The Chant of Savant

Monday 12 November 2012

Kikwete anaposhutumu kile alichoanzisha!



“Vitendo vya kuchambuana mwishowe ili mharibiane mwishowe mnakuwa dhaifu.. vita ya panzi sherehe ya kunguru,” Rais Jakaya Kikwete akihutubia mkutano wa chama chake . Alitoa maneno haya wakati akikemea wanaoutafuta urais baada yake. Kwa wanaofahamu jinsi Kikwete alivyoasisi mchezo wa kuchafuana akiwatumia hired guns kama Salva Rweyemamu na waandishi wengine wa habari nyemelezi na wachumia tumbo, wanashangaa Kikwete anapata wapi jeuri ya kuwananga wenzake. Je ni yale yale ya nyani haoni kundule au  unafiki wa kawaida? Je Kikwete ana udhu wa kuwananga wenzake wakati yeye ndiye mwanzilishi na mnufaika wa jinai na kadhia hii?
Hebu angalia nukuu nyingine ya Kikwete, “Niacheni…. nitakuwa mwenyekiti wa ajabu sana, eti wanataka niwe kwenye kambi zao hivi nikiwa kwenye kambi zao nitatenda haki?”
Kweli Kikwete haishi maajabu na sanaa. Haki gani anaweza kutenda iwapo ameshindwa kutenda haki ya kutimiza ahadi zake? haki gani anayoijua Kikwete iwapo utawala wake umeghubikwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu? ni haki gani anayoongelea Kikwete iwapo ameshindwa kutenda haki ndogo tu ya kukemea mafisadi achilia mbali kuwakamata?
Kikwete ataondoka madarakani na kuacha historia ya kuwa rais asiyeeleweka wala kuelewa. Ataacha legacy ya kukuza na kudumisha ufisadi na ugeugeu hata mahali pasipostahiki.
Je maneno ya Kikwete ni ya kuamini na kuaminika iwapo anajulikana yupo kwenye mtandao upi? Je kwanini Kikwete anadanganya na kujidanganya mwenyewe? Hakika time will tell.

No comments: