The Chant of Savant

Friday 17 August 2012

Tanzania na kukodi midege mibovu, Ethiopia inanunua mpya

Air Tanzania 5H-ATC aircraft at LanseriaA Dreamliner Boeing 787 lands at Bole International airport in Addis Ababa, Ethiopia, Friday, Aug.17, 2012.
Hiyo hapo juu ni ndege mpya aina ya Boeing Dreamliner mali ya shirika la ndege la Ethiopia. Ethiopia imenunua ndege kumi za aina hii na inakuwa taifa la pili duniani kupokea ndege hizi baada ya Japan. Ni aibu kuwa Tanzania, kutokana na kukosa uongozi wa kizalendo na wenye visheni,imekuwa ikiunguza mabilioni kwenye kukodi mikangafu ya ndege. Yote hii inasababishwa na kundi dogo la watu wanaoendekeza ten percent badala ya uzalendo. Inashangaza kwa nchi yenye raslimali nyingi kuliko Ethiopia kutokuwa na hata shirika lake la ndege. Rais wetu na mkangafu wake mara nyingi amekuwa akisafiria ndege za nchi nyingine bila hata kuona aibu. Ni bahati mbaya kuwa tunakodisha midege mibovu kutokana na kuwa na watu wenye fikra mbovu na mafisi wanaotanguliza matumbo yao badala ya taifa wasihangaike na mstakabali wa taifa. Ethiopia hii ambayo tunakamata watu wake wakikimbia maisha magumu inazidi kupiga hatua kwenda mbele wakati sisi tunapiga mbio kurudi nyuma. Je nani aliliroga taifa letu hadi likawa na watawala wenye tabia za panya za kutoboa hapa na pale ili mradi matumbo yao yajae? Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

No comments: