The Chant of Savant

Wednesday 29 June 2016

Dk Kanywaji kuwalinda watawala wastaafu no


             Baada ya Rahis Joni Kanywaji Makufuli kutoa hakikisho kwa walaji wakubwa, Kijiwe kimeamua kumtolea uvivu kumwambia kuwa hana power wala uhalali kisheria kufanya hivyo.
Mijjinga ndiye analianzisha, “Jamani mmesikia namna rahis anavyoanza kujichanganya na kutuchanganya kiasi cha kushindwa kuelewa nini kinaendelea?” Kabla ya kuendelea, Mbwamwitu anachangia, “Kumbe ulikuwa hujaliona hilo! Ulitegemea awe salama wakati nyuma yake kuna Chama Cha Maulaji (CCM) ambacho sera yake kubwa ni kulindana na kula pamoja?”
Mijjinga anaendelea, “Hili la chama cha maulaji na sera yao ya kulindana nalinyaka sana. Kilichoniponza ni mbio rahis za kupambana na ufisadi kiasi cha kuwakuna wachovu wengi wasijue ni mbio za sakafuni. Sikutegema kama mkuu angeweza kutamka aliyotamka kuwa atawapa ulinzi wale waliosababisha kaya yetu ifikie hapa ilipo kiasi cha kumhangaisha huku akilalamika mara kwa mara. Kumbe sharia yetu inatumika kwa kuangalia sura ya wahalifu siyo? Nadhani walindwa sasa wanafurahi wakitononoa usingizi wasijue ndiyo sekeseke linaanza. Wallahi mie sikubali kura yangu itumike kuwalinda wahalifu hata wawe wakubwa kama tembo.”
“Kaka siasa hizo. Warabu wa Pemba hujuana kwa vilemba hukuambiwa? Kumbe m wenzangu ulisahau ule msemo wa usanii uliokuwa ukitawala wakati wa usanii uliopita siyo! Na bado mtanganyikiwa zaidi msijue la kufanya usawa huu wa kutumbuana kwa upendeleo na kuangalia sura.” Anachomekea mzee Maneno huku akibwia gahawa yake.
Mgosi Machungi anakatua mic, “Hapa azima aisi ajue; sisi tiinchagua na kumtuma afanye kazi tiiyomtuma ya kuhakikisha usaaama na maendeeo ya wanakaya na si wazito kama anavyoanza kufanya. Yeye ni mtumishi wetu na si mtumikishaji wetu.”
Msomi Mkatatamaa leo hangoji. Anamua kula mic, “Tuache kujidanganya. Huyu bwana hana uwezo huo kikatiba kwani kazi ya kuwalinda wanakaya ni ya kila mwanakaya na katiba na si rahis. Hapa atapaswa asaidiwe na wataalamu wa katiba tusije kufikishana kwenye vyombo vya sharia kimataifa. Haiwezekani tuone madudu yanafanyika nasi tuwe mashahidi. Mbona kila jambo liko wazi kuwa tunachotaka ni utawala wa katiba na bora si bora utawala unaoweza hata kuvunja katiba? Hata hivyo, naona kama kuchanganyana, kuchanganyikiwa na kujichanganya. Kwani, juzi nilishuhudia na kusikia mwenyewe pale Biafra akisema kuwa anachotaka kufanya ni kupambana na wezi wachache waliokuwa wakila njuluku za umma. Aliongeza kusema kuwa kama wanataka kula waende wakale njuluku za bibi zao. Kwani hawa anaotaka kuwalinda si wachache na hawana bibi zao wanaopaswa kula njuluku zao?”
Mpemba anachomekea, “Hata miye nilikkuwepo pale wallahi akitoa vipande kwa wezi wa fedha za umma. Na mie hii kauli wallahi ilinchanganya na kunifanya nianze kushuku kuwa kumbe kilichokuwa kikinkata hadi kunshabikia huyu bwana nkubwa sasa chaanza kuwa mbio za sakafuni.”
Kanji akawanyua mic,”Kweli dugu yangu mimi iko sikitika sana. Iko anza ona shaka kuba sana jamani. Kama katiba nasema nalinda chovu vote kwanini sasa linda kuba tu? Hapa iko kitu kama naona vatu naanza piga tama venyeve. Aibu kuba kweli kweli dugu zanguni.”
Mipawa anaamua kumchomekea Kanji, “Hata mimi nahisi kuchanganyikiwa na kizungumkuti kugundua kuwa kuna wanakaya wasioona madudu kama EPA,Richmonduli,Kiwila,NBC, Lugumi, Escrew,UDA na mengine si wizi wa fedha za umma. Je umma huo anaomaanisha huyu bwana ni upi kama haoni huu umma unaotaka wanene waliovurunda wapelekwe kwa pilato? Au jamaa amejigeuza pilato kiasi cha kulewa maulaji asijue kila jambo lina mwanzo na mwisho?”
Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kukamua,”Mie wala sishangai. Tangu mjomba wangu alipovunjiwa nyumba yake wakati walioiba nyumba za umma wanahakikishiwa ulinzi, sina hamu na kinachoendelea na najutia hata hiyo kura yangu ya kula. Hatuwezi kuendelea hivi. Lazima kijiwe kichukue hatua ili kuondoa haya mazabe kabla hayajageuza majipu. Lazima yatumbuliwe bila kujali nani anamtumbua nani. Hii kaya ni yetu sote na si ya wakubwa wala nini. Si yao wala ya bibi zao.”
Msomi anarejea tena, “Kwa hali iliyojitokeza hivi karibuni kiasi cha kuchafua hali ya hewa, nadhani tendo lolote huwa ufisadi au halali kutegemea nani aliyelitenda. Kosa likitendwa na mkubwa linasamehewa. Likitendwa na mlalahoi linakuzwa na kuwa big deal even from nothing. Hayo madudu yote uliyoongelea yangekuwa kashfa na jinai kama yangetendwa na wachovu. Yakitendwa na wakubwa ni halali hasa ikizingatiwa kuwa sasa mamlaka yameamua kujifichua kuwa yako pale kuwalinda wanene kwa kuwaumiza wadogo. Hamuoni wanavyolipwa mabilioni ya madafu kwa kutuibia na kuvuruga kaya yetu kiuchumi? Hii ndiyo Bongolalaland ambayo huwa mzee Mpayukaji anaongelea mara kwa mara kama alivyo-coin hili jina.”
Mchuguliaji aliyekuwa akisoma gazeti anaamua kuchomekea, “Namna hii sijui tumwamini nani wakati tunarudishwa kwenye arifu na ujiti na wale tuliozugika na kuwaamini kuwa wangetuvusha wakati lengo lau ni kutuingiza mkenge na kutuzamisha.”
Kapende anachomekea, “Tusipokuwa makini na wakali dhuluma hii inaweza kufanikiwa. Hukuwasikia wanene wakisema kuwa kuanzia sasa hakuna siasa bali kuchapa kazi ili wakubwa wanaolindwa waendelee kuhomola ima kwa kutumia waliowaacha nyuma au kuongezewa marupurupu? Hapa–wakati mwingine–unashindwa kutofautisha jipu ni lipi usawa huu wa kuchanganyana hadi kuchanganyikiwa na kujipiga mitama hadharani.”
Mgosi naye anarejea tena, “Mimi naona tisikubai hii dhuuma. Azima tipange mikakati ya kuandamana ii kupinga hii agizo la kuindana na kupeana motisha kutiibia zaidi. Haiwezekani kama mbwai mbwai.”
Mpemba naye hajivungi, “Yakhe sasa nimeelewa kwanini jamaa alishindwa na kupuuzia dhulma ya Zenj aliyofanya yule habith Jechia Salimuni Jechia ya uchakachuaji.”      
Kijiwe kikiwa kinanoga ulipita msafara wa munene. Wala hatukuushangilia zaidi ya kuzomea kimoyomoyo.
 Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Sunday 26 June 2016

