ya siku yako ya kuzaliwa kaka mpayukaji. Uzidishiwe miaka mingi zaidi ....

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Miss K
Shukrani kwa salamu zako hujachelewa.