Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Sunday, 5 June 2016

Mgogoro wa Visiwani: Mrema haisaii Tanzania

            Hakuna kitu kibaya kama kuishiwa. Mtu aliyeishiwa hana tofauti na mtu aliyechanganyikiwa hasa kama hakubali kuwa ameishiwa. Hivi karibuni mwenyekiti Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema, aliwaacha wengi hoi kama si kuwaudhi alipojigeuza jaji kiasic ha kumtuhumu Katibu mkuu wa Chama cha Wananachi (CUF), Maalim Seif Sharrif Hamad, kuwa ni mhaini bila kujua hata ukubwa wa tuhuma kama hizo.
Mrema aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kujivua nguo. Hata hivyo, kutokana na hali yake kiafya, kuna uwezekano; uwezo wake wa kufikiri unazidi kumtupa mkono. Pia, tokana na elimu yake kiduchu, Mrema ameonyesha wazi kuwa hata hiyo shahada aliyodai aliipata Marekani ni feki; na inapaswa kuchunguzwa; ili ikiwezekana atumbuliwe sawa na wengine walioghushi sifa na vyeti vya kitaaluma. Kama Mrema angejua uzito na athari za madai yake, wala asingejivua nguo. Ina maana yeye ndiye anajua sheria kuliko mamlaka zote za Tanzania ambaye ameuona “uhaini” wa Seif ambao serikali imeshindwa kuuona? Kama ni mhaini, kwanini hakamatwi na kufunguliwa mashtaka? Jamani, hata kama ni kutetea mtu au ulaji, angalau wanaofanya hivyo watumia japo akili lau kidogo tu. Hata unapotaka kumnasa samaki, angalau, huweka kitu kidogo kwenye chambo. Kwanini Mrema anataka kupaka rangi upepo au kutaka kuung’ao mbuyu kwa kijiko?
Mrema alimtuhumu Seif kuwa ni mbinafsi bila kujua kuwa naye alichokuwa akifanya pale licha ya kuwa ubinafsi wa kujipendekeza ili akumbukwe lau kwa cheo ni kujidhalilisha na kuchochea vurugu; sijui ili apate nini? Kwanini Mrema hakubali kuwa kwake game is up; na akajiuguze aone mwisho wa hali yake? Pia, Mrema alimtuhumu Seif kuwa anautaka urais kwa gharama yoyote; hata kama ni kwa njia ya kumwaga damu. Madai ya ajabu, hovyo na uongo wa wazi wazi.  Inaonekana Mrema hana kumbukumbu tena ya jana tu? Sijui ni kwa kukosa kumbukumbu au makusudi mazima Mrema alishindwa kukumbuka kuwa ni maalim Seif huyu huyu aliyewahamasisha wazanzibari wasifanye fujo tena wengi wa wafuasi wake walipokuwa tayari kuingia mitaani kuitangazia dunia kuwa wamedhulumiwa! Sijui kwanini Mrema hakumbuki kuwa ni Seif huyu huyu–anayemzushia ubinafsi, uhaini na uroho wa madaraka bila kutoa ushahidi–ndiye aliyekutana na rais John Pombe Magufuli ikulu na kumhakikishia kuwa hataunga mkono vurugu. Je huo umwagaji damu anaoongelea Mrema ni upi?
Ajabu ya maajabu ni madai ya Mrema kuwa aliyopayuka yalitokana na uzoefu wake wa kuwa waziri wa mambo ya Ndani wa muda mrefu bila kutaja huo muda mrefu ni miaka mingapi na kwa vigezo vipi? Kwani uwaziri wake wa Mambo ya Ndani ni taaluma? Kwanini Mrema hataki kuwa mkweli kwake binafsi na umma kuwa anasumbuliwa na kusukumwa na njaa kiasi cha kujipendekeza kwa rais Magufuli ili lau amkumbuke kwa cheo lau agangie njaa kali inayomkabili? Ama kweli wahenga walisema; adui yako muombee njaa na mwenye njaa kweli hana miiko.  Pia, hili la kutaka apewe lau ubunge wa kuteuliwa nalo linapaswa liangaliwe vilivyo na kwa makini hasa ikizingatiwa hali ya kiafya ya Mrema. Hivi Mrema anadhani Magufuli ni mtu wa kutapeliwa kirahisi hivyo; abugi step amteue mtu ambaye anapaswa kutumia muda uliobaki kujiuguza? Hata kutoka kwenye mkutano wenyewe alikorushia makombora yake alitoka akiwa ameshikiliwa kuonyesha asivyo timamu kiafya. Hivi kwa udhaifu wa kiafya alio nao Mrema, anaweza kufanya kazi gani zaidi ya kutaka ateuliwe ale dezo jambo ambalo nalo ni ubinafsi, ufisadi, upotezaji fursa na matumizi ya fedha za umma ukiachia mbali kuwa ujipu ambao Magufuli akiufanya atakuwa anajipiga mtama? Tunamshauri Seif na Magufuli wampuuzie Mrema. Kwani, inavyoonekana, anataka afe na mtu. Hebu tuwe wakweli kidogo. Unawezaje kumteua mgonjwa; au Mrema anajigonga ili aendelee kugharimiwa matibabu India?
Kwanini Mrema–kama kweli si mbinafsi tena wa kunuka–anaamua kuwapakazia wengine ndiyo apate mradi wake? Kama tukiwa wakweli, kuna mwanasiasa mbinafsi Tanzania kama Mrema ambaye kila alipohamia aliua vyama kwa sababu ya ubinafsi na ukosefu wa usomi na busara na uzalendo? Kwanini Mrema anataka kuwageuza watanzania majuha na wasio na kumbukumbu kiasi hiki; wakati wanajua historia yake iliyojaa ubinafsi, ujanja ujanja, utatanishi ukiachia mbali uchu wa madaraka? Kama Mrema amepoteza kumbukumbu, basi asidhani watanzania wote wamepoteza kumbukumbu kama yeye. Mgogoro wa matokeo ya uchaguzi wa Visiwani si wa kufanyia usanii wala kugangia njaa. Wengi walidhani; Mrema angewahimiza wahusika wakae kwenye meza ya mduara. Bahati mbaya sana, tena sana, Mrema anaonekana kumwaga mafuta kwenye moto. Hata hivyo, kutokana na kuishiwa kwake, sijui kama Seif atapoteza muda kumjibu hasa ikizingatiwa kuwa hamna hoja ya msingi ya kujibu; ukiachia mbali kutaka umaarufu kupitia mgongoni mwake na UKAWA. Je anadhani watanzania wamemsahau Mrema muungu mtu aliyetaka kila tatizo la kitaifa litatuliwe kijijini kwake Kiraracha? Nani hamkumbuki Mrema mpenda makuu? Kama Mrema anataka kurejea CCM, si arejee tu badala ya kuanza kutafuta kuwachafua wenzake? Kwanini Mrema amejigeuza mpinzani wa wapinzani na kwa faida ya nani?
Ni bahati mbaya kuwa Mrema hakutoa hata suluhisho wala m change kwenye tatizo zaidi ya tuhuma za uongo ambazo alishindwa hata kuzithibitisha achia mbali kushindwa kujenga hata hoja. Amekuwa tatizo badala ya kuwa jawabu.
Tuhitimishe kwa kumuuliza Mrema kwanini anashindwa kuwa refa mzuri kwa kuangalia mapungufu ya pande zote? Au ni ile hali ya kuwa njaa inapopanda kichwani basi hubongo huacha kutumika na badala yake utumbo hutumika?
Chanzo: Tanzania Daima.

Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 08:07

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

I Love My Country Tanzania

I Love My Country Tanzania

The Curse of Salvation

The Curse of Salvation

Gen Z and Internet Revolution

Gen Z and Internet Revolution

I Cry for Ambazonia and Darfur

I Cry for Ambazonia and Darfur

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

The Story of Stories

The Story of Stories

The Chant of Savant

The Chant of Savant

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presid...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the ho...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon where...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete Pea...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaidi....
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (84)
    • ►  December (1)
    • ►  November (11)
    • ►  October (9)
    • ►  September (7)
    • ►  August (12)
    • ►  July (8)
    • ►  June (7)
    • ►  May (5)
    • ►  April (4)
    • ►  March (6)
    • ►  February (8)
    • ►  January (6)
  • ►  2024 (92)
    • ►  December (7)
    • ►  November (4)
    • ►  October (11)
    • ►  September (9)
    • ►  August (7)
    • ►  July (9)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (7)
    • ►  March (6)
    • ►  February (7)
    • ►  January (8)
  • ►  2023 (118)
    • ►  December (10)
    • ►  November (10)
    • ►  October (9)
    • ►  September (2)
    • ►  August (4)
    • ►  July (6)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (18)
    • ►  March (13)
    • ►  February (9)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ▼  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ▼  June (24)
      • Dk Kanywaji kuwalinda watawala wastaafu no
      • Punguza na toza kodi mafao ya marais wastaafu
      • Je Gwajima anatumwa au anajituma?
      • Poor Lee pumba! What’s wrong?
      • Mrema anapaswa kujishangaa
      • Dk Makufuli lazima uwatumbue akina Nkapa na wenzake
      • Kijiwe chamkaribisha Pumba kijiweni
      • Boozers want their former biggies probed
      • Mama Magufuli achana na biashara ya NGO fichi
      • Magufuli tumbua hata vilaza wazito
      • Mlevi kumpa vidonge mke wa munene
      • Nasi tujiandae kuwachunguza marais wetu
      • Kijiwe chashinikiza posho ya makalio ifutwe
      • Watanzania hakikisha mnamlinda Magufuli
      • Mugful: Spit Fire on 'em for Boozers' Sake
      • Mlevi kutia timu mjengoni na michupa
      • Hiyo ndiyo gusagusa bendi yetu
      • Kijiwe chamshangaa Tuliya
      • Tunajitahidi kufaidi Summer kabla mambo hayajahari...
      • Mgogoro wa Visiwani: Mrema haisaii Tanzania
      • Boycott everything Hindi boozers
      • Tujikumbushe alikotokea Mohamed Ali marehemu
      • Mlevi kumlinda Makufuli
      • Kijiwe chalaani akina Mkamia
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (399)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (33)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (597)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (94)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.