Punguza na toza kodi mafao ya marais wastaafu


            Hakuna ubishi kuwa viongozi wetu wastaafu wanapewa marupurupu mengi na makubwa, jambo ambalo kiasi fulani linawakwaza watanzania wengi hasa walio maskini. Hii ni kutokana na kutwisha mzigo wa kuwatunza viongozi wastaafu kuanzia marupurupu, kulipia matibabu yao na familia zao, kulipia wafagizi, watunza bustani, walinzi, madereva, wapishi na wengine. Kimsingi, viongozi wetu wanaishi–kwa kukopa maneno ya rais John Pombe Magufuli–wanaishi peponi wakati wanaowagharimia wakiishi motoni au wanaishi kama malaika wakati wanaowagharimia wanaishi kama shetani.
 Hata hivyo, rais Magufuli alionyesha mfano wa uongozi alipoamuru mafao ya wabunge yakatwe kodi. Magufuli hakuishia hapo; aliamuru na mafao yake yakatwe kodi. Huu ni mfano wa kuingwa na kupongezwa. Tunamshauri rais asonge mbele kwa kupunguza na kutoza kodi mafao na marupurupu ya viongozi wastaafu ambao–kwa nchi maskini kama yetu–wanapewa fedha nyingi hata wasizohitaji wakati umma ukiendelea kuteseka na kubebeshwa mzigo. Kwa mfano, huwa nashangaa kulipia matibabu ya marais wastaafu ndani ya nje hata kwa wale walioua huduma za afya. Tunawalipa kwa kazi gani? Wanalipiwa walinzi, wafagizi, watunza bustani na maeneo mengine kiasi cha kuishi peponi wakati watanzania walio wengi wakiishi motoni. Tunaunga mkono hatua za makusudi za Magufuli za kupambana na ufujaji na wizi wa fedha za umma. Unashangaa, kwa mfano, kuona marais wastaafu wakirundikiwa marupurupu huku wananchi walipa kodi na wachapakazi wakizidi kuminywa. Marais wetu wastaafu wanaishi peponi. Unaweza kuona hili kwenye namna ya wanavyoishi.
Hakuna kitu kinafanya wananchi wawachukie viongozi wao kama kuona wanavyojipenda wakijilimbikizia marupurupu kwa upande mmoja na kuwa kama wafalme huku wakihubiri usawa kwa upande mwingine. Unashangaa kama kweli wanaamini katika yale wanayofanya ukilinganisha na kuangalia walichofanya wakiwa madarakani. Unashangaa na kuhoji mantiki, kwa mfano, ya kumpa marupurupu kiongozi mstaafu ambaye kuna ushahidi wa wazi kuwa uongozi wake uliingizia taifa hasara. Je mtu kama huyu–anayepaswa kufikishwa mahakamani kwa makosa aliyotenda–anazawadiwa marupurupu yote haya kwa kazi gani kama siyo kulea majipu yanayopaswa kutumbuliwa bila simile wala huruma? Je hii–licha ya kuwachochea na kukakatisha tamaa wafanyakazi wa chini–inaleta picha gani na kutoa mfano gani? Heri Magufuli ameliona hili na kulifanyia kazi. Hata hivyo, inashangaza kwa rais Magufuli–kwa mfano–kupunguza mshahara wake na ile ya baadhi ya watendaji wa umma huku akifumbia macho marupurupu ya viongozi wastaafu ambayo ni makubwa bila sababu. Tungeomba rais aliltolee hili ufafanuzi ili kuwapunguzia walipa kodi masikini mizigo isiyo na ulazima. Tunadhani tumpe muda tuone atafanya nini kuliangalia na kulishughulikia hili ili kuondoa ubaguzi katika kufaidi keki ya taifa ambayo imegeuzwa ya watawala familia zao, marafiki zao na wote wenye ushawishi iwe wa kifedha au kimadaraka.
Wapo wanaopendekeza hata hizi kinga walizojipa viongozi ziondolewe au kuwekewa masharti mfano, mhusika apewe marupurupu baada ya kubainika kuwa alifanya kazi aliyochaguliwa kufanya vizuri na kwa ufanisi ili kuepuka kulinda na kuwazawadia waovu jambo ambalo ni kishawishi cha uchu wa madaraka na utendaji maovu. Watahofia nini iwapo wana kinga. Kuondoa kinga, licha ya kuleta uwajibikaji na uchapakazi, utaondoa dhana kuwa urais ni sehemu ya kuchumia utajiri wa haraka kwa mwenye kuushika, familia yake na marafiki na washirika wake. Tufike mahali tubadilike na kuyaangalia mambo kama yalivyo.
Marais wastaafu hawastahili marupurupu makubwa wanayopata hasa ikizingatiwa kuwa walikuwa wakijilipa mishahara mikubwa walipokuwa madarakani ukiachia mbali wengine kutumia ofisi kujineemesha. Ushahidi wa kujipa mishahara mikubwa uko wazi. Rejea hatua adhimu za rais Magufuli kupunguza mshahara wake. Alifanya hivyo kutokana na kugundua kuwa mshahara husika ni mkubwa hasa kwa nchi maskini na ombaomba kama yetu. Hata hivyo, Magufuli alikaririwa juzi akiwakiwazodoa wanaotaka viongozi wastaafu washughulikiwe. Amewahakikishia ulinzi kiasi cha kuwachanganya watanzania wanaodhani anataka kutenda haki kwa watanzania wote kwa usawa katika kupambana na ufisadi. Kilichojitokeza ni kwamba Magufuli–kama alivyokaririwa akisema hivi karibuni–yupo madarakani kuwalinda watawala wa zamani na si watanzania. Sijui huku ni kujichanganya au kuwekwa sawa, sijui; na kweli sijui.
Je Magufuli anaanza kujipambanua kuwa siyo yule yule tunayemuona na kumsikia majukwaani? Je ameonywa kuwa naye ataondoka madarakani siku moja? Je kuna yake tusiyoyajua ambayo–hawa aliwaahidi ulinzi hata wale anaowalaumu wazi wazi kuharibu nchi–wanayojua ambayo hatuyajui na Magufuli asingependa yajulikane? Je ni ule ule usanii wa CCM na sera yake kuu ya kulindana? Hakika sijui.
Tumalizie kwa kusema kuwa hakikisho la ulinzi kwa viongozi wastaafu ni ushahidi kuwa sheria za nchi yetu zinatumika kitabaka kwa kuwapatiliza wasio na madaraka na kuwalinda wenye madaraka. Hakiki, hili, litammaliza Magufuli kiasi cha watanzania kujutia ni kwanini waliiamini tena CCM wakati wakijua kuwa ni ile ile iliyotekwa na wenye madaraka pindi tu alipong’atuka baba wa taifa. Hata hivyo, tuseme; Tanzania si mali ya watawala wala ya Magufuli bali ni mali ya watanzania. Wanachotaka kinapaswa kupewa kipaumbele kuliko maslahi uchwara na haramu ya watawala. Ni vizuri wahusika wakaelewa na kutambua kuwa taifa ni zaidi ya genge la watu wachache wenye madaraka au ushawishi.
Chanzo: Mwanahalisi Jumatatu.

Je Gwajima anatumwa au anajituma?


            Katika kutapatapa ima kujiweka karibu na rais John Pombe Magufuli au kuficha maovu yake, askofu bandia na wa kujipachia Josephat Gwajima amelikoroga asijue jinsi ya kulinywa. Kwa waliosikiliza matusi, kashfa, uchochezi na maudhi yaliyomwagwa na anayejiita askofu Josephat Gwajima unashangaa kwanini nchi yetu inawavumilia viongozi wa kiroho waroho wa mali na madaraka wasioheshimu hata vyeo vyao. Unashangaa, kwa mtu kama Gwajima asiyejua jinsi ya kutumia kichwa na ulimi wake anachohubiri. Je ni kwa faida ya nani na kwanini na ili iweje? Je kuna kinachomsukuma Gwajima kusema anayosema? Si bure; k una namna. Gwajima anasikika kwenye mahubiri yake ambayo yako kwenye mtandao akisema vitu ambavyo haviingii akilini hasa pale anapojifanya mtetezi na msemaji wa rais John Pombe Magufuli. Je ametumwa au amejituma na ili iweje? Je Gwajima anadhani anaweza kumtapeli Magufuli ambaye sifa zake zinamtosha kiasi cha kutohitaji mtetezi? Hata kama Magufuli angehitaji mtetezi, si mtetezi na utetezi uchwara kama alivyobainisha Gwajima. Je Gwajima amesahau kuwa Magufuli na washauri na wasaidizi wake wanamjua alivyokuwa kipenzi cha Edward Lowassa, mgombea wa Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi (UKAWA) ambaye anamsaliti na kutaka kujitenga naye? Kama amemsaliti Lowassa, Gwajima anaweza kumsaliti yeyote kama alivyofanya kwa Mungu wake ambaye amekuwa akimuuza badala ya kumtangaza. Je Gwajima anadhani watanzania ni wasahaulifu kama yeye? Kwanini asikubali kuwa alikosea na kuendelea na msimamo wake? Kama anaijua siasa vizuri basi avue joho na aanzishe au kujiunga na chama ili ajulikane yuko upande gani badala ya kutumia madhabahu kufanya uhuni.
Gwajima alitoa madai kuwa vyanzo vyake vya ‘kiufufuo’ vimemtaarifu kuwa kuna watu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wana mpango wa kumhujumu na kumzuia Magufuli asiwe mwenyekiti wa CCM kwa hofu ya kutumbuliwa. Ya CCM yanamhusu nini wakati yeye si mwanasiasa? Nadhani vyanzo vya Gwajima si vya ufufuo bali ufu unaomsumbua kiasi cha kuhubiri uongo, uchochezi na kashfa bila sababu zozote za msingi. Bila shaka serikali haitamwacha hivi hivi. Gwajima alikwenda mbali akiwatuhumu marais wastaafu Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete kwa mambo mbali mbali amabyo hakuyatolea ushahidi. Alitaka wachunguzwe. Nadhani ni wakati muafaka kwa Gwajima kuchunguzwa alivyopata ukwasi wa kutisha kiasi cha kumilki helkopta. Je alifanya biashara gani halali au haramu tena kwa muda mfupi hivi? Gwajima alidai kuwa kuna genge la watu linalotaka kumzuia Magufuli asiwe mwenyekiti wa CCM.  Ni bahati mbaya kuwa Gwajima–katika kujikomba kwake–alishindwa kutoa ushahidi kwa kutaja majina ya waliopo nyuma ya hujuma hii. Magufulil awe au asiwe mwenyekiti wa CCM inamhusu nini Gwajima? Kwanini mambo ya Ngoswe asimuachie Ngoswe mwenyewe?
Gwajima licha ya kuonyesha ubabaishaji, kigeugeu na unafiki eti anasikika akilaani ufisadi kuanzia ujangili, mita za mafuta, kupitisha makontena bila kulipiwa na mengine mengi. Je Gwajima alikuwa wapi? Kwanini hakuyasema haya wakati yakitendeka hadi angojee ujio wa Magufuli? Mbona hakufanya kama maaskofu waliokuwa wakikemea serikali ya Kikwete?
Gwajima anadai kuwa alipigiwa simu kuombwa msaada wa kumhujumu Magufuli. Hapa ndipo utamu ulipo. Lazima abanwe awataje waliompigia simu.
Ili kumsaidia Gwajima na wengine wenye mawazo na tabia kama zake, serikali inapaswa kufanya yafuatayo:
Kwanza, achunguzwe ana mali kiasi gani na amezipataje
Pili, achunguzwe kama analipa kodi na kama vyanzo vyake vya kipato ni halali na ni vipi.
Tatu, achunguzwe alivyopata uaskofu anaoutumia kisiasa na kibinafsi.
Nne, aitwe na vyombo vya usalama ili kuthibitisha madai yake na akishindwa afikishwe mahakamani.
Tano, achunguzwe kama kuna watu wanaomtuma au anajituma na anafanya hivyo kwa sababu gani.
Sita, afahamishwe kuwa wakati huu si wa siasa za kibabaishaji, kupakana matope, majitaka na kulindana.
Saba, afahamishwe na kuonywa kuwa Magufuli ahitaji utetezi wake.
Nane, afahamishwe kuwa hawezi kumtapeli Magufuli na wala asijifanye mtetezi au msemaji wa Magufuli ambaye ana watu wa kufanya kazi hii tena walioisomea na walioajiriwa na si wa kujipendekeza au kujiajili.
Tisa, aeleze alikuwa wapi au alifanya nini kupinga maovu anayotaja kwa sasa na amesukumwa na nini ambacho kilishindwa kufanya hivyo wakati maovu yakifanyika wakati alikuwa nchini na akiwa na nafasi–hata kama ni ya kujipachika–aliyo nayo sasa.
Na kumi, je ana ugomvi binafsi na anaowatuhumu au ana taarifa ambazo wengi wangependa kuzijua baada ya kutolea ushahidi madai yake.
Tumalizie kwa kuuliza; Je Gwajima anatumwa au anajituma na ili iweje? Je anamchafua Magufuli ili iweje?
Chanzo: Mwanahalisi Jumatatu.

Poor Lee pumba! What’s wrong?

