The Chant of Savant

Friday 17 August 2012

Hii picha inakufundisha nini?


Si maneno yangu. Kuna rafiki yangu kaniambia kuwa Jakaya anamwambia Zuma kuwa: Mbona wewe unaweka hadharani badala ya kuchukua kimya kimya kama sisi?  Mwenzio huwa mwenzio huwa sitangazi nyumba ndogo. Kweli watanzania usanii wanauweza. Maana jamaa aliponipa hii nikaona heri niwamegee na wengine ingawa najua wapenzi wa magamba itawaudhi. Tusameheana. Tabia ya mtu huwezi kuificha hata kama unampenda kiasi gani. Hamuoni jamaa pembeni alivyostuka na kujitoa haraka. Ni kama anasema: Wazee yenu siyawezi ngoja niangalie upande mwingine nisijehesabiwa  nanyi kundi moja. Je nini siri ya hawa vizee kutozeeka na kujiona vijana? Je ni ili vimwana wawapende? Unagundua nini vichwani mwao? Mmoja ananyoa kuficha kipara. Na mwingine anaweka piko kuficha mvi. Ngoma droo.

No comments: