The Chant of Savant

Thursday 22 November 2012

Hatimaye ICC yamfungulia mashitaka mke wa Gbagbo


Message to the International Criminal Court’s Judges
Dk Simone Gbagba hivi karibuni ataungana na mumewe Laurent Gbagbo kukabiliana na kesi ya uharifu. Kwa wanaojua tabia chafu na hatari ambapo wake wa marais wa Afrika wanatumia madaraka ya waume zao, watakumbuka jinsi Simone alivyokuwa nguzo nyuma ya uovu uliotendwa na Gbagbo. Kwa wenye kuchukia tabia hii, kufungliwa mashtaka kwa Simone licha ya kuwa faraja ni ushindi kwa wapenda haki. Pia ni somo kwa wanaowaruhusu wake au waume zao hata watoto wao kutumia madaraka yao kinyume cha sheria. Kwa habari zaidi Bonyeza hapa.

1 comment:

Jaribu said...

Ingawa naamini wakina wake wa Rais waonyeshwe huruma kidogo, hiyo ni kwenye kutoa hotuba za kizungu. Wakijiingiza kwenye mambo ya kuvunja sheria, nao wafungwe miaka mingi tu kama waume zao.