Mrema anapaswa kujishangaa


            Baada ya mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP) Augustine Mrema kugeuza kujikomba sera yake na chama chake, juzi alikuja na mpya. Baada ya kujigonga sana kwa rais John Magufuli bila mafanikio katika madai ya ajabu kuwa katibu mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Seif Sharrif Hamad ni mhaini kudharauliwa na kutojibiwa, Mrema ameamua kubuni mbinu mfu ya kuwashambulia wapinzani wote kwa ujumla.
            Tokana na kuendelea kuishiwa, Mrema alidai juzi kuwa wapinzani wanamshutumu rais Magufuli udikteta ili kumharibia, kumkwamisha na kuvuruga amani. Sijui kama Mrema anajua dhana nzima ya amani kuwa inatokana na ukweli na si uongo na ubabaishaji kama anaofanya. Kibaya zaidi, Mrema anataka wapinzani wote wageuke vigeugeu kama yeye; waache kutetea maslahi ya wananchi; watetee matumbo yao kama yeye. Sijui kama upinzani unaweza kujirahisi na kujikomba na kuisha na kuishiwa kiasi hiki.
             Kwanini Mrema hataki kukubali kuwa ameisha na kuishiwa. Si arejee kijijini kwake akapumzike? Kwanini Mrema hataki kuona ukweli kuwa, kwa sasa, hana nguvu wala akili za kuwa kiongozi wa umma? Je Mrema–kwa hali aliyo nayo–anataka kufa na mtu; au ndiyo kuharibikiwa? Kwa mwenye akili timamu, hawezi kuwalaumu wapinzani kwa kutimiza wajibu wao wa kuikosoa serikali na si kulala nayo kitanda kimoja. Kwanini Mrema hataki kutofautisha upinzani wa Tanzania na ule wa kisanii wa Zaire ya Mobutu aliyekuwa akiwapa fedha vibaraka na waramba makalio yake waanzishe vyama kuwazuga wananchi? Kwanini Mrema hataki kukubali kuwa siasa za uchumiatumbo na usaka tonge hazina nafasi tena katika karne hii?
            Ukimtathmini na kumchambua Mrema, unashinda hata pa kumueweka; kwani huwezi kujua kama anatumiwa au anajitumia tokana na kuishiwa kisiasa na kimkakati. Laiti angekuwa amesoma, lau angejifanya refarii kama wale madaktari uchwara wa chuo fulani ambao hujifanya watetezi na wasemaji wa CCm ili wakumbukwe. Ambacho kwa wanaompenda Mrema na kutaka kumsaidia ni kwamba akubali kuwa muda unazidi kumtupa mkono. Unaweza kuliona hili pale Mrema anapoongelea yaliyopita akiishi kwenye kile kiitwacho ukale (golden era) alipokuwa amevishwa mkenge na kupewa cheo cha Naibu Waziri Mkuu bila kuwapo kwenye katiba.
            Zaidi, ni vizuri kumfahamisha Mrema kuwa wakati umebadilika. Hivyo, hana haja ya kubadilika kiasi cha kuachana na kuendelea na fikra na mbinu mgando na za kikale bila kuangalia hata tabia ya anayemlenga.  Magufuli si dhaifu wa kulewa sifa kama waliomtangulia ambao walikuwa wakisifiwa kidogo wanaingizwa mkenge. Magufuli si mtu wa kujisifu wala kusifiwa kirahisi. Ni mtumbua majipu ambaye anapaswa kumnyamazisha Mrema aache kujigeuza msemaji wake wakati anaye msemaji anayemlipa na mwenye elimu na ujuzi wa kazi hii. Anachofanya Mrema–licha ya kutaka apewa tonge–anamtumia Magufuli kujipatia sifa rahisi asijue janja yake imeishajulikana kiasi cha kupuuzwa na kudharauliwa. Kama Magufuli angekuwa anamhitaji Mrema, asingemwacha aendelee kujivua nguo hadharani hivi. Kimsingi, anachofanya Magufuli ni kumpuuzia Mrema kwa vile anajua anayoongea hayatoki moyoni bali tumboni. Ni njaa tu inayomhagaisha.
            Pia wengi wanamjua Mrema kama mwanasiasa uchwara aliyezoea siasa za kibabaishaji ambazo mara nyingi hutumia uongo, utapeli na fitina kwa wanaozifanya kuweza kuishi. Huu si wakati wa siasa za namna hii. Huu ni wakati wa “Hapa Kazi Tu” ambapo Magufuli ametangaza wazi kuwa hana ugomvi na wapinzani wala tofauti za kiitikadi. Mtu wa namna hii si rahisi kumuingiza mkenge hata kidogo. Itakuwa ni jambo la ajabu kwa Magufuli kuingizwa mkenge na mchovu anayedandia kila anayepita ili aonekane anamtetea. Magufuli ahitaji mapambio wala utetezi. Kazi na sifa zake zilizomvusha kwenye siasa za ushindani mkubwa ndani ya CCM zinamtosha; ahitaji msaada. Hata kama angehitaji msaada, basi asingetegemea kuupata kwa wachovu na watu wenye mawazo mgando wanaoweza kujipayukia bila kufikiri kama anavyofanya Mrema. Magufulil anajua ubovu wa Mrema. Alimjua sana siku aliposimama jukwaani jimboni mwake Vunjo kujivua nguo akiwataka wapiga kura wake wasimpe kura mgombea wa chama chake bali wampe Magufuli.  Mwanandoa yoyote anayeweza kumpa mwenzie mtu mwingine amtumie hawezi kuaminika na hata hayawani. Kitendo alichofanya Mrema kwa chama chake kwa kumnadi Magufuli licha ya kuwa usaliti na uhujumu wa chama kinamwonyesha kama opportunist anayeweza kufanya lolote ilmradi mkono uende kinywani. Huu kwa lugha nyepesi huitwa uchangudoa wa kisiasa. Mwanasiasa anayefikia hatua hii huwa ameisha na kuishiwa kiasi cha kutorekebishika. Kama ni mgonjwa si wa kupona.
            Tumalizie kwa kumtaka Mrema arejee CCM kama anaona sera za Magufuli zinamkuna kiasi hicho. Kwanini Mrema anataka kuendelea kutumikia mabwana wawili yaani upinzani na CCM ambayo–hata hivyo–ahitaji huduma yake hasa ikizingatiwa kuwa kama Mrema alikuwa nyama basi limebakia fupa kavu tu ambalo hata fisi bingwa wa tamaa halitamani wala hawezi hata kulinusa. Kama Mrema anatafuta mtu wa kufa naye, amekosea. Hakuna anayemwelewa wala kumwamini kwa sasa. Safu hii–huko nyuma–iliwahi kumsahauri Mrema aachane na siasa za tumbo na majitaka aende kujitibia. Na kama anataka msaada wa matibabu aseme wazi kwa kuomba msaada achagiwe badala ya kuwachafua wenzake. Wapinzani si saizi yake.
Chanzo:Tanzania Daima Jumapili.

Saturday 25 June 2016

Dk Makufuli lazima uwatumbue akina Nkapa na wenzake


            Juzi nilinusurika kujinyotoa roho. Si pale nilipokwenda kwenye kongamano na Kigoda cha Mwl Nchonga. Nikiwa nimepiga pamba zangu bila bangi na gongo nimejipendezea tu si kidhabu mmoja aitwaye Big Ben Nkapa akanichefua nusu ninyanyuke na kufanya kitu mbaya kama si kumheshimu marehemu Mchongo (Bwana God Amuwekee Patamu) stori ingekuwa nyingine. Wakati sisi tukilewa mma, wajivuni wanalewa madaraka na kujisahau wakidhani tumesahau uchafu wao. Bila chembe ya aibu wala utu wanatuomba msamaha.  Sisi hatuombi msamaha kuwasulubu na kuwatumbua.
Kuna kipindi nilishindwa kujizui kusikiliza porojo na upuuzi kiasi cha kutaka kumkichaka Ben kama yule jamaa wa kwa Saddam aliyefanya shambulizi la kiatu. Ilibidi nijizuie; kwa vile hiyo si jadi ya walevi ambao jadi yao ni kufanya kweli bila kujali nini kitatokea. Anyway, shetani na Ben washindwe.
 Leo nataka namtumia kidhabu huyu na wajivuni na wezi wenzake; waache kututia madole vinginevyo tunaweza kuamua kama mbwai mbwai. Wanadhani tumesahau walivyochomoa njuluku na mimali yetu? Tuliwaminyia; sasa wanatutia madole kana kwamba hatunayo ya kuwatia? Hivi Ben anadhani tumesahau yeye na marafiki na kaya yake walivyokwapua Kiwila? Anadhani walevi wameishasahau au kusamehe alivyopiga mnada Banki Biyashara aliyotupa kihasara kwa makaburu wenzake?
Kama Big Ben ana kumbukumbu ndogo au hana kabisa, asidhani walevi ni wasahaulifu na mabunga kiasi hicho. We still vividly remember how he robbed us. He must stop kvelling. Samahani. Nimechukia hadi kikameruni kinanitoka bila kujua wala kuhiari.
Sijui kwanini Ben hataki kukubali kuwa hana power tena na tukimbana Dk Kanywaji anaweza kutumbuliwa wakati wowote? Sasa ajue; nitahamasisha walevi na michupa yao kuingia mitaani kuhakikisha Ben, Njaa Kaya na mzee Ruxa wanashikwa na kutupwa lupango ili wachunguzwe.
Hivi huyu anadhani walevi wameishasahau HEPA yake na Njaa Kaya? Pamoja na ulevi wetu, bado tunajua kuwa HEPA iliasisiwa na Nkapa, Mangulangula, Njaa Kaya na Pita Noni ili kushinda kwenye uchakachuaji. Tunajua walioshirikiana na Net Problems Group iliyopewa kuua Tanisco waliletwa na makampuni ya shemeji za Ben baada ya nkewe bi Anna Tamaa kumzidi kete. Yethu, unafanya mchezo na mbesha! Rua, Ben tafadhali usinifanye niape kwa majina ya miungi wakali wakamnyotoa roho hata kabla hajakanyaga Keko au Ukonga.
Kwanini Ben hataki kukumbuka kuwa hata mijengo yetu aliyojitwalia yeye na wenzake bado tunaitaka na kuikumbuka? Ngoja Dk Kanywaji apate rungu la pili amtumbulie mbali. Lazima mijengo yetu irejeshwe na Ben na wenzake watumbuliwe tena kavu kavu. Utaachaje watu waliotumia akili uchwara kuibia kaya? Utaachaje wavivu wa kufikiri waibie kaya halafu waendelee kuwakonga walevi  nawe udai unapambana kwa ajili ya kuwaletea maisha bora na kubadili kaya?
Kwanini Ben anasahau kuwa walevi walitaka asulubiwe muda mrefu ila Njaa Kaya akamkingia kifua akiwa Sweden ambako nami nilikuwa nimealikwa kutoa mhadhara juu ya faida ulevi wa usawa ambapo wanawake na warume hunywa pamoja bila kupigana wala kukwaruzana.
Hivi kwanini Ben anusurike wakati washirika zake kama Dan son of Jonah na Pesambilimbili Mrambaramba walishapatikana na hatia kwa makosa waliyotenda wakiongozwa na Ben huyu huyu? Hakuna sehemu alituboa walevi kama kutuasa tuchape kazi kwa bidii wao waibe na kula kwa bidii. Eti li jiBen lilisema tusiulize kaya imetutendea nini bali tumeitendea nini! Lenyewe–zaidi ya kuiibia kaya–liliifanyia nini? Ama kweli nyani haoni nonihino lake. We ngoja walevi waendelee kuchukia uone tutakavyofanya kweli pakawa hapakaliki. Basi kama Ben anadhani walevi wamemsahau au wanamuogopa, anajidanganya. Rejesha mijengo yetu badala ya kuleta rongorongo uchwara. Mwizi ni mwizi hata aitwe mheshimiwa.
Mbali na Ben kutusisitiza tuchape mzigo yeye ahomole atakavyo, aliwashambulia waandishi wa umbea kuwa hawajui kufanya uchambuzi. Aliongeza kuwa wanalalamika badala ya kushauri. Umshauri nani wakati ukifanya hivyo, gendaeka linakwambia u mvivu wa kufikiri? Ungelishaurije jitu lenye kujitiatia na kujua kila kitu japo sasa limeisha na kuishiwa? Ben alinasema eti watu hawajui kufanya analysis kana kwamba yeye anajua. Huo ugwiji wa analysis wa Ben uko wapi iwapo kila alichofanya ni hovyo? Hata alivyoongea hakuonyesha chembe ya utafiti wala uchambuzi anaotaka wengine waujue. Unawezaje kusema walevi wote hawajui kuongea kana kwamba umeongea nao wote halafu uitwe pumba zako uchambuzi? There’s no sacregious sin in research like generalization that Ben made. Ohooo! Nisameheni. Kila ninapochemka kikameruni kinamwagika chenyewe.
Kama Ben hatafunga domo lake, atanifanya niingie mtaani na kwenda moja kwa moja Magogoni kuhahakikisha anatumbuliwa tena chap chap na kavu kavu. Apange jinsi ya kurejesha njuluku zetu, mijengo yetu, Kiwila na kunyea debe badala ya kuleta ngebe. Kwa taarifa yake, hata nkewe tunachunguza ili atumbuliwe. Hata ntangulizi wake na aliyenrithi wote tutawatumbua tu. Sijui nani anawapa kiburi wajivuni hawa hadi wakajilisha pepo wakati wana kongwa shingoni mwao? Shame on them all! Rejesheni njuluku na mali mlizotuibia badala ya kututisha na kutuhubiri upuuzi wa kuomba misamaha ya kisanii na kimagamba wakati nyinyi ni majipu na magamba yanayotucheka na kutuzomea kimoyomoyo.
Kwa vile nimechonga sana, nahisi kiu kiasi cha kuhitaji msokoto na kachupa ka gongo lau nipoze hasira nisijekwenda kufanyia gendaeka kitu mbaya.
Chanzo: Nipashe Jumamosi.

Wednesday 22 June 2016

Kijiwe chamkaribisha Pumba kijiweni

Baada ya kuisha na kuishiwa kiasi cha kujirahisi, Kijiwe kimemuonea huruma Profwedheha Ibra Pumba kuja kujiunga nacho na kupiga kahawa badala ya kuendelea kujivua nguo.
Mpemba analianzisha, “Yakhe mmensikia yule porofedheha alokikimbia chama cha Kafu halafu eti ajirudisha ataka aendelee kuwa mwenyekiti? Wallahi mie kama atakubaliwa kurejea hiko cheo naregesha kadi yangu. Itakuwaje chama kigeuzwe choo ambapo yeyote ajisikiaye haja ya kuingia huingia humo?”
Mgosi Machungi anachomekea, “Huyu waa isitipe tabu. Kama aitaka taaka akapewa anaudi kufanya nini wakati wameishamchezea na kumtupa kama ganda? Uzui nimesikia Kafu wakisema kuwa huwa hawana taala rejea. Abaki huku huko na hao hao waiomdanganya na kumchezea haafu wakamtema. Nani anataka mabaki jamani?”
Msomi Mkatatamaa anakula mic, “Wahenga walisema; adui yako muombee njaa. Ama kweli njaa kitu kibaya. Yaani prof mzima unaamua kujivua nguo hadharani bila hata kufikiri japo kidogo! Sijui nani walimdanganya huyu ndugu yetu kiasi cha kujigeuza pumba kirahisi hivi? Ama kweli kuchamba kwingi kuondoka na  mavi! Kwanini hakutumia usomi wake lau kuangalia mbele hata kama ni meta moja? Nijuavyo mimi, huyu jamaa hatafanikiwa.”
Anapiga chafya mara mbili na kuendelea, “Ushauri wangu wa bure ni kwamba arejee shule akapige chaki kama bado anahitajika; kama hakuna anayemhitaji basi arejee kijijini kwake akalime tumbaku au mahindi mchezo uishe.”
Dada Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic, “Ama kweli hujafa hujaumbika; usipoangalia unaweza kuumbuka. Nikikumbuka nyodo za jamaa yetu akijiondoa kwenye ulaji sina hata hamu wala la kusema zaidi ya kumshauri atafute shughuli nyingine ya kufanya.”
Mbwamwitu anachomoa mic, “Mie namshauri aje hapa awe akitupa somo la jinsi ya kunywa kahawa kiuchumi.”
Mzee Maneno anamnyang’nya mic Mbwamwitu, “Jamaa yangu shushu alinitonya kuwa jamaa aliahadiwa uwaziri wa njuluku kama angejitoa Kafu wakati ule asijue alikuwa akiukwaa mkenge mchana kweupe. Sijui kwanini baadhi ya wasomi wetu wanaonyesha ukilaza hata kwenye mambo madogo? Ama kweli tamaa mbele mauti nyuma,” anamalizia akimpa kikombe muuza kahawa amuongezee kahawa.
Mijjinga anaamua kutia guu, “Mie nadhani mnaomshangaa profwedheha Pumba mnakosea. Kwani, najua kinachomsukuma ni kudhani kuwa kile chama ni mali ya wakubwa wake wanaoweza kukitumia kama NGO kujipatia ulaji. Sioni tofauti kati yake na wale walioingia ndoa ya mkeka na wabaya wao wakaisha kutumika kwa muda na kubwagwa; na sasa wanalialia wasijue mustakabali wao. Kumbuka hii Bongo jamani.”
Mheshimiwa Bwege naye anatia guu, “Japo wengi wanadhani mwenye jina la Bwege ni mimi peke yangu wasijue ni kinyume chake, wapo mabwege wa kweli kweli kweli. Huwezi kujiuzulu kwa hiari yako ukatagemea kurejea kwa hiari yako. Huu ndiyo ubwege wa kweli achia huu wa jina. Kwanza, siamini kama Kafu wameisha na kuishiwa kiasi hiki kiasi cha kupwakia matapishi ukiachia mbali mabaki. Pili, anataka kurejea kufanya nini wakati yeye, kama kamanda wa vita, alijiuzulu wakati majeshi yakielekea vitani? Sasa vita imekwisha eti anataka ukamanda tena. Hii akili au matope au wehu tena wa mchana?”
Kapende aliyekuwa akibofya kijisimu chake anaamua kula mic, “Hata mimi simshangai huyu nyanda. Nadhani ameshindwa kutofautisha vyama vya mfukoni na vyama vya wananchi. Kwanini msomi aliyekubuhu kama huyu hajitofautishi na kina Joni Cheo, Gus Mlemavu na Fahamu Duvutwa? Alidhani Kafu ni NGO kama zile za wake wa marahis kutumia kujitengenezea ulaji kirahisi hivi? Kwa alivyoishiwa hata akina Mlemavu na wababaishaji wengine hawamtaki.”
Kanji anaamua kukamua, “Sasa hii pumba kwanini napoteza muda. Kama nataka laji kwa chama basi unda chama yake. Sasa kama Kafu nasema hapana regea yeye, yeye iko gangania nini? Kama veve nauzuru chamani na vatu haiko taka veve tena nenda unda chamani yako tumia kama dukani yake chezo kwisha.”
Mipawa aliyekuwa akitabasamu muda wote anaamua kula mic, “Mimi nitachukua mrengo tofauti. Badala ya kumlaumu Pumba kwa masahibu yaliyomkumba tokana na upumba wake, namshauri atulie kwanza. Aje hapa kijiweni tumpe michoro ya kuweza ku-survive katika hali hii. Hata hivyo, kwa muda wa miaka mingi aliyokuwa mwenyekiti bila kuleta mabadiliko yoyote, anapaswa kukubali kuwa zake zimekwisha; na lazima wengine waje wajaribu. Nadhani hili halimhusu Pumba pekee. Hata maalimu Madevu naye anapaswa kuwapisha wenye nguvu na mawazo mapya kukwamua chama kama kweli wanalenga kushika dola. Hata hivyo, kama wanataka kutengeneza dola kwa mgongo wa chama, wawili hawa wanaweza kuendelea na biashara yao ya siku zote.”
Msomi anakula mic,”Dk Mipawa umetoa pwenti kubwa sana. Umeingia ndani zaidi kwa kukangalia mfumo mzima wa ulaji wa kisiasa kwenye vyama. Kama vipindi vya urahis ni viwili tu, inakuwaje mtu aongoze chama kwa zaidi ya vipindi viwili yaani miaka kumi? Hata Chama Cha mafisadi (CCm) kimewapiku katika hili. Nadhani wakati wa kuandaa benchi ya Pumba hapa kijiweni umewadia.”
Kabla ya kuendelea simu ya Msomi ililia. Anapokea na kusema, “Halo profedheha Pumba, unasema eti unataka kujiunga na kijiwe chetu? Basi wakaribishwa hata sasa.” Msomi anakata simu na kutupa taarifa kuwa Pumba ameamua kujiunga na kijiwe lau kujadili yanayoendela kayani.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Sunday 19 June 2016

Boozers want their former biggies probed

            When boozers got wind of how some hunks are taxing their former biggies to come clean on their past, they asked me to pen this piece demanding that our hunk follows suit. Boozers aren’t happy with some of their former rulers especially those who screwed them up openly so as to become poorer and poorer while some buggers became richer and richer thanks to ripping them off. From this milieu thus, I’d like to officially petition the govt to start probing such venal biggies. Boozers would like to see their closets open so that all skeletons can be cleansed.
            It recently came to light that biggies and their spouses and pals in Brazil, Israel and Nigeria are probed. Essentially, what transpired in these hunks alerted boozers to ponder on taking on their former biggies–though not all–as the way of knocking sense into all those who still wrongly believe that Bongolalaland is grandma’s garden.
            It recently came to light that in Brazil, the hunk’s started the journey of shedding its grungier and gloomier past. Authorities started with president madam Dilma Rousseff who’s been suspended so that she’d be probed without any interloping.
            Nigeria followed suit by probing their former president Goodluck Jonathan. Israel went a mile ahead by probing the wife of their Prime Minister Sarah Netanyahu after it came to light that she wickedly spent public dosh on personal matters.
            Sometimes, this might be seen as witch-hunting, our hunk needs to tax everybody who once led it to come clean on all allegations they face especially robbing our coffers and misusing our taxes. This is nothing but doing justice to them even to boozers. I wonder; why’d we exempt big and powerful criminals from facing the music while some junior officials have already faced it? In boozers’ lingua, this is called the moment of truth.
            If we look back at how our hunk was raped, robbed and abused, we find a tremendous need of having those behind such heinous crime should not only be probed but also put behind bars; regardless they’re sharks or small fish. Like Israel, we need to probe biggies’ spouses whom we know to have robbed us using their bogus Non-Governmental Organisations (NGOs) such as MAWA and EOTFL.
            The examples from Brazil, Nigeria and Israel are crucial for our hunk shall justice be delivered; and be seen done. We need to not only probe our former biggies but also their family members, consigliore and partners in crime. If we can probe and fire other public workers, why can’t we do the same to our rulers who used to be public employees though in high positions?
            Probing our former biggies has many gains:
            Firstly, it’ll help them to do away with rumours and accusations that they either mismanaged or robbed our hunk.
            Secondly, it’ll unearth corrupt biggies, especially those who took boozers for a ride thinking they’d get away with murder. Thirdly, it will restore the code of ethics, accountability and limpidity.
            Fourth, it’ll create a precedent that; nobody’s above the law. Fifth, it’ll send a clear message to corrupt biggies especially those who turn public offices into dosh-making ventures at the detriment of boozers.
            The history of our hunk shows that almost all former biggies minus the late Mwl Julius Nyerere have skeletons in their closets. For instance, mzee Ruxa has always been accused of engineering Loliyondo scam in which the part of our national park was vended to an Arab who killed many animals indiscriminately. As for Ben, Kiwila scam’s always become a cross on his neck not to mention doing illegal biz in the holy of the holy of Magogoni. So, too, Ben is accused of entering bogus contracts under the guise of investment that saw our NBC and other lucrative parastatals robbed.
 When it comes to Jake Kiquette, his mess is bigger than all of his predecessors put together. Allegations against him are clear; and have been going on for a long time. EPA scam opened the curtain even before the dude came to power. Thereafter, Richmond kicked in. Before the dust settled, UDA and Escrow scams kicked in not to mention his irresponsible rule that saw our hunk wasting billions of dough on a draft constitution that’s butchered for fear of prosecution after abdicating. We’re talking of scams. Jake’s also accused of spending much dosh and time globetrotting so as to force boozers to coin a say that their hunk was on out pilot during Jake’s tenure.         The other day at Mwl Nyerere’s symposium, I heard Ben defending Jake when General Ulimwengu wanted him charged for embezzlement. Ben said we’d advise them instead of blaming them.  How so if we advised them and they said we are lazy at thinking? We need to kick ass to see to it we move forward as a hunk.
Given that other sane hunks have started to open the closets of their former biggies, Boozers think; and would like to see their big suspects being probed and those found culpable should be put behind bars at least.
Source: Guardian on Sunday,

Mama Magufuli achana na biashara ya NGO fichi

           
            Hivi karibuni mke wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli, Janet, alikaririwa na vyombo vya habari akiwa mkoani Mtwara alikotoa msaada wa takriban shilingi milioni 200 kwa wazee. Hakika hili ni jambo jema japo nyuma yake kuna namna.
            Mumewe alipoingia madarakani, binafsi niliandika makala ya kumpongeza kwa kutoanzisha NGO kama watangulizi wake ambao walionekana kuwa wafanyabiashara zaidi ya wenzi na washauri wa rais.  Hata hivyo, kutokana na hili la juzi, hali inaanza kubadilika kiasi cha kuchanganya na kutia shaka. Kwa mfano, wengi wangetaka kujua alikopata fedha nyingi kiasi hiki; na nani walimpa na kwanini sasa wakati wazee na wenye shida wamekuwapo nchini hata kabla ya Magufuli kuingia madarakani?
            Kwa tunaojua wake wa marais waliopita ukimuondoa mama Maria Nyerere, hawana heshima waliyostahili mbele ya jamii kutokana na kujiingiza kwenye biashara hii kwenye migongo ya waume zao. Hivyo, tutamshauri mama Magufuli mambo kadhaa ili kumuepusha na kashfa, na madhara yatokanayo na biashara hii ya NGO.
            Mosi, tungemshauri atumie muda wake kujisomea. Achukue mfano toka kwa mama Tunu Pinda mke wa waziri mkuu mstaafu Mizengwe Pinda ambaye–tokana na nafasi yake na kiwango chake cha elimu–anaweza kuiga mfano mzuri kwake.  Mama Pinda alitumia muda wa uwepo wa mme wake madarakani kujiendeleza kielimu hadi kufikia shahada ya pili. Tofauti na yeye, mke wa rais mstaafu Jakaya Kikwete, Salma alipoteza muda mwingi kwenye biashara ya NGO kiasi cha kuendelea na kuwa na elimu haba bila sababu ya msingi zaidi ya kutoona mbali.             Mwanzilishi wa hii biashara ya NGO za wake wa marais, Anna Mkapa, aliondoka na sifa mbaya sana ya kumrubuni mumewe aliyekuwa ameanza kazi vizuri kufanyia biashara ikulu hadi kufikia kijimilkisha mali ya umma kama vile Machimbo ya Makaa aya Mawe ya Kiwira ambayo yamegeuka kongwa shingoni mwa Mkapa. Mpaka tunapoandika, Mkapa hana jeuri aliyokuwa nayo wakati akinadiwa na Nyerere au kipindi cha kwanza cha urais wake. Ni mtu anayeishi kwa kutegemea kulindwa na rais aliyeko madarakani kama ilivyotokea wakati wa Kikwete ambaye alisema tumuache mzee Mkapa astaafu apumzike pale baadhi ya watu walipotaka awajibishwe kuhusiana na kashfa ya Kiwira. Huyu naye ni jipu; na hizi NGO ni majipu tu yanayopaswa kutumbuliwa na kuepukwa na mke wa rais anayeonyesha kufanya hii biashara kwa mlango wa nyuma.
            Pili, tunamshauri mama Magufuli aachane na biashara ya NGO; itamchafua na kumchafulia mumewe hasa ikizingatiwa kuwa watu wengi wenye kutia shaka watakuwa tayari kumtumia kwa kisingizio cha kutoa misaada kupitia kwake. Mfano, hivi karibuni mama Magufuli alikaririwa akimsifia aliyemuita Nabii TB Joshua ambaye biashara yake ya kuchuuza roho za watu inajulikana.
            Tatu, afahamu na kujiuliza swali jepesi: hawa akina Joshua walikuwa wapi kabla ya Magufuli hajawa rais? Kwani wazee wa Tanzania wameanza kupata matatizo alipoingia Magufuli? Kwanini hawakutoa misaada husika kwa wizara husika kama kweli wana nia njema na mama Magufuli hata hao wazee wanaojidai kuwasaidia? Je wanataka kumtumia kama walivyomfanyia rais wa zamani wa Malawi, Joyce Banda, waliyemhadaa kuwa wangemuwezesha kushinda kwenye uchaguzi wa urais nchini humo akaishia kuangikia pua? Nani anahitaji kushinda kwa maombi kama si upuuzi? Rais anashinda kwa sifa na si miujiza wala maombi. Ni jambo la kutia shaka kwa Magufuli aliyekiri kuwa ni muumini wa kiroma tangu kuzaliwa kuruhusu mkewe, hata naye binafsi, kuyumbishwa na manabii wa uongo kama huyu tapeli wa kinegeria ambaye miaka miwili iliyopita hosteli yake ilianguka na kuua watu wengi waliokuwa wameingia mkenge kuja kuombewa. Pia mamlaka za Nigeria zilikuta kuwa ujenzi wa hosteli yenyewe ulifanyika kitapeli na chini ya viwango. Mhalifu kama huyu kweli anaweza kuwa nabii? Nilimsikia mama Magufuli akimshukuru na kumwita nabii Joshua wakati akijua fika kuwa enzi za manabii wa kweli ziliisha zamani zikabaki na manabii wa uongo alioonya Yesu kuwa wangekuja na kupoteza wengi.
Nne, mama Magufuli anapaswa kujua kuwa si wengi wanaokuja kwa gea ya kumpa misaada wana nia njema naye. Wanaangalia kiti alichokalia mumewe ili kuwa karibu na jungu kuu wapate miradi yao. Mbona Nigeria ina wazee wengi wanaoadhirika? Kwanini Joshua asianze kwao hasa ikizingatiwa kuwa hisani huanzia nyumbani?
            Tano, atangaze hiyo NGO anayoonyesha kuiendesha kichini chini. Juzi juzi alitoa misaada ya shilingi za kitanzania milioni 200 bila kutoa maelezo ya ni nani walitoa fedha hiyo. Kwanini wasiitoe kwa wizara husika na wizara itafanya kazi gani kama mke wa rais anaingilia kazi zake? Si lazima kila mke wa rais afanye biashara ya NGO. Tumeona madhara yake na uchafu uliowakumba waliozianzisha kwa tamaa ya utajiri kwa kisingizio cha kuhudumia watu ambao wana wizara ya kuwahudumia tayari. Kama lengo ni kuwasaidia basi mama Magufuli awaambie wanaotaka kumsaidia waelekeze misaada hiyo wizarani.
Mwisho, najua makala hii haitawapendeza wahusika na wale wanaopenda kuwahadaa ili kulinda kitumbua chao mbali na wanaojipendekeza ili lau wakumbukwe. Lazima niseme wazi; naandika kuwasaidia na kuwakosoa badala ya kuwasifia mambo ya kipuuzi. Rais Magufuli aliomba watanzania tumsaidie katika uongozi wake. Hii nayo ni mojawapo ya kumsaidia kimawazo ili asiingie mkenge akapoteza sifa zake njema na kujuta kama Mkapa ambaye kwa sasa anajiishia tu akiomba Mungu asitokee rais mwenye kuchukia ufisadi akafichua uovu alioufanya kwenye uwekezaji ambao umeiingiza nchi kwenye umaskini bila ulazima.
Janet pia anaweza kuiga mfano mwingine toka kwa mama Maria Nyerere ambaye hakujiingiza kwenye biashara yoyote eti kwa vile mumewe alikuwa rais. Mama huyu hadi sasa anaheshimika kwa kumsaidia mumewe kuipusha ikulu kuwa pango la wezi kama ilivyokuja kugeuka pindi tu mwalimu alipong’atuka wakati ruksa na vimemo vya first lady.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Saturday 18 June 2016

Magufuli tumbua hata vilaza wazito

William Lukuvi cropped.pngDiodorus Kamala (12746453754) (cropped).jpgRIO DE JANEIRO - JUNE 13: The Humanidade Event on June 13, 2012 in Rio de Janeiro ,Brazil - stock photoMary Nagu.jpgImage result of saada mkuya
          Akiweka jiwe la msingi la maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM) hivi karibuni, rais John Pombe Magufuli alisikika akilaumu kitendo cha Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kudahili watu wasio na sifa ambao aliwaita vilaza akimaanisha wasio na uwezo mkubwa kiakili.
            Katika hotuba yake ya takriban saa nzima, Magufuli aliimwagia sifa lukuki UDSM akisema kuwa imedahili vipanga akimaanisha watu wenye akili zinazochemka ingawa hili nalo linatia shaka hasa ikizingatiwa kuwa madudu na rushwa na upendeleo vimo katika idara nyingi na karibia kila sehemu nchini. Sijui kama kweli waliodahiliwa na kujiunga na UDSM ni vipanga watupu.
            Magufuli alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Una D, D unasajiliwa kuchukua digrii chuo kikuu na unapata mkopo wa serikali, ni aibu ya ajabu, haiwezekani, haiwezekani, haiwezekani.” Magufuli alionyeshwa kukasirishwa na kashfa hii; na kusisitiza kuwa asingeweza kuvumilia madudu kama haya.
            Aliongeza, “Lakini wakati tunawalipia wanafunzi 489 waliomaliza kidato cha nne na kupata D, D manaake wengine ni divisheni 4, kuchukua digrii, wapo wanafunzi wengine wa kidato cha sita wamekosa mikopo, wapo wanafunzi wengine walio na diploma wamekosa mikopo.” Huu ni ushahidi kuwa kuna watu wenye sifa hawakuwezeshwa kujiunga na vyuo vikuu wakati wasio na sifa wakiwezeshwa. Ndiyo maana tunasema; hatujui kama UDSM haina vilaza hata kama si wengi kama waliogunduliwa UDOM.
            Baada ya kufichuka kashfa hii, tunapaswa tujiulize maswali magumu kidogo na kuyapatia majibu sahihi tena kwa wakati. Je hapa vilaza ni wale waliohonga wakadahiliwa na kufanikiwa kuingia chuoni au wale waliowadahili ilhali wakijua kufanya hivyo–licha ya kuua elimu–ni kinyume cha sheria na tararibu hata akili ya kawaida common sense? Je hawa wote si vilaza japo kwenye maeneo tofauti? Waliosajili ni vilaza wasiojua aina ya watu waliopaswa kuwadahili na kuwaruhusu kujiunga na chuo. Je kuna vyuo vingapi vyenye kujaza vilaza ili kujipatia fedha badala ya kutoa elimu nchini? Je tatizo ni vyuo au mfumo mzima wa elimu nchini? Je kwanini wameadhibiwa wadahiliwa bila kuwahusisha wenzao waliowadahili. Waingereza husema; it take two to tango yaani hii ni ngoma ya wawili. Iweje waliosababisha kashfa hii wasiwe korokoroni wakingojea kupewa haki yao? Je ni vilaza wangapi wameishajipatia shahada kinyume cha sheria? Je serikali ina mpango gani kuwabaini na kuwachukulia hatua mojawapo ikiwamo kutotambua shahada zao au kuwalazimisha warudie masomo kwa gharama zao?
            Kama tutakuwa wakweli kwa nafsi zetu na kusema ukweli kama ambavyo–mara nyingi –rais Magufuli amesisitiza, Tanzania ina vilaza karibu kila idara na nyanja. Wapo kwenye mahakama, bunge, wakuu wa wilaya na mikoa, kwenye baraza la mawaziri; na wamo hata kwenye ofisi ya rais. Mfano wa karibuni ni kwa mtuhumiwa mmojawapo wa kughushi sifa za kitaaluma aliyefichuliwa na mwanaharakati Keinerugaba Msemakweli. Huyu si mwingine ni waziri William Lukuvi aliyetajwa sambamba na mawaziri na wazito wengine wa wakati ule. Waliotajwa na Msemakweli ni pamoja na Deodorus Kamala, Emanuel Nchimbi, Mary Nagu, Makongoro Mahanga, Victor Mwambalaswa, na Raphael Chegeni. Pia wapo mawaziri na vigogo wa zamani ambao CVs zao zinaonyesha shaka. Hawa ni aliyekuwa waziri wa fedha Saada Mkuya, naibu wake Adam Malima na aliyekuwa meya wa jiji la Dar Es Salaam Didace Massaburi. Malima na Mkuyu–kwa mujibu wa CVs zao–walipata shahada za pili bila kuwa na shahada za kwanza.
            Hakuna kitu kilishangaza wengi kama wawili hawa kupewa wizara nyeti ambayo matokeo yake ni majipu kama vile Escrow. Hata waliowateua nao wanatia shaka bila shaka.
            Msemakweli hakutaja tu bali aliandika kitabu alichokiita Mafisadi wa Elimu Tanzania. Baada ya Msemakweli kurusha kombora lake, Tume ya Vyuo vikuu, Tanzania Commission of Universities (TCU) iliwataka wahusika kufika mbele yake na kujitetea. Hadi sasa wananchi walio wengi hawajui kilichoendelea. Kwani si wahusika wala serikali waliokuwa tayari kueleza ukweli na uongo ni upi kiasi cha kuacha madai ya Msemakweli yakisimama kama ukweli usiopingika. Alipotoa shutuma hizi, wapo waliotishia kumshitaki wasifanye hivyo. Je hii maana yake ni nini? Ni kwamba waligwaya ima kutokana na madai ya Msemakweli kuwa ukweli mtupu au kuogopa kumwaga mtama kwenye kuku wengi kiasi cha kuumbuliwa zaidi. Hili hakika nalo ni jipu linalopaswa kutumbuliwa haraka huku watuhumiwa wakiwajibishwa kwa kutoza faini na kurejesha mapato yote waliyopata kwa kutumia sifa za kughushi. Kwa wale waliomo serikalini, wanapaswa kufukuzwa mara moja huku walioko bungeni wakifungashiwa virago haraka pia.
            Haiingii akilini kuwaadhibu wanafunzi tena vijana wadogo waliosukumwa na shida na uwepo wa mazingira kutenda kosa walilotenda huku serikali ikiwaacha mafisadi wakubwa wa elimu kama alivyowaita Msemakweli. Huku ni kutekeleza sheria kibaguzi na kuifanya iwatumikie wenye nacho wakati ikiwapatiliza wasio nacho.
            Tumalizie kwa kumtaka rais Magufuli awatumbue vilaza wazito ili kuondoa dhana ya upendeleo na kulindana. Maana kama atatumbua wanafunzi waliogundulika juzi wakati kuna vigogo waliojipatia vyeo na marupurupu bila kustahili, ataonekana kama anaendeleza mchezo ule ule uliokaribia kukiua Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa “Huyu ni Mwenzetu.” 
Chanzo: Mwanahalisi.